Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110182 articles
Browse latest View live

Dkt. Abbasi Awapa Siri Tano za Mafaniko Wahitimu Kidato cha Nne Jitegemee

$
0
0
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akimkabidhi cheti cha kuhitimu Kidato cha Nne mmoja wa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Jitegemee ya Jijini Dar es Salaam alipokuwa mgeni rasmi katika Mahafali ya 33 ya Shule ya hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule hiyo Brigedia Jenerali Mstaafu Lawrence Magere. Kushoto ni Mkuu wa Shule hiyo Luten Kanali Robert Kessy.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akikabidhiwa risala ya wanafunzi wa Kidato cha Nne Shule ya Sekondari Jitegemee ya inayomilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wakati wa Mahafali ya 33 ya Shule hiyo leo Jijini Dar es Salaaam.
Mkurugenzi Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akizungumza alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 33 ya Shule ya Sekondari ya Jitegemee inayomilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa leo Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Jitegemee ya Jijini Dar es Salaam inayomilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Luten Kanali Robert Kessy akizungumza wakati wa mahafali ya 33 ya shule hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi na Mwenyekiti wa Bodi ya Shule Brigedia Jenerali Mstaafu Lawrence Magere.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akiangalia vitabu alipotembelea Maktaba ya Shule ya Sekondari ya Jitegemee ya Jijini Dar es Salaam inayomilikiwa ma Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wakati wa Mahafali ya 33 ya Shule hiyo leo Jijini Dar es Salaam.

NYUMBA 58 ZA WATU WALIOVAMIA ENEO LA SHULE YA TABORA WASICHANA ZATEMBEZEWA NYUNDOOZZZ

$
0
0
NA TIGANYA VINCENT, RS-Tabora

MANISPAA ya Tabora kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora imeendesha zoezi la kuwaondoa watu waliovamia eneo la Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Tabora na kufanikiwa kuvunja nyumba zaidi ya 58 za watu waliokuwa wamejenga katika eneo hilo. Hatua hiyo imechukuliwa jana baada ya wahusika kuombwa waondoke kwa hiari kwa kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja uliopita lakini walikaidi kutekeleza agizo hilo na kuendelea kuishi katika la Shule hiyo

Akizungumza na waandishi wa habari Mwanasheria kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora Richard Lugomela alisema kuwa wavamilizi hao walipewa taarifa ya kuondoka katika eneo shule muda mrefu ambao unazidi mwaka mmoja lakini wamekuwa wakikaidi kuondoka kwa hiari. Alisema kuwa zoezi hilo ambalo limeanzia katika Shule hiyo lina lengo la kuhakikisha maeneo yote ya Taasisi yalivamiliwa yanarejeshwa na yatumika kwa ajili ya maendeleo yao ili  kutoa huduma bora kwa wananchi.

Lugomela aliongeza kuwa hivi sasa ilikuwa ni vigumu kwa Shule kama Tabora wasichana kuweka miundo mbinu zaidi kwa sababu ya kuwepo kwa wavamizi hao. Alisema kuwa wavamizi hao walipewa taarifa na kuomba wapewe muda wa kujiandaa ili waweze kuondoka lakini badala yake wameendelea kukaa kimya na kupuuzia agzio la kuwataka kuondoka katika eneo walilolivamia.

Alitoa wito kwa watu wengine wanaojijua kuwa wamevamia maeneo ya Taasisi nyingine za elimu kama vile Shule ya Sekondari Milambo, Tabora wavulana na hata yasiyokuwa yao kuanza kuondoka wao kwa hiari yao la sivyo watalazimika kulipia gharama za uvunjaji wa nyumba zao endapo Serikali itatekeleza zoezi la kuwaondoa. Lugomela alisema kuwa eneo hilo lilitengwa na Serikali kwa ajili ya matumizi ya Shule ya Wasichana toka mwaka 1958 na pia katika sehemu hiyo lipo eneo ambalo ni chanzo cha maji.

Kwa upande wa Mhandisi wa Maji wa Manispaa ya Tabora Mohamed Almasi alisema kuwa watu waliojenga katika eneo hilo hawana vibali vya ujenzi na hivyo ni wavamili ambao walipaswa kuwa wameshaondoka siku nyingi. Alisema kuwa baada ya kumalizika kwa zoezi la kuwaondoa wavamizi hao katika shule hiyo ya wasichana ya Tabora watahamia katika maeneo mengine ya Taasisi na kwa watu binafsi ambao maeneo yao yamekaliwa na watu wengine kinyume cha sheria.

Almasi alitoa wito kwa wakazi wa Manispaa ya Tabora wanaotaka kujenga wapelekea ramani zao katika Manispaa ya Tabora ili waweze kupatiwa kibali cha ujenzi kabla ya kuendeleza maeneo yao. Mmoja wa waathirika wa bomoa bomoa Hawa Katabi alisema kuwa hakupata taarifa ya zoezi hilo jambo liliwafanya washindwe hata kuondoa mabati na matofauli.

Alisema ni vema zoezi hilo linapotaka kufanyika wakapewa muda wa kutosha ili waweze kuokoa mali zao

MABARAZA YA MADIWANI SIMIYU YARIDHIA HALMASHAURI ZIKOPE BILIONI 17.1 KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (katikati) akizungumza na Madiwani na baadhi ya wakulima Bonde la Mwamanyili wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega (hawapo pichani) katika kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani, kilichofanyika Nyashimo kwa lengo la kujadili suala la maombi ya mkopo kwa ajili kutekeleza Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili Wilayani humo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Mhe.Vumi Magoti(wa pili kulia)akizungumza na Madiwani na baadhi ya wakulima wa Busega(hawapo pichani) katika kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani kilichofanyika Nyashimo kwa lengo la kujadili maombi ya mkopo kwa ajili kutekeleza Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili Wilayani humo
Madiwani na baadhi ya Wafugaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu wakifuatilia mjadala kuhusu suala la maombi ya Mkopo kwa ajili ya Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Wilayani Meatu katika kikao cha dharura cha Baraza kilichofanyika Mjini Mwanhuzi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Wilaya ya Busega (meza kuu) na baadhi ya wakulima baada ya kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani kilichofanyika kwa lengo la kujadili suala la maombi ya mkopo kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili wilayani humo.

