Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live

WAZIRI UMMY AZINDUA HUDUMA YA UPANDIKIZAJI KIFAA CHA USIKIVU KWA WATOTO WENYE TATIZO LA KUTOKUSIKIA


RC KILIMANJARO ANNA MGHWIRA AANZA KAZI RASMI,AHANI MSIBA WA MZEE NDESAMBURO

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mghwira akisaini kitabu cha Wageni na baadaye kutoa pole kwa familia ya Marehemu Philemon Ndesamburo nyumbani kwake Kiboroloni, Moshi Mjini .
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mghwira ameshawasili mkoani kwake tayari kwa kuanza kazi rasmi,ambapo leo ameanza  majukumu yake kwa kukutana na kamati ya siasa  ya Mkoa huo.
 RC Mghwira akisaini kitabu cha Wageni kabla ya kuanza kuzungumza na kamati ya siasa ya mkoa wa Kilimanjaro mapema leo.
 Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,RC Anna Mghwira akisalimiana na viongozi mbalimbali wa kamati ya Siasa ya Mkoa,mapema leo
RC Mghwira akisalimiana na baadhi ya Wafanyakazi mara baada ya kuwasili nje ya ofisi yake,tayari kwa kuanza kazi kama Mkuu wa Mkoa mpya mkoani Kilimanjaro. 

Tanzania yafanikiwa kudhibiti mfumuko wa bei Afrika Mashariki

$
0
0
Benny Mwaipaja, WFM, Dodoma

Pamoja na malalamiko na manung’uniko ya hali ngumu ya maisha kwa watanzania wengi, Tanzania ndio yenye kiwango cha chini cha mfumuko wa bei wa wastani wa asilimia 6.1 kwa mwezi Mei 2017 kwa nchi za Afrika Mashariki.

Hayo yamebainishwa leo bungeni Mjini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akiwasilisha Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo kwa mwaka 2017/18.

Mhe. Dkt. Mpango amesema mfumuko wa bei katika nchi za Afrika Mashariki kwa mwaka 2016 uliendelea kuwa wa kiwango cha tarakimu moja, ambapo Rwanda ilikuwa na asilimia 7.1, Uganda asilimia 5.4, Tanzania asilimia 5.2, Kenya asilimia 6.3 na Burundi asilimia 5.6.

Alisema kufikia mwezi Aprili 2017, mfumuko wa bei kwa nchi hizi ulipanda, ambapo kwa Burundi ulifikia asilimia 21.10, Rwanda asilimia 13.0; Kenya asilimia 10.28; Uganda asilimia 6.4 na Tanzania asilimia 6.4. 

“Hata hivyo, kwa upande wa Tanzania mfumuko wa bei umeendelea kushuka mpaka asilimia 6.1 kwa mwei Mei 2017” amesema Dkt. Mpango

Mhe. Dkt Mpango amesema kwa miaka minne mfululizo, wastani wa mfumuko wa bei kwa Tanzania umeendelea kupungua, ukibaki katika kiwango cha tarakimu moja.

Amesema kwa mwaka 2016, mfumuko wa bei ulifikia wastani wa asilimia 5.2 ikilinganishwa na asilimia 5.6 mwaka 2015. Kupungua kwa wastani wa mfumuko wa bei nchini kulichangiwa kwa kiasi kikubwa na: mwenendo wa kushuka kwa bei za mafuta ya petroli katika soko la dunia na nchini; kuimarika kwa upatikanaji wa vyakula nchini na hivyo kuimarisha wastani wa bei; na kuwepo kwa sera madhubuti za usimamizi wa bajeti na fedha.

Mhe. Dkt. Mpango amesema mfumuko wa bei uliongezeka kidogo, ambapo ulifikia asilimia 6.4 mwezi Aprili 2017 lakini ukiwa ndani ya maoteo ya wastani wa tarakimu moja (asilimia 5 – 8) kwa mwaka 2017.

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI TAARIFA YA HALI YA UCHUMI 2016 NA MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA KWA MWAKA 2017/18

MSUVA AAHIDI USHINDI DHIDI YA LESOTHO JUMAMOSI

$
0
0
Winga wa timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' Simon Msuva amesema kuwa wanaamini watapata ushindi katika mchezo wao wa kufuzu kombe la Mataifa Afrika mwaka 2019 yatakayofanyika nchini Cameroon.

