Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110088 articles
Browse latest View live

Mkurugenzi Mkazi wa USAID bwana Andy Karas atembelea walengwa wa TASAF mkoani Iringa.

$
0
0
Na Estom Sanga – Iringa 

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Misaada ya Kimataifa la Marekani –USAID-bwana Andy Karas amepongeza jitihada za serikali ya Tanzania kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF katika kuwafikia wananchi wanaokabiliwa na umasikini kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini ambao umeanza kuonyesha mafanikio makubwa katika maeneo mbalimbali nchini, jambo linalovutia wadau wa maendeleo kuendelea kusaidia jitihada hizo. 

Bwana Karas ameyasema hayo alipokutana na Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Igingilanyi kata ya Nduli katika halmashauri ya Wilaya ya Iringa ,mkoani Iringa ambako licha ya kuelezwa namna TASAF inavyoendelea kutekeleza Mpango huo, lakini pia alishuhudia namna walengwa wa mpango huo walivyoboresha maisha yao kwa kutumia fedha za ruzuku za mfuko huo. 

Amesema hamasa inayoonyeshwa na Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kujiletea maendeleo kwa kuanzisha miradi midogo midogo kwa kutumia fedha zinazotolewa na Serikali kupitia TASAF, imelivutia Shirika hilo na kuahidi kuwa litaendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania katika kuboresha utaratibu wa kuwainua wananchi kiuchumi . 

Bwana Karas amesema utaratibu wa kuwafikia na kuwasaidia moja kwa moja wananchi wanaoishi katika mazingira magumu ya kiuchumi umekuwa ukitumika katika nchi nyingi duniani na umeonyesha mafanikio makubwa kwa kusisimua shughuli za kiuchumi na kijamii kwa kaya masikini . 

Aidha Mkurugenzi Mkazi huyo wa USAID amevutiwa na masharti ya Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini kupitia TASAF hususani katika nyanja za elimu, afya, lishe na uwekezaji kwenye shughuli za kiuchumi kwa walengwa wa Mpango huo kuwa umeamusha ari ya kutokomeza umasikini miongoni mwao. 
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Misaada la Marekani USAID bwana Andy Karas akipokea zawadi ya kuku kutoka kwa mmoja wa walengwa wa Mpango wa kunusuru Kaya Masikini unaoratibiwa na TASAF katika kijiji cha Igingilanyi wilaya ya Iringa Vijijini ambako akutana na walengwa wa Mpango huo kuona namna wanavyonufaika na Mpango huo.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Misaada la Marekani nchini USAID bwana Andy Karas akisoma taarifa kwenye mkutano wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Igingilanyi kata ya Nduli wilaya ya Iringa Vijijini ambako alitembelea kuona namna walengwa wa Mpango huo wanavyonufaika na ruzuku inayotolewa na serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF.
Baadhi ya Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Igingilanyi wilaya ya Iringa Vijijini wakiwaburudisha wageni kutoka Shirika la Misaada la Marekani –USAID waliotembelea kijiji hicho kuona shughuli za Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaoratibiwa na TASAF .
Mkurugenzi mkazi wa Shirika la Misaada la Marekani Bwana Andy Karas akisalimiana na mmoja wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Igingilanyi kata ya Nduli wilaya ya Iringa Vijijini wakati alipotembelea kijiji hicho.Katikati yao ni Mkurugenzi wa miradi wa TASAF bwana Amadeus Kamagenge.


VODASTAR YAICHAKAZA NOKIA MAGOLI 8-1 MECHI YA KIRAFIKI

$
0
0
 Mashabiki watimu ya VodaStar, wakifurahia kombe lao  baada ya timu yao kiichakaza timu ya Nokia kwa magoli 8-1 wakati wamchezo wakirafiki uliofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Ferrao (kushoto) akimshuhudia Mkurugenzi wa Nokia Tanzania,Martin Talbot ( kulia) akimvisha medali nahodha wa timu ya VodaStar, Ngayama Matongo baada ya kuilaza timu hiyo kwa magoli 8-1 wakati wa mechi yakirafiki  uliofanyika katika  viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
 Mshambuliaji wa timu ya  VodaStar, Ian Ferrao ambaye pia ni Mkurugenzi mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, (kushoto) akipongezwa na Mkurugenzi mtendaji wa Nokia Tanzania, Martin Talbot  kwa kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo  wakati wa mchezo wa kirafiki kati ya kampuni hizo ambapo VodaStar iliichapa Nokia kwa magoli 8-1 mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Nahodha wa timu ya Nokia Tanzania,Charles Domingos(kulia) akiachia shuti kali na kuifungia goli timu yake na lapekee wakati wa mechi yakirafiki iliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam kati ya timu yake na VodaStar ambapo VodaStar waliichakaza timu hiyo kwa magoli 8-1.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

WAZIRI UMMY AWATAKA WAGANGA WAKUU WA MIKOA KUANZISHA ZOEZI LA WAZI LA UCHUNGUZI WA SARATANI YA KIZAZI KWA WANAWAKE

$
0
0
NA WAMJW-DAR ES SALAAM.

WAZIRI Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu amewaelekeza waganga wakuu wa mikoa yote nchini kuanzisha zoezi la wazi la uchunguzi wa saratani ya kizazi angalau mara moja katika mwezi ili kusaidia kutokomeza tatizo kwa wanawake hilo nchini.

Hayo amesema wakati wa kupokea vifaa vya kuchunguza saratani vyenye thamani ya shilingi milioni 98  ambavyo vimetolewa na Taasisi isiyo ya Kiserikali ya JHPIEGO kwa kushirikiana na USAID ili kusaidia kupambana na tatizo hilo nchini.

“Angalau ifikapo Desemba 2018 nataka  vituo vya Afya vya Serikali  524  viwe vinatoa huduma ya matibabu ya awali ya Saratani ya mlango wa kizazi na kufikia  wanawake milioni 3 watakaopata huduma hii ili kuokoa wanawake wa vijijini  kwani mpaka sasa hivi tunavyo vituo vya afya  265 vinavyotoa huduma hii ” alisema Waziri Ummy.

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa uchunguzi na kutoa chanjo ya Saratani ya mlango wa kikazi  kwa wasichana kuanzia miaka 9 mpaka 14 ili kuweza kupunguza vifo vitokanavyo na tatizo hilo kwani katika kila wanawake 100 vifo vinavyotokana na ugonjwa huo ni 32.
 Waziri  wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa kupokea vifaa vya kuchunguza saratani vyenye thamani ya shilingi milioni 98  leo jijini Dar es salaam .
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,  Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) akipokea moja ya vifaa vya uchunguzi wa saratani ya kizazi kutoka kwa Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchini Tanzania Bw. Jeremia Zoungran (kushoto) wakati wa makabidhiano ya vifaa vya kuchunguza saratani ya kizazi leo jijini Dar es salaam.
 Waziri  wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) akipokea moja ya nyenzo za  kufundishia juu ya uchunguzi wa saratani ya kizazi kutoka kwa Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchini Tanzania Bw. Jeremia Zoungran (kushoto) wakati wa makabidhiano ya vifaa vya kuchunguza saratani ya kizazi leo jijini Dar es salaam katikati ni Afisa Afya kutoka USAID Bi. Ananth Thambinygan .

