Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110173 articles
Browse latest View live

MAKALA YA SHERIA:AINA MBILI ZA MALI ANAZOSTAHILI MJANE.

$
0
0
Na Bashir Yakub.

Maudhui katika makala haya yanatoka katika Sheria ya Ndoa, sura ya 29, iliyofanyiwa marekebisho 2010, pamoja na Sheria ya Usimamizi na Uendeshaji wa Mirathi,Sura ya 325, R;E 2002. Ziko aina mbili za mali anazostahili mjane.

 Kwanza ni mali inayotokana na machumo ya pamoja yeye na marehemu mme wake . Pili ni urithi anaostashili kupata kama mrithi wa marehemu.

Kwa mfano, mume amefariki. Lakini kabla hajafa huko nyuma walijenga nyumba yeye pamoja na mke wake. Au walinunua kiwanja yeye na mke au gari nk. Mme sasa amefariki na kuacha hizo mali. Katika mali ya namna hii kuna sura mbili.

Sura ya kwanza ni kuwa katika mali hii kuna “share” ya mme na kuna “share “ ya mke. Na “share” ya kila mmoja inatokana na ukweli kuwa kila mmoja kati yao alichangia kupatikana kwa hiyo mali. Kwahiyo kila mmoja ana “share” yake kutokana na kile kiwango alichochangia. Na mchango tulishasema kuwa sio leta ni lete. Hata kazi za nyumbani kama kupika, kufua, kulea watoto nk. nazo ni mchango katka kupatikana kwa mali.

Sura ya pili, ni kuwa kama mume amekufa basi mwanamke kama mke halali anastahili urithi kutoka mali za mumewe. Urithi huu utatoka katika zile mali anazomiliki mumewe yeye kama yeye. Urithi utatoka katika “share” ya mume na si katika “share” nyingine.

Kwahiyo katika mali ileile mjane atakuwa na haki za aina mbili. Haki ya kupata sehemu yake aliyochangia katika kupatikana kwa mali, na haki ya kurithi mali ya mme wake.



AFYABANDO KAMPENI KUWAKOMBOA WATANZANIA

$
0
0
Mtaalam Mwelekezi wa Afyabando-Nordic Foundation Tanzania, Dkt. Respicius Salvatory akiongea na waandishi wa habari Dar es Salaam leo Septemba 3 2017, wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya kujishindia kadi ya bima ya Afya ijulikanayo kama ‘AfyaBando’. Kulia ni Afisa Mwandamizi Mipango na Utawala wa Taasisi ya Nordic, Maria Nimrod na Afisa Tehama wa Taasisi hiyo, Dickson Leonard.

Afisa Mwandamizi Mipango na Utawala wa Taasisi ya Nordic, Maria Nimrod akifafanua jambo kwa waandishi wa habari Dar es Salaam leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya kujishindia kadi ya bima ya Afya ijulikanayo kama ‘AfyaBando’. Pamoja naye ni Mtaalam Mwelekezi wa Afyabando-Nordic Foundation Tanzania, Dkt. Respicius Salvatory (wa pili kulia) , Afisa Tehama wa Taasis hiyo, Dicson Leonard Afisa Afya na Teddy Uledi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII YATEMBELEA HIFADHI YA MAZINGIRA ASILIA ULUGURU NA JUMUIYA YA HIFADHI YA WANYAMAPORI YA WAMI MBIKI MKOANI MOROGORO

$
0
0
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (katikati) akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakati wa ziara yao ya kikazi katika eneo la Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya Wami Mbiki/Ushoroba mkoani Morogoro ambayo iliyolenga kubaini changamoto mbalimbali za uhifadhi kwa ajili ya kuishauri Serikali namna bora ya kukabiliana nazo.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (kulia) na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos Santos Silayo (wa tatu kulia) wakiongoza Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kupanda mlima katika Hifadhi ya Mazingira Asilia Uluguru mkoani Morogoro wakati wa ziara yao iliyolenga kubaini changamoto mbalimbali za uhifadhi kwa ajili ya kuishauri Serikali namna bora ya kukabiliana nazo. 
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos Santos Silayo (kulia) akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakati wa ziara yao ya kikazi katika Hifadhi ya Mazingira Asilia Uluguru mkoani. 
 Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Mazingira Asilia Uluguru, Cathbert Mafupa (kushoto) akitoa maelezo kwa Wajumbe wa Kamati hiyo kuhusu Hifadhi hiyo. 
 Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Mary Chatanda (wa tatu kushoto) akizungumza kutaka ufafanuzi wa baadhi ya mambo kuhusu Hifadhi ya Mazingira Asilia Uluguru wakati wa ziara ya kamati kwenye hifadhi hiyo. Wengine pichani ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (wa tatu kulia), Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhandisi Atashasta Ndetiye (wa nne kulia) na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu, Prof. Dos Santos Silayo (wa pili kulia). 
 Wajumbe wa Kamati wakikagua eneo la Hifadhi ya Mazingira Asilia Uluguru mkoani Morogoro wakati wa ziara yao ya kikazi ya kuangalia changamoto mbalimbali za uhifadhi zinazoikabili hifadhi hiyo kwa ajili ya kuishauri Serikali namna bora ya kukabiliana nazo. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MAGAZETI YA JUMANNE LEO SEPT 5, 2017

RATIBA YA MAZISHI YA MAREHEMU MUHINGO RWEYAMAMU.

$
0
0

Leo Jumanne,Septemba 5,2017

Asubuhi Saa 2:00 -300: Chai nyumbani kwa Marehemu, Mbezi Msigani.