Taifa Stars inamenyana na timu ya taifa ya Lesotho mechi itakayopigwa siku ya Jumamosi majira ya saa 2 usiku kwenye Uwanja wa Chamazi.

Timu hiyo iliyoweka kambi ya wiki moja nchini Misri imerejea jana majira ya saa 6 mchana kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya mchezo huo.

Akizungumza na globu hii, Msuva amesema kuwa wao kama wachezaji wamefanya maandalizi ya kutosha kwa ajili ya mchezo huo siku ya Jumamosi na cha zaidi nawaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi.

Msuva amesema kuwa, mechi hiyi ni muhimu sana ili kuweza kuweka matumaini ya kuingia fainali za Mataifa Afrika na watakachokifanya ni kuhakikisha wanapata ushindi.

"Tumejipanga kuhakikisha tunashinda katika mchezo wetu dhidi ya Lesotho ili malengo yetu yaweze kutimia na kuingia fainali za mataifa Afrika," amesema Msuva.

Winga huyo amesema kambi ya nchini Misri imeweza kuwajenga kiushindani na hata ukiangalia mazingira ya kule na hali ya hewa hakuna tofauti.

Stars inakabiliwa na mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi dhidi ya Lesotho utakaofanyika siku ya Jumamosi katika dimba la Uwanja wa Chamazi.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

DC HAPI AIAGIZA TRA KINONDONI KUBORESHA MFUMO WA UKUSANYAJI KODI

$
0
0
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii 

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi ameiagiza Mamlaka ya mapato nchini TRA ngazi ya Wilaya ya Kinondoni kubadilisha mfumo wa ukusanyaji wa kodi ili kuongeza mapato ya serikali kutoka Bilioni 40 na kuendelea.

Hapi amesema hayo katika ufunguzi wa mkutano wa Baraza la Wafanyabiashara la Wilaya ya Kinondoni  katika hoteli ya Traventine Magomeni, amesema kuwa serikali ni lazima ikusanye kodi ambayo inatokana na wafanyabiashara.

Hapi amesema  kuwa  kufikia malengo ya zaidi ya  ukusanyaji wa sh. bilioni  40  kwa kuwaingiza katika mfumo wafanyabiashara ndogo ndogo (Machinga) kwa kuwa na vitambulisho maalum ili waweze kulipa kodi .

Amesema  kuwa kuwaingiza machinga katika mfumo  ndio utakuwa urasimishaji wa machinga hao kwa kuweza kukopesheka katika taasisi za fedha ikiwa ni pamoja kwa TRA  kuweka vituo vya forodha katika Bandari Bubu za Mbweni ili kudhibiti mizigo inayoingia kinyemela  kutokea visiwa Zanzibar.

Mkuu wa Wilaya, Hapi Amesema kuwa kumekuwa na tatizo la uwepo wa leseni feki za biashara ambazo zinatolewa na watu feki nje ya ofisi za TRA na Manispaa ili waweze kukwepa kodi na kutafuta rekodi mpya ya wafanyabiashara ambao wamekuwa wakibuka kila siku katika Wilaya hiyo ambao wanastahili kulipa kodi kwa kuanza kupewa elimu.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Wafanyabiashara Wilaya ya Kinondoni katika mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Traventine Magomeni.
Afisa Biashara wa Manispaa wa Manispaa ya Kinondoni, Mohamed Nyasama akizungumza juu ya hali ya biashara  katika Manispaa hiyo .
Sehemu Wajumbe wa Baraza la Wafanyabiashara la Wilaya ya Kinondoni katika mkutano uliofanyika katika Hotel ya Traventine Magomeni leo jijini Dar es Salaam

WAZIRI WA MALIASILI, PROF. JUMANNE MAGHEMBE AFANYA MAZUNGUMZO BALOZI WA FINLAND NA UJUMBE WA UBALOZI WA MAREKANI LEO MJINI DODOMA