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

CCM Z'BAR YATUMA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KIFO CHA MWANAHABARI WA ZBC

$
0
0
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimepokea kwa mshituko na huzuni mkubwa taarifa ya kifo cha Mwandishi wa habari wa Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC) Marehemu Maridadi Aman kilichotokea jana katika Hospitali ya Tasakhtaa Grobal, Vuga Zanzibar.

Kutokana na msiba huo mzito kwa Tasnia ya Habari nchini, CCM Zanzibar inatambua na kuthamini mchango mkubwa wa marehemu enzi za uhai wake alikuwa mstari wa mbele katika kutangaza taarifa za Chama Chetu kwa jamii.

Tunaamini kwamba juhudu, maarifa na busara za marehemu Maridadi zitabaki kama kumbukumbu na muongozo wa kuongeza hamasa ya kujituma kiutendaji kwa Wanahabari wote nchini.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi anawapa pole Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo, Wanahabari wote, ndugu wa familia pamoja na walioguzwa na msiba huo.

Mpendwa wetu ametangulia mbele ya Haki , ataendelea kubaki katika kumbukumbu zetu daima na tunamuomba Mungu aiweke roho ya Marehemu mahali pema peponi Amin.

Imetolewa na:-

NDG.WARIDE BAKAR JABU

KATIBU WA KAMATI MAALUM WA NEC,
IDARA YA ITIKADI NA UENEZI CCM -ZANZIBAR,
20, NOVEMBA 2017.

Wabunge wawapongeza NSSF, PPF na magereza mradi wa kiwanda cha sukari cha Morogoro

$
0
0
KAMATI ya Bunge ya Katiba na Sheria imepongeza namna mifuko ya hifadhi ya jamii ya NSSF na PPF inavyotekeleza mradi wa pamoja wa ujenzi wa kiwanda cha sukari unaofahamika kama Mkulazi huku ikitoa wito kwa wadau hao kuhakikisha wanakamilisha mradi huo kwa wakati ili kulinusuru taifa na uhaba wa bidhaa hiyo.

Mwisho mwa wiki kamati hiyo ilitembelea mradi huo unaotekelezwa katika gereza la Mbigiri, lililopo Dakawa mkoani Morogoro kupitia kampuni Hodhi ya Mkulazi Holding inayoshirikiana na Jeshi la Magereza nchini.

"Baada ya kusikiliza mpango mikakati na kisha kutembelea shamba husika kiukweli kamati yetu imeridhishwa sana na jinsi wadau hawa wanavyotekeleza mradi huu. Ni wazi kuwa walifanya utafiti wa kutosha kabla na matunda yake kiukweli yameanza kuonekana kikubwa tu tunachowaomba wamalize mradi huu kwa wakati .'' alisisitiza  Mwenyekiti wa kamati hiyo Bw Mohamedi Mchengelwa.

Aidha, wajumbe wa kamati hiyo walionyesha kuridhiswa zaidi na namna mradi huo unavyohusisha wananchi walio jirani na maeneo ya mradi ambao mbali na kupata ajira za moja kwa moja pia wamepatiwa fursa ya kulima miwa ili kukiuzia kiwanda hicho, hatua waliyosema kuwa itapunguza tatizo la ajira na kuongeza kipato cha wananchi.

"Kingine kikubwa zaidi kwa wadau hawa ni kuhakikisha kuwa mradi huu hauishii kwenye kuzalisha sukari tu bali pia bidhaa zitokanazo na mabaki ya malighafi za miwa ikiwemo ethanol, vyakula vya mifugo pamoja na uzalishaji wa nishati umeme,'' alisema mjumbe Selemani Zedi huku akiungwa mkono na wenzie akiwemo Mbunge wa Wawi Ali Salehe.

Akijibu baadhi ya hoja za wabunge hao ambao pia walitaka kufahamu uwezekano wa mifuko hiyo kuwekeza kwenye sekta ya uvuvi hapa nchini  Waziri wa Kazi, Ajira, Sera, Bunge, Vijana na wenye ulemavu, Jenista Mhagama  alisema uwezekano huo upo ikiwa mamlaka zinazosimamia mifuko hiyo zikiwemo bodi pamoja na Mamlaka ya usimamizi na udhibiti wa sekta ya hifadhi ya jamii (SSRA) zitaridhia miradi hiyo kwa kuangalia vigezo muhimu.

"Ili kuwekeza kwenye miradi mikubwa kama hii inahitaji ruhusa za mamlaka mbalimbali zinazosimamia mifuko hiyo kwa kuwa mamlaka hizo pia zinahitaji kujiridhisha pasipo kuacha chembe ya shaka kuwa utekelezaji wa miradi hii haihatarishi fedha za wanachama japo habari njema ni kwamba kati ya miradi 27 inayotarajiwa kutekelezwa na mifuko hii tayari miradi 15 imepatiwa ruhusa ya utekelezwaji na mamlaka hizi,'' alisema.

Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Mkulazi ambae pia ni Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Prof Godius Kahyarara pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw.William Erio, waliihakikishia kamati hiyo, serikali, wananchama na wadau wote wa mifuko hiyo kuwa hadi kufikia mwishoni mwa mwaka ujao mradi huo utakuwa tayari umeanza kuzalisha sukari pamoja na baadhi ya bidhaa ambatanishi kulingana na wito wa wabunge hao.

"Mradi huu mliotembelea leo unaolenga kuzalisha tani 50 za sukari kwa mwaka na ni sehemu tu ya mradi mkubwa unaotekelezwa na mifuko yetu miwili yaani NSSF na PPF ukiwepo mwingine mkubwa zaidi katika eneo la Ngerengere, Wilaya ya Morogoro Vijijini unaofahamika kama Mkulazi I ambao unaolenga kuzalisha tani 200,000 za sukari kwa mwaka,'' alisema Prof Kahyarara.

"Zaidi tuwahakikishie tu waheshimiwa wabunge kuwa hoja zenu tumezipokea na tutasimamia kuhakikisha kwamba mradi huu unakamilika kwa wakati na zaidi si tu kwamba tutalisha soko la ndani bali pia soko la nje hususani mataifa jirani ya Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,'' aliongeza Bw Erio.

