Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live

WATOTO NA VIJANA WA KAMBI YA ARIEL WATEMBELEA MAKUMBUSHO YA KISUKUMA – BUJORA MWANZA

$
0
0

Watoto na vijana 50 kutoka mikoa ya Geita,Mwanza na Shinyanga wanaoshiriki katika kambi ya Ariel 'Ariel Camp 2017’  jijini Mwanza iliyoandaliwa na shirika la Ariel Glaser Pediatric Aids Healthcare Initiative (AGPAHI) linalojihusisha na mapambano dhidi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) na Ukimwi, wametembelea makumbusho ya kabila la Kisukuma   ‘Sukuma Museum’ ya Bujora Kisesa Mwanza ili kujifunza tamaduni na mila za Kisukuma. 
Bango linaloonesha makumbusho ya Kisukuma ya Bujora Mwanza,pichani kushoto ndiye mwanzilishi wa makumbusho hayo David Clement Fumbuka aliyezaliwa mwaka 1922 na kufariki dunia mwaka 1986.
Mwongozaji wa wageni katika makumbusho ya Kisukuma Bujora ,Yasinta Salum akielezea historia ya makumbusho hayo kwa watoto na vijana kutoka mikoa ya Shinyanga,Geita na Mwanza walioshiriki katika Kambi ya Ariel jijini Mwanza.
Yasinta akiendelea kutoa historia ya Makumbusho ya Bujora.


MTAALAMU WA UWANJA KUTOKA TIMU YA EVERTON ATOA VIFAA VYA KUTUNZA MAZINGIRA YA UWANJA WA TAIFA

$
0
0
Mtaalamu  kutoka Timu ya Everton Bw. Shane Mcgeown (kushoto) akitoa maelekezo ya matumizi ya  mashine ya kushindilia na kutoa uchafu kwa ajili ya kusafishia uwanja  kwa uongozi na maafisa wa Idara ya Maendeleo ya Michezo wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo  leo Jijini Dar es Salaam katika Uwanja wa Taifa.
 Mtaalamu  kutoka Timu ya Everton Bw. Shane Mcgeown (kulia) akionyesha   mashine ya kukatia majani  na  kusafishia uwanja  kwa uongozi na maafisa wa Idara ya Maendeleo ya Michezo wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo  leo Jijini Dar es Salaam katika Uwanja wa Taifa.
Mtaalamu  kutoka Timu ya Everton Bw. Shane Mcgeown (Mwenye kofia) akionyesha  mashine ya kubebea uchafu  katika ziara ya kukagua vifaa vinavyoyumika katika ukarabati wa uwanja  kwa uongozi na maafisa wa Idara ya Maendeleo ya Michezo wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo  leo Jijini Dar es Salaam katika Uwanja wa Taifa .
Mkurungezi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo ya Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bw.Yussuph Singo (kulia) akimpa mkono wa shukrani Mtaalamu wa Uwanja kutoka Timu ya Everton Bw. Shane Mcgeown (kushoto) baada ya kutoa maelekezo ya vifaa mbalimbali vya kutunza mazingira ya Uwanja wa Taifa leo Jijini Dar es Salaam.
 (Picha na Lorietha Laurence WHUSM).

INTRODUCING NEW AUDIO BY GALATONE "NAWEE"

