Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110029 articles
Browse latest View live

WAWEKEZAJI KUTOKA INDIA WAOMBWA KUJA KUWEKEZA HAPA NCHINI.

$
0
0
 WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles John Mwijage ameaomba wawekezaji wa viwanda wa nchini India waje hapa nchini kuwekeza kwenye sekta za viwanda. 

Hayo ameyasema leo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Pia amewaomba wakulima wa kilimo cha mbaazi za aina mbalimbali walime kwa wingi ili kuendana na soko la nchini India ambapo nchini Kwao zao hilo ni lulu kwao.

Pia amewaomba wataalum wa Kompyuta kutoka nchini India kuja hapa nchini ili kubadilishana uzoefu na watanzania hapa nchini.
 
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles John Mwijage akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo akiwaaomba wafanyabiashara na wakulima wa mbaazi hapa nchini kuzilima kwa wingi ili kuliteka soko la nchini India. Pia amewaomba wawekezaji wa nchini india waje wawekeze hapa nchini ili kukuza ushirikiano wa kibiashara kati ya India na wafanyabiashara hapa nchini.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles John Mwijageakizungumza jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kutoka nchini china.
 Amewasihi wawekezaji hapa nchini wawekeze katika viwanda vya kubangua korosho ili kurahisisha ubanguaji wa korosho hapa nchini ili kutimiza ndoto ya Tanzania ya Viwanda hapa nchini.

KAMPENI YA UZALENDO KWANZA YAZINDULIWA LEO JIJINI DAR,KUHAMASISHWA NCHI NZIMA

$
0
0

Mwenyekiti wa Kampeni ya Uzalendo Kwanza, Steven Mengele almaarufu kwa jina la kisanii Steven Nyerere, akizungumza mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema leo jijini Dar kuhusina na uzinduzi wa kampeni yao itakayojulikana kwa jina la UZALENDO KWANZA. Pichani kulia ni Msanii wa Filamu Wastara na kulia kwake ni Misayo Ndumbagwe.

kampeni hiyo imezinduliwa rasmi leo, ikiwa na lengo la kuunga mkono jitihada na juhudi zinazofanywa na Rais Dkt John Pombe Magufuli katika suala zima la kuhakikisha Tanzania inasonga mbele kimaendeleo ambapo wasanii wa muziki na filamu wapatao 250 wameshirkishwa pamoja na wachezaji wa mpira.

Steve amesema kuwa, ni wakati sasa kwa Watanzania kujenga utamaduni wa kuvienzi na kuvipenda vitu vyao kwa namna moja ama nyingine katika nyanja mbalimbali za kimaendeleo, kwa sababu nchi ni Yetu,rasimali zilizopo ni zetu,madini ni yetu,mbuga za wanyama ni vya kwetu, hivyo ni muhimu Watanzania wakaamka sasa na kuonesha uzalendo wao halisi kama ambavyo Rais Dkt John Pombe Magufuli amekuwa akionesha kwa vitendo na kusisitiza suala zima la Uzalendo ndani ya nchi yetu.

"Sisi kama Wasanii, kwa moyo mmoja tumeamua kushikamana kwa pamoja na baraka zote tunazo kushikamana na kuiunga mkono kauli mbiu ya Rais Dkt Joh Pombe Magufuli ya UZALENDO KWANZA kuwa na harakati za kuifanya Tanzania yetu na Watanzania wenyewe kuwa Wazalendo kwa nchi yao",alisema Steve Nyerere na kuongeza kuwa kauli mbiu hiyo sio kwa ajili ya Dar Es Salaam tu bali,ni kwa ajili ya Tanzania nzima.
Wasanii wa mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi wa kampeni ya UZALENDO KWANZA.
Mwenyekiti wa Kampeni ya Uzalendo Kwanza Steven Mengele almaarufu kwa jina la kisanii Steven Nyerere akitoa ufafanuzi zaidi kuhusina na kampeni hiyo ya UZALENDO KWANZA mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema leo jijini Dar,kampeni hiyo inatarajia kuhamasishwa mikoa mbalimbali nchini .Pichani kushoto ni Msanii wa Filamu ni Misayo Ndumbagwe pamoja na Kemmy .
Baadhi ya Wasanii mbalimbali wakiwa kwenye mkutano huo wa uzinduzi wa kampeni hiyo ya UZALENDO KWANZA,itakayosambazwa nchi nzima kuhakikisha wananchi wanaelewa dhana nzima ya kuwa mzalendo na nchi yako.
Mkutano ukiendelea mapema leo wa uzinduzi wa kampeni ya UZALENDO KWANZA.
Msanii wa Filamu Wastara Juma akiwahimiza Watanzania kuwa WAZALENDO KWANZA katika mambo mbalimbali ikiwemo kuvithamini vya vyumbani,pia amewaomba Watanzania kuwaunga mkono Wasanii wao kwa kununu kazi zao zilizo halisi na halali ili kuhakikisha dhama nzima ya UZALENDO KWANZA inatimia.
Baadhi ya Wasanii wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri wakati wa uzinduzi wa kampeni ya UZALENDO KWANZA,itakayopita mikoa mbalimbali kuwahamasisha wananchi kuwa Wazalendo na nchi yao na pia kumuunga mkono Rais Dkt John Pombe Magufuli katika suala zima la kuhakikisha Tanzania inasonga mbele kimaendeleo.

MAKALA MICHEZO: GADIEL MICHAEL ANAWEZA KUWA MSAADA WA NAFASI YA WINGA YANGA

$
0
0
Na. Honorius Mpangala.

