Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live

KAMATI YA SAA 72 YAMFUNGIA KOCHA WA STAND MOROCCO MECHI TATU

$
0
0



Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

Kamati ya Bodi ya Ligi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi (Kamati ya Saa 72), imemfungia Kocha wa Stand United, Hemed Suleiman ‘Morocco’ kushiriki michezo mitatu uwanjani na faini ya Sh 500,000 (laki tano).

Katika mechi Na. 160 ya Ligi Kuu ya Vodacom uliozikutanisha timu za JKT Ruvu na Stand United iliyochezwa Januari 30, mwaka huu kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, Morocco aliondolewa kwenye benchi (Ordered off) kwa kosa la kupiga maamuzi ya mwamuzi na kutoa lugha chafu.

Kamati hiyo ya Saa 72 imechukua hatua hiyo kwa mujibu wa Kanuni ya 40 (11) ya Ligi Kuu kuhusu udhibiti wa Makocha. Morocco hata kama atakuwa amemaliza mechi tatu nje ya benchi, hataruhusiwa kukaa kwenye benchi hadi awe amelipa faini hiyo.

Adhabu hiyo ya Morocco itaendelea kumhusu hata kama utakuwa umehamia kwenye timu nyingine na katika msimu mwingine wowote.

SERENGETI BOYS YAENDELEA NA MAANDALIZI YA AFCON 2017

MAKAMU WA RAIS AHUDHURIA MKUTANO WA UMOJA WA MATAIFA WA KUWAWEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI MJINI DUBAI

$
0
0


Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amehudhuria mkutano wa Jopo la Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa la Kuwawezesha Wanawake Kiuchumi kama mmoja wa wajumbe wa jopo hilo.

Mkutano huu umefanyika mjini Dubai, Falme za Kiarabu na Ufunguzi rasmi ulihudhuriwa na Mrithi wa Mtawala wa Dubai Mtukufu Sheikh Hamdan Bin Mohammed Bin Rashid Al Maktoum pamoja na viongozi na wakuu wa Serikali wa Falme za Kiarabu .

Lengo la Mkutano huu ilikuwa ni kupitia Ripoti ya Kwanza ya Jopo hilo iliyowasilishwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki Moon kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, mwezi Septemba 2016. Mkutano huu wa Dubai, unategemea kutoa Ripoti ya Pili ambayo itatoa muelekeo wa namna Serikali zitashirikiana na wadau mbalimbali kama vile sekta binafsi, Asasi za kiraia na wadau wengine wa maendeleo katika jitahada za kumkwamua mwanamke kiuchumi.

Wajumbe wa Jopo hili, walipata fursa ya kujadili changamoto mbalimbali zinazomkabili mwanamke; pamoja na kubadilishana uzoefu na kutoa mapendekezo yatakayoleta matokeo chanya katika kumuinua mwanamke kiuchumi. Mbali na kupendekeza maboresho ya Ripoti hiyo, wajumbe walijadili na kupendekeza hatua ambazo wadau watatakiwa kuchukua ili kumkomboa mwanamke kiuchumi. 

Tanzania kama nchi mwanachama ilipata fursa ya kutoa uzoefu wake jinsi Serikali imeweka mikakati mbalimbali ya kuwawezesha wanawake hususani wale walio katika sekta isiyo rasmi; hasa wakulima na wafanyabiashara wadogo wadogo wanawake ili kuhakikisha wanafaidika na mifumo ya kifedha na kijiditali kama vile kupata mikopo ya gharama nafuu; kuingizwa kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii na huduma zingine. 

Makamu wa Rais alisema pamoja na kila bara kuwa na changamoto zake, bado kuna umuhimu wa dunia kuhakikisha inaweka misingi madhubuti ya kuinua wanawake kiuchumi hasa kwa wanawake wa ngazi za chini ambao wengi wao wanaishii vijijini.

Alitaja baadhi ya changamoto hizo kuwa ni pamoja na mifumo ya sheria na sera zilizopo kuwa bado zinawanyima wanawake haki ya kurithi na kumiliki ardhi hata kama haki hizo zimewekwa kisheria."Hii inatokana na utekelezaji mbaya wa sheria, inayosababishwa na kuwepo kwa mianya kwenye hizo sheria na utendaji wa kubagua ambapo unaondoa ule mfumo rasmi wa kisheria unaotegemewa," alisema Makamu wa Rais.

