Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110175 articles
Browse latest View live

NHIF YAZINDUA MPANGO WA TOTO AFYA KADI

$
0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akikata Utepe kuashiria uzinduzi wa bima ya afya ya Mtoto 'Toto Kadi' leo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema kuwa kiu yake katika sekta ya afya ni kuona kila mtu ana bima ya afya.

Waziri Ummy ameyasema hayo leo wakati wa uzinduzi wa Kadi ya Bima ya Afya kwa Mtoto ‘Toto Kadi’ , amesema kuwa taifa kuwa lina maendeleo linatokana na msingi wa afya  ambapo msingi huo unatokana  na kuwa watoto wanaopata huduma za afya kwa uhakika.

Amesema kuwa  gharama za kulipa matibabu katika ukuaji watoto na hali uchumi  ni kubwa lakini kuwepo kwa bima hiyo kutanya wazazi kuwa na  furaha wakati wote hata ikitokea ugonjwa bima ndio inamaliza matatizo.
Ummy amesema kuwa wakati  anaingia madarakani alikutana na Rais Dk. John Pombe  Magufuli  alichoendanacho ilikuwa ni kuongeza ghrarama lakini Rais alisema hakuna kuongeza ghrama yeyote cha msingi waangalie jinsi ya kusaidia watanzania kuwa na bima.

Aidha Waziri  Ummy amewaomba Mfuko wa  Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)  kuja na bima ya mama mjamzito itakayotumika wakati ujauzito na badaa ya kujifungua.

Ummy amesema kuwa kampeni hiyo iwe endelevu kwa nchi nzima ili watoto wote kuwa na bima ya afya hapo tutakuwa tunajenga taifa lenye msingi bora wa afya.Waziri  huyo ameitaka kuweka utaratibu wa kubandika mabango katika kila kumbi za starehe ili wanavyotumia vinywaji waweze kuangalia watoto kama wana kadi ya afya bima ya afya.

Nae Mwenyekiti wa Bodi NHIF, Anne Makinda amesema kuwa wanafanya kazi nguvu kuhakikisha watanzania wanapata huduma za afya  pamoja na kulipa watu wanaotoa huduma kwa bima ya afya.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akiangalia muundo wa kadi ya bima ya afya ya Mtoto mara baada ya kuzindua leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akipeana Mkono na Mwenyekiti wa Bodi wa NHIF, Anne Makinda  mara baada ya kuzindua bima  kadi ya bima ya afya kwa watoto leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akizungumza katika uzinduzi wa bima ya afya kwa mtoto katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bernad Konga akizungumza juu ya mpango wa bima ya afya ya Mtoto katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza juu ya bima ya afya kwa mtoto katika jiji la Dar es Salaam wakati uzinduzi wa bima hiyo katika viwanja vya mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI

KAMATI MAALUM YA MAKINIKIA YA TANZANIA YAANZA MAZUNGUMZO NA BARRICK GOLD CORPORATION JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0

Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati Maalum iliyoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kufanya mazungumzo na uongozi wa Barrick Gold Corporation juu ya biashara ya madini yanayochimbwa na migodi ya kampuni hiyo hapa nchini akiulaki ujumbe wa kampuni hiyo kabla ya kuanza kwa mazungumzo hayo leo tarehe 31 Julai, 2017 Jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU 
  

Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati Maalum iliyoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kufanya mazungumzo na uongozi wa Barrick Gold Corporation juu ya biashara ya madini yanayochimbwa na migodi ya kampuni hiyo hapa nchini akipata picha ya pamoja na ujumbe wa kampuni hiyo kabla ya kuanza kwa mazungumzo hayo leo tarehe 31 Julai, 2017 Jijini Dar es Salaam 
Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati Maalum iliyoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kufanya mazungumzo na uongozi wa Barrick Gold Corporation juu ya biashara ya madini yanayochimbwa na migodi ya kampuni hiyo hapa nchini akizungumza akiwa na Afisa Mwendeshaji Mkuu wa kampuni hiyo Bw. Richard Williams kabla ya kuanza kwa mazungumzo hayo leo tarehe 31 Julai, 2017 Jijini Dar es Salaam.

