Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110105 articles
Browse latest View live

JUMIA TANZANIA WAZINDUA KAMPENI YA SIKU YA BLACK FRIDAY KWA MIKOA SITA

$
0
0
Ikiwa imebaki takribani miezi miwili mwaka 2017 kuisha, Jumia Tanzania imejizatiti kuja na kampeni iliyopewa jina la ‘BLACK FRIDAY’ ambayo itawawezesha wateja wake kufanya manunuzi ya bidhaa mbalimbali mtandaoni kwa punguzo la mpaka alisimia 70 kuanzia Novemba 24 mpaka Desemba 4 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ujio wa kampeni hiyo Meneja Mauzo wa Jumia Tanzania, Bw. Idd Mkumba amebainisha kuwa kutokana na mafanikio makubwa ya kampeni hiyo iliyofanyika mwaka jana na kushuhudia watanzania wakifanya huduma za mtandaoni ambapo takribani oda 600 kwa siku wameona ni vema kuirejesha tena kwa kishindo mwaka huu.

“Mwaka 2016 ulikuwa ni wenye mafanikio kwa upande wa kampeni yetu ya BLACK FRIDAY kwani ndani ya muda wa siku tano tuliyoifanya wateja wengi waliweza kufanya manunuzi mtandaoni. Hivyo basi kwa mwaka huu tena tumeiboresha Zaidi kwa kuongeza siku kutoka tano mpaka 11 ambapo kampeni itaanza rasmi kuanzia Novemba 24 mpaka Desemba 4. 

Na kwa kuongezea hapo ni kwamba safari hii wateja wa Dar es Salaam hawatofaidika pekee yao kwani tumejitanua Zaidi mpaka mikoa mingine kwa mara ya kwanza na kuzifikia sehemu za Visiwani Zanzibar, Dodoma, Mwanza, Morogoro, Arusha, Kilimanjaro, Iringa na Musoma,” alisema Bw. Mkumba.

Meneja Mauzo huyo wa Jumia Tanzania aliendelea kwa kufafanua kuwa, “Lengo kubwa la kampeni hii ni kuhakikisha kwamba tunawajengea uwezo na kuwarahisishia watanzania kufanya huduma mbalimbali kwa njia ya mtandao mahali popote walipo huku wakiendelea na shughuli zao. 
Meneja Mauzo wa Jumia Tanzania, Iddy Mkumba akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa Black Friday utakaoweza kutoa punguzo la asilimia 70 kwa bidhaa atakayoinunua mteje kupitia tovuti ya Jumia Tanzania  itakayoanza mwezi wa Novemba 24 hadi Desemba 04 mwaka huu kwa mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Iringa, Mwanza,Morogoro, Mara na Zanzibar.
Afisa Masoko na Mahusiano ya Jamii wa Jumia Travel, Geofrey Kijanga, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Jumia Travel inavyotoa huduma za malazi na namna walivyopunguza bei kwa msimu huu wa sikukuu leo kwenye ofisi za Jumia Tanzania jijini Dar Es Salaam
Mkutano ukiendelea kwenye ukumbi wa ofisi ya Jumia Tanzania jijini Dar es Salaam leo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

TAARIFA YA MATENGENEZO YA DHARURA KITUO CHA KUZALISHA UMEME CHA KINYEREZI I

$
0
0
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu Wateja wake kuwa Wataalamu wetu wanafanya matengenezo ya dharura katika Mfumo wa kupokea gesi kwenye kituo cha kuzalisha umeme kwa njia ya gesi asilia cha Kinyerezi I.

Hivyo Kituo kitazimwa Saa 6:00 mchana hadi Saa 7:00 Mchana ili kupisha matengenezo. 

Baadhi ya maeneo mbalimbali ya nchi katika kipindi hicho yatakosa umeme.
Tunawaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza. 
Tafadhali usishike wala kukanyaga waya uliokatika au kuanguka.

Toa taarifa kupitia namba za simu zifuatazo
Kituo cha miito ya simu Makao Makuu 0222194400 na 0768 985100

Tovuti: www.tanesco.co.tz
Mitandao ya Kijamii
www.facebook/tanescoyetultd /twitter.com/tanescoyetu


Imetolewa na:- 
Ofisi ya Uhusiano

TANESCO Makao Makuu

31/10/2017

SHIRIKA LA HAKI ELIMU YASHIRIKIANA NA JAMII KUTATUA CHANGAMOTO ZA ELIMU.

$
0
0

Na Pamela Mollel-Arusha


Shirika lisilo la kiserikali nchini Haki Elimu limetoa shilingi milioni ishirini ya kuanzishwa kwa ujenzi wa kisima cha maji katika shule ya sekondari mukulat katika kijiji cha lemanyata kata ya lemanyata wilaya ya arusha vijijini ili kuwaondolea adha wanafunzi i wa shule hiyo wanaolazimika kusafiri umbali mrefu na kutumia muda mwingi  kwakutafuta maji.