Na Stella Kalinga, Simiyu
Mabaraza ya Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Busega na Meatu Mkoani Simiyu yameridhia Halmashauri hizo kukopa shilingi bilioni 17.1 kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), kwa ajili ya kutekeleza Miradi mikubwa miwili ya Maendeleo.

Maridhiano hayo yamefikiwa katika Vikao vya dharura vya mabaraza ya madiwani vilivyofanyika kwa nyakati tofauti, ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Busega imepanga kukopa shilingi bilioni 10.7 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili (eneo la ekari 2050)  na Meatu shilingi bilioni 6.4 kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda cha maziwa(MEATU MILK).

 Akiwasilisha taarifa ya Maendeleo ya Mpango wa Kilimo cha Umwagiliaji Wilayani Busega, Afisa Mipango wa Wilaya hiyo Josephat Joseph, amesema hadi sasa kazi za upimaji wa mashamba na njia ya kupita bomba la maji, kupima udongo, kusanifu mfereji mkuu kwenye chanzo, sehemu ya kuchukulia maji, nyumba za pampu, mifereji ya kuingiza na kutolea maji,kuandaa michoro na gharama za mradi zimeshakamilika.

VIDEO: DKT. HARRISON MWAKYEMBE ASHEREHEKEA NA WAHINDU MWAKA MPYA WA KIHINDU WA 2074 JIJINI DAR ES SALAAM

Tanzania yatwaa taji la Cana kanda ya tatu kwa mara ya pili mfululizo

$
0
0
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza akimkabidhi kombe nahodha wa Tanzania, Sonia Tumiotto pamoja a Natalie Sanford mara baada ya kutwaa ubingwa wa Cana Kanda ya Tatu.

Tanzania imefanikiwa kutetea ubingwa wa Cana Kanda ya Tatu Afrika baada ya kuibuka katika nafasi ya kwanza katika upande wa wanawake na wanaume. Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa juzi, timu ya Tanzania ilipata jumla ya pointi 1,394 na kufanikiwa kuzishinda timu maarufu na kali katika mchezo huo, Zambia ambayo ilipata pointi 968 na Kenya iliyomaliza ya tatu kwa pointi 957.

Uganda ambayo ndiyo nchi ya kwanza kuandaa mashindano hayo, ilimaliza ya nne kwa kupata pointi 759 na kufuatiwa na Afrika Kusini iliyopata pointi 469 ma Sudani iliyopata oint 459 katika mashindano hayo yaliyodhaminiwa na Vodacom Tanzania, Swissair, JCDecaux, Coca Cola, Label Promotions, Tanzania Sign Writers, Giraffe Ocean View, Print Galore na Slipway Hotel. 

Katika mashindano hayo ya siku tatu, timu ya wanawake wa Tanzania ndiyo ilikuwa kali zaidi kutokana na kuundwa na waogeleaji nyokta kama Sonia Tumiotto ambaye ndiye nahodha na Natalie Sanford. Mbali ya hao kulikuwa na nyota wengine kama Maia Tumiotto ambaye anakuja juu kwa kasi, Smriti Gorkan, Kayla Gouws, Amani Doggart, Tara Behnsen, Emma Imhoff, Rania Karume , Chichi Zengeni, Anjani Taylor, Anna Guild, Sanne Kleinveld , Angelica Spence, na Tami Triller.

Kwa upande wa wanaume , nyota alikuwa Marin De Villard pamoja na wakali wengine kama Collins Saliboko, Joseph Sumari, Denis Mhini, Hilal Hilal, Adil Bharmal, Judah Miller, Elia Imhoff, Delvin Barick, Caleb O'Sullivan, Khaleed Ladha, Matthew Guild , Chris Fitzpatrick, Harry McIntosh, Dhashrrad Magesvaran na Joseph Sumari.

Kwa upande wa timu ya Platnum, nayo ilionyesha kuwa kuna nyota wa baadaye wa Tanzania ambapo timu ya wanawake iliindwa na Shivan Bhatt, Natalia, Charlotte Sanford, Vanessa Dickson ), Rebecca Guild, Meredith Boo , Maria Bachmann ), Kayla Temba na Maya Somaiya.

Kwa wanaume walikuwa Aravind Raghavendran, Mohameduwais Abdullatif (Bluefins), Abraham Kayugwa, Terry Tarimo, Aliasgar Chakera, Zeke Boos , Yuki Omari, Augustino Lucas , Fallih Ahmed, Carter Helsby , Ian Lukaza na Emmanuel Stenson. Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza aliwapongeza waogeleaji wa Tanzania kwa kutwaa ubingwa huo huku akiahidi kutoa ushirikiano mkubwa kwa chama cha kuogelea cha Tanzania (TSA).
Waogeleaji wa timu ya Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kutetea vyema ubingwa wa Cana kanda ya tatu.
Muogeaji nyota wa Tanzania, Sonia Tumiotto akipigania Taifa lake katika mashindano ya Cana kanda ya tatu.
Collins Saliboko wa Tanzania akishindana katika mashindano ya Cana Kanda ya Tatu Afrika.
Makocha wa timu ya Tanzania wakishangilia mara baada ya kutwaa ubingwa wa Cana Kanda ya Tatu kwa mchezo wa kuogelea.

BREAKING NYUZZZZZ: MAHAKAMA YAMKUTA LULU NA KESI YA KUJIBU KUHUSU KIFO CHA KANUMBA

$
0
0
Mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Dar es Salaam leo Oktoba 23, 2017 imemkuta Msanii maarufu wa filamu nchini, Elizabeth Michael Maarufu kama Lulu, anakesi ya Kujibu.

Ni kuhusu tuhuma zinazomkabili za kumuua msanii mwenzake, marehemu Steven Kanumba ambaye pia alikuwa ni mpenzi wake, April 6 mwaka 2012.
Hatua hiyo imekuja baada ya upande wa Jamhuri kufunga ushahidi wao kwa kuita mashahidi wanne.

Kesi imeahirishwa hadi saa tano kamili ambapo Lulu ataanza kujitetea.

