Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110171 articles
Browse latest View live

Serikali ifikirie upya marufuku ya kukaririsha darasa

$
0
0
HIVI karibuni Serikali kupitia Kamishina wa elimu Dk. Edicome  Shirima ilitoa taarifa kwa umma ikizitaka shule binafsi kuwarejesha mara moja katika madarasa yao wanafunzi waliokaririshwa madarasa au kuhamishiwa shule zingine

Kwa kigezo cha kushindwa kufikia wastani uliowekwa na shule husika hadi kufikia tarehe 20 mwezi huu.

Taarifa hiyo inaeleza kitendo cha kuwakaririsha madarasa, kuwafukuza shule ama kuwahamisha wanafunzi ambao wamefaulu mtihani wa kitaifa wa Darasa la Nne, Kidato cha Pili au ule wa Kidato cha Nne ni kwenda kinyume na Waraka wa Elimu Namba 7 wa mwaka 2004.



Kwa maoni yangu nasema hii inaweza kudhoofisha shule binafsi na huenda ukawa ni mkakati wa Serikali kutaka kujaribu kuleta uwiano baina ya shule binafsi na zile za umma jambo ambalo litachukua miaka mingi sana kutokea.

Walianza na ada elekezi na sasa hivi wamehamia kulazimisha wanafunzi wasikariri madarasa.Ingawa sikatai kuwa uendeshaji wa shule binafsi lazima uzingatie sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa na Serikali,

Lakini binafsi naona kuna haja ya Serikali kuacha kuingilia baadhi ya mambo yanayofanywa na shule hizo binafsi.Ni lazima ifahamike kusoma shule binafsi siyo haki ya kila Mtanzania isipokuwa tu shule hizo zipo kwa ajili ya wale ambao watakubaliana na vigezo na masharti ya kujiunga na shule hizo ikiwemo uwezo wa kulipa ada na ufaulu.

Naomba ninukuu kauli ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Suleiman Jaffo aliyowahi kuitoa hivi karibuni kwamba " hatutaziua shule binafsi kwa kuzifungia badala yake zitakufa zenyewe kwa kukosa wateja pale tutakapoboresha na kuimarisha mazingira ya shule zetu za umma”.



Amirali Karim is No More With Us

$
0
0
Salaams and Dwa.
Tunachukua nafasi hii kutoa Pole kwa familia ya ndugu Amirali Karim. Kwa msiba mkubwa iliotokea.
Ila yote haya ni mipango ya Allah.
Tumuombee Allah umpumzishe kwa amani.
​  From Izaas Staff

Utambulisho wa nyimbo mpya inayoitwa BROTHER kutoka kwa DABO

$
0
0
DABO Tanzanian Best Reggae and Ragga / Dancehall Star Artist. Occupations: Songwriter, Singer, Melody Maker, Performer, Entertainer, Actor, Story Maker and Script Writer. Achievements: Awards Winner Best Reggae and Best Ragga/Dancehall Awards

MAWAZIRI WANNE WATEMBELEA JULIUS NYERERE INTERNATIONAL AIRPORT DAR ES SALAAM

MICHUZI TV: AMSHA KIPAJI CHAKO NA TBREAKER.

MPIGIE KURA LADY JAYDEE NA WASANII WENGINE WASHINDE

$
0
0
Piga kura kwa kufungua website hii, 
kisha fuata maelekezo:
https://www.amiawardsafrika.com/pc-nominees

Michuzi TV: HARUSI YA SHILOLE YATIKISA..

DAILY NEWS DIGITAL: AJALI, LORY LA COCACOLA LAANGUKA TAZARA JIJINI DAR ES SALAAM


MC GARA B: TAZAMA PERFORMANCE YA KWANZA YA PAPII KOCHA TANGU AWE HURU

UNNewsKiswahili: Walinda amani kutoka Tanzania wajikita na operesheni maalum Sudan

SERIKALI KUPITIA DAWASA KUJENGA MITAMBO MITATU YA KISASA YA KUCHAKATA MAJI TAKA JIJINI DAR ES SALAAM

WAVUVI WALIA NA UPEPO MPALI BAHARINI

$
0
0
 Wavuvi wakiwasili katika ufukwe wa Kunduchi jijini Dar es salaam baada ya kutoka kuvua samaki, Baadhi ya wavuvi hao wamesema kuwa kipindi hiki ambacho ni cha upepo mkali kumekuwa na uhaba sana wa upatikaji wa samaki, hali inayowalazimu kwenda mbali zaidi kutafuta samaki na wakati mwingine hurudi bila mafanikio.

MWENYEKITI WA UVCCM AINGIA RASMI KAZINI

$
0
0
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Kheri D James akisalimiana na Mtumishi wa Makao Makuu ya Umoja wa Vijana  wa CCM Bi.Sheila Alipowasili katika Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya Umoja wa Vijana Wa CCM Upanga.
 Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana(UVCCM) Taifa Ndg.Shaka Hamdu Shaka (kwanza kushoto)akimtambulisha Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Ndg.Kheri D James kwa Makatibu wasaidizi wakuu alipowasili ofisi ndogo za UVCCM Upanga.

 Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM(UVCCM) Ndg.Shaka Hamdu Shaka akimuonyesha Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Ndg.Kheri D James moja ya Ofisi ya Makao makuu.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

VIONGOZI WANNE WASHTAKIWA KAMATI YA MAADILI

$
0
0
Sekretarieti ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF imewapeleka kwenye kamati ya Maadili viongozi wanne kwa kughushi na udanganyifu. 

Viongozi walioshtakiwa kwenye Kamati ya Maadili ni msimamizi wa Kituo cha Mtwara Dunstan Mkundi, Katibu wa Chama cha soka mkoa wa Mtwara Kizito Mbano, Muhasibu msaidizi wa klabu ya Simba Suleiman Kahumbu na Katibu msaidizi wa Klabu ya Ndanda FC ya Mtwara Selemani Kachele. 

Sekretarieti inawashtaki viongozi hao kwa makosa ya kughushi pamoja na udanganyifu wa mapato kwenye mchezo namba 94 kati ya Ndanda FC ya Mtwara dhidi ya Simba ya Dar es Salaam iliyochezwa Disemba 30, 2017 kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara.

Kwa tuhuma hizo viongozi hao watatakiwa kufika mbele ya kamati Januari 18, 2018.

Kamati ya maadili iko chini ya mwenyekiti Wakili Hamidu Mbwezeleni, Makamu Mwenyekiti Wakili Steven Zangira, Wajumbe ni Glorious Luoga, Walter Lungu na Amin Bakhresa

TASWIRAZZ

KABATI ATOA MSAADA WA MAFUTA MAALUM YA KUPAKA KWA WATU WENYE ULEMAVU WA NGOZI MKOA WA IRINGA

$
0
0

Na Fredy Mgunda,Iringa

JAMII imetakiwa kuwalea, kuwatunza na kuwajali watu wenye ulemavu wa ngozi albino kwa kuhakikisha kwamba wanaishi katika mazingira mazuri, yenye usalama na sio kuwanyanyapaa pale wanapohitaji mahitaji yao ya msingi.

Aidha Chama cha walemavu wa ngozi (TAS) mkoa wa Iringa kimeshauriwa kuendelea kushirikiana na serikali, ili walemavu hao pia waweze kupata elimu juu ya afya ya usalama wa ngozi pamoja na kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili katika maisha yao.

Hayo yalisemwa na mbunge wa viti maalum Ritta Kabati wakati alipokuwa akitoa msaada wa mafuta maalum ya kupaka watu wenye ulemavu wa ngozi albino katika hafla fupi iliyohudhuriwa na walemavu hao ambayo ilifanyika kwenye ukumbi wa halmashauri ya manispaa ya Iringa

“Nampongeza Mwenyekiti wa TAS mkao wa Iringa kwa jitihada zake alizozifanya juu ya namna ya kupata mafuta haya, kama chama endeleeni kuwa wabunifu namna ya kulisaidia kundi hili tete la walemavu kwa kuwalea na kuwatunza katika mazingira mazuri”, alisisitiza mbunge Kabati 

Vilevile Kabati aliongeza kwa kuwataka viongozi wa chama hicho kutumia fursa waliyopewa na wanachama wao, kuhakikisha kwamba wana ainisha matatizo waliyonayo walemavu wa mkoa wa Iringa na kuyafikisha katika ofisi za serikali ili yaweze kufanyiwa kazi.
Mbunge wa viti maalum Ritta Kabati akimkabidhi box la mafuta hayo katibu wa Tas mkoa wa Iringa bwana Leo Sambala katika ukumbi wa halmashauri ya manispaa ya Iringa  
 Mbunge wa viti maalum Ritta Kabati akimkabidhi boxi  la mafuta hayo katibu wa Mufindi bwana Andrea Kihwelo
 Mbunge wa viti maalum Ritta Kabati akimkabidhi  mafuta hayo moja ya walemavu wa ngozi
 Mbunge wa viti maalum Ritta Kabati akimkabidhi boxi la mafuta hayo mwenyekiti wa wilaya ya Kilolo ndugu Anna Masasi .



Mitambo ya Kisasa Kutumika Kusafisha Maji Taka Dar

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Ali Hapi amepongeza utendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam DAWASA na hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa miradi ya Maji Taka katika Wilaya ya Kinondoni ikiwa ni moja ya mikakati ya Serikali kuhakikisha kuwa Wananchi wanapata huduma Bora.

Akizungumza wakati wa ziara yakukagua maeneo yenye changamoto za majitaka na mradi wa uboreshaji wa huduma za maji taka ili kujionea hatua iliyofikiwa na DAWASA katika kutekeleza miradi hiyo Mhe. Hapi amesema kuwa ameridhishwa na kazi inayofanywa na Mamlaka hiyo katika Wilaya hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya Habari iliyotolewa na Mamlaka hiyo bomba lenye jumla ya kilomita 563 litajengwa ili kusafirishia maji taka hadi kwenye mitambo mikubwa itakayojengwa Mbezi beach, Jangwani na Kurasini jijini Dar es salaam. Mtambo utakaojengwa eneo la Kilongawima utakuwa na uwezo wa kusafisha lita za ujazo 16,000 kwa siku na utajumuisha mfumo wenye urefu wa kilomita 97 utakojengwa katika eneo la mbezi Beach, Kawe, Tegeta na maeneo ya jirani na kutekelezwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Benki ya Dunia na unatarajiwa kugharimu dola za Marekani milioni 65.

