Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110173 articles
Browse latest View live

UHAMIAJI YAFUNGA ‘MITAMBO’ YA UTAMBUZI KATIKA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA MWALIMU JULIUS NYERERE

$
0
0

Idara ya Uhamiaji katika Kituo cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) imefunga Vifaa vyenye mfumo mpya wa utambuzi na ulinganisho wa sura (Facial Recognition and Matching System) kwa abiria wanaoingia nchini.

Akiongea baada ya kupokea vifaa hivyo, Kamishna wa Uhamiaji anayesimamia Divisheni ya Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka Samwel Rhobby Magweiga, amesema kuwa huo ni muendelezo wa mikakati ya Idara katika kuimarisha na kuhuisha KANZIDATA ya wanaoingia nchini.

“Vifaa na mfumo huu utasaidia sana katika kukusanya taarifa za abiria wote wanaoingia nchini kupitia hapa (JNIA), kama mlivyofahamishwa, mfumo huu unachukua sura ya mtu na kulinganisha na sura nyingine zilizomo kwenye kanzidata ili kuhakikisha taarifa zilizo kwenye pasipoti yake ni za pekee na hakuna mtu mwenye sura kama yake au mtu mwenye sura ingine kuwa na taarifa kama zake.”Alieleza Kamishna Samwel Magweiga.

Awali wakati akabidhiana vifaa hivyo, Mwakilishi mkazi wa Shirika la Uhamiaji la Kimataifa (IOM) Dr. Qasim Sufi alisema kwamba IOM itashirikiana na Idara ya Uhamiaji katika suala zima la udhibiti wa uingiaji na utokaji wa raia na wageni.

Idara ya Uhamiaji kwa kushirikiana na shirika hilo, wamefunga vifaa vingine vyenye mfumo huo kwenye vituo vya Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro (KIA) pamoja na mpaka wa Holili kwa pande zote mbili za Tanzania na Kenya.

Kupitia ushirikiano huo na IOM, Idara ya Uhamiaji itaendelea kuimarisha maeneo yote ya mipaka kwa kufunga vifaa na mfumo huu wa kisasa zaidi kutumiwa hapa Afrika Mashariki.
Dr. Qasim Sufi Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji akifanyiwa majaribio katika mfumo wa utambuzi wa sura (Facial Recognition and matching system) katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam
Kamishna wa Uhamiaji (Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka) Samwl Magweiga (wa kwanza kulia) akisikiliza kwa makini namna mfumo huo unavyofanya kazi wakati wa ufungaji wa vifaa vyenye mfumo huo.
Kamishna wa Uhamiaji (Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka) akikabidhiwa nyaraka za mfumo huo na Mwakilishi Mkazi wa IOM Dr. Qasim Sufi mara baada ya ufungaji wa vifaa hivyo.

USAJILI VITAMBULISHO VYA TAIFA WAENDELEA MBEYA

$
0
0
Mamlaka ya Vitambuisho vya Taifa (NIDA) inaendelea na zoezi la Usajili na Utambuzi wa watu mkoani Mbeya ambapo wananchi wengi wamejitokeza ambapo kwa sasa usajili unaoendelea niwa mkupuo (mass registration) ambapo wananchi wanakusanyika kwenye mitaa na vijiji wanakoishi kusajiliwa ambapo Usajili huo unahusisha ujazaji fomu, uchukuaji alama za vidole picha na saini ya kielektroniki. 

Akitoa elimu kwa umma kuhusu taratibu za Usajili mwakilishi wa kitengo cha Mawasiliano NIDA Bw. Deodatus Alexander Mchaki amesema zoezi hilo ni fursa ya kipekee kwa wananchi kutambuliwa na kusajiliwa.

Amesisitiza zoezi la usajili ni Bure na wananchi hawatakiwa kutozwa gharama zozote Ili kusajiliwa mwananchi ni lazima afike na nakala (photocopy) ya nyaraka/viambatisho vifuatavyo kuthibitisha Umri, Uraia na Makazi yake ikiwemo cheti cha kuzaliwa, Passport (Pasi ya kusafiria), Kadi ya kupigia kura, leseni ya udereva, ID ya Mzanzibar mkazi, TIN, Pasi ya kusafiria na vyeti vya elimu.
Wananchi wa Kata ya Mwakidete mtaa wa Mwakidete mkoani Mbeya wakiendelea na Usajili Vitambulisho vya Taifa.
Mmoja wa wananchi wa Mtaa wa Mwakidete akiweka saini kwenye mashine maalumu ya uchukuliaji alama za kibaiolojia, picha na saini ya kielektroniki.
Wanaoonekana kwenye picha ni Baadhi ya Maafisa Usajili wa NIDA wakiendelea na zoezi la kuwasajili wananchi wa Kata ya Mwakidete mkoani Mbeya. Kushoto ni Afisa Usajili Wilaya ya Mbeya Bi. Alavuya Ntalimwa akitabasamu jambo na wananchi wa Mtaa wa Mwakidete.
Mwananchi akichukuliwa alama za Vidole na afisa Usajili wa NIDA wakati zoezi la kuwasajili wanannchi likiendelea. 
Msururu wa wananchi wa Mtaa wa Mwakidete wakisubiri huduma ya usajili.

UJENZI MAGOMENI KOTA KUKAMILIKA MACHI MWAKANI

$
0
0

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mheshimiwa Elias Kwandikwa (Mb), ameutaka Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), kufanya kazi kwa bidii katika miradi yote inayopewa na Serikali ili kuhakikisha inakamilika kwa wakati na ubora unaotakiwa.

