Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110171 articles
Browse latest View live

MWELEKEO WA MVUA ZA MASIKA NCHINI TANZANIA MARCH - MEI, 2017


MICHUZI TV: SIMON MWAKIFWAMBA AFUNGUKA JUU YA TAARIFA FEKI ILIYOSAMBAZWA MITANDAONI

KAMA ULIKOSA KUANGALIA MECHI YA YANGA NA SIMBA JUMAMOSI HII HAPA DAKIKA 90 ZOTE

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA MKUU WA MKOA WA SIMIYU

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka aliyemtembelea Makamu wa Rais ofisini kwake leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwake, Ikulu jijini Dar es salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana na Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwake ,Ikulu jijini Dar es Salaam.

(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Askofu  Mokiwa aondoa kesi mahakamani.

$
0
0
Na Karama Kinyunko-Glob ya Jamii.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeondoa kesi ya madai iliyofunguliwa na aliyekuwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Dar es Salaam, Dk. Valentino Mokiwa.

Kesi hiyo imeondolewa leo baada ya Wakili ambaye ni muwakilishi wako kisha Askofu Mokiwa, Mathew Kabunga kuiomba Mahakama kuiondoa kwai hiyo chini ya kifungu cha sheria cha 23(2)(b).

Akiqasilisha ombi hilo mbele ya Hakimu Mkazi, Thomas Simba alisema" mheshimiwa, Nina hoja."" Baada ya kujadiliana na mteja wangu (Mokiwa) hayupo tayari kuendelea na kesi, tu naomba kuiondoa chini ya kifungu cha 23(2)(b).

Wakili wa upande wa wadaiwa, Emmanuel Nkoma amekubaliana na ombi hilo la mdai kwa kuwa yeye ndiye aliyepeleka shauri mahakamani.

Aidha aliiomba Mahakama wamuamuru mdai kulipa garama za kesi kwa kuwa wadaiwa walishaingia garama za kuwaweka mawakili na zile za kuendeshea kesi

Hakimu Simba hakuwa na pingamizi, aliwataka upande zote mbili kukaa na kujadiliana garama za kesi.Mapema Askofu Mokiwa alifungua kesi ya madai mahakamani akiiomba itengue uamuzi wa kuvuliwa uaskofu na kumtangaza kuwa askofu.

Dk. Mokiwa kwa kupitia kampuni ya uwakili ya M. B Kabunga and Co. Advocates, Mathew Kabunga, alifungua kesi hiyo namba 20, ya mwaka huu, dhidi ya Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dk. Jacob Chimeledya na bodi ya wadhamini ya kanisa hilo, akipinga kuvuliwa uaskofu.

Kwa kupitia hati yake ya maadai, Dk. Mokiwa anadai kwamba waumini takriban 28, wa kanisa hilo, waliandika barua ikiwa na mashitaka 10, dhidi yake, lakini barua hiyo haikuwasilishwa kwake na ilionesha kuna nakala.

Januari 7, mwaka huu, Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dk. Chimeledya alimvua uaskofu mkuu Dk. Mokiwa, kutokana na mashitaka 10, aliyofunguliwa na walei 32, wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Dar es Salaam, yakiwemo ya ufisadi wa mali za kanisa.
 Wakili Mathew Kabunga,  anayemuwakilisha Askofu Valentino Mokiwa, akiondoka katika viunga vya mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya ombi lake la kuiondoa kesi ya madai iliyofunguliwa na Askofu Mokiwa kupinga kuvuliwa uaskofu kuondolewa.
Wakili  wa wadaiwa katika kesi ya madai iliyofunguliwa na Askofu Mokiwa,  dhidi ya Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglicana Tanzania, Jacob Chimeledya na Bodi ya wadhamini ya kanisa hilo, Emmanuel Nkoma akifafanua jambo kwa waandishi wa habari.

wananchi watakiwa kuzibua mitaro katika kipindi hiki cha mvua

$
0
0

Na Karama Kenyunko, blog ya jamii

Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA), amewataka wananchi kuzibua mitaro ili kuepuka mafuriko yanayoweza kutokea katika mvua za masika za mwezi Machi hadi Mei Mwaka huu.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dk. Agnes Kijazi amesema licha ya kwamba mvua hizo zinatarajiwa kuwa za wastani na nyingeni juu ya wastani katika maeneo mingi nchini ni vema wananchi wakachukua tahadhari mapema.