KAMPUNI YA PIMAK YAFUNGUA DUKA LA KUUZA VYOMBO JIJINI DAR

$
0
0
KAMPUNI ya kimataifa inayojihusisha na utengenezaji na uuzaji wa vifaa vya mbalimbali vya mapishi kwenye hoteli , PiMAK imefungua duka hapa nchini lililopo Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.

Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Ali Donmez alisema, kampuni hiyo imebainisha soko kubwa la bidhaa zake hapa ambapo imekuwa ikifanya biashara kwa muda mrefu kwa kushirikiana na mawakala, na kwa sasa licha ya kufungua duka hilo lakini bado inaona kuna fursa kubwa zaidi za uwekezaji.

Akizungumzia kuhusiana na bidhaa hizo, alisema kuwa ni bidhaa kwa ajili ya matumizi ya hoteli, migahawa na huduma kubwa za mapishi vikiwamo vya kukatia nyama, kuhokea mikate, kuoshea vyombo, kupikia na huduma nyingine za kihoteli. 

Aliongeza kampuni hiyo imeshafanya kazi hapa nchini kwa miaka minne ikishirikiana na mawakala ambapo vifaa hivyo vinatumiwa na hoteli nyingi hapa nchini, huku akiweka wazi kuwa inatoa huduma za utengenezaji wa bidhaa hizo pia. 

"Kampuni hii ina miaka 25 na makao yake makuu ni Instabul, Uturuki kwa Tanzania tumekuwapo kwa miaka minne tukifanya biashara kwa kushirikiana na mawakala lakini leo tumefungua (jana) tumefungau duka letu huku tukiwa na lengo na kuja kuanzisha kiwanda cha uundwaji wa vifaa hivi hapa hapa nchini" alisema Donmez. 

Pia alisema kuwa kampuni hiyo kwa miaka ya baadae itafungua kiwanda hapa nchini kwa lengo la kurahisha upatikanaji wa bidhaa zake kwenye soko la Afrika Mashariki na Kati na pia kuongeza ajira zaidi kwa watanzania.
Kampuni hiyo kwa sasa inafanya kazi nchi 16 na kwa hapa nchini imeshaajiria wafanyakazi 15 huku ikitoa huduma za ukarabati wa vifaa vya upishi hoteli mbalimbali nchini.
 
Mmiliki wa Kampuni ya PiMAK, Riza Ergun akikata utepe kuashiria uzinduzi wa duka la kuuza vifaa mbalimbali vya mapishi lililofunguliwa eneo la Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. 
Mmiliki wa Kampuni ya PiMAK, Riza Ergun akiwa na wadau kadhaa waliojitokeza kwenye uzinduzi huo wakisoma menu ya baadhi ya vifaa vinavyouzwa dukani hapo mara baada ya kuzinduliwa
Wafanyakazi na wageni waliojitokeza siku hiyo ya uzinduzi wa duka la kuuza vifaa mbalimbali vya mapishi wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kufunguliwa eneo la Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. 

BALOZI WA KUWAIT ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Nchini, liko katika mkakati wa kuingia ushirikiano na Serikali ya Kuwait katika shughuli zake za kukabiliana na majanga ya moto ikiwa ni juhudi zake katika kuyafikia maeneo mengi nchini. 

Akizungumza alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji jijini Dar es salaam, Balozi wa Kuwait Nchini, Jasem Al-Najem, alisema serikali ya Kuwait ipo tayari kubadilishana mafunzo na kutoa msaada wa vifaa kwa Jeshi hilo.

“Ni vema tukatengeneza mpango ambao wataalam wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kutoka nchini Tanzania wataweza kubadilishana uzoefu na wataalamu kutoka nchini Kuwait kwa ajili ya kujifunza mbinu mbalimbali za kukabiliana na majanga pindi yanapotokea, ’’ Alisema Balozi huyo.

Akizungumza wakati wa kikao hicho, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye alimshukuru kwa kumtembelea na kusema kuwa ujio wa balozi huyo, umefungua ukurasa mpya kwa upande wa misaada na mafunzo kwa Askari wa Jeshi hilo, kwani watapata fursa ya kubadilishana uzoefu na kuongeza tija kwa Jeshi lake.

“Tutapata nafasi ya kubadilishana uzoefu na kupata mafunzo kutoka Nchi ya Kuwait na kuongeza ufanisi katika majukumu yetu ya kila siku, lengo ikiwa ni kukabiliana na majanga mbalimbali yakiwemo ya moto,’’ alisema Kamishna Jenerali.

