Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109979 articles
Browse latest View live

WAZIRI MKUU AWAASA WATUMISHI WANAOFANYAKAZI VIWANDANI

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewasihi Watanzania wanaofanya kazi katika viwanda mbalimbali nchini kufanya kazi kwa bidii na kuwa waaminifu. 
Amesema Tanzania imedhamiria kukuza uchumi wake kupitia sekta ya viwanda hivyo ni vema watakaopata fursa ya ajira katika viwanda hivyo kuwa waadilifu.
Ameyasema hayo leo (Jumapili, Julai 30, 2017) wakati akizungumza na wafanyakazi wa kiwanda cha gesi cha Ikama kilichoko wilayani Rungwe. Waziri Mkuu amesema wakati Serikali ikiendelea kuwakaribisha wawekezaji nchini, wananchi walioajiriwa kwenye maeneo hayo wawe waaminifu.
“Mnatakiwa muwe waaminifu, msibebe kitu chochote ndani ya kiwanda bila ya ridhaa ya wamiliki kwa kuwa mtaonyesha taswira mbaya kwa wawekezaji.” Amesema uaminifu wao ndio utawezesha Watanzania wengi kupata ajira kwenye viwanda hivyo ambavyo vimejengwa katika maeneo yao.
Awali, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa kiwanda hicho kinachomilikiwa na kampuni ya TOL Gases, Mhandisi Harold Temu alisema kiwanda kinauwezo wa kuzalisha tani 46 kwa siku. Alisema gesi inayozalishwa kiwandani hapo ni ya Carbon Dioxide ambayo inauzwa nchini na nchi jirani za Zambia, Malawi, Zimbabwe na Congo.
Mhandisi Temu alisema wateja wakubwa wa gesi hiyo ni viwanda vya kutengenezea soda, bia na pia hutumika katika kuhifadhia chakula na kwenye vifaa vya kuzimia moto. Mapema Waziri Mkuu alitembelea kiwanda cha kuchakata majani ya chai cha Katumba, ambapo alisema Serikali inaimarisha Ushirika wa zao hili ili wakulima waweze kupata tija. 

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi wa umma wa wilaya ya Rungwe Julai 30, 2017. Kulia ni Naibu Spika, Dkt. Tulia Ackson na kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makalla. 
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akitembelea kiwanda cha chai cha Katumba wilayani Rungwe Julai 30, 2017. Kulia ni Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makalla na kushoto ni Meneja Uzalishaji wa kiwanda hicho, Bw. Ramadhani Kampasili. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akitazama chai iliyosindikwa na kufungashwa tayari kwa kuuzwa wakati alipotembelea kwianda cha chai cha Katumba wilayani Rungwe Julai 30, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Ufundi, Bw. McJohn Mbiri (kulia Kwake) kuhusu mitambo ya kuzaisha gesi ya hewa ya ukaa wakati alipotembelea kiwanda cha TOL Limited kilichopo katika kijiji cha Ikama wilayani Rungwe Julai 30, 2017. Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,  Mhe. Amos Makalla. 
Sehemu ya watumishi wa umma wa wilaya ya Rungwe wakimsikiliza Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa alipozungumza nao leo Julai 30, 2017. 

(Picha na Ofisi ya Waziri ) 


MAGAZETI YA JUMATATU LEO JULAI 31,2017

NIC NDANI YA MAONESHO YA 12 YA TUME YA VYUO VIKUU TANZANIA MWISHONI MWA WIKI

$
0
0
Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es Salaam, wakipewa maelezo na Afisa Mwanadamizi wa Shirikala Bima la Taifa(NIC) Konjeta Mwaipopo juu ya namna ya kujiunga na huduma za bima wakati walipotemblea banda la Shirika hilo, kwenye maonesho ya 12 ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) yaliyomalizika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Mkazi wa Dar es Salaam, ambaye ni mjasiriamali Manoko Marikishua (kushoto) akipewa maelezo na Afisa Bima wa shirika la Bima la Taifa (NIC)) juu ya bima ya mazao wakati alipofika kwenye banda la Shirika hilo, kwenye maonesho ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) yaliyomalizika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.
Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam,wakipata maelezo juu ya huduma za bima toka kwa Afisa Bima wa Shirikala Bima la Taifa (NIC)) wakati walipofika kwenye banda la Shirika hilo, kwenye maonesho ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania yaliyomalizika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam 

MBUNGE GULAMALI AFANYA ZIARA YA KUONA MAENDELEO YA UFUFUAJI WA KIWANDA CHA MANONGA GENERY

$
0
0

NA RAYMOND URIO.

Mbunge wa Jimbo la Manonga kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Seif Khamis Gulamali  jana ametembelea kiwanda cha Manonga Ginery kinachohusika na kutengeneza pamba, kilichokuwa kimesimama kwa takribani miaka ishirini (20) bila ya kufanya.

Mapema leo hii Mbunge Gulamali aliwasili katika eneo la kiwanda hicho, iliyopo Jimbo la Igunga Kata ya Choma akiwa pamoja na Mmiliki wa kiwanda hicho, ndugu Urvesh Rajan pamoja na viongozi wa Serikali za mitaa, wahandisi na mafundi wa viwanda.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutembelea na kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hicho ili kianze kufanya kazi upya, baada ya kukaa kwa miaka kadhaa bila ya kufanya kazi, Mbunge Gulamali alisema, leo nimekuja kuoana maendeleo ya kufufuliwa wa kiwanda hichi ikiwa ni sehemu ya kutaka kutimiza tena ahadi yangu niliyo itoa kwa wanachi wa Igunga na Manonga kwamba lazima kiwanda cha Manonga Ginery, kianze kazi ili wananchi waweze kunufaika katika zao biashara ya pamba na wengine kupata ajira kwa kuendesha maisha na kukuza uchumi wa viwanda nchini.

