Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109981 articles
Browse latest View live

EU injects TZS. 1.4 billion to counter child marriage and FGM

$
0
0

The European Union Delegation in Tanzania has funded and launched today a TZS. 1,400,000,000, equivalent to EUR 600,000, three- year project (2017 – 2020) to counter child marriage and female genital mutilation (FGM) that will be implemented by Plan International Tanzania in partnership with Children’s Dignity Forum (CDF) and New Light For Children Organisation (NELICO), Tackle Africa and Tanzania Football Federation (TFF) in Geita and Tarime Districts.
The Head of Delegation of the European Union to Tanzania Ambassador Roeland van de Geer (pictured standing) underlined the EU's commitment to acting in genuine partnership with Tanzania, international and regional organizations, and civil society to combat violence and harmful practices against women and girls. "Child marriage and FGM are a violation of girls’ human rights. These harmful practices have a devastating impact on a girl's health, her well-being and personal development but they also have a detrimental ripple effect on the society as a whole. Ending child marriage means a positive effect on the health and education of girls and their children, it contributes to a lower fertility rate and increases women’s expected earnings and household welfare."
Plan International Tanzania Deputy Country Director, Ms. Gwynneth Wong, said that Child Marriage in Tanzania prevails at the rate of 37%, where three out of ten girls enter into marriage before the age of 18 with Mara having the highest rate of 55% and Geita 37%. The Deputy Country Director also revealed that while the national prevalence rate of Female Genital Mutilation is at 10%, Mara is at the rate of 32%, three times the national rate. All these practices deprive the girl child of their potential to contribute to both national and personal developments.
“The girls are deprived of their right to enjoy their childhood and reaching their goals. Subjecting them to early marriages and mutilating their genitals puts them at risk of maternal health complications and even deaths. This fuels the poverty cycle and is against the UN Sustainable Development Goals”, said Gwynneth Wong.
The project targets over 1,500 in-school and out-of-school girls aged between the age of 10 – 24, and aims to prevent the incidences of harmful traditional practices of Child Marriage and FGM through empowering girls and strengthening of community, civil society and government support systems to respond to girls’ rights violation and challenges.

MAISHA NA MUZIKI, BURUDIKA NA MDAU TOKA MTAANI...

Article 14

RC MAKONDA AOMBA WADAU KUUNGA MKONO UJENZI WA OFISI ZA WALIMU JIJINI DAR ES SALAAM

BBC DIRA YA DUNIA JUMANNE 01.08.2017

WAUZA DAWA FEKI ZA KUUWA WADUDU WA ZAO LA PAMBA KUKIONA –MPINA

$
0
0


NA EVELYN MKOKOI – MWABUSALU MEATU

Hatua kali zitachuliwa kwa wafanyabiashara wanaouza dawa feki za kuuwa wadudu wa zao la Pamba nchini, Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina alipokuwa akizungmza na baadhi ya wakulima wa zao la Pamba katika kata ya Mwabusalu Wilayani Meatu Mkoani Simiyu, wakati wa ziara yake jimboni Kisesa.

Mpina alisema kuwa wapo wafayabiashara wanaodhoofisha wakulima wa zao la Pamba kwa kuwauzia madawa yasiyo na nguvu na kutoweza kufanya kazi kabisa katika zao la Pamba na kupelekea kufa kwa zao hilo na kuwataka watu hao kuwaletea wakulima dawa bora kabisa na kinyume na hapo wizara husika itachukua hatua dhidi yao.

Aidha amewataka wakulima wa kijiji hicho kinacholima zao hilo la mfano nakutoa mbegu Bora Pekee ya pamba nchini kuacha kilimo cha mazoea na kutumia fursa hiyo kuangalia kwanza maeneo wanayoishi kutokana na faida itokanayo na biashara ya zao la pamba kuninunulia chakula cha kutosha na kutoka kwenye nyumba za tembe na kujenga nyumba za kisasa.

Sambamba na hilo Mpina amewataka wakulima hao kuzingatia sauala la utunzaji wa mazingira kwa kuyaandaa mashamba yao kwa wakati huku wakizingatia changamoto ya mabadiliko ya tabianchi wanayokabilina nayo.