Aidha alisema ushiriki mdogo wa wanawake ambao wengi ni wajasiriamali, katika kutumia mifumo ya kifedha ikiwemo mifumo mipya ya teknolojia ya fedha mtandao inachangia kuwafanya wanawake wakose mapato na hivyo kushindwa kufanikisha azma ya kuwezesha wanawake kiuchumi. Aliwaasa wanawake waungane na kuinuana wenyewe kwa wenyewe ili kuweza kutoachwa nyuma kwenye kufikia malengo yao ya kiuchumi na kwamba sambamba na utekelezaji wa Malengo Mapya ya Maendeleo Endelevu na Ajenda ya mwaka 2030. 

Jopo hilo linatakiwa kuwasilisha ripoti yake ya Pili kwenye Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani mwezi Machi mwaka huu.

Mkutano huo ulileta washiriki takriban 45 kutoka sekta mbalimbali ikiwemo serikali, Taasisi binafsi, wachambuzi mbalimbali wa masuala ya kumwezesha mwanamke kiuchumi kutoka Jumuiya ya Kimataifa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifuatilia kwa makini kwenye mkutano wa Kuwezesha wanawake kiuchumi ambapo wajumbe wa Jopo maalum walikutanna mjini Dubai kujadili Ripoti ya awali ya Jopo hilo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mkutano wa kuwawezesha wanawake kiuchumi pamoja na wajumbe wengine wa Jopo hilo mjini Dubai.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na Siriel Shaidi Mchembe kwenye mkutano wa Kuwezesha wanawake kiuchumi ambapo wajumbe wa Jopo maalum walikutanna mjini Dubai kujadili Ripoti ya awali ya Jopo hilo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifuatilia kwa makini kwenye mkutano wa Kuwezesha wanawake kiuchumi ambapo wajumbe wa Jopo maalum walikutanna mjini Dubai kujadili Ripoti ya awali ya Jopo hilo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Mrithi wa Mtawala wa Dubai Sheikh Hamdan Bin Mohamed bin Rashid Al Maktoum pamoja na wajumbe wa Jopo wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Jopo la Umoja wa Mtaifa la Kuwawezesha Wanawake Kiuchumi ulioanza tarehe 6 februari mjini Dubai.

RAIS DK. JOHN POMBE MAGUFULI AMUAPISHA MKUU WA MAJESHI JENERALI VENANCE MABEYO

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Jenerali Venance Mabeyo akila kiapo cha utii mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt. John Pombe Magufuli leo Ikulu jijini Dar es Salaam. Katikati ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.
Mnadhimu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Luteni Jenerali James M. Mwakibolwa akila kiapo cha utii mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt. John Pombe Magufuli leo Ikulu jijini Dar es Salaam. Katikati ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Kamishna Jenerali wa Magereza Dr. Juma Malewa wakati wa hafla ya kuwapisha wateule hao leo jijini Dar es Salaam.
Balozi Paul Mella ambaye ataiwakilisha nchi ya Tanzania nchini katika Jamhuri ya Demokrasia ya Congo akila kiapo cha utii mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt. John Pombe Magufuli leo Ikulu jijini Dar es Salaam. Katikati ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.
Balozi Samweli William Shelukindo ambaye anakwenda kuiwakilisha Tanzania nchini Ufaransa akila kiapo cha utii mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt. John Pombe Magufuli leo Ikulu jijini Dar es Salaam. Katikati ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma Nyakimura Mathias Mhoji akila kiapo cha utii mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dkt. John Pombe Magufuli leo Ikulu jijini Dar es Salaam. Katikati ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) Kamishna Robert Boaz Mikomangwa akila kiapo cha utii mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Inspekta Jenerali Ernest Mangu katika hafla ya kuwaapisha baadhi ya viongozi walioteuliwa na Mhe. Rais kushika nyazifa mbalimbali leo Ikulu jijini Dar es Salaam.

KIMONDO SUPER FC YASHUSHWA HADI LIGI YA MKOA

$
0
0
Timu ya Kimondo Super SC imeshushwa madaraja mawili (hadi Ligi ya Mkoa), na matokeo ya mechi zake zote ilizocheza katika kundi la B yamefutwa kwa kushindwa kufika uwanjani kucheza mechi dhidi ya JKT Mlale bila sababu za msingi.