MICHUZI TV LIVE: RAIS DKT MAGUFULI AKIWATUNUKU VYETI WAJUMBE WA KAMATI YA MAKINIKIA, IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

WASHINDI WA AFYABANDO WA DROO YA TATU WAPATIKANA

$
0
0


Mtaalam wa Tehama wa Nordic Foundation Tanzania Dickson Leonard (katikati) akibadilishana mawazo na Mkaguzi kutoka Bodi ya Taifa ya Michezo ya kubahatisha, Emmanuel Ndaki (kushoto) na Mkurugenzi mwendeshaji wa Kampuni ya Bima ya Zurich Group/ Jubilee wakati wa zoezi la kuendesha kampeni ya Afyabando ya tatu kuwapata washindi 10 watakaokabidhiwa kadi za Bima ya afya kwa ajili ya matibabu pamoja na familia. Mchezo huo umechezeshwa jijini Dar es Salaam Oktoba 22. 2017. (Imeandaliwa na Robert Okanda Blogs)

Mtaalam wa Tehama wa Nordic Foundation Tanzania Dickson Leonard (kulia) akiwasiliana na mmoja wa washindi wa kampeni ya Afyabando ambapo washindi 10 watakaokabidhiwa kadi za Bima ya afya kwa ajili ya matibabu pamoja na familia. Mchezo huo umechezeshwa jijini Dar es Salaam Oktoba 22. 2017. Kushoto ni Mkaguzi kutoka Bodi ya Taifa ya Michezo ya kubahatisha, Emmanuel Ndaki.

Mtaalam wa Tehama wa Nordic Foundation Tanzania Dickson Leonard (kulia) akiwasiliana na mmoja wa washindi wa kampeni ya Afyabando ambapo washindi 10 watakaokabidhiwa kadi za Bima ya afya kwa ajili ya matibabu pamoja na familia. Mchezo huo umechezeshwa jijini Dar es Salaam Oktoba 22. 2017. Kushoto ni Mkaguzi kutoka Bodi ya Taifa ya Michezo ya kubahatisha, Emmanuel Ndaki.

Mtaalam wa Tehama wa Nordic Foundation Tanzania Dickson Leonard (kulia) akibonyeza kitufe kuwapata washindi wa kampeni ya Afyabando ambapo washindi 10 watakaokabidhiwa kadi za Bima ya afya kwa ajili ya matibabu pamoja na familia. Kushoto ni Mkaguzi kutoka Bodi ya Taifa ya Michezo ya kubahatisha, Emmanuel Ndaki. 


Naibu Waziri Shonza:Vijana jiungeni na vikundi vya Mazoezi

$
0
0
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza (mwenye tisheti nyeupe katikati) akiwa katika mazoezi ya jogging na kikundi cha Kawe Jogging Social Club katika sherehe za miaka mitano ya kikundi hicho zilizofanyika leo jijini Dar es Salaam (aliyenyoosha kidole kushoto) ni Katibu wa Kawe Jogging Social Club Bw.Alhaj Seif Muhere.
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza (mwenye tisheti nyeupe katikati)akifanya mazoezi ya viungo na wanachama wa vikundi mbalimbali vya jogging mkoani Dar es Salaam katika sherehe za miaka mitano ya kikundi cha Kawe Jogging Social Club leo,(kushoto) Katibu wa Kawe Jogging Social Club Bw.Alhaj Seif Muhere na kulia ni Mwanachama wa Jogging Kawe Social Club Bi Felister Mwijage.
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza akizungumza na wanachama wa vikundi mbalimbali vya jogging Mkoani Dar es Salaam katika sherehe za maadhimisho ya miaka mitano ya kikundi cha Kawe Jogging Social Club zilizofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Na Anitha Jonas – WHUSM

Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza ametoa wito kwa vijana kujiunga na vikundi vya mazoezi maarufu kama (Jogging Club) kwa ajili ya kuimarisha afya zao na kujikwamua kiuchumi.

Mheshimiwa Naibu Waziri ametoa wito huo katika sherehe za maadhimisho ya miaka mitano ya Kawe Jogging Social Club zilizofanyika leo jijini Dar es Salaam ambapo aliwapongeza wanachama wa Klabu hiyo kwa kuweza kudumu kwa muda wote huo.

“Napenda kuwapongeza kwa juhudi zenu pamoja na ubunifu mliyoutumia katika kujiongezea kipato kupitia klabu yenu kwa kuanzisha mgahawa ambao unawaongezea kipato na kukuza uchumi wenu kwa hakika mmekuwa ni mfano wa kuigwa,”Mhe. Shonza.

Akiendelea kuzungumza katika sherehe hizo Naibu Waziri huyo amewahakikishia wanaklabu hao ushirikiano pamoja na kushughulikia maombi yao ya kupatiwa mashine ya maximalipo.

Naye Mwenyekiti wa Kawe Jogging Social Club Bw. Abdul Risasi alimshukuru Naibu Waziri kwa kujumuika nao katika sherehe hiyo na kutoa ombi la kusaidiwa kupata mfadhili atakayeweza kuwasaidia kufanikisha ushiriki wao katika mashindano ya Kilimarathon yanayotarajia kufanyika Mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro.

“Tumekuwa tunashiriki katika mashindano ya Kilimanjaro Marathon kwa miaka minne mpaka sasa na Kawe Jogging Social Club imekuwa ndiyo kikundi pekee nchi nzima ambacho kimepata nafasi ya kuweza kushiriki mashindano hayo ambapo wanachama wake hukimbia mpaka kilometa 21,”alisema Bw.Risasi.

Pamoja na hayo Mwenyekiti huyo aliendelea kutoa wito kwa vijana kujiunga katika vikundi vya jogging kwani kupitia umoja huo wanaweza kujitengeneza fursa za kiuchumi na kujiongezea kipato badala ya kukaa vijiweni na kulalamikia hali ngumu ya maisha.

Kwa upande wa mmoja wa wanachama wa Msasani Jogging Club Bi Asha Said alitoa maoni yake na kusema jogging clubs ni nzuri kwani zinasaidia kupata marafiki pamoja na kuimarisha afya.

UNNEWSKISWAHILI KWA HABARI YA KILA SIKU KUTOKA IDHAA YA KISWAHILI YA UMOJA WA MATAIFA

Dkt. Kigwangalla afuta vibali vyote vya uwindaji kwa makampuni nchini

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla amefuta vibali vyote vilivyotolewa na Wizara yake vya Uwindaji wa makampuni ili kuwa na utaratibu mpya wa uombaji kwa njia ya mnada.

Waziri Dk.Kigwangalla ametoa agizo hilo jana jioni wakati wa kuhitimisha mazungumzo yake na wadau mbalimbali wa sekta ya Utalii na Maliasili aliokutana nao mjini hapa Dododma.