Amesema kuwa, taadhari hizo zitasaidia wananchi kuondokana na kukumbwa na mafuriko kwa baadhi ya maeneo nchini, kuepuka vifo na magonjwa ya mlipuko.

Aidha amewataka wananchi kutunza maji katika mvua hizo zinazoanza kunyesha ili kuepuka athari za upungufu wa maji uliojitokeza

Aliongeza kuwa, msimu wa mvua za November hadi Aprili mwaka huu ni mahususi kwa maeneo ya Magharibi mwanchi, kanda ya kati, nyanda za juu kusini-magharibi, kusini mwa nchi na pwani ya kisini.

Amesema mvua katika mikoa ya Njombe, Songwe Ruvuma, Mtwara, Lindi, pamoja na eneo la Morogoro Kusini (Mahenge) zinatarajiwa kuwa za wastani.

Aidha aliongeza kuwa katika mvua zinazoendelea katika mikoa ya Kigoma, Tabora, Katavi na Rukwa zinatarajiwa kuwa za wastani hadi juu ya wastani na pia zinatarajiwa kuisha katika wiki ya pili na ya tatu ya mwezi Aprili mwaka huu

"Mikoa ya Mbeya, Songwe, Iringa, Njombe, kusini mqa Morogoro na ile ya kusini na pwani ya kusini inatarajiwa kuwa na mvua za wastani.

Dk Kijazi Aliongeza kuwa mvua za msimu huu zinatatarajia kuisha katika wiki ya nne ya mwezi Ap. rili hadi wiki ya kwanza ya mwezi Mei mwaka hui.
Mkurugenzi wa Mkuu wa TMA Dk. Agnes Kijazi akizungumza na wanahabari juu ya mwelekeo wa mvua za masika za mwezi Machi  hadi Mei mwaka huu.Leo jijini Dar es Salaam.
Wanahabari wakimsikiliza Dk. kijazi kwenye  mkutano wa Uelekeo wa mvua za Masika mwezi Machi hadi Mei mwaka huu Leo jijini Dar Es Salaam.
Mkurugenzi wa utafiti wa Mamlaka ya Hali ya Hewa, Ladislaus Chan'ga akifafanua jambo mbele ya wanahabari Leo jijini, kulia ni Mkurugenzi Mkuu Dk. Kijazi

MEYA ILALA AFUNGUA RASMI DARAJA LA BONYOKWA-KINYEREZI

$
0
0
MSTAHIKI MEYA wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko jana alifungua rasmi daraja linalounganisha Kata ya Bonyokwa na Kata ya Kinyerezi katika Manispaa ya Ilala, jijini Dar es salaam.

Awali akizungumza katika hafla hiyo Mhandisi wa Manispaa ya Ilala ndugu Benjamin Maziku alisema  daraja hili limejengwa kwa takribani mwaka mmoja na kugharimu Tsh.million  478 hadi kukamilika kwake leo hii. Ujenzi wa daraja hili umesua sua kwa siku nyingi kutokana na sababu mbali mbali lakini kutokana na usimamizi imara wa Mstahiki Meya wa Ilala Mhe. Charles Kuyeko sasa historia imebadilika.

Meya Kuyeko akizungumza na umati wa wananchi waliokusanyika kushuhudia ufunguzi huo amewasitiza kulilinda na kulitunza vyema daraja hilo kwani limejengwa kwa kodi zao.