Asubuhi Saa 3:00- 5:00:Ibaada Kanisa la KKT Mbezi Luisi,lilipo Kibanda cha Mkaa,Mbezi.

Saa 5:00-6:00:Msafara kwenda Viwanja vya Mnazi Mmoja.

Mchana Saa 6:00-8:00: Hafla ya kuaga mwili Mnazi Mmoja

Mchana Saa 8:00-8:20:Kuelekea Kinondoni Makaburini

Mchana Saa 8:20-9:00:Maziko Kinondoni Makaburini.

Jioni Saa 9:00-10:00:Kurejea nyumbani kwa Marehemu Mbezi Msigani

Kwa Mawasiliano zaidi:

Stella Nyemenohi 0758295529
Joyce Mmasi 0714233929
 Sanduku lenye mwili wa Marehemu Muhingo Rweyamamu,nyumbani kwake tayari kwa ratiba ya kuagwa mapema leo katika viwanja vya Mnazi mmoja na baadae maziko yake kufanyika katika makaburi ya Kinondoni,jijini Dar Es Salaam
Pichani kulia Waziri wa Habari,Sanaa,Utamaduni na Michezo Mh.Dkt Harrison Mwakyembe akizungumza na ndugu wa marehemu jana usiku nyumbani kwa marehemu Muhingo kwa ajili ya kufariji wafiwa.
  Waziri wa Habari,Sanaa,Utamaduni na Michezo Mh.Dkt Harrison Mwakyembe akisaini kitabu cha maombolozo jana usiku nyumbani kwa marehemu Muhingo.

BANDARI TANGA YAZIDI KUCHANUA KILIMANJARO CUP YAITANDIKA SCOPION YA ARUSHA VIKAPU 91-60

$
0
0
Wachezaji wa timu ya Bandari Tanga wakichuano na timu ya Scopion ya Arusha ambapo Bandari Tanga iliendelea kung'ara kwa kuibuka na ushindi wa vikapu 91 kwa 60 kwenye mashindano ya Kilimanjaro Cup yanayoendelea kwenye viwanja vya KCMC Mjini Moshi

 Wachezaji wa timu ya Bandari Tanga wakichuana na timu ya Scopion ya Arusha ambapo Bandari Tanga iliendelea kung'ara kwa kuibuka na ushindi wa vikapu 91 kwa 60 kwenye mchezo uliochezwa kwenye viwanja vya KCMC Mjini Moshi.
 Wachezaji wa timu ya Bandari Tanga wakipewa mawaidha na Kocha Mkuu wa timu hiyo,Mohamed Fazal wakati wa mapumziko katika mchezo wa michuano ya kikapu ya Kilimanjaro Cup ambapo Bandari Tanga illibuka na ushindi wa vikapu 91 kwa 60 ambapo leo Bandari watawavaa timu ya Mtwara.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

SERIKALI YA AWAMU YA TANO YA RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFURI IMERUDISHA IMANI KWA WANANCHI

$
0
0
Na David John Mwanza

 KADA wa   Chama cha Mapinduzi na Mwenyekiti Mstaafu wa Serikali  ya Mtaa wa kiloleli B Jijini Mwanza Joshua Mnana amesema kazi nzuri inayofanywa na Serikali inasababisha kukimarisha Chama  cha Mapinduzi CCM.

Mwenyekiti huyo mstaafu alisema kwamba hivi Sasa Makada na wanachama wa CCM wanatembea kwa kujidai na hiyo nikutokana na serikali iliyopo madarakani inafanya  vizuri ukilinganisha na huko nyuma.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Jijini hapa Mnana alisema hata kuhairishwa kwa baadhi ya Chaguzi ambazo zinaendelea kufanyika ndani ya Chama hicho niwazi kwamba hivi watu wanakipenda chama hivyo yeye haoni Kama kasoro.

 "Unajuwa ndugu waandishi zamani kulikuwa hakuna hiyo hali nasababu ilikuwa wanachama walikuwa wanashindwa kuchukua hata fomu ya kugombea kutokana na chama kilivyokuwa."alisema Mnana

  Aliongeza kuwa kuingia madarakani kwa serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt.John Magufuli kumefanya watu kukubali kazi zinazofanyika na kurudisha imani kubwa kwa Chama cha Mapinduzi.

Aidha akizungumzia mtaa wake wa kiloleli alisema kihalisia eneo hilo ni la milima lakini chini ya uongozi wa Rais Magufuli hivi wamepata barabara ya kiwango cha lami ambayo pia zimewekwa na taa nakufanya eneo hilo kuwa tofauti na mitaa mingine mkoani Mwanza.

  Pia Mnana aliomba viongozi wa eneo hilo ambao wapo madarakani hivi sasa kufanya utaratibu ili barabara izinduliwe na Rais Dkt Magufuli huku akiipongeza Kampuni ya Nyanza Road kwa kazi nzuri ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha juu.

  "Binafsi nitaendelea kuwa Mwanachama mwadilifu wa Chama cha Mapinduzi ccm na naunga mkono kwa asilimia mia moja kazi nzuri inayofanywa na rais Magufuli. "alisema Mnana

RC MTAKA APIGA MARUFUKU USHURU WA BIASHARA NDOGONDOGO MAARUFU KAMA MATANDIKO

$
0
0

Na Stella Kalinga, Simiyu

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka amepiga marufuku Halmashauri zote Mkoani humo kutoza ushuru wa biashara ndogondogo zinazofanywa na wananchi kwa kutandika na kupanga bidhaa zao chini au kuuzwa katika mabeseni maarufu kama matandiko.