Naye Mwakilishi wa jeshi la Magereza, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro (RPO), Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP)Mzee Nyamka mbali na kuishukuru mifuko hiyo pia alitoa wito kwa mifuko mingine ya hifadhi ya jamii pamoja na  wadau wengine kujitokeza ili kushirikiana na Jeshi hilo katika utekelezaji wa miradi mingine huku akibainisha kuwa jeshi hilo lina eneo kubwa la ardhi pamoja na nguvu kazi ya kutosha.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dk Stephen Kebwe alisema mkoa wake umekuwa ukiupa kipaumbele kikubwa mradi huo kuwa utekelezaji wake pamoja na mambo mengine unalenga kuongeza ajira kwa wananchi wa mkoa huo na kupunguza kabisa kasi ya mfumuko wa bei ya sukari kwa kuongeza uzalishaji wa bidhaa hiyo muhimu. 
 Waziri wa Kazi, Ajira, Sera, Bunge, Vijana na wenye ulemavu, Jenista Mhagama  (wa tatu kulia) akiwaongoza baadhi ya wajumbe wa kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria  kukagua shamba hilo.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria Bw Mohamedi Mchengelwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua shamba kubwa la miwa lililopo katika gereza la Mbigiri lililopo Dakawa mkoani Morogoro ambalo ni sehemu ya mradi wa ujenzi wa kiwanda cha sukari kinachojengwa kwa ubia kati ya mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya NSSF, PPF na jeshi la Magereza nchini.
 Waziri wa Kazi, Ajira, Sera, Bunge, Vijana na wenye ulemavu, Jenista Mhagama  akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua shamba hilo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Mkulazi ambae pia ni Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Prof Godius Kahyarara akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua shamba hilo. Kwa mujibu wa Prof. Kahyarara hadi kufikia mwishoni mwa mwaka ujao mradi huo utakuwa tayari umeanza kuzalisha sukari pamoja na baadhi ya bidhaa ambatanishi ikiwemo uzalishaji wa umeme.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

WATAKWIMU WATAKIWA KUTUMIA TEKNOLOJIA YA KISASA KATIKA UKUSANYAJI WA TAKWIMU BORA

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Alibina Chuwa akisisitiza jambo wakati wa hafla ya maaadhimisho ya Siku ya Takwimu Barani Afrika leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Shughuli za Kitakwimu Bw. Irenius Ruyobya, Mwakilishi wa Gavana wa Benki Kuu ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchumi wa benki hiyo Bw. Johnson Nyera, Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya Watakwimu Tanzania (TASTA) na Mwakilishi kutoka Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Bw. Abdalah Ramadhan Abeid. Kauli mbiu ya mwaka huu ni " Takwimu Bora za Uchumi kwa Maisha Bora".
 Mwakilishi wa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchumi wa benki hiyo Bw. Johnson Nyera akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Takwimu barani Afrika iliyofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mwl. Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Meneja wa Takwimu za Ajira na Bei Bibi. Ruth Minja na Mwakilishi wa Asasi za Kiraia Bw. Stephen Chacha. Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni "Takwimu Bora za Uchumi kwa Maisha Bora".
 Mwakilishi kutoka Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Bw. Abdalah Ramadhan Abeid akitoa neno la shukrani  katika hafla ya maaadhimisho ya Siku ya Takwimu Barani Afrika leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Mwakilishi wa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchumi wa Benki hiyo Bw. Johnson Nyera, Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Alibina Chuwa na Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya Watakwimu Tanzania (TASTA.) Bibi. Yasinta Kijuu. Kauli mbiu ya mwaka huu ni " Takwimu Bora za Uchumi kwa Maisha Bora".
 Mwakilishi wa Benki ya Dunia nchini Tanzania Bibi. Elizabeth Talbert akizungumza katika hafla ya maaadhimisho ya Siku ya Takwimu Barani Afrika leo Jijini Dar es Salaam. Kauli mbiu ya mwaka huu ni " Takwimu Bora za Uchumi kwa Maisha Bora".
 Mwanafuzni wa Kidato cha Tano kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana Kisutu Bi. Felister Mande akipongezwa na Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Alibina Chuwa baada ya kuwa mshindi wa pili katika shindano la insha kuhusu kauli mbiu ya maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika mwaka huu inayosema " Takwimu Bora za Uchumi kwa Maisha Bora".Kutoka kulia ni Mwakilishi wa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchumi wa hiyo Bw. Johnson Nyera, Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya Watakwimu Tanzania (TASTA.) Bibi. Yasinta Kijuu, Mwakilishi kutoka Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Bw. Abdalah Ramadhan Abeid na Mkurugenzi wa Shughuli za Kitakwimu Bw. Irenius Ruyobya.
 Mwanafuzni wa Kidato cha Tano kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana Kisutu Bi. Edda Magesa akipokea zawadi ya shilingi laki tatu kutoka kwa mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Uchumi wa BoT Bw. Johnson Nyera baada ya kuwa mshindi wa kwanza katika shindano la insha kuhusu kauli mbiu ya maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika mwaka huu inayosema " Takwimu Bora za Uchumi kwa Maisha Bora".Kutoka kulia kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Alibina Chuwa Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya Watakwimu Tanzania (TASTA.) Bibi. Yasinta Kijuu, Mwakilishi kutoka Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Bw. Abdalah Ramadhan Abeid na Mkurugenzi wa Shughuli za Kitakwimu Bw. Irenius Ruyobya.
 Mgeni rasmi wa katika hafla ya maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchumi toka Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Bw. Johnson Nyera akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi kutoka Shule za Sekondari Kisutu Wasichana na Azania walioshiriki shindano la insha kuhusu kauli mbiu ya maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika mwaka huu inayosema " Takwimu Bora za Uchumi kwa Maisha Bora" wakati wa maadhimisho hayo leo Jijini Dar es Salaam.  Wanafunzi kutoka kushoto ni Edda Magesa (mshindi wa kwanza), Fred Komba (mshindi wa tatu) na Felister Mande (mshindi wa nne).(Picha na: Frank Shija - MAELEZO)