“Kwa mamlaka niliyonayo. Natamka kwamba, nafuta rasmi vibali vyote vya Uwindaji kwa makampuni vilivyotolewa na wizara yangu kwa mwaka huu. Pia naagiza Watendaji wote wanaosimamia ili, wahakikishe wanaandaa mchakato ndani ya siku 60 ili mchakato huo wa mnada ufanyike na uwe wa uwazi” alieleza Dkt. Kigwangalla.

Pia ametoa onyo na maagizo mazito kuhakikisha kuwa vitalu vyote vyenye migogoro ikiwemo vile vya Loliondo, Natroni na maeneo mengine kutotolewa kwa vibali vya uwindaji mpaka hapo watakapokamilisha tatizo la migogoro hiyo.
Aidha, ametoa agizo kwa hoteli 10 zilizobinafsishwa kutoka Serikalini zirejeshwe ndani ya siku 60 kuanzia sasa huku akiagiza watendaji waandike barua kwa msimamizi wa hazina.

BREAKING NYUZZZZ......: RAIS DKT. MAGUFULI AMTEUA PROF. FLORENS LUOGA KUWA GAVANA WA BENKI KUU YA TANZANIA

$
0
0
Rais Dkt. John Pombe Magufuli, ametangaza kuteua Profesa Florens Luoga kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania akipokea kijiti kutoka kwa Gavana wa awali, Profesa Benno Ndulu. Rais Dkt. Magufuli ametangaza uteuzi huo wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vyeti kwa Kamani ya zilizofanya uchunguzi wa kiwango, aina na thamani ya madini katika makinikia yaliyopelekea mazungumzo na Kampuni ya Barrick Gold. Profesa Luoga alikuwa ni mmoja wa Wajumbe wa Kamati hiyo.

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA ZA KISHERIA WALE WOTE WANAOANZA KUJENGA MIJINI KWENYE MAENEO YASIYOPIMWA NA BILA VIBALI VYA UJENZI

$
0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen wakati walipoenda kutatua mgogoro wa ardhi wa shamba la mifugo la Malonje wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa lenye ukubwa wa ekari 12,750, ambapo ameagiza eneo hilo lirejeshwe serikalini.

Na. Hassan Mabuye, Wizara ya Ardhi
Serikali kuanzia sasa imewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Ardhi, Maafisa Ujenzi na Maafisa Mipangomiji kuvunja majengo yote yanayoanza kujengwa katika miji yao bila ya kibali na yale yanayojengwa kwa dhuruma na watu wasio na hati katika viwanja vya watu wengine walio na hati miliki zao za ardhi.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi ameyasema hayo alipofanya ziara wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa alipoenda kutatua mgogoro wa ardhi ambapo ameagiza eneo ya lililokuwa shamba la mifugo la Malonje wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa lenye ukubwa wa ekari 12,750, lirejeshwe serikalini kwa vile utaratibu wa kuligawa umekiukwa kwa kiwango kikubwa, na masharti ya uendeshaji hayajazingatiwa kabisa.

Waziri Lukuvi amesema tatizo la ujenzi holela lianaanza pale ambapo Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Ardhi, Maafisa Ujenzi na Maafisa Mipangomiji wanawaacha majengo yanaibuka katika miji yao bila kujua ujenzi huo una kibali au unajengwa katika kiwanja chenye hati na muhusika wa hati hiyo ndio anayejenga.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiongea na Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Ardhi, Maafisa Ujenzi na Maafisa Mipangomiji na kuwaagiza kuweka alama za x na kuvunja majengo yote yanayojengwa katika miji yao bila kibali na yale yanayojengwa katika viwanja vya watu wengine walio na hati za kumiliki ardhi kwa dhuruma.

“japokuwa serikali inaendelea na kurasimisha maeneo, Hatuwezi kuendelea na zoezi la kufanya urasimishaji wa makazi kila siku wakati chanzo cha tatizo hilo kinajulikana, kwa hiyo naagiza kuanzia sasa Wakurugenzi, Maafisa Ardhi, Maafisa Ujenzi na Maafisa Mipangomiji kuondoa majengo yote yanayoanza kujengwa bila vibali na ujenzi unaofanywa na watu wanaodhulumu viwanja vya watu masikini” amesema Lukuvi.

 *Lukuvi amesema atapambana na viongozi ambao wataruhusu watu wasio na hati za kumiliki ardhi kujenga katika viwanja vya wamiliki wengine wenye hati zao.*

Waziri Lukuvi amezitaka Halmashauri zote nchini kutoa vibali vya ujenzi katika muda mfupi na kutenga viwanja vingi vilivyopimwa ili kuwapa fulsa wananchi kujenga katika maeneo yaliyopimwa na yaliyopangwa vizuri katika miji yao.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen amemhakikishia Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi kuwa atayafanyia kazi mapendekezo yake kikamilifu na kwa haraka ili kuondoa migogoro na kero zinazoukabili mkoa wake katika masuala yote ya ardhi.
Baadhi ya viongozi, Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Ardhi, Maafisa Ujenzi na Maafisa Mipangomiji wa mkoani Rukwa wakimsikiliza kwa makini Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi.

Aidha, katika hatua nyingine Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi amesema Serikali imekusudia kuwanyang’anya mashamba watu wote waliokopeshwa kwa kuyatumia kama dhamana kwa ajili ya kupata mikopo kutoka kwenye mabenki ndani na nje ya nchi lakini mikopo hiyo hawaitumii kuinufaisha nchi wala kuiendeleza ardhi waliyoitumia kama dhamana.

Waziri Lukuvi ameongeza kuwa kumekuwa na changamoto kubwa ya wawekezaji wengi wenye mashamba makubwa kutumia ardhi kama dhamana kwa ajili ya kupata mikopo kutoka kwenye mabenki ndani na nje ya nchi lakini mikopo hiyo wanaitumia kuwekeza nje ya nchi na kujenga majengo nchi za Ulaya, dubai na kwingine duniani.

Lukuvi amesema Haiwezekani mtu atumie ardhi yetu kujipatia fedha halafu fedha hizo azitumie kuendeleza nchi nyingine na kuiacha ardhi yetu kama pori jambo ambalo linaleta migogoro mikubwa katika jamii inayoyazunguka maeneo hayo.
Baadhi ya viongozi, Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Ardhi, Maafisa Ujenzi na Maafisa Mipangomiji wa mkoani Rukwa wakimsikiliza kwa makini Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi.

