Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live

UTENGENEZAJI WA KATUNI HAI (ANIMATION) NCHINI


maendeleo ya mchezo wa Baseball na Softball Tanzania

$
0
0
Taarifa kutoka kwa Katibu Mkuu wa Chama cha mchezo wa Baseball na Softball Tanzania ndugu Alpherio Nchimbi zinasema kwamba mafunzo kwa walimu pamoja na wachezaji wa Baseball Mkoani Mbeya yamekamilika kwa mfanikio makubwa ambapo zaidi ya washiriki 50 wamepata mafunzo hayo na kukabidhiwa vyeti vya kuhitimu. Mafunzo hayo yalitolewa na mwalimu mbobezi kutoka Japan ndugu Hiroki Iwasaki, yalianza tarehe 15 Julai na kukamilika jana Jumapili tarehe 16 Julai, 2017 yalikuwa ni ya siku nzima. "Intensive training program". Picha hizo zinaonyesha washiriki wakiwa viwanjani.
 mafunzo kwa walimu pamoja na wachezaji wa Baseball Mkoani Mbeya
 mafunzo kwa walimu pamoja na wachezaji wa Baseball Mkoani Mbeya
 Baadhi ya washiriki 50 ambao wamepata mafunzo hayo na kukabidhiwa vyeti vya kuhitimu wakiwa na na mwalimu mbobezi kutoka Japan ndugu Hiroki Iwasaki

CHAMA CHA ADC CHAIPONGEZA SERIKALI KWA KUWASEMEHE KODI WAZEE

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Allianc Democrtc Change (ADC) Taifa, Hamad Rashid akifafanua jambo mbele ya wanahabari  juu ya kuipongeza serikali kwa kuwasamehe kodi za majengo wazee wa zaidi ya miaka 60,kwenye nyumba ambazo wanaishi na hazizalishi kipato chochote, jijini Dar es Salaam jana. kulia ni Katibu Mkuu wa Chama hicho, Doyo Hassan.

Wanaume watakiwa kuacha kukimbia watoto wenye ulemavu - DC Kasesela

$
0
0
Jumamosi, Julai 15, 2017 Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Atufigwege Kasesela alitembelea kituo cha kulea watoto wenye ulemavu kiitwacho Nyumba Ali kilichopo Wilolesi. Nyumba Ali iliundwa na umoja wa wazazi wenye watoto waishio na ulemavu mkoani Iringa. 

Lengo la kuunda umoja huo ulikuwa ni kuwakutanisha wazazi ili waweze kuwa na sauti moja katika kubainisha na kusaidiana katika kutatua changamoto mbalimbali zinazo ikumba jamii ya watoto waishio na ulemavu. Akitoa taarifa Mbele ya Mkuu wa wilaya mratibu wa kituo hicho, Adam Duma alisema wamefungua vituo hivyo viwili kimoja kikiwa Wilolesi na kingine Ngome. 
Kituo kimoja kinapokea watoto 35. Wamekuwa wanawafanyia mazoezi ya viungo pamoja na kuwafundisha kazi za mikono mbalimbali watoto wenye ulemavu wa viungo na akili.

Akizungumza na wazazi na walezi wa kituo hicho, Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela alisema “ Nasikitishwa na baadhi ya wazazi ambao wanajaliwa kupata watoto wenye ulemavu na kuwatelekeza hili halikubaliki. 

Kila afisa tarafa afanye utafiti nyumba hadi nyumba kubaini kama kuna mtoto mlemavu, Nachukia sana tabia ya baadhi ya wakina baba kukimbia watoto wenye ulemavu na kuwachia wakina mama. Hebu wanaume tuache tabia ya kukimbia watoto wenye ulemavu.” alisema. Pia aliwataka wakina baba wajitokeze kufika kwenye kituo sio kuwachia wakina mama peke yao.

