Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live

CHANGAMOTO ZA WASANII WA NYIMBO ZA INJILI ZAWEKEWA MIKAKATI YA KUTATULIWA

$
0
0
Na: Genofeva Matemu – WHUSM

Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Harrison Mwakyembe amekutana na wasanii wa nyimbo za Injili leo Jijini Dar es Salaam kusikiliza changamoto zinazoikabili tasnia ya muziki wa nyimbo za injili na kuweka mikakati ya kuzitatua changamoto hizo hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu.

Akizungumza wakati wa mkutano na wanamuziki wa nyimbo za Injili Mhe. Mwakyembe amesema kuwa serikali ina wajibu wa kufuatilia changamoto za tasnia ya muziki ukiwemo muziki wa injili na kuzitatua ili kuweza kukuza kazi za wasanii kwa maslahi ya mtu mmoja mmoja na taifa.

“Muziki ni tasnia ambayo imewabeba vijana wengi hapa nchini, serikali ina wajibu wa kutetea, kulinda na kuhakikisha maslahi ya kazi za sanaa ikiwemo muziki wa injili inaheshimiwa na kulindwa” Amesema Mhe. Mwakyembe

Kwa upande wake Katibu Mtendaji Chama cha Hakimiliki Tanzania (COSOTA) Bibi. Doreen Sinare amewataka Wasanii wa Muziki wa Injili kutoshawishiwa kutoa malipo yoyote katika vyombo vya habari ili nyimbo zao ziweze kuchezwa kwenye vyombo hivyo bali vyombo vya habari ndio vinapaswa viwalipa wasanii wakati wanapotumia nyimbo zoa.

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza na Wasanii wa Nyimbo za Injili (hawapo pichani) wakati wa mkutano na wasanii hao kujadili changamoto zinazowakabili na namna ya kutatua changamoto hizo leo Jijini Dar es Salaam. 
Katibu Mtendaji Chama cha Hakimiliki Tanzania (COSOTA) Bibi. Doreen Sinare akifafanua jambo wakati wa mkutano na wasanii wa nyimbo za Injili kujadili changamoto zinazowakabili na namna ya kutatua changamoto hizo leo Jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Chama cha Muziki wa Injili Tanzania (CHAMWITA) Bw. Addo Novemba akiwasilisha changamoto zinazokabili muziki wa injili hapa nchini wakati wa mkutano na wasanii wa nyimbo za Injili kujadili changamoto zinazowakabili na namna ya kutatua changamoto hizo leo Jijini Dar es Salaam. 
Mwanamuziki wa Nyimbo za Injili Bi. Christina Shusho akichangia hoja wakati wa mkutano na wasanii wa nyimbo za Injili kujadili changamoto zinazowakabili na namna ya kutatua changamoto hizo leo Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (waliokaa katikati) katika picha ya pamoja na viongozi kutoka serikalini pamoja na viongozi wa chama cha Muziki wa Injili Tanzania baada ya mkutano na wasanii hao kujadili changamoto zinazowakabili na namna ya kutatua changamoto hizo leo Jijini Dar es Salaam. Picha na: Genofeva Matemu – WHUSM .


KATIBU MTENDAJI BODI YA FILAMU AFUNGA SEMINA YA MAMENEJA WA USAMBAZAJI WA KAZI ZA FILAMU KUTOKA MIKOA 25 YA TANZANIA

$
0
0

Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo (katikati) akizungumza na mameneja wa usambazaji wa kazi za filamu (hawapo pichani) kabla ya kufunga semina elekezi kwa mameneja hao leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Barazani Entertainment Bw. John Kalage na kulia ni Mkuu wa Kitengo cha uenezi Bw. Singo Mtambalike

Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Barazani Entertainment Bw. John Kalage (Kulia) alipotembelea ofisi hizo leo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufunga semina ya mameneja wa usambazaji wa kazi za filamu kutoka mikoa 25 ya Tanzania.
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo (kushoto) akiteta jambo na viongozi wa Barazani Entertainment kabla ya kufunga semina ya mameneja wa usambazaji wa kazi za filamu kutoka mikoa 25 ya Tanzania leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni mkuu wa Mawasiliano kutoka Barazani Entertainment Bw. Jacob Steven na katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Barazani Entertainment Bw. John Kalage
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo (katikati) katika picha ya pamoja na viongozi wa Barazani Entertainment na mameneja wa usambazaji kazi za filamu baada ya kufunga semina elekezi kwa mameneja hao leo Jijini Dar es Salaam.

Picha na: Genofeva Matemu – WHUSM

WAZIRI MKUU AWAONYA WATU WANAOCHUKUA DAWA KATIKA HOSPITALI ZA SERIKALI NA KUZIPELEKA KATIKA MADUKA YAO.

$
0
0

Na Tiganya Vincent-RS-Tabora

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amewaonya wamiliki wa maduka ya madawa ya binadamu na watumishi wa sekta ya afya wanaochukua dawa ambazo zinapaswa kupelekwa katika Hospitali za Serikali ili kuwahudumia wananchi na kuziweka katika maduka yao.

Mhe. Majaliwa alitoa kauli hiyo jana Wilayani Sikonge katika mkutano wa hadhara na wananchi katika Kiwanja cha TASAF.

