Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109981 articles
Browse latest View live

SERIKALI YAONGEZA MUDA WA KUNYONYESHA KWA WATUMISHI WA UMMA NA MASHIRIKA NA SEKTA BINAFSI

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii .

SERIKALI imeongeza masaa ya unyonyeshaji kwa watoto kwa watumishi wa serikali, mashirika pamoja sekta binafsi ili kuwezesha watoto kuwa na afya bora inayotokana na maziwa ya mama.

Hayo ameyasema Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati akifungua Wiki ya Unyonyeshaji, amesema kuwa mama mzazi baada ya kumaliza miezi mitatu ataingia kazini 3:30 na kuondoka saa 7:30 katika kumuwezesha mama kunyonyesha mtoto bila kuingiliwa na majukumu ya kikazi.

Ummy amesema kuwa watendaji wa Umma na mashirika pamoja na taasisi lazima wafanye hivyo katika kutambua umuhimu wa mama mzazi kunyonyesha kwa muda uliowekwa kwa kipindi cha miezi sita.

Amesema kuwa ni gharama kubwa katika kuhudumia watoto walio na utapiamlo ambao unatokana moja ni kukosa maziwa ya mama kwa muda mrefu hivyo kuepuka ni njia rahisi ikiwemo kutengwa kwa masaa hayo.

Waziri Ummy amesema kuwa suala la lishe lazima liangaliwe kwa ukaribu na wadau wote katika kuweza kuwaondoa watoto katika utapiamlo ambao unafanya kudumaa kwa akili.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akipata maelezo juu masuala ya lishe kutoka kwa mtaalam wa lishe wa Taasisi ya Chakula lishe nchini (TFNC),Neema Joshua wakati maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji leo.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akizungumza wakati wa ufunguzi wa wiki ya unyonyeshaji na uzinduzi usambazaji taarifa kwa njia ya simu leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chakula na Lishe Nchini(TFNC), Joyceline Kaganda akizungumza juu ya mikakati ya lishe na umuhimu wa unonyeshaji leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Lishe nchini (Panita), Tumaini Mkindo akitoa salamu za mashirika yasio ya kiserikali yanavyofanya kazi katika sehemu ya lishe kwa kuwa miradi mbalimbali.


RAIS DKT. MAGUFULI AMUAPISHA BALOZI WA TANZANIA NCHINI MALAWI PIA APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO WA MABALOZI WATANO IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Benedict Mashiba kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za utambulisho kutoka kwa Balozi wa Vietnam hapa nchini Nguyeni Kim Doahn, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Indonesia hapa nchini Prof. Ratlan Pardede, Ikulu jijini Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Vatican hapa nchini Mhashamu Askofu Mkuu Marek Solcynski, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Ujerumani hapa nchini Dkt. Detlef Wachter akijitambulisha kabla ya kuwasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za utambulisho kutoka kwa Balozi wa Uganda hapa nchini Richard Tumisiime Kabonero Ikulu jijini Dar es Salaam.

WAKUU WA VYUO VYA MAENDELEO YA JAMII WAENDELEA NA MAFUNZO KUHUSU UDHIBITI WA VIASHIRIA HATARISHI KATIKA UTENDAJI WA VYUO MKOANI MOROGORO

$
0
0
Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii na Mwenyekiti wa Mafunzo Bw. Paschal Mahinyila akiwakaribisha washiriki katika mafunzo Wakuu wa vyuo hao kuhusu Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Utendaji wa Vyuo hivyo yanayofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti mkoani Morogoro leo tarehe 01.08.2017. 
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii Bw. Patrick Golwike (kushoto) akifafanua umuhimu wa uadilifu kwa Wakuu wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii(hawapo pichani) katika utendaji kazi wa vyuo wakati wa mafunzo kwa wakuu wa vyuo hao kuhusu Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Uendeshaji wa Vyuo hivyo yanayofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti, mkoani Morogoro leo.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Bibi Deodata Makani(kulia) akifafanua mambo mbalimbali ya kiutawala kwa Wakuu wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii nchini katika mafunzo kwa wakuu wa Vyuo hao kuhusu Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Utendaji wa Vyuo hivyo yanayofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti, mkoani Morogoro leo.
Mkurugenzi wa Ugavi na Manunuzi kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Bibi Martha Chuma (katikati) akifafanua mambo mbalimbali yahusuyo ugavi na manunuzi kwa wakuu wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii nchini katika mafunzo kwa wakuu wa Vyuo hao kuhusu Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Utendaji wa Vyuo hivyo yanayofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti, mkoani Morogoro.