Awali, Naibu Waziri Mpina alikitembelea kiwanda cha Pamba cha Geki Investiment limited na kuutaka uongozi wa kiwanda hicho kuanza uzalishaji mapema mwakani ili wakulima wa kata ya Mwabusalu waweze kunufaika kutokanana mauzo ya pamba yao karibu. “Serikali hii inalenga katika kuinua na kuimarisha uchumi wa viwanda hivyo kiwanda hiki sasa wakati umefika wakuanza uzalishaji kisikae hapa na kutumika kama ghala kianze kazi mara moja, vinginevyo hatuta mvumilia muwekezaji huyu kama atashindwa Wizara husika itafanya kazi yake”. Alisisitiza Mpina.

Serikai ya awamu ya tano toka iingie madarakani imepandisha bei ya zao la pamba kutoka bei ya awali ya shilingi 600 kwa kilo mpaka mpaka sh. 1,200 imeelezwa kuwa kata ya Mwabusalu, ni kata ambayo imepata upendeleo kwa wakulima kuuza Pamba hiyo kwa kiasi cha shilingi 1,320 kwa kilo.

Tafiti zinaonyesha kuwa kata ya Mwabusalu inalima Pamba ambayo pamoja namatumizi mengine inatoa Mbegu ambayo inapatika pia katika maeneo mawili tuu nchini yanii mwabusalu na Ingunga Mkoani Tabora.


katika Picha Roli lililobeba pamba za wakulima tayari kwenda kuuzwa
Naibu Waziri Mpina akingalia ubora wa Pamba ya wakulima katika kijiji cha Mwabusalu leo.
Naibu Waziri Mpina akipima furushi la Pamba katika Mzani Maalum kabla ya kuongea na baadhi ya wakulima wa Pamba katika kijiji cha Mwabusalu jimboni kisesa leo.
Baadhi ya wakulima wa Pamba wakimsikiliza Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira (hayupo pichani) alipokuwa akingumzanao katika kijiji cha Mwabusalu mapema leo.
Picha ya pamoja ya Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira ambaye pia ni Mbunge wa Kisesa na baadhi ya wakulima wa zao la Pamba kijijini Mwabusalu, Meatu Mkoani Simiyu leo.

ATE yaanza kundi la pili la Programu ya Mwanamke wa Wakati Ujao (Female Future)

$
0
0
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya TPB Plc, Sabasaba Moshingi (katikati) akisalimiana na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Sanjay Rughani wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya miezi tisa ya program ya Mwanamke wa Wakati Ujao ya kundi la pili yanayoendeshwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE)  kwa kushirikiana na Shirikisho la Vyama vya Waajiri Nchini Norway (NHO) jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo yana lengo la kuwaandaa wafanyakazi wanawake kushika nafasi za juu za uongozi katika makampuni na bodi za wakurugenzi.
 Mwenyekiti wa Bodi ya ATE, Bi. Jayne Nyimbo (wa pili kushoto), Mkuu wa Idara ya Sheria ya ATE, Suzan Ndomba (kushoto) ma Mkurugenzi Mtendaji wa ATE, Dk. Aggrey Mlimuka (katikati), wakifurahi na Mkuu wa Kitengo cha mafunzo na maendeleo wa Acacia Mining, Janeth Lekashingo katika hafla hiyo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya ATE, Bi. Jayne Nyimbo (kushoto), akisalimiana na Mkurugenzu wa Kampuni ya Statoil Tz,  Gunnar Mentzsen    huku Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Sanjay Rughani akiangalia  wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya  program ya Mwanamke wa Wakati Ujao yanayoendeshwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE)  kwa kushirikiana na Shirikisho la Vyama vya Waajiri Nchini Norway (NHO) jijini Dar es Salaam. 
 Mhadhiri wa Taasisi ya  Uongozi ya Afrika Mashariki na Kusini (ESAMI), Prof. Apollonia Kerenge (kulia), akizungumza na washiriki wa kundi la pili wa mafunzo ya miezi tisa ya program ya Mwanamke wa Wakati Ujao yanayoendeshwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE)  kwa kushirikiana na Shireikisho la Vyama vya Waajiri Nchini Norway (NHO) jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo yana lengo la kuwaandaa wafanyakazi wanawake  kushika nafasi za juu za uongozi katika makampuni na bodi za wakurugenzi.   
  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TIB Corporate, Frank Mugeta (kulia), akizungumza na washiriki  wa mafunzo ya miezi tisa ya program ya Mwanamke wa Wakati Ujao yanayoendeshwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE)  kwa kushirikiana na Shireikisho la Vyama vya Waajiri Nchini Norway (NHO) jijini Dar es Salaam juzi. Mafunzo yana lengo la kuwaandaa wafanyakazi wanawake  kushika nafasi za juu za uongozi katika makampuni na bodi za wakurugenzi.

