Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live

TAARIFA KWA UMMA: VIPINDI VYA MVUA KUBWA VINATARAJIWA KATIKA BAADHI YA MAENEO YA UKANDA WA PWANI YA TANZANIA.


MWAMUZI ALITUNYIMA PENATI MBILI DHIDI YA YANGA - MANARA

$
0
0
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Hajji Sunday Manara akitoa lawama kwa mwamuzi Hery Sasii katika 

mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya mahasimu wao wa jadi, Yanga SC uliomalizika kwa sare ya 1-1 Jumamosi Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.


KLABU ya Simbe imelalamika kunyimwa penalti mbili na refa Hery Sasii katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya mahasimu wao wa jadi, Yanga SC uliomalizika kwa sare ya 1-1 Jumamosi Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.


Akizungumza na Waandishi wa Habari leo makao makuu ya klabu, Mtaa wa Msimbazi, Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Hajji Sunday Manara amesema refa alikwenda na matokeo yake uwanjani. 

Manara aliwawekea Waandishi wa Habari video ya mchezo huo kuwaonyesha namna ambavyo refa Sasii hakutoa penalti licha ya mpira kuwagonga mikononi beki, Kevin Yondan na kiungo Mkongo, Papy Kabamba Tshishimbi Jumamosi.


Manara aliyewabeza watani wao hao wa jadi, kwamba ni kawaida yao kupendelewa na marefa kila wanapokutana na Simba amesema watapeleka malalamiko Bodi ya Ligi dhidi ya refa huyo na wengine walioionea timu yao katika mechi zilizotangulia.


Akasema huo ni mwendelezo wa matukio ya klabu yake kutotendewa haki na marefa katika mechi za Ligi Kuu msimu huu, akidai walinyimwa pia penalti mbili katika mechi dhidi ya Mbao FC Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza, kabla ya wapinzani wao wengine, Singida United kupewa penalti ya utata Uwanja wa CCM Kambarage Shinyanga.

Simba ilitoa sare ya 2-2 na Mbao FC kabla ya kushinda 3-1 dhidi ya Stand United, katika mchezo ambao pia walikataliwa bao zuri la mshambuliaji wao, Laudit Mavugo.

Pamoja na hayo, Manara amelalamikia kitendo cha Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo kukataa ombi la klabu, Simba na Yanga kutaka mchezo wao ufanyike Uwanja mkubwa wa Taifa na kuupeleka Uwanja mdogo wa Uhuru.


Manara amesema hali hiyo ilizikosesha klabu fedha kutokana na watazamaji kutojitokeza kwa wingi kwa kuhofia usalama wao kutokana na udogo wa Uwanja wa Uhuru. 


Aidha, Manara  amesema kwamba kikosi cha Simba sasa kinaelekeza nguvu zake katika mchezo wake ujao dhidi ya Mbeya City Jumapili Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya na  kikosi kitaondoka  Ijumaa kwenda Mbeya na  kitakaa kwa muda mrefu kutokana na kukabiliwa na mechi nyingine pia za Ligi Kuu Nyanda za Juu Kusini. 

KUNDI LA SPACIOUS AFRICA LAJA KUKOMBOA WASANII WA BONGO

$
0
0
 Meneja wa Kampuni ya Specious Afrika Hennesseyy Mdendwa akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu uzinduzi wa lebo mpya iliyo chini ya kampuni hiyo, kulia ni msanii aliyechini ya lebo hiyo Eliud Modest na kushoto ni msanii aliyechini ya lebo hiyo Akil Mohamed.
 Msanii Akil Mohamed (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu yeye kuwa chini ya lebo ya Specious Music mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kulia ni msanii mwenzake Eliud Modest.
Msanii Eliud Modest (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu yeye kuwa chini ya lebo ya Specious Music mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kulia ni msanii mwenzake Akili Mohamed. Picha na Eliphace Marwa - Maelezo

PTA BANK BECOMES TDB - WITH INCREASED COMMITMENT FOR FUNDING IN EASTERN AND SOUTHERN AFRICA

$
0
0
 The Eastern and Southern African Trade and Development Bank, commonly known as PTA Bank, has changed its official brand name to TDB (Trade and Development Bank). 

Since its establishment over three decades ago, the Bank has operated under its legal name ‘’Eastern and Southern African Trade & Development Bank” as well as two trading names in English and in French: PTA Bank / Banque de la ZEP. Through the revitalization of its corporate branding, the Bank will be trading under one trade name (Trade and Development Bank – TDB) and a new logo while its legal name ’Eastern and Southern African Trade & Development Bank” will remain unchanged.

The leading regional multilateral Development Finance Institution (DFI) has also announced that it will continue to increase financing for priority sectors such as infrastructure, manufacturing, industry and agribusiness across the 21 member states it operates in, over the next five years.

“Our rebranding represents our rejuvenation and recommitment to innovate and play a more active role in promoting trade, economic development and regional integration, at a crucial time when the region is looking to more vigorously advance economic transformation and ratchet up the tapering growth ,” said Admassu Tadesse, President and Chief Executive of the Trade and Development Bank.
Trade and Development Bank (TDB), Principal Project and Infrastructure Finance Officer, Neema Siwingwa (right), addresses a press conference in Dar es Salaam yesterday to announce the changes of its trade name which were former known as Eastern and Southern Africa Trade and Development Bank (PTA Bank) to TDB. Looking on is Trade and Development Bank (TDB), Director Corporate Affairs & Investor Relations, Mary Kamari. 