MAREHEMU PROF NAGU KUZIKWA ALHAMISI NYUMBANI KWAKE ENDASAKI,WILAYANI HANANG

$
0
0

Marehemu Prof. Nagu alikuwa Mhadhiri ktk chuo kikuu Mzumbe. Marehemu pia ni mume wa Mbunge wa Hanang- Mhe. Mary Nagu ambaye pia alikuwa Waziri katika serikali ya awamu ya tatu na ya nne. Marehemu Prof. Nagu ni baba wa Dr. Tumaini, Neema na Deogratias. 

Tunapenda kuwajulisha kuwa Marehemu atapumzishwa katika nyumba yake ya milele nyumbani kwake Endasaki Wilaya ya Hanang siku ya Alhamisi tarehe 3/8/2017 

leo saa kumi jioni kutakuwa na Ibada ya kumuaga Marehemu katika kanisa katoliki St Peters, kisha mwili utaenda kulala nyumbani kwake Regent Estate Mikocheni tayari kusafirishwa siku ya tarehe 02/07/2017 kuelekea Manyara, Hanang', Kijiji cha Endasaki. 

Raha ya milele umpe ee Bwanana na mwanga wa milele umwangazie.

Apumzike kwa Amani Mzee wetu Prof Joseph Nagu.

MASAUNI AWATAKA WANAFUNZI VYUO VIKUU NCHINI KUONGEZA KASI YA UBUNIFU, AFUNGUA MAONYESHO YA SAYANSI CHUO CHA ST. JOSEPH DAR

$
0
0

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akikata utepe kuashiria kufungua Maonyesho Makubwa ya Sayansi na Teknolijia yaliyoandaliwa na wanafunzi wanaosoma fani ya uhandisi Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph, jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Mkuu wa Chuo hicho, Dk. Prakabahran Anath. Masauni baada ya kuangalia kazi za ubunifu mbalimbali uliofanywa na wanafunzi hao, aliwataka wanafunzi hao kuongeza kasi zaidi ya kuongeza ubunifu kutokana na taaluma wanayoipata chuoni hapo.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (aliyevaa suti) akimsikiliza Mwanafunzi wa mwaka wanne fani ya uhandisi Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph cha jijini Dar es Salaam, Tumaini Lutufyo (kushoto) wakati alipokuwa anatoa maelezo ya gari la kuzima moto ambalo linatumia gesi lililotengenezwa na wanafunzi wa chuo hicho. Masauni alifungua Maonyesho ya Sayansi na Teknolojia chuoni hao ambapo aliangalia kazi mbalimbali za ubunifu uliofanywa na wanafunzi hao, pia aliwataka wanafunzi hao kuongeza kasi zaidi ya kuongeza ubunifu kutokana na taaluma wanayoipata chuoni hapo 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akiliendesha gari linalotumia umeme wa jua lililotengenezwa na wanafunzi wa fani ya uhandisi Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph cha jijini Dar es Salaam. Masauni alifungua Maonyesho ya Sayansi na Teknolojia chuoni hao ambapo aliangalia kazi mbalimbali za ubunifu uliofanywa na wanafunzi hao, pia aliwataka wanafunzi hao kuongeza kasi zaidi ya kuongeza ubunifu kutokana na taaluma wanayoipata chuoni hapo .
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph cha jijini Dar es Salaam, mara baada ya kufungua Maonyesho ya siku mbili ya Sayansi na Teknolojia yaliyoandaliwa na Chuo hicho kwa lengo l kuonyesha ubunifu mbalimbali wa wanafunzi hao. Masauni baada ya kuangalia kazi za ubunifu mbalimbali uliofanywa na wanafunzi hao, aliwataka wanafunzi hao kuongeza kasi zaidi ya kuongeza ubunifu kutokana na taaluma wanayoipata chuoni hapo. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akimsikiliza Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph cha jijini Dar es Salaam, Dk. Prakabahran Anath alipokua anatoa historia ya chuo hicho kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri huyo kufungua Maonyesho Makubwa ya Sayansi na Teknolijia yaliyoandaliwa na wanafunzi wanaosoma fani ya uhandisi chuoni hapo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.



KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NC

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU TAASISI ZA UMMA ZINAZOTUMIA MKAA NA KUNI KUBADILISHIWA MATUMIZI NA KUTUMIA GESI

$
0
0
Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba(wa kwanza kulia) akiongea na Waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa akitoa tamko  kuhusu Taasisi za Umma zinazotumia mkaa na kuni kubadilishiwa matumizi na kutumia gesi jijini Dar Es Salaam.

KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI NA WATENDAJI WAKE WAKUU WAPITIA MPANGO WA MANUNUZI WA MWAKA WA FEDHA 2017/2018

$
0
0
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira akizungumza na Watendaji Wakuu, Maofisa Bajeti na Mipango wa Wizara yake wakati wa Kikao cha kupitia Mpango wa Manunuzi wa Wizara wa mwaka wa fedha 2017/2018 kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Jeshi la Polisi Makao Makuu ya Jeshi hilo.Wa kwanza kulia ni Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dk. Anna Makakala, akifuatiwa na Kamishna wa Polisi Jamii Mussa Alli Mussa pamoja na Kamishna wa Polisi wa Fedha na Logistiki Albert Nyamuhanga.
 Mkurugenzi wa Ununuzi na Ugavi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi David Mwangosi, akiwasilisha Mpango wa Ununuzi wa Wizara hiyo wa mwaka wa fedha 2017/2018 kwa Watendaji Wakuu, Maofisa Bajeti na Mipango wa Wizara hiyo wakati wa Kikao cha kupitia Mpango wa Manunuzi wa Wizara wa mwaka wa fedha 2017/2018 kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Jeshi la Polisi Makao Makuu ya Jeshi hilo. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira wa hiyo.
 Kamishna wa Polisi wa Fedha na Logistiki Albert Nyamuhanga    akichangia hoja kwa Watendaji Wakuu, Maofisa Bajeti na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi (hawapo pichani) wakati wa Kikao cha kupitia Mpango wa Manunuzi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wa mwaka wa fedha 2017/2018 kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Jeshi la Polisi Makao Makuu ya Jeshi hilo. Kulia ni Kamishna wa Polisi Jamii Mussa Alli Mussa. 
Kamishna wa Uhamiaji Utawala na Fedha Edward Peter Chogero akichangia hoja kwa Watendaji Wakuu, Maofisa Bajeti na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi (hawapo pichani) wakati wa Kikao cha kupitia Mpango wa Manunuzi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wa mwaka wa fedha 2017/2018 kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Jeshi la Polisi Makao Makuu ya Jeshi hilo. Kulia ni Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dk. Anna Makakala. 

Imeandaliwa na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali  Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA BALOZI WA MAURITIUS HAPA NCHINI NA WAWEKEZAJI WA SUKARI

$
0
0



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Mauritius nchini Tanzania Mhe. Jean Pierre Jhumun mwenye makazi yake mjini Maputo,Msumbiji aliyeongozana na Wawekezaji wa Uzalishaji Sukari ambao wameonyesha nia na utayari wa kuwekeza nchini.

Mbali ya ujumbe kutoka Mauritius, wengine waliohudhuria mazungumzo hayo ni Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Profesa Godius Kahyarara na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw.WilliamErio .
Katika mazungumzo hayo  Makamu wa Rais amewahakikishia wawekezaji hao ushirikiano wa Serikali na kuwaeleza kuwa Tanzania ina mazingira bora ya uwekezaji.