Kituo cha Nyumba Ali kimekuwa kikiendeshwa kwa msaada wa wahisani mbalimbali ambapo mahitaji makubwa ni pamoja na chakula, baiskeli za walemavu pamoja na gharama za uendeshaji. 
Katika kituo hiki yupo mtoto aitwaye Zawadi ambaye amesomeshwa hadi kiwango cha darasa la saba, Mtoto huyu hawezi kutumia mikono anatumia miguu kwa shida akisaidiwa na kompyuta na amefanikiwa kuandika kitabu kinacho elezea maisha yake.​
Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Atufigwege Kasesela akizungumza na mmoja wa watoto wanaolelewa katika kituo cha kulea watoto wenye ulemavu kiitwacho Nyumba Ali kilichopo Wilolesi, Wilayani Iringa.
bofya hapa kwa picha zaidi

ILALOO FC MABINGWA KOMBE LA DIWANI SARANDA

$
0
0
MASHINDANO ya ligi ya kombe la Diwani wa kata Saranda, Tarafa ya Kilimatinde, wilayani Manyoni, Mkoani Singida yamefikia tamati kwa timu ya soka ya ILALOO FC kuwa mabingwa wa kombe hilo kwa mwaka huu wa 2017 baada ya kuifunga timu ya Saranda FC kwa jumla ya magoli 2-1.

Ligi hiyo iliyoanza kuchezwa juni, 29 mwaka huu kwa makundi mawili yaliyokuwa yakivitumia viwanja vya michezo vya Shirika la reli Tanzania (TRC) ilizishirikisha jumla ya timu sita za kata hiyo ambazo ni pamoja na Saranda FC, Ilaloo FC, Irucha, Mlimani A, Mlimani B na Mhegahega FC.

Akitangaza matokeo ya mashindano hayo, Katibu wa Chama Cha mpira wa miguu wilaya ya Manyoni (MADIFA), Joshua Msemakweli aliwataka vijana hao kuwekeza kwenye mchezo wa soka kwa kuamini kwamba michezo ni afya na michezo ni ajira.  

“Mashindano ngazi ta kata ya Saranda yalishirikisha timu sita kutoka katika vijiji na vitongoji,ambavyo ni Kijiji cha Saranda ambapo ndipo makao makuu ya kata  pia Ilaloo na Irucha zipo Kijiji cha Saranda Kijiji cha Saranda kilikuwa na timu tatu”alifafanua Msemakweli.

Kwa upande wake muandaaji wa kombe hilo ambaye pia ni diwani wa kata ya Saranda,Joseph Ndahani aliyataja baadhi ya malengo ya michezo hiyo kuwa ni kuhakikisha wanakuza pamoja na kuvitangaza vipaji wa vijana wa kata hiyo kupitia sekta ya michezo.

Naye Mwalimu wa timu ya soka ya Ilaloo FC ambao ndiyo mabingwa wa kombe hilo, Rashid Juma alikishukuru kituo hiki kwa kuweza kufika katika Kata hiyo na kuwawezesha kusikika maana haijawahi kutokea bahati kama hiyo kwa vituo vingine kufika huko. 
Katibu wa Chama Cha Mpira wa miguu wilaya ya Manyoni (MADIFA) Joshua Msemakweli (wa pili kushoto) akitoa maelekezo kwa viongozi wa timu pamoja na wachezaji wa timu zilizoshiriki mchezo wa fainali katika kata ya Sanjaranda.

Standard Chartered Bank’s Group Chief Information Officer to visit Tanzania

$
0
0
Standard Chartered Bank’s Group Chief Information Officer, Dr. Michael Gorriz is expected to visit the Bank’s offices in Tanzania today. According to a statement issued by Standard Chartered Bank Tanzania Limited, during his visit Dr. Gorriz will meet with various internal and external stakeholders of the Bank in Tanzania with a view of exploring ways in which the Bank can further enhance its business and support economic growth in the country.

Dr. Gorriz was appointed Group Chief Information Officer on 25 March 2015 and is responsible for the banking operations, systems development and technology infrastructure which underpin the Bank’s client services, and defines and implements the Bank’s digital and innovation agenda.