Awali, Meya akitoa historia ya daraja hilo amesema kuwa, waliokuwa wanatakiwa kujenga daraja hilo ni wakala wa Barabara Tanzania (Tanroad) lakini kutokana na kusuasua kwao, Mimi (Meya)  niamua kuingilia kati kwa Manispaa kutenga Fedha kujenga daraja la muda ili kuwasaidia wananchi wa Bonyokwa kuondokana na atha ya kuwa Kisiwa hususani wakati wa Mvua.
 Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko, akihutubia wananchi baada ya kufungua rasmi  daraja linalounganisha Kata ya Bonyokwa na Kata ya Kinyerezi katika Manispaa ya Ilala, jijini Dar es salaam.
 Mbunge wa Viti Maalumu, Anatropia Theonesti (Chadema) akihutubia wakati wa ufunguzi wa daraja hilo
 Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko, akikiwa amekata utepe ikiwa ni ishara ya  kufungua rasmi  daraja linalounganisha Kata ya Bonyokwa na Kata ya Kinyerezi katika Manispaa ya Ilala, jijini Dar es salaam.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

WAZIRI DK.CHARLES TIZEBA KUFUNGUA KONGAMANO LA WADAU WA KILIMO JIJINI DAR ES SALAAM KESHO

$
0
0
Enles Mbegalo


WAZIRI wa Kilimo ,Chakula,Mifugo na Uvuvi Dk. Charles Tizeba (pichani), anatarajia kufungua kongamano la siku  tatu la wadau wa sera za kilimo kesho jijini Dar es Salaam.


Aidha, kongamano hilo litahudhuriwa na wadau zaidi ya 200 kutoka nchi mbalimbali.


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa  Kampuni ya Agricultural Non State Actors Forum (ANSAF), Audax Rukonge, alisema serikali imekusudia kuweka kipaumbele kwenye viwanda vya uchakataji wa mazao ya kilimo.


Kongamano hilo litalenga kuongeza uelewa miongoni mwa watunga sera kuhusu mchango wa kilimo katika kuhamasisha ukuaji wa viwanda Tanzani.


“Wadau  watajadili kupata tafsiri halisi ya sekta ya uchakataji mazao ya kilimo katika muktadha wa mageuzi ya viwanda Tanzania,”alisema


Rukonge alisema kongamano hilo limedhaminiwa na USAID, Benki ya Dunia,ANSAF,JICA na wadau wengine ambao wamesaidia kuleta watalamu wakiwamo wakulima, watafiti,wafanyabiashara na watunga sera.


Mratibu wa Jukwaa la Sera ya Kilimo na Mchumi mwandamizi Wizara ya Kilimo, Sophia Mlote alisema kongamano hilo la tatu litajadili maendeleo ya kilimo nchini ikiwamo kujadili namna ya kutetea sera,sheria,kanuni.


Pia alisema kongamano hilo litajikita katika kujadili juu ya mpango wa kilimo cha mihogo,mikunde, samaki, mazao, usafirishaji pamoja na vifungashio kwa kuwa wazalishaji wengi hawana vifungashio.



NHIF YATOA ELIMU KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA

$
0
0
 Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Ally Mwakababu akizungumza wakati wa kikao cha pamoja baina yao na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Mkinga kuhusu umuhimu wa kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) ili waweze kunufaika na huduma zitolewazo
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mkinga,kushoto ni Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)Ally Mwakababu kulia ni Mratibu wa CHF wilaya ya Mkinga,Rashid Gembe
Afisa Matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Miraji Kisile akieleza umuhimu wa watumishi wa halmashauri hiyo kujiunga na mfuko huo ili kuweza kunufaika na huduma zinazotolewa wakati wa kikao hicho kilichofanyika ukumbi wa Halmashauri hiyo.
Daktari akiwapima baadhi ya watumishi wa halmashauri huo

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA KAMISHNA ANDENGENYE

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye, ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).

WASANII WALIOSHIRIKI KAMPENI 2015 (MAMA ONGEA NA MWANAO) WAPINGA UVUMI ULIOENEA KUWA HAWAKULIPWA

$
0
0
Na Chalila Chibuda wa Blogu ya Jamii.