Mbali ya fursa ya uwekezaji katika Sukari, Makamu wa Rais aliainisha maeneo mengine ya kuwekeza kama vile viwanda na TEHAMA.
Aidha alisema pindi uwekezaji huo ukifanikiwa , Tanzania itafaidika na soko la nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na masoko mengine duniani kwa ujumla.
Uwekezaji huu utakuwa wa Ubia kati mashirika ya hifadhi ya mifuko ya jamii na pia kampuni nyingine za wazawa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  akiagana na  Balozi wa Mauritius nchini Tanzania Mhe. Jean Pierre Jhumun mwenye makazi yake mjini Maputo,Msumbiji mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwake Ikulu jijini Dar Es Salaam
17
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  akiagana na  Balozi wa Mauritius nchini Tanzania Mhe. Jean Pierre Jhumun mwenye makazi yake mjini Maputo,Msumbiji aliyeongozana na Wawekezaji wa Uzalishaji Sukari ambao wameonyesha utayari wa kuwekeza nchini Tanzania.
15
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  akiwa kwenye picha ya pamoja na  Balozi wa Mauritius nchini Tanzania Mhe. Jean Pierre Jhumun mwenye makazi yake mjini Maputo,Msumbiji , Wawekezaji wa Uzalishaji Sukari na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Profesa Godius Kahyarara na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw.William Erio .Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais
……………………………..

TAARIFA ZA MICHEZO KUTOKA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

$
0
0
DK. NDUMBARO, MGONGOLWA WATEULIWA TFF
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, imeteua Kamati ya Rufaa ya Leseni za Klabu, ikiwa ni maandalizi ya kuanza msimu mpya wa mashindano ya soka yanayosimamiwa na kuendeshwa na TFF.
Viongozi na wajumbe waliteuliwa na kupitishwa Jumapili Julai 30, 2017 katika Mkutano wa Kamati ya Utendaji uliofanyika Ukumbi wa Hosteli za TFF, zilizopo Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Ilala jijini Dar es Salaam yaliko Makao Makuu ya shirikisho.
Viongozi na Wajumbe walioteuliwa ni Msomi Wakili Dk. Damas Ndumbaro atayekuwa Mwenyekiti; Msomi Wakili Alex Mngongolwa (Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo) wakati Wajumbe ni Meneja wa zamani wa Uwanja wa Taifa, Charles Matoke, Tumainiel Mlango na Ahmed Menye.
Viongozi wa Kamati hiyo watakuwa na majukumu ya kusililiza rufaa kutokana na uamuzi wa Kamati ya Leseni za Klabu inayoongozwa na Msomi Wakili Lloyd Nchunga ambayo inasimamia utekelezaji wa Kanuni ya 11 ya Ligi Kuu.
Kwa mujibu wa kanuni hiyo ya 11, Klabu za Ligi Kuu zinawajibika na kutakiwa kuwasilisha maombi ya kupatiwa Leseni ya Klabu kwa TFF katika muda utakaotangazwa na Kamati ya Utendaji ya TFF na kuhakikisha zinakidhi masharti na vigezo vyote vya msingi kupatiwa leseni ili kuweza kushiriki Ligi Kuu.
Kanuni hiyo ya 11 inasema kwamba Klabu itakayoshindwa kukidhi kiasi cha kukosa Leseni haitashiriki Ligi Kuu kwa msimu husika. Vigezo hitajika kwenye kupata leseni ya klabu ni kuwa na Uwanja wa nyumbani wa mechi, uwanja wa mazoezi, umiliki wa klabu moja, kuwa na timu ya vijana, uwepo wa ofisi rasmi na watendaji wake akiwamo mtendaji mkuu (CEO) na maofisa masoko, habari na mhasibu mwenye taaluma ya uhasibu.
Tayari Klabu zilielekezwa kuwasiliana na Meneja wa Leseni za Klabu, Jemedari Said ambaye ni Ofisa Maendeleo ya Mpira wa Miguu Tanzania wa TFF kwa ajili ya maelezo ya kuchukua na kurejesha fomu kwa mujibu wa taratibu na kanuni za mashindano kabla ya kuanza rasmi mashindano.

Dkt. Hassan Abbasi- Ripoti Nyingi Duniani Zinasema Uchumi wa Tanzania uko Imara

SERIKALI YASAJILI VIWANDA 2,536

$
0
0
Na Bushiri Matenda- MAELEZO

Wizara ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji imekanusha taarifa iliyotolewa na uongozi wa CHADEMA kuhusu suala la ubinafsishaji na kuwa hakuna viwanda vipya vilivyojengwa katika awamu hii kwa vile hakuna mkopo wa kuanzisha viwanda .