His visit to Tanzania comes as the Bank commemorates its centenary anniversary since it first opened its doors in Tanzania in 1917. The visit is a continuation of key Group visits that have been taking place to mark the Bank’s historical milestone in Tanzania as well as further reiterate the Group’s commitment to Tanzania. Dr. Gorriz will be accompanied by Top Team Members of the Group’s Information Technology and Operations Segment. These include; Bhupendra Warathe, the Global Head of the Bank’s Operations, Venkatesh Rathnam, the Global Head of Business Operations covering the Bank’s Retail Banking, Wealth Management and Private Banking Segments, and Toby Blythen, the Chief Financial Officer for the Information Technology and Operations Segment.

READ MORE HERE

ZOEZI LA KUORODHESHA KAYA KWA AJILI YA UTAFITI WA MAPATO NA MATUMIZI LAENDELEA KUFANYIKA NCHINI

$
0
0
Na: Veronica Kazimoto

ZOEZI la kuorodhesha kaya kwa ajili ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi Tanzania Bara wa Mwaka 2017/18 linaendelea nchi nzima ikiwa ni maandalizi ya utafiti huo unaotarajia kufanyika hivi karibuni.

Akizungumzia zoezi hilo, Meneja wa Takwimu za Jamii na Watu, Sylvia Meku wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu amesema mpaka sasa mikoa kumi na tatu (13) imekamilisha zoezi hilo ambapo ni sawa na silimia 50.

“Zoezi la kuorodhesha kaya kwa ajili ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi Tanzania Bara wa Mwaka 2017/18 linaendelea vizuri na mpaka sasa wadadisi wamekamilisha kuorodhesha kaya katika mikoa 13,” amesema Sylvia Meku.

Ameitaja mikoa iliyokamilisha zoezi la uorodheshaji wa kaya kuwa ni pamoja na Dar es Salaam, Arusha, Manyara, Iringa, Njombe na Morogoro. Mikoa mingine ni Mwanza, Tabora, Katavi, Mbeya, Mara, Kagera na Lindi. Zoezi la Uorodheshaji wa Kaya linafanyika mikoa yote ya Tanzania Bara na linatarajia kumalizika mwishoni mwa mwezi Julai, 2017.

Utafiti kama huu mara ya mwisho ulifanyika Mwaka 2011/12 ambao ulionesha kuwa asilimia 28.2 ya Watanzania wanaishi chini ya mstari wa Umaskini wa mahitaji ya Msingi.

Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi Tanzania Bara wa Mwaka 2017/18 unafanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango na baadhi ya Wadau wa Maendeleo kwa lengo la kupata viashiria vya kupima hali ya umaskini nchini.
Mdadisi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) akihoji taarifa za kaya wakati wa zoezi la kuorodhesha kaya kwa ajili ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi Tanzania Bara wa Mwaka 2017/18 linaloendelea kufanyika nchini ikiwa ni maandalizi ya utafiti huo unaotarajia kufanyika hivi karibuni.
Mdadisi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) akihoji taarifa za kaya wakati wa zoezi la kuorodhesha kaya kwa ajili ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi Tanzania Bara wa Mwaka 2017/18 linaloendelea kufanyika nchini ikiwa ni maandalizi ya utafiti huo unaotarajia kufanyika hivi karibuni.
Mdadisi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) akiwaoneyesha wasimamizi namna alivyojaza taarifa za kaya wakati wa zoezi la kuorodhesha kaya kwa ajili ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi Tanzania Bara wa Mwaka 2017/18 linaloendelea kufanyika nchini ikiwa ni maandalizi ya utafiti huo unaotarajia kufanyika hivi karibuni. (PICHA ZOTE NA EMMANUEL GHULA).