Katika kikao hicho Balozi wa Kuwait, Nasem Al-Najem alipokea taarifa ya changamoto zinazolikabili jeshi hilo ikiwemo uhaba wa vitendea kazi huku akiahidi kuzifanyia kazi na akisisitiza mchakato wa kusaini makubaliano ya hiari ukamilike kwani utakuwa msaada wa kutekeleza kwa haraka program za mafunzo ya muda mfupi.

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA HABARI NA ELIMU KWA UMMA-MAKAO MAKUU YA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye, akimkabidhi zawadi Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem (kushoto), baada ya mazungumzo na Balozi huyo alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi hilo, jjini Dar es Salaam leo. Katika Kikao hicho Balozi huyo aliahidi kushirikiana na Jeshi kubadilishana utaalamu katika masuala ya kukabiliana na majanga mbalimbali. Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye, akizungumza na Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem (Wakwanza kulia) alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi hilo jijini Dar es Salaam leo. Katika Kikao hicho Balozi huyo aliahidi kushirikiana na Jeshi hilo kubadilishana utaalamu katika masuala ya kukabiliana na majanga mbalimbali. Wengine ni Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo. Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem, akizungumza wakati wa kikao na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye (katikati) na Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo, alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi jijini Dar es Salaam leo. Katika Kikao hicho Balozi huyo aliahidi kushirikiana na Jeshi hilo kubadilishana utaalamu katika masuala ya kukabiliana na majanga mbalimbali.Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

WAUMINI WA KANISA LA EFATHA MJINI SONGEA WACHANGIA DAMU

$
0
0
Waumini wa kanisa la EFATHA MINISTRY lililopo katika manispaa ya SONGEA mkoani RUVUMA wamejitokeza kwa wingi kuchangia damu kwa watu wenye uhitaji wa damu, ambapo zoezi hilo la kuchangia limefanyika kanisani hapo. PHILIPO GUNI ni baba wa kiroho katika kanisa hilo anasema kutokana na mateso mengi wanayoyapata ndugu zetu hususani akina mama wajawazito na watu wanaopata ajali ndicho kilicho wasukuma zaidi.habari kamili hii hapa video yake

MSAFARA WA MAGARI YA KIZAMANI KUANZA ZANZIBAR

$
0
0

Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Rashid Ali Juma mwezi ujao,anatarajia kuzindua msafara wa magari ya zamani mjini humo ili kuamsha aina mpya ya utalii.

Msafara huo unatarajiwa kuanzia Hyatt Park hoteli iliyopo mjini Zanzibar na kumalizikia Melia hoteli Kiwengwa.

Waziri Juma amesema hayo leo na kuongeza kuwa lengo la safari hiyo ni kuamsha aina mpya ya utalii itakayopelekea watalii wengi kuja nchini.

Amesema magari hayo ya miaka ya 60 yalikuwa yakitumiwa na wafalme na masultani, lakini hadi leo yanaweza kutembea."Utalii unachangia pato la Zanzibar kwa asilimia 27 huku ukichangia asilimia 80 ya fedha za kigeni kwani mambo mengi ya kitalii yamekuwa ya kawaida".

Amesema kwa kushirikiana na Hyatt hoteli tumekuja na mbinu mpya ya kuwavutia watalii wengi zaidi.Amesisitiza kuwa hakutakuwa na mbio za magari bali ni msafara wa magari hayo ya zamani ambayo yatatembea umbali wa kilomita 30 na kwa kuanzia yatakuwa magari sita, matatu ya watu binafsi na matatu ya Hyatt.

Aidha amewahakikishia usalama wa kutosha katika msafara huo ambapo vyombo vya ulinzi vitakuwa vikisindikiza mwanzo mpaka mwisho wa safari.
Nae Meneja mkuu wa Hyatt hoteli Garry Friend alisema msafara huo utaanzia Hyatt park hoteli Zanzibar ukipitia mji mkongwe na kumalizikia Melia Kiwengwa Agosti 26 ambayo ndiyo siku ya ufunguzi rasmi. 