Southampton ni moja ya klabu ambayo inaaminika kuwa na shule nzuri ya soka. Kuaminika huko kunatokana na matunda yaliyotokana na shule hiyo katika kukuza soka la vijana.

Katika klabu Southampton ndiko walikopita vijana kama Theo Walcott,Alex Oxlade-Chamberlain,Gareth Bale,Adam Lallana,Luke Shaw,Calum Chambers. Imani hiyo ya uwepo wa shule bora inatokana na uwezo wa vijana wanaoibuaka katika klabu Hiyo na kuhitajika sana wakati sa soko la usajili kwa wachezaji.

Licha ya kuwa na mmiliki mwanamke Katharina Liebherr,klabu hiyo imeweza kuimarika katika ufanyaji wa biashara na 
Kuhimili katika ligi kwa maana ya kutumia rasilimali zao ndani ya klabu.
Uwezo wa kasi aliyokuwa nayo Bale,Walcott na Chamberlain umetoka katika shule ya Southampton. Baada ya kufanya vyema katika klabu hiyo Ilikuwa ni Tottenham Hotspur waliamua kumsajili Bale. Wakati bale anasajiliwa ilikuwa tayari Arsenal walishamsajili Walcott. 

Bale alipofika katika klabu ya Tottenham alisajiliwa kama mlinzi wa kushoto.Alifanya vyema sana katika nafasi hiyo akiwa chini ya kocha Harry Rednap. Unaweza kusema Majeruhi ya nyota hufanikisha kumtoa kinda au kutoa nafasi kwa mchezaji mwenza katika nafasi moja.

Baada ya Bale kupata majeraha na kumweka nje kwa ya kikosi cha Tottenham,nafasi yake ilichukuliwa na Benoit Assou-Ekotto. Mkameruni huyo aliitendea vyema nafasi ile ya mlinzi wa kushoto kiasi kwamba ilitia shaka endapo Bale angelejea.

Hivyo ndivyo ilivyokuwa kurejea kwa Bale kulimfanya Rednap amtumie kama Kiungo wa pembeni kushoto. Bale alifanya vyema katika nafasi hiyo huku ile ya mlinzi ikikabidhiwa moja kwa moja kwa Ekotto.
Bale wa leo ni matokeo ya kiwango bora cha Ekotto kilichomfanya Kocha ambadilishe nafasi. Maamuzi ya Rednap ndiyo yaliyofanya Bale aje kununuliwa kwa kiasi cha pesa cha paundi milioni 85 kwenda Real Madrid.

Katika klabu ya Yanga kuna Gadiel Michael ambaye kwasasa amekuwa mlinzi bora kwa klabu na timu ya taifa.Kwa kipindi hiki ambacho Yanga wamepungua makali katika maeneo yao ya winga kulia na kushoto ingekuwa kamari nzuri endapo Mwalimu George Lwandamina angejaribu kumchezesha Gadiel kama winga na Nafasi ya ulinzi ikarejea kwa Mwinyi Haji Mngwali.


MCHENGA BBALL STARS MABINGWA WAPYA WA SPRITE BBALL KINGS 2017

$
0
0
Mabingwa wa Michuano ya Sprite BBall Kings  Mchenga BBall Stars wakiwa pamoja na Afisa Masoko msaidizi wa kampuni ya Coca-Cola Pamela Lugenge (aliyevaa t-shirt ya kijani) baada ya kukabidhiwa mfano wa hundi yenye thamani ya kiasi cha Shilingi Milioni 10 sambamba na kukabidhiwa kikomne baada ya kushinda katika mchezo wa fainali uliomalizika kwa Mchenga kushinda kwa pointi 104-94 dhidi ya TMT..



Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

TIMU ya Mchenga BBall Stars wamefanikiwa kutwaa ubingwa wa Sprite BBall Kings 2017 baada ya kuibugiza wapinzani wao TMT kwa pointi 104-94 katika fainali ya mwisho iliyofanyika mwishoni mwa wiki hii kwenye Viwanja vya Don Bosco Oysterbay Jijini Dar es salaam.

Mchenga wanakuwa mabingwa wa Kwanza wa michuano hiyo wakijinyakulia kitita cha shilingi Milioni 10 sambamba na kombe huku TMT ikijinyakulia milioni tatu baada ya kushika nafasi ya pili.

Katika mchezo wa kwanza hadi wanne TMT walifanikiwa kushinda mara mbili sawa na Mchenga na kupelekea mchezo wa tano kuwa wa kasi na ushindani huku kila upande akijaribu kutokufanya makosa na kuibuka kidedea.

Pamoja na hayo, mechi ya leo iliweze kuonyesha utofauti na ufundi mkubwa kutokana na timu zote mbili kupania kuwa bingwa jambo ambalo lilipelekea timu hizo kujikuta zikitoka sare ya pointi 84-84 kwa mara ya kwanza na kupelekea waamuzi kulazimika kuongeza dakika nyingine tano ili aweze kupatikana mshindi wa mashindano hayo na ndipo Mchenga BBall Stars alipomchapa TMT jumla ya pointi 102-94

Timu ya TMT ikiwa imeshikilia mfano wa hundi yenye thamani ya Milioni tatu baada ya kushinda nafasi ya pili michuano ya Sprite BBall Kings 2017.


Kwa upande mwingine, mchezaji Rwahabura Munyagi kutoka timu ya Mchenga BBall Stars ameweza kushinda nafasi ya mchezaji bora 'MVP' kwa kuweza kuipigania timu yake kushinda mchezo wa leo.