Baadhi ya wasanii walioshiriki katika kampeni 2015 (Mama ongea na mwanao) wamepinga uvumi ulioenea kuwa wasanii hao waliofanya kampeni nchi nzima na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassani hawakulipwa.

Akizungumza leo na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam,msemaji wa Mama Ongea na Mwanao,Ndumbago Misayo (Thea) amesema taarifa hizo za kutokulipwa katika kampeni sio za kweli na kinachofanyika ni kumchafua Makamu wa Rais ,Mama Samia pamoja na kikundi cha wasanii walioshiriki kampeni za uchaguzi 2015.

Kwa upande wake mwenyekiti wa muda wa kundi hilo, Yobnesh Yussuf (Baturi) amesema shutuma hizi zinatokana na baadhi ya wasanii kushawishiwa kuongea uongo kwa masilahi yao.

"Wasanii wote tumelipwa na mikataba ipo na haiwezekani mtu mwenye jina ukajitokeza mbele ya vyombo vya habari kuzungumza uongo wakati wewe ndio uliokuwa unalipa wenzio hicho kitu hakiwezekani" amesema.

Aliongeza kuwa kundi la Ongea na Mwanao bado lipo na linaendelea vizuri chini ya Makamu wa Rais , Mama Samia Hassan Suluhu.

"Msanii aliotangaza kuwa sisi wasanii hatujalipwa ni Wema Sepetu wakati yeye ndio alikuwa mlipaji wa kundi hilo.
 Msemaji wa Mama Ongea na Mwanao,Ndumbago Misayo (Thea) akizungumza na waandishi wa habari juu ya taarifa katika mitandao ya kijamii  inayodai kuwa wasaanii waliozunguka na Makamu wa Rais, Samia Hassan Suluhu hawakulipwa  leo jijini Dar es Salaam.kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Mama Ongea na Mwanao, Yobnesh Yussuf (Baturi). Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.
 Makamu Mwenyekiti wa Mama Ongea na Mwanao, Yobnesh Yussuf (Baturi) akizungumza katika mkutano  na waandishi habari juu ya madai ya kutolipwa katika kampeni za mwaka 2015  leo jijni Dar es Salaam. kulia ni Msemaji wa Mama Ongea na Mwanao, Ndumbago Misayo (Thea)
Baadhi ya wasanii wakiwa katika picha ya pamoja leo jijini Dar es Salaam.

WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI YAHAMIA MAKAO MAKUU YA SERIKALI DODOMA KUANZIA 13 FEBRUARI, 2017.

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU VIFUNGASHIO VYA POMBE KALI – VOROBA

$
0
0


Mtakumbuka tarehe 20 Februari 2017 Ofisi ya Makamu wa Rais ilitoa tamko la Serikali la utaratibu utakaotumika kutekeleza agizo la kusitisha utengenezaji, uuzaji na matumizi ya pombe kali zinazofungashwa kwenye vifungashio vya plastiki (viroba)kuanzia tarehe 1 Machi 2017. Utekelezaji wa katazo hili utazingatia Ibara ya 8(1) (b) na 14, Sheria ya Mazingira ya mwaka 2004 na Kanuni zake zilizotungwa kupitia kifungu 230 (2) (f) cha sheria hiyo, na Sheria ya Leseni za Vileo Namba 28 ya mwaka 1968 pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2012.

Napenda kusisitiza na kuujulisha umma wa Tanzania kuwa utekelezaji wa maamuzi haya ya Serikali kuhusu usitishaji uingizaji, uzalishaji, uuzaji na matumizi ya vifungashio vya plastiki vya kufungia pombe kali utaanza rasmi tarehe 01 Machi, 2017, katika Mikoa yote ya Tanzania Bara. 