RC MAKONDA AOKOA BILLION 1.11 KUFUFUA MAGARI MENGINE YA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA YALIYOKUFA

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda leo amekabidhi Mabasi 10 chakavu ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa kampuni ya Dar Coach kwa ajili kufufuliwa upya na kuwa ya kisasa. 

Mabasi hayo 10 chakavu yanatoka kwenye Vyombo vya Ulinzi na Usalama ikiwemo Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ Magari 3, Jeshi la Polisi Magari 4 pamoja na Jeshi la Magereza Magari 3 ambapo yote kwa pamoja Matengenezo yake yameokoa kiasi cha Shilingi Billion 1,110,000,000 ya Serikali. 

Makonda amesema kuwa Gari hizo zitatengenezwa na kukamilika ndani ya Siku 90 hadi 120 ambapo ameipongeza Kampuni ya Dar Coach kwa kujitolea kukarabati Magari hayo bila kutumia pesa ya Serikali. Aidha Makonda amesema Magari hayo yatafungwa Vifaa vya Kisasa ikiwemo Kiyoyozi (AC), Mfumo wa Chaji ya Simu kila Seat, Runinga, Radio, Viti vya kisasa, Vyoo vya Ndani, Bodi mpya pamoja na mwonekano mzima wa Gari ili ziwe za kisasa. 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akikaribishwa na viongozi wa jeshi wakati alipokwenda kukabidhi Mabasi 10 chakavu ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa kampuni ya Dar Coach kwa ajili kufufuliwa upya na kuwa ya kisasa. 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akimkabidhi Mabasi 10 chakavu ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa Mkurugenzi wa kampuni ya Dar Coach kwa ajili kufufuliwa upya na kuwa ya kisasa wakishuhudiwa na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaviva,Kamanda wa Polisi Dar es Salaam Lazaro Mambosasa, Mkurugenzi wa usafirishaji JWTZ Kanal RAajab Mwenyumbu, Mnadhimu wa Jeshi la Magereza ACP. Noel James. 
Mabasi 10 chakavu yakiwa yanatoka katika Chuo cha Polisi Kilwa Road kuelekea Mkuranga kwenye ofisi za Kampuni ya Dar Coach kwa ajili ya kufanyiwa marekebisho na kuwa ya kisasa zaidi. 
Mkuu wa Mkoa Paul Makonda akiwa ndani ya basi la Magereza. 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akiwa sambamba na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaviva,Kamanda wa Polisi Dar es Salaam Lazaro Mambosasa, Mkurugenzi wa usafirishaji JWTZ Kanal RAajab Mwenyumbu, Mnadhimu wa Jeshi la Magereza ACP. Noel James wakati wa kukagua mabasi 10 chakavu kabla ya kupelekewa kwenye gereji ya Dar Coach kwa ajili ya matengenezo.Picha zote na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MAVUNDE ASISITIZA KUWA NA NGUVU KAZI YA VIJANA WENYE UJUZI KATIKA UJENZI WA UCHUMI WA TAIFA

$
0
0
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu(Kazi,Vijana na Ajira) Mh. Anthony Mavunde leo ametembelea Chuo cha Ufundi Don Bosco kilichopo mkoani Kilimanjaro na kukagua maendeleo ya Vijana ambao wanasomeshwa hapo na Serikali kupitia mpango wa Ukuzaji Ujuzi Nchini.

Akizungumza na Vijana hao ambao wanasomea masomo ya Komputa,Mavunde amewataka Vijana hao kuutumia ujuzi watakaoupata hapo chuoni kujiajiri kwa  kuunda vikundi na Makampuni ili wapate nafasi ya kuwezeshwa kupitia mifuko ya uwezeshwaji wananchi kiuchumi nchini na hivyo kusaidia kutatua changamoto ya ukosefu wa Ajira kwa Vijana.

Mavunde pia amewaeleza Vijana hao kwamba watambue siku zote wao ndio moyo wa Taifa  na hivyo ndio nguvu kazi inayotegemewa kwa kiasi kikubwa ndio maana Serikali inaona umuhimu wa kuwekeza katika Mpango huu wa ukuzaji Ujuzi ili kuhakikisha Taifa linakuwa na nguvu kazi yenye ujuzi stahiki katika kuelekea nchi Uchumi wa Viwanda na ya kipato cha kati.

Kwa upande wao Vijana hao wanufaika na Mpango huu wameishukuru serikali kwa kutekeleza mpango huu wa ukuzaji ujuzi ambao utawasaidia kupata ujuzi na baadaye kuweza kujiajiri na Kuajiri Vijana wengine.