 Afisa Masoko msaidizi wa kampuni ya Coca-Cola Pamela Lugenge aliweza kuwakabidhi mabingwa hao wapya wa Sprite BBall Kings 2017 mfano wa hundi ya kiasi cha Milioni 10 pamona na kombe, aliweza pia kuwakabidhi Timu ya TMT na mchezaji bora wa mashindano hayo 'MVP' Rwahabura Munyagi kutoka Mchenga.

Mratibu wa Mashindano hayo, Basilisa Biseko ameweza kuipongeza timu ya Mchenga kwa ushindi huo walioupata wakiwa ndio mabingwa wa kwanza wa Sprite BBall Kings na kuwataka wawe mabalozi wazuri wa mpira wa kikapu mtaani ili kuweza kuhamasisha watoto na vijana kuupenda mchezo huo na kurejesha thamani ya Mpira wa Kikapu.

Amesema Mwitikio mkubwa wa watu umeonekana katika mashindano hayo hasa katika michezo iliyokuwa inachezwa kwenye Viwanja vya Don Bosco na anaamini mwakani yatakuwa na hamasa zaidi tofauti na mwaka huu.

Mashindano hayo yalianza rasmi mwezi Mei mwaka huu kwa kuanza kufanya usaili kwa timu 54 katika Wilaya za Mkoa wa Dar es salaam zikianza kwa mtoano kwenye Viwanja mbalimbali na kuhitimishwa wikiendi hii ya Septemba 02.
 Mchezaji bora 'MVP' wa michuano ya Sprite BBall Kings kwa mwaka 2017. Rwahabura Munyagi akiwa ameshikilia kikombe chake sambamba na kupata kiasi cha shilingi Milioni 2.

RATIBA MPYA LIGI KUU YA VODACOM

$
0
0
Kikosi kazi, kilichopewa kazi maalumu ya kupitia upya Ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), kimemaliza majukumu yake na sasa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawatangaza ratiba mpya.

Kwa mujibu wa ratiba mpya, baada ya michezo ya Agosti 26 na 27, Ligi Kuu ya Vodacom kwa sasa itaendelea Septemba 9 na 10 kama ambavyo inajionyesha kwenye kiambatanisho.

MASHINDANO YA CBA KOMBE LA MWENYEKITI YAFANA

$
0
0
Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa benki ya CBA, Salomon Kawiche (kulia ) akisisitiza jambo  kwa  baadhi ya wafanyakazi wenzake wakati wa michuano  ya Mashindano ya Kombe la CBA Golf Mwenyekiti  yaliyothaminiwa na benki hiyo ,yaliyofanyika kwenye viwanja vya Lugalo jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa benki ya CBA,Dkt. Gift Shoko (katikati)akiongea na wa chezaji wenzake wa Golf  Dkt. Edmond Mndolwa (Kushoto) na Joseph Marwa (kulia)wakati wa michuano  ya Mashindano ya CBA Golf ya Kombe la Mwenyekiti  yaliyodhaminiwa na benki hiyo,yaliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Lugalo jijini Dar es Salaam.

 Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa benki ya CBA ,Dkt.Gift Shoko(wapilia kushoto)  pamoja na baadhi ya viongozi wa Golf  klabu ya Lugalo  wakimshuhudia mwanamuziki mkongwe wa bendi ya Mark band, Rashidi Pembe akionyesha umahiri wake kwenye hafla ya kuwapongeza washiriki wa  mashindano ya CBA   Kombe la Mwenyekiti,yaliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya golf vya Lugalo jijini Dar es Salaam.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

TMA yatabiri msimu wa mvua za vuli mwezi Oktoba hadi Disemba 2017.

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), Dk Agnes Kijazi (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) alipokuwa akitoa utabiri wa msimu wa mvua za vuli unaoanza mwezi Oktoba hadi Disemba 2017. Kushoto ni Mkurugenzi Huduma za Utabiri TMA, Dk. Hamza Kabelwa akishiriki katika mkutano huo.
 Sehemu ya waandishi wa habari wakishiriki katika mkutano huo na TMA ikitoa utabiri wa msimu wa mvua za vuli unaoanza mwezi Oktoba hadi Disemba 2017.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), Dk Agnes Kijazi (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) alipokuwa akitoa utabiri wa msimu wa mvua za vuli unaoanza mwezi Oktoba hadi Disemba 2017. Kushoto ni Mkurugenzi Huduma za Utabiri TMA, Dk. Hamza Kabelwa pamoja na Mkurugenzi Matumizi ya Hali ya Hewa, Dk. Ladslaus Chang’a (kulia) wakishiriki katika mkutano huo.

MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa utabiri wa msimu wa mvua za vuli unaoanza mwezi Oktoba hadi Disemba 2017. Kwa mujibu wa taarifa ya utabiri iliyotolewa leo kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk. Agnes Kijazi ambapo mvua za Vuli zinatarajiwa kuanza Septemba, 2017 katika maeneo mengi ya Ziwa Viktoria na mwezi Oktoba, katika ukanda wa pwani, na baadaye mwezi Novemba katika maeneo ya nyanda za juu kaskazini mashariki. 

Alisema ongezeko la mvua linatarajiwa katika miezi ya Novemba na Disemba, 2017 na hali kadhalika kutakuwa na vipindi virefu vya ukavu kujitokeza zaidi katika mwezi wa Oktoba, 2017.

Hata hivyo alisema mvua zinatarajiwa kuwa za wastani katika maeneo mengi ya mikoa ya Kagera, Mara, Mwanza, Geita, Simiyu, Shinyanga, Dar es Salaam, Tanga, Pwani, Kilimanjaro, Arusha na Manyara, kaskazini mwa mkoa wa Morogoro pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba. 