Akikagua hatua zilizofikiwa katika mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni kota, Naibu Waziri Kwandikwa, amesema kuwa Serikali itaendelea kuanisha miradi mingine ili kuhakikisha fedha za Serikali zinaokolewa na kusimamiwa kwa uzalendo.

“Hakikisheni mnafanya kazi zenu kwa weledi, uzalendo na kukamilisha miradi kwa wakati na kuokoa fedha ambazo zitatumika katika utekelezaji wa miradi mingine hapa nchini”, amesisitiza Mhe. Kwandikwa.

Ametoa wito kwa wataalamu wengine kuja kupata mafunzo kwa TBA ambao ni chachu ya utekelezaji wa miradi mingi hapa nchini kwa kuwa wanatumia mfumo wa kisayansi na mitambo yenye kusaidia kupunguza gharama za ujenzi.

Aidha, Naibu Waziri huyo ameushukuru uongozi wa TBA kwa kutoa ajira za vibarua takribani 200 kwa siku katika mradi huo na kuwataka wafanyakazi hao kuwa waadilifu na waaminifu ili kuwa na sifa za kupata ajira za kudumu.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Mhe. Elias Kwandikwa (katikati), akitoa maelekezo kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Msanifu Majengo Elius Mwakalinga (kulia) wakati akikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es Salaam.
Muonekano wa mtambo wa kuchakata zege unaotumiwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), katika mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Mhe. Elias Kwandikwa, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota, jijini Dar es Salaam.
Muonekano wa baadhi ya vitalu vya makazi eneo la Magomeni Kota zinazojengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 35.

MAGAZETI YA JUMANNE LEO NOVEMBA 21,2017

Mama Salma Kikwete ashiriki ufunguzi wa mkutano "First Silk Road NGO Corporation Network Forum" mjini Beijing nchini China.

$
0
0
 
 Mmoja wa wadau akizungumza kwenye mkutano huo wa "First Silk Road NGO Corporation Network Forum" ulioanza kufanyika leo Beijing nchini China,ambapo Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne na Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA Mhe. Mama Salma Kikwete (MB),ameshiriki
 Washiriki wa mkutano "First Silk Road NGO Corporation Network Forum" wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ndani ya ukumbi huo.
Pichani kulia ni  Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne na Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA Mhe. Mama Salma Kikwete (MB), pamoja na washiriki wengine wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa katika mkutano huo "First Silk Road NGO Corporation Network Forum" uliofunguliwa leo mjini Beijing nchini China.
Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne na Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA Mhe. Mama Salma Kikwete (MB), akiwa katika picha ya pamoja na mshiriki mwenza wa mkutano wa "First Silk Road NGO Corporation Network Forum" uliofunguliwa leo mjini Beijing nchini China.

DC HANDENI ATOA SIKU 14 WATAALAMU WA ARDHI KUAINISHA MPAKA UNAOTENGANISHA HALMASHAURI YA WILAYA NA MJI KATA YA MISIMA.

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe amewapa siku 14 wataalamu wa ardhi wa Wilaya kuainisha mipaka baina ya Kata ya Misima iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Handeni na Halmashauri ya Mji ili kuondoa mkanganyiko wa mpaka uliodumu kwa muda mrefu. 

Mkuu wa Wilaya ameyazungumza hayo jana alipokuwa kwenye mkutano wa Hadhara uliofanyika kwenye Kijiji cha Msomera Kata ya Misima baada ya uongozi wa Kijiji hicho kuomba msaada wa kusikilizwa ili kuainishiwa mipaka baina ya Kata na Vijiji ili kuondoa muingiliano.

Mh. Gondwe alisema kuwa wataalamuwa ardhi watapima na kuonesha mipaka baina ya Halmashauri ya Mji na Wilaya ili wafahamu mipaka yao na kutambua wanapaswa kuitika wapi na kuondoa migongano inayokwamisha wananchi kushiriki katika maendeleo.

Alisema kuwa Msomera ni Kijiji kilichoanzishwa kisheria na kipo kwenye mpango wa matumizi bora ya ardhi hivyo wananchi wote wanapaswa kuheshimu na kufuata taratibu zilizowekwa kwa mujibu wa sheria na kuwataka wananchi wote wanaokuja kwenye Kijiji hicho na maeneo mengine kufuata masharti ya maeneo husika kwani Tanazania ni huru kuishi kwa kila mwananchi isipokuwa kwa kufuata taratibu zilizowekwa. 
 Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe akizungumza na wafugaji   wa Kijiji cha Msomera na akiwasisitiza kuwa Kuwa Kijiji hicho ni cha wafugaji wote bila kujali kabila.
 Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw.William Makufwe akiwaeleza wafugaji wa Kijiji cha Msomera kuwa  wakulima kuingia kwenye eneo la kufugia mifugo kunatokana na baadhi ya viongozi kutokuwa waadilifu kwa kuuza maeneo bila kufuata taratibu na kuwataka kushirikisha wananchi kwa kila jambo kwani viongozi sio watu wenye maamuzi ya mwisho.
Baadhi ya wafugaji na wakulima walioshiriki mkutano wa hadhara.
 mmoja wa wafugaji akitoa malalamiko yake kuhusu wakulima kuvamia eneo la mifugo na kuanza kulima kinyume na taratibu na kuomba kuanishiwa mipaka kuepuka muingiliano.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

TAARIFA KWA UMMA

BODI YA PAMBA TANZANIA YATAKIWA KUONGEZA MBEGU MKOANI TABORA

$
0
0
NA TIGANYA VINCENT.