" Leo nimekuja kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hichi ikiwa ni sehemu yangu ya ahadi niliyo itoa kwa wananchi wangu wa jimbo la Manonga pamoja na Igunga kwamba lazima kiwanda hiki kifanye kazi tena, ili biashara ya zao la pamba lirudi tena na wananchi na waweze kupata ajira katika kiwanda hichi pia kukuza uchumi wa nchi ya Viwanda.

" Kufufuliwa kwa kiwanda hiki ni fursa kubwa ya maendeleo kwa jamii ya wana Igunga na Manonga na hasa wakulima wa zao la pamba hata kwa wananchi wanao lilia ajira, hivyo fursa kwa sasa iko wazi, alisema Gulamali.
 Mmiliki wa kiwanda cha Manonga Genery, Urvesh Rajan akizugumza na Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali (katikati), alipotembelea kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hicho jana Wilayani Igunga kata ya Choma. Kushoto ni Mwenyekiti wa Igombensabo Lazaro Ngullo .
 Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali akipewa moja ya maelezo ya mashine ya ya zao la pamba ndani ya kiwanda cha Manonga Genery,jana alipotembelea kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hicho kilichopo Wilayani Igunga kata Choma.
 Mmiliki wa kiwanda cha Manonga Genery, Urvesh Rajan akimpa maelekezo Mbunge wa Manonga Seif Khamis Gulamali ndani ya kiwanda hicho (katikati), jana alipotembelea na kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda kilichopo Wilaya ya Igunga kata ya Choma.
 Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali (kushoto) akizungumza na Mwenyekiti wa Igombensabo.
 Mbunge wa Jimbo la Manonga, Seif Khamis Gulamali akiongozana na viongozi wa serikali pamoja na wahandisi alipotembelea kiwanda hicho jana kilichopo Wilayani Igunga kata ya Choma.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

UNCDF YAWEZESHA UFUGAJI SAMAKI KIBIASHARA BWAWA LA KALEMAWE

$
0
0
ERIKALI ya Tanzania, imeshukuru Mfuko wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNCDF) kwa kuwezesha watanzania kupambana na umaskini kupitia miradi wanayoidhamini au kuitafutia fedha. Kwa miongo miwili UNCDF imekuwa ikifanya kazi kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia ofisi ya rais Tawala za Mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) katika mpango wa kupeleka madaraka kwa umma na shughuli za maendeleo ya kiuchumi . 

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhandisi Mussa Iyombe katika hotuba yake iliyosomwa na Katibu Tawala wa mkoa wa Kilimanjaro Aisha Amour kwenye ufunguzi wa kongamano la siku 2 la Wadau wa Ufugaji Samaki Kibiashara Bwawa la Kalemawe lililoko wilaya ya Same mwishoni mwa wiki.

“Tunafurahishwa kwa namna ya pekee na UNCDF kwa jitihada zake zinazoendeshwa kupitia katika Mpango wa Ufadhili Miradi ya kiuchumi (LFI),” alisema Iyombe na kuongeza: “Tunapokutana hapa tunapewa fursa na kufunuliwa uzoefu wa ushiriki wa UNCDF katika miradi mbalimbali, safari hii tukishuhudia hatua yake ya kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Same katika Mkoa wa Kilimanjaro.” Meneja wa Shamba la Samaki la Ruvu, Khambo Kanthenga (kulia) akitoa maelezo kuhusu mradi wa ufugaji samaki katika shamba hilo kwa viongozi mbalimbali wa Serikali wa wilaya ya Same na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) waliofanya ziara fupi ya mafunzo juu ya ufugaji wa samaki kibiashara katika shamba hilo lililopo wilaya ya Bagamoyo. Kushoto ni mbunge wa Jimbo la Same Mashariki, Mh. Naghenjwa Kaboyoka na Watatu kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Same, Rosemary Staki pamoja na Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Mitaji ya Maendeleo (UNCDF)-Tanzania, Peter Malika (wa pili kulia).

 Pamoja na kushukuru kwa hatua mbalimbali zilizofikiwa na taasisi hiyo katika kusaidia watanzania, aliwataka wakazi wa Same kuhakikisha kwamba mradi huo ulioundiwa kampuni ili kwenda kibiashara unafanikiwa na kuwa mfano kwa wengine. Halmashauri ya wilaya ya Same, na jamii inayozunguka bwawa la Kalemawe wanashirikiana na UNCDF kuboresha miundo mbinu ya bwawa hilo na kuwezesha uwapo wa uwekezaji kwa kuanzisha kampuni. 