MIPANGO MADHUBUTI YATAKIWA KATIKA MIRADI MBALIMBALI KATIKA KURAHISISHA HALMASHAURI KUKAMILISHA - MCHUMI MKURANGA

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 
Watendaji katika ngazi ya vijiji pamoja na kata wametakiwa kuwa na mipango madhubuti ya miradi yao kuitekeleza ili serikali iweze kuingiza katika bajeti . 
Hayo ameyasema leo Mchumi wa Halmashauri ya Mkuranga, Kaunga Amani wakati alipotembelea miradi ya ujenzi wa kituo cha afya Tengerea pamoja na Zahanati ya Dondwe. 
Kaunga amesema kuwa miradi ya ujenzi wa vituo hivyo vinatakiwa kufikia hatua ya boma ndipo Halmashauri inachukua kwa kumalizia ambavyo ni sawa na asilimia 80. 
Amesema kushiriki kwa wananchi katika miradi kutaka kuwa na umiliki wa kitu hicho kutokana na nguvu walizowekeza kaka miradi. 
Aidha amesema kuwa miradi hiyo ikifika katika hatua ya boma kati ya Agosti na Septemba mwaka huu basi wataiingiza katika bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019 ili nguvu za wananchi zisipotee bure. Hata hivyo amewataka wananchi kujitoa kwa nguvu kutekeleza miradi hiyo ili kuweza kuipa kazi halmashauri katika kupanga bajeti ya miradi hiyo. 
Diwani wa Kata ya Tengerea, Shaban Manda amesema kuwa wananchi wamekuwa wakitjjitoa katika uchangiaji wa nguvu zao katika hatua za awal za miradi. Amesema kuwa katika kata hiyo hakuna zahanati wala kituo cha afya hali ambayo ni hatari kwa wananchi pamoja na wanawake wakati wa kujifungua.
Diwani wa Kata ya Tengerea, Shaban Manda akizungumza na watendaji wa Halmashauri, vijiji juu ya uharakishaji wa miradi ili serikali iweze kuipokea leo 

Mwakilishi  wa Mbunge wa Mkuranga, Omary Kisatu , Mchumi wa Halmashauri ya Mkuranga, Kaunga Amani , pamoja na  Diwani wa Kata ya Tengerea, Shaban Manda  wakitembelea  mradi wa Ujenzi wa Zahanati  katika Kijiji cha Dondwe leo.

Mchumi wa Halmashauri ya Mkuranga, Kaunga Amani akitoa maelekezo kwa watendaji Vijiji na Kata wanaotekeleza miradi ya Ujenzi wa Kituo Afya, Zahanati  leo .Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

BENKI YA DTB KUPANUA WIGO WA HUDUMA ZAO MKOANI TANGA

$
0
0
BENKI ya Diamond Trust(DTB) Tawi la Tanga wanakusudia kupanua wigo wa huduma zao kwa wateja kwa kukarabati na kuongeza namba ya wahudumu ikiwa ni mkakakti wa ujio wa fursa mbalimbali mkoani hapa ukiwemo mradi mkubwa wa bomba la mafuta kutoka hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga.

Hayo yalibainishwa juzi na Meneja wa Benki ya Diamond Trust Bank Mkoani Tanga (DTB) Athumani Juhudi wakati futari iliyoandaliwa na Benki hiyo kwa wateja wao wa mkoa wa Tanga iliyofanyika kwenye ukumbi wa Tanga Beach Resort mjini hapa na kuhu dhuiwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wakuu wa wilaya za Handeni na Tanga.
Alisema wao wanakusudia kufanya hivyo ili kuweza kuendana na wigo mpana wa ukuaji wa uchumi kwa mkoa wa Tanga ambao unatarajiwa kufanyika kutokana na mradi huo mkubwa .
“Benki yetu ipo kwenye nafasi ya tano kati ya mabenki zenye amana kubwa za wateja hivyo tumeona kuwaandalia futari hiyo ni namna bora ya kuwashukuru wao kwa kuwasapoti”Alisema.
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella akizungumza wakati wa futari iliyoandaliwa na Benki ya DTB kwa ajili ya wateja wao mkoani Tanga  iliyofanyika kwenye hotel ya Tanga Beach Resort,kulia ni Shehe wa Mkoa wa Tanga,Juma Luwuchu na kushoto ni Meneja wa Benki ya DTB Mkoani Tanga,Athumani Juhudi
 MKUU wa wilaya ya Tanga,Thobias mwilapwa akizungumza wakati wa futari hiyo
 Shehe wa Mkoa wa Tanga,Juma Luwuchu akitoa neno kwenye futari hiyo
 Meneja wa Benki ya Diamond Trust BankMkoani Tanga (DTB) Athumani Juhudi akizungumza na waandishi wa habari.
Kwa habari kamili BOFYA HAPA