Dk. Agnes Kijazi alibainisha kuwa mvua za chini ya wastani na vipindi virefu vya ukavu vinatarajiwa kujitokeza hususan katika maeneo ya mikoa ya Kagera, Kilimanjaro, Dar es Salaam, Pwani, Tanga, kaskazini mwa mkoa wa Morogoro pamoja na maeneo ya visiwa vya Unguja na Pemba.

"Pamoja na matarajio hayo ya mvua za wastani katika maeneo mengi ya nchi, uwezekano wa matukio ya vipindi vya mvua kubwa unatarajiwa hususan katika mwezi wa Disemba, 2017. Mtawanyiko hafifu wa mvua na vipindi virefu vya ukavu vinatarajiwa kujitokeza katika baadhi ya maeneo katika kipindi cha msimu wa mvua wa Oktoba hadi Disemba, 2017 hususan katika maeneo ya mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Pwani, Kilimanjaro, Arusha na Manyara, kaskazini mwa mkoa wa  Morogoro pamoja na visiwa vya Unguja and Pemba," alisema Mkurugenzi Mkuu.

Pamoja na hayo, Kijazi aliwashauri wakulima katika maeneo hayo kuandaa mashamba yao mapema na kupanda mazao yanayokomaa katika muda mfupi, huku akizitaka mamlaka husika, kama vile wadau wa Afya, menejimenti za maafa, Mamlaka za miji na wadau wengine kuchukua hatua stahiki katika kupunguza athari mbaya zinazoweza kutokea katika msimu wa mvua za Vuli 2017.

Aidha alisema kwa ujumala maeneo mengi yaliyopo kaskazini mwa nchi yanatarajiwa kupata mvua za wastani na uwezekano wa vipindi vifupi vya mvua kubwa hususan katika mwezi wa Desemba 2017.

Msimu wa mvua wa Oktoba hadi Disemba (vuli) ni mahususi kwa maeneo yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka (Ukanda wa Ziwa Viktoria, nyanda za juu kaskazini mashariki, Pwani ya kaskazini na maeneo ya kaskazini mwa mkoa wa Kigoma). Na TMA inatarajia kutoa utabiri wa mvua katika maeneo mengine ya nchi yaliyosalia mwezi wa Oktoba 2017.

SPIKA NDUGAI AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA UONGOZI LEO MJINI DODOMA

$
0
0
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati)akiongoza kikao cha kamati ya uongozi kilichofanyika leo katika ukumbi wa Spika Mjini Dodoma, ikiwa ni Maandalizi kabla ya kuanza Mkutano wa 8 wa Bunge la 11 unaoendelea kesho tarehe 5 Septemba, 2017 Mjini Dodoma.
 Naibu Spika wa Bunge, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson akizungumza jambo wakati wa kikao cha kamati ya uongozi kilichofanyika leo katika ukumbi wa Spika Mjini Dodoma, ikiwa ni Maandalizi kabla ya kuanza Mkutano wa 8 wa Bunge la 11 unaoendelea kesho tarehe 5 Septemba, 2017 Mjini Dodoma. kushoto ni Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas kashililah.
Wajumbe wa kamati ya uongozi wakiwa katika kikao cha pamoja kilichoongozwa  na Spika wa Bunge katika ukumbi wa Spika Mjini Dodoma, ikiwa ni Maandalizi kabla ya kuanza Mkutano wa 8 wa Bunge la 11 unaoendelea kesho tarehe 5 Septemba, 2017 Mjini Dodoma.  kulia ni Mhe. Andrew Chenge, Mhe. Stanslaus Nyongo (katikati) na Mhe. Christine Ishengoma (kushoto).
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)


BASATA yatoa cheti cha utambuzi kwa Tasnia ya Injili nchini

$
0
0
  Katibu Mtendaji BASATA, Godfrey Mngereza  akimkabidhi  cheti cha kutambua umuhimu wa wasanii wa sanaa ya tasnia ya Injili kwa Rais wa TAGOANE , Godwine  Maimu Nnyaka leo jkatika ofisi za BASATA jijini Dar.

Na Agness Francis , Globu ya Jamii.
Mtandao wa wasanii wote  wa tasnia ya injili  na maadili ya Utaifa, Tanzania Gospel  Artists Nertwork (TAGOANE) wamekabidhiwa  cheti kilicho sajiriwa  kisheria  kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kupitia chombo chenye dhamana BASATA  na kupewa namba ya usajiri  BST/00020 kwa mujibu wa sheria Na.23 ya mwaka 1984.

Zoezi hilo limeongozwa na  Katibu Mtendaji BASATA, Godfrey Mngereza  ambaye ndiye amekabidhi  cheti hicho leo  katika ofisi zake zilizoko BASATA  Ilala Sharif Shamba  Jijijni Dar es Salaam.

Katibu Mtendaji BASATA, Godfrey Mngereza amesema kuwa maadili mema  huleta amani kwa wananchi na amewapongeza  wasanii hao kwa hatua waaliofikia  hadi sasa kwa kutembelea mikoa tofauti tofauti nchini  kwa lengo la kuwaunganisha na fursa mbalimbali ulimwenguni  katika kukuza huduma na kukua kiuchumi .

 Hata hivyo Rais wa TAGOANE , Godwine  Maimu Nnyaka ametanabaisha kuwa watashirikiana na Seriakali  katika kukuza pato la taifa kwa kudhibiti wauzaji haramu, wanyonyaji  na matapeli wa kazi za wasanii  kwa kuchukuliwa hatua za kisheria  kwa dhumuni la kuongezea kipato Taifa na kwa wasanii pia.