Amesema lengo la kutumia magari hayo yaliyotumika miaka ya 60 ni kusisimua utalii."Watu wengi watavutiwa na aina hii ya utalii" alisema Friend.
 Waziri wa Habari utalii Utamaduni Sanaa na Michezo Mh.Rashidi Juma Kushoto Akizungumza na Waandishi wa Habari mapema Jijini Leo
Kulia ni Meneja Mkuu wa Hyat Hotel Bwn Garry Friend

TANZANIA EXCELS IN STATISTICAL CAPACITY AMONG SUB-SAHARAN AFRICAN NATIONS, WB REPORT SHOWS

$
0
0
A graph showing Tanzania as a second country among  Sub - Saharan countries in better statistical capacity. According to the World Bank report,  Tanzania scored 90 percent for periodicity, 80 percent for source data and 50 percent for methodology which contributed to an overall of 73.3 percent. 

Tanzania has been ranked second, behind South Africa in statistical capacity among Sub-Saharan African nations. 
This is according to the World Bank (WB) 2016 Statistical Capacity Indicator (SCI). 
WB has been assessing national statistical capacity in developing countries since 2004 and has produced overall SCI score as well as scores for three categories, Methodology, Source Data and Periodicity. Regional overall and specific category SCI are also produced to allow for comparison.

For every dimension, a country is scored against specific criteria, using information available from the WB, IMF, UN, UNESCO, and WHO. 

A composite score for each dimension and an overall score combining all three dimensions are derived for each country on a scale of 0 - 100. A score of 100 indicates that the country meets all the criteria. 

FORE MORE NEWS CLICK HERE


TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI YAITAHADHARISHA CUF

$
0
0
Na Margareth Chambiri, NEC

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imekishauri Chama cha Wananchi (CUF) kumaliza mgogoro unaoendelea ndani ya Chama hicho kwani unaweza kusababisha kupoteza nafasi za Udiwani katika Uchaguzi Mdogo unaotarajiwa kufanyika wakato wowote kuanzia sasa.

Tahadhari hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume hiyo Bw. Kailima Ramadhani katika mahojiano maalum Ofisini kwake kuhusu tuhuma  mbalimbali zilizoelekezwa Tume hiyo ikiwemo suala la Uteuzi wa Wabunge wa Viti Maalum kupitia CUF.
Bw. Kailima amesema mvutano unaoendelea ndani ya Chama cha Wananchi (CUF) hauna tija, hivyo ameshauri pande mbili zinazovutana kukutana na kumaliza tofauti zao kwani hali hiyo itawanyima nafasi ya kutoa wagombea kwenye uchaguzi huo mdogo.

 ‘Mimi niwashauri, CUF wana mgogoro wao wamalize mgogoro wao. Ni vizuri wakutane wamalize mgogoro wao kwani hii inaweza kuwaletea matatizo wagombea wakati wa Uchaguzi.’ alisesema Kailima na kusisitiza kuwa mgogoro ndani ya chama hicho hauna tija na badala yake unakidhoofisha. 

Amesema Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, inakitaka Chama cha Siasa kumsimamisha Mgombea mmoja kwa nafasi moja, lakini pia mgombea wa nafasi ya Rais na Mbunge  lazima fomu yake isainiwe na Viongozi wa ngazi ya Taifa wanaotambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa.

‘Lakini ukisoma Maelekezo ya Vyama vya Siasa na Wagombea yanasema iwapo chama cha Siasa kina mgogoro ni lazima fomu zake zisainiwa na kiongozi wa juu wa ngazi ya Mkoa, sasa kwa hali hii iwapo CUF wasipokutana watapoteza nafasi.’ Amesema Mkurugenzi huyo wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.  

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

VIJIJI VYOTE KUWA NA UMEME IFIKAPO 2021 –DKT. KALEMANI

$
0
0
Na Tiganya Vincent
Serikali imesema kuwa jumla ya vijiji 7873 na vitongoji vyake vyote hapa nchini vitakuwa vimeshaunganisha na umeme chini ya Mradi wa Umeme Vijijini Awamu wa Tatu ifikapo mwaka 2021.