Operesheni ya kukagua utekelezaji wa agizo la serikali la usitishaji utengenezaji, uuzaji na matumizi ya pombe zinazofungashwa kwenye vifungashio vya plastiki itaendeshwa nchini kote kuanzia tarehe 2 Machi 2017 kwa kupitia Kamati za Ulinzi na Usalama na Kamati za Mazingira katika ngazi ya Mkoa, Wilaya, Tarafa, Kata, Vijiji na Mtaa. Kamati hizi zitawajibika kuwasilisha taarifa za operesheni wakati na baada ya operesheni hiyo Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na nakala Ofisi ya Makamu wa Rais.

Mnamo terehe 24 Februari 2017, kiliitishwa kikao cha Mawaziri na viongozi wa taasisi za Serikali kujadili mpango wa utekelezaji wa zuio hili. Katika kikao hicho, Wizara na taasisi za Serikali zilipewa majukumu mbalimbali, kama ifuatavyo: 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Mamkamba. (MB) akitoa Taarifa kwa Umma kuhusu marufuku ya uzalishaji, uingizaji , usambazaji,na matumizi ya vifungashio vya plastiki maarufu kama viroba vinavyotumika kufungashia pombe kali, alipozungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake Mtaa wa Luthuli Jijini Dare es Salaam Leo.
Katikati Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba. (MB) akitoa Taarifa kwa Umma kuhusu marufuku ya uzalishaji, uingizaji , usambazaji,na matumizi ya vifungashio vya plastiki maarufu kama viroba vinavyotumika kufungashia pombe kali, kulia ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Profesa Faustin Kamuzora na Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Mazingira, Waziri Makamba alizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake mtaa wa Luthuli Jijini Dare es Salaam Leo.

MWAKIFAMBA AKANUSHA UJUMBE ULIONEZWA MITANDAONI

$
0
0
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.

Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifamba amekana kuhusika na utumaji wa ujumbe katika mitandao ya kijamii juu ya kuitisha mkutano na waandishi wa habari. 

Kauli hiyo imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Rais wa Shirikisho hilo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya ujumbe huo uliokuwa ukisambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii na kumuhusisha Rais wa Shirikisho hilo. 

Mwakifamba amesema kuwa ujumbe huo umeeleza kuwa Rais wa shirikisho hilo atakuwa na mkutano na waandishi wa habari utakaohusu wasanii waliokipigia kampeni Chama cha Mapinduzi (CCM) na kutolipwa fedha zao pamoja na kuunga mkono jitihada za msanii Wema Sepetu kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

“Kiukweli sikushiriki kwa namna yoyote katika kuuandika ujumbe huo na nimesikitishwa kuona kwamba huo ujumbe unasambazwa ukiwa na jina langu hivyo umeniletea picha mbaya kwani ni kinyume na taratibu na sheria za Shirikisho,”alisema Mwakifamba.

WAZIRI MKUU ANUSA MADUDU MINADA YA MADINI

$
0
0
*Amuagiza Kamishna wa Madini aende Mererani
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema anafuatilia kwa makini minada ya madini inayofanyika nchini kwa sababu anazo taarifa za kukiukwa utaratibu kwenye minada hiyo.

Amesema ukiukwaji huo unachangia kutobadilika kwa mapato ya mauzo yatokanayo na mnada hata kama kuna vito viliyokakatwa au havijakatwa.

Ametoa kauli hiyo jana jioni (Jumatatu, Februari 27, 2017) wakati akihitimisha kikao alichokiitisha kwenye makazi yake Oysterbay jijini Dar es Salaam kilichojumuisha Mawaziri wa Fedha pamoja na Nishati, Mkuu wa Mkoa wa Manyara na watendaji wake, Mbunge wa Simanjiro, wamiliki wa mgodi wa Tanzanite One, watumishi waliofukuzwa kazi na wachimbaji wadogo. 

Alisema licha ya kuwa Kitengo cha Uthaminishaji wa Madini ya Almasi na Vito cha Wizara ya Nishati na Madini (TANSORT) kinasifiwa kwa kuongeza mapato ya madini, bado kuna kazi ya ziada inabidi ifanyike kwenye minada hiyo ili Serikali iweze kunufainika na madini hayo.