Mradi mwingine ni ule wa ujenzi wa mtambo wa kusafisha mita za ujazo 11,000 kwa siku utakaojengwa Kurasini ukihusisha maeneo ya Keko, Changombe, Kurasini, Temeke na Uwanja wa Taifa ambapo mfumo wake utakuwa na urefu wa kilomita 90. Aidha, katika eneo la Jangwani mtambo wenye uwezo wa kusafisha lita za ujazo 200,000 kwa siku utajengwa ambapo mabomba yatalazwa kutoka Ubungo,Kinondoni, Mwanenyemala, Msasani, katikati ya Jiji na Ilala hadi Jangwani ambapo awamu ya kwanza ikikamilika itahusisha mtambo wa kusafisha kiasi cha lita za ujazo 25,000 za maji taka kwa siku.

Mradi huo katika eneo la Jangwani utagharimu dola za marekani milioni 90 ambapo taratibu za manunuzi zinaendelea ili kumpata mshauri na hatimaye mkandarasi, lengo ni kuanza kwa ujenzi huo mapema mwaka huu.

DAWASA imekuwa ikishirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Wakuu wa Wilaya katika kutekeleza majukumu yake ya kutoa huduma bora kwa wananchi kwa kuzingatia dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano.
Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi wa Mamalaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) Modester Mushi akitoa maelezo kwa Mkuu wa Wilaya Kinondoni Ali Hapi kuhusu mradi wa ujenzi wa mtambo wa kusafisha Majitaka, Jangwani Beach, Dar es Salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ali Hapi akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO), Shabani Mkwanya, wakati akikagua mashine ya kusukuma majitaka, na mradi wa ujenzi wa mtambo wa kusafisha majitaka unatekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Majitaka DaresSalaam (DAWASA).
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ali Hapi akizungumza mara baada ya kukagua mashine ya kusukuma Majitaka katika eneo la Msasani Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ali Hapi akitoa maagizo kwa Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO) Shabani Mkwanya wakati akikagua chemba za Majitaka katika eneo la Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Fundi wa DAWASCO akifunua chemba wakati Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ali Hapi (mwenye suti nyeusi) akikagua chemba hiyo katika eneo la Msasani.

Waziri wa Kilimo Dkt.Tizeba atembelea Taasis ya Naliendele.

$
0
0
 Kaim Mkurugenzi wa Taasisi yaUtafiti wa Kilimo NALIENDELE Iliyopo Mkoani Mtwara Dkt Omar Mponda akitoa maelezo kwa Waziri wa Kilimo Dkt.Charles Tizeba kuhusiana na Mbegu za Muhogo ambazo zinazalishwa na Taasisi ya Hiyo.

Jumla ya miche ya Mikorosho Million10 imezalishwa na  Taasisi ya utafiti wa Kilimo NALIENDELE Iliyopo mkoani Mtwara kwa kushirikiana na Bodi ya Korosho Tanzania CBT kwa ajili ya kusambaza katika mikoa yote inayozalisha Zao la korosho.
 Waziri wa Kilimo Dr.Charles Tizeba akimsikiliza Mkuu wa Idara ya Udhibiti wa wadudu na Magonjwa wa Zao la Korosho Taasisi ya NALIENDELE Dr.Wilson Nene aliyevalia Tishet Nyeupe wakati waziri wa Kilimo Dr.Tizeba alipofanya Ziara katika Taasis Hiyo.
 Waziri wa Kilimo Dkt Charles Tizeba akioneshwa Shamba la Mfano la  Karanga lililopo Taasisi ya Utafiti ya Kilimo NALIENDELE Iliyopo Mkoani Mtwara.
Waziri wa Kilimo Dr.Charles Tizeba akimsikiliza Mkuu wa Idara ya Udhibiti wa wadudu na Magonjwa wa Zao la Korosho Taasisi ya NALIENDELE Dr.Wilson Nene aliyevalia Tishet Nyeupe wakati waziri wa Kilimo Dr.Tizeba alipofanya Ziara katika Taasis Hiyo.

NAIBU WAZIRI KWANDIKA AMESEMA BARABARA YA MBINGA HADI MBAMBA BAY NYASA ITAKAMILIKA KWA WAKATI

$
0
0
Wilaya ya nyasa nI kati ya wilaya zenye vivutio vingi vya utalii kutokana na uwepo wa ziwa nyasa, kufungaka kwa barabara ya mbinga hadi nyasa ambayo ujenzi wake unatarajia kuanza hivi karibuni kutafungua fursa nyingi za ajira kwa vijana na kuongeza uchumi na kipato kwa halimashauri hiyo.
Viewing all 110171 articles
Browse latest View live




Latest Images