Kampuni hiyo iliyosajiliwa ya Kalemawe Dam Investment Limited katika mpango maalum (SPV) inamilikiwa na wadau mbalimbali ikiwemo Halmashauri ya wilaya ya Same, halmashauri ya vijiji sita, wakala wa serikali, watu binafsi pamoja na makundi ya kijamii. Kuwapo kwa kampuni hiyo ni juhudi zinazofanywa za kuwezesha uhusiano mahsusi wa kibiashara unaohusisha ubia wa Serikali, Binafsi na jamii (PPCP) kwa kutoa umiliki linganifu mpaka katika ngazi za chini za mamlaka za kijiji, ambazo kimsingi ndizo wamiliki wa maliasili muhimu ya ardhi kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi ya Vijiji ya Mwaka 1999. Viongozi mbalimbali wa Serikali wa wilaya ya Same na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) wakiwa kwenye ziara fupi ya mafunzo kuhusu ufugaji wa samaki kibiashara katika shamba la ufugaji samaki la Ruvu lililopo wilaya ya Bagamoyo.

Mradi huo wa Ufugaji wa Samaki Kibiashara wa Bwawa la Kalemawe ni zao la ushirikiano kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Same, Kata za Ndungu na Kalemawe, asasi zisizo za kiserikali na wadau wa maendeleo walioazimia kukarabati na kufufua bwawa hilo na mfumo wake wa kilimo cha umwagiliaji. UNCDF kwa kushirikiana na wabia wake waitwao Mikono Tayari (ambao ni kundi linaloundwa na washirika kutoka Tanzania na Norway) ni wataalamu katika mradi hu wa ufugaji samaki kwa pamoja na SPV ya Same na washirika wake. 

Katika kongamano hilo Mkuu wa wilaya ya Same Rosemary Staki amesema wilaya yake ipo tayari kutekeleza mradi huo ambao una manufaa makubwa si tu kwa watu wa Kalemawe na vijiji vinavyozunguka bali pia na halmashauri ya wilaya ya Same. Meneja wa Shamba la Samaki la Ruvu, Khambo Kanthenga (kulia) akitoa maelezo kuhusu vyakula vinavyotumika kulisha samaki wanaofugwa kwenye shamba hilo kwa viongozi mbalimbali wa Serikali wa wilaya ya Same na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) waliofanya ziara fupi ya mafunzo juu ya ufugaji wa samaki kibiashara katika shamba hilo lililopo wilaya ya Bagamoyo.

RC Rukwa aagiza operesheni ya usafi wa vyoo wilaya nzima

$
0
0
Mwezi mmoja uliopita Wilaya hiyo ilikumbwa na ugonjwa wa kipindupindu na kuua mtu mmoja na kuwaacha wengine ishirini katika hali mbaya jambo ambalo serikali haitaki ijirudie.

“Juzi hapa kulitokea kipindupindu kule Kijiji cha Samazi, hapana hatutaki watu wafe kwa kipindupindu, sasa nimeona choo kinamwaga maji machafu kinyesi kinatoka nje bata wanapokea wanakula, hatupo salama,” Alimalizia.

Pamoja na hayo Mh. Zelote alisisita kuwa usafi ni wa kila siku si lazima kusubiri jumamosi ya mwisho wa mwezi na kueleza kuwa siku hiyo imewekwa maalum ili kuwakumbusha wananchi kuwa wanahitajika kufanya usafi maeneo wanayofanyia biashara pia na kuwa usafi ni muhimu. 
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen amemuagiza afisa afya wa wilaya ya Kalambo kuhakikisha anakagua usafi wa vyoo na maeneo yanayo zunguka nyumba kwa wilaya nzima ili kujiepusha na ugonjwa wa Kipindupindu katika Wilaya hiyo.
 Ametoa agizo hilo katika mkutano na wananchi siku ya usafi wa mwisho wa mwezi maarufu kama “Magufuli Day” baada ya Mkuu huyo kukagua nyumba 12, maduka ya wafanyabiashara pamoja na soko katika makao makuu ya wilaya hiyo huku nia ikiwa ni kutaka kujua hali ilivyo wanakojisaidia, wanakohifadhi taka pamoja na hali ya upatikanaji wa maji katika eneo hilo.
 Katika ukaguzi huo amebaini kuwa wananchi wengi husafisha nje ya nyumba tu huku nyuma ya majumba yao hali ikiwa mbaya jambo ambalo hupelekea kuibuka kwa kipindupindu na kuisababishia serikali kuwa katika wakati mgumu kwa magonjwa ambayo yanaweza kuzuilika endapo usafi utazingatiwa.
 “Leo nilipenda nione usafi wa matai, nimeuona na nimetoa “marks” 60, Nimepita karibu maeneo mbali mbali, usafi mnaoufanya ni wakuficha uchadu kidogo, huku mbele kusafi lakini nyuma kuchafu sana, nawaomba hilo mlirekebishe” Alisema.

Pia aliishauri halmashauri hiyo ya kalambo kuweza kusimamia sharia za usafi zilizopo bila ya huruma ili kuleta mabadiliko na kuitaka halmashauri hiyo kutenga fedha za makusanyo ya ushuru ili kuweza kuboresha hali ya usafi katika mji huo.

MCHENGA YATINGA FAINALI SPRITE BBAAL KINGS, KURASINI VS TMT MBABE KUPATIKANA KESHO

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii


TIMU ya mpira wa Kikapu ya Mchenga Bball Stars imefanikiwa kuingia hatua ya fainali moja kwa moja baada ya kutoka na ushindi katika mchezo wa pili wa nusu fainali kwa kuinyuka Flying Dribblers vikapu 114 dhidi ya 52.

Katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya Sprite Bball Kings 2017, Mchenga walifanikiwa kutoka na ushindi wa vikapu 119 dhidi ya 70 vya Flying Dribblers na kupelekea Mchenga kwenda hatua ya fainali baada ya kuibuka kidedea katika michezo miwil baina ya mitatu.