UONGOZI wa Bodi ya Pamba Tanzania umeombwa kuongeza tani 148 ya mbegu za zao hilo baada ya wakazi wengi wa Mkoa wa Tabora kujitokeza kwa ajili ya kulima zao hilo katika msimu wa mwa 2017/18. Ombi hilo limetolea jana katika kijiji cha Mwanasimba Wilayani Igunga na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati wa uzinduzi wa msimu ujao wa kilimo cha pamba nchini.

Alisema kuwa baada ya zoezi la uhamasishaji wa kufanyika katika vijiji mbalimbali kwenye Wilaya za Igunga, Uyui, Urambo, Nzega na Kaliua watu wamehamasika na kujitokeza kulima zao hilo na kusababisha upungufu wa mbegu kutoka walizokisia za awali. Mwanri alisema kuwa kabla ya zoezi hilo kulikuwa na mahitaji ya tani 672.57 lakini baada ya kuendesha zoezi hilo idadi ya wanaohitaji mbegu imeongezeka na kufikia mahitaji ya tani 820.12 wakati hadi hivi sasa wamepokea tani 672.03. Alisema kuwa Tabora ndio imechaguliwa kuwa mzalishaji wa mbegu za pamba na kitalu cha taifa  kwa ajili ya maeneo mengine nchini na kwa hiyo mbegu pekee itakayopandwa ni UKM08.

Mwanri alitoa wito kwa uongozi wa Bodi hiyo kuhakikisha kuwa upungufu wa mbegu hizo unaondolewa na zinawafikia wakulima mapema kwa sababu mvua zikishaanza kunyesha kuna baadhi ya maeneo hapa mkoani ni vigumu kufikika. Kwa upande wa Bodi ya Pamba Tanzania (TCB), Mkurugenzi wa Bodi hiyo Marco Mtunga alisema kuwa katika msimu ujao wa kilimo jumla ya tani 25,000 za mbegu zimetengwa kwa ajili ya wakulima ambapo 11,548 ni aina ya UKM08 na tani 13,452 ni UK91.

Alisema kuwa kwa upande wa Mkoa wa Tabora ikiwa ndio imechaguliwa kuwa kitalu cha taifa cha mbegu aina iliyosambazwa kwa ajili ya kulimwa katika msimu huu ni UKM08 ikiwa ni maandalizi ya mbegu kwa ajili ya maeneo mengine kwa Msimu wa 2018/19. Mkurugenzi Mkuu huyo alisisitiza kuwa baada ya hapo ni mbegu hiyo itakayolimwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini. Aidha Mtunga aliongeza kuwa jumla ya ekari milioni moja na laki tatu zinatarajiwa kupandwa pamba msimu ujao wa kilimo katika mikoa 16 inayolima zao hilo hapa nchini.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Igunga John Mwaipopo alisema kuwa tayari wameshapokea tani 500 za mbegu za pamba ambapo wameshazishambaza katika maeneo yote  yanayolima zao hilo. Alisema kuwa tayari viongozi mbalimbali wanaendelea kutoa elimu kwa wakulima ili waweze kuzalisha kulinga na sharia na kanuni za kilimo hicho kwa ajili ya kulinda heshima ya Wilaya ya Igunga kuwa kitalu cha Taifa.

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI, MHE. JAPHET HASUNGA AKABIDHI MSAADA WA MABATI KWA SHULE YA MSINGI ILIYOATHIRIKA NA KIMBUNGA MKOANI IRINGA

$
0
0
Na Hamza Temba - WMU

Katika jiihada za Serikali za kuendeleza ushirikiano na jamii zinazozunguka maeneo ya hifadhi nchini, Wizara ya Maliasili na Utalii imetoa msaada wa mabati sitini kwa ajili ya kuezeka madarasa ya shule ya msingi Kipanga baada ya kuezuliwa na kimbunga hivi karibuni katika kijiji cha Ubwachana Wilaya ya Iringa mkoani Iringa.

Msaada huo umetolewa jana na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga alipotembelea kituo cha Malikale cha Isimila mkoani humo ambacho kinapakana na shule hiyo wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja Mkoani humo.

Akikabidhi mabati hayo, Naibu Waziri Hasunga alisema Serikali inatambua mchango wa wananchi wanaoishi jirani na maeneo ya hifadhi kwenye uhifadhi shirikishi hivyo ni jukumu la Serikali kuwaunga mkono pale wanapopatwa na majanga ya aina mbalimbali.