Taarifa iliyotolewa Jijini Dar es Salam imesema kuwa viwanda vilivyokuwepo viliuzwa kwa bei rahisi kwa kuwa wawekezaji waliovichukua waliingia mikataba ya kuviendeleza na Serikali, hivyo vilichangia mapato ya serikali na kutoa ajira.

Aidha baadhi ya wawekezaji wa viwanda vilivyobinafsishwa waliviendeleza na mpaka sasa vimeendelea kutoa mchango mkubwa katika uchumi wa nchi. Baadhi ya viwanda hivyo ni kiwanda cha Bia (TBL),KIWANDA CHA Sigara (TCC), viwanda vya saruji vya Mbeya,Tanga na Twiga.

Hata hivyo viwanda vilivyokiuka mkataba vitarudishwa serikalini ili vitangazwe kwa wawekezaji wenye uwezo wa kuviendeleza ili viendelee na uzalishaji ambao utatoa fursa ya ajira na kuingiza mapato serikalini.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

BENKI YA CRDB YAKABIDHI GARI KWA KITUO CHA POLISI KAWE, JIJINI DAR LEO

$
0
0

Mkurugenzi wa Masoko, Utafitii na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB PLC, Tully Mwambapa (wa pili kulia) akikabidhi funguo ya gari mpya aina ya Toyota Land Cruser kwa aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni aliyehamishiwa Makao Makuu ya Jeshi hilo Kitengo cha Mafao na Fidia, SACP Suzan Kaganda (wa nne kushoto) ikiwa ni makabidhiano ya gari la kusaidia doria kwa Kituo cha Polisi Kawe, Jijini Dar es salaam. Gari hilo lenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 70, limetolewa na Benki ya CRDB kwa kituo hicho. Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika mchana wa leo katika Kituo cha Kawe jijini Dar es salaam. Wengine pichani kutoka kulia ni Kamanda wa Polisi wa Kinondoni wa sasa, ACP Murilo Jumanne Murilo, Afisa Mtendaji Kata ya Kawe, Husna Nond, Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kinondoni, OCD Jackson Simba pamoja na Mkuu wa Kituo cha Polisi Kawe, ASP Samson Mwambungu. 
Mkurugenzi wa Masoko, Utafitii na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB PLC, Tully Mwambapa akizungumza katika hafla ya kukabidhi gari kwa Jeshi la Polisi Kituo cha Kawe, jijini Dar es salaam.
Kamanda wa zamani wa Polisi Mkoa wa Kinondoni aliyehamishiwa Makao Makuu ya Jeshi hilo Kitengo cha Mafao na Fidia, SACP Suzan Kaganda akizungumza katika hafla ya kukabidhi gari kwa Jeshi la Polisi Kituo cha Kawe, jijini Dar es salaam.
Meneja Masoko na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB PLC, Godwin Semunyu akiongoza hafla hiyo.
Meza kuu.

LUKUVI AWATAHADHARISHA WANANCHI KUHUSU MATAPELI WA NYARAKA ZA UMILIKI ARDHI

$
0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, amekutana na wakazi wa Wilaya ya Temeke na Kigamboni katika kusikiliza na kutatua kero za Sekta ya ardhi. Katika mahojiano na wananchi hao, Mhe. Lukuvi amewaonya wananchi kuwa makini na matapeli wanaochukua nyaraka halali za umiliki na kutengeza nyaraka feki.

Hayo yamebainika baada ya baadhi ya wananchi kulalamikia mmliki wa kampuni ya Holland Investment iliyopo  jijini Dar es Salaam kwamba, amekuwa akichukua nyaraka halali za umiliki kwa wananchi kwa lengo la kuwasaidia na baadae kuwabadilishia na kuwarudishia nyaraka feki.
Mmoja wa wananchi kutoka Wilaya ya Temeke (aliyesimama) akieleza kero yake kwa Mhe. Lukuvi wakati wa kusikiliza na kutatua kero za Sekta ya ardhi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi akisisitiza jambo kwa wananchi waliofika ofisini kwake kwa ajili ya kutoa kero zao za masuala ya ardhi.