Michuano hiyo ya Sprite Bball Kings 2017 inayoendelea katika viwanja vya Don Bosco Oysterbay ilizikutanisha timu nyingine katika mchezo wa pili wa nusu fainali baina ya Kurasini Heat dhidi ya TMT.

Kutokana na ushindi wa TMT wa mchezo wa pili kwa kuibuka kidedea kwa kuwabamiza Kurasini Heat vikapu 92 dhidi ya 61 huku katika mchezo wa kwanza Kurasini Heat wakiibuka kidedea kwa kushinda alama za vikapu 87 kwa 80.

Mchezo wa nusu fainali ya tatu ili kuweza kumpata mshindi atakayeungana na Mchenga katika hatua ya fainali, mchezo huo utapigwa siku ya Kesho katika Viwanja vya Don Bosco.

Fainali ya mchezo huo inatarajiwa kuanza siku ya Jumamosi katika Uwanja wa Ndani wa Taifa ikichezwa katika hatua tano ili kuweza kumpata bingwa wa Sprite Bball Kings 2017 na kuondoka na kitita cha Milion 10 huku mshindi wa pili akichukua Milion 3 na mchezaji bora wa Mashindano (MVP) akijinyakulia milion 2.

 Mpambano baina ya Mchenga (Nyeupe) dhidi ya Flying Dribblers (Bluu) ulimalizika kwa Mchenga kuingia katika hatua ya fainali baada ya kuibuka na ushindi aktika michezo miwili ya nusu faimali ikiwa inazisubiri timu za Kurasini Heat na TMT watakaovaana kesho katika fainali ya tatu Viwanja vya Don Bosco Oysterbay.

KATIBU MKUU SIHABA NKINGA AHIMIZA WAKUU WA VYUO VYA MAENDELEO YA JAMII KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI NA TARATIBU KATIKA UTENDAJI KAZI.

$
0
0
Na Erasto Ching’oro WAMJW.

Katibu Mkuu, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Wazee na Watoto (Idara Kuu Maendeleo ya Jamii) Bibi. Sihaba Nkinga amewahimiza Wakuu wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii, kuzingatia sheria, kanuni na taratibu katika utendaji wao wa kazi katika kuendesha vyuo wanavyovisimamia.

Ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo kwa wakuu wa vyuo hao  kuhusu udhibiti wa viashiria hatarishi vya utendaji na utawala ikiwa ni pamoja na  kuzingatia nidhamu ya matumizi ya fedha katika utendaji wao wakazi wa kila siku ili kuepuka hoja za ukaguzi wa fedha.

Amesisitiza kuwa wakuu wa vyuo ni watumishi wa Umma na wanapaswa kuzingatia weledi mahala pa kazi kwa mujibu wa sheria kanuni na taratibu zote za utumishi wa Umma katika kutimiza majukumu yao.

“Niwatake Wakuu wa Vyuo mliopo hapa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo katika kundesha vyuo mnavyoviongoza tuondokane na dosari katika suala la udhibiti wa Fedha katika matumizi” alisema Bibi Sihaba.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Mendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba Nkinga (katikati) akizungumza na Wakuu wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii wakati wa ufunguzi wa Mafunzo ya Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Utendaji wa Vyuo hivyo yanayofanyika katika Ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti, mkoani Morogoro leo 31.7.2017. 
 Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Bw. Patrick Golwike akizungumza na washiriki wa mkutano wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Mendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba Nkinga (katikati) aweze kufungua mafunzo ya Udhibiti wa Viashiria Hatarishi katika Utendaji wa Vyuo hivyo yanayofanyika katika Ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti, mkoani Morogoro leo 31.7.2017.
 Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Buhare ambaye ni Mwenyekiti wa mafunzo (kulia) Bw. Paschal Mahinyika akiwatambulisha washiriki wa mafunzo ya kudhibiti viashiria hatarishi kabla ya kukaribisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Mendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba Nkinga (katikati) aweze kufungua mafunzo yanayofanyika katika Ukumbi wa Wakala wa Mbegu za miti , mkoani Morogoro leo 31.7.2017. 
  Washiriki wa mafunzo ya udhibiti wa viashiria hatarishi kutoka vyuo vya Maendeleo ya Jamii vinavyosimsmiwa na Wizara wakifuatilia kwa makini mazungumzo ya Katibu Mkuu (hayupo pichani) wakati wa uendeshaji wa mafunzo hayo katika ukumbi wa Mbegu za miti , mkoani Morogoro leo 31.7.2017. 

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

UZINDUZI WA BARAZA LA WAZALISHAJI WAFANYIKA ZANZIBAR.