Aidha, aliwataka baadhi ya wananchi wanaochimba mchanga kwenye maeneo ya vivutio katika kituo hicho waache mara moja kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria kwakuwa wanahatarisha uhai wa kingo za miamba ya kale ambayo na kivutio kikubwa cha utalii wa asili katika ukanda wa kusini.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela wakitwanga Kinu wakati wa ziara yake katika Makumbusho ya Utamaduni wa Mkoa wa Iringa (Boma) jana Mkoani humo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (wa tatu kushoto) akimkabidhi Mwenyekiti wa Kijiji cha Ubwachana, Donatus Lihoha mabati 60 kwa ajili ya kuezeka vyumba vya madarasa vya shule ya msingi Kipanga ambayo iliezuliwa na kimbunga hivi karibuni ikiwa ni kutambua mchango wa wananchi katika uhifadhi shirikishi wa Kituo cha Mali Kale cha Isimila jana Mkoani Iringa.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wa pili kushoto) akimsikiliza Mhadhiri wa Chuo Kikuu Iringa, Jimson Sanga ambaye pia ni Meneja Msaidizi wa Mradi wa Fahari Yetu unaojishughulisha na Uhuishaji, Uendelezaji na Utangazaji wa utalii Nyanda za Juu Kusini kuhusu Makumbusho ya Utamaduni wa Mkoa wa Iringa (Boma) wakati wa ziara yake jana Mkoani humo. Anayeshuhudia ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela (wa tatu kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Kale wa Wizara hiyo Digna Tillya.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia) akimsikiliza Mhadhiri wa Chuo Kikuu Iringa, Jimson Sanga ambaye pia ni Meneja Msaidizi wa Mradi wa Fahari Yetu unaojishughulisha na Uhuishaji, Uendelezaji na Utangazaji wa utalii Nyanda za Juu Kusini wakati akitoa maelezo kuhusu Makumbusho ya Utamaduni wa Mkoa wa Iringa (Boma) wakati wa ziara yake jana Mkoani humo. Anayeshuhudia ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela (kulia kwake).
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia) akizungumza na watumishi wa Makumbusho ya Utamaduni wa Mkoa wa Iringa (Boma) alipotembelea Makumbusho hiyo jana wilayani Iringa.

MBUNGE MGAYA AWASAIDIA WANAWAKE VYEREHANI 370 NJOMBE

$
0
0
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Njombe, Neema Mgaya ametoa msaada wa vyerehani 370 vyenye thamani zaidi ya Milioni 90 kwa wanawake mkoani humo ili wajikwamue kiuchumi huku akiunga mkono juhudi za Serikali inayohimiza uchumi wa viwanda. Akizungumza Mjini Makambako wakati wa hafla ya kukabidhi vyerehani hivyo kwa baadhi ya wanawake, Mgaya amesema amefikia uamuzi huo ili kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuifanya Tanzania kuwa taifa la uchumi wa kati kupitia viwanda. Akibainisha zaidi ameeleza juhudi za kumkomboa mwanamke wa mkoa wa Njombe ni jambo linalopiganiwa kwa miaka mingi hivyo vyerehani hivyo vitawafungulia njia kuweza kujikwamua kiuchumi.

“Nimekuwa sina papara katika utendaji wangu, mwaka jana nilitoa msaada wa vitabu vya ziada kwa Shule za Sekondari Halmashauri ya Makambako, ambapo kwa mwaka huu nimeamua kuunga mkono juhudi za serikali upande wa viwanda kwa kuwasadia wanawake hawa vyerehani hivi 370,” alisema Mgaya.

Akifafanua amesema anatambua thamani kubwa walionayo wanawake hivyo kwa kuwawezesha vyerehani hivyo kutainua familia na jamii zinazowazunguka kwani fedha zitakazopatikana zitasaidia huduma za kijamii na mahitaji mengine.

“Mtu ninayemthamini huwa nampa kitu ambacho kitadumu na kumsaidia kwa muda mrefu, mimi nimeamua kutowapa samaki kwani mtamla ataisha, nimewapa nyavu ambayo mtaitumia kuvua samaki, nendeni mkavitunze vyerehani hivi kujiletea maendeleo endelevu,” alisema Mgaya.

Akizungumza baada ya kupokea cherehani yake Diwani wa Viti Maalum Lupembe Neema Limbanga amesema alilolifanya Mbunge huyo wa Viti Maalum halijawahi kutokea katika maisha yake na kwamba vyerehani hivyo vimewafungulia njia kimaisha.

Naye Diwani wa Viti Maalum CCM Njombe, Stella Francis amesema Mgaya amewapa zawadi ambayo licha ya kuwainua kiuchumi itakuwa mkombozi hasa katika ndoa zao, kwani sasa wataweza kuhudumia familia kwa kushirikiana na wanaume zao.

Kutolewa kwa vyerehani hivyo 370 ambavyo ni sawa na viwanda vidogo 92 kwa dhana ya vyerehani vinne sawa na kiwanda kimoja kidogo kunaufanya mkoa wa Njombe kuitikia vilivyo wito wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuhamasisha uchumi wa viwanda. Lengo la Mkoa kupitia wanawake ni kuwa na viwanda vidogo 35 hivyo kwa vyerehani  370 ambavyo Neema amevitoa ni kwamba lengo la kimkoa kupitia wanawake limeshafikiwa.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Njombe Neema Mgaya (katikati mstari wa mbele) akiwa na baadhi ya wanawake aliowakabidhi vyerehani 370 vyenye thamani zaidi ya Shilingi Milioni 90 Halmashauri ya Makambako Mkoani Njombe ili wajikwamue kiuchumi.
Mbunge wa Viti Maalum CCM mkoa wa Njombe, Neema Mgaya (mbele) akiwa na baadhi ya wanawake aliowakabidhi vyerehani 370 vyenye thamani zaidi ya Shilingi Milioni 90 Halmashauri ya Makambako Mkoani Njombe ili wajikwamue kiuchumi.
Baadhi ya vyerehani 370 vyenye thamani zaidi ya Shilingi Milioni 90 vilivyolewa na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Njombe, Neema Mgaya vikiwa tayari kukabidhiwa kwa baadhi ya wanawake wa Mkoa wa Njombe ili wajikwamue kiuchumi.