VIKOSI VYA MAJESHI YA SADC KUFANYA ZOEZI LA PAMOJA MKOANI TANGA

$
0
0

VIKOSI vya Majeshi ya Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC SPECIAL FORECES) vimeamua kupambana na ugaidi, uharamia kwa kushirikiana kufanya zoezi la pamoja lililopewa jina la “EX MATUMBAWE” ikiwa ni mkakati wa kutokomeza vitendo hivyo. 

Zoezi hilo litakaloshirikisha vikosi vya Makomandoo, Ndege za
kivita,meli za kivita na makomandoo watakaoruka na miavuli huku wote kwa pamoja kutoka nchi zote shiriki watafanya mazoezi hayo kubadilishana uzoefu litafanyika kuanzia Agosti 2 mpaka Septemba 1 mwaka huu katika maeneo ya Mapango ya Mleni.
 

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Tanga,Msimamizi wa Mazoezi hayo,Meja Generali Harison Msebu alisema kuwa lengo la zoezi hilo ni kufanya mazoezi ya pamoja kwa vikosi maalumu vya Majeshi ya SADC,ili kuviwezesha kuwa na utayari na harakati katika kupambana na matishio mbalimbali ya usalama. 
Aidha alisema kuwa kutasaidia kuviwezesha vikosi hivyo kukabiliana na masuala ya Ugaidi,Uharamia na maafa yatokanayo na  mabadiliko ya hali ya hewa na kusaidia vikundi vya kulinda amani kama ilivyoelekezwa na Jumuiya ya SADC pamoja na umoja wa Afrika (AU).
 
Alisema Nchi za Jumuiya ya Maendeleo  Kusini mwa Mwaafrika zimejiwekea mikakati ya kuondoa uhasama wao na zaidi kuunganisha mahusiano ikiwa na lengo la kupambana mambo ambayo yanaweza kuleta madhara katika nchi zote za Jumuiya hiyo na Afrika kwa ujumla.
Alisema yapo madhumuni ya kimkakati,utendaji kivita na kimbinu haya yote yakitekelezwa kwa ufanisi zaidi kwa nchi zote upo uwezekano wa hali ya juu katika mafanikio ya mapambano ya kigaidi na kiharamia. 
“Tunajenga misingi mizuri kwa majeshi yetu na kuondoa dhana ya kupambana wenyewe kwa wenyewe sasa tunaelekeza nguvu zetu katika mapamabano ya kigaidi na kiharamia zaidi jambo ambalo litasumbu katika nchi hizi za Afrika”Alisema Meja Jenerali Masebu.
 
Alisema zoezi hilo litashirikisha Nchi saba za Jumuiya hiyo zikiwa Botswana,Lesotho,Malawi,
 Jumuiya ya Afrika ya kusini,Zambia, Zimbabwe na Tanzania ambao ndio watakauwa wenyeji katika zoezi hilo ambalo linafanyika hapa kwa mara ya kwanza.
Mkuu wa Mkoa Tanga Martin Shigela aliwaomba wananchi wasiwe na wasiwasi pindi watakapokutana na vikosi hivyo vikiwa vinaendelea na majukumu yao huku akiwataka kutoa ushirikiano pindi watakapo hitajika. 
Alisema wananchi wasiokote vitu vyovyote wasivyovielewa na watoe taarifa katika vyombo vya ulinzi na usalama kwa kitu ambacho watakiona kinawapa mashaka.
 Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.
Msimamizi wa Zoezi la pamoja kwa vikosi maalumu vya Majeshi
ya SADC ambalo limepewa jina la  Matumbawe Meja Jenerali Harrison Msebu katika kupambana na matishio mbalimbali ya usalama (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na kuanza zoezi hilo ambalo litaanza Agosti 2 hadi Septemba 1 Jijini Tanga. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Martine Shigella