Mpango huu wa ukuzaji ujuzi unatarajia kuwanufaisha Vijana 3445 ambao serikali itagharamia mafunzo yao katika kozi za Tehama,Umeme,Ushonaji,Useremala,Uchomeleaji,Kuweka vigae,Ufundi bomba,Upigaji chapa na Ufundi Magari.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu(Kazi,Vijana na Ajira) Mh. Anthony Mavunde akikagua maendeleo ya Vijana ambao wanasomeshwa na Serikali kupitia mpango wa Ukuzaji Ujuzi Nchini katika Chuo cha Ufundi Don Bosco kilichopo mkoani Kilimanjaro.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu(Kazi,Vijana na Ajira) Mh. Anthony Mavunde akizungumza na vijana katika Chuo cha Ufundi Don Bosco kilichopo mkoani Kilimanjaro.

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU WALIOTEULIWA KUGOMBEA UDIWANI KATIKA KATA 43 ZITAKAZOFANYA UCHAGUZI MDOGO TAREHE 26 NOVEMBA, 2017

$
0
0
Tarehe 26 Oktoba, 2017, Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilifanya Uteuzi wa Wagombea Udiwani kwa ajili ya Uchaguzi Mdogo katika Kata 43 zilizopo kwenye Halmashauri 36 za Tanzania Bara unaotarajiwa kufanyika tarehe 26 Novemba, 2017.

Jumla ya Wanachama Wagombea 177 wa vyama mbalimbali walichukua Fomu ya Uteuzi Na. 8C na Fomu ya Maadili ya Uchaguzi Na. 10, kati yao 174 sawa na asilimia 92.7 ni wanaume na 13 sawa na asilimia 7.3 ni wanawake.

Jumla ya Wanachama 155 sawa na asilimia 87.6 ya waliochukua fomu za Uteuzi walizirejesha na kuteuliwa kuwa Wagombea ambapo 145 sawa na asilimia 93.6 ni Wanaume na Wagombea 10 sawa na asilimia 6.4 ni Wanawake.

Hadi muda wa mwisho wa Uteuzi ulipofika saa 10.00 jioni jumla ya Wanachama 22 sawa na asilimia 12.4 ya waliochukua fomu hawakuteuliwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kutorudisha fomu, kurudisha fomu nje ya muda uliotakiwa kisheria na fomu kutojazwa ipasavyo.

Vyama 13 vimesimamisha Wagombea na idadi ya Kata kwa kila Chama ni kama ifuatavyo: ACT-Wazalendo Wagombea 18 (sawa na asilimia 40), ADA-TADEA Mgombea 1 (sawa na asilimia 2), ADC Wagombea 4 (sawa na asilimia 7), CCM Wagombea 43 (sawa na asilimia 100) CHADEMA Wagombea 42 (sawa na asilimia 98), CHAUMA Mgombea 1 (sawa na asilimia 2), CUF Wagombea 30 (sawa na asilimia 70), DP Wagombea 3 (sawa na asilimia 5), NCCR-MAGEUZI Wagombea 6 (sawa na asilimia 16), NRA Wagombea 2 (sawa na asilimia 5), SAU Wagombea 2 (sawa na asilimia 5), TLP Mgombea 1 (sawa na asilimia 2) na UDP asilimia 2 (sawa na asilimia 5).

Aidha jumla ya Wagombea 30 sawa na asilimia 19.4 ya Wagombea walioteuliwa waliwekewa pingamizi na Wagombea wenzao na Msajili wa Vyama vya Siasa kutokana na sababu mbalimbali. Kwa mujibu wa Ratiba ya Uchaguzi Kampeni za Uchaguzi tayari zimeanza na zitaendelea hadi tarehe 25 Novemba, 2017 ikiwa ni siku moja kabla ya Siku ya Uchaguzi.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi inavikumbusha Vyama vya Siasa na Wagombea wao kuwa vinapaswa kuzingatia Maadili ya Uchaguzi wa Rais Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2015 wakati wote wa Kampeni na hata Siku ya Uchaguzi. Taarifa zaidi kuhusu walioteuliwa na vyama vyao inapatikana kwenye tovuti ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi. www.nec.go.tz na NEC ONLINE TV-TANZANIA.

Imetolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi tarehe 31 Oktoba, 2017.

INTRODUCING MAHABUBA - NANDY & ASLAY


MICHUZI TV: RAIS MAGUFULI AWAASA WASOMI KUTUMIA ELIMU ZAO KWA MANUFAA YA TAIFA

RAIS MAGUFULI: HATUWEZI KUWA NA TAIFA LA WATU AMBAO HAWANA AJIRA

WAKULIMA WILAYA YA CHATO WAFURAHIA KUPATA MBEGU BORA KUTOKA COSTECH

$
0
0
Na Dotto Mwaibale, Chato

WAKULIMA Wilaya Chato mkoani Geita wamefurahia mbegu bora ya mihogo, mahindi na viazi lishe waliopewa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) ili kuanzisha mashamba darasa ya mbegu hizo na kuzisambaza kwa wakulima wengine katika maeneo mengine.

Wakizungumza wilayani hapa leo kwa nyakati tofauti wakati wa uzinduzi wa mashamba darasa ya mbegu hizo katika vijiji vya Kibehe, Ipandikilo, Kitongoji cha Kaseni, Kijiji cha Itale na Bukiliguru kilichopo Kata ya Bwanga walisema mbegu hizo walizokabidhiwa na COSTECH kwa kushirikiana na Jukwaa la Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo ni mkombozi kwao.