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

DR NTUYABALIWE FOUNDATION YAHAMASISHA WANAFUNZI KUJIAMINI NA KUSOMA KWA BIDII

$
0
0
Wanafunzi wamehamasishwa kujiamini na kusoma kwa bidii ili kujijengea msingi imara ya mafanikio katika maisha yao.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Muasisi wa Dr. Ntuyabaliwe Foundation, Bi. Jacquiline Mengi alipowatembelea wanafunzi wa shule za msingi za Muungano na Serengeti zilizopo Manispaa ya Temeke, siku  ambayo duniani kote inaadhimishwa siku ya mtoto Duniani.
Akizungumza na wanafunzi hao Muasisi wa Dr. Ntuyabaliwe Foundation amesema ujumbe wake muhimu kwao wakati wa kuadhimisha siku ya mtoto Duniani ni kujiamini na kusoma kwa bidii, kwani ndiyo ufunguo wa mafanikio katika maisha
Akizungumza katika hafla hiyo Mkurugenzi wa Huduma ya simu kwa Mtoto ( C-SEMA)  Bw. Michael Marwa amewataka watoto kuripoti mara moja kwa njia ya simu vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watoto ili wahusika wachukuliwe hatua.
Akitoa shukrani Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi ya Muungano, Esther Matowo amesema ujio wa Muasisi wa Taasisi ya Dr Ntubaliwe umewahamasisha  wanafunzi kujitambua na kujua wajibu wao. 
Hafla hiyo ilihudhuriwa pia na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke Salum Upunda, Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Serengeti Daud Sabai na walimu wa shule hizo mbili.
Mkurugenzi wa Dr.Ntuyabaliwe Foundation na Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi akizungumza na wanafunzi wa shule ya Msingi ya Muungano na Serengeti alipowatembelea katika maadhimisho ya Siku ya Mtoto Duniani yanayofanyika Novemba 20 ya kila mwaka.
Mkurugenzi wa Huduma ya simu kwa Watoto( C-SEMA)  Bw. Michael Marwa akionesha namba ya huduma zinazotumika kuripoti mara moja kwa njia ya simu vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watoto ili wahusika wachukuliwe hatua wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto Duniani yanayofanyika Novemba 20 ya kila mwaka yaliyofanyika katika shuleni hapo.
Afisa Elimu na Ufundi manispaa ya Temeke, Salum B. Upunda aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya watoto Duniani mara ya viongozi wa Dr. Ntuyabaliwe Foundation walipotembelea shuleni hapo leo.
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Muungano, Esther Matowo akitoa shukrani kwa uongozi wa Dr.Ntuyabaliwe Foundation kutembelea shuleni hapo na kuzungumza na wanafunzi wa shule hiyo wakati wa maadhimisho ya siku ya mtoto Duniani.
Mkurugenzi wa Dr.Ntuyabaliwe Foundation na Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi ya Serengeti na Muungano mara baada ya kuzungumza na wanafunzi hao wakati wa maadhimisho ya siku ya mtoto Duniani.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

WAZIRI KALEMANI AKUTANA NA BALOZI WA MAREKANI, INDIA NCHINI

$
0
0
Leo tarehe 20 Novemba, 2017, Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amekutana na Balozi wa Marekani Nchini, Dkt. Inmi Patterson na Balozi wa India Nchini, Sandeep Arya kwenye Ofisi za Wizara ya Nishati zilizopo jijini Dar es Salaam. Lengo la ziara ya mabalozi hao lilikuwa ni kufahamiana na kujadili namna ya kushirikiana katika miradi ya nishati nchini.

Akizungumza na Balozi wa Marekani Nchini Dkt. Inmi Patterson aliyeambatana na wawakilishi kutoka Shirika la Misaada la Marekani (USAID), Mfuko wa Changamoto za Milenia (MCC) na Mradi wa Power Africa uliopo chini ya MCC, Dkt. Kalemani alielezea mikakati ya Serikali ya kuhakikisha nishati ya uhakika inapatikana nchini kuwa ni pamoja na mradi wa kuzalisha umeme kwa kutumia nguvu za maji wa Stieglers Gorge uliopo Rufiji mkoani Pwani, miradi ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi ya Kinyerezi I, Kinyerezi II na Kinyerezi III na miradi ya nishati jadidifu kama vile upepo, jua na jotoardhi.

Dkt, Kalemani alisema Serikali kupitia Wizara ya Nishati imeweka malengo ya kuhakikisha ifikapo mwaka 2020 kiasi cha Megawati 5000 za umeme zinazalishwa na vijiji vyote nchini kupata nishati ya umeme wa uhakika na kwa gharama nafuu. Waziri Kalemani alitumia fursa hiyo kualika wawekezaji kutoka Marekani kuwekeza kwenye sekta ya nishati ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa malengo ya Wizara ya kuhakikisha nishati inachangia kwa kiasi kikubwa katika ukuaji wa uchumi. Naye Balozi wa Marekani Nchini, Dkt. Inmi Patterson alipongeza mikakati mizuri ya Wizara katika kuhakikisha nishati ya uhakika inapatikana kwani pasipo umeme wa uhakika hakuna maendeleo yoyote.

Balozi Patterson alimhakikishia Waziri Kalemani kuwa nchi ya Marekani ipo tayari kushirikiana na nchi ya Tanzania hususan katika sekta ya nishati pamoja na sekta nyingine ili kuchochea kasi ya maendeleo nchini. Wakati huo huo Waziri Kalemani akizungumza na Balozi wa India Nchini, Sandeep Arya aliyemtembelea ofisini kwake mbali na kueleza mipango ya serikali katika kuhakikisha nishati ya uhakika inapatikana, aliomba nchi ya India kusaidia kupitia wataalam wake kushirikiana na wataalam wa Tanzania katika sekta ya nishati kutokana na kuwa na uzoefu mkubwa.

Aliendelea kusema kuwa Tanzania imekuwa na historia ndefu ya ushirikiano na kusisitiza kuwa umefika wakati wa kuboresha ushirikiano katika sekta nyeti ili uchumi wa nchi uweze kukua kwa kasi na Serikali kutimiza Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Mwaka 2025 yenye kufafanua kuwa nchi kuingia kwenye orodha ya nchi zenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 kupitia uboreshaji wa huduma za jamii.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (kulia) akisalimiana na Balozi wa India Nchini, Sandeep Arya (kushoto) mara baada ya kuwasili kwenye Ofisi za Wizara ya Nishati zilizopo jijini Dar es Salaam.

Rais Magufuli hajatengua utengua uteuzi wa Dkt. Laurian Ndumbaro

Waziri Kairuki, Benki ya Dunia Wajadili Rasilimali Madini

$
0
0
Na Rhoda James, DSM

Waziri wa Madini Angellah Kairuki mwishoni mwa wiki alikutana na Ujumbe wa Benki ya Dunia jijini Dar es Salaam kwa lengo la kufahamiana na kuangalia hatua mbalimbali zilizofikiwa katika utekelezaji wa Miradi ya Madini inayotekelezwa kupitia Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali Madini (SMMRP) unaofadhiliwa na Benki hiyo kwa kushirikiana na Serikali.

Pamoja na mambo mengine yaliyojadiliwa katika kikao hicho, Waziri Kairuki aliitaka Benki ya Dunia kuona namna ya kuwaendeleza Wataalam wa Sekta ya Madini ili kuwezesha uwepo wa Watalaam wa kutosha hususan katika masuala ya Uthaminishaji wa Madini ya Almasi, tanzanite na madini mengine ya vito na pia masuala ya uongezaji thamani madini kwa ujumla.