Akizungumza katika maadhimisho ya wiki ya huduma kwa jamii iliyoambatana na uapandaji wa miti na utunzaji wa mazingira katika shule ya sekondari ya Mukulat Mkurugenzi wa haki elimu nchini john kalaghe amesema shirika la haki elimu limeamua kushirikiana na jamii katika kuondoa changamoto katka sekta ya elimu katika shule hiyo ikiwamo tatitzo la maji pamoja na kuboresha mazingira kwa kupanda miti pamoja na kukarabati majedarasa hayo kwa kupiga rangi.


Shirika hilo la haki elimu kwa kupitia kwa mkurugenzi huyo wameahidi kutoa ufadhi kwa kuwalipia karo wanafunzi wa shule ya sekondani ya mukulat  watakaofanya vizuri kwa ufaulu wa daraja la kwanza katika mtihani wa kidato cha nne unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni ili kutoa hamasa kwa wanafunzi wengine kufanya vizuri katika mitihni hasa kwa mtoto wa kike ambaye anaonekana yuko nyuma kwa mambo ya elimu hasa katika jamii ya kifugaji.


Akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi wa halmashauri ya wilaa ya Arusha vijijini katika maadhimisho ya wiki ya huduma kwa jamii  ,afisa elimu wa wilaya hiyo B akari kimath amelipongeza shirika la haki elimu kwa kuanzisha mradi wa maji katika shule hiyo pamoja na upandaji wa miti na ukarabati wa madarasa na amesema miradi hiyo itapunguza changamoto za elimu zinazozikabili shule za msingi na sekndari wilayani humo na kuliomba shirika hilo kuendela na msaada huo katika shule zilizoko pembezoni mwa wilaya ili kuwawezesha wanafunzi kupata elimu bora.


 Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la  Haki Elimu nchini John Kalage akipanda mti katika maadhmisho ya wiki ya huduma kwa jamii iliyoambatana na upandaji wa miti na utunzaji wa mazingira katika shule ya sekondari ya Mukulat iliyopo Mkoani Arusha shughuli iliyohudhuriwa na wafanyakazi wa shirika hilo ,wazazi na wadau wa elimu jana (Habari Picha Na Pamela Mollel,Arusha)

 Wafanyakazi wa shirika la Haki Elimu nchini wakiongozwa na Mkurugenzi wao John Kalage wa tatu kushoto, wakichimba shimo kwaajili ya kuhifadhi taka ngumu katika shule ya Sekondari Mukulat katika maadhimisho ya wiki ya huduma kwa jamii.
  Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la  Haki Elimu nchini John Kalage akipongezwa na Mkuu wa shule hiyo Vitalis Nada mara baada ya kumaliza zoezi la upandaji miti katika shule hiyo jana.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

RC DKT NCHIMBI ATOA MWEZI MMOJA KWA HALMASHAURI YA IRAMBA KUJENGA VYOO KATIKA MNADA WA MALENDI.

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amempa mwezi mmoja Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Iramba, kujenga vyoo bora katika Mnada uliopo Kijiji cha Malendi, kata ya Mgongo Wilayani humo.

Dkt Nchimbi ametoa agizo hilo mara baada ya kutembelea mnada huo ambapo wananchi wamelalamika kukosa huduma za vyoo na maji kwa kipindi kirefu huku halmashauri ikikusanya ushuru bila kuwaboreshea miundombinu ya mnada huo.

“Mkurugenzi nakupa mwezi mmoja hapa kuwe na vyoo bora vikiwa na matundu sita kwa ajili ya wananchi hawa pamoja na huduma za maji, kipindi cha mvua kinaanza, lazma muwajali wananchi hawa kwakuwa kipindupindu kinaweza kulipuka hapa”, ameeleza Dkt Nchimbi.

Ameongeza kuwa kwakuwa hakuna vyoo wananchi watajisaidia maeneo ya jirani na mnada na mvua zikianza zitatiririsha uchafu huo katika eneo la mnada na makazi ya wanakijiji cha Malendi na hivyo kusababisha mlipuko wamagonjwa hasa Kipindupindu.
 Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt Rehema Nchimbi akizungumza na wananchi waliokuwa wamepanga foleni kulipa ushuru katika mnada wa Malendi Wilayani Iramba.
 Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt Rehema Nchimbi akikagua mnada wa Malendi Wilayani Iramba ambapo amemuagiza Mkurugenzi wa halmashauri hiyo kuhakikisha anajenga vyoo na kufikisha huduma za maji ndani ya mwezi mmoja.

Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Malendi na maeneo ya jirani waliokuwa katika mnada huo wakinyoosha mikono kumsalimia Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi alipowatembelea mnadani hapo.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

ATHMANI ANAWAOMBA MSAADA WATANZANIA

$
0
0
Na Yeremias  Ngerangera, Namtumbo

Athmani  Amani  mkazi wa kijiji  cha Naikesi  kata ya kitanda  wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma  anawaomba  watanzania  kumsaidia  fedha  za kugharimia  matibabu  ya mtoto  wake  Shaziri  Athmani (12) anayesumbuliwa  na tatizo  la moyo kuwa  mkubwa.