Diamond asema mwaka huu ni ngoma juu ya ngoma ( EFM TANZANIA)

MICHUZI BEAT: BEKA 1 FLAVOUR WA YAMOTO BAND

KUMBUKUMBU

$
0
0
Marehemu Edmund Lawrence Mushi

Kuzaliwa:07/12/1973
Kufariki:22/06/2015

Leo 22/06/2017 Umetimiza miaka miwili tangu umefariki Huko Houston,TX,USA.Sisi ndugu zako umetuachia Huzuni na pengo ambalo halitazibika.Unakumbukwa sana na watoto zako Luis(Anwar) na Jermaine.

Unakumbukwa na Baba yako Mzazi mzee Lawrence Mushi Kimbori,Wadogo zako Rudolf(dofu),Gaudence,Fulgence,Renatus(Kulwa),Claudia,Martha(Dotto/Manka) na Mary(Mkakeni).Unakumbukwa na Ukoo wote wa Kimbori na Massawe.

Unakumbukwa na ndugu Jamaa na marafiki zako wote.Pia Unakumbukwa na wanajumuiya wa Tanzania Houston Community (THC) Houston TX, USA.Bwana alitoa,Bwana ametwaa Jina lake Lihimidiwe,
Amen.

BALOZI SEIF AKUTANA NA MKUU WA JESHI LA POLISI NCHINI IGP SIMON SIRRO

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) Simon Sirro amesema mwamko mdogo wa kielimu walionao Wananchi wengi ndio unaopelekea ongezeko kubwa la vitendo vya udhalilishaji vinavyoendelea kushuhudiwa kufanyika kila kukicha katika maeneo mbali mbali hapa nchini.
Alisema baadhi ya Watu wakorofi wamekuwa wakitumia udhaifu huo kwa kuendeleza vitendo viovu dhidi ya Wanawake na Watoto ambao huathirika kiakili na kimwili na kuwapa wakati mgumu wa kuendelea na maisha yao ya kawaida ndani ya Jamii inayowazunguuka.
IGP Simon Sirro alieleza hayo wakati alipofika Ofisini kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Vuga Mjini Zanzibar kujitambulisha rasmi baada ya kuteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli kushika wadhifa huo.
Kamanda Sirro alimueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba katika kukabiliana na vitendo hivyo viovu vinavyoonekana kuleta fadhaa inalazimika kwa Jamii wakati huu kubadilika kwa kuwa tayari kutoa ushahidi pale wanaposhuhudia vitendo hivyo.
Alisema kesi yoyote inategemea kuendeshwa katika misingi na taratibu za Kisheria kwa kuzingatiwa ushahidi unaotolewa na mashahidi ili haki inapotolewa iende sambamba na stahiki ya pande zote husika.
Kamanda sirro aliitahadharisha Jamii inayopenda kulalamika zaidi kwamba nje ya kukosekana kwa ushahidi wa tuhuma zozote zinazowasilishwa Polisi na hatimae kwenye Ofisi ya Muendesha Mashtaka maana yake hakuna kesi itakayoendelea hata kama kuna mtu aliyedhulumiwa.
Alisema zipo kesi nyingi za udhalilishaji hasa zile za utelekezaji wa familia zinazofanywa na baadhi ya Wanaume zaidi upande wa Tanzania Bara zinazofikia zaidi ya asilimia 80% na kusababisha familia husika kukosa matunzo jambo ambalo huchangia ongezeko la Watoto wa Mitaani wanaokosa malezi ya Familia.

“ Tunafarajika kuona kwamba ipo Sheria ya adhabu dhidi ya Watu wanaotupa na kutelekeza Familia zao kwa upande wa Tanzania Bara ambayo imekuwa ikitumika na kupunguza matukio kama hayo ”. Alisema Kamnada Simon Sirro.