Pia, alishauri umuhimu wa kuboreshwa kwa Mtandao wa Huduma za Leseni kwa Njia ya Mtandao (Online Mining Cadastre) ikiwa ni pamoja na kuunganisha mtandao huo na Mamlaka nyingine ikiwemo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) ili taarifa zote zinazohusu madini na mapato yatokanayo na madini ziweze kupatikana kupitia mtandao huo.

Vilevile, aliishauri Benki hiyo kuhusu uuzwaji wa Madini ya Almas kwa njia ya Mnada kama vile inavyofanyika kwa Madini ya Tanzanite, lengo likiwa ni kuwezesha Serikali kunufaika na madini hayo. Aliongeza kuwa, baada ya Serikali ya Tanzania kupitisha Marekebisho ya Sheria ya Madini kupitia Sheria ijulikanayo kama (The written laws (Miscellaneous Amendements) Act, 2017), alisema kuwa, baadhi ya wawekezaji wameonesha wasiwasi kuhusu marekebisho hayo.

Hivyo, Waziri Kairuki amewataka wawekezaji kutokuwa na hofu kwani mabadiliko hayo yanalenga kuhakikisha kuwa Serikali inanufaika ipasavyo kutokana na rasilimali zake za madini. Aidha, alisema kwamba, nia ya Serikali kuhusu kuvutia wawekezaji iko palepale ilimradi wazingatie Sheria na taratibu. Vilevile, Waziri Kairuki alieleza kwamba, ni vema Benki ya Dunia ikaangalia namna bora ya kuhakikisha madini yote ya Tanzanite yanayouzwa nje ya nchi yanakuwa na Hati ya Uhalisia inayoonyesha chanzo cha madini hayo suala ambalo litawezesha Taifa kupata mapato stahiki kutokana na rasilimali hiyo.

Vievile, Waziri Kairuki alizungumzia suala la udhibiti wa utoroshaji madini na kusisitiza kuhusu kuwepo na namna bora ya kuzuia utoroshwaji wa madini ya Tanzanite ikiwemo kujulikana kwa idadi ya wachimbaji wadogo, wa kati, kiasi kinachopatikana na mahali madini hayo yanapouzwa. Pia, Waziri Kairuki aliishukuru Benki ya Dunia kutokana na ushirikiano ambao umekuwepo baina ya Serikali kwa kipindi chote na kueleza kuwa, Serikali iko tayari kutekeleza miradi husika kikamilifu kwa lengo la kukuza uchumi wa nchi.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

MWENYEKITI WA CCM RAIS DKT MAGUFULI AENDESHA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM

$
0
0
Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt John Pombe Magufuli, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar) na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Ndugu Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM na sekretarieti yake baada ya kikao jijini Dar es salaam leo Novemba 20, 2017.
Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt John Pombe Magufuli, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar) na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakiongea baada ya kikao cha Kamati Kuu ya CCM jijini Dar es salaam leo Novemba 20, 2017.Picha na IKULU.

UKATILI DHIDI YA WANAWAKE TATIZO KUBWA HAPA NCHINI - DKT. NDUGULILE

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya, Maendelego ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Faustine Ndugulile akitoa hotuba ya ufunguzi wakati wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Dawati la Jinsia na Watoto linalosimamiwa na Jeshi la Polisi Tanzania.
Mkurugenzi wa CDF Koshuma Mtengeti akikabidhiwa cheti cha mdau wa Dawati la Jinsia aliyetukuka na Mhe. Naibu ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dr. Faustine Ndugulile.
Naibu Waziri wa Afya, Maendelego ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Faustine Ndugulile akiwa katika picha ya pamoja na Wadau wa Maendeleo mara baada ya kupokea vyeti kutoka Dawati la Jinsia la Jeshi la Polisi wakati wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Dawati la Jinsia na Watoto linalosimamiwa na Jeshi la hilo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendelego ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Faustine Ndugulile akiwa katika picha ya pamoja na Makamishina wa Jeshi la Polisi wakati wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Dawati la Jinsia na Watoto linalosimamiwa na Jeshi la hilo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendelego ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Faustine Ndugulile akipokea Maandamano ya Jeshi la Polisi wakati wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Dawati la Jinsia na Watoto linalosimamiwa na Jeshi la hilo.

Na Anthony Ishengoma

Takwimu za shirika la Afya Duniani zinaoenesha kuwa asilimia 35 ya wanawake ulimwenguni ni wahanga wa vipigo na ukatili wa kingono au vyote kwa pamoja wakati hapa nchini Tanzania taarifa ya hali ya watu na Afya ya waka 2015 inaonesha kuwa asilimia 40 ya wanawake wenye umri kati ya miaka 15-49 wamefanyiwa ukatili wa kupigwa katika kipindi cha mwaka mmoja. Naibu Waziri wa Afya, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Faustine Ndugulile amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa mkutano Mkuu wa wa mwaka wa Dawati la Jinsia na Watoto wa Jeshi la Polisi unaondealea kwa siku tatu.

Aidha Mhe. Ndugulile ameongeza kuwa pamoja na kuwepo ukatili wa kingono na vipigo kwa wanawake lakini pia vitendo vya ukeketaji bado ni tatizo kubwa hapa nchini akisema liko juu kwa kiwango cha asailimia 30 akiutaja mkoa wa Manyara kuwa na kiwango cha ukeketaji kwa asilimia 58. Aidha Mikoa mingine inayaoongoza kwa vitendo vya ukeketaji ni pamoja na Mkoa wa Dodoma kwa sailimia 47,Arusha asilimia 41 ikifutiwa na Mkoa wa Mara na Singida yenye kiwango cha asilimia 32.

Aidha ameonya kuwa ukatili wa kijinsia haukubaliki akitaja kuwa bado kuna kiwango kikubwa cha ukatili hapa Nchini na kinagharimu Jamii na Taifa letu katika Nyanja za kijamii, kisiasa na kiuchumi ikiwemo kuzorota kwa afya ya walengwa. Wakati huhuo Mwakilishi wa Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi, Kamishina wa Polisi Jamii hapa Nchini Mussa Ally Musa amesema kuwepo na ongezeko kubwa la taarifa za ukatili wa kijinsia na unyanyasaji kwa watoto tangu kuanzishwa kwa dawati hilo hapa Nchini ambapo kwa kipindi cha Januari-Desemba 2016 jeshi la polisi limepokea matukio 10,551 ya ukatili wa kijinsia kwa watoto ukilinganisha na matukio 9541 katika kipindi kama hicho 2015 na 2488 ya mwaka 2014.

Aidha ameitaja mikoa inayoongoza kwa matukio haya kuwa ni mkoa wa Moarogoro 1403, Rukwa 850, Singida 697,Iringa 649 na Dodoma kiwango cha matukio hayo ni 609 akiongeza kuwa kwa upande wa Tanzania visiwani Mikoa inayoongoza ni Mkoa wa Kusini pemba, Kusini unguja na Kasikazini unguja. Aidha kamishina Musa ameyataja makosa ya ubakaji kuwa ndiyo yanayoongoza ambapo Jeshi la Polisi mpaka sasa limepokea jumla ya matukio 4,423 ya ubakaji , shambulio 1,801 na shambulio la kudhuru mwili 1,021 na matukio yan kujerui 819.