Kauli hiyo imetolewa jana mjini Tabora  na Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani wakati alipomtembelea Mkuu wa Mkoa wa Tabora Bw. Aggrey Mwanri.
Dkt. Kalemani alisema REA III itasaidia kukamilisha vijiji vilivyobaki ambavyo havijaunganishwa na umeme ifikapo mwaka 2021 kwa ajili ya kuchochea maendeleo ya uchumi kati kuelekea uchumi wa viwanda.
Alisema kuwa lengo la Serikali ni kutaka wananchi wote hata wale wanaoishi visiwani waweze kufikiwa na huduma ya umeme kwa ajili ya matumizi yao na kwa ajili ya uendeshaji wa viwanda.
Aidha kwa upande wa Mkoa wa Tabora alisema vijiji vipatavyo 510 na vitongoji vyake vinatarajiwa kuwa vimeshaunganishwa na umeme wa uhakika wa ifikapo mwaka 2021 kupitia mradi wa REA III.
Aliongeza kuwa ili kuhakikisha lengo hilo la kuunganisha vijiji vyote vinakuwa na umeme, Serikali imeamua kuweka Wakandarasi wengi katika kila mradi na kuwaagiza kugawa kazi kwa Wakandarasi wadogo ambao ni wazawa na wenye sifa ili kurahisisha kazi na kuifanya iwe na ufanisi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

RAIS DK.SHEIN AZUNGUMZA NA UONGOZI BODI SHIRILA LA MELI,BANDARI NA MAMLAKA YA USAFIRI BAHARIN

$
0
0
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji pamoja na Uongozi wa Bodi ya Wakurugenzi  wa Mamlaka ya Usafirishaji Baharini na Uongozi wa Mamlaka ya Usafirishaji  Baharini katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji pamoja na Uongozi wa Bodi ya Wakurugenzi  ya Shirika la Meli na Uongozi wa Shirika la Meli Zanzibar katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo.
 Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi  ya Shirika la Meli na Uongozi wa Shirika la Meli Zanziba wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji pamoja na Bodi hiyo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo (Picha na Ikulu).

KATIBU MKUU SIHABA NKINGA AHIMIZA WAKUU WA VYUO VYA MAENDELEO YA JAMII NCHINI KUZINGATIA SHERIA, KANUNI NA TARATIBU KATIKA UTENDAJI WAO WA KAZI.

Taarifa ya Raia 16 waliodaiwa kupita katika Jengo la VIP kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA).

VIONGOZI TUMSAIDIE RAIS KUTATUA KERO - JAJI WARIOBA

$
0
0
Na Judith Mhina – MAELEZO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, anahitaji kupata usaidizi wa kutosha kutoka kwa viongozi na hasa wasaidizi  kuanzia ngazi ya nyumba kumi hadi taifa.
Maneno hayo yametamkwa na Waziri Mkuu mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba alipofanya mahojiano na Idara ya Habari – MAELEZO - ofisini kwake Oysterbay Jijini Dar-es-Salaam.

Jaji Warioba ameona kuna udhaifu mkubwa wa kiutendaji ambapo wananchi hawatoi changamoto zinazowakabili mpaka wamuone Rais amefika katika eneo lao, au wanaeleza changamoto zinazowakabili kwa viongozi husika ila, viongozi hawazifanyii kazi, ambapo wananchi wanaamua kuziwasilisha kwa Rais mara wanapomuona.

 “Rais hawezi kufanya kazi peke yake naomba tuimarishe utendaji wetu wa kazi, kama utendaji ungekuwa mzuri suala la makontena kufika hadi bandarini lisingekuwepo, na hata kugundulika kwake kusingefanywa na Rais,” amesema Jaji Warioba.


“Nampongeza sana Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan na  Waziri Mkuu  Kassim Majaliwa, kwa utendaji wao wa kazi. Viongozi hawa ni wasikivu na wanatekeleza kazi zao bila mihemko kwa kutoa maagizo na maelekezo kwa wahusika ili wayatekeleze”, aliongeza  Mhe. Warioba.

WAZIRI DKT. MAHIGA AKUTANA NA MCHUNGAJI ONGERE NA BALOZI WA IRAN NCHINI

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akisalimiana na Mchungaji John Oscar Ongere ambaye alifika ofisini kwa Mhe. Waziri kujadili maandalizi ya Kongamano kubwa la uwekezaji linalotarajiwa kufanyika nchini mwezi Novemba 2017. Kongamano hilo litakalofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam litajumuiya wafanyabiashara wakubwa kutoka kote duniani na wa hapa nchini kujadiliana namna bora ya kutumia fursa lukuki za uwekezaji zilizopo hapa nchini.