Mechi hiyo namba 47 (JKT Mlale vs Kimondo Super SC), ilitakiwa kuchezwa Januari 28, 2017 kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea, lakini Kimondo Super SC haikutokea uwanjani wala kutoa taarifa yoyote hadi Februari 1, 2017 ilipotuma taarifa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), na kutoa sababu ambazo hazikukubaliwa na Kamati.

Pia Kimondo Super SC imetozwa faini ya sh. 2,000,000 (milioni mbili) ambapo kati ya hizo sh. 1,000,000 (milioni moja) itachukuliwa na TPLB, na sh. 1,000,000 (milioni moja) italipwa JKT Mlale. Adhabu dhidi ya Kimondo Super SC ni utekelezaji wa Kanuni ya 28(1) na (2) ya Ligi Daraja la Kwanza.

MABUSHA, MATENDE NA USUBI BADO NI TATIZO MUFINDI

$
0
0
Halmshauri ya Wilaya ya Mufindi, italazimika kurudia zoezi la utoaji kinga tiba kwa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele baada ya utafiti wa kitabibu kutoka wizara ya afya kubaini uwepo wa vimelea vya magonjwa hayo kwa asilimia kubwa ya wakazi wa halmashauri hiyo.

Taarifa ya idara ya afya kupitia Afisa habari na mawasiliano wa halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Bw. Ndimmyake Mwakapiso , imeyataja magojwa hayo manne kuwa ni Ugonjwa wa Mabusha na Matende, Mivyoo ya tumbo sanjari na ugonjwa wa usubi ambao huathiri macho ya binadamu kwa kusababisha upofu.

Amesema baada ya kukamilika kwa zoezi la utoaji kinga tiba mapema mwaka jana, ni kawaida kwa wizara ya afya kuendesha utafiti kwa lengo kutadhimini na kujiridhisha kama kinga tiba iliyotolewa imekidhi matarajio au la, na ndipo ilipogundulika kuwa bado kunavimelea vya maabukizi ya magonjwa hayo miongoni mwa jamii ndani ya halmashauri hiyo.

Mwakapiso, ameongeza kuwa kinga tiba hiyo itatolewa na watoa huduma waliopo katika ngazi ya jamii husika ambao wamepata mafunzo maalum na kujengewa uwezo wa kutekeleza jukumu hilo kwa weledi mkubwa, zoezi ambalo litaendeshwa kuanzia jumatatu ya tarehe 06 mwezi huu na litadumu kwa muda wa siku 06 pekee.

Aidha, ametoa rai kwa wakazi wote wa halmashauri ya wilaya ya Mufindi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa watoa huduma watakaofika katika kaya kuwapatia kinga tiba hiyo muhimu kwa ustawi wa afya zao na maendeleo ya taifa, kwa kuzingatia kuwa afya njema ndio chimbuko la maendeleo ya familia na taifa lolote duani.

Visiwa Ukerewe kupata umeme Juni 2018

$
0
0
Na Greyson Mwase, Dar es Salaam

Visiwa vidogo vilivyopo katika Ziwa Viktoria vinatarajiwa kupata umeme wa uhakika ifikapo Juni mwakani.

Hayo yalielezwa na Kamishna Msaidizi- Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Styden Rwebangila, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa akielezea mafanikio yaliyopatikana Sekta ya Nishati kupitia Nishati Jadidifu chini ya Idara ya Nishati katika upatikanaji wa umeme wa uhakika.

Alisema kuwa, wakandarasi wameshaanza kuweka miundombinu kwa ajili ya umeme wa jua ambapo miradi hiyo inatarajiwa kukamilika kwa asilimia mia moja ifikapo mwezi Juni mwakani.

Akielezea mipango ya Serikali katika kuhakikisha kuwa nishati ya umeme inakuwa ni ya uhakika Mhandisi Rwebangila alisema Wizara inahamasisha vyanzo vingine vya uzalishaji wa umeme kama vile jua, upepo, jotoardhi na kuongeza kuwa inakaribisha wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi kutafiti na kutumia vyanzo hivyo.

Alisema kwa upande wa jotoardhi utafiti ulifanyika na kuonesha maeneo ya Songwe na Ziwa Ngozi mkoani Mbeya na Mlima Meru mkoani Arusha yana viashiria vya jotoardhi.Aliongeza kuwa mara baada ya utafiti kukamilika mwishoni mwa mwaka huu, visima vinatarajiwa kuanza kuchimbwa kwa ajili ya uzalishaji wa nishati ya jotoardhi.