Pamoja na ongezo hilo la matukio hayo pia dawati la jinsia la jeshi la polisi limekuwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ushirikiano mdogo kutoka kwa familia husika, uchache wa vifaa na majengo, uelewa mdogo wa wananchi na watendaji wa serikali pamija na ukosefu wa meaneo ya kuifadhi waanga wa ukatili.

Aidha Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Faustine Ndugulile ameongeza kuwa changamoto inayokabili Dawati la Jinsia la Jeshi la Polisi ni ufinyu wa bajeti, upungufu wa rasilimali watu, akisema serikali itaendelea kufanyia kazi mapungufu yaliyoplo huku akitaja juhudi mojawapo ni uwepo wa Mpango Kazi wa Kitaifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto.

MOI YAOKOA BILIONI 5 KWA KUPUNGUZA RUFAA ZA NJE YA NCHI.

$
0
0
Patrick Mvungi- MOI

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu (MOI) imeokoa zaidi ya shilingi Bilioni 5 ambazo zingetumika kusafirisha wagonjwa nje ya nchi kufuata matibabu baada ya MOI kuanzisha huduma za kibingwa ambazo awali zilikua hazipatikani hapa nchini.

Hayo yamebainishwa katika ziara ya Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii , Jinsia Wazee na watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya alipotembelea MOI na kukagua hali ya utoaji wa huduma, mazingira , miundombinu na kuwajulia hali wagonjwa pamoja na kukutana na menejimenti.

Akizungumza na menejimenti ya MOI, Dkt. Ulisubisya amepongeza kazi nzuri na kubwa inayofanywa ambayo imepelekea watanzania kupata huduma bora za kibingwa ambazo wangepaswa kuzifuata nje ya nchi.

“Mnafanya kazi nzuri sana, jambo ambalo linatupa faraja kubwa sisi viongozi wenu, naomba muongeze ubunifu zaidi, hamtakiwi kuifikiria MOI kwenye ukanda huu wa Afrika pekee bali duniani, hii ni changamoto kwetu sote kuifikisha hapo ”alisisistiza Dkt. Ulisubisya

Aidha, Dkt Ulisubisya amesema MOI imepunguza rufaa za kwenda nje ya nchi kwa asilimia 95% na asilimia 5% iliyobaki MOI inaweza kuimaliza kabisa na kusiwepo mgonjwa wa kwenda nje ya nchi.

Pia, amewaelekeza viongozi wa MOI kushirikiana na Wizara ya Afya kutafuta namna ya kufuta rufaa kwa kutoa mapendekezo na ushauri utakaosaidia kutatuliwa kwa changamoto hiyo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia , Wazee na Watoto Dkt Mpoki Ulisubisya akizungumza na menejimenti ya MOI (hawapo pichani) katika ukumbi wa Mikutano wa MOI.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akimjulia hali mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji mkubwa wa mgongo, anayetoa ufafanuzi wa namna upasuaji huo ulivyofanyika ni Dkt. Nicephorus Rutabansibwa (Daktari bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mgongo). Kushoto ni Mganga mkuu wa Serikali Profesa Muhamed Kambi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia , Wazee na Watoto Dkt Mpoki Ulisubisya akikagua mashine mojawapo katika benki ya damu ya MOI.
Mtaalamu wa Maabara Bwana Mbuta Jackson akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia , Wazee na Watoto Dkt Mpoki Ulisubisya kuhusu namna benki mpya ya damu inavyofanya kazi kwa kushirikiana na Mpango wa Taifa wa damu salama.

WAKAZI WA MKOA WA DAR ES SALAAM WAJITOKEZA KUPATA HUDUMA KATIKA MELI YA CHINA

IGP SIRRO AKUTANA NA BALOZI WA CHINA

$
0
0
 Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro (kulia), akizungumza na balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke, alipomtembelea ofisini kwake Makao Makuu ya Jeshi hilo leo jijini Dar es salaam kwa lengo la kujitambulisha tangu alipoteuliwa kuwa Balozi hapa nchini. Picha na Jeshi la Polisi.

 Balozi wa  China nchini Mhe. Wang Ke, akizungumza na Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro (kulia), alipomtembelea ofisini kwake Makao Makuu ya jeshi hilo leo jijini Dar es salaam kwa lengo la kujitambulisha tangu alipoteuliwa kuwa Balozi hapa nchini na kuahidi serikali ya nchi yake itaendelea kushirikiana na jeshi hilo. Picha na Jeshi la Polisi.



ASASI ZA KIRAIA ZAIOMBA SERIKALI KUBORESHA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI

$
0
0





Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA), Bi. Edda Sanga (kushoto) akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa Kuwakumbuka Wahanga wa Ajali za Barabarani. Kulia ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la Walemavu Tanzania (SHIVYAWATA), Felician Mkude.

Mtandao wa wadau kutoka asasi za kiraia unaotetea marekebisho ya sheria na sera ihusuyo usalama barabarani umeiomba Serikali kuifanyia maboresho sheria ya Usalama barabarabi ya mwaka 1973 ili iweze kukabiliana ipasavyo na suala la ajali za barabarani pamoja na athari zinazotokana na ajali hizo.

Kauli hiyo imetolewa mwishoni mwa wiki  jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA), Bi. Edda Sanga alipokuwa akisoma tamko la pamoja la asasi hizo katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa Kuwakumbuka Wahanga wa Ajali za Barabarani.

“Pamoja na mambo mengine, katika kuadhimisha siku hii tunaisihi serikali na watunga sheria kuifanyia maboresho sheria ya Usalama barabarabi ya mwaka 1973 ili iweze kukabiliana ipasavyo na suala la ajali za barabarani pamoja na athari zinazotokana na ajali hizo,” alisema Bi. Sanga.

Alisema miongoni mwa maeneo wanaoshauri marekebisho/maboresho ni pamoja na matumizi ya mikanda, ambapo Sheria ya sasa ya Usalama barabarani inasema ni kosa kisheria kwa dereva na abiria anayekaa kiti cha mbele kutokufunga mkanda wakati wa safari lakini sheria haisemi chochote kwa abiria wanaokaa viti vya nyuma. 

Alisema licha ya Kanuni za SUMATRA zinamtaka abiria yeyote kufunga mkanda ila kwa vile sheria mama (Road Traffic Act of 1973) ipo kimya katika eneo hilo utekelezaji wa kanuni hii unakuwa mgumu. 