$
0
0
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (kushoto) akizungumza na Balozi wa Finland nchini, Pekka Hukka ofisini kwake mjini Dodoma leo ambapo wamejadili namna ya kuimarisha sekta ya misitu nchini ikiwemo kuwakaribisha wawekezaji kutoka Finland kuwekeza katika viwanda vya kuchakata mazao ya misitu pamoja na uzalishaji wa nishati mbadala.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (katikati) akimsikiliza Balozi wa Finland nchini, Pekka Hukka (kulia) ofisini kwake leo mjini Dodoma. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali, Gaudence Milanzi. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza na Naibu Mkuu wa Ujumbe wa Ubalozi wa Marekani nchini, Inmi Patterson ofisini kwake mjini Dodoma leo ambapo wamezungumza kuimarisha mahusiano baina ya nchi hizo mbili katika kuendeleza sekta ya Maliasili hususan vita dhidi ujangili, kuongeza idadi ya watalii pamoja na mapato yatokanayo na utalii.
 Naibu Mkuu wa Ujumbe wa Ubalozi wa Marekani nchini, Inmi Patterson (katikati) akizungumza na Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe alipomtembelea ofisini kwake mjini Dodoma leo. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (katikati) akimkabidhi Naibu Mkuu wa Ujumbe wa Ubalozi wa Marekani nchini, Inmi Patterson majarida mbalimbali yanayozungumzia vivutio vya utalii vya Tanzania ofisini kwake mjini Dodoma. Kushoto ni Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali, Gaudence Milanzi (kushoto) akizungumza katika kikao hicho cha Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (katikati) na Naibu Mkuu wa Ujumbe wa Ubalozi wa Marekani nchini, Inmi Patterson leo mjini Dodoma. (PICHA NA HAMZA TEMBA - WMU)

Makamu wa Rais Mh. Samia Suluhu Hassan ashiriki kazi ya Uchomaji wa Nyavu Haramu

$
0
0


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ameagiza vyombo vya dola nchini kuwakamata bila kuwaonea huruma viongozi watakaobainika kujihusisha au kuhujumu kazi ya kupambana na uvuvi haramu nchini. 

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa agizo hilo wakati akishiriki katika zoezi la uchomaji wa zana haramu za uvuvi 5,662 kwenye eneo la Buhongwa wilayani Nyamagana mkoani Mwanza zilizokamatwa katika Ziwa Victoria. 

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema kumekuwa na tabia ya baadhi ya viongozi kushiriki katika shughuli za uvuvi haramu hivyo inabidi wachukuliwe hatua ili kukomesha kabisa tatizo la uvuvi haramu katika Ziwa Victoria na maeneo mengine nchini. 

Ameeleza kuwa uvuvi haramu katika Ziwa Victoria umekuwa ni tatizo sugu na hali ambayo imesababisha kupungua kwa samaki na mapato kwa Serikali ambayo ni muhimu kwa ajili ya shughuli maendeleo. 

Amesema licha ya uvuvi haramu kupunguza mapato ya Serikali kutoka kwenye viwanda hali ya ajira nayo sio nzuri zilizokuwa zinatoka kwenye viwanda ambazo zimepungua kwa asilimi 49. 

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amepongeza kazi kubwa iliyofanyika ya ukamataji wa zana haramu za uvuvi katika Ziwa Victoria na amewahakikishia viongozi wa mkoa wa Mwanza kuwa Serikali ipo pamoja nao katika kazi hiyo. 

“Serikali yenu itaendelea kushirikiana nayi katika kuhakikisha kuwa rasilimali za uvuvi katika Ziwa Victoria zinaendelea kuwepo kwa kuendelea kutoa fedha na vitendea kazi ili kuongeza ufanisi katika utendaji wa kazi kwa lengo la kuhifadhi ziwa Victoria” Amesisitiza Makamu wa Rais. 

Kwa upande wake, Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongela amesema oparesheni za uvuvi haramu katika Ziwa Victoria zitaendelea kuimarishwa ipasavyo mkoani Mwanza mpaka vitendo hivyo vikomeshwa. 