Akizungumzia hali ya Amani Nchini Tanzania Mkuu huyo wa Jeshi la Polisi Tanzania alimueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba Nchi bado iko shwari licha ya matukio ya hapa na pale yanayoshuhudiwa katika Maeneo ya Rufiji.
IGP Sirro kupitia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwaomba Wananchi waendelee kushirikiana na vikosi vya ulinzi katika kutoa Taarifa za matukio ya uhalifu, Ujambazi na Uhujumu Uchumi kwenye maeneo yao ili vyombo vya Ulinzi vitumie maarifa yake katika kuwasaka wahalifu hao.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) Simon Sirro Kushoto akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipofika Ofisini kwake Vuga kujitambulisha Rasmi baada ya kuteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli kushika wadhifa huo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akifafanua tatizo la Udhalilishaji dhidi ya Wanawake na Watoto linaloonekana kuathiri Jamii wakati akizungumza na Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) Simon Sirro.

Article 10

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AONYA KUHUSU MIMBA ZA UTOTONI

CRDB BANK tawi la Azikiwe Premier yaadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika kwa Kuwakumbuka Watoto Waishio Katika Mazingira Magumu

$
0
0
Benki ya CRDB ndio benki yenye huduma bora Tanzania kuliko benki nyingine yoyote, imeendeleo kuonyesha kuwajali Watanzania ambapo Menejmenti na Wafanyakazi wa CRDB Bank Tawi la Azikiwe Premier, la jijini Dar es Salaam, wameadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika, kwa kuwakumbuka watoto wanaoishi katika mazingira magumu, kwa kuwatembelea watoto wanaotunzwa katika kituo cha Jeshi la Wokovu kwa kuwapelekea zawadi mbalimbali za mahitaji muhimu, na kuwadhamini baadhi yao kwa kuwafungulia akaunti, kuwachangia, kugharimia elimu zao, na kugharimia mahitaji yao.

CRDB Azikiwe Premier Photo 8.JPG 
Wafanyakazi wa CRDB BANK, tawi la Azikiwe Premier, wakikabidhi zawadi mbalimbali kwa watoto wanaotunzwa katika kituo cha watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha Jeshi la Wokovu, Kurasini jijini Dar es Salaam, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika ilioadhimishwa na benki hiyo kwa wiki nzima sasa.
CRDB Azikiwe Premier Photo 7.JPG 
Mfanyakazi wa CRDB BANK, tawi la Azikiwe Premier, akikabidhi zawadi mbalimbali kwa watoto wanaotunzwa katika kituo cha watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha Jeshi la Wokovu, Kurasini jijini Dar es Salaam, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika ilioadhimishwa na benki hiyo kwa wiki nzima sasa.
CRDB Azikiwe Premier Photo 17.JPG 
Mkurugenzi na wafanyakazi wa CRDB Bank, Tawi la Azikiwe Premier, kwenye picha ya pamoja na mtoto Mariam Stephen Jackson, aliyekuwa akiishi katika mazingira magumu. Marriam pia amefunguliwa akauti maalum ya watoto ya benki hiyo iitwayo Junior Jumbo,ambayo wafanyakazi wa Tawi hilo la Azikiwe Premier, wananchangia kugharimia elimu yake. Sherehe hiyo imefanyika wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Africa ilioadhimishwa na benki hiyo kwa wiki nzima sasa.
CRDB Azikiwe Premier Photo 19.JPG 
Mkurugenzi na wafanyakazi wa CRDB Bank, Tawi la Azikiwe Premier, wakiwa na keki ya mtoto Mariam Stephen Jackson, aliyekuwa akiishi katika mazingira magumu. Marriam pia amefunguliwa akauti maalum ya watoto ya benki hiyo iitwayo Junior Jumbo,ambayo wafanyakazi wa Tawi hilo la Azikiwe Premier, wananchangia kugharimia elimu yake. Sherehe hiyo imefanyika wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Africa ilioadhimishwa na benki hiyo kwa wiki nzima sasa.
CRDB Azikiwe Premier Photo 5.JPG 