Ofisa Kilimo wa Kata ya Kachwamba,  Hamisi  Matesi alisema Costech kuwapelekea wakulima mbegu hizo itawasaidia sana kupata chakula wananchi wa kata hiyo ziada watauza.

Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Ipandikilo, Clara Fidelis akizungumza kwa niaba ya wananchi wa kijiji hicho alisema wakulima walikuwa wakipata mavuno machache ya mahindi na mihogo kwa kuwa hawakuwa na mbegu bora hivyo baada ya kufunguliwa kwa shamba darasa la mbegu hizo katika maeneo yao wanategemea kupata mazao mengi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Chato, Mhandisi Joel Hari aliwataka wananchi hao kutambua kuwa mpango huo wa serikali ya awamu ya tano unawategemea sana wakulima katika kilimo hivyo fursa hiyo walioipata ya kupelekewa mbegu hizo wasiipoteze.

“Hakikisheni  mbegu hizi bora za mihogo mnazopewa mnazitunza  ili kutoa nafasi kwa wananchi wengi zaidi kujifunza mbinu bora za kilimo hiki kupitia shamba darasa hili ili kila mkazi wa Chato aweze kulima na kuzalisha kwa tija” alisema Mhandisi Hari.
 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi na Viumbe Hai wa COSTECH, Dk.Bakari Msangi (kushoto), kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), akimkabidhi mbegu ya viazi lishe kwa ajili ya shamba darasa la Kijiji cha Kibehe, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Mhandisi Joel Hari wakati wa uzinduzi wa shamba hilo wilayani Chato leo. 
 Wanakikundi cha Umoja cha Kijiji cha Kibehe kilichopo Kata ya Kigongo wakiandaa shamba lao la mbegu.
 Wanakikundi cha Umoja cha Kijiji cha Kibehe kilichopo Kata ya Kigongo wakiwa kwenye uzinduzi wa shamba darasa la viazi lishe na mihogo.
 Mtafiti wa Mazao ya Mizizi wa Wilaya ya Chato, Monica Mulongo akizungumzia vitamini A inayopatikana kwenye viazi lishe ambayo ni muhimu kwa watoto.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

SPIKA NDUGAI MGENI RASMI KATIKA UFUNGUZI WA MAONESHO YA MAADHIMISHO YA JUBILEE YA MIAKA 90 YA KANISA KUU LA ROHO MTAKATIFU, DAYOSISI YA CENTRAL TANGANYIKA

$
0
0
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katika) akikata utepe wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Maadhimisho ya Jubilee ya Miaka 90 ya Dayosisi ya Central Tanganyika (DCT) yaliyofanyika leo katika Viwanja vya kanisa kuu la Roho Mtakatifu Mjini Dodoma. wa tatu kulia ni Askofu wa Dayosisi hiyo, Dkt. Dickson Chilongani. Spika wa Bunge, alikuwa mgeni rasmi katika Maonesho hayo.


Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akizungumza na waumini wa kanisa kuu la Roho Mtakatifu, Dayosisi ya Central Tanganyika (DCT) wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Maadhimisho ya Jubilee ya Miaka 90 ya Dayosisi ya Central Tanganyika (DCT) yaliyofanyika leo katika Viwanja vya kanisa hilo Mjini Dodoma. Spika wa Bunge, alikuwa mgeni rasmi katika Maonyesho hayo.
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC), Mheshimiwa Albert Obama akiongoza kikao cha pamoja kati ya kamati hiyo na watendaji kutoka kituo cha zana za kilimo na Teknolojia Vijijini (KAMATEC) wakati wakipokea, kujadili na kuchambua taarifa ya Msajili wa Hazina kuhusu uwekezaji na utendaji wa KAMATEC kilichofanyika leo Mjini Dodoma.




Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati) akizungumza na Wajumbe wa kamati ya fedha kutoka Bunge la Ghana, katika kikao cha kubadilishana uzoefu katika utendaji wa kazi kilichofanyika leo ofisini kwake Mjini Dodoma. wa pili kushoto ni kiongozi wa msafara na Mwenyekiti wa Kamati ya fedha kutoka Bunge la Ghana, Mheshimiwa Dkt. Mark Yeboah na wanne kulia ni katibu wa Bunge, Ndg. Stephen kagaigai




Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wa pili kulia) akimsikiliza kiongozi wa msafara na Mwenyekiti wa Kamati ya fedha kutoka Bunge la Ghana, Mheshimiwa Dkt. Mark Yeboah (wa pili kushoto) wakati wa kikao na wajumbe wa kamati ya fedha kutoka Bunge la Ghana, kikilenga kubadilishana uzoefu katika utendaji wa kazi kilichofanyika leo ofisini kwake Mjini Dodoma. kulia ni katibu wa Bunge, Ndg. Stephen kagaigai
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia) akipatiwa maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wa kanisa kuu la Roho Mtakatifu, Dayosisi ya Central Tanganyika, Ndg. Grace Lisasi (katikati) alipotembelea Banda la Umoja wa Wanawake wa Kikristo (UWAKI) wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Maadhimisho ya Jubilee ya Miaka 90 ya Dayosisi ya Central Tanganyika (DCT) yaliyofanyika leo katika Viwanja vya kanisa hilo Mjini Dodoma. Spika wa Bunge, alikuwa mgeni rasmi katika Maonesho hayo.