Amesema mkoa wa Mwanza ulikuwa na viwanda Sita vya kuchakata samaki lakini kutokana na kupungua kwa samaki katika Ziwa Victoria ni viwanda Vinne tu mpaka sasa ndio vinafanya kazi hali ambayo imepunguza kwa kiasi kikubwa mapato kwa Serikali na ajira kwa vijana mkoani huo. 

Mkuu huyo wa Mkoa wa Mwanza John Mongela ameeleza kuwa kutokana na viwanda hivyo kusitisha shughuli za uzalishaji zaidi ya watu mamia ya watu wamekosa ajira.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki kuchoma nyavu za uvuvi haramu kwenye dampo la Buhongwa, wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia kwenye shughuli za mazingira ambapo nyavu zilizotumika kwenye uvuvi haramu zimeteketezwa katika dampo la Buhongwa, wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 

MAJALIWA ASALIMIANA NA MABALOZI WA UINGEREZA NA MAREKANI- BUNGEN

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi wa Uingereza nchini, Mheshimiwa, Sarah Cooke kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma Juni 8, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi wa Marekani nchini, Mheshimiwa Inmi Patterson kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Juni 8, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Dk.Shein azungumza na Wauguzi na Wakunga

$
0
0


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wauguzi na Wakunga la Zanzibar walipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo,[Picha na Ikulu.] 08/06/2017.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wauguzi na Wakunga la Zanzibar walipokuwa wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) alipozungumza nao leo walipofika Ikulu Mjini Zanzibar,[Picha na Ikulu.] 08/06/2017.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la Wauguzi na Wakunga la Zanzibar pamoja na Viongozi wengine baada ya mazungumzo yalitofanyika katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo,[Picha na Ikulu.] 08/06/2017.

WAZIRI MWIGULU NCHEMBA AZINDUA ALBAMU YA KWAYA YA CECILIA MJINI MAFINGA

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Iramba Magaharibi Mwigulu Nchemba amezindua albamu ya kwaya ya Cecilia uliofanyika katika Kanisa la Katoliki Mjini Mafinga na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa mkoani humo.

Katika uzinduzi wa albamu hiyo, Mwigulu aliweza kuchangisha harambee ya uzinduzi na kufanikiwa kupata milioni 25 na kuzidi kufanikisha mafanikio ya kwaya hiyo.

Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa (CCM) Rose Tweve amesema kuwa anamshukuru sana Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Iramba Magaharibi Mwigulu Nchemba kwa kuweza kuwatembelea na kukubali kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo na kufanikisha zoezi zima la uzinduzi wa kwaya ya Cecilia.

"Namshukuru sana Waziri  Mwigulu kwa kuweza kukubali kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa kwaya ya Cecilia na kufanikisha zoezi zima ikiwemo kupatikana kwa milioni 25 ikiwa ni harambee ya uzinduzi,"amesema Rose.

Katika uzinduzi wa albamu hiyo baadhi ya viongozi mbalimbali waliweza kuwepo ikiwemo Mbunge wa Jimbo la Mafinga Cosato Chumi na Mkuu wa Wilaya Mafinga Jamhuri William.
Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Iramba Magaharibi Mwigulu Nchemba akiwa katika picha ya pamoja  Mchungaji wa Kanisa Katoliki la Mjini Iringa Leornad Muli na viongozi mbalimbali wa jimbo la Iringa Mjini akiwemo Mbunge wa Jimbo la Mafinga Cosato Chumi (wa nne kulia), Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa (CCM) Rose Tweve
 Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Iramba Magaharibi Mwigulu Nchemba akizindua albamu ya kwaya ya Cecilia katika kanisa la Katoliki la Mjini Mafinga akiwa ameambatana na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa (CCM) Rose Tweve
  Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Iramba Magaharibi Mwigulu Nchemba akiwa na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa (CCM) Rose Tweve (kulia) wakati wanawasili katika kanisa la Katoliki la Mjini Mafinga.. 
 Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Iramba Magaharibi Mwigulu Nchemba na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa (CCM) Rose Tweve wakiwa wanatoa sadaka  katika  Kanisa Katoliki la Mjini Mafingawakati wa uzinduzi wa Albamu ya kwaya ya Cecilia iliyozinduliwa mwishoni mwa wiki iliyopita.
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa (CCM) Rose Tweve akiwa anawasalimia waumini wa  Kanisa Katoliki la Mjini Mafinga akiwa amembatana na Mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri William wakati wa uzinduzi wa Albamu ya kwaya ya Cecilia iliyozinduliwa mwishoni mwa wiki iliyopita na Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Iramba Magaharibi Mwigulu Nchemba.
Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Iramba Magaharibi Mwigulu Nchemba akiwa na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa (CCM) Rose Tweve (kushoto) pamoja na Mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri William wakifuatilia misa katika  Kanisa Katoliki la Mjini Mafinga wakati wa uzinduzi wa Albamu ya kwaya ya Cecilia iliyozinduliwa mwishoni mwa wiki iliyopita.