“Kwa hiyo Wizara yangu imekusudia mwezi ujao kupeleka Bungeni marekebisho ya sheria namba 4 ya mwaka 1999 ili kuongeza vifungu ambavyo vitadhibiti mikopo inayopatikana kwa kutumia ardhi kama dhamana” amesema Waziri Lukuvi.

Marekebisho haya tunalenga kuwezesha fedha zinazopatikana kutokana na mikopo iliyotolewa itumike kuendeleza sehemu ya ardhi husika iliyotumika kama dhamana ya kuomba mkopo katika mabenki. Kwa kuwa Tathmini iliyopo inaonesha, baada ya wekezaji hao kupata mikopo kwa kutumia ardhi kama dhamana fedha hizo hawazitumii kuendeleza ardhi husika au katika uwekezaji wowote hapa nchini.

Lukuvi amesema, kuanzia mwezi Novemba tatizo hilo litakwisha kabisa kwa kuwa jukumu hili yatapewa mabenki na wakopeshaji wote ambao watafuatilia kwa karibu maombi ya mikopo kutokana na mpango mkakati uliowasilishwa katika Benki husika.

“na kama Benki husika haitowafuatilia na kuamua kumuachia mtu huyo kwa kuwekeza fedha hizo anavyotaka bila kuendeleza ardhi husika, basi Serikali itamyang’anya mkopeshwaji huyo shamba hilo kwa kuwa atakua amekiuka sheria halafu Benki ambayo itamuachia mtu achukue fedha na asiendeleza shamba lile itakuwa imekula hasara yenyewe” amesema Waziri Lukuvi.

MHASHAMU BABA ASKOFU MAPUNDA AHIMIZA JUU YA UMUHIMU WA KUJITEGEMEA WENYEWE NA KUONDOKANA NA TABIA YA UTEGEMEZI

$
0
0
Mhashamu Baba Askofu Jimbo Katoliki Singida,Edward Mapunda akiongoza misa ya ibada ya maadhimisho ya Jubilee ya miaka 50 tangu kuzaliwa kwa Parokia ya Kupaa Bwana Manyoni iliyofanyika katika viwanja vya kanisa hilo mjini Manyoni.

Na Jumbe Ismailly, MANYONI.

MHASHAMU Baba Askofu Jimbo Katoliki Singida,Edward Mapunda amewataka waumini wa madhehebu hayo kuondokana na tabia ya kutegemea wafadhili wakati wa utekelezaji na ukamilishaji wa miradi mbali mbali ya maendeleo na kuwataka watambue kuwa bwana bure amekufa na aliyebakia kwa sasa ni bwana kujitegemea peke yake. Mhashamu Baba Askofu ametoa wito huo kwenye misa takatifu aliyoiongoza wakati wa maadhimisho ya sherehe za Jubilee ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Parokia ya Kupaa Bwana Manyoni iliyofanyika katika viwanja vya Kanisa la Parokia hiyo mjini Manyoni.

“Lakini ninachotaka kusisitiza jambo moja la kujitegemea,jambo moja la kujitegemea..enh tumesikia wazee wetu hapa walichanga hela,wazee wetu walichanga hela….wazeeeeee mlichanga hela sasa na sisi tunataka kuchanga hela ninyi mbona mlichanga tunataka kujenga Parokia.”alisisitiza baba Askofu Mapunda.
baadhi ya viongozi wa Parokia jimbo Katoliki Singida wakiwa katika maandamano ya kuadhimisha Jubilee ya miaka 50 tangu kuzaliwa kwa Parokia ya Kupaa Bwana Manyoni kwenye sherehe za maadhimisho hayo yaliyofanyika mjini,Manyoni.

Aidha Kiongozi huyo mkuu wa Kanisa hilo alisisitiza kwa wakazi wa wilaya ya Manyoni kwamba suala la kujitegemea halina budi kupatiwa kipaumbele katika shughuli za kukamilisha ujenzi wa majengo ya makanisa pamoja na vigango. Akifafanua zaidi Baba Askofu huyo aliweka bayana kuwa jukumu la kukamilisha ujenzi wa makanisa ni la waumini wenyewe na wenye moyo ambapo hata hivyo aliwatoa hofu waumini wa Manyoni kwa kuweka wazi msimamo wake kuwa anaamini kabisa waumini wa Manyoni ni waumini wenye moyo wa dhati wa kukamilisha majengo hayo.

Kutokana na moyo huo walionao wana Manyoni,Baba Askofu huyo alitumia wasaa wa maadhimisho hayo ya miaka 50 ya Jubilee kwa kuwataka waumini wa Jimbo hilo la Manyoni wajitoe bila kujibakiza,ili mipango na mikakati waliyojiwekea katika Jubilee hiyo iweze kufanikiwa zaidi.

“Namkumbuka sana Askofu Balina,askofu Balina alikuwa wa jimbo Katoliki la Shinyanga tunamuombea kwa Mungu ametangulia kwa Mungu lakini alikuwa anawaambia wasukuma wenzake maneno mazuri sana,na mimi nataka niwaambie hayo wana Manyoni kwa sababu mikakati hii ni mizito,mipango hii ni mizito,maazimio haya ni mazito tusipojitoa yote yatakwama”alisema huku akishangiliwa na waumini.


baadhi ya waumini wa kanisa hilo waliohudhuria kuadhimisha miaka 50 tangu kuzaliwa kwa Parokia ya Kupaa Bwana Manyoni,iliyofanyika mjini Manyoni.Picha zote Na Jumbe Ismailly.

Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa madhehebu ya Kikatoliki askofu Banila alikuwa akiwaambia wanashinyanga kwamba bwana bure amekufa na kwa kutokana na kauli hiyo naye Baba Askofu Mapunda alitumia pia kauli hiyo kwa kuwaasa waumini wa jimbo hilo kwamba bwana bure amekufa na bwana misaada yupo taabani na hivyo aliyebakia ni bwana kujitegemea.
Hata hivyo Askafu Mapunda aliwatahadharisha waumini wa jimbo hilo kwamba suala la kujitegemea lina umuhimu wake na kwa hali hiyo hawana ujanja wa kulikwepa jukumu hilo la kuondokana na utegemezi na kwenda kwenye tabia ya kujitegemea wenyewe kutokana na changamoto nyingi zinazowakabili Mapadrii zikiwemo changamoto za kutokuwa na vyombo vya usafiri.