Aliendelea kutaja mipango mingine kuwa ni pamoja na uanzishwaji wa mwongozo kwa ajili ya mfumo wa umeme kwenye majengo na wa udhibiti wa matumizi ya umeme viwandani.

Alisema pia, Wizara inatarajia kuanzisha mfumo mpya wa uhifadhi data na utoaji taarifa za Nishati Jadidifu ujulikanao kama Tanzania Renewable Energy Management Information System (TREMIS) utakaowezesha wawekezaji ndani na nje ya nchi kubaini fursa za uwekezaji zilizopo katika sekta ya Nishati Jadidifu.

Alisema katika mfumo huo kutawekwa taarifa mbalimbali kuhusu, tafiti mbalimbali na fursa za uwekezaji katika nishati jadidifu , sera, sheria na taratibu ili kuvutia wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi.

“Kupitia mfumo huu kutakuwa hakuna haja ya mwekezaji kutoka nje ya nchi kufunga safari hadi Tanzania kwa ajili ya kupata taarifa, taarifa zote zitakuwepo katika mfumo huu utakaounganishwa na tovuti ya Wizara,” alisema Mhandisi Rwebangila.
Kamishna Msaidizi- Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Styden Rwebangila, (kushoto) akielezea mafanikio ya sehemu ya nishati jadidifu chini ya Idara ya Nishati katika upatikanaji wa umeme wa uhakika katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam mapema tarehe 06 Februari, 2017. Kulia ni Mtaalam wa Nishati Jadidifu, Emillian Nyanda.

NAMAINGO WATAKIWA KUCHANGAMKIA UZALISHAJI WA MALIGHAFI YA VIWANDA

$
0
0
Na Richard Mwaikenda

SERIKALI imeutaka Ushirika wa Vibidar Namaingo kuanza kuzalisha mazao mengi kwa ajili ya malighafi ya viwanda vilivyopo na vinavyotarajiwa kuanzishwa nchini.

Ushauri huo ulitolewa juzi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mary Mashingo wakati wa sherehe ya kukabidhi cheti kwa ushirika huo wa Vikundi vya Biashara Dar es Salaam (Vibidar), kwenye Uwanja wa Magereza, Ukonga.

Mashingo, aliipongeza Kampuni ya Namaingo Business Agency Ltd, kwa kuanzisha vikundi hivyo vya ujasiriamali na kuviatamia hadi kufikia kuunda ushirika wa Vibidar utakaoongeza viwango vya maarifa, taaluma pamoja na tija, jabo litakalowezesha wajasiramali wengi kuondokana na ujasriamali mdogo kwenda kwenye ujasiriamali mkubwa na hatimaye kuongeza pato la kaya na Taifa kwa ujumla.

Alisema kuwa ushirika huu umekuja wakati muafaka, wakati Serikali ya Awamu ya Tano, imekuwa ikitoa kipaumbele katika kuhamasisha maendeleo ya sekta ya viwanda, ambapo sekta ya kilimo kupitia vikundi shirikishi inayo fursa kubwa ya kuweza kuzalisha malighafikwa ajili ya maendeleo ya viwanda.

"Ushirika wa vikundi mbalimbali kama Vibidar, vina uwezo wa kuzalisha malighafi ya kutosha kwa ajili ya kusindika mazao kutosheleza mahitaji ya viwanda, hivyo ushirika huu umeanzishwa katika muda muafaka wakati serikali inatilia mkazo katika kuchochea maendeleo ya sekta za kiuchumi zinazoweza kuchoche viwanda nchini," alisema Mashingo.

Mashingo, aliahidi serikali kuendelea kushirikiana na wadau kuimarisha ushirika ili kuzitatua changamoto mbalimbali kwa kutumia mikakati na mbinu za kila aina. Alizija baadhi ya changamoto zinaikabili sekta ya kilimo kuwa ni;uongezaji wa tija katika uzalishaji, mifumo ya soko yenye mpangilio mzuri, kujenga mitandao thabiti ya mawasiliano na kuwaunganisha wadau katika mlolongo wa thamani.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mary Mashingo (katikati),akimkabidhi cheti Mwenyekiti wa Ushirika wa Vikundi vya Biashara Dar es Salaam (Vibidar Namaingo), Grace Lobulu katika sherehe iliyofanyika kwenye Uwanja wa Magereza, Ukonga juzi. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya ushirika huo, Ubwa Ibrahim. 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mary Mashingo (katikati),akimkabidhi hati Mwenyekiti wa Bodi ya Ushirika wa Namaingo Vibidar, Ubwa Ibrahim. 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mary Mashingo (katikati),akimkabidhi cheti Mwenyekiti wa Ushirika wa Vikundi vya Biashara (Vibidar Namaingo), Wilaya ya Kinondoni, Loiruck Mollel katika sherehe iliyofanyika kwenye Uwanja wa Magereza, Ukonga juzi. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya ushirika huo, Ubwa Ibrahim. (PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA)