Alisema kuwa vitendo hivyo ndivyo vimekuwa vikisababisha upungufu wa dawa katika Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali mbalimbali za Serikali na kufanya baadhi ya wananchi kuendelea kuteseka na maradhi kwa sababu ya kushindwa gharama za ununuzi wa dawa katika maduka ya watu binafsi.

Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa aliwaonya watumishi wa afya na wamiliki hao wenye tabia hizo kuacha mara moja endapo watabainika kuendesha vitendo hivyo watachukuliwa hatua kali.

Alisema kuwa Serikali inatumia fedha nyingi kwa ajili kununua dawa ili zinasaidia kutoa huduma ya matibabu kwa wananchi wake lakini kuna baadhi ya watumishi wa afya wasio waadirifu ambapo wamekuwa wakitorosha dawa na kuwauzia wamiliki wa maduka ya dawa na ksuababisha upungufu katika vituo vya Serikali.

Waziri Mkuu kuwa Serikali haiwezi kuwavilimia watumishi wa afya wasio waaminifu wanaochukua dawa na kuzipeleka katika maduka binafsi huku wakisababisha upungufu katika baadhi ya hospitali za umma.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwahutubia Wananchi wa Wilaya ya Sikonge Mjini leo Agosti.10.2017 katika viwanja vya Tasaf Waziri Mkuu yupo Mkoani Tabora kwa ziara ya Kikazi .



NAIBU MEYA WA MANISPAA YA DODOMA JUMANNE NGEDE ATETEA NAFASI YAKE

$
0
0

Na Ramadhani Juma-Ofisi ya Mkurugenzi

NAIBU Meya wa Manispaa ya Dodoma aliyemaliza muda wake Jumanne Ngede amefanikiwa kutetea nafasi yake katika uchaguzi uliofanyika jana katika ukumbi wa Manispaa ya Dodoma ambapo wajumbe 56 walishiriki uchaguzi huo.

Katika uchaguzi huo Ngede ambaye ni Diwani wa Kata ya Chamwino kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) alishinda nafasi hiyo kwa kupata kura 47 dhidi ya mpinzani wake kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Samwel Mziba ambaye ni Diwani wa Kata ya Hazina aliyepata kura 9.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma ambaye ni Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Dodoma Mjini Godwin Kunambi alimtangaza rasmi Ngede kuwa Naibu Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma.

Baada ya kufanikiwa kutetea nafasi yake, Ngede aliwashukuru wajumbe kwa kumchagua kwa kura nyingi jambo linaonesha kuwa wana imani kubwa na utendaji wake na kwamba ataendelea kufanya kazi kwa uadilifu mkubwa na kwa kushirikiana na Madiwani wote.

Kwa upande wake, mgombea aliyeshindwa Samweli Mziba aliwashukuru wajumbe na kumpongeza mshindi huku akidai uchaguzi umepita na sasa ni kuchapa kazi tu.
 Mgombea aliyeshinda nafasi ya Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jumannne Ngede (CCM) akitoa neno kwa wajumbe mara baada ya kushinda nafasi hiyo kufuatia uchaguzi uliofanyika jana katika ukumbi wa Manispaa hiyo.
   Mgombea aliyeshindwa nafasi ya Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Samwel Mziba  (CHADEMA) akitoa neno kwa wajumbe mara baada ya matokeo kutangazwa kufuatia uchaguzi uliofanyika jana katika ukumbi wa Manispaa hiyo.

DAWASCO WATOA ELIMU KWA WANANCHI JUU YA MFUMO MPYA WA UTOAJI NA UPATIKANAJI WA TAARIFA MUHIMU.

$
0
0
MENEJA Uhusiano wa DAWASCO, Bi. Everlasting Lyaro, amewataka wananchi wa Dar es Salaam na Pwani kupakua mfumo huu kwani ni rahisi kuutumia na hauna gharama zozote. Anasema ni mfumo ambao utamrahisishia mteja kupata taarifa muhimu zinazohusu huduma ya maji zikiwamo ankara ya mwezi, taarifa za lini mteja alifungiwa huduma ya maji, muda ambao alifanya malipo, lini mita yake ya maji ilisomwa na taarifa nyingine nyingi.
“Nawasihi wateja wetu na wananchi wote kupakua mfumo huu mpya katika simu zenu za mkononi ili kuweza kufurahia huduma zetu, hakuna gharama zozote ambazo utatozwa. Kupitia mfumo huu utaweza kupata taarifa zote muhimu za huduma ya majisafi zikiwemo taarifa za mivujo ya maji na ankara za maji za kila mwezi,”amefafanua Bi. Lyaro.
Amesema kwa sasa Wateja hawana haja ya kutumia muda mrefu katika ufuatiliaji wa kuunganishwa huduma ya maji, bali kilichorahisishwa ni mteja kuweka taarifa zake sahihi kwenye mfumo huo na DAWASCO.
Meneja Uhusiano wa DAWASCO, Bi Everlasting Lyaro akitoa elimu juu ya matumizi ya mfumo wa DAWASCO kwa kwa njia ya simu kwa watumiaji wa vyombo vya Moto hususani Bajaj na Pikipiki katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam. Mfumo huo umezinduliwa rasmi ili kutoa nafasi kwa wananchi kupata na kutoa taarifa sahihi za DAWASCO.
Mmoja ya waendesha bodaboda akimuuliza swali Meneja Uhusiano wa DAWASCO, Bi. Everlasting Lyaro juu ya matumizi ya mfumo mpya wa DAWSCO katika utoaji na upatikanaji wa taarifa.
Mwendesha bajaji akihojiwana ITV juu ya matumizi ya mfumo mpya wa DAWASCO katika utoaji na upatikanaji wa taarifa.