Mtaka ametoa agizo hilo baada ya Mwenyekiti wa Kijiji cha Igaganulwa, Mhe.Nhandi Masaka Kachala na baadhi ya wananchi kutoa malalamiko yao kuhusu ushuru huo, wakati wa ziara yake wilayani Bariadi yenye lengo la kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi .

Amesema suala hilo lilishatolewa maelekezo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli, hivyo Halmashauri zinapaswa kubuni vyanzo vipya vya mapato vyenye tija kwa Halmashauri na wananchi badala ya kutegemea kutoza ushuru unaowakwaza wananchi.

“Kama kuna Halmashauri bado inatoza ushuru wa matandiko wamechelewa sana, kuanzia kesho hamna huo ushuru, kama ninyi mnafikiri mapato ni kutoza tandiko la nyanya, dagaa, mchicha na ninyi kama wakuu wa idara hiki ndicho chanzo mnachokifikiria kichwani hiyo kazi haiwafai, mkatafute kazi nyingine ya kufanya” alisema Mtaka.

“Halmashauri lazima ibuni chanzo cha mapato chenye tija kwenye Halmashauri na watu. Sasa mtu anahangaika na beseni lake la nyanya wewe unamtoza ushuru, umechangia nini, beseni si lako nyanya si zako” alisema Mtaka.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na wananchi wa Kata ya Dutwa(hawapo pichani) Wilayani Bariadi katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Igaganulwa wakati wa ziara yake aliyofanya kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga akizungumza na wananchi wa Kata ya Dutwa (hawapo pichani)katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Igaganulwa wakati wa ziara Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka aliyofanya Wilayani humo kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
Diwani wa Kata ya Dutwa Wilayani Bariadi, Mhe.Mapolu Nunde Mkingwa akizungumza na wananchi wa Kata hiyo (hawapo pichani)katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Igaganulwa wakati wa ziara Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka aliyofanya Wilayani humo kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha Igaganulwa Kata ya Dutwa (hawapo pichani) Wilayani Bariadi katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika Kijijini hapo wakati wa ziara yake aliyofanya kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.


China na Tanzania kuongeza Nguvu katika kupunguza Umaskini Nchini

$
0
0

Na Adili Mhina.

Taasisi ya Kimataifa ya Kupunguza Umaskini China (IPRCC) imeahidi kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano baina yake na Wizara ya Fedha na Mipango kupitia Tume ya Mipango kwa lengo la kuongeza kasi ya maendeleo na kupunguza umaskini nchini.

Uamuzi huo umefikiwa katika kikao cha wataalamu kutoka Wiraza ya Fedha na Mipango kupitia Tume ya Mipango wakiongozwa na Kaimu Katibu Mtendaji Bw. Maduka Kessy na ujumbe kutoka taasisi hiyo kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika kikao hicho kiongozi wa ujumbe kutoka China Bw. Xia Gengsheng alieleza kuwa maeneo mapya yanayotarajiwa ni pamoja na kuanzisha vituo vingingine vya mfano vya kilimo katika vijiji mbalimbali hapa nchini.

Bw. Xia alieleza kuwa wameamua kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano kutokana na mafanikio yaliyojitokeza katika juhudi za kupambana na umaskini nchini hususan katika kutoa elimu ya kilimo kwa wakulima kupitia kuanzishwa kwa Kijiji cha mfano cha Peapea Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro.

“Ndugu Kaimu Katibu Mtendaji naomba nikuhakikishie kwamba tutaanzisha vijiji vingine vya mfano kama kile cha Peapea na kutoa fursa kwa wananchi wengi zaidi kujifunza mbinu bora za kilimo ili waweze kuendesha kilimo chenye tija na waondokane na umaskini,” alieleza Bw. Xia.
Kaimu Katibu Mtendaji, Wizara ya Fedha na Mipango – Tume ya Mipango Bw. Maduka Kessy (wa tatu kutoka kushoto, mwenye tai nyekundu) na kiongozi wa ujumbe kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Kupunguza Umaskini China, Bw. Xia Gengsheng (wanne kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na wataalamu kutoka China na viongozi wa Tume ya Mipango.
Wataalamu kutoa Tume ya Mipango wakiwa katika kikao na Ujumbe kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Kupunguza Umaskini China (hawapo pichani).
Ujumbe kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Kupunguza Umaskini China wakiwa katika kikao na wataalamu wa Wizara ya Fedha na Mipango – Tume ya Mipango (hawapo pichani) katika ofisi za Tume ya Mipango, jijini Dar es Salaam.
Kaimu Katibu Mtendaji, Wizara ya Fedha na Mipango – Tume ya Mipango Bw. Maduka Kessy (katikati), Naibu Katibu Mtendaji, Klasta ya Biashara za Kimataifa na Mahusiano ya Uchumi Bw. Paul Sangawe (kulia) na Kaimu Naibu Katibu Mtendaji anayesimamia Klasta ya Huduma za Jamii na Idai ya Watu, Tume ya Mipango, Bw. Ibrahim Kalengo (kushoto) wakimsikiliza mjumbe (hayupo pichani) kutoka China wakatika wa kikao.