Mrisho Mpoto Ft Kassim Mganga - KITENDAWILI

$
0
0
Msanii wa muziki wa asili nchini Tanzania, Mrisho Mpoto ameachia wimbo wake mpya Kitendawili akiwa amemshirikisha mkali wa nyimbo za mahaba, Kassim Mganga. Wimbo huo umeandaliwa katika studio za Combination Sound chini ya producer, Man Walter.

MICHUZI TV: MTAZAME MLA MACHUNGWA WA KULIPWA KUTOKA MJINI ARUSHA...


NIDA YASHIRIKI MAONYESHO YA NANENANE KITAIFA MKOANI LINDI, WANANCHI KUPATA VITAMBULISHO VYAO NDANI YA MUDA MFUPI

$
0
0
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)ni miongoni mwa Taasisi za Serikali zinazoshiriki maonyesho ya Kitaifa ya Nanenane, yanayofanyika katika Mkoa wa Lindi katika viwanja vya  Ngongo.
Maonyesho hayo ambayo yamezinduliwa na Waziri wa Nchi ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. George Simbachawene; ambaye amewasili na kukagua baadhi ya mabanda kabla kuwahutubia wananchi wa Lindi waliokusanyika kwa wingi kushuhudia tukio hilo.
NIDA inashiriki kwenye maonyesho hayo kwa kutoa huduma ya Usajili kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi ambapo kwa wale watakaokamilisha taratibu zote za Usajili watapatiwa Vitambulisho vyao ndani ya mwezi mmoja. Huduma nyingine zinazotolewa ni pamoja na Ugawaji wa Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi ambao walisajiliwa kwenye maonyesho hayo mwaka Jana, wananchi kupata taarifa za vitambulisho vyao kwa wale ambao wamekamilisha taratibu za Usajili, elimu kuhusu matumizi, faida na umuhimu wa Vitambulisho vya Taifa pamoja na kusoma taarifa za mwananchi kwenye Kitambulisho chake kutumia Tovuti Salama iliyoundwa kurahisisha matumizi ya  vitambulisho vya Taifa.
Kauli Mbiu ya maonyesho hayo kwa mwaka huu “Zalisha kwa Tija mazao na bidhaa za kilimo, mifugo na uvuvi ili kufikia uchumi wa kati”. Ili kufikia malengo haya; kupitia mfumo wa Taifa wa Usajili na Utambuzi wa Watu kuwatambua Wakulima na Wafugaji, uzalishaji wenye tija na ufugaji wa kisasa unawezekana. Hivyo wananchi wanahimizwa kujitokeza kwa wingi kusajiliwa ili kunufaika na manufaa mapana ya mfumo huu katika kuinua uchumi na maendeleo ya Taifa.
Maonyesho ya Nanenane Kitaifa yanafanyika kwa awamu ya Nne mkoani Lindi ili kutoa fursa pana kwa wakulima na wafugaji kunufaika na elimu pana inayotolewa na Taasisi na Mashirika mbalimbali kwa lengo la kufanikisha ndoto kubwa ya Taifa la Uchumi wa Kati.
 Mmoja wa wananchi wa Lindi akipata maelekezo toka kwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano NIDA, Bi. Rose Mdami.
 Banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa katika viwanja ya Ngongo, karibu kabisa na Jukwaa Kuu la Maonyesho.
 Baadhi ya Wananchi waliotembelea Banda la NIDA wakifuatilia maelelezo ya namna ya kujisajili toka kwa Afisa Usajili mkoa wa Lindi Ndugu Oliver Walles Mahinya.
 Kikundi cha ngoma za jadi kikitumbuiza wakati wa uzinduzi wa Maonyesho ya Nanenane Viwanja vya Ngongo Lindi.
Wananchi wa Mkoa wa Lindi waliojitokeza kushuhudia uzinduzi rasmi wa maonyesho ya Kitaifa ya Nananenane yanayofanyika mkoani humo kwenye viwanja vya Ngongo. Maonyesho ya Nanenane yaliasisiwa mwaka 1990 mkoani Mbeya na yameendelea kwa mzunguko kwa kila mkoa kupata fursa ya kuandaa na kushiriki.