Mkurugenzi wa CRDB Bank, Tawi la Azikiwe Premier, Fabiola Musula, na wafanyakazi wa tawi hilo, na wateja, wakionyesha fedha walizomchangia mtoto Mariam Stephen Jackson, aliyekuwa akiishi katika mazingira magumu. Marriam pia amefunguliwa akauti maalum ya watoto ya benki hiyo iitwayo Junior Jumbo,ambayo wafanyakazi wa Tawi hilo la Azikiwe Premier, wananchangia kugharimia elimu yake. Sherehe hiyo imefanyika wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Africa ilioadhimishwa na benki hiyo kwa wiki nzima sasa.

Mradi wa maji wenye thamani ya shilingi milioni 68 wazinduliwa kwa wakazi wa Chang’ombe,jijini Dar

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia Serengeti (SBL), Helene Weesie (kulia) pamoja na Meneja Uwajibikaji wa SBL, Hawa Ladha (kulia) wakimtwika ndoo ya maji mkazi wa Chang'ombe B, Mgeni Hamisi Ramadhani leo ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji wenye thamani ya shilingi milioni 68 uliopo eneo la Chang’ombe ‘B’ wilayani Temeke, jijini Dar es Salaam. Mradi huo umefadhiliwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL).
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia Serengeti (SBL), Helene Weesie (kulia) pamoja na Diwani Kata ya Chang'ombe, Benjamin Ndalichako (kushoto) wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa mradi wa maji wenye thamani ya shilingi milioni 68 uliopo eneo la Chang’ombe ‘B’ wilayani Temeke, jijini Dar es Salaam. Mradi huo umefadhiliwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL).
Baadhi ya wananchi wakiwa katika mradi wa maji wenye thamani ya shilingi milioni 68 uliopo eneo la Chang’ombe ‘B’ wilayani Temeke, jijini Dar es Salaam. Mradi huo umefadhiliwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL).


KAMPUNI ya Bia Serengeti leo imezindua mradi wa maji wenye thamani ya shilingi milioni 68 uliopo katika eneo la Chang’ombe ‘B’ wilayani Temeke, jijini Dar es Salaam ikiwa ni jitihada za kuwaletea maji safi na salama wakazi wa eneo hilo.

Ukiwa na uwezo kwa kuhudumia watu 4,000 mradi huo unajumuisha kisima pamoja na mifumo yake, pampu ya maji inayotumia nishati ya jua na tenki la maji ambapo zinazalishwa lita 20,000 za maji kwa kila masaa ishirini na nne.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa SBL, Helene Weesie alisema kuwa mradi huo ambao unajulikana, “Maji kwa Uhai” ni miongoni mwa mikakati kama hiyo ambayo kampuni ya bia imeiendesha katika mikoa ya Iringa, Kilimanjaro, Mwanza, Tanga, Ruvuma, Dar es Salaam, Pwani na Dodoma ikiwa inawanufaisha zaidi ya watu milioni moja kwa maji safi na salama.

Weesie alisema kwamba mradi wa Chang’ombe sio tu kwamba utaboresha afya za wakazi wa eneo hilo bali pia utaongeza tija kiuchumi, “hususani kwa watoto wa kike na wanawake ambao hawatahitaji kutumia saa nyingi kutafuta maji safi sehemu nyingine. Hii inawapa fursa ya kuhudhuria shule wakiwa huru.”

AKINAMAMA WALIMA NYANYA KINYEREZI DAR WAJIFUNZA KILIMO CHA UYOGA

$
0
0
AKINAMAMA wanaojishughulisha na kilimo cha nyanya, spinachi, kabichi na mapapai kutoka Kinyerezi jijini Dar es Salaam wameamua kujifunza pia kilimo cha uyoga kutoka kwa wenzao wa Bunju ikiwa ni hatua ya kuongeza fursa ya ujasiriamali pamoja na kubadilishana uzoefu.