    

TUME YA HAKI ZA BINADAMU YAMTEMBELEA KAIMU JAJI MKUU WA TANZANIA

$
0
0
JAJI1
Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe.Prof. Ibrahim Juma akiwa ofisini kwake na Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Bahame Nyanduga pamoja na ujumbe alioongozana nao. Ujumbe huo kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ulifika Ofisini kwa Kaimu Jaji Mkuu kwa ajili ya kujitambulisha kwake, kumpongeza kwa kuteuliwa pamoja na kuzungumzia masuala ya Ushirikiano baina ya Tume hiyo na Mahakama ya Tanzania.
JAJI2JAJI3

MATUKIO KATIKA PICHA: YALIYOJIRI KATIKA KIKAO CHA 44, MKUTANO WA SABA BUNGE LA 11 MJINI DODOMA LEO JUNI 08, 2017.

$
0
0


NGA1
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Job Ndugai akiongoza kikao cha 44 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 08, 2017.
NGA2
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais –(TAMISEMI) Mhe.George Simbachawene akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha 44 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 8, 2017.
NGA5
Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa akifurahia jambo na Mbunge wa Ndanda (CHADEMA) Mhe.Cecil Mwambe  katika kikao cha 44 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 8, 2017.

ZANTEL YATOA MSAADA WA SARUJI NA MABATI KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO WA MKOA WA KUSINI PEMBA

$
0
0

Mkuu wa Kampuni ya mawasiliano ya Zantel-Zanzibar, Bw. Mohamed Khatib Baucha (kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe. Mwanajuma Majid Abdallah mifuko ya Saruji kwa kwa ajili ya waathirika wa mafuriko yaliyotokea hivi karibuni katika mkoa huo. Zoezi la makabidhiano ya msaada huo lilifanyika jana mkoani humo ambapo Zantel walitoa jumla ya mabati 350 na Saruji mifuko 350, vyote vikigharimu Sh. 13 milioni.

Mkuu wa Kampuni ya mawasiliano ya Zantel-Zanzibar, Bw. Mohamed Khamis Baucha (kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe. Mwanajuma Majid Abdallah mabati kwa kwa ajili ya waathirika wa mafuriko yaliyotokea hivi karibuni katika mkoa huo. Zoezi la makabidhiano ya msaada huo lilifanyika jana kisiwani Pemba-Zanzibar ambapo Zantel walitoa jumla ya mabati 350 na Saruji mifuko 350, vyote vikigharimu Sh. 13 milioni.

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe. Mwanajuma Majid Abdallah akiwakabidhi wakuu wa wilaya za mkoa huo mabati yalitolewa na Kampuni ya Mawasiliano ya Zantel kwa ajili ya waathirika wa mafuriko yaliyotokea hivi karibuni katika mkoa huo. Zoezi hilo lilifanyika jana kisiwani Pemba-Zanzibar ambapo jumla ya mabati 350 na Saruji mifuko 350 kwa pamoja vilikabidhiwa na Kampuni ya Zantel. (Katikati) ni Mkuu wa Wilaya ya Chakechake Mhe. Salama Mbarouk Khatib na kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Mkoani Mhe. Hemed Suleiman Abdallah.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Kusini Pemba, Ndg. Yussuf Mohammed Ali (kushoto) akimtambulisha Mkuu wa Zantel-Zanzibar, Bw. Mohamed Khamis Baucha (wa pili kushoto) kwa Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe. Mwanajuma Majid Abdallah (hayupo pichani) kabla ya Mkuu huyo wa Zantel kukabidhi msaada wa Saruji na Mabati kwa ajili ya waathirika wa mafuriko mkoani humo. Msaada huo una gharama ya Sh 13 milioni na lilifanyika jana kisiwani Pemba-Zanzibar. Wa tatu Kulia ni Ofisa wa fedha na Utawala wa Tawi la Zantel–Pemba, Yakoub Fadhil Juma.