MUHIMBILI KUADHIMISHA SIKU YA WAKUNGA KATIKA WIKI YA UNYONYESHAJI

Balozi wa Kuwait nchini akabidhi vifaa tiba kwa ajili ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete

$
0
0
 Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Jasen Al Najem akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa tiba kwa ajili ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete mapema hii leo jijini Dar es Salaam, katikati ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo Prof. Mohamed Janabi.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa tiba kwa ajili ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Jasen Al Najem na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo Prof. Mohamed Janabi.
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu (katikati) akikata utepe wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa tiba kwa ajili ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kulia ni Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Jasen Al Najem na kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo Prof. Mohamed Janabi.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu na Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Jasen Al Najem (katikati) wakikabidhi kwa watoto wenye matatizo ya moyo zawadi ya madaftari wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa tiba kwa ajili ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kulia ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akizungumza na baadhi ya wazazi wenye watoto wenye matatizo ya moyo wakati wa hafla ya kupokea vifaa tiba toka Ubalozi wa Kuwait kwa ajili ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kulia ni Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Jasen Al Najem. Picha na Eliphace Marwa - Maelezo

Prime Minister Kassim Majaliwa launches a Methadone Clinic at the Mbeya Zonal Referral Hospital (MZRH) in the Southern Highlands.

$
0
0
The Prime Minister, Honorable Majaliwa Kassim Majaliwa yesterday launched the Methadone Clinic at the Mbeya Zonal Referral Hospital (MZRH) in the Southern Highlands.

Launching the clinic and services for People Who Inject Drugs (PWIDs) in Mbeya, the Prime Minister commended the Mbeya Zonal Referral Hospital for launching the methadone dispensing services for heroin users in the region. 

“This is the fifth methadone clinic in the country; it is encouraging to see that the Mbeya Zonal Hospital will now, offer services to our youth who are injecting opioid drugs. Providing Opioid Substitution Therapy (OST) or Medically Assisted Treatment (MAT) is one of the HIV prevention strategies the government is working on, through the Ministry of Health in its attempts to reduce the risk factors for HIV/AIDS,” said Honorable Majaliwa.


The newly- opened methadone clinic is a gift to the people of the United Republic of Tanzania from the American People and is  financially supported by  the US Department of Defense-Walter Reed Program (WRP)/President’s Emergency Plan for AIDS Relief (PEPFAR), with technical assistance from  the US Centers for Disease Control and Prevention (CDC) .
The clinic offers Medically Assisted Treatment (MAT) for heroin injectors in Mbeya and the Southern Highlands zone in general; it is expected to serve up to 600 clients in the first 12 months of operation. 
The MAT clinic will dispense methadone as an alternative to opiate use for the heroin injectors and will also offer HIV counselling, testing and care and treatment; TB clinic services; cervical cancer screening services, STI diagnosis and treatment, and substance abuse counseling and psychosocial support. 

 The Prime Minister, Honorable Majaliwa Kassim Majaliwa  speaks at the launch of  the Methadone Clinic at the Mbeya Zonal Referral Hospital (MZRH) in the Southern Highlands. Others from right are the Commisioner General of the Drug Control and enforcement Authority Rogers William Sianga, Dr. Godlove F. Mbwanji, Director of Mbeya Zonal Referral hospital and the Deputy Speaker Dr. Tulia Ackson Mwansasu.
 (From Right to left) Dr. David Elkins, Executive Director Global Health Program Tanzania-HJFMRI, Honorable Kassim Majaliwa, the Prime Minister, Dr. Mbwanji, Director of Mbeya Zonal Referral hospital and Member of Parliament for Mbeya City Honorable Joseph Mbilinyi during the launch of Methadone clinic at the Mbeya Zonal Referral Hospital.
(From Right to left) Dr. David Elkins, Executive Director Global Health Program Tanzania-HJFMRI, Honorable Kassim Majaliwa, the Prime Minister, Dr. Mbwanji, Director of Mbeya Zonal Referral hospital and Member of Parliament for Mbeya City Honorable Joseph Mbilinyi during the launch of Methadone clinic at the Mbeya Zonal Referral Hospital. 

MICHUZI TV: SIMBA SC KUMENYANA NA RAYON SPORTS YA RWANDA SIMBA DAY - HAJI MANARA

Viewing all 109981 articles
Browse latest View live




Latest Images