Mtoto  Shaziri  Athamani  ni mwanafunzi  wa darasa  la nne  shule  ya msingi Naikesi  iliyopo  kata ya Kitanda  wilayani Namtumbo  awali  alikuwa anasumbuliwa  na kuvimba  miguu  hali iliyokuwa  inamkosesha  masomo  yake  darasani  mara kwa  mara kuanzia  mwaka  2016.
Mwaka  huo  huo  mwezi  Septemba  baba yake  alilazimika kumpeleka  Hospitali  ya Mkoa  Songea  kuangalia tatizo  la kuvimba  kwa  miguu  ya mtoto huyo  na  baada ya kupata  vipimo  wakashauriwa  kuenda  Hospitali  ya  Peramiho  .

Bwana  Athamani  alidai  kuwa  hakuwa  na fedha  za kumpeleka  mtoto  peramiho  kwa  kipindi  hicho  na badala yake  alirudi  naye  nyumbani  Naikesi  kwenda  kuuza  mifugo  lakini fedha hizo  hazikumwezesha  kukidhi  mahitaji  ya  kumtibu  mwanoa katika  Hospitali  ya  Peramiho  baada  ya  kufika  katika  Hospitali  hiyo  na kumaliza  fedha  yake  yote  aliyokuwa  nayo  katika  vipimo  pekee .

Baada  ya kupatiwa  vipimo  na  kubaini  Tatizo la  mwanae  alirudi  na mwanae  mpaka  kijijini  kwake  kujipanga  upya  kwa  ajili  ya  matibabu ya  mwanae  na  kujitahidi  kwa kile  anachokipata  anunue  dawa  kwa  ajili  ya  mwanae  huyo.

NKINGA AKUTANA NA WADAU KUPITIA RASIMU YA MFUMO JUMUISHI WA KITAIFA WA USIMAMIZI WA MASHAURI YA WATOTO

$
0
0
  Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bibi. Sihaba Nkinga akiwashukuru wadau wa masuala ya watoto wakati wa kikao na wadau hao kutoka Shirika la JSI kujadili Rasimu ya Mfumo Jumuishi wa Kitaifa wa Usimamizi wa Mashauri ya Watoto na Mwongozo wa Kitaifa wa Utambuzi wa Watoto Wanaoishi Katika Mazingira Hatarishi kilichofanyika katika Ukumbi wa Wizara ulipo UDOM Dodoma.
 Afisa Ustawi wa Jamii, Dkt. Philibert Kawemame akiwasilisha  kwa Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi. Sihaba Nkinga(wanne kushoto) Rasimu ya Mfumo Jumuishi wa Kitaifa wa Usimamizi wa Mashauri ya Watoto na Mwongozo wa Kitaifa waUtambuzi wa Watoto Wanaoishi Katika Mazingira Hatarishi katika kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Wizara ulipo UDOM Dodoma.
 Kaimu Kamishna wa Ustawi wa Jamii Bw. Rabikira Mushi akifafanua jambo kwa Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi. Sihaba Nkinga(kulia) kuhusu Rasimu ya Mfumo Jumuishi wa kitaifa wa Usimamizi wa Mashauri ya Watoto na Mwongozo wa Kitaifa wa Utambuzi wa Watoto Wanaoishi Katika Mazingira Hatarishi katika kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Wizara ulipo UDOM Dodoma.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA VIWANDA VIWILI JIJINI MWANZA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Waziri wa Viwanda na Biashara Charles Mwijage mara baada ya kufungua kiwanda cha Victoria molders and polybags kilichopo Igogo jijini Mwanza.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono mafundi wa Kiwanda cha Victoria molders and polybags mara baada ya kutengeneza Tanki la kuhifadhia maji.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia utengenezaji wa viti vya plastiki katika kiwanda cha Victoria molders and polybags katika eneo la Igogo jijini Mwanza.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia mfuniko uliotengenezwa katika kiwanda hicho cha Victoria molders and polybags Igogo jijini Mwanza.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Meya ya jiji la Mwanza James Bwire mara baada ya kufungua kiwanda cha Victoria molders and polybags Igogo jijini Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifungua kiwanda cha madawa cha  Prince Pharmaceuticals kilichopo Buhongwa nje kidogo jijini Mwanza. PICHA NA IKULU
 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi katika eneo la kona ya Butimba wakati akitokea Igogo jijini Mwanza.

 Wananchi wa Butimba na Mkuyuni wakifurahi wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akizungumza nao katika eneo la kona ya Butimba wakati akitokea Igogo jijini Mwanza. 

New students urged to make the most of their time at SUZA

$
0
0
Prof. Idris Rai (standing), the Vice Chancellor gives welcome remarks to new students

 Prof. Idris Rai, the SUZA Vice Chancellor informed the new students that SUZA tends to put students at the centre of everything it does so their experience at SUZA and their success is important to each and every SUZA community member. “Your arrival here marks a new chapter in the history of your life so do utilize to the maximum the opportunities built in your programmes at the University”, he added.

He informed the new candidates that Zanzibar in the past was the fulcrum of various disciplines of education for Eastern Africa region and now the State University of Zanzibar intends to reclaim this seemingly lost status through the candidates it admits by imparting to them the appropriate skills and knowledge.