Mchungaji Ongere akifanya maombi kwa ajili ya kuiombea nchi amani na utulivu ili iweze kukua kiuchumi
Picha ya pamoja
 Balozi wa Iran
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mhe. Mousa Farhang ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo.  Mazungumzo yao pamoja na mambo mengine walijadili maandalizi ya sherehe za kumuapisha Rais Mteule wa Iran, Mhe. Hassan Rouhani zitakazofanyika Tehran tarehe 05 August 2017.

Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia mazungumzo hayo, Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Bi. Zainab Angovi-Mrutu, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Bw Ayoub Mndeme na Katibu wa Waziri, Bw. Gerald Mbwafu.

Ujumbe aliofuatana nao Balozi wa Iran ukifuatilia mazungumzo.

HALMASHAURI YA MJI NJOMBE YANG’ARA KWA HATI SAFI RIPOTI YA CAG, IDARA ZAASWA KUTOKIONA KITENGO CHA UKAGUZI WA NDANI KAMA MWIBA WA PORI.

$
0
0
Na Hyasinta Kissima, Njombe

Halmashauri ya Mji Njombe imerudisha heshima yake kwa kupata Hati safi katika ripoti ya mthibiti na mkaguzi wa serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2015/2016) ambapo kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Halmashauri hiyo ilipata hati inayoridhisha na yenye maswala ya msisitizo.

Akitoa mapendekezo yake wakati wa Mkutano Maalumu wa Baraza la Madiwani la kujadili hoja za Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Katibu Tawala Mkoa wa Njombe  Jackson Saitabahu ameipongeza Halmashauri kwa kupata hati safi na kwa kukusanya mapato kwa asilimia 100.1 na amezitaka idara na vitengo vya Halmashauri kutoona Ofisi ya Ukaguzi wa ndani kama mwiba wa pori na mahali pasipoingilika kwani Kitengo hicho kipo kwa ajili ya kutoa ushauri lakini pia kuiandaa Halmashauri kwa Ukaguzi Mkuu hivyo wasisite kuomba ushauri pale inapobidi.

“Hati safi haiji kwa bahati mbaya, napenda niwapongeze kwa jitihada kubwa mlizoonyesha lakini pia niwasihi sana msikwepe Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, Kitengo hiki kinatakiwa kiwezeshwe vizuri na Halmashauri ijenge mahusiano mazuri na Kitengo cha Ukaguzi kwani wakaguzi wa ndani ndio wanatuandaa kwa ajili ya ukaguzi wa nje.Tunapoimarisha mahusiano mazuri miongoni mwetu hatutakua na hoja za ukaguzi.Tusiwe mabingwa wa kujibu hoja zaidi ya kuwa wataalamu wa kuzuia hoja zisitokee.”Alisema Katibu Tawala.

Sambamba na hilo Halmashauri pia imeendelea kuimarika kwa kufikia asilimia 35% za kuweza kujitegemea jambo ambalo limeendelea kuifanya Halmashauri ya Mji Njombe kufanya vizuri katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

Kwa mwaka 2017/2018 Halmashauri imejipanga kuhakikisha kuwa hoja zote zinafungwa, kukusanya mapato zaidi ya mwaka uliopita na kuhakikisha kuwa Halmashauri haitoruhusu kufanya biashara na Wakandarasi na wazabuni wasio na mashine za kielektroniki na kuhakikisha kuwa nyaraka na kumbukumbu zote za manunuzi zinatunzwa ipasavyo.

 Mweka Hazina wa Halmashauri ya Mji Njombe Dorcas Mkello akiwasilisha hoja za ukaguzi mbele ya Mkutano Maalumu wa  Baraza Kuu la Madiwani.
 Wakuu wa Idara na Vitengo Halmashauri ya Mji Njombe wakisikiliza kwa Makini mapendekezo ya Baraza la Madiwani.
 Katibu Tawala Mkoa wa Njombe Jackson Saitabahu akitoa mapendekezo yake mara baada ya kupitia hoja za ukaguzi.
Madiwani wakipitia makabrasha yenye hoja za Ukaguzi.