Nae Katibu mkuu TAGOANE,  Mchungaji Lucy Wilson ametoa wito kwa wakidada na wakinakaka wajitokeze kwa wingi  kujiunga na  mtandao huo  wa wasanii wote wa tasnia ya injili na maadili ya utaifa na waichukulie sanaa ya injili kama kazi zingine.
Rais wa TAGOANE , Godwine  Maimu Nnyaka akizungumza na waandishi wa habari  kuhusu kuwaunganisha wasanii wote wa Tasnia ya Injili ili kuwa na sauti moja na lugha moja ili kufikia malengo yao kiroho na kimwili leo walipokuwa wakikabidhiwa cheti na BASATA cha kutambua umuhimu wa wasanii wa sanaa ya tasnia ya Injili.
 Katibu Mtendaji BASATA, Godfrey Mngereza akiwapongeza Viongozi wa wasanii wote wa Tasnia ya Injili kwa hatua waliofikia kwa kutembelea baadhi ya mikoa mbalimbali hapa nchini  kwa lengo la kuwaunganisha na fursa mbalimbali ulimwenguni  katika kukuza huduma na kukua kiuchumi 
Baadhi ya viongozi wa wasanii wote wa Tasnia ya Injili pamoja na wasaii wakiwa kwenye picha ya pamoja.

WAFANYAKAZI WA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) WAAGANA NA MADAKTARI BINGWA WA MOYO KUTOKA NCHINI CHINA

$
0
0
 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya  Magonjwa ya Moyo ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Peter Kisenge akimkabidhi zawadi Daktari Bingwa wa upasuaji wa Moyo kutoka China Sun Long wakati wa hafla fupi ya kuwaaga madaktari hao iliyofanyika hivi karibuni. Serikali ya China kila baada ya miaka miwili inatuma madaktari wake kwa ajili ya kufanya kazi ya Matibabu ya Moyo katika Taasisi hiyo.  
 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Magonjwa ya  Moyo ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Peter Kisenge akimkabidhi zawadi Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo kwa watoto kutoka China Qu Xianfeng wakati wa hafla fupi ya kuwaaga madaktari hao iliyofanyika hivi karibuni. Serikali ya China kila baada ya miaka miwili inatuma madaktari wake kwa ajili ya kufanya kazi ya Matibabu ya Moyo katika Taasisi hiyo.  
 Madaktari bingwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka China wakiwa katika picha ya pamoja na  Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Magonjwa ya  Moyo ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Peter Kisenge mara baada ya kuwakabidhi  zawadi wakati wa hafla fupi ya kuwaaga iliyofanyika hivi karibuni. Serikali ya China kila baada ya miaka miwili inatuma madaktari wake kwa ajili ya kufanya kazi ya Matibabu ya Moyo katika Taasisi hiyo.  
 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Magonjwa ya  Moyo ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Peter Kisenge akimkabidhi zawadi Daktari Bingwa wa chumba cha wagonjwa walioko katika uangalizi maalum (ICU) kutoka China Xie Weifeng  wakati wa hafla fupi ya kuwaaga madaktari hao iliyofanyika hivi karibuni. Serikali ya China kila baada ya miaka miwili inatuma madaktari wake kwa ajili ya kufanya kazi ya Matibabu ya Moyo katika Taasisi hiyo.  
Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimsikiliza Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo kwa watoto kutoka China Qu Xianfeng (hayupo pichani) wakati akizungumza katika hafla fupi ya kuwaaga madaktari hao iliyofanyika hivi karibuni. Serikali ya China kila baada ya miaka miwili inatuma madaktari wake kwa ajili ya kufanya kazi ya Matibabu ya Moyo katika Taasisi hiyo.  Picha na JKCI

SIMBA,YANGA SASA KWENDA KUKIPIGA UWANJA WA AZAM COMPLEX

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

BAADA ya Malalamiko ya muda mrefu kwa timu ya Azam kutaka kutumia Uwanja wao wa Azam Complex  kwa mechi dhidi ya Yanga na Simba hatimaye Bodi ya Ligi ya Shiriukisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) limetoa ratiba mpya leo.

Katika ratiba hiyo mpya, Bodi ya Ligi imeweka wazi mechi ya Septemba 9 baina ya Azam dhidi ya Simba itachezwa katika dimba la Uwanja wa Azam Complex Chamazi huku Desemba 29 wakiwakaribisha pia mabingwa watetezi wa ligi kuu Vodacom Yanga michezo hiyo yote ikipigwa saa 1 usiku .

Hatua hii inakuja sasa hivi baada ya mara kadhaa Azam kupeleka mapendekezo ya kutaka watumie uwanja wao kwa mechi zote ikiwemo Yanga na Simba ingawa walikuwa wanakataliwa kutokana na idadi kubwa ya mashabiki wa timu hizo mbili.

Ratiba hiyo iliyotolewa leo ikiwa ni ya marekebisho baada ya ile ya kwanza TFF kuikataa na kuuunda kikosi kazi kwa ajili ya upangaji wa ratiba npya itakayokuwa haina mabadiliko ya ubadilishwaji kila wakati sambamba na kwenda na kalenda ya michezo ya kimataifa ya FIFA.

Maoni ya baadhi ya wadau wa michezo wameonekana kufurahia ratiba hiyo ila wanajua katika kuutumia uwanja huo changamoto mbalimbali zinaweza kujitokeza ila kwa sasa hawawezi kuziona ila mpaka pale kitu kitakapofanyika.