Uchumi wa Tanzania Waendelea Kuimarika-Dkt. Abbasi

$
0
0

By Bushiri Matenda-MAELEZO

Licha ya kuyumba kwa uchumi na kuongezeka kwa mfumuko wa bei duniani, Tanzania imeendelea kuongoza kwa ukuaji wa uchumi miongoni mwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo takwimu za Benki Kuu ya Tanzania (BOT) na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) zimetaja uchumi wa Tanzania kuwa imara.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi alibainisha hayo wakati akitoa ufafanuzi kwa Waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam kuhusu hali ya uchumi nchini.

“Uchumi wa Tanzania kwa miaka mitatu mfululizo sasa bado uko katika ukuaji usiopungua asilimia 7.0 hadi 7.2 ikiwa ni ukuaji wa juu katika ukanda wa Afrika Mashariki ambapo Rwanda inakua kwa asilimia 6, Uganda asilimia 5 na Kenya asilimia 6.4”, alisema Dkt. Abbasi.

Alieleza kuwa sambamba na ukuaji wa uchumi, Tanzania imeendelea kudhibiti mfumuko wa bei ambapo taarifa ya hivi karibuni zilizotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) zinaonesha kuwa mfumuko wa bei nchini umeshuka kutoka asilimia 6.1 mwezi Mei hadi kufikia asilimia 5.4 mwezi Juni mwaka huu.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Hassan Abbasi akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hali ya uchumi nchini leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara hiyo Sehemu ya Habari na Picha Bw. Rodney Thadeus.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Hassan Abbasi (hayupo pichani) alipokuwa akiwasilisha mada kuhusu hali ya uchumi mbele ya waandishi wa habari leo Jijiji Dar es Salaam.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mkurugenzi Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Hassan Abbasi akiwasilisha mada kuhusu hali ya uchumi wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam.
Picha zote na: MAELEZO.


RAIS WA ZANZIBAR DK.SHEIN AZUNGUMZA NA UJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI SHIRIKA LA NYUMBA,UONGOZI WA WIZARA UJENZI,MAWASILIANO NA USHAFIRISHAJI

$
0
0
Na Rajabu Mkasaba, IKULU
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, amesema kuwa kuwepo kwa mabadiliko makubwa ya kimaendeleo baada ya kuundwa kwa Mamlaka ya Viwanja vya ndege vya Zanzibar kumeweza kuongeza mapato na kuahidi kuimarika zaidi hali hiyo ndani ya kipindi chake cha uongozi. 
Dk. Shein aliyasema hayo leo, alipokutana na uongozi wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji, Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege pamoja na Uongozi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege katika vikao vinavyoendelea Ikulu mjini Zanzibar. 
Dk. Shein alitumia fursa hiyo kuipongeza Mamlaka hiyo kwa kufanya mabadiliko makubwa katika viwanja vya ndege vya Zanzibar hatua ambayo imeweza kusaidia kwa kiasi kikubwa ongezeko la mapato katika viwanja hivyo. 
Katika maelezo yake Dk. Shein alisema kuwa licha ya baadhi ya changamoto zilizopo lakini Mamlaka imeweza kupata mafanikio makubwa na hivi leo viwanja vya ndege Unguja na Pemba viweza kuimarika na kuleta tija kwa kuongeza mapato. 
Akizungumza suala zima la fidia kwa wananchi waliojenga pembezoni mwa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar Dk. Shein alisema kuwa ni vyema likatafutiwa ufumbuzi kwa kuwatafuta wahusika na kuwasikiliza madai yao ili hatua za malipo ziendele kuchukuliwa. 
Akizungumza na uongozi wa Wizara hiyo kupitia Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Nyumba pamoja na Uongozi wa Shirika hilo, Dk. Shein alisisitiza haja ya Shirika hilo kuzitambua na kuziorodhesha ili kujua idadi ya nyumba zao zote za Unguja na Pemba pamoja na zile za Wakala hatua ambayo pia, itasaidia kuepusha udanganyifu.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akionesha Ramani ya Ujenzi wa Mji wa kisasa utakaojengwa  sambamba na ufukiaji wa Bahari ya  Eneo la pwani ya Gulioni  katika kikao cha siku moja kilichojumuisha  Uongozi wa Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji pamoja na Wajumbe  wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Nyumba na Uongozi wa Shirika la Nyumba  katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja 