Mshindi wa Milioni 20 za Biko Kimara Suka akabidhiwa fedha zake

$
0
0
MSHINDI wa Shilingi Milioni 20 za Biko kutoka kwenye Bahati Nasibu ya Biko ‘Ijue Nguvu ya Buku’, Anthony Chitanda, amekabidhiwa fedha zake mapema jana katika benki ya NMB, Tawi la Bank House, Posta, jijini Dar es Salam, sambamba na kupewa ushauri wa kifedha.

Chitanda aliibuka kidedea katika droo ya 30 ya Biko iliyochezeshwa juzi Jumatano na kuvuna Sh Milioni 20 zinazotolewa na waendeshaji hao wa Biko, mchezo wa kubahatisha unaoendelea kutingisha katika wilaya na mikoa mbalimbali ya Tanzania.


Akizungumza katika Makabidhiano hayo, Mratibu wa Matukio na Mawasiliano wa Biko, Hassan Melles, alisema kwa kila anayecheza bahati nasibu yao, lazima ajiandae kulala masikini na kuamka tajiri.

Alisema ushindi wa Biko ni rahisi kwa wale wanaocheza kwa kutumia mitandao ya simu ya M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money ambapo namba ya Kampuni ni 505050 na kumbukumbu ni 2456, huku kianzio cha kuchezea Biko kikianzia Sh 1,000 na kuendelea.

“Mbali na kushinda Sh Milioni 20 kama alivyoshinda Chitanda na hatimae kumkabidhi fedha zake siku moja baada ya kushinda, pia Watanzania wanaweza kushinda zawadi za papo kwa hapo kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni moja, huku wanaocheza mara nyingi zaidi kwa kufanya miamala kwenye simu zao wakiwa na nafasi kubwa zaidi ya kushinda zawadi za papo kwa hapo pamoja na kuingia kwenye droo kubwa ya Jumatano na Jumapili kwa ajili ya kuwania donge nono la Sh Milioni 20,” Alisema.
Mratibu wa Matukio na Mawasiliano wa Bahati Nasibu ya Biko, Hassan Melles kulia amkabidhi mshindi wao wa droo ya 30 Anthony Chitanda katikati katika benki ya NMB, Tawi la Bank House, Posta, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa wa NMB. Makabidhiano hayo yalifanyika jana mchana.
Mshindi wa droo ya 30 Biko Ijue Nguvu ya Buku, Anthony Chitanda kushoto akiwa na mke wake baada ya kukabidhiwa hundi ya fedha zake Sh Milioni 20 saa chache kabla ya kuelekea benki ya NMB, Posta jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kukabidhiwa fedha zake jana.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

DKT TIZEBA ATEUA WAJUMBE WA BODI ZA WAKURUGENZI WA BODI ZA MAZAO CHINI YA WIZARA YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI

Kaya 6019 katika halmashauri ya wilaya ya Kishapu kunufaika na fedha za TASAF

$
0
0
Sehemu ya walengwa wa kaya maskini wakiwa katika zoezi la kupokea ruzuku kijij cha Mwigumbi.

Na Robert Hokororo.

Kaya  6019 katika halmashauri ya wilaya ya Kishapu, mkoani Shinyanga, zinatarajia kunufaika na fedha sh. milioni 204.6 zinazotolewa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) awamu ya tatu. Hayo yamebainishwa na Mratibu wa TASAF wilayani humo, Sospeter Nyamuhanga ofisini kwake wakati akizungumzia zoezi la uhawilishaji fedha hizo linalotarajiwa kuvifikia jumla ya vijiji 78.

Alisema kuwa zoezi hilo linatarajiwa kuanza kufanyika kuanzia Agosti 7 hadi 11 mwaka huo katika vijiji lengwa kwenye kata zilizo katika mpango wa TASAF III wilayani humo .
Nyamuhanga alifafanua kwa kusema kuwa zoezi la uhawilishaji fedha kwa kaya hizo linaanza kwa lengo la kuziwezesha kaya maskini ili zikwamuke kutoka hali ya umaskini.

Mratibu huyo alisema kuwa katika kipindi cha mwaka 2016/2017 jumla ya wanakaya 54 wameingizwa kwenye mpango huo wa TASAF III wakiwemo watoto waliozaliwa katika kipindi hicho.

“Lengo la mpango wa TASAF ni kuhakikisha walengwa wanatimiza masharti kama ya kuwapeleka watoto shule ili baadaye wapate elimu ambayo itawaondoa katika umaskini na pia kuhakikisha wanawapeleka kwenye huduma za afya kupitia fedha hizi,” alisema. Mratibu huyo aliongeza kwa kubainisha kuwa mpango wa TASAF wilayani Kishapu umeonesha mafanikio yakiwemo baadhi ya kaya kubadilika kimaisha kwa kufuga mifugo kama ng’ombe na mbuzi.