MCHANGANYIKOBIASHARATECHNOLOJIABURUDANIMICHEZOSIASAMAGAZETITV Latest News KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ARDHI,YATEMBELEA HIFADHI YA MAZINGIRA ASILIA ULUGURU NA JUMUIYA YA WANYAMAPORI YA WAMI MBIKI Home / MCHANGANYIKO / WANUFAIKA WA TASAF WAPANDE MIKOROSHO KUTUNZA MAZINGIRA NA KUJIONGEZEA KIPATO; RC NCHIMBI WANUFAIKA WA TASAF WAPANDE MIKOROSHO KUTUNZA MAZINGIRA NA KUJIONGEZEA KIPATO; RC NCHIMBI

$
0
0
Wanufaika wa mpango wa Kunusuru kaya masikini Tasaf, Mkoa wa Singida wametakiwa kupanda mikorosho ili waweze kutunza mazingira pamoja na kujiongezea kipato kutokana na zao la korosho.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi ametoa rai hiyo wakati akifungua mafunzo ya uwezeshaji kwa wasimamizi 67 wa miradi ya kutoa ajira za muda kwa wanufaika wa mpango wa Tasaf kutoka halmashauri na manispaa ya Singida.

Dkt Nchimbi amesema kutokana na kuwa ajira za muda kwa awamu hii zimelenga katika utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti hivyo amewataka Tasaf mkoa wa Singida kuwasiliana na Bodi ya Korosho waweze kupatiwa mbegu ili isipandwe miti mingine bali mikorosho.

Amesema kwa kufanya hivyo mkoa wa Singida utaweza kuwa mzalishaji mkubwa wa Korosho huku ajira hiyo ya muda ya kutunza mazingira kwa kupanda mikorosho, ikiwa imewatengenezea wanufaika hao ajira yao ya kudumu.

“Tukiweza kupanda mikorosho kwa zoezi hili la ajira za muda baada ya muda wanufaika hawa wataweza kuwa na kipato kikubwa kwa kuweza kuuza korosho zao, hii itakuwa ndio maana halisi ya mpango wa kunusuru kaya masikini ambapo zinatakiwa pia zishiriki katika kukuza uchumi”, amesema na kuongeza kuwa,
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akizungumza na wasimamizi wa miradi ya kutoa ajira za muda kwa wanufaika wa mpango wa Tasaf kutoka halmashauri na manispaa ya Singida wakati akifungua mafunzo ya uwezeshaji wa kusimamia miradi hiyo.
Wasimamizi wa miradi ya kutoa ajira za muda kwa wanufaika wa mpango wa Tasaf kutoka halmashauri na manispaa ya Singida wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Mkoa wa Singida (hayupo pichani) wakati akifungua mafunzo ya uwezeshaji wa kusimamia miradi hiyo.
Mratibu wa Tasaf Mkoa wa Singida Patrick Girigo Kasango akiwa na Afisa Ufuatiliaji kutoka Tasaf Sinith Haule wakifurahia jambo wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya uwezeshaji wa kusimamia miradi ya ajira za muda kwa wasimamizi wa kutoka halmashauri na manispaa ya Singida.

BAADA YA POLISI KUMALIZA MAHOJIANO YA MANJI NA WENZAKE WATATU,WAREJESHWA MAHAKAMANI KUENDELEA NA KESI YAO

$
0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya Jamii.

Baada ya jeshi la Polisi kumaliza mahojiano yao dhidi ya mshtakiwa  Yusuf Manji na wenzake watatu juu ya tuhuma zinazowakabili za uhujumu uchumi, mapema leo wamemkabidhi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kama ilivyoamriwa Jana.

Mbali na Manji ambaye ni mfanyabiashara maarufu nchini, washitakiwa wengine waliokabidhiwa ni Meneja Rasilimali watu wa Kampuni ya Quality Group Ltd, Deogratius Kisinda, Mtunza stoo, Abdallah Sangey na Thobias Fwere.
 
Akiwakabidhi watuhimiwa hao, wakili wa serikali mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa washtakiwa hao wamerudishwa mahakamani kama ilivyoamuriwa, baada ya polisi kumaliza kuwahoji.
Baada ya washtakiwa kukabidhiwa wakiwa salama na afya zao nzuri, Hakimu Shaidi alisema kesi hiyo itaendelea na utaratibu kama ulivyokuwa awali, ambapo itatajwa September 8/2017.

Jana mchana mahakama hiyo iliruhusu Manji na wenzake kwenda kuhojiwa na Polisi  ili kukamilisha upelelezi katika kesi ya uhujumu uchumi.

KESI YA MENO YA TEMBO INAYOMKABIRI YUSUF ALI ALMAARUFU MPEMBA WA MAGUFULI KUPELEKWA MAHAKAMA YA MAFISADI

$
0
0

Na Karama Kenyunko, blogu ya Jamii.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeelezwa kuwa, hati ya mashtaka ya kesi ya kujihusisha na biashara ya meno ya tembo dhidi ya mfanyabiashara Yusuf Alli maarufu kama mpemba wa Magufuli’ inatarajiwa kupelekwa Mahakama ya mafisadi.

Hayo yameelezwa na wakili wa serikali, Elia Athanas mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba kesi hiyo ilipokuja kwa kutajwa. "Mheshimwa, jalada la kesi hii limekamilika, hivyo naomba muda ili wapeleke hati ya mashtaka Mahaka Kuu Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi 'Mahakama ya Mafisadi'.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi September 19/2017.

Yusuf anashtakiwa pamoja na Charles Mrutu, mkazi wa Mlimba, Morogoro, Benedict Kungwa, mkazi wa Mbagala Chamazi, Jumanne Chima, mkazi wa Mbezi, Ahmed Nyagongo, dereva na Pius Kulagwa, wanakabiliwa na mashitaka manne ya kujihusisha na biashara ya meno ya tembo yenye thamani ya Sh.milioni 785.6.