WAUZA NYAMA WATENGA FEDHA KWA AJILI YA KUSAIDIA KULIPIA KAYA MASKINI BIMA YA AFYA

$
0
0
Na Woinde Shizza,Arusha

Umoja wa wauza nyama jijini Arusha (wanjamuco) umetenga shilingi laki tano kwa ajili ya kulipia bima ya afya katika kaya mbili kwa kila kata zinazoishi katika mazingira magumu ili kuwawezesha kupata matibabu bure katika zahanai na hospitali zote za jijini humo. 

Mwenyekiti wa umoja huo Alex Lasiki, amesema hayo leo jijini Arusha wakati wa maadhimisho ya mwaka mmoja wa umoja huo.

amesema katika kusherehekea mwaka mmoja wa umoja wao, wanachama wamekubaliana kuwa watenge kiasi hicho kutoka kwenye mapato yao waliyoyapata kwa mwaka mzima ili wawezeshe familia mbili zenye watu 12 zinazoishi katika mazingira magumu kupata bima ya afya ijulikanayo kama lita inoyosimamiwa na jiji la Arusha .
Lasiki ameongeza, kupitia bima hiyo familia hizo zitapata huduma za matibabu bure, kwenye zahanati au hospitali yoyote ambapo fedha hizo ni sehemu ya kurudisha faida wanayoipata katika jamii wanayoiudumia kupitia biashara yao ya kuuza nyama.

Pamoja na mchangohuo, Lasiki amesema, moja wa huo pia unakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo ya uanzishwaji wa mabucha feki haswa eneo la Samunge yasiyokuwa na viwango yanayouza nyama ambazo hazina viwango hivyo kuhatarisha afya za walaji.

Mbali na hilo, Wanjamuco wanaiomba serikali iwajangee kiwanda cha kuchakata ngozi kwani kwa sasa wanakabiliwa na changamoto kubwa ya sehemu màalum ya kuuzia ngozi kutokana na serikali kupiga marufuku usafirishwaji wa ngozi hizo nje ya nchi.

Naye Diwan wa Kata ya Olerian, Zakaria Absalum, akizungumza katika maadhimisho hayo amesema, kero kubwa ambazo zinawakabili wafanyabiashara wa nyama jijini hapo ni pamoja na usafirishwaji wa ng'ombe kwenda nchi jirani ya Kenya ambapo, wanaosafirsha hawalipi kodi na wanakifika mpakani mtu mmoja mwenye leseni yeye ndio analazimika kuingiza mifugo yote kwenda kufanya biashara kwenye ardhi ya kenya bila kuilipia ushuru na hivyo kuisababishia serikali hasara.

Absalum ambaye pia ni mfanyabiashara wa nyama ameongza kuwa, kutokana na kero hiyo ni vema serikali ikajenga mnada maalum eneo la Namanga ili ilete ushindani kwa wafanyabiashra hao kuziba mianya ya wale wanaoingiza mifugo bila kuwa na leseni za biashara.

NEEMA YA UPIMAJI AFYA BURE KUTOLEWA KWA WANA DAR ES SALAAM

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda anawatangazia Wananchi wote wa Mkoa huo kujitokeza kwa wingi kwenye Kampeni ya Upimaji wa Afya Bure kuanzia siku ya Jumatano ya Septembe 06 -10 kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja.

Zoezi hilo litaendeshwa na Madaktari bingwa na Wauguzi zaidi ya 200 kutoka Hospital za Umma, Jeshi na za Watu Binafsi zilizomuunga mkono RC Makonda.

Makonda amesema kuwa hatopenda kuona Mwananchi anapoteza maisha kwa kukosa huduma ya Afya ndio maana ameamua kuendesha zoezi la upimaji wa Afya Bure ili Wananchi wapate fursa ya kujua Afya zao na kuwa na utaratibu wa kupima Afya zao mara kwa mara.

Aidha amezipongeza Hospital na zilizomuumga mkono ikiwemo Muhimbili, Ocean Road, Amana, Temeke, Mwananyamala, Muhimbili, TMJ, Sanitas, Agha Khan, Regency, Kairuki, TANCDA, IMMI Life, APHTA, CCP Medicine, MDA, NHIF, Wandile wa kaya, P Consult, Besta Diagnestics, Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete, Jamii Bora na Damu salama.

Makonda amesema watakaopimwa na kubainika kuwa na matatizo ya kiafya watapelekwa Hospital na kupatiwa matibabu Bure.

Hata hivyo amesema kuwa kutakuwepo na vifaa tiba vya kisasa, Magari ya kubeba Wagonjwa, Vyoo, Sehemu za watoa huduma na Sehemu za kupumzika wakati wa kusubiri huduma.

WANANCHI WA MKOA WA KASKAZINI UNGUJA WAHIMIZWA KUJIUNGA NA JUMUIYA YAO.

$
0
0
Na Miza Kona, MAELEZO .

MAKAMU wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi, ameitaka Jumuiya ya Maendeleo ya Mkoa wa Kaskazini Unguja kuzidisha mshikamano  ili kuweza kubadilika kielimu na kuleta maendeleo mazuri mkoani humo.

Balozi Seif ameyasema hayo katika ukumbi wa  zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni mjini Zanzibar katika mkutano wa Jumuiya hiyo.
Alisema vijana wengi wa mkoa huo wanakosa kuingia katika ushindani wa soko la ajira kutokana na kukosa sifa zinazohitajika.