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akionesha Ramani ya Ujenzi wa Mji wa kisasa utakaojengwa  sambamba na ufukiaji wa Bahari ya  Eneo la pwani ya Gulioni  katika kikao cha siku moja kilichojumuisha  Uongozi wa Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji pamoja na Wajumbe  wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Nyumba na Uongozi wa Shirika la Nyumba  katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja 
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Nyumba wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) wakati alipofanya kikao cha siku moja pamoja na Uongozi wa Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja. Kwa Taarifa kamili BOFYA HAPA

Changamkieni fursa Mradi wa Bomba la Mafuta – Dkt. Pallangyo

$
0
0

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo amewataka wananchi wanaoishi katika mikoa itakayopitiwa na miundombinu ya bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi katika Bandari ya Tanga nchini Tanzania kuchangamkia fursa mbalimbali zitakazojitokeza wakati wa utekelezaji wa mradi.

Dkt. Pallangyo aliyasema hayo mapema jana jijini Dar es Salaam kupitia kipindi maalum cha 360 kilichorushwa na kituo cha televisheni cha Clouds wakati akielezea maandalizi ya uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Tanga nchini Tanzania unaotarajiwa kufanyika Agosti 05, mwaka huu.

Alisema kuwa wananchi katika maeneo husika wanatakiwa kujiandaa kwa ajira wakati wa maandalizi na utekelezaji wa mradi, ikiwa ni pamoja na utoaji wa huduma mbalimbali za vyakula, usafiri na ufundi.

“Fursa zitakazokuwepo ni nyingi mno, vijana waliomaliza Vyuo vya Ufundi wataweza kufanya kazi za uchomeleaji wa vyuma, madereva wenye leseni kupata kazi, wakina mama lishe kuuza vyakula, wakulima kuuza mazao kwa walaji watakaoongezeka kutokana na uwepo wa mradi huo, alisema Dkt. Pallangyo.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia) akifafanua jambo kwa mwandishi wa habari na mwongozaji wa kipindi cha 360 cha Clouds TV, Hassan Ngoma katika mahojiano maalum kuhusu uzinduzi wa mradi wa wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Tanga nchini Tanzania unaotarajiwa kufanyika Agosti 05, mwaka huu yaliyofanyika mapema Julai 31, mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Mwandishi wa habari na mwongozaji wa kipindi cha 360 cha Clouds TV, Hassan Ngoma akiuliza swali kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia) kwenye mahojiano hayo.

WAZIRI MKUU ATEMBELEA MTAMBO WA KUSAFISHA DHAHABU CHUNYA

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea na kujionea mtambo wa kisasa wa kusafisha dhahabu kwa asilimia 99 unaomilikiwa na kampuni ya Sunshine Group uliopo katika kata ya Matundasi wilayani Chunya mkoani Mbeya.

Ametembelea mtambo huo leo (Jumanne, Agosti 1, 2017) wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Mbeya na kusema kuwa mtambo huo ni wa kwanza kuweza kusafisha dhahabu kwa kiwango hicho hapa nchini.

Amesema kwa Tanzania kampuni ya Sunshine Group ndiyo yenye mtambo wa kuweza kusafisha dhahabu na kufikia asilimia 99 ukilinganisha na makampuni mengine yanayomiliki migodi.Pia Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea kufanya mazungumzo na makampuni mbalimbali kwa ajili ya kuwekeza katika mradi wa ujenzi wa mtambo wa kuchenjulia makinikia ili kuweza kusafirisha dhahabu halisi.

Naye Ofisa Madini Mkoa wa Mbeya, Mhadisi Said Makwama amesema dhahabu inayosafishwa katika mtambo huo ikipelekwa nje ya nchi inaingizwa sokoni moja kwa moja tofauti na migodi mingine.