Prof. Rai advised students to be more self-reliant as they will be responsible for what they do and that they will have to ensure that they do the work required for them to do. “There will be no one to check up on you, you are matured enough and accountable to yourself., make sure you attend your lectures, labs and tutorials, do the assignments and read the material advised by your lecturers and tutors also ensure that you make enough time for private study; develop a study plan; go to the library and use the on-line learning resources which are fortunately accessible at SUZA”, he insisted.
A cross-section of the newly admitted students for 2017/2018 academic year pay attention listening to instructions from the SUZA Management Team.

He then enlightened the new students that some of them who will manage to come out with flying colours in their studies may have the opportunities to pursue collaborative education abroad through partnerships which SUZA has engaged in with other higher learning institutions which enable SUZA students to spend at least one semester abroad.


MAHAKAMA YAMKUTA "SCORPION" NA KESI YA KUJIBU

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii.

Mahakama ya Wilaya ya Ilala imemkuta mshtakiwa Salum Njwete, maarufu kwa jina la ‘Scorpion’ anayekabiliwa na shtaka la unyang’anyi wa kutumia silaha na kujeruhi ana kesi ya kujibu na anatarajiwa kuanza kujitetea, Novemba 14, mwaka huu.

Uamuzi huo umetolewa leo Oktoba 31/2017 na Hakimu Mkazi Flora Haule wa mahakama hiyo baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na zaidi ya mashahidi kumi  walioletwa mahakamani pale na upande wa Mashtaka.

Kabla ya kutolewa uamuzi huo, Hakimu Haule alimkumbushia mshtakiwa mashtaka yake. 

Baada ya uamuzi huo kutolewa, mshtakiwa Scorpion amedai kuwa atajitetea kwa kiapo na pia atakuwa na mashahidi wawili ambao walitoa ushahidi upande wa mashtaka.

Hata hivyo, upande wa mashtaka ukiongozwa na wakili Ester Kyala ulipinga hoja hiyo na kudai kuwa mshtakiwa huyo hawezi kutumia mashahidi ambao wamekwisha toa ushahidi wao kwa upande wa Jamhuri na kama anaweza atafute mashahidi wengine.

Kutokana na pingamizi hilo Scorpion amedai atajitetea mwenyewe na pia akaomba mahakama itumie pia ushahidi wa wale mashahidi wawili.

Kufuatia hayo kesi hiyo imeahirishwa hadi November 14 mwaka huu. Mshtakiwa amerudishwa rumande kwa kuwa hana makosa anayoshtakiwa nayo hayana dhamana.

Katika kesi hiyo, Njwete anakabiliwa na mashtaka mawili ambayo ni  unyang’anyi wa kutumia silaha na kumjeruhi Said Mrisho kwa kumchoma kisu sehemu mbalimbali za mwili zikiwemo, tumboni na mabegani na kisha kumtoboa macho kitendo anachodaiwa kutenda Septemba 6, mwaka jana  katika eneo  la Buguruni Sheli, jijini Dar es Salaam.

Pia, anadaiwa kumwibia mali yenye thamani ya Sh 476,000/-. 

UJENZI WA MELI MPYA ZIWA VICTORIA WAIVA

$
0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amekagua eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa meli mpya na yakisasa itakayotoa huduma za usafirishaji katika  Ziwa Victoria.

Akizungumza na wafanyakazi wa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL), Profesa Mbarawa, amewataka wafanyakazi wa Kampuni hiyo kutoa ushirikiano kwa Mkandarasi ili kazi hiyo ianze mara moja na kukamilika kwa wakati.

“Mkandarasi ameshapatikana hivyo hakikisheni mnatoa ushirikiano na mnafanya uhakiki wa kimahesabu vizuri ili kazi hii ifanyike kwa gharama nafuu, ubora na muda mfupi”, amesema Profesa Mbarawa.Katika hatua nyingine, Waziri Mbarawa, amekagua maendeleo ya ukarabati wa meli ya Mv. Clarias na Mv. Umoja ambapo ameeleza kuridhishwa kwake na hatua zilizofikiwa, na hivyo kuwataka MSCL kutafuta mizigo ya kusafirisha kutoka Bandari ya Mwanza kwenda Bandari  ya “Port Bell”, nchini Uganda.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (mbele), akitoka kuangalia ukarabati wa meli ya Mv.  Clarius, katika Bandari ya Mwanza, leo. Meli hiyo inatoa huduma katika visiwa vilivyo kwenye ziwa Victoria.
 Muonekano wa Meli ya Mv. Umoja yenye uwezo wa kubeba behewa 22. Meli hiyo inasafirisha mizigo kutoka Bandari ya Mwanza kuelekea Bandari ya “Port Bell” Uganda.
 Mhandisi Mkuu wa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL), Xavier Kapinga, akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (Wa tatu kushoto mbele) wakati alipokagua maendeleo ya ukarabati wa meli katika Bandari ya Mwanza, leo.
Mafundi wakiendelea na ukarabati wa meli ya Mv. Clarius leo katika Bandari ya Mwanza. Kukamilika kwa ukarabati wa Meli hiyo inayotoa huduma katika visiwa vilivyo katika ziwa Victoria kutarudisha huduma za usafirishaji na abiria katika visiwa hivyo.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