$
0
0
Waziri wa Biashara Viwanda na Masoko Balozi Amina Salum Ali akiangalia bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na Wafanyabishara wa Zanzibar katika Uzinduzi wa Baraza la Wazalishaji lililofanyika katika Hoteli ya Grand Palace Malindi mjini Unguja.
Katibu wa Baraza la Wazalishaji Zanzibar Madam Cheherezade Chukh akitoa hotuba ya makaribisho katika uzinduzi wa Baraza la Wazalishaji lililofanyika katika Hoteli ya Grand Palace Malindi mjini Unguja.
Mwenyekiti wa Baraza la Wazalishaji Zanzibar Ahmed Yussuf Baalawy akizungumza machache katika uzinduzi wa Baraza la Wazalishaji lililofanyika katika Hoteli ya Grand Palace Malindi mjini Unguja.
Baadhi ya Wageni waalikwa waliohudhuria katika  uzinduzi wa Baraza la Wazalishaji lililofanyika katika Hoteli ya Grand Palace Malindi mjini Unguja.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

ZANTEL YATOA ELIMU KUHUSU HUDUMA ZAKE KWA WAKAZI WA MBAGALA NA KONGOWE JIJINI DAR

$
0
0


Afisa wa Zantel Kassongo Faraji (katikati) akifafanua jambo kwa mteja mara baada ya Kampuni hiyo kuwatembelea wakazi wa Mbagala jijini Dar es salaam mwishoni mwa juma na kutoa elimu kuhusiana na huduma zake.
Afisa wa Zantel, Abdallah Mabuga (kulia) akifafanua jambo kwa mkazi na mfanyabiashara wa Mbagala Zakhem Juma Pazi (katikati) mara baada ya Kampuni hiyo kuwatembelea wakazi wa Mbagala jijini Dar es salaam mwishoni mwa juma na kutoa elimu kuhusiana na huduma zake. Kushoto ni Afisa usajili wa Kampuni ya Mawasiliano ya Zantel, Hussein Ahmed Abdallah.
Afisa wa Zantel Thadey Lucas (kulia) akimsajili Mkazi wa Mbagala, Hamdan Ally (katikati) mara baada ya Kampuni hiyo kuwatembelea wakazi wa Mbagala jijini Dar es salaam mwishoni mwa juma na kutoa elimu kuhusiana na huduma zake. Anayeshuhudia kushoto ni mkazi wa Kongowe Abdul Ally.
Maafisa wa Zantel Rehema Tarimu (kushoto) na Hussein Ahmed Abdallah (kulia) wakimsajili mteja mpya mara baada ya kampuni hiyo kuwatembelea wakazi wa Kongowe jijini Dar es salaam mwishoni mwa juma na kutoa elimu kuhusiana na huduma zake.

15 WAFUZU SHINDANO LA EUROPEAN SHORT FILM

WAZIRI MAHIGA AKUTANA NA MCHUNGAJI ONGERE

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akisalimiana na Mchungaji John Oscar Ongere ambaye alifika ofisini kwa Mhe. Waziri kujadili maandalizi ya Kongamano kubwa la uwekezaji linalotarajiwa kufanyika nchini mwezi Novemba 2017..Kongamano hilo litakalofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam litajumuiya wafanyabiashara wakubwa kutoka kote duniani na wa hapa nchini kujadiliana namna bora ya kutumia fursa lukuki za uwekezaji zilizopo hapa nchini. 
Mchungaji Ongere akifanya maombi kwa ajili ya kuiombea nchi amani na utulivu ili iweze kukua kiuchumi 
Picha ya pamoja Balozi wa Iran
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mhe. Mousa Farhang ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo. Mazungumzo yao pamoja na mambo mengine walijadili maandalizi ya sherehe za kumuapisha Rais Mteule wa Iran, Mhe. Hassan Rouhani zitakazofanyika Tehran tarehe 05 August 2017. 
Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia mazungumzo hayo, Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Bi. Zainab Angovi-Mrutu, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Bw Ayoub Mndeme na Katibu wa Waziri, Bw. Gerald Mbwafu. 
Ujumbe aliofuatana nao Balozi wa Iran ukifuatilia mazungumzo. 

WASHIRIKI 15 WATAJWA KATIKA MASHINDANO YA EUROPEAN YOUTH FILM

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MASHINDANO ya European Youth Film 2017 imewatangaza washiriki 15 waliofanikiwa kuingia hatua hiyo baada ya kutengeneza filamu fupi zenye maudhui tofauti.

Shindano hilo liliwashirikisha washiriki zaidi ya 120 na kuwachuja na kufikia 35 na tayari wamewapata washiriki 15 walioingia katika
kinyang'anyiro hicho na maamuzi yatakuwa mikononi mwa wananchi.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa utangazaji wa washiriki hao, Balozi wa Umoja wa Ulaya Roeland Van De Geer amesema kuwa wameziangalia filamu hizo katika maudhui tofauti na wamechujwa kwa kushirikiana na Bodi ya Filamu nchini.
Balozi wa Umoja wa Ulaya Roeland Van De Geer akizungumza na waandishi wa habari wakati wa utangazaji wa washiriki 15 waliofanikiwa kuingia hatua hiyo baada ya kutengeneza filamu fupi zenye maudhui tofauti.Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Huduma za Ufundi wa Bodi ya Filamu Wilhad Tairo na Kulia ni Afisa wa habari wa Umoja wa Ulaya Sussane Mbise.
Kaimu Mkuu wa Huduma za Ufundi wa Bodi ya Filamu Wilhad Tairo akuzungumza na kuupongeza Umoja wa Ulaya kwa mashindano waliyoaanzisha ya kuibua vipaji kwa waandaaji wadogo wa Filamu nchini, kushoto ni Mratibu wa mashindano Mussa Sakala.

De Geer amesema kuwa, filamu hizo 15 zitaoneshwa katika maeneo ya wazi ndani ya Jiji la Dar es salaam kwenye Viwanja vya Biafra Agost 5, Zakhem Agosti 12, Mwembe Yanga Agosti 19 na ukimbi wa Alliance Francais Septemba 02 ambapo washiriki watano wataingia hatua ya fainali.