Alisema kuwa baadhi ya walengwa tayari wamebadilisha aina za makazi yao kutoka nyumba za tembe na nyasi na kuanza kujenga nyumba za kisasa za bati hali inayoleta matumaini katika miradi kama hii.
Mratibu huyo amesema mfuko huo unatoa ruzuku za aina mbili, ya msingi inayotolewa kwa kaya zote masikini zilizoandikishwa kwenye mpango na nyingine ni ya utimizaji masharti ambayo hutolewa kwa kaya zenye watoto wanaotakiwa kwenda shule na vituo vya kutolea huduma za afya.

Aidha,  Nyamuhanga aliwataka wanufaika kuwa na matumizi sahihi ya fedha wanazopata ili lengo la TASAF la kuwatoa katika umaskini na kuwafanya wajitegemee litime.

Kishapu ni miongoni mwa halmashauri za wilaya 161 za Tanzania Bara, Unguja na Pemba zinazotekeleza Mpango wa TASAF III ili kuongeza kipato na fursa za kuboresha upatikanaji wa mahitaji muhimu.
Walengwa wa mpango wa kunusuru kaya maskini unaoendeshwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wilayani Kishapu wakiwa katika zoezi la kupokea ruzuku katika kijiji cha Mwigumbi kata ya Mondo.

Lukuvi kugawa hati za ardhi 2,111 Kilombero, Morogoro

$
0
0
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia Programu ya Kuwezesha Umilikishaji Ardhi (Land Tenure Support Programme - LTSP) itazindua rasmi utoaji wa Hati za Hakimiliki ya Kimila katika kijiji cha Nyange, wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro tarehe 15 Agosti, 2017.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi atakuwa mgeni rasmi katika tukio hilo ambapo atagawa hati 2,111 kwa wananchi wa kijiji cha Nyange na kuzindua ofisi na masjala ya ardhi ya kijiji hicho. Ofisi na masjala ya ardhi ya kijiji cha Nyange imejengwa kwa nguvu za wananchi na msaada wa Serikali kupitia mradi wa LTSP.

LTSP ni Programu iliyo chini ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Programu hii ni mahsusi kwa wilaya za Kilombero, Ulanga na Malinyi ambapo takribani vijiji 160 vitanufaika. Hadi sasa, Programu imehakiki na kupima vipande vya ardhi 21,154 katika vijiji 18 vya Wilaya za Kilombero na Ulanga. Kati ya vipande vilivyohakikiwa na kupimwa, jumla ya vipande 9,112 vimeandaliwa Hati za Hakimiliki ya Kimila.

Kazi nyingine zilizotekelezwa na Programu ni pamoja na:
  • Kusimika alama za msingi 54 za mtandao wa kijiodesia katika Wilaya za Kilombero, Ulanga, Malinyi na Mufindi;
  • Kupima mipaka ya vijiji 50 na kutatua migogoro 18 ya mipaka ya vijiji iliyodumu kwa muda mrefu;
  • Kuandaa vyeti vya Ardhi ya Kijiji kwa vijiji 57;
  • Kuandaa mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji kwa vijiji 50; na
  • Kuchangia katika ujenzi na ukarabati wa masjala za ardhi na ofisi za vijiji katika vijiji 61.
Wadau mbalimbali, wakiwemo washirika wa maendeleo wanaofadhili Programu ya LTSP na wananchi watashiriki katika uzinduzi huo.
Programu hii inafadhiliwa na mashirika ya maendeleo ya DFID, DANIDA na SIDA. Wananchi wote wanakaribishwa kushuhudia tukio hili.

SAFARI LAGER YAADHIMISHA MIAKA 40 KWA BURUDANI.

$
0
0

BIA ya Safari Lager inayozalishwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) inasheherekea miaka 40 tangu kuzalishwa hapa nchini mwaka 1977 ikiwa bia ya kwanza ya Kitanzania. Shamrashamra hizo zitaanza rasmi siku ya Jumamosi 12 Agosti katika viwanja vya Leaders Club ambapo wasanii mbalimbali maarufu watatoa burudani ya muziki.

Akiizungumzia Safari Lager Meneja wa bia ya Safari Lager Bi. Edith Bebwa Nasuwa  alisema kuwa hatua ya mafanikio iliyofikiwa na bia ya Safari ni ya kujivunia na hasa kwa sababu bado inaendelea kuwa moja ya kinywaji kinachopendwa zaidi katika soko lenye chapa nyingi za bia.Safari Lager ni bia inayoongoza kwa tuzo za ubora wa kimataifa hivyo inampa mnywaji thamani ya pesa yake.”

“Ili kuzindua kampeni hii ya kusherehekea miaka 40 ya Safari yetu tumeandaa burudani kabambe zitakazoanzia jijini Dar es Salaam na kuelekea mikoani ili kuwashukuru wateja watu wetu kwawa nasi katika safari hii.”

Tutashuhudia safari ya burudani kutoka kwa wanamuziki mbalimbali katika uzinduzi wa sherehe za miaka 40. Safari ya burudanu itaanzishwa na mwimbaji maarufu Hassani Bichuka akiwa na Ali Choki, wakipiga nyimbo zao na msanii wa kizazi kipya Barnaba na Odama band, wanamuziki wa bongo fleva Sir Juma Nature, Dully Sykes, Ray C na wa kizazi kipya  Joh Makini. Kwa kuongeza burudani kuna maDJ maarufu akiwemo DJ John Dilinga, DJ Zero na DJ Fast Eddie.