SPIKA NDUGAI APOKEA UJUMBE MAALUM KUTOKA SPIKA WA IRAN LEO OFISINI KWAKE MJINI DODOMA

$
0
0
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akipokea ujumbe Maalum kutoka kwa Spika wa Bunge la Iran, uliowasilishwa leo na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mhe. Mousa Farhang (kulia), katika tukio lililofanyika leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akizungumza na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mhe. Mousa Farhang (katikati), katika kikao kilichofanyika leo Ofisini kwake Mjini Dodoma. kulia ni Msaidizi wa Balozi wa Iran Ndg. Zuhura Ally. (PICHA NA OFISI YA BUNGE)

PROF. MBARAWA AWATAKA TBA KUMALIZA NYUMBA YA JAJI MFAWIDHI

$
0
0
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kushoto), akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Zainab Tellack, mara baada ya kuwasili mkoani humo kwa ziara ya kikazi.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kushoto), akifafanua jambo kwa viongozi wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara alipokutana nao mkoani humo kwa ziara ya kikazi.
 Meneja wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), mkoa wa Shinyanga Eng. Amosi Manyete akimuonesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, mfumo wa maji taka uliowekwa nje ya jengo la Mahakama Kuu ya Tanzania, kanda ya Shinyanga iliyopo mkoani humo. Kushoto ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda hiyo Mhe. Jaji Richard Kibella.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

VIDEO: WALIOCHAGULIWA KWENYE USAILI KUSHIRIKI UCHAGUZI WA KLABU YA MAJIMAJI

BRAZUKA KIBENKI: Maofisa kuonyeshana kazi viwanjani

$
0
0
MSIMU wa tatu wa michuano ya BRAZUKA KIBENKI unaoshirikisha taasisi za kibenki katika michezo ya mpira wa miguu na kikapu unatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu jijini Dar es Salaam.

Katika msimu huu michuano hiyo itashirikisha timu 15 ambazo ni NMB (Mabingwa watetezi), DTB, Barclay’s, BancABC, Exim, Stanbic, BOA, UBA, Letshego, EcoBank, CRDB, BOT, Azania, TPB, Access na UBA.

Mmoja wa maofisa wa benki ya Exim, Frank Rweyemamu ambaye pia ni mwanachama wa tawi la Simba Makini linalomiliki mtandao huu alivitaja viwanja vitakavyotumika kuwa ni Gymkhana na DonBosco.
Martin Komba wa DTB (kulia) akimtoka Hezbo wa NMB katika pambano la jana

“Michuano ya mwaka huu itafanyika katika viwanja vya Gymkhana kwa mpira wa miguu huku mechi za mpira wa kikapu zikitarajiwa kuchezwa katika uwanja wa DonBosco.” Alisema Rweyemamu.

Jana kulikuwa na mchezo wa ngao ya hisani ambapo mabingwa watetezi NMB walikubali kichapo cha mabao 4-0 kutoka kwa DTB katika mchezo wa kuashiria kuanza kwa michuano hiyo.

Bingwa wa msimu huu atakabidhiwa kikombe pamoja na medali.

PPF YATANGAZA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KWA USAILI NAFASI YA MENEJA UDHIBITI WA MAJANGA NA MENEJA WA UTAFITI NA MIPANGO

MBUNGE wa Ilala,Mussa Azzan Zungu kutoa mifuko 100 ya saruji kwa nyumba za wasanii