PICHA NA OFISI YA BUNGE

SERIKALI YAWASILISHA MUSWADA WA SHERIA YA WAKALA WA MELI WA TAIFA

$
0
0
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imewasilisha Muswada wa Sheria ya Wakala wa Meli Tanzania mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kwenye kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni mjini Dodoma.

Muswada huo umewasilishwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye kwa niaba ya Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Prof. Makame Mbarawa. Wakati akiwasilisha Muswada huo, Mhandisi Nditiye alisema kuwa Muswada huu unapendekeza kutungwa kwa Sheria itakayoanzisha Shirika la Uwakala wa Meli ambalo pamoja na majukumu mengine litakuwa na jukumu la kutoa huduma ya uwakala wa meli na kudhibiti huduma za usafiri na usalama wa vyombo vya majini.

Ameongeza kuwa, Muswada huu utaweka mfumo madhubuti wa uendeshaji wa biashara ya uwakala wa meli na udhibiti wa huduma za usalama wa usafiri wa meli hivyo utaimarisha udhibiti wa sekta ndogo ya usafiri wa meli na kuifanya sekta hii kuchangia vyema katika uchumi na kuongeza pato la Taifa. Muswada huu ni moja ya jitihada za Serikali za kuhakikisha kuwa taasisi zake zinajiendesha kwa faida, kibiashara, kwa ushindani na kutoa gawio kwa Serikali ili iweze kuhudumia wananchi kwa kujenga miundombinu ya kisasa na kuwapatia wananchi huduma mbali mbali za kijamii.

Mhandishi Nditiye aliyataja majukumu ya Shirika kuwa ni pamoja na uhakiki wa shehena inayoingia na kutoka kupitia bandari za Tanzania, uondoshaji shehena za madini, makinikia, wanyama hai, nyara za Serikali, na bidhaa zinazotokana na madini na udhibiti wa watoa huduma katika sekta ndogo ya usafiri majini, usalama wa meli na mazingira ya bahari. 
Naibu Waziri wa Sekta ya Uchukuzi na Mawasiliano wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Atashasta Nditiye (mwenye koti) akifuatilia majadiliano baada ya kuwasilisha Muswada wa Sheria ya Wakala wa Meli wa Taifa mbele ya Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Miundombinu kwenye kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni mjini Dodoma. Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Prof. Norman Sigalla King (katikati) akichangia maoni yake kuhusu Muswada huo. Wa kwanza Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Selemani Kakoso.
Mjumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Bandari Tanzania Mzee Renatus Mkinga (aliyesimama) akitoa maoni yake mbele ya Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Miundombinu kuhusu Muswada wa Sheria ya Wakala wa Meli wa Taifa kwenye kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni mjini Dodoma. Naibu Waziri wa Sekta ya Uchukuzi na Mawasiliano wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Atashasta Nditiye (mwenye koti) akifuatilia majadiliano hayo na wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Prof. Norman Sigalla King.
Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Miundombinu Mhe. Rukia Kassim akichangia maoni yake kuhusu Muswada wa Sheria ya Wakala wa Meli wa Taifa mbele ya Kamati hiyo na wadau wa sekta ndogo ya usafiri wa majini kwenye kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni mjini Dodoma.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

SERIKALI YATUMIA BILIONI 514 KUMALIZA TATIZO LA MAJI JIJINI ARUSHA

$
0
0
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa kushirikiana na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Jijini Arusha (AUWSA), leo imeingia mikataba ya Dola za Marekani 233,915,581 ambazo ni takribani Shilingi 514,614,278,200 za Tanzania kumaliza kabisa tatizo la maji katika Jiji la Arusha na Wilaya ya Hai, Mkoani Kilimanjaro.

Fedha hizo ni mkopo wa masharti nafuu kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) ambao wamechangia Dola za Marekani 210,962,581 na Serikali ya Tanzania ikichangia Dola 22,953,000 ili kukamilisha mradi huo.

Kazi zitakazotekelezwa ni uchimbaji wa visima virefu, ujenzi wa matenki, ulazaji wa mabomba ya majisafi na majitaka, ujenzi wa mtambo wa kutibu maji, ujenzi wa mabwawa mapya ya kutibu majitaka, ujenzi wa Makao Makuu ya Mamlaka na Ofisi za Kanda pamoja na ununuzi wa vitendea kazi.

Kukamilika kwa mradi huu kutawezesha upatikanaji wa huduma ya majisafi na salama kwa wakazi wa Jiji la Arusha kwa asilimia 100 hadi mwaka 2030 na kutapunguza kiasi cha maji yanayopotea kutoka asilimia 45 ya sasa mpaka kufikia asilimia 20. Aidha, mradi utaongeza mtandao wa kuondoa majitaka kwa asilimia 30. Mradi huu unategemea kuchochea ukuaji wa uchumi wa viwanda na kuboresha huduma nyingine za kijamii zikiwemo Afya na Elimu.

Hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Jijij la Arusha kwa sasa ni asilimia 44, sawa na wastani wa lita milioni 40 kwa siku na mradi huu unategemea kuongeza kiwango na kufikia lita milioni 200 kwa siku.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (AUWSA), Mhandisi Ruth Koya wakipeana mikono na Mkandarasi-Kampuni ya Jiangxi Geo-Engineering ya China, Chen Xianghua mara baada ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa mradi wa kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira kwa Jiji la Arusha.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (AUWSA), Mhandisi Ruth Koya akisaini mkataba wa utekelezaji wa mradi wa kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira kwa Jiji la Arusha, kushoto ni Mkandarasi kutoka Kampuni ya Jiangxi Geo-Engineering ya China, Chen Xianghua wanaotekeleza mradi huo.
Sehemu ya wageni waliohudhuria hafla ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa mradi wa kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira kwa Jiji la Arusha.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (AUWSA), Mhandisi Ruth Koya (kushoto), Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Gabriel Daqarro (katikati) na Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe katika hafla ya kusaini wa mkataba wa utekelezaji wa mradi wa kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira kwa Jiji la Arusha.Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe akizungumza katika hafla ya kusaini wa mkataba wa utekelezaji wa mradi wa kuboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira kwa Jiji la Arusha.

MAGAZETI YA JUMATANO LEO NOVEMBA MOSI,2017

BASHE FANYA MKUTANO NA WANANCHI WAKE,AUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS DKT MAGUFULI KATIKA KUSIMAMIA RASIMALI,KUFUNGA MIANYA YA RUSHWA NA KURUDISHA NIDHAMU YA KAZI KWA WATUMISHI WA UMMA

$
0
0


Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini Mhe. Hussein Mohammed Bashe amekua na mkutano wa wazi na wananchi uliojikita katika kuelezea mafanikio na changamoto za miaka miwili ya kipindi cha ubunge wake.

Aidha Malengo makubwa ya mkutano huo yalikuwa ni:
1. Kusikiliza na kutatua kero za wananchi kwa uwazi ili kuongeza nafasi ya ushiriki na ushirikishwaji wa wananchi katika mijadala ya maendeleo.

2. Kueleza juhudi za kuleta maendeleo zilizokwishafanywa na Ofisi ya Mbunge katika kipindi cha miaka miwili (2)

3. Kutambulisha miradi mikubwa ya Elimu, Afya na Maji inayoendelea ndani ya Jimbo la Nzega Mjini;
Elimu
- Ujenzi wa Shule ya kwanza ya wanawake
- Utoaji wa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi wote wanaofaulu Jimboni kupitia Bashe Scholarship Awards 
- Ugawaji wa Vifaa vya shule na madaftari 37,000 
- Ujenzi wa Shule ya Kwanza ya Kidato cha Tano na Sita 
- Ujenzi wa zaidi ya vyumba vya madarasa 32 ya Shule za Msingi  kwenye kata 10 jimboni


 Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini Mhe. Hussein Mohammed Bashe akiwahutubia wananchi jimboni kwake katika mkutano wa wazi na wananchi,Mh Bashe alijikita katika kuelezea mafanikio na changamoto za miaka miwili ya kipindi cha ubunge wake.

 Baadhi ya Wananchi wa Nzega wakimsikiliza Mbunge wao,Mh Bashe alipokuwa akiwahutubia katika mkutano wa wazi.

PPF KANDA YA MASHARIKI WATOA ELIMU YA MWONGOZO WA MAFAO KWA VIONGOZI NA WASIMAMIZI WA SEHEMU ZA KAZI KUTOKA TAASISI BINAFSI, AFYA NA ZA ULINZI

$
0
0
Na John Nditi, Morogoro

MFUKO wa Pensheni wa PPF umedhamiria  kuwafikia na kuandikisha wanachama kutoka sekta rasmi na isiyo rasmi wakiwemo vijana ili baada ya kustaafu wabaki katika maisha mazuri  ya uzeeni.

Meneja wa Mfuko wa PPF Kanda  ya Mashariki inayojumisha mkoa wa Morogoro na Tanga ,Joseph Fungo  alisema hayo Oktoba 30, 2017  wakati akitoa mafunzo na elimu kuhusu Mwongozo wa mafao ya mfuko huo kwa baadhi ya wasimamizi wa kazi kwa niaba ya waajiri katika taasisi  binafsi zinazotoa huduma ya Afya , pamoja na za Ulinzi zilizopo Manispaa ya Morogoro. 

Alisema  ,watanzania wengi wanauelea mdogo kuhusu  sheria ya Mfuko wa hifadhi ya jamii , hivyo ni jukumu la Mfuko wa PPF  kuendelea kutoa  elimu   iwafikie kundi kubwa  waweze uelewa sheria hiyo na hatimaye wajiunge na  Mfuko wa PPF kunifaika na mafao mbalimbali yaoyoewayo kwa faida yao. Hivyo aliwataka vijana waliopo katika  ajira rasmi na zisizo rasmi kuwekeza fedha zao kwenye mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Pensheni wa PPF  ili  baada ya kustaafu  waweze  kunufaika na mafao yao yatakayowaweka wabakie katika maisha mazuri  ya uzeeni.