BALOZI JENSEN WA DENMARK AWAHASA WAPIGA PICHA NCHINI

$
0
0
Balozi wa Denmark nchini Mh Einar H. Jensen akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa onesho la KARIBU TANZANIA , kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Prof Audax Mabula na kushoto ni mpigapicha mkongwe Bw Jesper Kirknaes.
Balozi wa Denmark Mh Einar H. Jensen akipata maelezo ya picha za kihistoria kutoka kwa mpiga picha hizo Bw Jesper Kirknaes kwenye onesho la KATIBU TANZANIA lililopo Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam.

Na SIXMUND BEGASHE

Wapiga picha nchini wameshauriwa kutembelea onesho la picha zinazo elezea historia ya maisha ya watanzania Miaka 50 iliyopita ili kujifunza umuhimu wa uhifadhi wa kumbukumbu muhimu za kihistoria ili vizazi vilivyopo na vijavyo viweze kujifunza kwa kuwa Tanzania ya leo sivyo itakavyo kuwa miaka 50 ijayo.

Ushauri huo umetolewa na Balozi wa Denmark Mh Einar H. Jensen kwenye ufunguzi wa onesho maalum la picha zilizo sheheni uridhi wa kihitoria ya maisha ya watanzania miaka 50 iyopita lijulikanalo kama KARIBU TANZANIA lililopo Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam, ambali limeandaliwa na Makumbusho ya Taifa kwa kushirikiana na mpiga picha hizo Bw Jesper Kirknaes

“Picha hizi sasa zimerudi nyumbani Tanzania, baada ya kuwa kwenye nchi za Denmark na Sweden ampapo zilioneshwa huko, niimani yangu kuwa zitakuwa ni mchango mkubwa na muhimu sana kwa Makumbusho ya Taifa, zitatoa nafasi kwa watu kujifunza historia ya maisha ya watanzania na pia zitakuwa ni ushawishi kwa wapigapicha wa hapa Tanzania kuona umuhimu wa kutunza kumbukumbu kwa kupitia picha”. Aliongeza Balozi Jensen

Balozi Jensen alimalizia kwa kuipongeza Makumbusho ya Taifa kwa kazi nzuri ya uhifadhi Uriridhi wa Utamaduni wa Mtanzania, kutumia vyema miundo mbinu na hata kushirikisha wadau katika shughuli za kiutafiti na uwekaji wa maonesho kama ilivyo fanya kwenye onesho la KARIBU TANZANIA.

Akizungumzia onesho hiyo mpigaji wa picha hizo Bw Jesper Kirknaes ameeleza kuwa onesho la KARIBU TANZANIA linaelezea maisha ya watanzania miaka zaidi ya 50 iliyopita, namna walivyo kuwa wakifanya kazi pamoja, walivyo kuwa wakivaa, wakila, na hata kufanya mambo mengine yakimaendeleo kwa ajili ya familia yake na nchi kwa ujumla.

Licha ya kuushukuru Ubalozi wa Denmark nchini kwa kulifadhili onesho hilo, Mkurugenzi wa Makumbusho ya Taifa Prof Audax Mabula ametoa wito kwa watanzania hasa vijana kutembelea Makumbusho kwa lengo la kujionea onesho hilo ili waweze kujifunza historia ya maisha ya watanzania, namna walivyo kuwa wabunifu katika kuanzaisha viwanda.

“Serikali ya awamu ya tano nchini chini ya Rais wetu John Pombe Magufuli, inatupeleka katika uchumi wa kati kwa kuifanya Tanzania iwe ni nchi ya viwanda ifikapo 2020, hivyo si vyema watanzania hasa vijana waka kaa tu bila kujishughulisha kama walivyo jishughulisha watanzania huko nyuma na kuweza kuwa na viwanda vidogo vidogo na hata vikubwa, niimani yangu kuwa onesho hili litarudisha hari kwa vijana ili wawe sehemu ya maendeleo hapa nchini”. Alimaliza Prof Mabula.

Naibu Waziri Ulega akutana na wananchi wa kijiji cha Sunguvuni

$
0
0

 Naibu wa Waziri na Uvuvi, Abdallah Ulega akipokea taarifa ya ujenzi wa Zahanati ya Sunguvuni mkoani Pwani.


Na Chalila Kibuda,Globu ya jamii.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega  amesema miundombinu ya barabara za vijiji ikijengwa itafanya vijiji kuinuka kiuchumi.

Ulega aliyasema hayo wakati alipokutana na wananchi wa kijiji cha Singuvuni kata Mkuranga  wilayani Mkuranga, kuwa taasisi ya barabara za vijijini na Mijini Tarura ni suluhisho kwa barabara za vijijini.

Amesema kuwa wananchi wa sunguvuni wanachangamoto ya barabara ambapo changamoto hiyo itatatuliwa na Tarura katika wilaya ya Mkuranga na hatimaye wananchi wataweza kuinuka kiuchumi kutokana na miundombinu hiyo.

Katika ziara hiyo ametoa mifuko 50 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya Sunguvuni pamoja na kuahidi mifuko 20 ya Saruji ili ujenzi huo uende kwa kasi

Aidha amesema kuwa wanachi Sunguvuni wafanye kazi kwa ajili ya kujiletea maendeleo kutokana na kuwa na ardhi yenye Rutuba.

Meneja wa Tarura wilaya ya Mkuranga,Peter Shirima amesema wameshatenga milioni 18 kwa ajili ya kushughulikia sehemu korofi na amesema barabara zote wameshazipitia na kilichobaki ni utekelezaji.
 Naibu Waziri wa Uvuvi na Mifugo ,Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa Sunguvuni mkoani Pwani.
 Meneja wa Tarura,Peter Shirima akitoa ufafanuzi wa ujenzi wa barabara.
 Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mkuranga, Ally Msikamo akizungumza juu ilani ya CCM na wananchi wa Sunguvuni mkoani Pwani.Picha zote na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii
 Wananchi wa unguvuni mkoani Pwani  wakimsikiliza  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega
Muonekano wa jengo la  Zahanati ya Sunguvuni mkoani Pwani.