Naye Paroko wa Parokia  ya Kupaa bwana Manyoni Jimbo Katoliki Singida,Padri Thomasi Wambura  alisema mwaka jana ulikuwa mwaka wa Jubilee ya 100  wa Mapadri Tanzania mwaka huu wao nao wanaadhimisha miaka 50 ya Jubilee ya Parokia yao na mwaka ujao wa 2018 wataadhimisha Jubilee ya miaka 150 tangu ukristo ulipoingia nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa Padri Wambura waumini wote wana wajibu wa kuyatekeleza yale yote waliyoaswa na Baba Asskofu kama mchungaji wao mkuu lakini hakusita kusisitiza kwamba wajibu walionao ni kuyatekeleza yale waliyoyapata katika ukrito. Kwa upande wao baadhi ya waumini wa Kanisa hilo,Elizabeth Mkyalu  alishauri kwamba fedha zilizochangwa na waumini wa kanisa hilo hazina budi kuanza shughuli zilizokusudiwa za ujenzi wa majengo hayo huku akionya tabia ya kusubiri wafadhili kwamba kwa namna moja au nyingine hukwamisha miradi iliyoanzishwa pale wanapojitoa au kutochangia.

Naye Flora Lyimo kwa upande wake alisema kwamba njia pekee ya kujikwamua kiuchumi na kijamii na kuhakikisha maeendeleo endelevu yanapatikana ni kujiamini na kusimama wenyewe kwa miguu yao na siyo kusubiri kusaidiw a na watu wengine kwani endapo watasubiri misaada upo uwezekano wa malengo waliyojiwekea kutokamilika.

JUMIA E-COMMERCE TANZANIA ANNOUNCES PLANS FOR THE UNPRECEDENTED BLACK FRIDAY DEALS LAUNCHING THIS NOVEMBER

$
0
0
Jumia Market Tanzania announces the launch of Black Friday this November, giving Tanzanians access to more deals than ever before. Exclusive deals and discounts of up to 75% will be revealed across all product categories including electronics, appliances and fashion - and for the first time, the leading online marketplace will offer Black Friday discounts for a 11 days period. Selected discounts will launch from Friday  24th November leading up to Friday 4th December, when Jumia Mall will unlock the best of the best deals.

Last year, Jumia Market’s Black Friday broke records by attracting 17x more orders than on a normal day and 10x more traffic. Jumia Mall Tanzania ’s Marketing Manager, aims to surpass customers’ expectations with exclusive deals this year: “We understand that consumers in Tanzania have faced a rough year economically. With customer satisfaction as our top priority, Black Friday will last 11 days to give even more people the opportunity to shop for discounts.”

The leading online marketplace advises consumers to research their favorite products in advance, and place them on their wish list to prepare for the discounts. For convenience, you can receive your order at your home or office - or at the pickup stations in Kariakoo/Masaki(Nakumatt super market first floor and City Mall Hubs - Dar es Salaam. Jumia Mall will continue to post updates on its social media platforms to keep fans informed about all things to do with Jumia Tanzania Black Friday and all the activities to be rolled out.

“With vast of activities that fans will get to win different giveaways,Will provide awesome deals that are worthwhile and put a smile on our customers” Says Albany. With Wheel of fortune(Spin and Win),Lottery and gift vouchers this black Friday will be Bigger, Better and with more deals.


About Black Friday

 “Black Friday” originated from the U.S. and from the phenomenon that takes place after the day of thanksgiving, when retailers see a pike in sales. The day became the biggest shopping day of the year with retailers offering discounts and special deals. Now, “Black Friday” is a global movement and Ugandans search for the best deals and discounts they would otherwise not get on a regular day.


Facebook: JumiaTZ
Twitter: @JumiaTZ
Instagram: @jumiatanzania

MAHAKAMA IMEAMBIWA KUWA MWILI WA MAREHEMU KANUMBA ULIKATWA VIPANDE VIPANDE

$
0
0
 Msaanii wa Bongo Muvi,Elizabeth Michael maarufu kama Lulu akiwa na wazazi waki wakiteta jambo na Wakili Peter Kibatala kabla ya shahidi amaye ni Daktari wa Hospitali ya Muhimbili kutoa ushahidiwake mbele ya mahakama kuu Kanda ya Dar es Salaam leo.
 Msaanii wa Bongo Muvi,Elizabeth Michael maarufu kama Lulu akipitia maelezo aliyochukuliwa na Polisi kipindi alipokamatwa ambayo aliyatoa kwaajili ya ushahidi kwa kuhusishwa na kifo cha Msanii Mwenzake Steven Kanumba. Maelezo hayo ameyapitia leo katika mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Dar es Salaam. 
 Msaanii wa Bongo Muvi,Elizabeth Michael maarufu kama Lulu akitoka katika Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam leo mara baada ya kusikiliza Shahidi aliyeufanyia uchungunguzi Mwili wa Steven Kanumba.
 Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.

Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.
MAHAKAMA Kuu kanda ya Dae es Salaam leo imeambiwa kuwa mwili wa Marehemu Steven Kanumba ulikatwa vipande vipande na kupelekwa kwa mkemia kwaajili uchunguz zaidi.

Daktari bingwa wa uchunguzi wa magonjwa mbalimbali ya binadamu na vifo vyenye utata kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Inocent Mosha ameeleza hayo mbele ya Jaji Sam Rumanyika wa mahakama hiyo.

Amedai, vipande vilivyopelekwa kwa mkemia ni pamoja na kipande cha utumbo, chakula kilichomo, kipande cha ini, figo, mkojo, damu, mamji maji kwenye jocho na kucha.

Akiongozwa  na wakili wa serikali Faraja George shahidi huyo amedai , Aprili 9, 2012 akiwa kazini kwake katika hospitali ya Muhimbili alipokea amri halali ya polisi ikimuamuru kufanya uchunguzi wa Mwili wa Kanumba uliokuwa umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti.

Amedai kuwa wakati wa uchunguzi huo walikuwa na mashahidi wawili walioenda kusaidia kutambua mwili wa marehemu  na kuongeza kwenye uchinguzi walianza kuangalia kama ana majera ya nje ya mwili.