“Tunajivunia kuwa nchini kwa miaka 40 na bado Safari lager inatazamia kuwepo miaka 40 ndiyo maana tunasema #40naBaado. Tunawaalika wateja wetu wote na wapenzi wa Safari Lager waje kusheherekea nasi jumamosi, kiingilio ni Safari Lager mbili tu. Tunataka wateja wetu wajivunie na wao kwa hatua hii ya mafanikio kwa sababu wao ndio wadau wetu wakubwa,” aliongezea Edith.

Tunawaambia wakazi  wa miji ya Arusha, Moshi, Mbeya, Tunduma, Tukuyu, Makambako, Mbinga, Babati, Singida, Mtwara, Tandahimba, Nachingwea, Babati na Songea kwani baada ya Dar es Salaam safari hii ya burudani inenda kwao, #40NABAADO.

NAIBU SPIKA WA BARAZA LA WAKILISHI ZANZIBAR AKUTANA NA VITAL VOICES GROW MJINI UNGUJA

$
0
0
Kikundi cha VVGrow kiko mjini Zanzibar  kwa lengo la kujumuika na pia kutathmini na kujadili mawazo ambayo yatawasaidia kukua kwa wanakikundi wao binafsi na pia kukuza  biashara zao kwa kujenga ajira na kukuza uchumi.
VV GROW Fellowship ni fursa kwa wanawake ulimwenguni wenye ushindani mkubwa wa mafunzo ya mwaka mmoja wenye lengo la kusaidia wanawake wamiliki wa biashara ndogo ndogo na za kati katika mataifa ya Amerika Kusini na Caribbean, Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, na Afrika kusini mwa Sahara.
Image may contain: 1 person, sitting 
Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi, Mheshimiwa Bi. Mgeni Hassan Juma  Akizungumza na Wanawake wa Kikundi cha Vital Voices Grow Kutoka Nchi za Kusini mwa Bara la Afrika Mjini Unguja.
Kikundi cha Vital Voices Grow (VVGrow) kutoka Afrika Kusini  mwa Jangwa la Sahara (Sub-Saharan Africa) kwa mwaka 2015/2016  kimemtembelea Mheshimiwa Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi, Mheshimiwa Bi. Mgeni Hassan Juma katika ofisi zake mjini Unguja, Zanzibar.
Kikundi hicho kilichokuwa na ujumbe wa watu sita wakiongozwa  na mwenyeji wao Bi.  Shekha Nasser ambaye ni Mkurugenzi wa kampuni ya Shear Illusions na muasisi wa vipodozi vya Manjano walipata fursa ya kumtembelea Naibu Spika kwa lengo la kubadilishana mawazo kuhusu masuala ya kumuwezesha mwanamke kiuchumi.
Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi, Mheshimiwa Bi. Mgeni Hassan Juma Akiwa Katika Picha ya Pamoja na Wanakikundi hao.
Mheshimiwa Bi. Mgeni ni Mwanamke wa kwanza kushika wadhifa wa Unaibu Spika katika historia ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar. 
Katika ziara hiyo, VVGrow pia walipata fursa ya kujifunza mambo mbalimbali yahusuyo wanawake na maendeleo ya kiuchumi kutoka kwa Bi. Mgeni ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Wabunge Zanzibar (UWAWAZA). Pia ilikuwa ni fursa kwao kuonesha heshima yao kwa viongozi wa wanawake ambao wanaboresha ulimwengu na kuhamasisha usawa.

WANAOMILIKI VIWANJA BILA KUVIENDELEZA WILAYANI KIBAHA WAJISALIMISHE, LASIVYO VINAFUTWA - DC MSHAMA

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

MKUU wa wilaya ya Kibaha, Assumpter Mshama ametoa wiki tatu kwa kwa taasisi, makampuni mbalimbali na wananchi waliokumbatia viwanja vyenye hati zaidi ya 1,000 pasipo kuviendeleza kuhakikisha wanafanya hivyo ndani ya muda huo. Amezitaka taasisi na watu hao kwenda kufanya mazungumzo na makubaliano na idara ya ardhi wilayani hapo katika kipindi hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusiana na agizo hilo, Assumpter alisema kati ya viwanja 1,080 viwanja kumi vinamilikiwa na taasisi mbalimbali bila kutimiza malengo husika. Alifafanua kati ya viwanja hivyo 735 vipo Kibaha Vijijini na 345 vipo mji wa Kibaha.

Assumpter alitaja baadhi ya taasisi na makampuni hayo kuwa ni pamoja na CRDB makao makuu, mamlaka ya mapato Tanzania (TRA), Tanesco makao makuu na National Audit (NAOT). Taasisi nyingine ni Njuweni Institute Ltd -Kibaha, The Open university (OUT), SF Group Companies Ltd, Hazina Ndogo na Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa na Apex Housing Development.

Assumpter alisema, wamechoka kuchezewa akili kwa kudanganywa miaka yote huku watu wakitumia ardhi kwa maslahi binafsi huku wilaya ikikosa mapato. Alieleza kwamba, Kibaha imeshakuwa mji na unakua kila kukicha ni lazima uendelezwe. Assumpter alibainisha, wadau na taasisi mbalimbali ziunge mkono juhudi za serikali kujenga viwanda na mahotel ili kuinua maendeleo na uchumi.