Inadaiwa katika tarehe tofauti kati ya Januari, 2014 na Oktoba, mwaka huu wakiwa Dar es Salaam, Tanga, Iringa na Mtwara, walijihusisha na mtandao wa ujangili kwa kukusanya na kuuza nyara za serikali ambazo ni

vipande 50 vya meno ya tembo vyenye thamani ya Dola za Marekani 180,000 sawa na Sh milioni 392.8 bila kuwa na kibali cha Mkurugenzi wa Wanyamapori.
Watuhumiwa hao wakiwa katika viunga vya Mahakama ya Kisutu,mapema leo kwenye kesi yao ya kudaiwa  kujihusisha na biashara ya meno ya tembo,ambayo kwa sasa inatarajiwa kupelekwa Mahakama ya mafisadi.

HALOTEL, FINCA WAZINDUA HUDUMA MPYA YA KIBENKI KUPITIA SIMU YA MKONONI

$
0
0
 Mgeni rasmi katika uzinduzi wa huduma mpya ya HaloYako ya Kampuni ya Simu ya Halopesa kwa kushurikiania na Finca Microfinance Bank, Kamishna  wa Fedha za Nje wa Wizara ya Fedha na Mipango, John Rubuga (katikati) akiwa pamoja na Mkurugeni Mkuu wa Kampuni ya Simu ya Halotel Tanzania, Le Van Dai (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Finca Microfinance Bank, Issa Ngwegwe wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma hiyo, uliofanyika kwenye ukumbi wa Hoteli ya Serena, Jijini Dar es salaam Septemba 5, 2017.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa huduma hiyo, Mgeni rasmi ambaye alimuwakilisha Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara ya Fedha na Mipango, John Rubuga amesema kuwa serikali imeendelea kutengeneza mazingira rafiki ya uwekezaji kwa wafanyabiashara wakubwa na wadogo ili kurahisisha huduma na kutatua changamoto zinazowakabili Watanzania hususan katika maendeleo ya kiuchumi.

 “Serikali iko tayari kushirikiana na kampuni mbalimbali zenye malengo ya kuondoa umaskini kwa watanzania kwa kukuza kipato chao ili kuboresha maisha. Tunaamini pia kupitia huduma hii ya Haloyako Watanzania wengi zaidi ambao hawatumii huduma za benki wanaweza kutumia ili kuweza kufanikisha malengo yao ya kifedha,” alisema na kuongeza kuwa “Halotel na FINCA wana malengo sawa, ambayo wanalenga kuwasaidia watanzania wenye hali ya chini na wakati ambao wengi wao wako maeneo ya vijijini, ni Imani yetu kuwa ushirikiano huu utakuwa na manufaa makubwa kwa jamii ya Watanzania na tutajenga utamaduni wa kujiwekea akiba”.
Aidha, amezitaka kampuni hizo kuhakikisha zinatoa elimu ya kutosha ili Watanzania waweze kuelewa umuhimu wa huduma hiyo na kuweza kuitumia vyema huku akitoa wito kwa jamii ya Watanzania kuepuka kuhifadhi hela ndani na kujenga utamaduni ya kujiwekea akiba.

Kwa upande wa Halotel, Mkurugenzi Mtendaji wake, Le Van Dai alisema “Tunashukuru sana kwa uhusiano huu ambao tumeujenga kati yetu na FINCA ambao kwa miaka mingi wamekuwa wakitoa huduma za kifedha kwa jamii ya Watanzania, Kwa uapnde wetu sisi hii ni hatua kubwa sana katika kuhakikisha tunatatua changamoto ya huduma za kifedha kwa Watanzania, Tumejitahidi kwa kiasi kikubwa kuhakikisha hatuishii kuwa tu kampuni ya Mawasiliano ila tunataka kuwa kampuni inayoishi maisha ya Watanzania”

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Finca, Issa Ngwegwe Aliongeza kuwa lengo kubwa ya FINCA ni kutoa suluhisho la kutokomeza umaskini kwa kusaidia watu kujenga mitaji, kutengeneza ajira na kuboresha maisha.

“Haloyako sio tu huduma ya kifedha kupitia simu ya mkononi bali ni akaunti ya akiba ya malengo ambayo itakuwa jibu kwa Watanzania ambao wanataka huduma za kifedha ili kuweza kuweka akiba kutimiza mahitaji yao ya kifedha kama vile kulipa karo, kodi ya nyumba, kuwekeza, kulipia huduma za afya na pia kusafiri, Kupitia Haloyako mteja anaweza kuweka mipango na kuanza kuweka akiba ili kutimiza lengo lake na hivyo kuepuka madeni au kushindwa kukidhi mahitaji ya kifedha ya familia.  Alihitimisha Ngwegwe.

Huduma ya HALOYAKO inapatikana kupitia huduma ya HALOPESA inayotolewa na kampuni ya mawasiliano ya Halotel ambayo ni huduma ya kifedha inayomwezesha mteja kutuma na kupokea fedha kwa urahisi na kwa usalama.
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa huduma mpya ya HaloYako ya Kampuni ya Simu ya Halopesa kwa kushurikiania na Finca Microfinance Bank, Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara ya Fedha na Mipango, John Rubuga (katikati) akiwa pamoja na Mkurugeni Mkuu wa Kampuni ya Simu ya Halotel Tanzania, Le Van Dai (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Finca Microfinance Bank, Issa Ngwegwe wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma hiyo, uliofanyika kwenye ukumbi wa Hoteli ya Serena, Jijini Dar es salaam Septemba 5, 2017.
Picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi
Picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa Kampuni ya ya Halotel na Finca Microfinance Bank.