Kaimu Mkuu wa Huduma za Ufundi wa Bodi ya Filamu Wilhad Tairo amesema kuwa mashindano haya yana tija kubwa sana katika kuibua vipaji ya sanaa na zaidi lazima tuanze kuangalia kutoka chini ili kupata waandaaji wapya na wenye ubunifu katika sekta ya sanaa hususani Filamu.

Mashindano hayo yatafikia tamati mwezi Septemba mwaka huu na yanaratibiwa na Umoja wa Ulaya nchini Tanzania.

Police Commends SGA Security for Training Standards

$
0
0
The OCD for Kawe, Kinondoni in Dar es Salaam, SP Jiliyo Simba  has praised the standards of SGA Security training . He was the chief guest in a pass-out parade during the graduation of 75 officers who successfully completed basic guard training.  The ceremony was held on Saturday July 29, 2017 at SGA training base in Mbezi Beach. Only 75 made the cut out of 179 who were in training, showing the high standards of the training.  The rest will continue to train. 

Mr Simba also inspected the company facilities including the response vehicles, fire response and the control room systems.  He was impressed by the investment made by the company and the controls in place within their operations, particularly the tracking systems. 'I didn't expect this level of preparedness and training standard from a security company given that we are used to shoddy work of many companies ', he added. 
He lauded SGA efforts and implored them remain as great examples to the rest of the companies.  He urged the guards to remain a good example to the rest and remain true to the training received during the course. 

SGA Security HRM , Ebenezer Kaale, explained that the course  contains several units including customer care, fire fighting,  first aid, principles of human rights, amongst many core security subjects.

 'We believe that we have imparted basic security training to enable perform their duties diligently', he said. Before recruitment,  rigorous vetting is carried out on all applicants. Fingerprints are taken to check against crime record by Ministry of Home Affairs officers.  Medical examination is also carried out to test fitness and stamina before being subjected to training. 

During the ceremony, best performing trainees were awarded and feted by the chief guest.  Also feted were two guards who pre-empted theft of their customers' property during performance of their duties. It is the culture of the security company to recognise outstanding performance and certificate and cash reward issued during parades to motivate the rest. 


Also present was Kinondoni RCO SSP John Malulu, who was the immediate OCD for Kawe. Mr Malulu lauded SGA Security for cooperation given to his team when he was in charge in Kawe police district,   saying that it made the job of the police lighter.  


He pointed out that SGA provided patrol vehicles during weekends and holidays and supprted police in repairing some of their vehicles. 'SGA was always first in response to their customers and their neighbours and that contributed to  reduced crime rate.  I count on your support in my new role ' ,  he added. 

SGA Security Managing Director ,  Mr Eric Sambu,  said that the company, which is the largest in the country, focuses more on training to empower their employees to perform their duties to meet and surpass the expectations of their customers. 'Training for us is the key ingredient to our success story and we focus on all categories of employees nationally ', he added. The concluded yesterday another training for internal audit team for ISO 9001 : 2015, on Quality Management, which the company is certified since 2001. 
SGA Security provides guarding services, cash-in-transit services, electronic security solutions, alarm response services, tracking solutions,  courier amongst other services. It operates countrywide and employs over 5,000 employees with customers in all the sectors of the economy.

JAFO:ACHENI KUFANYA KAZI KWA MAZOEA

$
0
0
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo amewataka watumishi wa halmashauri ya mji wa Tarime na Halmashauri ya wilaya ya Tarime kuacha tabia ya kufanyakazi kwa mazoea. 

Jafo aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na wafanyakazi wa halmashauri hizo mbili wakati wa ziara yake leo wilayani Tarime mkoani Mara.

Katika ziara hiyo, Jafo alifanikiwa kutembelea miradi ya afya, elimu, daraja na ujenzi wa nyumba za watumishi.

Jafo ameiagiza viongozi wa halmashauri hizo mbili kukaa na kufanya maamuzi ya majengo ya halmashauri ya wilaya ya Tarime yaliyopo ndani ya eneo la halmashauri ya mji yatumike kwa matumizi ya kiofisi ya halmashauri ya mji.

Aidha ameagiza fedha zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa halmashauri ya mji zihamishiwe halmashauri ya wilaya ili waende kuanza ujenzi wa ofisini katika eneo lao badala ya kukaa ndani ya eneo la halmashauri mji.

“Kitendo hichi kinawakosesha wananchi haki yao ya kupata huduma kwa ukaribu jambo ambalo ndilo lilikuwa msingi wa kugawa halmashauri hizo,”amesema Jafo

Naibu Waziri Jafo amemaliza ziara yake na kuelekea wilaya ya Rorya, mkoani Mara.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo alipotembelea eneo la mapokezi la hospitali ya Tarime na kuagiza lijengwe banda kwa ajili ya kukaa wananchi badala ya kukaa juani kama ilivyo hivi sasa. 
Watumishi wa Halmashauri mbili za Tarime wakiwa katika mkutano wa pamoja na Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo. 
Majengo yaliyojengwa na wadau wa mgodi wa North Mara kwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya ya Tarime. 
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa Halmashauri ya wilaya ya Tarime. 

BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA -AfDB KUSHIRIKI UJENZI WA RELI YA KATI YA KISASA TANZANIA

$
0
0


Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam

Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) imeahidi kushirikiana na Tanzania kujenga mradi mkubwa wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa (SGR) kwa kuipatia mkopo wenye masharti nafuu.