Taarifa ya Serikali toka Bungeni

WASTAAFU WANAOLIPWA NA HAZINA WASIOHAKIKIWA KUONDOLEWA KWENYE MALIPO YA PENSHENI

$
0
0
Na Benny Mwaipaja-WFM, Mtwara

WIZARA ya Fedha na Mipango, imesema kuwa wastaafu wanaolipwa na Wizara hiyo ambao hawatahakikiwa wataondolewa kwenye orodha ya malipo ya pensheni kwa kuwa watakuwa wamekosa sifa.

Kauli hiyo imetolewa Mjini Mtwara na Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali Msaidizi, Bw. Stanslaus Mpembe, wakati wa uzinduzi wa uhakiki wa wastaafu wanaolipwa pensheni zao na Wizara hiyo katika Mikoa ya Lindi na Mtwara.

Alisema kuwa lengo la uhakiki huo ni kuiwezesha Wizara kuhuisha taarifa za wastaafu ili kupata kanzidata (database) iliyo sahihi, kuwatambua wastaafu na kuiwezesha serikali kulipa wastaafu wanaostahili.

“Kwa kuwa zoezi hilo ni la lazima na kwa wale wastaafu ambao hawajahakikiwa kwa sababu mbalimbali katika mikoa ambayo uhakiki umekamilika watalazimika kufika katika ofisi za Hazina katika mikoa husika na kujiandikisha na baada ya uhakiki kukamilika wataelekezwa utaratibu utakaotumika kuwahakiki” aliongeza Bw. Mpembe

Aidha Bw. Mpembe alisisitiza wastaafu hao kufika wenyewe na sio kutuma wawakilishi, wakiwa na nyaraka zote muhimu zikiwemo barua ya tuzo la kustaafu, barua ya kustaafu au kupunguzwa kazini, nakala ya hati ya malipo ya kiinua mgongo au mkupuo, barua ya ajira ya kwanza, kitambulisho cha pensheni, barua ya kuthibitishwa kazini, kadi ya benki na picha mbili ndogo zilizopigwa hivi karibuni.

Akijibu kuhusu malalamiko ya pensheni ndogo kwa wastaafu, Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali Msaidizi, Bw. Stanslaus Mpembe, amesema kuwa watakapo kamilisha zoezi la uhakiki wataandaa taarifa namna zoezi zima lilivyo endeshwa na kuiwasilisha kwa uongozi wa juu wa Wizara, likiwemo suala hilo la malalamiko ya pensheni ya wastaafu.
Mkaguzi wa ndani wa Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara, Bw. Hussein Mussa, pamoja na maafisa wengine wakiendelea na zoezi la uhakiki wa wastaafu wanaolipwa na Wizara ya Fedha na Mipango, mkoani Mtwara.
Baadhi ya Wastaafu wanaolipwa na Wizara ya Fedha na Mipango, wakikagua nyaraka zao muhimu kabla ya kufika katika dawati la huduma kwenye zoezi la uhakiki linaloendelea mkoani Mtwara
Afisa TEHAMA Mwandamizi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Jacqueline Nyamugali (wa kwanza kushoto) akiwa na maafisa wengine, wakitoa maelekezo kuhusu nyaraka muhimu za mmojawapo ya wastaafu wanaolipwa na Wizara ya Fedha na Mipango wakati wa zoezi la uhakiki linaloendelea mkoani Mtwara.
Kaimu Mhasibu Mkuu Pensheni, Scolastica Mafumba, akikagua nyaraka na kutoa maelekezo muhimu kwa mmojawapo ya wastaafu wanaolipwa pensheni na Wizara ya Fedha na Mipango waliofika kuhakikiwa mjini Mtwara.

WALENGWA WA TASAF MKOANI SINGIDA WABORESHA MAKAZI YAO KWA KUTUMIA FEDHA ZA RUZUKU.