WAKAZI WA BAGAMOYO WAKUNWA NA TAMASHA LA EFM MZIKI MNENE

$
0
0
 Msanii wa Muziki wa Hip Pop Nchini, Izo Busines akitoa Burudani kwa wakazi wa Wilaya ya Bagamoyo katika Tamasha Maarufu la Mziki Mnene lililofanyika katika Bar ya Dunda Dunda linaloandaliwa na Efm Radio kwa kushirikiana na Tv E
 Mkali wa Muziki wa Bongo Fleva nchini, Prince Dully Sykes akiimba na Mashabiki wakati wa Tamasha la Muziki Mnene linaloandaliwa na Radio ya Efm na Tv E ambalo lilifanyika katika Bar ya Dunda Dunda Wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani.
 RDJ Mamy kutoka Efm Radio akitoa burudani kwa wakazi wa Wilaya ya Bagamoyo kwenye Tamasha la Mziki Mnene lililofanyika katika Bar ya Dunda Dunda
  Mkali wa Muziki wa Bongo Fleva nchini, Prince Dully Sykes akiimba na Mashabiki wakati wa Tamasha la Muziki Mnene linaloandaliwa na Raido ya Efm na Tv E ambalo lilifanyika katika Bar ya Dunda Dunda Wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani.

TANZANIA YAWA KINARA KATIKA MAPAMBANO YA UKATILI WATOTO BARANI AFRIKA

$
0
0
Na Humphrey Shao Globu ya Jamii

TANZANIA imetajwa kuwa ni nchi ya kwanza barani afrika katika mapambano dhidi ya ukatili watoto kulinganisha na mataifa mengine.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa shirika la Kimataifa linaloshughulikia haki za watoto, Elimu na Ushauri, Michael Gibbons alipokuwa akitoa mada katika mkutano wa kujadili masuala ya ukatili kwa watoto na Wanawake uliofanyika jijini Dar es Salaam Leo.

Gibbons amesema Tanzania ndio nchi pekee Afrika iliyoweka nguvu kubwa katika mapambano ya ukatili wa mtoto pamoja na kuweka mazingira wezeshi ya elimu kutokana na sera yake ya Elimu Bure.

Akizungumza kwa Niaba ya Waziri wa afya jinsia Wanawake na Watoto, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto, Magreth Mussai amesema Serikali inatumia takribani Bilioni 6.7 kutibu naa kushughulikia matokeo ya ukatili.

“katika kulinda watoto baada ya matukio ukatili kutokea Taifa linatumia Bilioni 6.7 kwa ajili ya kushughulikia Mahakamani, Matibabu na hatua zote anazostaili mtoto na Wanawake baada ya ukatili kutokea.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Haki Elimu nchini John Kalaghe amesema asilimia 52.6% ya vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watoto hutokea mashuleni jambo ambali limekuwa likipigiwa kelele na wazazi wengi.

Kalaghe amesema ukatili wa watoto ni moja ya jambo ambalo linasumbua katika ukanda huu wa Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania na kutaja watoto wa kike na wakiume hapa nchini upitia ukatili wa kupigwa mashuleni kwa asilimia 52.6 %.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Haki Elimu,John Kalaghe akizungumza wakati wa mkutano wa kujadili Masuala ya haki za Watoto na Wanawake katika ukanda Afrika Mashariki
Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa linaloshughulikia haki za Watoto, Elimu na Ushauri, Michael Gibbons akizungumza katika Mkutano wa kujadili Masuala ya haki za Watoto na Wanawake katika ukanda Afrika Mashariki
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto na Wanawake , Magreth Mussai akizungumza katika mkutano huo kwa Niaba ya Waziri wa Afya Wanawake jinsia na watoto.

OFISI YA MAKAMU WA RAIS YAANDAA WARSHA YA UZINDUZI WA MRADI WA KUJENGA UWEZO KWA TAASISI KATIKA UDHIBITI WA KEMIKALI NA TAKA SUMU

$
0
0
Nchi zinazoendelea zinakabiliwa na changamoto katika suala zima la usimamizi na udhibiti wa kemikali na taka sumu. Taka sumu nyingi zimekua tishio kwa Wananchi hasa Wanawake na Watoto. 

Hayo yamesemwa na Mgeni Rasmi  ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais,  Bwana Richard Muyungi alipokua akifungua warsha ya uzinduzi wa mradi wa kujenga uelewa kwa Taasisi za Serikali katika udhibiti na usimamizi wa kemikali na taka sumu jijini Dar Es Salaam.

Pia ametoa shukrani kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira (UNEP) kwa msaada wa kifedha katika kuanzishwa kwa mradi huo, ameongeza pia  Wajumbe waliohudhuria warsha hiyo wakaitumie vema elimu watakayoipata katika sehemu zao za kazi ili kuongeza weledi na maarifa.
 Mgeni Rasmi katika warsha ya uzinduzi wa Mradi wa kujenga uwezo kwa Tasisi katika udhibiti wa kemikali na taka sumu , Bwana Richard Muyungi ambaye ni Mkurugenzi idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais akiongeakatika uzinduzi wa warsha hiyo.
 Mkurugenzi Msaidizi wa Mazingira katika Ofisi ya Makamu wa Rais Bi Magdalena Mtenga akiongea wakati wa warsha hiyo iliyoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais, Idara ya Mazingira.
 Sehemu ya Washiriki wa warsha hiyo wakifuatilia kwa makini hotuba ya Mgeni Rasmi (hayupo pichani).