Ahadi hiyo imetolewa Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo anayesimamia kanda ya Afrika Mashariki, Dkt. Nyamajeje Weggoro, alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji.

Dkt. Weggoro amesema kuwa Benki yake imeridhika na utendajikazi wa Serikali ya Awamu ya Tano ikiongozwa na Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli na hivyo kuifanya Bodi ya Wakurugenzi ya Benki hiyo kukubali kufanikisha ujenzi wa Reli hiyo kwa ajili ya maendeleo ya nchi.

Amesema kuwa Reli ya Kati kwa Kiwango cha Kimataifa ni muhimu kwa uchumi wa Taifa lakini pia kwa uchumi wa nchi za Maziwa Makuu kwa kuunganisha nchi kama vile Rwanda, Burundi, Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na baadae itaunganishwa na Reli ya Kaskazini upande wa Kenya.

“Benki iko tayari na inasubiri Tanzania ilete mapendekezo ama maombi ili yafanyiwekazi, tutakaa pamoja ili tuone Benki itasaidia kiasi gani na Benki pia inaweza kuwatafuta wadau wengine tunaosaidiana nao katika miradi mikubwa kama hii” Aliongeza Dkt. Weggoro

Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (kulia) akisikiliza kwa makini maelezo ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, Kanda ya Afrika Mashariki Dkt. Nyamajeje Weggoro (hayupo pichani) kuhusu ushirikiano mzuri na Benki hiyo katika Maendeleo ya kiuchumi nchini Tanzania, Makao Makuu ya Wizara ya Fedha, Jijini Dar es Salaam.


Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Kanda ya Afrika Mashariki, Dkt. Nyamajeje Weggoro (hayupo pichani) alipokutana naye ofisini kwake Jijini Dar es Salaam. 
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (kulia), akiishukuru Benki ya Maendeleo ya Afrika, AfDB, kwa namna inavyoshirikiana na Tanzania kukuza uchumi wake, wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo anayesimamia  Kanda ya Afrika Mashariki, Dkt. Nyamajeje Weggoro, Jijini Dar es Salaam 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, Kanda ya Afrika Mashariki, Dkt. Nyamajeje Weggoro, akizungumza namna Benki yake itakavyofadhili ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwando cha Kimataifa (Standard gauge) pamoja na kuhuisha Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania-TANESCO, alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (hayupo pichani), Jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, anayehudumia Kanda ya Afrika, Dkt. Nyamajeje Weggoro (katikati) akimwonesha Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), zawadi ya picha, baada ya kumalizika kwa mazungumzo yao, Jijini, Dar es Salaam

MAKAMU WA RAIS AZINDUA MPANGO MKAKATI WA WATER AID TANZANIA

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassana leo amezindua Mpango Mkakati wa Water AID Tanzania .

Katika mkutano huo uliofanyika kwenye hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Mhandisi Gerson Lwenge, Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Mahmoud Thabit Kombo, Mkurugenzi wa Water Aid Kanda ya Afrika Mashariki Bi. Olutayo Bankole –Bolawole,Mkurugenzi WaterAid Tanzania Dkt. Ibrahim Kabole na wadau mbali mbali wa maji, afya na mazingira.

Mpango Mkakati wa miaka mitano wa Water Aid Tanzania wenye lengo la “ Kuweka Maji Safi na Usafi wa Mazingira (WASH)” katika mipango ya Maendeleo ya Jamii.

Makamu wa Rais aliwapongeza Water Aid Tanzania kwa mpango wake huo, alisema Maji ni rasilimali ambayo haijawahi kutosheleza mahitaji ya dunia na hapa kwetu pia kwani kuna mahitaji makubwa ya maji kwa ajili ya shughuli za kijamii, kiuchumi na kuhuisha na kutunza mazingira.

Vilevile vyanzo vya maji vinaathiriwa sana na Ukame,kufurika n, kuvuruga mtiririko asilia, mabadiliko ya hali ya hewa ongezeko la idadi ya watu na viumbe wengine (Wanyama).
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa Water Aid Tanzania kwa mwaka 2016-2021 wenye kauli mbiu "Kuweka Maji na Usafi wa Mazingira kuwa kitovu cha Maendeleo"iliyofanyika kwenye hotel ya HyattRegency jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Mhandisi Gerson Lwenge wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa Water Aid Tanzania kwa mwaka 2016-2021 wenye kauli mbiu "Kuweka Maji na Usafi wa Mazingira kuwa kitovu cha Maendeleo"iliyofanyika kwenye hotel ya HyattRegency jijini Dar es Salaam. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Mohamoud Thabit Kombo wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa Water Aid Tanzania kwa mwaka 2016-2021 wenye kauli mbiu "Kuweka Maji na Usafi wa Mazingira kuwa kitovu cha Maendeleo"iliyofanyika kwenye hotel ya HyattRegency jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akionyesha kitabu maalumu chenye mpango mkakati wa Water Aid ​.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AZUNGUMZA NA WATUMISHI WA MANISPAA YA MBEYA