“Uzoefu wa kwenye minada ya korosho unaonyesha kuwa wanaushirika ndiyo wanaiba fedha za wakulima. Nimekuwa ninafuatilia kwa muda sasa uendeshaji wa hii minada na sijaridhishwa na uendeshaji wake. Hakuna tofauti ya bei madini ya Tanzanite yanapokuwa yamekatwa au la,” alisema.
 Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa akisisitiza jambo katika kikao alichokiitisha kuhusu masuala ya madini kati yake na viongozi wa Serikali, viongozi wa kampuni ya uchimbaji madini ya Tanzanite One na baadhi ya wachimbaji wadogo ,kwenye Makazi yake Oysterbay jijini Dar es salaam jana  Februari 27, 2017. 
 Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika kikao alichokiitisha kuhusu masuala ya madini kati yake na viongozi wa Serikali, viongozi wa kampuni ya uchimbaji madini ya Tanzanite One na baadhi ya wachimbaji wadogo,kwenye makazi yake, Oysterbay jijini Dar es salaam jana  Februari 27, 2017.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimsikiliza Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alipokuwa akifafanua jambo katika kikao kilichoitishwa na Waziri Mkuu kwenye Makazi yake Oysterbay jijini Dar es salaam Februari 27, 2017, kwa ajili ya kujadili masuala ya madini. Watatu kushoto ni Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango na  ni Mkuu wa Mkoa wa Manyara Dkt. Joel Bendera.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

KWA HABARI ZAIDI BOFYA HAPA


HALMASHAURI YA KAKONKO SHULE ZA KATA ZANG’ARA MATOKEO KIDATO CHA NNE

$
0
0
Lusubilo Joel Ded Kakonko
Na Judith Mhina –MAELEZO
Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko yafaulisha wanafunzi 743 kati ya watahiniwa 784 na kushika nafasi ya Tatu Kitaifa kati ya Halmashauri 178hapaTanzania.
Katika mahojiano maalum na Idara ya Habari MAELEZO Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kakonko Bw Lusubilo Joel Mwakabibi amesema: “Shule za serikali zimeanza kurudisha heshima ya kufaulu kama ilivyokuwa miaka ya 1970 na 1980, mara baada ya matokeo ya kidato cha Nne mapema mwezi huu”.
Mwakabibi ameeleza kuwa Halmashauri hiyo inajumla ya shule           za sekondari 14, kati ya hizo 11 ni za Serikali na 3   za binafsi. Matokeo ya kidato cha nne mwaka huu
Yanaonesha daraja  la  kwanza shule za binafsi ni 10,  pili  35, tatu 40, nne 41 na zilizopata ziro ni 13. Kwa upande wa Shule za Serikali daraja la kwanza 6, pili 47, tatu 149, nne 400 na ziro 38.
 “Siri ya mafanikio yetu ni usimamizi wa karibu na ufuatiliaji shuleni, umoja na mshikamano kati ya Walimu, wazazi, Viongozi wa Halmashauri na Ofisi ya Mkuu wa wilaya; walimu wetu tupo pamoja nao, tunawatia moyo katika kazi ya kufundisha”. Anafafanua Mkurugenzi huyo.
Aidha, Mkurugenzi Mwakabibi amesema mwaka 2016 Halmashauri imeshika na fasiyatatu, Kitaifa katika Halmashauri 178 Tanzania, kwani matokeo ya kidato cha Nne na Pili mwaka 2015, Halmashauri yetu, ilikuwa ya kwanza kitaifa na kuzawadiwa ngao ya ushindi toka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia.

 Hata hivyo ameeleza kuwa mikakati ya Halmashauri yake ni kurudi namba moja, lengo likiwa ni kuhakikisha wanafunzi wote watakao sajiliwa kufanya mtihani wa kufaulu kwa viwango vya juu na kufuta kabisa aibu ya kufeli..