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MKURUGENZI ILEJE ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA MRADI TANKI LA MAJI ITUMBA ISONGOLE

$
0
0
 Mkurugenzi wa Wilaya ya Ileje Haji Mnasi  akikagua  mradi mkubwa wa ujenzi wa tanki la maji wa ujazo wa lita laki Tano unaofanywa na m/s singilimo enterprises ltd ambapo utagharimu kiasi  Shilingi 557073162/= ambapo utakapokamilika januari mwakani utawezesha watu zaidi ya watu 20000 wa i Kata ya tumba na Isongole na maeneo jirani wilayani ileje kupata Maji Safi na Salama kwa uhakika zaidi.
 Mkurugenzi wa Wilaya ya Ileje Haji Mnasi akimsikiliza Mhandisi wa Mradi Mkubwa wa Maji unao hudumi kata ya Itumba na Isongole kwa zaidi ya lita 5000
 Mkurugenzi wa Wilaya ya Ileje Haji Mnasi  akikagua  mradi mkubwa wa ujenzi wa tanki la maji wa ujazo wa lita laki  tano unaofanywa na m/s singilimo enterprises ltd ambapo utagharimu kiasi  Shilingi 557073162/= ambapo utakapokamilika januari mwakani utawezesha watu zaidi ya watu 20000 wa i Kata ya tumba na Isongole na maeneo jirani wilayani ileje kupata Maji Safi na Salama kwa uhakika zaidi.
--

MAKANDARASI KUKUTANA JIJINI DAR, KUJADILI MAENDELEO YA UKUAJI WA VIWANDA

$
0
0
Na.Paschal Dotto-MAELEZO.

Chama cha Makandarasi (CATA) kinachounganisha wakandarasi wote nchini kinatarajia kukutana Novemba 17, 2017 kujadili kuhusu ukuaji wa viwanda nchini mkutano utakaofanyika katika ukumbi wa Diamondi Jubilee Jijini Dar es Salaam.

Akizungumuza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Mhandisi Lawrence Mwakyambiki alisema kuwa  Serikali ya Aawamu ya Tano chini ya uongozi wa Rais John Pombe Magufuli iko kwenye njia ya ujenzi wa viwanda kwa hiyo sekta ya ujenzi inahitajika kwa kiasi kikubwa kwenye sera hii ya viwanda.

“Lengo la mkutano huu kwa wakandarasi hawa ni kutaka kuleta mchango wao katika ujenzi wa uchumi wa Tanzania na wameona kwamba kama wazawa wanaowajibu wa kutoa mchango katika katika ujenzi wa viwanda nchini”, alisema Mhandisi Mwakyambiki.

Aidha Mhandisi Mwakyambiki aliseka kuwa katika maendeleo ya taifa tasnia ya ujenzi ni muhimu kwani inabeba vitu vingi na kuwawezesha wananchi kupata huduma stahiki kama elimu na afya na kuwataka makandarasi kufanya kazi zo kwa ufanisi mkubwa.
 Mwenyekiti wa Chama cha Makandarasi Mhandisi Lawrence Mwakyambiki (katikati) akieleza jambo kwa waandishi wa habari(hawapo pichani) katika utambulisho wa mkutano wa chama hicho utakaofanyika Novemba 17, 2017 Diamondi Jubilee Jijini Dar es Salaam,kulia ni Meneja Mauzo wa benki ya cba Bi.Kunenguda Dedede na kushoto ni Mkuu wa Masoko kutoka NMB Bi.Linda Teggisa.

Meneja Mauzo wa benki ya cba Bi.Kunenguda Dedede akieleza jambo kwa waandishi wa habari( hawapo pichani)  kuhusu mkutano wa makandarasi hapo novemba 17, 2017 katika ukumbi wa diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam, wa kwanza kushoto ni Mkuu wa masoko  kutoka NMB Bi.Linda Teggisa na Mwenyekiti wa Chama cha Makandarasi Mhandisi Lawrence Mwakyambiki.(Picha na Paschal Dotto-MAELEZO).

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA


ZIARA YA NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, MHE. JAPHET HASUNGA KATIKA SHAMBA LA MITI SAO HILL NA KITUO CHA MALIKALE CHA ISMILA NA KALENGA MKOANI IRINGA