NEWZ ALERT: JENGO LA CLOUDS MEDIA GROUP LAWAKA MOTO MAPEMA LEO.

$
0
0
 Magari ya ya Jeshi la zimamoto yakiwa yamefika eneo la tukio,katika jengo la Ofisi za Clouds Media Group lililopo Mikocheni jijini Dar, kukabiliana na moto uliozuka mapema leo kwenye moja chumba cha ofisi na kusababisha baadhi ya vifaa kuungua na kuharibika kabisa,aidha mpaka sasa Globu ya jamii haijaelezwa haswa chanzo cha moto ni nini.Hivyo Tunaendelea kufuatilia na kupata taarifa kamili.
 Sehemu ya jengo la Ofisi za Clouds Media Group kama lionekanavyo pichani huku shughuli za uzimaji moto huo ukiendelea .
  Mmoja wa Askari wa jeshi la Zimamoto  akiendelea kuudhibiti  moto uliokuwa umezuka ndani ya moja ya Ofisi za jengo hilo
 Baadhi ya Wafanyakazi wa Clouds Media Group pamoja na baadhi ya ndugu jamaa na marafiki wa Clouds wakiwa nje ya jengo hilo wakifuatilia tukio la uzimaji moto uliozuka katika jengo hilo mapema leo,Mikocheni jijini Dar.


Introducing "Hauna" Official Video by Aslay Isiaka

Airtel Money kugawa gawio la bilioni 2 kwa wateja

$
0
0
Wakati msimu wa sikukuu ya krismasi umewadia kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imeupokea msimu huo kwa kuendelea kuwanufaisha wateja pamoja na mawakala wa huduma ya Airtel Money nchi nzima kwa kuwagawia gawio la shilingi bilioni 2 kutokana na utumia wao wa huduma ya Airtel Money .Taarifa ilitolewa na kampuni hiyo leo ikiwa na kauli ya Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Bw, Sunil Colaso imethibitisha kuwa,

Gawio la faida kutokana na huduma ya Airtel Money hutolewa katika kila robo ya mwaka ambapo gawio la awali lilianza kutolewa Mwaka 2015, hadi kufikia leo hii jumla ya shilingi bilioni 11.8 zimeshagawiwa kwa wateja wa Airtel Money. Kila mteja wa Airtel Money hupata sehemu ya gawio hilo kulingana na salio linalosalia katika akaunti yake ya Airtel Money kila siku.

“Tunapoingia katika shamrashamra za msimu wa sikukuu, Airtel tunatambua umuhimu wa kuwazawadia wateja wetu. katika msimu au wakati kama huu watu wengi hupanga ratiba za jinsi watakavyosherehekea kwa kupeana zawadi wakiwa na familia zao, tunafurahia kuona tuko katika wakati sahihi kwa kutoa gawio hili ili kutoa fursa kwa wateja wetu kuweza kutumia wakiwa na familia au wawapendao kwa kujipatia mahitaji yao muhimu ndani ya msimu wa sikukuu”.

Gawio hili la Airtel Money linaloaanza kutolewa leo linalotokana na faida iliyopatiikana kuanzia ya robo mwaka kuanzia mwezi Juni hadi Septemba 2017, ambapo watakaofaidika ni wateja wote wanaotumia huduma ya Airtel Money pamoja na mawakala wake nchini nzima. Tunajisikia furaha sana kugawa gawio hili ambapo kila mteja wa Airtel Money tapata na kisha mteja mweyewe ataamua kuitumia pesa yake atakavyo iwe kununua bando, muda wa maonge, kulipia LUKU au kufanya malipo ya bili za huduma mbalimbali” ilieleza taarifa hiyo

Airtel Tanzania itaenendelea na utekelezaji wa dhamira yake ya kutoa huduma za kifedha bora kwa njia ya mtandao ili kuongeza tija kwa watumiaji , unafuu na usalama wakati wowote. Huduma ya Airtel Money imekuwa na kuongeza watumiaji kutokana kuwa na umuhimu zaidi kwa wateja. Tunapenda kuwashauri wateja wa Airtel wot kutumia huduma hii ya Airtel Money kwa kukamilisha au kutimiza baadhi ya mahitaji yao ya huduma za kifedha ili kuwa sehemu ya gawio kama hili linayotolewa sasa” ilieleza taarifa hiyo.

Mkurugenzi wa Mawasiliano Kampuni ya Airtel Tanzania, Beatrice Singano, akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam kuhusu mgao wa gawio la faida la bilioni 2 kwa wateja na watumiaji wa huduma ya Airtel Money. Kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni hiyo, Isack Nchunda.
Kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Isack Nchunda, akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam kuhusu gawio la bilioni 2 kwa wateja na watumiaji wa huduma ya Airtel Money. Kulia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano Kampuni ya Airtel Tanzania, Beatrice Singano.

NAIBU WAZIRI,KAMISHNA JENERALI WA UHAMIAJI WAZUNGUMZA NA WANANCHI

$
0
0
Na Abubakari Akida-WMNN.

NAIBU Waziri Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, amewataka wananchi na wafanyabiashara wanaofanya shughuli zao karibu na Kituo cha Mpaka wa Sirari unaotenganisha nchi za Tanzania na Kenya kuhakikisha wanashirikiana na Jeshi la Polisi mkoani Mara kudhibiti matukio ya uhalifu kwa kutoa taarifa za wahalifu hao kwa jeshi hilo.