Wakiongozwa na Dkt. Sophia Mlote, akinamama hao wa kikundi cha Kinyerezi Green Voice wameamua kuchukua hatua hiyo katika awamu ya pili ya kutekeleza Mradi wa Green Voices unaolenga kuwawezesha wanawake kujihusisha na shughuli za kiuchumi zinazoendana na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na uhifadhi wa mazingira.

Ziara hiyo ya mafunzo ya siku moja ilifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita ikiwahusisha akinamama 13 wa kikundi hicho cha Kinyerezi ambao wanashiriki kilimo hai katika maeneo yao kwa kutumia mabanda maalum ambapo kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita wameweza kunufaika na bidhaa wanazozalisha.

Awamu ya pili ya mradi huo wa Green Voices imeanza mwezi Aprili 2017 na itaishia Aprili 2018, ambapo mradi huo unafadhiliwa na taasisi inayojihusisha na maendeleo ya wanawake wa Afrika, ijulikanayo kama Foundation for Women of Africa inayoongozwa na Makamu wa Rais mstaafu wa Hispania, María Teresa Fernández de la Vega.

Dkt. Mlote alisema kwamba, wameamua kwenda kujifunza kilimo chau yoga siyo tu katika kubadilishana uzoefu, bali pia kuongeza ujuzi ili kupata tija katika shughuli za kilimo rafiki wa mazingira katika utekelezaji wa mradi huo wa Green Voices.

“Tunataka kujifunza aina mbalimbali za kilimo kwa sababu hii ni fursa nzuri ya kumwezesha mwanamke kujiajiri na kuongeza pato kiuchumi,” alisema Dkt. Mlote.

Dkt. Mlote, ambaye ni Ofisa Mwandamizi katika Wizara ya Kilimo, Chakula na Mifugo, alisema mazingira walioyonayo katika kuendesha kilimo hifadhi cha nyanya, kabichi na mapapai huko Kinyerezi hhayana tofauti na mazingira ya kilimo cha uyoga kwani shughuli zote zinafanyika katika maeneo madogo ya nyumba zao huku wakihitaji kiasi kidogo cha maji.

Mafunzo kwa vitendo. Akinamama wa Kinyerezi Green Voices wakiweka udongo kwenye mifuko kama maandalizi ya kilimo cha uyoga.

Mafunzo ya nadharia: Mkufunzi wa kilimo chau yoga wa kikundi cha Bunju Tunza Women, Bi. Esther Chiombola, akitoa mafunzo kwa wanakikundi wa Kinyerezi Green Voices waliotembelea mradi wa akinamama wa Bunju kwa nia ya kubadilishana uzoefu. 
Mshiriki kiongozi wa kikundi cha akinamama walima uyoga Bunju, Bi. Magdalena Bukuku, akimkabidhi Dkt. Sophia Mlote kitabu cha namna ya kulima uyoga.

Mkufunzi wa kilimo chau yoga, Bi. Esther Chiombola, akiwapatia vipeperushi washiriki wa mafunzo hayo ya siku moja. 
Akinamama wa kikundi cha Kinyerezi Green Voices wakipita kwenye banda (shamba) la uyoga walipokwenda hivi karibuni kwa mafunzo ya siku moja ya kubadilishana uzoefu.

MRITHI WA DKT. MDEGELA KKKT DAYOSISI YA IRINGA, MCHUNGAJI BLASTON GAVILE, KUWEKWA WAKFU JUMAPILI

$
0
0
IBADA ya kuwekwa wakfu kwa Askofu Mteule wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Iringa, Mchungaji Blaston Tuluwene Gavile, inatarajiwa kufanyika Jumapili Juni 25, 2017 mjini Iringa.

Ibada hiyo, ambayo itaambatana na kuingizwa kazini kwa Msaidizi wa Askofu, Mchungaji Himid Sagga, itafanyika ikiandika historia kwenye Dayosisi hiyo ambapo Askofu Mteule Gavile anachukua nafasi ya Askofu Dkt. Owdenberg Moses Mdegela ambaye amestaafu.