FAINALI YA SPORTPESA SUPER CUP NI TIMU ZA KENYA,YANGA YAONDOLEWA NUSU FAINALI

$
0
0
 Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MABINGWA Ligi Kuu Tanzania Bara Vodacom (VPL) Yanga leo wameaga amashindano ya SportPesa Super Cup kwa mikwaju ya penati 4-2 katika mchezo wa hatua ya nusu fainali yanayoendelea kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Mechi hiyo iliyochezwa katika uwanja wa Uhuru ulianza majira ya saa 8 kamili kwa kuzikutanisha timu ya Yanga dhidi ya AFC Leopard ya nchini Kenya.Mpaka dakika 90 za mpira zinamalizika timu hizo zilitoshana nguvu kwa kutoka suluhu na kuelekea kwenye mikwaju ya penati.

Timu zote zilionekana kushambulia kwa kupokezana lakini safu za ushambiaji hazikuwa makini na kupoteza nafasi walizozipata mara kadhaa.

Yanga walifanya mabadiliko kwa kumtoa Emanuel Martin na kuingia Said Musa, akatoka Maka Edward na kuingia Said Makapu, Yusuph Mhilu alitoka na kuingia Samwel Greyson na Pato Ngonyani alitoka na kuingia Babu Ally.
AFC Leopard wakafanya mabadiliko kwa kumtoa Abwao Marcus na kuingia Ingotsi Marselas.

Wachezaji waliopiga penati kwa upande wa Yanga ni Nadir Haroub, Obrey Chirwa ambao walipata na Said Makapu na Said Musa kukosa kwa upande wa Yanga.Kwa upande wa AFC Leopard ni golikipa Jan Otieno, Otieno Duncan, Bernad Mango na Katerega Allan ambao walipata na Ingotsi Marselas alikosa.
Beki wa Yanga, Juma Abdul, (kulia) akiruka kuwania mpira na beki wa AFC Leopards Abwao Marcus, wakati wa mchezo Nusu Fainali wa mashindano ya SportPesa Super Cup, uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, leo. Katika mchezo huo AFC Leopards wameibuka na uwashinda wa mikwaju ya penati 4-2 baada ya kumalizika dakika 90 kwa sare ya 0-0.
Mshambuliaji wa Yanga Juma Mahadhi (kulia) akiwania mpira na Kiungo wa AFC Leopards, Alan Katerega, wakati wa mchezo Nusu Fainali wa mashindano ya SportPesa Super Cup, uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Mshambuliaji wa Yanga Juma Mahadhi (kulia) akimtoka mpira na beki wa AFC Leopards, Abdallah Salim, wakati wa mchezo Nusu Fainali wa mashindano ya SportPesa Super Cup, uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. 

Mshambuliaji wa Yanga Obrey Chirwa, akijiandaa kupiga shuti huku akizongwa na mabeki wa AFC Leopards, wakati wa mchezo Nusu Fainali wa mashindano ya SportPesa Super Cup, uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

DED MSALALA: MFUMO WA UHASIBU NA UTOAJI TAARIFA - FFARS NI TIBA YA HATI ZA MASHAKA KWENYE HALMASHAURI

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga Simon Berege ameupongeza mfumo mpya wa uhasibu na utoaji taarifa za fedha kwa ngazi ya kituo cha kutolea huduma ‘Facility Financial Accounting and Reporting System – FFARS na kueleza kuwa mfumo huo ni suluhusisho la hati zenye mashaka katika halmashauri mbalimbali nchini.