Balozi Seif alisema jumuiya inaweza kuleta mafanikio makubwa  kwa kushirikana  pamoja na kuzidisha mshikamano katika dhamira ya kuibadilisha jamii ya mkoa huo kielimu.Alifahamisha kuwa elimu ndio silaha pekee inayoweza kuwakomboa vijana na kuwawezesha kukubalika katika ajira mbalimbali na hivyo kuondokana na umasikini.

“Ni wakati sasa wa kubadilika kwa kuwekeza katika elimu ya watoto wetu ili kuwainua vijana na kuwawezesha kuhimili ushindani kwa kuwa na sifa zitakazoweza kuajiriwa au kujiajiri,” alifahamisha Balozi Seif.
Alieleza vijana wengi wa mkoa huo hawana mwamko wa kusoma, jambo linachangia mkoa wa Kaskazini kuwa nyuma kielimu na kimaendeleo ikilinganishwa na mikoa mingine nchini.

Amehimiza kuwepo ushirikiano wa pamoja baina ya viongozi na wana jumuiya katika kuishajiisha jamii ili iweze kubadilika kiuchumi na kuacha kuingiza itikadi za siasa katika suala la kuleta maendeleo.
Balozi Seif alisema jumuiya ina nia ya kuimarisha umoja na kuleta maendeleo katika mkoa huo.

Aidha Makamu wa Pili  wa Rais amewasisitiza viongozi wa majimbo na serikali katika mkoa huo kudumisha ushirikiano na kuwasaidia vijana wasio na uwezo wa kujikimu kwa kuwapa msukumo wa kimaendeleo pamoja na kuishajiisha jamii kujiunga jumuiya hiyo.

Jumuiya Maendeleo ya Mkoa wa Kaskazini Unguja (NUDO), imeasisiwa mwezi Aprili 2016, na sasa ina zaidi ya wanachama zaidi ya 1000.
Lengo la kuanzishwa kwake ni kuendeleza, kuwezesha na kuijengea uwezo jamii ya mkoa huo katika kuinua ustawi wake kiuchumi, kijamii na mazingira.
Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi akifungua mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo ya Mkoa Kaskazini Unguja katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani Kikwajuni.
 Mjumbe wa Kamati ya Uongozi wa Jumuiya ya Maendeleo ya Mkoa Kaskazini Unguja Ayoub Mohammed Mahmoud akieleza mafanikio ya Jumuiya tokea ilipoasisiwa mwaka jana katika mkutano uliofanyika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani Kikwajuni.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Uchumi wa Jumuiya ya Maendeleo ya Mkoa Kaskazini Unguja Ali Juma Ali akiwaeleza wananchama wa Jumuiya hiyo mikakati na mipango ya kuiendeleza ili kufikia malengo yake katika mkutano uliofanyika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani Kikwajuni.
aadhi ya wajumbe wa mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo ya Mkoa Kaskazini Unguja wakifuatilia mkutano huo uliofanyika Baraza l a Wawakilishi la zamani Kikwajuni Mjini Zanzibar.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Mkoa Kaskazini Unguja Ali Juma Ali akiagana na Makamu wa pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi baada ya mkutano wa Jumuiya hiyo uliofanyika Ukumbi wa Baraza la wawakilishi la zamani Kikwajuni.Picha na Makame Mshenga.

MKUTANO WA NANE WA BUNGE KUANZA KESHO MJINI DODOMA


WAZIRI UMMY MWALIMU AZINDUA UGAWAJI WA VITAMBULISHO VYA TIBA KWA WAZEE MANISPAA YA UBUNGO

$
0
0

Na Mathias Canal, Dar es salaam

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy A. Mwalimu leo Septemba 4, 2017 amezindua Ugawaji wa vitambulisho vya awali 7296 vya matibabu Bure kwa Wazee katika Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Jijini Dar es salaam.

Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika katika Viwanja vya TP Sinza E Waziri Ummy alipongeza uongozi wa Wilaya ya Ubungo kwa kutambua umuhimu wa kutekeleza kwa vitendo maelekezo ya serikali ya kuwatambua Wazee katika Halmashauri na kuwapatia vitambulisho vitakavyo wawezesha kupata Huduma za matibabu bila vikwao.

Alisema kuwa Wazee ni asilimia 5.6 ya wananchi wote wa Tanzania idadi ambayo kwa kiasi kikubwa inaleta msukumo wa nchi kuweka mifumo madhubuti ya kuhudumia Wazee ikiwemo kurahisisha upatikanaji wa Huduma katika matibabu.

Alisema kuwa Jambo hilo ni kuzingatia ukweli kwamba Wazee wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazosababishwa na umri mkubwa na mtazamo wa Jamii ambao umekuwa ukichangia ukiukwaji wa haki na maslahi ya Wazee katika ngazi mbalimbali.

Alisema Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo imeingia kwenye rekodi kwa kuwatambua Wazee wasio na uwezo kwani watapatiwa vitambulisho vitakavyo wawezesha kupata Huduma za matibabu Bure.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy A. Mwalimu akizungumza wakati wa uzindua wa Ugawaji wa vitambulisho vya matibabu Bure kwa Wazee katika Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Jijini Dar es salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy A. Mwalimu (Wa Tatu Kushoto) akionyesha vitambulisho vya Wazee akiwa na viongozi wengine wa Chama na serikali Wilaya ya Ubungo wakati wa Ugawaji wa vitambulisho vya matibabu Bure kwa Wazee katika Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Jijini Dar es salaam.
 Zoezi la Uzinduzi wa Ugawaji wa vitambulisho vya awali 7296 vya matibabu Bure kwa Wazee katika Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Jijini Dar es salaam Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kwa ajili ya uzinduzi wa Ugawaji wa vitambulisho vya awali 7296 vya matibabu Bure kwa Wazee katika Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Jijini Dar es salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy A. Mwalimu akimpatia Mzee Ferooz Kafuru kitambulisho Cha matibabu wakati wa uzindua wa Ugawaji wa vitambulisho vya matibabu Bure kwa Wazee katika Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Jijini Dar es salaam.