Hayo ameyasema akiongea na wananchi wakati wa ziara ya kikazi katika mkoa wa Mara, ikiwa na lengo la kutembelea mipaka iliyopo katika mkoa huo inayotenganisha nchi ya Tanzania na nchi jirani za Kenya na Uganda ambapo katika ziara hiyo aliongozana na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dk. Anna Makakala, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Uzalishaji Vitambulisho vya Taifa, Alphonce Malibiche na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama.

“Tumekuwa tukipata taarifa wananchi wa hapa kushirikiana na wahalifu katika kupitisha mali za magendo hapa hasa wakitumia vijana wanaoendesha bodaboda kupitisha mizigo yao na kuripotiwa matukio mbalimbali yanayohatarisha usalama wa raia wetu, natoa wito kwa wananchi wa hapa kushirkiana na jeshi la polisi kudhibiti matendo hayo ya kihalifu,” alisema Masauni

Aidha,Naibu Waziri Masauni amewataka wananchi hao kuacha mara moja tabia inayokua kwa kasi katika eneo hilo ya kulizuia Jeshi la Polisi kufanya shughuli zake na endapo atabainika mtu yoyote atakumbana na mkono wa sheria huku akitoa ushauri kwa jeshi kuzifanyia utafiti taarifa zitakazoletwa ili kuepuka kumuonea mtu.
Naibu Waziri Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na wananchi wanaofanya shughuli zao katika Mpaka wa Tanzania na Kenya Sirari , wakati wa ziara ya kikazi aliombatana na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala(watatu kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa huo.Lengo la ziara hiyo ni kukagua shughuli mbalimbali zilizopo chini ya idara za wizara na kukagua mipaka iliyopo katika mkoa huo.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala, akizungumza na wananchi wanaofanya shughuli zao katika Mpaka wa Tanzania na Kenya Sirari, wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima, akijibu baadhi ya hoja zilizoulizwa na wananchi wanaofanya shughuli zao katika Mpaka wa Tanzania na Kenya Sirari, wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (wapili kulia), akiambata na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala (kulia) 
Naibu Waziri Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji,Dkt. Anna Makakala(wapili kulia),Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima() na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Glorius Luoga(kulia), wakisikiliza maswali ya mmoja wa wananchi wanaofanya shughuli karibu na kituo cha Mpaka wa Tanzania na Kenya Sirari , wakati wa ziara ya kikazi yenye lengo la kukagua mipaka iliyopo ndani ya mkoa huo. 

Naibu Waziri Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji,Dkt. Anna Makakala( kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima(watatu kulia) wakisikiliza maswali ya mmoja wa wananchi wanaofanya shughuli karibu na kituo cha Mpaka Tanzanua na Kenya Sirari , wakati wa ziara ya kikazi yenye lengo la kukagua mipaka iliyopo ndani ya mkoa huo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

WANACHAMA WA VYAMA VYA UPINZANI SITA WAREJEA CCM KATIKA MKUTANO WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA (NEC) WA CCM JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati akiwasili kuongoza Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama hicho jijini Dar es salaam leo November 21, 2017
 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli akifungua  Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama hicho jijini Dar es salaam leo November 21, 2017.

  Waliokuwa wanachama wa vyama vya upinzani wakiwasili ukumbuni kuomba ridhaa ya kurudi CCM wakati wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama hicho jijini Dar es salaam leo November 21, 2017

MKUU WA WILAYA YA MBOGWE AZINDUA UJENZI WA ZAHANATI YA KIJIJI CHA SHENDA

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe Mh Martha Mkupasi amezindua Ujenzi wa Zahanati ya Shenda ambayo inatarajiwa kujengwa kwa nguvu za wananchi kwa kushirikiana na serikali katika uzinduzi huo mkuu Wilaya ameshirikiana na wananchi kukamilisha zoezi la kumwaga Zege na kuendesha harambee ya kupata vifaa vya ujenzi.

Akiongea wakati wa uzinduzi huo Mkuu wa Wilaya amewataka wananchi wote kutoa ushirikiano wa nguvu kazi kwenye ujenzi wa zahanati hiyo kwani zahanati hiyo itahudumia wananchi wote wa Shenda bila ubaguzi. Mkuu wa wilaya amewasisitiza wananchi wote kuungana bila kuangalia itikadi za chama wala dini .

Pamoja na uzindinduzi huo Mkuu wa Wilaya amemwagiza Mtendaji wa Kata ya masumbwe kugawa zamu za kufanya kazi kwenye zahanati hiyo kwa vitongoji vyote vya Shenda kwani Serikali itagharamia gharama za Fundi tu kazi nyingine zote zitafanywa na wananchi wa kijiji husika ili kupunguza gharama na kwenda na kasi ya mkuu wa mkoa wa Geita inayotaka kila kijiji kumiliki Zahanati yake.

Kwa sasa wananchi wa shenda wanapata matibabu kwenye kituo cha afya Masumbwe ambacho kipo umbali wa zaidi ya kilometa mbili kitu ambacho kimekuwa kikileta changamoto kwa wakazi wa shenda zaidi wakinamama wajawazito na watoto.