Fungo  alitaja baadhi ya mafao  hayo , ni la uzeeni , mafao ya elimu ,  wategemezi , ugonjwa , uzazi , kifo na mafao ya kiinua mgongo  na sifahitajika  kwa ajili ya kuweza kunufaika na mafao hayo. Kuhusu Mfumo  wa Wote Scheme  alisema , umelenga kwa wananchi wasio kwenye sekta rasmi wakiwemo wajasiriamali kwa kutoa  fursa ya kujiunga na mfuko  huo.

 Alisema , wanachama wa kundi hilo watanufaika  na  mafao mbalimbali ikiwemo huduma za matibabu, mikopo ya elimu, maendeleo na mafao ya uzeeni. Meneja wa Mfuko wa PPF Kanda  ya Mashariki alisema, kila mwanachama atapaswa kuchangia kiasi kisichopungua Sh 20,000 kwa mwezi na kuwasilisha michango kadri awezavyo kwa kutegemeana na makubaliano.


Nao washiriki hao  waliupongeza uongozi wa PPF Kanda hiyo kwa kuona umuhimu wa kutoa  elimu kwao ambayo imewapa uelewa mpana kuhusu faida ya mwajiri na mfanyakazi pindi anapojiunga  kwenye  mfuko wa Pensheni kwa ajili ya manufaa  yao wakati wa   uzeeni.
Meneja wa Mfuko wa PPF Kanda ya Mashariki inayojumisha mkoa wa Morogoro na Tanga ,Joseph Fungo ( kulia) akimkabidhi cheti Sista Edna Mpilimba ( kushoto).ambaye ni msimamzi wa Shule za Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro baada ya kushiriki mafunzo yaliyoandaliwa na Mfuko huo oktoba 30, 2017 kwa viongozi na wasimamizi sehemu za kazi wa Taasisi binafsi za Afya , na za Ulinzi zilizopo Manispaa ya Morogoro.
Meneja wa Mfuko wa PPF Kanda ya Mashariki inayojumisha mkoa wa Morogoro na Tanga ,Joseph Fungo ( kulia) akimkabidhi cheti Mussa Msongamwanja ( kushoto) wa Kampuni ya Ulinzi ya SAKI baada ya kushiriki mafunzo yaliyoandaliwa na Mfuko huo Oktoba 30, 2017 kwa viongozi na wasimamizi sehemu za kazi wa Taasisi binafsi za Afya , na za Ulinzi zilizopo Manispaa ya Morogoro.
Baadhi ya viongozi na wasimamizi sehemu za kazi kutoka Taasisi binafsi za Afya ,na za Ulinzi zilizopo Manispaa ya Morogoro wakisikiliza kwa makini Meneja wa Mfuko wa PPF Kanda ya Mashariki inayojumuisha mkoa wa Morogoro na Tanga , Joseph Fungo Oktoba 30, 2017 alipokuwa wakitoa mafunzo ya elimu ya Mwongozo wa mafao ili kuwawezesha wafanyakazi kujiunga na mafao yanayotolewa na Mfuko huo. 
Baadhi ya viongozi na wasimamizi sehemu za kazi kutoka Taasisi binafsi za Afya , na za Ulinzi zilizopo Manispaa ya Morogoro wakiwa pamoja na Uongozi wa Mfuko wa Pensheni Kanda ya Mashariki inayojumuisha mkoa wa Morogoro na Tanga ,Oktoba 30, 2017 baada ya kumalizika kupatiwa mafunzo na elimu ya Mwongozo wa mafao ili kuwawezesha wafanyakazi wao kujiunga na mafao yanayotolewa na Mfuko huo.( Picha zote na John Nditi, Globu ya Jamii - Morogoro).

WILAYA YA CHATO YATAKIWA KUSIMAMIA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO

$
0
0
Mhandisi Robert Gabriel Lughumbi Mkuu wa Mkoa wa Geita amewataka Viongozi wa Serikali Wilayani Chato kusimamia na kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo Wilayani humo ili thamani ya fedha zinazotolewa ionekane. 

Akizungumza baada ya kuwasili wilayani Chato kwa mara ya kwanza tangu kuteuliwa kwake kuwa Mkuu wa Mkoa, amesema kuwa umefika wakati watendaji kuacha tabia ya kukaa Ofisini bali waende maeneo mbalimbali ya Wilaya ambapo kunatekelezwa miradi ili kusimamia kwa karibu miradi inayoendelea. 

" Wananchi wanatakiwa kusimamiwa ata kama fedha ni za kwao ili kuweka miradi katika ubora unaotakiwa"Alisisitiza Lughumbi. Aidha, alimuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chato kuhakikisha wananchi wanakuwa katika vikundi ili vishiriki katika ujenzi na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika vijiji kwa kuchangia michango midogo midogo kama vile kutafuta mawe, kokoto, mchanga. Kazi kubwa ya Halmashauri ni kuhakikisha wahandisi wanasaidia kupeleka michoro na kusimamia ujenzi wa miradi ya Zahanati na madarasa katika vijiji husika. 