"Waje wafanye makubaliano hatuwezi kuwa na mapori ambayo yanatumika hadi na uhalifu, akaekaidi hati yake itafutwa kwa mujibu wa sheria" alisema Assumpter. Alisema wanaacha pori maeneo hali inayosababisha kuwa maficho ya kiuhalifu.

Hata hivyo Assumper alisema NSSF ilikuwa na eneo lenye jumla ya hekta 7.5 sawa na hekari 18  mkoani B,ambalo walilichukua kwa ajili ya kujenga makazi lakini halijaendelezwa tangu mwaka 1997 lilipomilikishwa.

“Taasisi za aina hii siwezi kuzikumbatia hata kidogo ,haki lazima itendeke ,eneo hilo tumelirudisha kwa mwenyewe na tumeinyanganya NSSF
“alisema Assumpter.

Assumpter aliwaomba wawekezaji kwenda kuwekeza na kujenga viwanda wilayani hapo. Katika hatua nyingine ,aliwataka waandishi Wa habari na chama cha waandishi hao Mkoani Pwani kushirikiana nae ili kuiendeleza Kibaha.

INTRODUCING JANB ft FAVOLII (DANII)

MAENDELEO YA MABENKI NCHINI KUJINGA NA MFUMO WA KULIPA KODI KIELEKTRONIKI eRCS

RAIS WA ZANZIBAR DKT SHEIN AKUTANA NA KATIBU MKUU WA JUMUIYA YA MADOLA

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein akiwa katika Mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Patricia Scotland Ikulu mjini Zanzibar leo asubuhi
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi. Patricia Scotland wakiongea na wanahabari baada ya mazungumzo yao Ikulu mjini Zanzibar leo asubuhi

Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri,Mhe. Abdel Fattah Al Sisi anatarajia kufanya ziara ya Kitaifa wiki Ijayo.

$
0
0



Kufuatia mwaliko wa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Abdel Fattah Al Sisi, Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri atafanya Ziara ya Kitaifa nchini Tanzania wiki ijayo. Hii itakuwa ni ziara ya kwanza ya Mheshimiwa Abdel Fattah Al Sisi nchini Tanzania tangu Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli aingie madarakani. 

Lengo la ziara hii ni kuimarisha na kukuza zaidi mahusiano mazuri yaliyopo ya kidiplomasia, kiuchumi na kijamii kati ya nchi hizi mbili, ziara hii pia itatoa fursa kwa viongozi wetu kujadili masuala mbalimbali yanayohusu nchi hizi mbili, ya kikanda na kimataifa.

Mheshimiwa Rais Al Sisi atawasili nchini kupokelewa na mwenyeji wake, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha, Mheshimiwa Rais Al Sisi mchana atakuwa na mazungumzo (tete-a-tete) na mwenyeji wake kabla ya kushiriki mazungumzo rasmi (official talks) na baadae jioni Mheshimiwa Rais Al Sisi atahudhuria dhifa ya kitaifa itakayoandaliwa na mwenyeji wake. 

Tanzania na Misri zina mahusiano mazuri ya kidiplomasia ya muda mrefu ambayo yamezidi kuimarika hasa katika miaka ya karibuni. Ushirikiano huu unatokana na misingi ya mahusiano na mashirikiano ya karibu sana kati ya Marehemu Baba wa Taifa na muasisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Kiongozi mashuhuri wa Misri na muasisi wa Jamhuri ya Taifa la Kiarabu ya Misri, Marehemu Gamal Abdel Nasser.

Uhusiano wa nchi hizi mbili umejengwa katika misingi ya ushirikiano na maelewano katika Nyanja za kijamii, kiuchumi, kisiasa, kiulinzi na kiusalama pamoja na medani za siasa za ushirikiano kimataifa, kutetea haki za binadamu, kuimarisha umoja na maendeleo ya Afrika, ukombozi wa Bara la Afrika na kupinga ukoloni, dhuluma na aina zote za ukandamamizaji duniani. Uhusiano huu umejengwa katika Nyanja zote za uhusiano katika sekta za huduma za kijamii na kiuchumi zikiwemo elimu, afya, kilimo, mawasiliano, usafiri, ulinzi na usalama na ushirikiano wa kimataifa.

Misri ni nchi ya pili yenye uchumi mkubwa Barani Afrika. Takwimu za mwaka 2016, zinaonesha kwamba pato la taifa (GDP) la Misri lilikuwa Dola za Kimarekani Billioni 266.213. Sekta kubwa kabisa katika uchumi wa Misri ni sekta ya huduma ( huduma za benki, mawasiliano, usafirishaji na utalii) ambayo inachangia takribani asilimia 52.5 kwenye GDP. Viwanda (manufacturing) inachangia asilimia 36.3, na kilimo asilimia 11.2.