Vilevile Kaimu Muhandisi wa Ujenzi bi Filomena Bango amesema Zahanati hiyo inajengwa kwa nguvu za Wananchi ambao mpaka sasa wameshafyatua matofali 300 wameshaleta mawe ya kutosha na wanaendelea kushirikia na fundi . Bi Filomena amesema wananchi watakapoishia serikali itachukua jukumu la kumalizia wananchi walipoishia. 
  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mbogwe akimwaga maji kwenye nondo zilizoandaliwa kwa ajili ya msingi wa Zahanati
 Mkuu wa Wilaya y a Mbogwe Mh Martha Mkupasi akikagua matofali yaliyofyatuliwa na wananchi kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati ya Shenda
 Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe Mh Martha Mkupasi akihutubia wananchi wa kijiji cha Shenda wakati wa uzinduzi wa waujenzi wa Zahanati ya Shenda
Wananchi wa Kijiji cha Shenda wakishirikiana na kuchanganya Zege litakalotumika kujenga zahanati ya Shenda

MWENYEKTI WA CCM RAIS DKT MAGUFULI AONGOZA MKUTANO WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA (NEC) WA CCM JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli akifungua  Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama hicho jijini Dar es salaam leo November 21, 2017
Katibu Mkuu Wizara ya Maji Profesa Kitila Mkumbo aliyepata kuwa mwanachama mwandamizi wa chama cha ACT akiomba na kukubaliwa kurudi CCM mbele ya  Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli na wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama hicho jijini Dar es salaam leo November 21, 2017
Aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Mwanachama wa CHADEMA Bw. Lawrence Masha akiomba na kukubaliwa kurudi CCM mbele ya  Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli na wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama hicho jijini Dar es salaam leo November 21, 2017
 Aliyekuwa mwanachama mwandamizi wa ACT Bi. Edna sunga  akiomba kurudi na kukaribishwa  CCM mbele ya  Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli na wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama hicho jijini Dar es salaam leo November 21, 2017
Aliyekuwa  Katibu Mkuu wa Bw. Samson Mwigamba akiomba na kukaribishwa kurudi CCM mbele ya  Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli na wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama hicho jijini Dar es salaam leo November 21, 2017
Aliyekuwa  Mshauri wa Chama cha ACT Wakili Albert Msando  akiomba na kukaribishwa kurudi CCM mbele ya  Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli na wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama hicho jijini Dar es salaam leo November 21, 2017.
Aliyekuwa  Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la CHADEMA (BAVICHA)  Bw. Patrobas Katambi  akiomba na kukaribishwa kurudi CCM mbele ya  Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli na wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama hicho jijini Dar es salaam leo November 21, 2017
 Wanachama sita wa vyma vya upinzani wakionekana aada ya kukaribishwa kurudi CCM mbele ya  Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli na wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama hicho jijini Dar es salaam leo November 21, 2017
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli akiendesha Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama hicho jijini Dar es salaam leo November 21, 2017.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Ndg. Humphrey Polepole akiwapatia mashati wanachama sita wa vyama vya baada ya kukaribishwa kurudi CCM mbele ya  Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli na wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama hicho jijini Dar es salaam leo November 21, 2017.


KESI YA UCHOCHEZI DHIDI YA YERICKO NYERERE KUANZA KUSIKILIZWA MWEZI UJAO

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii.
Upande wa mashtaka katika kesi ya uchochezi kupitia mtandao inayomkabili mfanyabiashara Yericko Nyerere umeeleza kuwa katika ushahidi wa kesi hiyo, wanatarajia kuwaita mashahidi sita na kutoa vielelezo vitatu.

Wakili wa Serikali, Clara Charwe ameeleza hayo leo Novemba 21 mwaka huu baada ya kumaliza kumsomea maelezo ya awali (PH) mshtakiwa huyo mbele ya   Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage.

Katika kesi hiyo, Nyerere anashtakiwa kwa kuchapisha 
maneno yenye nia ya uchochezi kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook.

Akisomewa maelezo hayo, Yericko alikubali maelezo yake binafsi ikiwa ni jina lake, yeye ni Mfanyabiashara na kuwa alipelekwa mahakamani na kusomewa Mashtaka na kukanusha Mashtaka yote yanayomkabili.

Yericko anadaiwa  kuwa  Mei 28, 2017 kwa nia ya kuwachochea Watanzania alichapisha maneno kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook yasemayo;

Maazimio ya Baraza Kuu yalikuwa (1) Katiba Mpya (2) Tume Huru (3) Bunge (4) Haki ya Kikatiba ya kuishi (Ben Saanane) (5) Haki ya Kikatiba ya kukutana na kuzungumza (Mikutano ya Hadhara ya Kisiasa) Hayo ndio yatahubiriwa katika Operesheni Ukuta.

Baraza Kuu limeridhia kwa kauli moja kwamba vita rasmi ya kulikomboa taifa imezinduliwa na kama wewe Mtanzania unaogopa kulitetea taifa hili ni bora uka kaa kando, nenda huko CCM ambako michemsho na supu vipo kwa wingi…kufa kwetu ni ukombozi wa Tanzania…..

Yaani sasa tunarejesha siasa za jino kwa jino, uso kwa uso, mguu kwa mguu, weka mguu ni weke ugoko… Ni mwisho kuishi kinyonge, ni mwisho kulalamika, ni mwisho watu wetu kutekwa au kuuawa, ni mwisho watu wetu kuzuiwa kufanya mikutano ya hadhara…Tunasema sasa ni single touch double manifestational.” Mwisho wa kunukuu. Yericko yupo nje kwa dhamana.
Kesi hiyo itaanza kusikilizwa Decemba 16 mwaka huu.
Viewing all 110173 articles
Browse latest View live




Latest Images