Amedai kucha zake za vidole zilionekana kuwa na rangi ya bluu, pia walipofungua viungo vya ndani vya mwili wa marehemu, kwenye sehemu ya kisogo kulikuwa na mvilio wa damu aidha baada ya kufungua fuvu la kichwa ubongo ulikuwa umevimba.

Aliendelea kudai kwenye mishipa midogo iliyokuwemo kwenye ubongo inayosambaza damu ilivilia damu na sehemu ya chini ya ubongo kulikuwa na mkandamizo wa damu

Aliendelea kudai kuwa, alifungua mapafu, moyo, figo, maini, tumbo na mifumo mingine ya mwili haikuwa na tatizo lolote.

Shahidi huyo alidai katika ripoti yake aliyoiandaa kwenda kwa mkemia, ilionesha kuwa anatatizo kwenye mfumo wa upumuaji ambapo ulishindwa kufanya kazi kutokana na majeraha kwenye ubongo.

"Hakuwa na majeraha kwa nje lakini mapafu yalijaa damu ambapo tulikata kucha kufanya vina saba, tulichukua majimaji ya kwenye jicho kuangalia kiasi cha pombe na sukali kwenye mwili" alidai

 Pia alidai kuwa pombe haiwezi kusababisha matatizo hayo moja kwa moja  badala yake mabadiliko ya tabia yanayotokana na unywaji ndio yanaweza kuchangia.

Alipoulizwa swali na wakili wa utetezi Peter Kibatala shahidi alisema hatambui kama seth Bosco alikuwepo wakati wa uchunguzi kwa sababu sio lazima mtu kuwepo mwanzo mwisho.

Alieleza kuwa hafahamu kiwango cha pombe na hafahamu kama alijigonga kwasababu ya pombe na kwamba hawakuchukua sampuli ya ubongo.

TANZANIA’S FIRST HOUSING FINANCE COMPANY LAUNCHED

$
0
0
Tanzania’s first Housing Finance Company Limited – 1st Housing Finance (Tanzania) Limited - is commencing operations today. The company has been sponsored by Bank M Tanzania Plc, who is partnered by the International Finance Corporation (IFC), Washington, the private sector arm of the World Bank; Housing Development Finance Corporation Limited (HDFC), the largest housing finance company in Asia, the Karimjee family and Sanjay Suchak in establishing the mortgage finance company. 

1st Housing has been issued license by Bank of Tanzania on 18th of July 2017 to commence Housing Finance business in Tanzania under the provisions of Banking and Financial Institutions Act, 2006 (Cap. 342 R.E. 2002).

1st Housing Finance Tanzania Ltd shareholder Mr. Conrad D’souza briefing the press during the launch of the company in Dsm over the weekend. 1st Housing is the first dedicated Housing Finance Company in Tanzania has been promoted by Bank M in partnership with HDFC, IFC, Karimjee family and Sanjay Suchak. Mr. D’Souza is also a member of executive management and chief investor relations officer for HDFC. Others in the photo from left are Bank M Director Mr. Simon Gregory, Aris Group executive Chairman Mr. Sanjay Suchak, IFC Resident representative Mr. Dan Kasirye and Karimjee Jivanjee Director Mr. Mahmoud Karimjee.

1st Housing was incorporated under Tanzanian laws on 13th of July 2016 and its paid-up capital stands at TZS 21.80 Bln. Speaking at the launch, Omar Msangi, Chief Executive Officer of the company, articulated that Bank M partnered with renowned international partners like IFC and HDFC and reputed Tanzanian business families with a view to enter into this attractive housing finance segment in Tanzania. 1st Housing is the first dedicated Housing Finance Company in Tanzania with a focus on providing long term housing solutions to the citizens of Tanzania.

The CEO mentioned that 1st Housing aims to distinguish itself from the market by offering the lowest interest rates for mortgages in the country. The company has fixed its Prime Lending Rate (PLR) at 15%. This will be the rate at which 1st Housing will be lending to its prime customers.

Omar Msangi added that 1st Housing, being the pioneer in the housing finance market, would begin operations by offering 4 new mortgage products viz. for purchase of a home, for improving an existing home, for extending an existing home and for financing the equity in a home. Some of the products being offered are novel in the Tanzanian market.

Housing Finance (Tanzania) Ltd Chief Executive Officer Mr. Omar Msangi speaking during the launch of the company event which took place in Dar es salaam over the weekend.

Another feature which would really set 1st Housing as the leader in the market would be the offer for giving mortgages with tenor upto 20 years. As per the CEO of 1st Housing, this feature is expected to make home loans very affordable in the management of monthly cash flows of home seeking families.

Omar Msangi emphasized the customer focus of the company by stating that 1st Housing is coming to the market with a guaranteed turnaround time of 24 hours for processing of any application for mortgages. 1st Housing will commence operations from it’s offices at 19, Barack Obama Drive, Dar es Salaam. The company has plans to open branches across the country in a short timeframe.

Wabunge na Mawaziri kupewa Tuzo kwa utendaji wao

$
0
0
Na. Thobias Robert- MAELEZO.

Kamati ya utawala ya shindano la tuzo za utekelezaji maendeleo kwa kasi ya juu kwa Wabunge na Mawaziri imezindua shindano la kutoa tuzo kwa Wabunge na Mawaziri (THSDA) watakaofanya vizuri katika kutekeleza majukumu ya kuwaletea Wananchi maendeleo. Hayo yamesemwa Jijini Dar es Salaam leo na Katibu wa Kamati hiyo Bw. Wilson Maage alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, juu ya uzinduzi wa shindano hilo ambalo litafanyika kwa muda wa miezi miwili.

“Tuzo hizo zimetokana na kuwepo wazo bunifu (intellectual property) ambalo azma yake ni kuhamasisha utekelezaji wa shughuli za huduma na maendeleo kwa Wananchi wa Tanzania na kupima kasi ya utekelezaji wa shughuli hizo kwa viongozi wa ngazi mbalimbali katika sekta na taasisi za kiserikali hapa nchini,” alifafanua Bw. Maage.

Aliendelea kusema kuwa, vigezo vitakavyotumiwa katika kuteua viongozi hao ambao ni wabunge pamoja na Mawaziri ni pamoja na kuwa mtetezi wa Wananchi wake bila uoga akiwa ndani au nje ya Bunge, mtendaji bora wa maendeleo yenye kuonekana, sifa ya kutoa hoja zenye tija kwa kutumia lugha ya staha bila matusi, sifa ya utekelezaji wa haraka apatapo matatizo ya Wananchi wake pamoja na sifa ya kutetea demokrasia, uhuru na kutetea wanyonge.