$
0
0
MBUNGE wa Ilala,Mussa Azzan Zungu ameahidi kutoa mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya kujengea nyumba za wasanii wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA).
Akizungumza wakati wa kufunga tamasha la siku mbili lililowakutanisha wasanii zaidi ya 600 kutoka vikundi mbalimbali vikiwemo vya Tanzania One Theatre (TOT)Zungu alisema ametoa saruji hiyo ili kuwasaidia SHIWATA kuendeleza juhudi za kuwakomboa wasanii kwa kuwajengea makazi.
Mbunge Zungu pamoja ya kushuhudia michezo mbalimbali alishindwa kujizuia kuungana na wasanii kucheza na kutunza ngoma ya asili ya Sangura kutoka kabila la Wapogoro mkoani Morogoro.
>Bendi za muziki wa dansi za Hisia Sound ya Abdul Salvador,bendi ya TOT na Umoja Sound ziliwakonga wasanii na wengine waliohudhuria tamasha hilo.
Katika tamasha hilo lililofunguliwa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) Godfrey Mngereza wasanii wa fani mbalimbali walionesha vipaji vyao vya kucheza sarakasi,ngoma za asili,maigizo,muziki wa dansi,muziki wa asili na taarabu.
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega ambae tamasha hilo awali lilikuwa lifanyike kijiji cha Wasanii  Mkuranga na baadaye kuhamishiwa jijini Dar es Salaam kutokana na mvua ya msimu uliopita kuharibu barabara ya kwenda kijijini alisema jutihada zifanyike ili mwakani lifanyike  Mkuranga.
> > > > >
Mkurugenzi wa TOT,Gasper Tumaini alisema tamasha hilo limefana na wao wako tayari kushirikiana na SHIWATA katika matamasha mengine.

Pamoja ya kudhaminiwa na Kampuni ya SBC inayotengeneza soda za Pepsi, Kampuni ya Simu ya TTCL kulikuwa na msaada wa kisheria wa kujikinga na magonjwa ya UKIMWI.
 Katibu Mtendaji wa BASATA,Godfrey Mngereza akiwa na Mkurugenzi wa TOT,Gasper Tumaini.
 Wasanii wa Kikundi cha Kaole wakimkaribisha Katibu Mtendaji wa BASATA,Godfrey Mngereza katika tamasha la SHIWATA.
 Msanii maarufu nchini,Bakari Mbelemba (Mzee Jangala) na wageni wengine akifuatilia kwa karibu maonesho ya wasanii.
 Washiriki wa tamasha wakifuatilia kwa karibu maonesho ya wasanii.
 Wasanii wa Kaole wakicheza ngoma mbele ya wageni waalikwa.
Mbunge Zungu akituza  kikundi cha ngoma za asili cha Sangura.

RAIS MAGUFULI KUFUNGUA NA KUZINDUA MIRADI TISA YA BARABARA NA UWANJA WA NDEGE

SUZA to host Annual East African Cisco networking academy safari 2017 in ZANZIBAR


RATIBA YA MAZISHI YA MAREHEMU LINNAH MWAKYEMBE.

TSN GROUP YAINGIA MKATABA NA MIMOSA CONCIERGE KURAHISISHA HUDUMA KWA WATEJA WAO

$
0
0
  TSN Group Tanzania, katika kuhakikisha inatoa huduma bora kwa wateja wake hapa nchini, imeingia mkataba na MIMOSA CONCIERGE inayotoa MIMOSA Black Card ambayo ni kadi maalum kwa wateja wanaofika kupatiwa huduma kupitia kadi hizo. 

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kusaini mkataba huo na kampuni hiyo jijini Dar es Salaam, leo Meneja Masoko wa TSN alisema, Jahu M. Kessy amesema TSN imelenga kuongeza tija katika kutoa huduma zake.
 “Tunarahisisha na kuboresha huduma zetu kuwa bora na za kisasa. Pengine huduma hii itapanua wigo wa wateja wetu watumiao Black Cards kwa Dar es salaam lakini kwa Mwanza TSN Hypermarket inakuwa kampuni ya kwanza kupokea na kukubali malipo kupitia Black card ya Mimosa. Hatua ambayo ni kubwa kuchukuliwa na TSN katika kuwajali wateja wake.”
 “Sasa ukifanya malipo kupitia kadi ya Mimosa kwenye supermarket zetu na Petrol station unajiweka katika nafasi ya kushinda punguzo la zaidi ya asilimia 5 pamoja na kuponi ya zawadi wa kwateja watakao tumia kiasi cha shillingi laki moja kwa manunuzi ya mara moja,” alisema Jahu. 