Serikali Kuanzisha Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi

$
0
0
Mkurugenzi wa Barabara toka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi John Ngowi akielezea jambo wakati wa kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT) leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Kampuni ya EcomResearch ambayo ndio mshauri mwelekezi wa uanzishwaji wa taasisi hiyo Profesa Godwin Mjema na Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala toka wizara hiyo Bw. Stephen Mushi.
Mwenyekiti wa Kampuni ya EcomResearch ambayo ndio mshauri mwelekezi wa uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT), Profesa Godwin Mjema akifafanua jambo wakati wa kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi wa Barabara toka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi John Ngowi na Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala toka wizara hiyo Bw. Stephen Mushi.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Bi. Segolena Francis akifafanua jambo wakati wa kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT) leo Jijini Dar es Salaam.
Mtaalamu wa Utafiti kutoka Kampuni ya EcomResearch ambayo ndio mshauri mwelekezi wa uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT),akifafanua jambo wakati wa kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Barabara toka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi John Ngowi (wanne kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa sekta ya ujenzi mara baada ya kufungua kongamano la pili la majadiliano kuhusu uanzishwaji wa Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT) leo Jijini Dar es Salaam.

New Government of Tanzania Information Systems to Improve Delivery of Public Services

$
0
0
United States Embassy Chargé d’Affaires, a.i. Dr. Inmi Patterson delivers remarks during the launch of the Government of Tanzania’s redesigned Planning, Budgeting, and Reporting (PlanRep) System and the new Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS) at a ceremony in Dodoma.
Prime Minister Kassim Majaliwa, United States Embassy Chargé d’Affaires Dr. Inmi Patterson (on his left) and senior Government Ministers officials officiates the launch of the Government of Tanzania’s redesigned Planning, Budgeting, and Reporting (PlanRep) System and the new Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS) in Dodoma.
United States Agency for International Development (USAID), Mission Director, Andrew Karas (2nd left) and the Minister for Health, Community Development, Gender, Elderly and Children, Ms. Ummy Mwalimu (right), following the launch of the Government of Tanzania’s redesigned Planning, Budgeting, and Reporting (PlanRep) System and the new Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS) at a ceremony in Dodoma.

Dodoma (September 5) – Prime Minister of the United Republic of Tanzania, Kassim Majaliwa officiated the launch of the Government of Tanzania’s redesigned Planning, Budgeting, and Reporting (PlanRep) System and the new Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS) today at a ceremony in Dodoma. He was joined by U.S. Embassy Chargé d’Affaires Dr. Inmi Patterson and a number of senior Government officials and Ministers, reflecting the wide- reaching impact of PlanRep and FFARS across sectors and government institutions.

Developed in partnership with the U.S. Government through the United States Agency for International Development (USAID), these computer-based information management systems will play complementary roles in preparing plans and budgets and standardizing financial management at every level of government. In particular, these platforms will ensure the efficient, transparent, and accountable use of funds among Local Government Authorities (LGAs) and facilities, paving the way for improved delivery of public services to citizens.

Introduced over a decade ago as a planning, reporting, and budgeting tool for LGAs, PlanRep’s redesign marks a number of improvements over its predecessor. Whereas the original version was accessed offline, with users across the government relying on different versions of the software, the updated system provides a uniform, online format accessible anytime, anywhere. Additionally, the new web-based version allows PlanRep to share documents and information with other government information systems, eliminating the lengthy, error-prone process of uploading documents manually. With over 1,500 users trained to use the new system, PlanRep will operate across all public sectors to provide a more efficient, transparent, and accountable system of providing public services to citizens.

While PlanRep assists with planning, budgeting, and reporting revenue across multiple levels of government, FFARS serves as an accounting and reporting system for facilities such as schools and health centers, where funding for public services is increasingly being managed. FFARS offers service providers a simple, standardized, set of documents and processes that enable them to record the availability and source of their funding for core services at each facility. FFARS also tracks how funds are used and ensures compliance with procurement regulations and reporting requirements.

With this information, the Government of Tanzania will maintain a more robust public financial management system that increases transparency so that service providers are more accountable to the communities and organizations they serve. “The United States is proud to partner with Tanzania as you work toward a future marked by transparent government, sustainable development and shared prosperity,” remarked Chargé d’Affaires Inmi Patterson of the U.S. Embassy in Dar es Salaam during the ceremony. “Together, these two systems will increase efficiency and improve financial management, enabling the Government of Tanzania to more effectively distribute its financial resources and respond to citizen needs.”

U.S. Government support to PlanRep and FFARS falls under the USAID Public Sector Systems Strengthening (PS3) activity. Designed in partnership with the Government of Tanzania, PS3 works in 13 regions and 93 LGAs to strengthen public service delivery through improved governance, finance, human resources, and information systems. In addition to the design and rollout of PlanRep and FFARS, PS3 recently supported the launch of a standardized website layout for regional secretariats and LGAs nationwide earlier in March of this year.

MAKAMU WA RAIS AZINDUA TAMASHA LA JINSIA JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa uzinduzi wa Tamasha la Jinsia linalofanyika kwenye viwanja vya TGNP Mabibo jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akijadiliana jambo na Mwenyekiti wa Bodi ya TGNP Mtandao Dkt. Vicensia Shule (kushoto) wakati wa sherehe za uzinduzi wa Tamasha la Jinsia lililoandaliwa na TGNP Mtandao. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea tuzo ya Uongozi kwa kuwa Makamu wa Rais wa Kwanza Mwanamke na kutambua mchango wake katika kusimamia na kuhamasisha usawa wa kijinsia na uwezeshaji wanawake kutoka kwa mwenyekiti wa Bodi ya TGNP Mtandao Dkt. Vicensia Shule (kushoto) wakati wa sherehe za uzinduzi wa Tamasha la Jinsia lililoandaliwa na TGNP Mtandao.