Mfumo wa FFARS unatekelezwa katika mikoa 13 kwenye halmashauri 93 kwa ushirikiano wa serikali na mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma ‘ Public Sector Systems Strengthening – PS3’ unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID) pamoja na Mradi wa Tuimarishe Afya ‘ Health Promotion and System Strengthening – (HPSS) unaofadhiliwa na watu wa Uswizi (Swiss Tropical and Public Health Institute). 

Akifungua mafunzo kuhusu mfumo huo kwa maafisa elimu kata na Waganga Wafawidhi katika vituo vya afya kutoka kata 18 za halmashauri ya Msalala,yaliyofanyika leo katika ukumbi wa Submarine Hotel mjini Kahama,Berege alisema mfumo wa FFARS ni mwarobaini wa tatizo la halmashauri kupewa hati zenye mashaka. 

Alisema mfumo huo utawezesha takwimu nyingi za halmashauri za wilaya kukusanywa kwa usahihi zaidi kutoka vituo vya kutolea huduma ambavyo vitakusanya na kuhifadhi taarifa za mapato na matumizi ya fedha za serikali kwa kutumia mfumo huo. 

“Takwimu ni tatizo la kitaifa,hivyo mfumo huu utasaidia kuondoa tatizo hili kwa kuongeza uwazi na umakini katika masuala ya uhasibu na utoaji taarifa za fedha”,alieleza Berege. “Halmashauri zimekuwa zikipata hati zenye mashaka kwa sababu uwekaji takwimu haupo vizuri,FFARS ni tiba ya hati zenye mashaka,pamoja na kuendelea kutumia njia za vitabu/makaratasi,ni vyema halmashauri zikawa tayari kutumia njia za ki- elektroniki katika utunzaji takwimu”,aliongeza Berege. 

Aidha alilishukuru Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID) kwa kufadhili mradi huo na kuwataka watanzania kuutumia vizuri ili kuleta maendeleo katika halmashauri. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga Simon Berege akifungua kuhusu mfumo mpya wa uhasibu na utoaji taarifa za fedha kwa ngazi ya kituo cha kutolea huduma ‘Facility Financial Accounting and Reporting System – FFARS kwa maafisa elimu kata na waganga wafawidhi katika vituo vya afya kutoka halmashauri hiyo leo Alhamis June 8,2017 katika ukumbi wa Submarine Hotel mjini Kahama 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala Simon Berege akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala Simon Berege akifungua mafunzo hayo.Kushoto ni Mshauri wa kifedha kutoka PS3,Osoro Otieno,kulia ni Mratibu wa PS3 Halmashauri ya Msalala,Elikana Zabron .

SPIKA NDUGAI APATA UGENI WA BALOZI WA MOROCCO NCHINI TANZANIA PAMOJA NA KATIBU MKUU WA CCM TAIFA LEO OFISINI KWAKE MJINI DODOMA.

$
0
0
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia) akisalimiana na Balozi wa Morocco nchini Tanzania, Mheshimiwa Abdelilah Benryane (kushoto) pale alipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia)akizungumza jambo pale alipopata ugeni wa Balozi wa Morocco nchini Tanzania, Mheshimiwa Abdelilah Benryane (kushoto) katika kikao kilichofanyika leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia)akimsikiliza Balozi wa Morocco nchini Tanzania, Mheshimiwa Abdelilah Benryane (kushoto) katika kikao kilichofanyika leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akisisitiza jambo pale alipopata ugeni wa Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Ndg. Abdulrahman kinana (kulia) katika kikao kilichofanyika leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Ndg. Abdulrahman kinana (kulia) pale alipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati) akipiga picha ya pamoja na katibu Mkuu wa CCM Taifa, Ndg. Abdulrahman kinana (kulia) pale alipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma, kushoto ni katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah.

(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

ALIYOZUNGUMZA PROF ELISANTE OLE GABRIEL KATIKA MKUTANO WA SABA WA AFRICAN DIGITAL TV DEVELOPMENT

TANZANIA'S BUDGET SPEECH 2017 - 2018

JUST IN: BAJETI KUU YA SERIKALI MWAKA 2017/2018 ILIYOWASILISHWA BUNGENI MJINI DODOMA

$
0
0
WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2017/18
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live




Latest Images