INTRODUCING "NGA'RI NG'ARI: BY FATMA

MAWAZIRI WATANO WA TANZANIA NA UGANDA WAFANYA ZIARA MPAKANI MWA NCHI HIZO

$
0
0
Mawaziri watano wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania watembelea mpaka wa Tanzania na Uganda ili kutatua changamoto zinazoukabili mpaka huo na kuuboresha.
Mawaziri hao ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Masauni, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Suleman Jaffo, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Suzan Kolimba na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe.
Miongoni mwa maeneo yaliyotembelewa na Mawaziri hao ni eneo la mpaka ya Tanzania na Uganda kwa upande unapo pita mto Kagera na eneo la kivuko cha mpaka wa Tanzania na Uganda kilichopo Mtukula mkoani Kagera.
Katika ziara hii Mawaziri hao wameweza kujionea hali halisi ya maisha ya wakazi wa mipakani na jinsi wanavyohusiana na wenzao wa nchi ya jirani ya Uganda ambapo wamekuwa wakishirikiana na kuishi kwa amani katika shughuli zao za kila siku.Aidha, ziara hii ni maandalizi ya Mkutano wa ujirani mwema kati ya Mawaziri wa serikali ya Uganda na Mawaziri kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao unatarajiwa kufanyika mnamo tarehe 29 Julai 2017, Bukoba mkoani Kagera.

NMB YAZINDUWA SIKU YA WALIMU MKOANI DODOMA

$
0
0
Afisa Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Bi. Rehema Madenge akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma (wa kwanza kulia) akifurahi pamoja na maofisa wa Benki ya NMB mara baada ya uzinduzi rasmi wa hafla ya siku ya walimu katika Mkoa wa Dodoma. Hafla ya uzinduzi wa siku ya Mwalimu ilifanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya hazini jijini Dodoma.

BENKI ya NMB imezindua rasmi siku ya walimu katika Mkoa wa Dodoma. Uzinduzi huo wa siku ya walimu Mkoa wa Dodoma ulizinduliwa rasmi na Afisa Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Bi. Rehema Madenge akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Bw. Jordan Rugimbana. Hafla hii adhimu ilifanyika katika ukumbi wa Hazina na kuhudhuliwa na zaidi ya walimu 200 wa mkoa huo mwishoni mwa wiki. Uzinduzi wa hafla hii ni miongoni mwa mikakati ya NMB ya kuwafikia walimu nchini kote. Kusudi kubwa la hafla hiyo ya NMB na Walimu ni kuwaongezea uelewa walimu juu ya huduma za benki. Hii ni kutokana na umuhimu wa kundi hili kubwa katika jamii inayotuzunguka. 

NMB wanaimani kwamba mwalimu akielimika jamii nzima itakua imepata elimu ya huduma za kifedha. Lakini pia kwa kuzingatia ukubwa wa kundi hili NMB imekua ikitumia fursa hii kupokea mrejesho ya jinsi huduma za kibenki zinavyopokelewa na wateja wake. Akizungumza wakati wa hafla hiyo mjini Dodoma, Meneja mwandamizi wa wateja binafsi wa NMB, Omari Mtiga alisema NMB inazo huduma mbalimbali ambazo kusudi lake kubwa ni kumsaidia mteja aweze kujikwamua kiuchumi. 

Aliongeza kuwa zipo huduma za mikopo ya aina mbalimbali ambapo walimu wanaweza kunufaika nayo. Mikopo ambayo inatolewa na Benki ya NMB sio kwa ajili ya wafanyabiashara tu bali ni kwa ajili ya kila mtu mwenye vigezo vya kukopeshwa ambapo walimu ni miongoni mwa walengwa wa mikopo hii. Msichukue mkopo benki kama hamna mipango thabiti ya matumizi ya mkopo huo, Ni vyema kuchukua mkopo benki ukiwa na mipango endelevu," alisema Bw. Omari Mtiga. 

"...Tukiwa kwenye mikakati ya serikali ya Viwanda ni vyema mkatumia vizuri maonyesho ya Nane nane yanayotarajiwa kuanza kutembelea mabanda ambayo mtajifunza namna ya uwekezaji kwenye sekta viwanda ili kujikwamua kiuchumi kwa kutumia uwepo wa benki ya NMB kwenye jamii yetu bila kuathiri mwenendo wa jaira zetu. Alisema kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Bi. Rehema Madenge katika hafla hiyo. 
Mkuu wa Kitengo cha wateja binafsi wa NMB, Bw. Omari Mtiga (kushoto) akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa siku ya Mwalimu katika mkoa wa Dodoma mwishoni mwa wiki. Sehemu ya walimu waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa siku ya walimu mkoa wa Dodoma.
Picha za kumbukumbu na Sehemu ya walimu pamoja na Afisa Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Bi. Rehema Madenge.