ALTO MDENYE ATUSUA MAPENE YA VODACOM TANZANIA-NJOMBE

$
0
0
Meneja Mauzo wa Vodacom Tanzania Njombe,Benedict Kitongwa(kulia)akimkabidhi mshindi wa kitita cha shilingi Milioni 15/-Alto Mdenye(katikati)alizojishindia kupitia Promosheni ya Tusua Mapene inayoendeshwa na kampuni hiyo. Ili Mteja aweze kushiriki kwenye promosheni hii anatakiwa kutuma neno “CHECK” au “VODA” kwenda namba 15544, kwa gharama ya shilingi 300 tu,Anaeshuhudia kushoto ni Meneja wa Benki ya NMB Njombe,Aloycius Shija.
Meneja wa Benki ya NMB Njombe,Aloycius Shija, Mshindi wa kitita cha shilingi Milioni 15/-Alto Mdenye(katikati) wakifurahia jambo pamoja na Meneja Mauzo wa Vodacom Tanzania Njombe,Benedict Kitongwa,Wakati wa hafla fupi ya kukabidhiwa kitita chake alichojishindia kupitia Promosheni ya Tusua Mapene inayoendeshwa na kampuni hiyo. Ili Mteja aweze kushiriki kwenye promosheni hii anatakiwa kutuma neno “CHECK” au “VODA” kwenda namba 15544, kwa gharama ya shilingi 300 tu.

IDRIS SULTAN AZINDUA VIATU VYAKE

$
0
0
 Mshindiwa Big brother Afrika 2014 Idris Sultan amezindua viatu vyake viitwavyo SULTAN by FOREMEN akiwa pamoja na klabu ya GENTLEMAN ya Jack Daniel. Uzinduzi huu ulifanyika pamoja kama namna ya kuwaunganisha wanaume wa Tanzania kuwa sehemu ya viatu hivi maalum na umoja endelevu.
 SULTAN by FORMEN ni chapa ya viatu iliyotengenezwa kwa kuzingatia unadhifu, ubora, starehe (comfort) na hadhi ya uzito wa viatu vya mwanaume wa kitanzania.
“Tumetengeneza dizaini tofauti zit akazoingia sokoni kubadilisha ulimwengu wa fasheni katika usafi, unadhifu, furahanauchangamfu. Aina hii ya viatu inawakilisha mwanaume wa kitanzania anayefanya kazi zake kwa bidii, kwa ubunifu akiwa na muonekano wa tofauti unaopendeza” asema Idris.
 Chapa hii ya SULTAN by FOREMEN ni mafanikio mapya kwa Idris ukiacha mafanikio yake mengine aliyoyapata hivi karibuni kama kuchaguliwa kuigiza katika movie ya Hollywood marekani itakayogharimu takribani dola million 5. 
Idris ambaye alifanikiwa kukonga nyoyo za mashabiki wa filamu Tanzania baada ya kushiriki katika filamu ya KIUMENI ambayo imeshinda tunzo mbili katika tamasha la filamu la ZIFF
Idris ni mchekeshaji na kijana maarufu anayependa kuvaa vizuri na kwenda na wakati hivyo atauza viatu hivi kwa bei nafuu ilikila mtanzania aweze kuvimudu.
 Uzinduzi huu wa viatu vya SULTAN klabu ya GENTLEMAN ya Jack Daniel ulibarikiwa na viongozi wa serikali, wanamzuziki, wanamitindo, wabunifu, waigizaji na watu wengi mashuhuri.

SERIKALI YASIMIKA TAA ZA KUONGOZEA MAGARI NA ABIRIA JIJINI TANGA

$
0
0
 Mafundi wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wakifunga taa za kuongozea magari (traffic lights) katika makutano ya barabara za Taifa na Pangani jijini Tanga. Mradi huo wa kwanza kufanyika jijini Tanga unahusiha taa za kuongozea magari na waenda kwa miguu katika makutano ya barabara za Taifa na Pangani pamoja na makutano ya barabara za Swahili, Uhuru na ile ya Hospital ya Bombo. Taa hizo zitatumia nishati ya umeme jua.

Na Theresia Mwami – TEMESA TANGA
Serikali kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) inatekeleza miradi miwili ya taa za kuongozea magari na abiria (traffic lights) jijini Tanga katika makutano ya barabara za Taifa na Pangani, pamoja na makutano ya barabara za Swahili, Uhuru na ile inayoelekea hospitali ya Bombo. Ifahamike kuwa mji wa Tanga haujawahi kuwa na taa za kuongozea magari na waenda kwa miguu hapo kabla, zaidi ya kuwa na vipita shoto kwenye baadhi ya barabara zake.

Akiongea na Waandishi wa Habari Meneja wa Kikosi cha Umeme TEMESA Mhandisi Pongeza Semakuwa alisema miradi hii miwili ya taa za barabarani hapa Tanga inahusisha taa za kuongozea magari pamoja na zile za kuongoza waenda kwa miguu kuvuka makutano hayo ya barabara. Taa hizo zitakuwa zikitumia umeme jua, nishati ambayo itaziwezesha kufanya kazi muda wote hata pale umeme wa TANESCO unapokuwa na hitilafu.