ZANTEL YATOA ZAWADI YA MBUZI KATIKA KUSHEHEREKEA SIKUKUU YA 'EID AL HADHA',YAWAKUMBUKA YATIMA NA WAZEE

$
0
0

Mwakilishi wa Zantel-Tanga Mansoor Ally, (kulia) akikabidhi mbuzi kwa kituo cha kulea watoto yatima cha Goodwill & Humanity Foundation kilichopo jijini Tanga wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika kituo hicho, siku ya Alhamisi ya wiki iliyopita ikiwa ni moja ya hatua ya kujitolea kwa jamii kwa Kampuni hiyo. Zaidi ya mbuzi 100 walitolewa katika mikoa mbalimbali ya bara na visiwani katika kuadhimisha sikukuu ya Eid Al Adha.
Meneja wa Data na Vifaa vya Intaneti, Hamza Zuheri (kushoto) akikabidhi mbuzi kwa mwakilishi wa kituo cha kulea watoto yatima cha Malaika kilichopo Kinondoni Malongwe jijini Dar, wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika makao makuu ya ofisi za Zantel jijini Dar es salaam, siku ya Alhamisi ya wiki iliyopita ikiwa ni moja ya hatua ya kujitolea kwa jamii kwa Kampuni hiyo. Zaidi ya mbuzi 100 walitolewa katika mikoa mbalimbali ya bara na visiwani katika kuadhimisha sikukuu ya Eid Al Adha.
Afisa wa Zantel Abdallah Saadun (kushoto) akikabidhi mbuzi kwa Afisa rasilimali watu wa kituo cha kulea watoto yatima cha SOS-Zanzibar, Bw. Salum Abdallah Salum (wa pili kushoto) wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika ofisi kuu ya Zantel iliyopo Unguja, siku ya Alhamisi ya wiki iliyopita ikiwa ni moja ya hatua ya kujitolea kwa jamii kwa Kampuni hiyo ambapo zaidi ya mbuzi 100 walitolewa katika mikoa mbalimbali ya bara na visiwani katika kuadhimisha sikukuu ya Eid Al Adha.
Afisa wa Zantel Abdallah Saadun akikabidhi mbuzi kwa walezi na watoto wa kituo cha kulea watoto yatima cha Mazizini-Zanzibar wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika ofisi kuu ya Zantel iliyopo Unguja, siku ya Alhamisi ya wiki iliyopita ikiwa ni moja ya hatua ya kujitolea kwa jamii kwa Kampuni hiyo ambapo zaidi ya mbuzi 100 walitolewa katika mikoa mbalimbali ya bara na visiwani katika kuadhimisha sikukuu ya Eid Al Adha. Anayeshuhudia kushoto ni Meneja Chapa na Mawasiiano wa Zantel, Rukia Mtingwa.

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

WATUMISHI WA WIZARA YA MAMBO YA NJE WAHITIMU MAFUNZO YA JKT

$
0
0
Mgeni Rasmi, Balozi Mlima akikagua gwaride maalum lililoandaliwa kwa heshima yake na kikosi kilichohitimu mafunzo ya JKT ambacho kilijumuisha watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje
Mgeni Rasmi, Balozi Aziz Mlima wakiwa wamesimama pamoja na Mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (kulia) na Kamanda wa Kambi ya Oljoro kwa ajili kuangalia vikosi vikipita mbele yao katika mwendo wa pole na kasi
Kikosi kikipita mbele ya Mgeni Rasmi kwa mwendo wa pole 
Mgeni Rasmi akikabidhi zawadi kwa waliofanya vizuri zaidi. 
Picha ya pamoja kati ya Mgeni Rasmi na wahitimu wa JKT. 

TUVAE MAVAZI YENYE STAHA TUNAPOFUATA HUDUMA MBALIMBALI KATIKA OFISI ZA UMMA

$
0
0
Mmoja kati ya watangazaji wa Kipindi cha “LEO TENA” kinachotangazwa na kituo cha redio cha Clouds FM, Bw. Musa Hussein (aliyesimama) akiwa katika mjadala na Afisa Utumishi Mwandamizi kutoka Idara ya Ukuzaji Maadili, Ofisi ya Rais-Utumishi, Bi. Leila Mavika (kushoto).
Afisa Utumishi Mwandamizi kutoka Idara ya Ukuzaji Maadili, Ofisi ya Rais-Utumishi, Bi. Leila Mavika (kushoto) akishiriki mjadala kuhusu masuala ya maadili, hususan mavazi kwa watumishi wa umma na wateja wanaofuata huduma katika taasisi za umma katika kipindi cha LEO TENA kinachotangazwa na kituo cha redio cha Clouds FM.
Afisa Utumishi Mwandamizi kutoka Idara ya Ukuzaji Maadili, Ofisi ya Rais-Utumishi, Bi. Leila Mavika (kushoto) akifafanua kuhusu muonekano na aina ya mavazi yanayopaswa kuvaliwa na watumishi wa umma na wateja wanaofuata huduma katika taasisi za umma katika kipindi cha LEO TENA kinachotangazwa kituo cha redio cha Clouds FM.
Viewing all 110029 articles
Browse latest View live




Latest Images