Airtel washirikiana na UCSAF kufikisha mawalisiano vijiji 49 Dodoma

$
0
0
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel katika mpango wake wa kufikisha huduma za mawasiliano kwenye maeneo ya pembezoni imeshirikiana na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) kwa kujenga na kukamilisha miundombinu ya mawasiliano katika kata 10 zilizoko katika maeneo ya vijijini ili kutoa huduma bora ya mawasiliano.

Katika kufanikisha mkakati huo, Airtel na UCSAF leo imefanya uzinduzi wa kwanza wa minara minne iliyoko katika kata za Matomondo, Mbuga and Ipera wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma ambapo uzinduzi huo utawawezesha wakazi zaidi ya  38,000 katika vijiji 49 kuunganishwa na huduma za mawasiliano toka Airtel na kufurahia huduma na bidhaa mbalimbali ikiwemo huduma za intaneti, kupiga simu pamoja na huduma ya Airtel money ili kutatua changamoto zao

Akiongea wakati wa uzinduzi wa huduma za mawasiliano katika kata ya Matomondo Dodoma,  Meneja wa mauzo wa Airtel Dodoma, Bwn Pascal Bikomagu alisema” Airtel imejipanga katika kuboresha na kupanua upatikanaji wa huduma za mawasilino  ili kuchochea kukua kwa shughuli za kijamii na kiuchumi katika maeneo yaliyo na changamoto hususani vijijini
Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Jabir Shekimweri  akizugumza na Wakazi wa kijiji cha Mbori, Kata ya Matomondo Wilayani Mpwapwa wakati wa uzinduzi wa Mnara wa Matomondo. Aidha Airtel pamoja na USCAF ilizindua minara minne wilayani hapo na kuwawezesha wakazi katika vijjiji 49 kupata huduma za mawasiliano ya uhakika.
Meneja wa Kampuni ya Simu ya Airtel, Mkoa wa Dodoma Paschal Bikomagu akizugumza na Wakazi wa kijiji cha Mbori,  Kata ya Matomondo Wilayani Mpwapwa wakati wa uzinduzi wa Mnara wa Matomondo. Aidha Airtel pamoja na USCAF ilizindua minara minne wilayani hapo na kuwawezesha wakazi katika vijjiji 49 kupata huduma za mawasiliano ya uhakika.
Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Jabir Shekimweri akisalimiana na mchezaji wa timu ya Manchester United ya Mbori Wilayani Mpwapwa, Juma Athmani katika mchezo wa fainali iliochezwa juzi katika uwanja wa Ikulu kata ya Matomondo Wilayani Mpwapwa. Mchezo huo ulikuwa madhumuni kwa ajili ya uzinduzi wa mnara wa simu wa Matomondo uliojengwa na Kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na USCAF ili kufikisha huduma mawasiliano kwa wananchi waishio maeneo ya pembezoni mwa nchi. Manchester ilishinda kwa mabao 4-3 dhidi ya Liverpool.
Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Jabir Shekimweri akisalimiana na wachezaji wa timu ya Liverpool ya Mbori Wilayani Mpwapwa katika mchezo wa fainali uliochezwa juzi katika uwanja wa Ikulu kata ya Matomondo Wilayani Mpwapwa. mchezo huo ulikuwa na madhumuni kwa ajili ya uzinduzi wa Mnara wa simu wa Matomondo,uliojengwa Kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na USCAF ili kufikisha huduma mawasiliano kwa wananchi waishio maeneo ya pembezoni mwa nchi. Manchester ilishinda kwa mabao 4-3 dhidi ya Liverpool.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