TANZANIA EXCELS IN STATISTICAL CAPACITY AMONG SUB-SAHARAN AFRICAN NATIONS, WB REPORT SHOWS

$
0
0
By Veronica Kazimoto, Dar es Salaam

Tanzania has been ranked second, behind South Africa in statistical capacity among Sub-Saharan African nations. This is according to the World Bank (WB) 2016 Statistical Capacity Indicator (SCI).

WB has been assessing national statistical capacity in developing countries since 2004 and has produced overall SCI score as well as scores for three categories, Methodology, Source Data and Periodicity. Regional overall and specific category SCI are also produced to allow for comparison.

For every dimension, a country is scored against specific criteria, using information available from the WB, IMF, UN, UNESCO, and WHO.

A composite score for each dimension and an overall score combining all three dimensions are derived for each country on a scale of 0 - 100. A score of 100 indicates that the country meets all the criteria.

The statistical methodology aspect measures a country’s ability to adhere to internationally recommended standards and methods, by assessing guidelines and procedures used to compile macroeconomic statistics and social data reporting and estimation practices by looking at an updated national accounts base year, use of the latest Balance of payment, external debt reporting and IMF’s Special Data Dissemination Standard and enrolment data reporting to UNESCO.

On source data, this measures data collection activities in line with internationally recommended periodicity, and whether data from administrative systems are available and reliable for statistical estimation purposes and periodicity of population and agricultural censuses, the periodicity of poverty and health related surveys, and completeness of vital registration system coverage.

The third aspect concerned with the periodicity and timeliness looks at the availability and periodicity of key socio-economic indicators of which nine are MDG indicators.

Tanzania scored 90 percent for periodicity, 80 percent for source data and 50 percent for methodology which, contributed to an overall SCI of 73.3 percent. Although this overall score ranks Tanzania as second behind South Africa (82.2%) there is still room for improvements, especially in methodology.

The National Bureau of Statistics (NBS) is committed to continuing strengthening of the National Statistical System.
A graph showing Tanzania as a second country among Sub - Saharan countries in better statistical capacity. According to the World Bank report, Tanzania scored 90 percent for periodicity, 80 percent for source data and 50 percent for methodology which contributed to an overall of 73.3 percent.

OLD SCHOOL REUNION USIPIME WIKI 4 TU ZIMEBAKI COLUMBUS OHIO KIMATAIFA ZAIDI

$
0
0

RATIBA KAMILI NI KAMA IFUATAVYO
Ijumaa Sept 1, 2017

Kuanzia saa 3 usiku ni Africa Night chini ya DJ Burundi na kutakua na onyesho la mavazi kutoka kwa Missy T na Asya Idarous Khamsin anuani ni

4257 Eastland Square Dr,
Columbus, OH 43243

Jumamosi Sept 2, 2017
Kuanzia saa 8 mchana ni BONANZA la mpira wa kikapu kutoka kwa vijana wa Pazi, Vijana, Don Bosco na kwengineko anuani ni
6615 Dublin center Dr,
Dublin, OH 43017

Jumamosi Sept 2, 2017
kuanzia saa 12 jioni ni mechi ya Simba na Yanga itakayokua na wachezaji waliocheza ligi kuu Tanzania anuani ni
Avery Park,
7501 Avery Rd,
Dublin, OH
43017

Na baadae kuanzia saa 3 usiku ni Old School Reunion chini na Ma DJ bora North America DJ Dennis (Funky House) na The Mix Master DJ Luke Joe anuani ni 4257 Eastland Square Dr
Columbus, OH 43243

Jumapili Sept 3, 2017 
kuanzia saa 12 jioni
NYAMA CHOMA anuani 
Avery Park,
7501 Avery Rd,
Dublin, OH
43017

Na baadae kuanzia saa 3 usiku ni usiku wa Reggae anuani ni 
4257 Eastland Square Dr,
Columbus, OH 43243

MISOSI NA VINYWAJI VYAKUMWAGA

Viewing all 110175 articles
Browse latest View live




Latest Images