Katibu Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Iringa, Nayman Chavalla, amesema tukio hilo maalum ni la pili katika historia ya Dayosisi hiyo, kwani Mchungaji Gavile anakuwa ndiye askofu wa pili tangu kuanzishwa kwake.

Aidha, katika ibada hiyo Askofu Mteule Blaston Gavile atamuingiza kazini Msaidi wake Mchungaji Himid John Sagga.Awali akielezea jinsi ibada hiyo itakavyokuwa, Chavalla alisema itaanza kwa maandamano ya Wachungaji na washarika kutoka Usharika wa Kanisa Kuu Iringa Mjini mpaka viwanja vya Gangilonga ambako ndiko ibada hiyo itafanyika.

"Ibada hiyo inatarajiwa kuongozwa na Mkuu wa KKKT, Askofu Fredrick Shoo akisaidana na Baba Askofu Mstaafu Dkt. Mdegella," alisema.

Pia katika ibada hiyo viongozi wa Makanisa mbalimbali hapa nchini na nje ya nchi, Wawakilishi wa vyama vya Kimisionari, Viongozi wa Kiserikali, vyama vya siasa, wageni kutoka nchi mbalimbali, wawakilishi wa makampuni na mashirika mbalimbali watahudhuria.

Katibu Mkuu alitoa wito kwa jamii na Wakristo wote kuendelea kuliombea jambo hilo.

Alimalizia kwa kusema ibada inatarajia kuanza kwa maandamanao yatakayoanza saa mbili kamili asubuhi.

MUNGU AIENDELEE KUIBARIKI DAYOSISI YA IRINGA NA TAIFA KWA UJUMLA
Askofu Mteule Mchungaji Blastone Tuluwene Gavile (kushoto) akiwa na Msaidizi wa Askofu Mteule Mchungaji Himid John Sagga.

JPM AWAFUNDA WANA BAGAMOYO KUHUSU UMUHIMU WA ARDHI, ATOA ONYO KWA WALIOJIPATIA FIDIA KWA ULAGHAI

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNE 23,2017

MADEREVA WAASWA KUZINGATIA SHERIA NA ALAMA ZA BARABARANI KUEPUKA AJALI

$
0
0
 Askari wa Usalama Barabarani akichukua maelezo ya gari Noah yenye namba za usajili T338 BVU iliopata ajali mapema jana,njia panda Goba,Mbezi Beach jijini Dar.Baadhi ya Mashuhuda wa tukio hilo walieleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa gari dogo (daladala pichani chini yenye namba za usajili T912 CVY),iliyokuwa imebeba abiria ikitokea Goba kwenda Mwenge,na hivyo gari hiyo kukosa mwelekeo kufuatia kona kali iliyopo eneo hilo,Katika ajali hiyo hakuna aliyepoteza maisha.

Mashuhuda hao pia wakatoa wito kwa baadhi ya Madereva kuwa makini,kufuata sheria na kuzingatia alama za barabarani,kwani kwa kufanya hivyo ajali nyingi zitapungua kutokea. 
  Daladala yenye namba za usajili T912 CVY ikiwa imeacha barabara na kuvamia mtaro kufuatia gari hiyo kupoteza uelekeo kwa kile lichodaiwa na Mashuhuda kuwa ni mwendo kasi na kutaka kugongana uso kwa uso na gari nyingine aina ya Noah (pichani juu),sehemu yenye kona kali.
Baadhi ya watu wakishuhudia ajali ya gari aina  daladala pichani yenye namba za usajili T912 CVY,ikiwa imeacha njia na kuvamia mtaro,kama ionekavyo pichani.katika ajali hiyo hakuna aliyepoteza Maisha

CRDB YAWAKARIBISHA WATEJA WAKE KATIKA MAONYESHO YA SABASABA

TRA WATAKIWA KUTOWATOZA KODI YA MAJENGO WAZEE WA MIAKA 60

Viewing all 110186 articles
Browse latest View live




Latest Images