Nae Mbunge wa Jimbo la Tanga mjini Mheshimiwa Alhaj Mussa Mbaruku  ambae alipita katika eneo la mradi la makutano ya Barabara ya Pangani na Taifa maarufu kama “Taifa/Ring Junction” kujionea utekelezaji huo wa mradi wa Serikali, alisema kuwa kukamilika kwa mradi huo kutapunguza ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikitokea kwenye makutano ya barabara hizo na vile vile kuufanya mji wa Tanga kuwa wa kisasa zaidi.


Kwa upande wake Meneja wa TEMESA Tanga Mhandisi Margareth Gina alisema kuwa miradi hiyo ya usimikaji wa taa za kuongozea magari na waenda kwa miguu jijini Tanga imeiingizia TEMESA jumla ya shilingi za kitanzania milioni 434 fedha za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zitakazolipwa kwa TEMESA kupitia ofisi ya Mkurugenzi wa jiji la Tanga. Aliongeza kuwa miradi yote miwili iko mbioni kukamilika mapema mwezi huu.
 Mafundi wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wakifunga mabomba ya chuma kwa ajili ya kusimika mfumo wa taa za kuongozea magari katika makutano ya barabara za Taifa na Pangani jijini Tanga. Mradi huo wa kwanza kufanyika jijini Tanga unahusiha taa za kuongozea magari na waenda kwa miguu (traffic lights) katika makutano ya barabara za Taifa na Pangani pamoja na makutano ya barabara za Swahili, Uhuru na ile ya Hospital ya Bombo na utatumia umeme jua.
 Mafundi wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wakiunganisha nyaya kwenye “Panel za Solar” zitakazotumika katika mfumo wa taa za kuongozea magari na abiria (traffic lights) katika makutano ya barabara za Taifa na Pangani Jijini Tanga. Mradi huo wa kwanza kufanyika jijini Tanga unahusiha taa za kuongozea magari na waenda kwa miguu katika makutano ya barabara za Taifa na Pangani pamoja na makutano ya barabara za Swahili, Uhuru na ile ya Hospital ya Bombo. Taa hizo zitatumia nishati umeme jua.
Mbunge wa Tanga Mjini Mhe. Alhaj Mussa Mbaruku akiongea na watendaji wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) alipofika katika eneo la mradi wa kusimika taa za barabarani katika makutano ya barabara za Taifa na Pangani jijini Tanga. Mradi huo wa kwanza kufanyika jijini Tanga unahusiha taa za kuongozea magari na waenda kwa miguu katika makutano ya barabara za Taifa na pangazi pamoja na makutano ya barabara za Swahili, Uhuru na ile ya Hospital ya Bombo. Taa hizo zitatumia nishati ya umeme jua. kutoka kushoto ni Mhandisi Zuhura Semboja, Mhandisi Pongeza Semakuwa pamoja na Mhandisi Margaret Gina. Picha zote na Theresia Mwami - TEMESA

AZAM WAZIKARIBISHA SIMBA NA YANGA AZAM COMPLEX

$
0
0
Afisa habari  wa Azam Fc Jaffar Iddy.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

UONGOZI wa Klabu ya Azam umefurahiswa na maamuzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) kwa kuamua kutumia Uwanja wa Azam Complex kwa michezo ya nyumbani ya timu hiyo.

Hilo limekuja baada ya Bodi ya Ligi kutoa ratiba mpya na kuzitaka timu za Simba na Yanga kwenda kucheza mechi zao dhidi ya Azam katika Uwanja huo.

Akizungumza kwa niaba ya klabu ya Azam, Afisa habari Jaffar Iddy ameupongeza uongozi huo chini ya Rais mpya wa TFF Wallace Karia kwa kusimamia haki kwa kila timu kucheza katika uwanja wao wa nyumbani.

Iddy amesema kuwa, kwa miaka kadhaa wamekuwa wakilalamika hasa kushindwa kuutumia uwanja wao wa nyumbani na kwenda kutumia Uwanja wa Taifa kama wenyeji pindi wanapocheza na timu za Yanga na Simba.

"tumefurahishw ana maamuzi ya TFF na bodi ya ligi chini ya Rais Wallace Karia kwa kuamua klabu za Simba na Yanga kuja kucheza katika Uwanja wetu wa Azam Complex kwani miaka mingi sana hasa katika uongozi uliopita ulishindwa kufanya maamuzi hayo na kutunyima haki yetu ya msingi,"amesema Iddy.

Iddy amesema anawakaribisha sana Simba na Yanga katika Uwanja wa Azam kwani anakumbuka timu hizo zilishwahi kucheza kwenye Uwanja huo kipindi ambacho uwanja wa Uhuru ukiwa umefungwa.

Akiongelea maandalizi kuelekea mchezo wao Jumamosi dhidi ya Simba, Iddy amesema kuwa timu yao imejipanga vizuri kwa mchezo huo na kikosi kipo kambini wakiendelea kujifua zaidi ila watawakosa wachezaji wao wawili ambao wote ni majeruhi wakiwa katika matibabu.

Amewataja wachezaji hao ni Shaban Iddy Chilunda na Joseph Kimwaga aliyoko nchini Afrika Kusini akisubiri matibabu na akitarajiwa kufanyiwa upasuaji siku ya Alhamis.

Azam itavaana na Simba katika mchezo wa pili wa ligi kuu Vodacom huku baadhi ya wachezaji wa zamani wa timu wakiwa wamejiunga na Simba wakicheza kwa mara ya kwanza toka kuondoka katika klabu hiyo.
Viewing all 110173 articles
Browse latest View live




Latest Images