Mhandisi huyo alisema Sheria mpya ya Madini imesaidia Serikali kupata kodi ya juu itokanayo na Mrabaha wa asilimia 6 na ‘clearance and inspection fee’ ya asilimia moja ya thamani ya madini yanayosafirishwa ukilinganisha na mrabaha wa awali wa asilimia nne.

MHANDISI MAKANI ASISITIZA UTALII WA MISITU YA ASILI NCHINI KAMA CHANZO MUHIMU CHA KUONGEZA PATO LA TAIFA NA JAMII KWA UJUMLA

$
0
0
NA HAMZA TEMBA - WMU

Katika kuhakikisha sekta ya utalii nchini inaendelea kukua kwa kasi, Serikali imesema itaimarisha utalii wa Misitu ya Asili nchini iweze kutoa mchango mkubwa kwenye pato la taifa tofauti na ilivyo hivi sasa ambapo hutegemea zaidi utalii wa wanyamapori.


Hayo yamesemwa jana wilayani Lushoto na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani wakati akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku moja wilayani humo kwa ajili ya kutatua migogoro mbalimbali ya uhifadhi.


Alisema sekta ya utalii nchini imekuwa ikitegemea sana wanyamapori na kusahau vivutio vingine kama vile misitu ya asili ambayo ndani yake kuna mimea na viumbe hai mbalimbali adimu duniani na ambavyo hupatikana Tanzania pekee.


“Tumezoea zaidi utalii wa wanyamapori, utalii wa misitu unaweza kuzidi hata wa wanyamapori, kwenye misitu yetu ya asili tunajivunia mimea adimu ya asili na viumbe hai mbali mbali kama vile ndege, vyura, vipepeo, mijusi nakadhalika, tunachotakiwa kufanya ni kutunza misitu yote ya asili, tuiboreshe na kuitangaza ili kupata watalii wengi zaidi na pato la taifa liendelee kukua”, alisema Makani.


Kwa mujibu wa tovuti ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Tanzania ina jumla ya Hifadhi za Misitu ya Asili 100, idadi ambayo ni kubwa ukilinganisha na hifadhi za taifa ambazo zipo 16 pekee, idadi hiyo kubwa pamoja na upekee wake inatoa fursa pana ya kuendeleza sekta ya utalii nchini.
Naibu Waziri wa Maliasili, Mhandisi Ramo Makani (kulia) akijibu kero mbalimbali za uhifadhi kwa wananchi wa Kijiji cha Shume Nywelo, Wilaya ya Lushoto Mkoani Tanga wakati wa ziara yake ya siku moja ya kutatua migogoro ya hifadhi wilayani humo jana. 
Naibu Waziri wa Maliasili, Mhandisi Ramo Makani (wa pili kushoto) akisikiliza moja ya kero kuhusu uhifadhi kutoka kwa Abunio Abraham Shangali (wa pili kulia) ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Shume Nywelo, Wilaya ya Lushoto Mkoani Tanga jana wakati wa ziara yake ya siku moja ya kutatua migogoro ya hifadhi wilayani humo. 
 Naibu Waziri wa Maliasili, Mhandisi Ramo Makani (wa pili kulia) akizungumza na viongozi wa kikundi cha uhifadhi na utalii cha Friends of Usambara kilichopo Lushoto Mkoani Tanga wakati wa ziara yake ya siku moja ya kutatua migogoro ya hifadhi wilayani humo jana.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

CISA AND CISM DECEMBER 2017 EXAM REVIEW CLASSES

MAGAZETI YA JUMATANO LEO AUG 2,2017


Vito vya Thamani vyapitishwa kimagendo Rukwa

RC Rukwa Azionya Halmashauri Dhidi ya Matumizi Mabovu ya Mashine za EFD

$
0
0



Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen amezionya halmashauri zote mkoani Rukwa kuhakikisha wanazitumia vizuri manshine za EFD kwa kuongeza mapato katika halmashauri zao.