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Chato kufuatilia ujenzi wa Bweni la wanafunzi shule ya Sekondari Jikomboe ambalo limegharimu kiasi cha Shilingi milioni 75 ili kujiridhisha kama fedha hizo zimetumika kama ilivyokusudiwa na kuona kama thamani yake inaonekana. 

Akiwa Wilayani Chato Mheshimiwa Robert Gabriel ametembelea shule ya Msingi Chato na kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa sita na vyoo, ujenzi wa Zahanati ya kijiji Mganza, ujenzi wa Bweni shule ya Sekondari Zakia Meghj pamoja na Ujenzi wa Soko la dagaa Kasenda na kuagiza takukuru kufika katika miradi hiyo ili kufuatilia matumizi ya fedha katika miradi ya Zahanati, Bweni na madarasa. 

Vilevile Mkuu wa Mkoa ametembelea ujenzi wa uwanja wa ndege wa Chato na kupongeza jitihada za utekelezaji wa mradi huo zinazoendelea kwa kufikia asilimia 63. Awali Meneja wa Tanroads Mkoa wa Geita Mhandisi Haruna Senkuku alimweleza Mkuu wa Mkoa kuwa uwanja huo una Run way ya Kilometa 3 ambapo hadi kukamilika mradi utagharimu kiasi cha shilingi Bilioni 39. 
Utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa uwanja wa ndege Chato ukiendelea.
Mhandisi Robert Gabriel Lughumbi Mkuu wa Mkoa wa Geita akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na Wilaya ya Chato baada ya kuwasili Wilayani Chato.Wakwanza kulia ni Mbunge wa Chato pia ni waziri wa Nishati Mheshimi Dkt Medard Kalemani. 
Meneja wa Tanroads Mkoa wa Geita Mhandisi Haruna Senkuku akifafanua jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel Lughumbi wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa Uwanja wa ndege Chato alipotembelea na kujionea ujenzi katika moja kati ya ziara yake ya kikazi Wilayani Humo.
Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita akiongoza viongozi katika ukaguzi wa ujenzi wa uwanja wa ndege Chato.
Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita akitoa maelekezo wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa uwanja wa ndege Chato.(PICHA NA MAGESA JUMAPILI AFISA HABARI MKOA WA GEITA)

Taasisi ya kijamii ya The Desk and Chair Foundation yatoa msaada wa kisima cha maji jijini Mwanza

$
0
0
 Na David John Mwanza .

TAASISI ya kijamii ya The Desk and Chair Foundation ya jijini Mwanza imetoa rai kwa Serikali kuwa na mawasiliano ya karibu ili kujuwa changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo watanzania hususani wenye uhitaji maalum.

Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi Ofisini kwake jijini hapa Mwakilishi mkazi wa Taasisi hiyo hapa nchini yenye Makao yake Makuu nchini Uingereza Sibtain P.L Maghjee amesema kuwa taasisi yake inashughulika na matatizo ya watu hususani walemavu na hata jamii kwa ujumla.

Amesema kuwa changamoto kubwa wanayokutana nayo ni kukosekana kwa mawasiliano ya karibu kutoka Serikali ili kupata takwimu za watu au jamii yenye uhitaji. " Taasisi yetu imekuwa ikifanya kazi nyingi katika jamii ikiwamo kuchimba Visima pamoja na kusaidia Ambulence kwa ajili ya wagonjwa katika vituo vya afya. mbalimbali hapa nchini na zaidi vijijini "amesema Meghjee

Akizungumzia zaidi taasisi hiyo amesema mbali na huduma hizo lakini pia wamekuwa wakitoa mafunzo mbalimbali ya ufundi, wa aina mbalimbali kwa vijana ambapo mwisho wa siku wanajiajiri wenyewe. Amesema kuwa wao kama taasisi pia wanatengeneza Ambulence kwa kutumia mafundi hao ambao wanafundishwa kupitia Kalakana yao iliyopo Greenview eneo la Ghana jijini hapa.

Pia akizungumzia misaada wanayoitoa amewataka wananchi kutunza miundombinu hiyo hususani visima ambavyo wanakabidhiwa katika mikoa mbalimbali hapa nchini na kuvithamini. " Unajuwa Ndugu mwandishi lazima watu wajenge nidhamu ya kutunza na kuthamini vitu ambavyo wanapewa kwani kufanya hivyo kunawapa moyo hata watu wanaotoa. "amesema.

Amesema licha ya uchimbaji wa visima hivyo lakini pia taasisi imekuwa ikifanya mambo mbalimbali tangu kuazishwa kwaks mwaka 1979 hapa nchini na wametengeneza basikeli 30 kwa ajili ya walemavu ambazo zitakabidhiwa hivi karibuni.
Mwakilishi mkazi wa Shirika la The Desk and  Chair Foundation  Sbtain P.L Meghjee  (shati la drafti) akikabidhi kisima katika moja ya maeneo ambayo wametoa huduma hiyo hapa nchini . 
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live




Latest Images