EAST AFRICAN NGWASUMA ORINGINAL BAND WAWAPAGAWISHA WAKATI WA MKOANI KILIMANJARO

$
0
0
Kiongozi wa band ya  East African Ngwasuma Original Band Kingombe Blaise  wa pili kulia akiwa anafanya mambo katika ukumbi wa Filomena Bar uliopo Boma Ngo'mbe  mkoani Kilimanjaro  wakati wa onyesho lao walilofanya mwishoni mwa wiki hii.
 waimbaji na wanenguaji wa bendi ya East African Ngwasuma Original Band wakiwa wanawapagawisha wakazi wa Bomang'ombe na mitaa yake
 wanenguaji wa band ya  East African Ngwasuma Original Band wakiwa wanaonyesha viuno ikiwa  wanacheza staili yao mpya ya Kampa Kampa tena.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

TNRF yazindua mpango mkakati wa Ardhi

$
0
0
Kamishna wa Ardhi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mary Makondo(aliyesimama) akizungumza jambo wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa ardhi hapa nchini Tanzania ambao utajumuisha mradi wa majaribio katika mikoa mbalimbali kuona kama utawezekana maana swala la upatikanaji wa ardhi imekuwa ni changamoto kubwa sana hapa nchini.
Mkurugenzi wa Jumuiko la Maliasili Tanzania( TNRF), Joseph Olila akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati wa ardhi hapa nchini Tanzania uliodhaminiwa na Jumuiko la Maliasili Tanzania ili kuweza kupatikana kwa ardhi hasa maeneo ya vijijini .
Mkurugenzi Mtendani wa Taasisi ya MVUWATA ya Morogoro, Steven Ruvuga akizungumza jinsi wanavyoweza kuhamasisha watu kwenye matumizi mazuri yaardhi pamoja na kutatua migogoro ya ardhi kwenye mkutano uliofanyika kwneye ukumbi wa Hotel ya Wanyama jijini Dar es Salaam.
Bwana Alain Essimi  Biloa  akitoa mada juu ya matumizi mazuri ya ardhi kwenye jamii hasa kwa wananchi waishio vijijini.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

WAZIRI NAPE MGENI RASIMI FAINALI ZA ULEGA CUP ZITAKAZOFANYIKA MACHI 5 MKURANGA

$
0
0
Timu ya kata ya Tengelea, Tengelea FC  imefunzu kuingia katika fainali ya Ulega Cap baada ya kuifunga Timu ya Mwandege FC  bao 1 – 0 katika mcheezo uliochezwa jana katika viwanja vya shule ya Mkuranga jana .

Bao la timu ya Tengelea lilipatikana katika kipindi cha pili kupitia mchezaji  wao Andew Joseph aliyepokea cross ambayo ndio ilipa ushindi timu hiyo.
Timu ya kata ya Tengelea, itaingia fainali kwa kukipiga na timu ya Kisiju na mechi itanguliwa na mechi ya mshindi wa tatu kati ya Mwandege FC na Lukanga FC.

Mgeni rasmi katika fainali za Ulega CUP ni Waziri Habari, Michezo, Utamaduni na Sanaa, Nape Nnauye.

Akizungumza na waandishi wa habari muandaji wa mashindano hayo Mbunge wa  Mkuranga, Abdallah Ulega amesema kuwa mashindano yameibua vipaji ya vipya.

Amesema kuwa inahitaji uwekezaji katika michezo kutokana na vijana kuonyesha vipaji vyao ambavyo vinatakiwa kuendelezwa.
 Mbunge wa Mkuranga , Abdallah Ulega akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya Tengelea iliyopata ushindi wa kuingia fainali ya Ulega CUP katika mchezo uliochezwa jana katika viwanja vya shule ya Mkuranga jana.
 Mbunge wa Mkuranga , Abdallah Ulega akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya Mwandege ambao ni washindi wa tatu katika mashindano ya Ulega Cup baada ya kupata kichapo jana na timu ya Tengelea katika mchezo uliochezwa katika uwanja wa shule ya msingi Mkuranga.
  Vijana wakionyesha vipaji vyao katika mashindano ya Ulega CUP katika mchezo uliochezwa katika uwanja wa shule ya msingi Mkuranga.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Viewing all 110171 articles
Browse latest View live




Latest Images