Tanzania na Misri zinashirikiana katika ngazi za taasisi za serikali ambazo ni Taasisi ya Udhibiti wa utawala ya Misri (Administration Control Authority of Egypt) ambayo inashirikiana na Taasisi ya kupambana na kuzuia Rushwa ya Tanzania (TAKUKURU), Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Hospitali ya Rufaa ya Mnazi mmoja zimesaini makubaliano ya Ushirikiano na Hospitali ya El Shatby ya Chuo Kikuu cha Alexandria nchini Misri, Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) kina mashirikiano ya kubadilishana wataalamu na usimamizi wa pamoja wa Shahada za juu za uzamili na uzamivu na Chuo Kikuu cha Azhar cha Misri, Jeshi la Wananchi wa Tanzania kupitia SUMA JKT wamesaini Makubaliano ya Ushirikiano na Kampuni ya Polyserve ya Misri .

Aidha, kutokana na takwimu za kituo cha Uwekezaji (TIC) kimesajili jumla ya miradi nane kati ya mwaka 1990 hadi 2017, miradi hii ina jumla ya thamani ya Dola za Kimarekani 887.02 na kutoa ajira zipatazo 953, uwekezaji huo ni katika maeneo ya Kilimo, viwanda(mbao, mbolea, madini, dhahabu na shaba) na sekta ya Huduma.

Hivyo ziara hii ina umuhimu mkubwa sana hasa katika wakati huu ambapo msisitizo wa Serikali ni katika kujenga uchumi wa viwanda.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dar es Salaam
11 Agosti, 2017.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz P. Mlima akiongea na waandishi wa habari kuhusu ziara ya Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Mhe. Abdel Fattah Al Sisi itakayofanyika nchini wiki ijayo. 
Balozi Mlima akiendelea na mazungumzo yake na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga akifafanua jambo kwa waandishi wa habari.(hawapo pichani) 

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUANZA KWA VIKAO VYA KAMATI ZA BUNGE

Tanzania ya Kwanza Kutumia Mfumo wa PlanRep Kusini mwa Afrika

$
0
0
Tanzania imetajwa kuwa nchi ya kwanza Kusini mwa Afrika kuanza kutumia  mfumo wa kielektroniki wa PlanRep ulioboreshwa ambao husaidia katika mipango, bajeti na kutoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini kote.

Akizungumza katika mahojiano maalum mjini Kigoma, Mkuu wa Timu ya Mifumo ya TEHAMA kutoka mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)  Desderi Wengaa, amesema kuwa  mfumo huo utasaidia Taifa kufikia maendeleo endelevu kwa wakati kwani utaunganishwa na mifumo mingine iliyopo sasa na utawashirikisha wananchi wote.

“Mfumo huu utawezesha kutolewa kwa taarifa za miradi ya maendeleo zinazohusu sekta zote zilizoainishwa katika mipango na bajeti kwa wakati katika kipindi chote cha mwaka” alisema Wengaa.

Aliendelea kusema kuwa PlanRep iliyoboreshwa inaunganisha sekta zote katika mfumo mmoja ambao ni wa kitaifa tofauti na ilivyokuwa awali ambapo kila sekta ilikuwa na mfumo wake. Awali mfumo uliokuwa ukitumika haukuwa unaendana na mahitaji ya wakati hivyo kushindwa kufanya uchambuzi wa kina katika kusimamia rasilimali zilizokuwepo ikiwemo fedha. 

Aidha,watumiaji wa mfumo huo  wataweza kuutumia mahali popote  kwa kuwa ni wa kitaifa na utaondoa changamoto ya kuwepo kwa matoleo tofauti tofauti. Hali hii itasaidia kuokoa fedha nyingi zilizokuwa zikitumika kwa watoa huduma wa mifumo ya awali katika halmashauri na mikoa yote nchini.
Kiongozi wa Timu ya wataalamu wanaofanya maboresho ya mfumo wa kielektroniki wa PlanRep, Bi. Nseya Kipilyango akizungumza wakati wa mafunzo kwa watumiaji wa mfumo huo yanayoendelea Mjini Kigoma.
Mmoja wa Wawezeshaji wa Mfumo wa mfumo wa kielektroniki wa PlanRep Kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bi Jacqueline Manyanga akiwasilisha mada kwa watumiaji wa mfumo huo yanayofanyika Mkoani Kigoma yakihusisha Mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma.
Washiriki wa Mafunzo wakifuatilia mada wakati wa mafunzo hayo yanayoendelea mjini Kigoma.


Airtel yatoa vitabu vya sayansi kwa sekondari mkoa wa Sumbawanga

$
0
0
Ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano ya kuhakikisha kila mtoto kuanzia chekechekea mpaka kidato cha nne wanapata elimu bure, kampuni ya simu za mkononi Airtel Tanzania leo imetoa vitabu vya sayansi kwa shule za mkoa wa Sumbawanga vyenye thamani ya shilingi milioni kumi TZS 10,000,000. Vitabu hivyo vimepokelewa na Mbunge wa Jimbo la kalambo Mh, Josephat Kandege na kugaiwa kwa shule zenye uhabu wa vitabu jimboni humo.

 Akiongea wakati wa hafla ya kukabidhi vitabu, Mbunge wa Jimbo la kalambo Mh, Josephat Kandege alisema “ muhimu kutambua mchango wa makampuni binafsi kama Airtel Tanzania kwa juhudi za dhati za kuunga mkononi serikali yetu katika kuninua sekta ya elimu hapa nchini. sote tunajua ya kwamba serikali yetu inaongozwa na sera ya serikali ya viwanda. Kwa maana hiyo hatuwezi kuwa na viwanda bila ya kuwa na wanasayansi, hiyo basi vitabu hivi vitaongeza chachu kwa wanafunzi wetu wa kuendelea kufanya vizuri katika masomo ya sayansi na hatimaye kufanikisha ndoto zao pamoja na serikali”.