Alisema eneo linguine ni pamoja na matumizi sahihi ya kofia ngumu, kwani Sheria ya sasa ya usalama barabarani inatambua kosa kwa mwendesha pikipiki kutokuvaa kofia ngumu lakini sheria hiyo haisemi chochote kwa abiria anayepanda katika chombo hicho wala kutaja aina na ubora wa kofia inayofaa.

“Kwa matumizi ya vilevi na uendeshaji vyombo vya usafiri: Sheria ya sasa ya usalama barabarani inasema kuwa itakuwa kosa kwa mtu yoyote kuendesha chombo cha moto akiwa na kiwango cha kilevi katika damu yake kinachozidi asilimia 0.08% katika mfumo wa mwili,

“Kiwango hiki ni kikubwa sana kikilinganishwa na tafiti zilizofanywa na Shirika la afya duniani na kupendekeza kiwango asilimia 0.05% kwa dereva aliyebobea na asilimia 0.02% kwa dereva mchanga. Hivyo basi ni rai yetu kuwa sheria ifanyiwe marekebisho ili iendane na kiwango cha sasa cha kimataifa kilichofanyiwa utafiti,” alisisitiza Bi. Sanga.

Aidha aliongeza kuwa adhabu zinazotolewa kwa sasa hazikidhi wala kuleta hofu kwa maderava wasiotaka kutii sheria na kanuni hivyo kuendelea kufifisha juhudi za kudhibiti tatizo la ajali za barabarani. 

“Mwendokasi umeendelea kuwa sababu kubwa ya ajali zinazogharimu uhai wa watu wengi. Sheria yetu inayo mapungufu kadhaa pamoja na juhudi nyingi za Jeshi la Polisi na wadau wengine kutaka kudhibiti jambo hili lemeendelea kuwa tatizo. Mfano Sheria ya usalama barabarani ya 1973 Kifungu cha 51(8) inatambua maeneo machache katika kuzuia mwendokasi, ni muhimu Sheria sasa itamke maeneo yote na si yale ya mjini tu au makazi, itamke wazi kuhusu maeneo ya shule, nyumba za ibada, maeneo ya michezo na mbuga za wanyama,” aliongeza Bi. Sanga katika taarifa hiyo.

Pamoja na mambo mengine, alisema sheria ya sasa ipo kimya juu ya suala la vizuizi vya watoto katika vyombo vya moto hasa kwa magari binafsi na tumeendelea kushuhudia madhara makubwa katika ajali zilizohusisha watoto vikiwemo vifo. 

Hata hivyo mtandao huo umewasihi wananchi kuwa na taadhari pindi watumiapo vyombo vya moto bila kujali mapungufu yaliyopo kwenye sheria za usalama barabarani ili kupunguza matukio ya ajali.

Kwa upande wake, Mwakilishi kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) usalama barabarani Mary Kessy, akitoa ufafanuzi kwa wanahabari, alibainisha takwimu zinaonyesha takribani watu milioni 1.25 duniani hufariki kila mwaka; huku nchini Tanzania asilimia 76 ya ajali za barabarani husababishwa na uzembe wa madereva, asilimia 8 ubovu wa barabara na ubovu wa vyombo vya moto kuchangia ajali hizo kwa asilimia 16.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni “Ifikapo 2020: Kupunguza vifo na ajali za barabarani kwa asilimia 50%”. Mtandao wa Wadau kutoka asasi za kiraia unaotetea marekebisho ya Sheria za Sera zihusuyo usalama barabarani Tanzania unaundwa na asasi zifuatazo;- TAWLA, TAMWA, WLAC, TCRF, TLS, TMF, RSA, AMEND TANZANIA, SHIVYAWATA, TABOA pamoja na SAFE SPEED FOUNDATION.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Mabalozi wa Usalama Barabarani (RSA), John Seka akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa Kuwakumbuka Wahanga wa Ajali za Barabarani.Kushoto ni Isabela Nchimbi kutoka TAWLA na Bi. Edda Sanga wa TAMWA (kulia).





MWANJELWA AMNADI MGOMBEA UDIWANI KATA YA IBIGI, APOKEA WANACHAMA WAPYA 21

$
0
0

Na Mathias Canal, Mbeya

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa Kilimo amewasihi wananchi kwa kauli moja kuchagua kiongozi makini anayetokana na CCM.

Mhe Mwanjelwa alisema kuwa kumchagua diwani wa CCM ni dalili nzuri ya kumpongeza na kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli anazozifanya kwa muktadha wa kuwaletea maendeleo watanzania wote.

Mjumbe huyo wa NEC, aliyasema hayo Leo Novemba 20, 2017 katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Bujinga A na B kilichopo Kata ya Ibigi, Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya ambapo alimnadi mgombea Udiwani wa Kata hiyo Bi Suma Ikenda Fyandomo.

(Mnec), Mhe Mwanjelwa aliwakumbusha wananchi waliojitokeza katika mkutano huo kuwa Hawachagui ilani mpya Bali wanachagua Diwani kwa ajili ya kutekeleza ilani ya Ushindi ya CCM ya Mwaka 2015-2020 ambayo wananchi waliiamini na kuichagua Octoba 25, 2015.

Alisema kuwa nchini Tanzania hakuna chama chenye uwezo wa kuwaletea maendeleo wananchi Bali Chama Cha Mapinduzi pekee ndicho chenye uwezo na jukumu la kuwaletea maendeleo endelevu wananchi.

Katika Mkutano huo wanachama 21 walivutiwa na hotuba ya Mjumbe huyo wa Halmashauri kuu ya CCM wakati akimnadi mgombea hivyo kufanya maamuzi ya kujivua uanachama wa CHADEMA na kujiunga na CCM ambapo wameahidi kushirikiana na mgombea udiwani wa CCM ili kuhakikisha anashinda kwa kishindo.

Ushiriki wa kampeni hizo katika Kata ya Ibigi unajili wakati ambapo Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa yupo ziarani Mkoani Mbeya ambapo pamoja na mambo mengine Kesho Disemba 21, 2017 atashiriki ufunguzi wa Mkutano wa Makatibu Tawala na washauri wa kilimo wa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini juu ya mfumo wa ununuzi wa mbolea (BPS).

Mkutano huo utafanyika katika Ukumbi wa Benjamini Mkapa Jijini Mbeya.


Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa kilimo akimnadi Mgombea Udiwani Kata ya Ibigi Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya Bi Suma Ikenda Fyandomo, Jana Novemba 20, 2017. Picha Zote Na Mathias Canal
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa kilimo akimvalisha kofia ya CCM kijana aliyehama Chadema wakati wa kampeni za Udiwani Kata ya Ibigi Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya Bi Suma Ikenda Fyandomo, Jana Novemba 20, 2017.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa kilimo akifurahi na wananchama wa CCM wakati wa mkutano wa kumnadi Mgombea Udiwani Kata ya Ibigi Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya Bi Suma Ikenda Fyandomo, Jana Novemba 20, 2017.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa kilimo akifurahi na wananchama wa CCM wakati wa mkutano wa kumnadi Mgombea Udiwani Kata ya Ibigi Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya Bi Suma Ikenda Fyandomo, Jana Novemba 20, 2017.