$
0
0
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza alipotembelea shamba la miti Sao Hill kukakua shughuli mbalimbali zinazofanywa na shamba hilo mkoani Iringa hivi karibuni. Aliagiza uongozi wa shamba hilo kuongeza juhudi za upandaji miti ili kukidhi mahitaji makubwa yaliyopo nchini na hivyo kusisimua ukuaji wa uchumi wa viwanda.
Naibu Waziri wa Maliasili, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akikagua baadhi ya vifungashio vya asali alipotembelea shamba la miti Sao Hill kwa ajili ya kukakua shughuli mbalimbali zinazofanywa na shamba hilo mkoani Iringa hivi karibuni. Asali inayozalishwa na shamba hilo imefanyiwa vipimo nchini Ujerumani na kugundulika kuwa ni bidhaa bora isiyo na viambata vya kemikali ya aina yeyote. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza na Afisa Ufugaji Nyuki wa shamba hilo, Said Abubakar. 
Meneja wa shamba la miti Sao Hill, Salehe Beleko (kushoto) akimueleza Mhe. Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia) kuhusu moto uliovamia hekta 77 za shamba hilo na hatua zilizochukuliwa kuudhibiti alipotembelea  kukakua shughuli mbalimbali zinazofanywa na shamba hilo mkoani Iringa hivi karibuni, alisema moto huo uliozuka hivi karibuni ulianzia kwenye mashamba ya wananchi haukuwa na madhara makubwa. 
Meneja wa Shamba la Miti Sao Hill, Salehe Beleko (kulia) akimuelezea Naibu Waziri wa Maliasili, Mhe. Japhet Hasunga kuhusu utafiti unaofanywa na shamba hilo kwa kushirikiana na Kampuni ya Art International kuhusu uvunaji wa utomvu kwa ajili ya kutengeneza madawa mbalimbali, bazooka (chewing gums) na ‘gel’ kwa ajili ya kujiongezea kipato alipotembelea shamba hilo kukagua shughuli mbalimbali hivi karibuni. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Mhe. Jamhuri David. 
Meneja wa Shamba la Miti Sao Hill, Salehe Beleko (kulia) akimuelezea Naibu Waziri wa Maliasili, Mhe. Japhet Hasunga (hayupo pichani) kuhusu njia mpya ya kuzalisha mbegu za miti kwa njia ya vikonyo ili kuongeza zaidi uzalishaji alipotembelea shamba hilo kukagua shughuli mbalimbali hivi karibuni. Aliagiza uongozi wa shamba hilo kuongeza juhudi za upandaji miti ili kukidhi mahitaji makubwa yaliyopo nchini na hivyo kusisimua ukuaji wa uchumi wa viwanda.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

CLINIC YA METHANONE ZANZIBAR YAPATIWA VIFAA VYA KUCHUNGUZA WATEJA WAO

$
0
0

Na Ramadhani Ali – Maelezo .
          
Wagonjwa wanaotumia dawa aina ya Methadone kama tiba baada ya kuathirika kutokana na dawa za kulevya na wanaoutumia aina nyengine ya dawa  kwa njia za siri wamepatiwa muarubaini baada ya kupatikana vifaa maalumu vya kumgundua mtumiaji kwa kumpima mkojo.

Vifaa hivyo vinavyojulikana kwa jina la DOAKIT vimetolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na madawa ya kulevya na uhalifu (UNODC).Mratibu wa Mradi wa Taifa wa kupambana na HIV/AIDS kwa wafungwa, Immaculate Nyoni ambae ni afisa wa UNODC Tanzania amemkabidhi vifaa hivyo Mratibu wa huduma za ukimwi kwa watu wa makundi maalum Zanzibar Dkt. Shaaban Hassan katika hafla iliyofanyika Kliniki ya Methadone iliopo ndani ya hospitali ya wagonjwa wa akili Kidongo- chekundu.

Immaculate alisema UNODC itaendelea kuunga mkono juhudi zinazochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwapatia tiba sahihi wagonjwa walioathirika na dawa za kulevya.Alisema kwa kuanzia wameleta DOAKIT 1500 ambazo zinaweza kutumika kwa kipindi cha miezi mitatu kwa mujibu wa idadi ya wagonjwa wanaotumia Methadone waliosajiliwa katika kliniki hiyo.

Daktari dhamana wa hospitali ya Kidogochekundu Dkt. Khamis Othman alilishukuru shirika la UNODC kwa kuwapatia msaada huo ambao kwa kipindi cha mwaka mmoja walikuwa na upungufu mkubwa na kupelekea baadhi ya wagonjwa kutumia aina nyengine ya dawa bila kujulikana.
 Mratibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la dawa za Kulevya na Uhalifu  (UNODC) Bi. Immaculate Nyoni  akimkabidhi boksi lenye vifaa vya kupimia mkojo watumiaji dawa ya Methadon ambao wanatumia  aina nyengine ya dawa kinyume na taratibu katika hafla iliyofanyika Kliniki Methadone Kidongochekundu.
 Rais wa watumiaji dawa ya Methadon Zanzibar Hilal Nassor akizungumza na wandishi wa habari baada ya kukabidhiwa vifaa vya kuwatambua watumiaji wa tiba ya Methadone na baadae kutumia dawa aina nyengine.

Baadhi ya watumiaji dawa za Methadone wakisubiri kupatiwa huduma katika Kliniki yao iliyopo Hospitali ya wagonjwa wa akili Kidongo- Chekundu Mjini Zanzibar.Picha na Makame Mshenga.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

IGP SIRRO ATAKA JESHI LA POLISI KUDUMISHA MICHEZO

$
0
0
Na Jeshi la Polisi.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amewataka Maofisa na Askari Polisi kote nchini kushiriki michezo ili kujenga Afya,ukakamavu na urafiki baina ya wenyewe kwa wenyewe na raia.