“Faida za shindano la tuzo hizi ni kwamba zinaweka Wananchi karibu na viongozi, kuchochea utekelezaji huduma na maendeleo kwa kasi ya juu, utawla bora na uwajibikaji wa viongozi kwa Wananchi, uhusiano mzuri kati ya serikali na Wananchi na kuimarisha furaha, utulivu na amani,” alieleza Bw. Maage.

Kwa uapnde wake Mkurugenzi mkuu wa Kamati hiyo, Bw. Herman Mnenuka alisema kuwa Wananchi ndiyo nguzo kuu ya kupata kiongozi atakayepata tuzo hiyo kwani wao ndio watakaopendekeza kwa majina ya wabunge pamoja na wamaziri wanaofaa kuwania tuzo hiyo. Katika tuzo hiyo, hatua ya kwanza, wananchi wanapaswa kupendekeza wabumge 15 kwa kila kigezo shindanishi, pia Wananchi watawateua Mawaziri 5 kwa kila kipengele shindanishi kwaajili ya kuingia kwenye ushindani wa tuzo hiyo na wabunge watano watano na Mawaziri watatu watakaopata kura nyingi kwa njia ya ujumbe mfupi (SMS) kutoka kwa wananchi wataingia katika fainali ya king’anyiro kuwania tuzo hiyo.

Aidha aliongeza kuwa, katika hatua nyingine, Wananchi kupitia simu watawachuja washiriki waliofika hatua ya fainali kwa kutuma SMS na mbunge pamoja na waziri atakayepata kura nyingi ndiye atakaye kuwa mshindi katika kilele cha tuzo hiyo kitakachofanyika tarehe 23 Desemba Mwaka huu.

“Niwaombe wananchi washiriki kikamilifu ili kuweza kupata kiongozi anayejishughulisha na anayechapa kazi kupitia tuzo hii na mwisho wa kilele tutapata mshindi wa kila kipengele kilichowekwa ambacho kina tija muhimu katika taifa kupitia waheshimiwa wabunge na mawaziri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alieleza Bw. Mnenuka.

Aidha aliongeza kuwa, Wananchi watapendekeza majina kwa kutuma ujumbe mfupi simu kupitia namba 15555 kwa mitandao ya Tigo, Airtel, Vodacom, Halotel Smart na Zantel na kila SMS itatozwa gharama ya shilingi 500 vilevile kutakuwa na vipindi vya radio runinga na magazeti ili kuwakumbusha mwenendo na hatua za shindano la tuzo za THSDA hadi siku ya kilele. Hizi ni tuzo za kwanza kuandaliwa hapa nchini na kamati hiyo ambazo zitafanyika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa rasilimali fedha.

MSAMA AUCTION MART YAANZA KUWAKAMATA WATU WOTE WANAOFANYA UHARAMIA WA KAZI ZA SANAA NCHI NZIMA

$
0
0
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Auction Mart, Alex Msama akizungumza na Waandishi wa habari mara baada ya kukamilisha zoezi la ukamataji wa wezi wa kazi za sanaa kwa kurudufu bila kibali na kuwauzia watu kwenye simu zao za mkononi, jambo ambalo ni kinyume cha sheria ya haki miliki na haki shiriki.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Auction Mart, Alex Msama  akiwa amebeba vifaa  vilivyokamatwa ambavyo vinatumika kurudufu kazi za wasanii

 Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Auction Mart, Alex Msama  akionyesha watu wanaotakiwa kukamatwa ambao wamekutwa wanafanya kazi ya kurudufu kazi za wasanii
 Askari wa jeshi la Polisi wakiwa wamemkamata mmoja wa wezi wa kazi za wasanii wanaorudufu kwa kutumia kompyuta eneo la Kariakoo
 Askari wa jeshi la Polisi wakiwa wamemkamata mmoja wa wezi wa kazi za wasanii wanaorudufu kwa kutumia kompyuta eneo la Kariakoo
 Askari wa jeshi la Polisi wakiwa wamemkamata mmoja wa wezi wa kazi za wasanii wanaorudufu kwa kutumia kompyuta eneo la Kariakoo ambapo Msama SAuction Mart inafanya zoezi la kuwakamata watu wanaorudufu kazi za Wasanii kwa kutumia Kompyuta.
 Vijana wa kazi kutoka Msama Auction Mart wakipakia vyombo vinavyo tumika kurudufu kazi za wasanii kinyume cha Sheria.

RAIS DKT. MAGUFULI ATUNUKU VYETI VYA SHUKRANI NA PONGEZI KWA KAMATI MAALUMU ZA UCHUNGUZI NA MAJADILIANO KUHUSU RASILIMALI ZA MADINI NCHINI

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtunuku Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi cheti cha pongezi na shukrani  katika hafla iliyofanyika Ikulu jijjini Dar es salaam leo Oktoba 23, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtunuku Profesa Nehemiah Eliakim Osoro  cheti cha pongezi na shukrani katika hafla iliyofanyika Ikulu jijjini Dar es salaam leo Oktoba 23, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtunuku  Mwenyekiti wa Kamati ya Kwanza ya Makinikia Profesa Abdulkarim Mruma     cheti cha pongezi na shukrani  katika hafla iliyofanyika Ikulu jijjini Dar es salaam leo Oktoba 23, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtunuku Mama Fatuma Ndugai ambaye ni Mke wa Spika Mhe. Job Ndugai cheti cha pongezi na shukrani mwenyekiti wa Kamati Maalumu ya Uchunguzi wa Makinikia Profesa Osolo katika hafla iliyofanyika Ikulu jijjini Dar es salaam leo Oktoba 23, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Katibu wa Bunge Mhe. Stephen Kagaigai baada ya kumtunuku Spika Job Ndugai (kupitia kwa mkewe Mama Fatuma Ndugai) cheti cha pongezi na shukrani mwenyekiti wa Kamati Maalumu ya Uchunguzi wa Makinikia Profesa Osolo katika hafla iliyofanyika Ikulu jijjini Dar es salaam leo Oktoba 23, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtunuku  Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi  cheti cha pongezi na shukrani  katika hafla iliyofanyika Ikulu jijjini Dar es salaam leo Oktoba 23, 2017 .

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Viewing all 110182 articles
Browse latest View live




Latest Images