Akieleza zaidi juu ya huduma na faida wazipatazo wateja watumiayo kadi hizo, Mkurugenzi Msiaidizi wa MIMOSA, Leonce Mongi alisema kupitia kadi hii Mteja wa TSN hatapata tu punguzo la bei kutoka TSN pekee lakini pia atapata offer mbalimbali zitokanazo na kadi hiyo kupitia discount partners wengine ambao ni zaidi ya watoa huduma 71 Nchi Nzima.  
 Jahu alisema TSN inajiimarisha katika kutoa huduma zake kwa wateja, kuwasikiliza na kuwasaidia, hivyo basi kuona umuhimu wa kuwapatia wateja wake wenye MIMISA black card nafasi ya kufanya malipo yao kwa uhuru na furaha. 

WAAJIRI NCHINI WATAKIWA KUZINGATIA MGAWANYO SAHIHI WA RASILIMALIWATU

$
0
0
Waajiri nchini wametakiwa kuzingatia mgawanyo sahihi wa Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma ili kuwa na utendaji bora na wenye matokeo katika utumishi wa umma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) amesema hayo leo katika kikao kazi na Watumishi wa Umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, jijini Dar es Salaam.

Mhe. Kairuki amesema mwajiri anapoomba kibali cha kuajiri watumishi ni vema akazingatia mahitaji kulingana na majukumu yaliyopo ili kuondoa ziada ya watumishi wa umma wasio na kazi kuendana na fani walizosomea kwa lengo la kuwa na utendaji mzuri.

“Ni vizuri sana wakati tunaomba vibali vya kuajiri watumishi wa umma tukazingatia mgawanyo sahihi wa rasilimaliwatu katika maeneo yetu kulingana na majukumu ya watumishi tunaowahitaji badala ya kuomba watumishi wengi ambao wanasababisha kuwa na ziada ambayo haitumika ipasavyo” Mhe. Kairuki amesema.

Waziri Kairuki amesema katika vibali 10,184 vilivyotolewa hivi karibuni na Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretarieti za Mikoa, Wakala za Serikali, pamoja na Taasisi na Mashirika ya Umma ili kujaza nafasi zilizoachwa na watumishi wa umma waliobainika kughushi vyeti vya elimu, Halmashauri ya Manisapaa ya Ubungo imetengewa jumla ya nafasi 140.

Aidha, ameongeza kuwa, Halmashauri hiyo imetengewa jumla ya nafasi za ajira mpya 397 kwa mwaka wa fedha 2017/2018 hivyo zitendewe haki kwa kuhakikisha watumishi watakaoajiriwa wanafanya kazi kwa mujibu wa mpango uliopo.

Mhe. Kairuki yuko katika ziara ya kikazi katika mkoa wa Dar es salaama kwa lengo la kukutana na watumishi wa umma na kusikiliza malalamiko, ushauri na changamoto zinazowakabili katika maeneo yao ya kazi ili kuweza kuzifanyia kazi na kuleta mabadiliko katika Utumishi wa Umma nchini ili kufikia malengo yaliyopangwa na Serikali.
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe. Kisare Makori akimkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) katika Ofisi za Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam leo.
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe. Kisare Makori akimkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) kuzungumza katika kikao kazi na viongozi na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam wakati wa ziara ya kikazi katika Manispaa hiyo leo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akizungumza na viongozi na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo (hawapo pichani) alipofanya ziara ya kikazi katika Manispaa hiyo ili kupokea maoni, ushauri na kusikiliza kero za watumishi wa umma leo Jijini Dar es Salaam.

TAARIFA YA MSIMA WA PROF. HENSLAY KABISAMA

$
0
0
Ndugu, Jamaa, Marafiki ,Familia na wote  tuliopatwa na msiba huu wa marehemu Professor  Henslay William Kabisama uliotokea huko Marekani Ontario ,California .

Familia itawasili kutoka Marekani siku ya Jumatano tarehe 19th July usiku.

Tutaanza maombolezo siku hiyo hiyo ya Alhamisi ya tar 19 nyumbani kwa marehemu Ursino  Victoria nyuma ya Ofisi za Halotel.