IGP Sirro ameyasema hayo jijini Dar Es Salaam wakati hafla fupi ya kuwapongeza wachezaji wa TAEKWONDO waliofanya vizuri katika michezo ya Taekwondo Pumsae (kucheza Kata), Taekwondo Gyeokpa ( kuvunja kibao kwa kuruka Juu) na Taekwondo Gyeorugi (Mapigano) iliyomalizika hivi karibuni ambapo timu ya Polisi iliibuka na ushindi wa kwanza  katika timu 17 zilizoshiriki.

Sirro alisema Jeshi la Polisi litaendelea kutilia mkazo michezo ya aina mbalimbali na atahakikisha Askari na Maofisa wanapata fursa ya kushiriki michezo kwakuwa kwakufanya hivyo kutasaidia pia kulitangaza Jeshi la Polisi na kujenga mahusiano na jamii.

"Hakikisheni hamrudi nyuma,tutawapa sapoti ya kila namna ili tusiwe wasindikizaji bali tuweze kutoa ushindani na kufanya vyema na ni jambo linalowezekana kwa kuwa ari na morali ipo"Alisema Sirro.
  Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akiwa na viongozi wa Jeshi la Polisi  Sambamba na Askari Polisi walioshiriki na kujinyakulia medali mbalimbali katika mashindano ya mchezo wa Taekwondo iliyo andaliwa na Ubalozi wa Jamuhuri ya Korea ukishirikiana na Chama cha walimu wa Taekwondo kutoka Korea. (Korean Taekwondo Masters Association)
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akiwa na askari wa jeshi hilo wanaounda timu ya Taekwondo ambao walishiriki na kujinyakulia medali mbalimbali katika mashindano ya Taekwondo yaliyo andaliwa na Ubalozi wa Jamuhuri ya Korea ukishirikiana na Chama cha walimu wa Taekwondo kutoka Korea. (Korean Taekwondo Masters Association) yaliyoshirikisha vilabu 17 vya Taekwondo kutoka nchi nzima.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simoni Sirro akimvisha medali askari Polisi ambaye ni miongoni mwa askari waliojinyakulia medali katika mashindano taekwondo iliyo andaliwa na Ubalozi wa Jamuhuri ya Korea ukishirikiana na Chama cha walimu wa Taekwondo kutoka Korea. (Korean Taekwondo Masters Association). Picha zote na Jeshi la Polisi.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

RC Rukwa aahidi kuimarisha utendaji kazi wa watumishi wa Rukwa katika Sekta zote

$
0
0
​Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joackim Wangabo amewatahadharisha watumishi kutobweteka baada ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen kustaafu na kumkabidhi yeye kijiti cha utekelezaji wa shughuli za maendeleo ya mkoa.

Amesema kuwa hatomwangusha Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa kumuamini na kumkabidhi madaraka hayo na kuahidi kuwa ataimarisha elimu inayoonekana bado ipo chini kwa ufaulu lakini pia kuendeleza kasi ya uzalishaji katika kilimo.

“Baada ya kusoma kabrasha hili la kukabidhiana ofisi kuna mambo mengi ya kuyazingatia ikiwemo, elimu, kilimo, ulinzi na usalama, utunzaji wa mazingira, uvuvi na uwekezaji katika viwanda. Hasa katika elimu maana mimba ni nyingi, kuna upungufu wa madawati, upungufu wa vyumba vya madarasa lakini pia kiwango cha ufaulu hakijafikia kile kilichopo katika ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo ni asilimia 80 kwa darasa la saba,” Alisisitiza.

Mh. Wangabo ameyasema hayo katika makabidhiano ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa mapema leo hii tarehe 31/10/2017 katika ukumbi wa ofisi hiyo, jambo lililoshuhudiwa na watumishi wa sekretariet ya Mkoa pamoja na baadha ya Halamashauri.
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joackim Leonard Wangabo (kushoto) na Mh. Zelote Stephen (Waliokaa) katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya pamoja na baadhi ya Wakurugenzi wa Halmashauri na Mwenyekiti wa CCM Mkoa.
 Mkuu nwa Mkoa wa Rukwa, Mh. Joachim Leonard Wangabo akisalimiana na Meneja wa PS3 Mkoa wa Rukwa Bi. Rose wakati wa kumkaribisha Mh. Wangabo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa tayari kwaajili ya Kuanza kazi.
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Kamishna Mstaafu Zelote Stephen (kushoto) akimkabidhi nyaraka za ofisi Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joackim Wangabo. katika makabidhiano ya ofisi hiyo yaliyofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa. 

 Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Kamishna Mstaafu Zelote Stephen (kushoto) akisaini nyaraka za ofisi Mkuu wa Mkoa kwaajili ya Kumkabidhi ofisi hiyo Rukwa Mh. Joackim Wangabo. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

TIGO YAZINDUA TUMEKUSOMA

$
0
0
Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, juzi Jumapili ilizindua rasmi kampeni mpya ijulikanayo kama Tumekusoma sambamba na uzinduzi wa namba mpya ya menu iliyorahisishwa *147*00#. Menu hii mpya itamuwezesha mteja kupata huduma mbalimbali kwa urahisi. Uzinduzi huo ulifanyika kwenye tamasha la Tigo Fiesta 2017 mjini Moshi.
Viewing all 110105 articles
Browse latest View live




Latest Images