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi wa Umma, Viongozi wa Dini na Viongozi wa Taasisi Binafisi wa Manispaa ya Mbeya kwenye ukumbi wa Benjamin Mkapa jijini Mbeya Julai 31, 2017.  Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla na Kulia ni Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson.  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
 Baadhi ya Watumishi wa Umma, Viongozi wa Dini na Viongozi wa Taasisi Binafsi wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye ukumbi wa Benjamin Mkapa jijini Mbeya julai 31, 2017. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi Mkuu wa TAKUKURU wa Mkoa wa Mbeya, Mhandisi Emmanuel Kyabo taarifa zinaoonyesha ubadhirifu uliofanywa na baadhi ya watendaji katika ujenzi wa soko la Mwanjelwa jijini Mbeya ili afanye uchunguzi wa kina  na kumshauri Waziri Mkuu hatua zinazostahili kuchukuliwa kwa wanatakaobainika kuwa wamefanya makokosa. (PIcha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Vijana washauriwa kujiunga na awamu ya tatu ya program ya Via Jiandalie Ajira

$
0
0
Vijana wenye umri wa miaka 18 hadi 24 wameshauriwa kujiunga na awamu ya tatu ya program Via Jiandalie Ajira inayoendeshwa na Taasisi ya Ujasiriamali na Ushindani Tanzania (TECC) ili kupata mafunzo ya ujasiriamali, stadi za maisha, malezi ya kibiashara na kuunganishwa na taasisi za kifedha kupata mitaji kukabiliana na tatizo la ajira. 

Meneja Malezi wa Taasisi hiyo, Bw. Daniel Mghwira alisema hayo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari, kuwa vijana wajiunge na program hiyo ambayo imeingia katika awamu ya tatu kupata mafunzo hayo ili kukabiliana na tatizo la ajira. 

“Via Jiandalie Ajira awamu ya tatu inawalenga vijana wa Halmashauri zote za Mkoa wa Dar es Salaam, Mikindani Mtwara, Dodoma na Kibaha Pwani,” na fomu za kujiunga zinapatikana katika ofisi za kata, ofisi za maafisa vijana za manispaa za maeneo hayo, aliongeza kusema Bw. Mghwira ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi wa taasisi hiyo.

Meneja Malezi wa Taasisi ya Ujasiriamali na Ushindani Tanzania (TECC), Bw. Daniel Mghwira (katikati) akizungumza kuhusu kuanza kwa kwa awamu ya tatu ya program Via Jiandalie Ajira kwa halmashauri zote za Dar es Salaam, Mkindani Mtwara, Dodoma na Kibaha Pwani, kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Rais wa Kujitegemea (PTF),Bi. Haigath Kitala na kushoto Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Chemba ya Wafanyabiashara na Kilimo Tanzania(TCCIA),Bi. Magdalene Mkocha.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

WANANCHI MONDULI KUNUFAIKA NA MAJI

$
0
0
Zaidi ya kaya 700 za wananchi wa Kitongoji cha Irmorijo Kijiji cha Emairete Wilayani Monduli Mkoani Arusha, waliokuwa wanatumia maji ya kwenye bwana wanatarajia kunufaika na mradi wa kusafisha maji na kuchuja maji kuwa safi uliozinduliwa Kijiji hapo.

Awali, wananchi hao walikuwa wanatumia kwa shughuli mbalimbali ikiwemo kupika, kufua, kuoga na kunywa maji hayo ya bwawa ambayo pia yalikuwa yanatumiwa na mifugo ya eneo hilo.

Mkurugenzi wa kampuni ya Smart Vision ya Korea, Seo Young Kim akizungumza jana kwenye uzinduzi wa mradi alisema lengo ni jamii ya eneo hilo kunufaika na maji safi na salama yanayochujwa kupitia ubunifu wao.

Kim alisema kwa kuanza kuwanufaisha wananchi wa eneo hilo, wanatarajia kugawa majiko rafiki ya mazingira 22 na mitambo ya kuchuja na kusafisha maji ya bwawa kuwa safi na salama 22 kwa kaya 22 zitakazowanufaisha zaidi ya watu 220.

Alisema Smart Vision kupitia uwekezaji wa Korea Trade-Investment Promotion Agency. (KOTRA) jamii ya eneo hilo itanufaika na na mradi huo wenye lengo la kuondokana na matumizi ya maji yasiyo safi wala salama ambayo yanasababisha magonjwa ya tumbo.

“Jamii ya eneo hili kupitia mchungaji wa kanisa la Enyorata Daniel Vengei, walileta maombi kwetu kuwa wanatatizo la maji, hospitali na shule, ndipo tukaona tuanze kutatua hili suala la maji ndipo tukaleta mitambo hii ya kuchuja na kusafisha maji,” alisema Kim. 
Mkurugenzi wa kampuni ya Smart Vision ya Korea, Seo Young Kim (kushoto) na Andrew Chung ambaye ni mbunifu wa mtambo wa kusafisha maji wakionyesha mtambo huo kwenye uzinduzi wake kwenye kitongoji cha Irmorijo Kijiji cha Emairete Wilayani Monduli Mkoani Arusha
Mkurugenzi wa kampuni ya Smart Vision ya Korea, Seo Young Kim (kushoto) na mchungaji wa kanisa la Enyora Daniel Vengei wakiwa kwenye uzinduzi wake katika kitongoji cha Irmorijo Kijiji cha Emairete Wilayani Monduli Mkoani Arusha.
Wananchi wa kitongoji cha Irmorijo Kijiji cha Emairete Wilayani Monduli Mkoani Arusha wakishuhudia uzinduzi wa mtambo wa kusafisha maji na kuyachuja uliofanywa na kampuni ya Korea ya Smart Vision.

Viewing all 109979 articles
Browse latest View live




Latest Images