Ametoa onyo hilo kwenye kikao maalum cha kujibu hoja za ukaguzi wa hesabu za serikali kwa madiwani wa  Manispaa ya Sumbawanga katika kumalizia ziara yake maalum kwa halmashauri zote mkoani humo kujua namna Halmashauri zilivyojipanga ili hoja hizo zisijirudie miaka inayofuata.  
Akiongea huku akionesha risiti alizozikamata katika maeneo mbalimbali ya mauzo alisema kuwa serikali inafanya kila liwezalo katika kuhakikisha inakusanya maopato lakini bado kuna watumishi wanatafuta namna ya kuiskosesha serikali mapato hayo.

“katika kila sehemu za mauzo lazima mashine hizi ziwepo na kuwepo sio mtindo huu (akionesha msururu wa risiti zilizokatwa tayari kwa matumizi) hizi nimezikamata maeneo anajua Mkurugenzi, asubuhi watu wanagawana, ndio mchezo uliopo, pamoja na jitihada tunazofanya bado watu wanatafuta mbinu za kuiba, hii sio kwamba nimeleta iwe mfano, hapana, nimezikamata na mfahamu kuwa mimi ni mtaalamu wa kukamata,”Alisema. 
RC Rukwa  Mh. Zelote Stephen akiwaonesha waheshimiwa madiwani   (hawapo pichani)risiti ambazo tayari zimeshakatwa kabla ya kutumiwa. 
P_20170731_160828_vHDR_Auto
RC Rukwa akiwaonesha waheshimiwa madiwani   (hawapo pichani) kitabu cha hoja za mthibiti na mkaguzi wa serikali kwa  Manispaa ya Sumbawanga.
P_20170731_162142_vHDR_Auto
RC Rukwa akitoa ufafanuzi. 


NAIBU WAZIRI WA MALISILI NA UTALII,MHANDISI RAMO MAKANI AZUNGUMZA NA WAKAZI WA KIJIJI CHA MSHIRI WILAYANI MOSHI KUHUSU ENEO LA NUSU MAILI

$
0
0
Niabu Waziri wa Malisili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akizungumza na wananchi katika kijiji cha Mshiri wilayani Moshi ,alipotembelea kijiji hicho kusikiliza Changamoto zinazo wakabili hususani katika eneo la Nusu Maili lililopo chini ya Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro.
Baadhi ya Wakazi wa Kijiji cha Mshiri wilayani Moshi wakimsikiiza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani (Haupo pichani ) alipozungumza nao.
Mbunge wa jimbo la Vunjo ilipo kijiji cha Mshiri ,James Mbatia akizungumza katika mkutano huo kuhusu Changaoto mbalimbali zinazowakabili wananchi kaika kijiji hicho.
Mku wa wilaya ya Moshi ,Kippi Warioba akizungumza katika mkutano huo.
Baadhi ya viongozi kutoka Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) walioongozana na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani kutembelea kijiji cha Mshiri,kutoka kulia ni Meneja Mawasiliano wa TANAPA,Pascal Shelutete,Meneja Utalii wa Tanapa.Bw Manase na Mhifadhi Ujirani Mwema KINAPA,Bi Hobokela Mwamjengwa.

MAONI YA WAKUU WA VYUO VYA MAENDELEO NA USTAWI WA JAMII NCHINI KUHUSIANA NA MAFUNZO YA UDHIBITI WA VIASHIRIA HATARISHI KATIKA UTENDAJI WA KAZI.

"TWENZETU WASHINGTON DC " WATANZANIA KUFANYA RE-UNION LABOR DAY WEEKEND NDANI YA WASHINGTON DC !!

$
0
0


TWENZETU WASHINGTON D.C.

Hii ndio Habari Ya Mijini Kote U.S.A. Kila kona habari kubwa imekuwa "DMV-KAMA ZAMANI". Wana DMV wanayofuraha kubwa Kuwakaribisha Watanzania Wote kutoka kila Pande za America Kujumuika Pamoja Kama ilivyokuwa Desturi yetu Miaka ya Nyuma.
Soma Ratiba Nzima kujua Mpango Mzima. Kumbuka; Ukishafika tu hapa Washington DMV, Wageni Wote Chakula, Vinywaji vya aina zote na kiingilio ni "BURE".
Stay Tuned More Details to Come 
"We Ain't Done Yet"

#WashingtonDMV2017 #PositiveVIBESoNlyDMV#
Viewing all 109981 articles
Browse latest View live




Latest Images