$
0
0

Na Estom Sanga

Baadhi ya walengwa wa Mpango wa kunusuru Kaya Maskini unaotekelezwa na serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF mkoani Singida wameanza kuboresha makazi yao kwa kutumia sehemu ya fedha zinazotolewa na mfuko huo kwa njia ya ruzuku .

Wakizungumza na Waandishi wa Habari walioko katika ziara ya mkoa huo kuona namna walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya maskini wanavyonufaika kupitia utaratibu wa uhawilishaji fedha,baadhi yao wamewaeleza waandishi hao kuwa licha ya kutumia sehemu ya fedha hizo kununua chakula na sare za watoto lakini pia wameweza kununua mabati na kuezeka nyumba zao na hivyo kuboresha makazi yao.

“nimeepukana na shida ya kuvuja kwa nyumba yangu baada ya kununua mabati na kujenga nyumba ya matofali kutokana na fedha za TASAF”amesema mzee shaaban Mkondya anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 70 mkazi wa eneo la Mtipa nje kidogo ya manispaa ya Singida.

Naye bi.Mwajuma Omary amewaeleza waandishi wa habari kuwa tangu aanze kupata ruzuku ya fedha kutoka TASAF mwaka 2014 hali yake ya maisha imeboreshwa na kuwa na walau uhakika wa kupata chakula huku akitumia sehemu ya fedha hizo kununua mabati 10 yaliyomwezesha kuezeka nyumba yake na hivyo kuboresha makazi yake.

“ninaishukuru TASAF kwa kutufikiria sisi wanyonge kama mimi kwani tulikuwa na hali ngumu ya maisha lakini sasa walau tunauhakika wa kupata fedha kila mwezi kulingana na utaratibu uliowekwa” amesisitiza Bi Mwajuma Omary mwenye umri wa miaka 77.

Sehemu ya mtaro uliojengwa katika eneo la Mtipa nje kidogo ya manispaa ya Singida kupitia utaratibu wa ajira ya muda unaotekelezwa na walengwa wa Mpango wa Kunusuru kaya maskini kupitia TASAF.
Mmoja wa walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya maskini Mzee Shaaban Mkondya akiwa amesimama kando ya nyumba aliyoiezeka mabati kwa fedha za ruzuku ya TASAF na hivyo kuboresha makazi yake.
Mmoja wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini Mzee Shaaban Mkondya aliyesimama na mjukuu wake aliyevaa sare za shule akiwaonyesha waandishi wa habari nyumba yake ya zamani Kulia na ile mpya kushoto kwake aliyoezeka kwa mabati kwa ruzuku ya fedha za TASAF.
Bi. Mwajuma Omary (77) aliyeketi akiwaonyesha waandishi wa habari (hawapo pichani) nyumba yake mpya iliyoko kushoto kwake na kulia kwake ni nyumba yake ya zamani ikiwa katika mfumo wa tembe.  
Pichani ni Mama wenye watoto chini ya miaka 5 wakiwa katika kituo cha afya cha Mtipa nje kidogo ya manispaa ya Singida wakitimiza moja ya sharti la Mpango wa kunusuru kaya masikini kuhudhuria kliniki. 

WASOMI WAPONGEZA USAWA WA JINSIA UMOJA WA AFRIKA(AU)

$
0
0

Mwandishi Wetu,Arusha

Wasomi nchini wamepongeza uteuzi wa majaji wawili wanawake wa Mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu(AfCHPR)uliofanywa na Wakuu wa Umoja wa Afrika(AU) katika mkutano wa 28 uliofanyika nchini Ethiopia kuwa unaelenga kujenga usawa wa kijinsia katika chombo hicho cha maamuzi.

Mkutano huo pamoja na mambo mengine ulipitisha majina ya majaji wawili ambao ni Jaji Bensaoula Chafika kutoka Algeria na Jaji Chizumila Rose Tujilane wa Malawi ambao wataitumikia mahakama hiyo kwa kipindi cha miaka sita ijayo.

Majaji hao wanachukua nafasi zilizoachwa wazi na Jaji Fatsah Ouguergouz(Algeria) na Jaji Duncan Tambala(Malawi)ambao utumishi wao ulikoma tangu Septemba 5,2016.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Sebastian Kolowa Memorial(Sekomu),Dk Happiness Rwejuna aliyewaongoza wanafunzi wa sheria kutembelea Mahakama hiyo yenye makao yake jijini hapa alisema uamuzi uliofanywa na AU ni mzuri na ufaa kuigwa na nchi wanachama katika uteuzi wa wanawake wenye uwezo katika nafasi za maamuzi.