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

MEYA WA JIJI LA TANGA APOKEA VIFAA TIBA KUTOKA KUWAIT

$
0
0
Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Al-Najem amezindua visima sita vya maji safi na salama mwisho wa wiki katika Mkoa wa tanga ikiwemo shule ya Old Tanga Secondary School ,vilivyochimbwa na Jumuiya ya Direct Aid ya Kuwait ikiwa ni mwendelezo wa mradi ulioanzishwa na Ubalozi wa Kuwait nchini unaofahamika kwa jina la “KISIMA CHA MAJI KATIKA KILA SHULE”, uzinduzi ambao ulihudhuriwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Mhina Mustapha Selebosi, walimu, wanafunzi na wadau mbalimbali.

Aidha Balozi wa Kuwait alitembelea kituo cha afya cha Ngamiani ambapo alimkabidhi Mstahiki Meya wa Tanga mabeseni 50 yenye vifaa tiba kwa ajili ya akina mama wajawazito na watoto wachanga, mabeseni ambayo ni msaada kutoka taasisi ya Red Crescent ya Kuwait. Akiwa mjini Tanga Balozi Al-Najem alihudhuria mahafali ya kuhitimu wanafunzi wa Shule ya sekondari ya Kheri ya wanawake.

Kwa upande wake Meya wa Tanga aliushukuru Ubalozi wa Kuwait nchini kwa msaada huo na akamuomba Balozi wa Kuwait pia aweze kusaidia katika shule za jiji hilo 98 za msingi na 32 za sekondari Rkupata huduma ya visima vya maji.
Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Al-Najem (kushoto) akimkabidhi mabeseni 50 yenye vifaa tiba kwa ajili ya akina mama wajawazito na watoto wachanga, Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Mhina Mustapha Selebosi ,kulia 
Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Al-Najem atia saini katika kitabu cha wageni mara alipowasili katika uzinduzi wa Kisima 
Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Al-Najem akizungumza wakati wa uzinduzi huo
Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Al-Najem amezindua visima sita vya maji safi na salama katika Mkoa wa Tanga mwisho wa wiki,ikiwemo shule ya Old Tanga Secondary School vilivyochimbwa na Jumuiya ya Direct Aid ya Kuwait ikiwa ni mwendelezo wa mradi ulioanzishwa na Ubalozi huo.

CHUO CHA MAFUNZO YA KIJESHI MONDULI CHAZINDUA KOZI MPYA YA SAYANSI YA KIJESHI

$
0
0
Na Pamela Mollel,Monduli

Katibu Mkuu wa wizara ya ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa, Dkt Florens Turuka amesema kuwa jeshi hilo hivi sasa limejipanga katika kukabiliana na changamoto za ulinzi na usalama kwa kuwapatia askari wake mafunzo maalumu ya sayansi ya kijeshi. 

Aliyasema hayo Jana wakati akizungumza katika uzinduzi wa shahada ya kwanza ya sayansi ya kijeshi inayotekelezwa na chuo cha uhasibu Arusha kwa kushirikiana na Chuo cha mafunzo ya kijeshi Monduli (TMA). 

Alisema kuwa, kumekuwepo na matishio mengi ambayo yamekuwa yakijitokeza Kwa namna tofauti ambapo hivi sasa matishio hayo yamegeuka na kuhamia kwenye mitandao, hivyo kama jeshi wana wajibu wa kujipanga zaidi kwa kuwaandaa maaskari ili waweze kukabiliana na hali hiyo mahali popote. 

Dkt Turuka alisema kuwa, wao Kama jeshi ni wajibu wao kujipanga mapema kwa kuangalia namna ya kuwajengea uwezo hasa katika maswala ya sayansi na teknolojia ili kuboresha ulinzi na usalama hapa nchini. 

Kwa upande wa Mkuu wa majeshi nchini, Jenerali Venance Mabeyo alisema kuwa wamekuwa wakitoa mafunzo hayo kwa maaskari wake kulingana na mabadiliko ya kidunia hasa katika maswala ya sayansi na teknolojia kwani ni eneo ambalo linahitaji elimu kubwa zaidi.  Alisema kuwa, ni lazima wasonge mbele na kwenda na wakati kwani wasipofanya hivyo watabaki nyuma na kamwe hawataweza kukabiliana na vitisho vilivyopo hivi sasa. 

Naye Mkuu wa chuo cha mafunzo ya kijeshi Monduli (TMA), Dokta Paul Massao alisema kuwa, wamekuwa wakitoa masomo ya kijeshi na kiraia ili kuwaandaa vijana katika hatua ya ngazi za juu zaidi kielimu ambapo kwa kuanzia kozi hiyo watahiniwa 158 wataanza kozi hiyo mapema. 

Kwa upande wa Kaimu mkuu wa chuo cha uhasibu Arusha, Dokta Faraji Kasidi alisema kuwa, mahusiano kati yao na chuo hicho cha kijeshi yameanza muda mrefu ambapo wao wamekuwa wakifundisha askari hao mafunzo ya kiraia ambayo yamekuwa yakileta manufaa makubwa Sana. 
Mkuu wa majeshi nchini, Jenerali Venance Mabeyo akitoa hotuba fupi katika hafla fupi ya uzinduzi wa mafunzo ya shahada ya kwanza ya Sayansi ya kijeshi iliyofanyika chuoni hapo mapema jana.
Meja jenerali Paul Peter Masao ambaye ni mkuu wa chuo cha mafunzo ya maafisa wanafunzi jeshi la ulinzi la Tanzania(TMA) akizungumza kwenye hafla hiyo jana.
Katibu mkuu wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga taifa Florens Turuka akizungumza katika uzinduzi wa uzinduzi wa shahada ya kwanza ya Sayansi ya kijeshi iliyofanyika chuoni hapo
Kaimu mkuu wa chuo cha uhasibu Arusha, Dokta Faraji Kasidi akizungumza katika uzinduzi huo ambapo alisema mahusiano kati yao na chuo hicho cha kijeshi yameanza muda mrefu ambapo wao wamekuwa wakifundisha askari hao mafunzo ya kiraia.
kushoto aliyevalia suti ni Profesa Johannes Monyoambaye aliwahi kuwa mkuu wa chuo cha uhasibu Arusha(IAA)
Wanafunzi wa mafunzo ya shahada ya kwanza ya Sayansi ya kijeshi iliyofanyika chuoni hapo mapema jana.
Picha ya pamoja.


Viewing all 110088 articles
Browse latest View live




Latest Images