Mh Kandege aliendelea kusema kwamba “nawaomba Airtel na wadau wengine waendelee kutusaidia kwenye nyaja zingine mbali mbali ili kuendelea kutengeneza mazingira bora kwa wanafunzi kujifunza na hivyo kuongeza uelewa na kuwa na taifa lenye ueledi”.
Kwa upande wake Meneja Mauzo wa Airtel Rukwa na Katavi Bw, Hapson Kamanya  alisema “Airtel tunaamini jamii iliyoelimika inajengwa kutoka katika shule zenye vifaa vya kufundishia vya kutosha hususani vitabu,  ili kuwa na maendeleo endelevu ni muhimu kuwekeza kwenye elimu na leo tunathibitisha dhamira yetu kwa kutoa msaada wa vitabu katika shule hizi”.

Tunaamini ya kwamba msaada wa vitabu utachochea ufaulu mzuri katika masomo ya sayansi katika mkoa na  pia utaongeza idadi ya wanafunzi wanaosoma masomo ya sayansi” Aliongeza Kamenya.

Kwa upande Mkuu wa shule ya Mwazye Bw, Haron Mwaibabu akiongea kwa niaba ya shule zilizofaidika na msaada wa vitabu hivyo alisema “Msaada huu umekuja wakati muafaka wakati shule zetu zimekuwa na upungufu wa vitabu na tunaahidi kuvitunza na kuvitumia ipasavyo".

Aliongeza, ni ukweli kuwa shule zetu zina uhaba wa vitabu vya sayansi kitu ambacho kilikuwa kinatupa ugumu kwenye kufundisha na hata kupelekea baadhi ya wanafunzi wetu kutotamani kuchukua masomo ya sayansi. Tunashukuru sana Airtel kwa kuwa mkombozi kwenye hili’.
Diwani wa Kata ya Mambo Nkose Kanowalya Siwale (kushoto), Meneja Mauzo Airtel Tanzania Kanda ya Rukwa Hudson Kamenya (wa pili kushoto), Jimbo la Kalambo mkoani Sumbawanga Josephat Kandege wakimkabidhi vitabu vya sayansi Makamu wa shule ya Sekondari ya Kalambe Charles Mnkonya (kulia). Vitabu hivyo vyenye thamani ya TZS10,000,000 vimetolewa na Airtel Tanzania kwa shule za sekondari zenye uhaba wa vitabu vya sayansi kwenye Jimbo la Kalambo.
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kalembe wakiwa kwenye picha ya pamoja na Meneja Mauzo Airtel Tanzania kanda ya Rukwa Hudson Kamenya baada ya kampuni ya Airtel Tanzania kukabidhi vitabu vya sayansi vyenye thamani ya Tzs10,000,000/- mwishoni mwa wiki kwa jimbo la Kalambo mkoani Sumbawanga.
Meneja Mauzo Airtel Tanzania kanda ya Rukwa Hudson Kamenya (katikati) na Mbunge wa Jimbo la Kalambo mkoani Sumbawanga wakimkabidhi Mwalimu wa somo la Kemia kwenye shule ya sekondari ya Mwazye Aidin Mwaibabu baadhi ya vitabu vilivyotolewa na kampuni ya Airtel Tanzania kwa shule za sekondari zenye uhaba wa vitabu vya sayansi kwenye Jimbo la Kalambo.

NBS YAWATAKA WATOA TAKWIMU WANGATIE TARATIBU KUEPUSHA UPOTOSHAJI

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa Ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa 

Na Agness Moshi – MAELEZO.
Ni jambo la kawaida katika miaka hii kuona takwimu za tafiti mbalimbali zikitolewa na Taasisi , Serikali , Mashirika  au baadhi ya watu kwenye vyombo vya habari au mitandao ya kijamii ambayo kwa sasa imejizolea umarafu  kutokana  ongezeko la watumiaji wake Nchini.

Takwimu hizo zimekua zikitolewa kwa lengo la kutoa taarifa, kuelimisha au kusaidia katika kupanga mipango mbalimbali kwa maendeleo ya Taasisi, Shirika  husika au Nchi kwa ujumla . Wakati mwingine zimekua zikiibua hisia za wananchi kutaka kujua zaidi kuhusiana na taarifa hizo hivyo kupelekea vyombo vya habari kufuatilia taarifa hizo kwa undani.

Si jambo la ajabu kuona taarifa za takwimu kwenye magazeti, televisheni, mitandao ya kijamii au kuzisikia kwenye redio. Mtakua mashahidi wangu kwenye hili. Lakini je, takwimu hizi tunazozisikia na kuziona zinafuata Sheria na taratibu za utoji takwimu?

Ni wazi kila kitu kina utaratibu na sheria zake, vivyo hivyo utoaji takwimu una sheria na taratibu zake kuanzia ukusanyaji data hadi uwasilishwaji wake kwa jamii au taasisi husika.

SOMA ZAIDI HAPA
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live




Latest Images