“Naamini idadi ya wanawake wenye elimu ya juu wapo wengi na wanaweza kufanya kazi kwa umahiri mkubwa,isihishie katika ngazi ya AU tuu bali ishuke hadi kwa nchi moja moja kuona wanawake wana mchango muhimu katika maendeleo ya Afrika kwa ujumla,”alisema.
Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu(AfCHPR)Sukhdev Chhatbar akizungumza na wanafunzi wa mwaka wa tatu kozi ya sheria katika Chuo Kikuu cha Sebastian Kolowa Memorial(Sekomu)kilichopo Lushoto mkoa wa Tanga wakati wa ziara ya masomo katika mahakama hiyo mkoani Arusha.Picha na Filbert Rweyemamu
Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu(AfCHPR)Sukhdev Chhatbar akizungumza na wanafunzi wa mwaka wa tatu kozi ya sheria katika Chuo Kikuu cha Sebastian Kolowa Memorial(Sekomu)kilichopo Lushoto mkoa wa Tanga wakati wa ziara ya masomo katika mahakama hiyo mkoani Arusha. 
Wafanyakazi na wanafunzi wa sheria katika Chuo Kikuu cha Sebastian Kolowa Memorial(Sekomu)kilichopo Lushoto mkoa wa Tanga wakiwa kwenye chumba cha mahakama ya wazi katika Mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu(AfCHPR) wakati wa ziara ya mafunzo. 

MHADHARA WA 8 WA KISAYANSI WAFANYIKA KATIKA HOSPITALI YA KAIRUKI MIKOCHENI

$
0
0
Dokta Winnie Mpanju-Shumbusho akitoa mada kwenye mhadhara wa 8 wa Kisayansi kuhusu Uimarishaji wa Mifumo ya Utoaji Huduma za Afya na Uzuiaji wa Magonjwa kwenye nchi za Kiafrika katika Zama za Maendeleo Endelevu wakati wa Maadhimisho ya 18 ya Kumbukizi ya hayati, Prof. Hubert Kairuki jijini Dar es Salaam. (Picha na Francis Dande). 
 Prof. Moshi Ntabaye akizungumza katika mhadhara huo. 
 Baadhi ya washiriki wa mhadhara wa 8 wa Kisayansi kuhusu Uimarishaji wa Mifumo ya Utoaji Huduma za afya na Uzuiaji wa Magonjwa kwenye nchi za Kiafrika katika Zama za Maendeleo Endelevu. 
 Baadhi ya washiriki wa mhadhara wa 8 wa Kisayansi kuhusu Uimarishaji wa Mifumo ya Utoaji Huduma za afya na Uzuiaji wa Magonjwa kwenye nchi za Kiafrika katika Zama za Maendeleo Endelevu.
 Washiriki wa mhadhara wa 8 wa Kisayansi kuhusu Uimarishaji wa Mifumo ya Utoaji Huduma za afya na Uzuiaji wa Magonjwa kwenye nchi za Kiafrika katika Zama za Maendeleo Endelevu.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Serikali Kupiga Marufuku Matumizi ya Pombe Aina ya Viroba Nchini

$
0
0
Na: Lilian Lundo – MAELEZO – Dodoma

Serikali inatarajia kupiga marufuku utengenezaji na uingizaji wa pombe za bei rahisi maarufu kama “Viroba” Nchini, ndani ya miezi mitatu ijayo.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Hamisi Kigwangalla ameyasema hayo leo Bungeni, Mjini Dodoma alipokuwa akijibu hoja za wabunge waliokuwa wakilalamikia  kilevi hicho kinavyopunguza nguvu kazi ya Taifa, wakati wa uwasilishwaji wa taarifa za kamati ya kudumu ya Bunge ya masuala ya Ukimwi pamoja na Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa mwaka 2016/17.

Dkt. Kigwangalla amesema kuwa baada ya miezi mitatu kilevi hicho kitapigwa marufuku kutengenezwa au kuingizwa nchini pamoja na kuziba mianya yote ya uingizaji wa kilevi hicho ambacho kimekuwa kikitumiwa na vijana wengi, hivyo kuharibu nguvu kazi ya Taifa.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini Esther Matiko amesema kwamba pombe hiyo inasababisha vifo vya vijana wengi nchini ambao ndio tegemeo kubwa na nguvu kazi ya Taifa.