Siku ya Ijumaa  tar 21 July Mwili wa mpendwa wetu Prof Henslay Kabisama utawasili siku ya Ijumaa, tarehe 21st July saa tisa mchana.

Mazishi yatafanyika siku ya Jumamosi tarehe 22nd July. Ikitanguliwa Na Ibada ambayo itafanyika  katika kanisa la   St Alban Upanga saa saba kamili mchana na baada ya hapo tutaelekea  makaburi ya kinondoni kwa mazishi.

 Bwana alitoa na bwana ametwaa jina bwana libarikiwe.

KADA WA CCM LAWRENCE MABAWA AANZISHA KAMPENI YA MAGUFULI BAKI

$
0
0
Na Humphrey Shao-Globu ya Jamii.

Kada wa chama caha Mapinduzi (CCM) kutoka wilaya ya Sengerema Lawrence Mabawa ametangaza kampeni yake mpya itakayo kwenda kwa jina la 'MAGUFULI BAKI'.

Mabawa amesema kuwa Kama jinsi Watanzania na wasio Watanzania tunavyotambua kazi kubwa na nzuri ya kutetea na kupigania rasilimali za Taifa inayofanywa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dk. John Pombe Magufuli, Rais wa wananyonge na masikini wa Watanzania wote bila kujali jinsia, dini,kabila, kuchukuwa jukumu la kumpongeza na kumtia moyo Rais na Serikali yake na si kumkatisha tamaa.

" Mimi kama Mtanzania mzalendo na Kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) nimeamua kuchukuwa jukumu la kuanzisha kampeni ya ‘Magufuli Baki’ yenye lengo kumpongeza Rais kazi anayoifanya bila kujali itikadi zao. 

Kampeni ya Magufuli Baki itahusisha Mikoa yote ya Tanzania kwa kuwafikia wanafunzi wa Sekondary na wananchi kwa kufanya mikutano yenye nia njema ya kumwomba Mhe. Rais abaki katika msimamo wake wa kuwatetea Watanzania wanyonge na masikini"Amesema Mabawa.

Amesema kuwa Kampeni hii itawapa fursa wananchi kutoa maoni yao kupitia mikutano tutakayoifanya ambapo wataweza kutoa maoni kuhusu utendaji wa serikali kwa ujumla ikiwa ni kupongeza na hata kukosoa.

ametaja kuwa hili kukamilisha kampeni hii tutatumia Kurasa za Mitandao ya Kijamii maalum ambazo zimeandaliwa kwa kampeni hiyo ambapo tutaweka maoni na pongezi za kila mshiriki wa kampeni hiyo. Mbali na kutumia mitandao ya kijamii tutashirikiana bega kwa bega na vyombo vya habari pamoja na wanahabari kufanikisha kampeni hii.

Ameongeza kuwa lengo la kampeni hii mbali na kompongeza Mhe. Rais na Serikali yake pia tutapata fursa ya kuwasikiliza wananchi moja kwa moja ili kugundua ukweli halisi kutoka kwao wa namna gani wanaona utendaji wa serikali ya awamu ya tano.
Kada wa Chama cah Mapinduzi kutoka Wilaya ya Sengerema ,Lawrence Mabawa akizungumza na waandishi wa haabri juu ya kampmeni yake ya Magufuli baki ambayo ameitambulisha kwa Wanahabari kuhusu kuanza kampeni ya kumshinikiza Rais Magufuli aendelee kusimamia misimamo yake katika kuongoza nchi na kuacha kuyumbishwa na maneno ya kwenye mitandao
Afisa Habrai Idara ya Habari MAELEZO , Georgina Misama akimtambulisha Kada wa Chama cah Mapinduzi kutoka Wilaya ya Sengerema ,Lawrence Mabawa kwa Waandishi wa Habari.
Sehemu ya Waandishi walioshiriki mkutano huo wakimsikiliza Kada wa Chama cah Mapinduzi kutoka Wilaya ya Sengerema ,Lawrence Mabawa kwa makini
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live




Latest Images