“Katika kipindi hiki kifupi cha likizo yangu, nilikuwa jimboni kwangu na tumezika vijana wanne ambao wamefariki kutokana na matumizi ya viroba. Hivyo wananchi wa jimbo langu wameniagiza kuja kulieleza Bunge athari za pombe hiyo ili tuweze kujadili na kuona namna gani  ya kuliokoa Taifa hasa vijana kutoka katika janga hilo,” alifafanua Matiko.

Akiwasilisha taarifa ya Kamati, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile amesema kuwa Kamati imebaini uwepo wa uhusiano mkubwa kati ya matumizi ya pombe hizo na kuongezeka kwa tabia hatarishi zinazochangia ongezeko la vijana katika matumizi ya dawa za kulevya.


Aidha amesema kuwa hali hiyo inaathiri ufanisi wa nguvu kazi ya Taifa kutokana na madhara ya matumizi ya dawa za kulevya. Hivyo Kamati imeishauri Serikali kufungia kabisa uzalishaji na uuzwaji wa pombe hizo za viroba ili kulinusuru Taifa.

1 of 13 Print all In new window BBC DIRA YA DUNIA JUMATATU 06/02/2017


MDAU ANKO SAM WA JIJINI MBEYA ALOICHANGIA JESHI LA ZIMAMOTO MBEYA

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI

WEMA SEPETU KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUKUTWA NA BANGI NA LIZLA

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Msanii Maarufu nchini Wema Sepetu  pamoja  na Bakari Mcheni watapandishwa mahakamani kwa tuhuma za kukutwa na  bangi katika nyumba anayoishi.

Akizungumza na waandishi wa habari  Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi, Simon Sirro amesema kuwa Wema na mwenzake watapandishwa mahakamani kwa tuhuma za kukutwa na msokoto  wa bangi .

Amesema katika upekuzi Wema Sepetu alikutwa na Bangi  pamoja na karatasi za kuvutia bangi  zijulikanazo kama ‘Lizla’huku Bakari Mcheni akikutwa na misoko mitatu.

Kamanda Sirro amesema watu 10 watapelekwa mahakamani kwa ajili ya kula kiapo juu ya mwenendo wa kimaadili kutokana  kutumia dawa za kulevya ambapo  kwa ndani ya miaka miwili wasihusike na kutumia dawa hizo  pamoja na kuripoti Polisi  mara mbili kwa mwezi.

Watu hao ambao watakula kiapo hicho ni  Hamidu Chambuso, Rumeo George,  Sideo Mwandigo ,Khalidi Mohamed ‘TID’, Johanes Mansen, Said Masoud ‘PTT MAN’ Rajab Salum, Lulu Chelangwa,  Nasoro,  pamoja na Bakari Kierefu.

Katika operesheni hiyo walikamatwa watu 112  kati ya hao 12 ni wasanii Bongo fleva  na Bongo Movie.Aidha katika operesheni   dawa za kulevya  299 Puli 104  vilikamatwa na operesheni inaendelea .

Kamanda Sirro amesema kuwa watu wote waliokamatwa  hakuna mtu aliyeonewa katika hilo na walikuwa wazi katika mahojiano .

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam , Mhe. Paul Makonda amewaagiza Wenyeviti wa Serikali za Mtaa kutoa taarifa ya mtaa kwa wale ambao wanafanya biashara hiyo pamoja na kutumia pamoja na wazazi kwa watoto wanaotumia watoe taarifa .

Amesema ili kulifanya jiji la  Dar es Salaam kufuta  dawa za kulevya na kuzifanya kuwa historia ni mapambano ambayo sio ya mtu mmoja bali ni mapambano ya kila mtu.



 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam , Pau Makonda akizungumza na waandishi wa habari juu hatua mbalimbali za watu wanaojihusisha na dawa za kulevya  jijini Dar es Salaam. 
 Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi, Simon Sirro akizungumza na waandishi habari juu ya operesheni ya dawa za kulevya leo jijini Dar es Salaam
 Mama Mzazi wa Wema Sepetu akiwasili  katika kituo cha kati   jijini Dar es Salaam. 
Wananchi na waandishi wa habari wakiwa katika viwanja vya polisi katika kituo cha kati  jijini Dar es Salaam.
Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE FEBRUARY 7,2017

MAGAZETI YA LEO JUMANNE 7, 2017

Viewing all 110186 articles
Browse latest View live




Latest Images