Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida.
Viongozi, Watendaji na Watumishi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Singida wametakiwa kuhakikisha taarifa zote za mapato na matumizi zinawafikia wananchi wote katika ngazi ya Kata na Kijiji ili waweze kuelewa hasa kiasi cha fedha zilizoingizwa na Serikali katika Halmashauri na namna zinavyo tumika.
Agizo hili limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi katika ziara yake ya kuzitembelea Halmashauri zote za Mkoa huo kwa lengo la kujenga Uelewa wa pamoja, utumishi wa pamoja, na kasi ya pamoja ili kufikia lengo pamoja kwa maslai mapana ya Taifa.
Kwa upande wa Wakuu wa Idara na Vitengo Dkt Nchimbi amewaagiza wawe na taarifa za kila siku za watendaji na watumishi katika mnyororo wote wa kiutendaji na kiuongozi na kuepuka kutegemea taarifa za makaratasi na ili kuimrisha utendaji wa kuzingatia matokeo yanayo onekana.
Niaibu sana kwa Mganga Mkuu wa Wiwala (DM) kushindwa kutoa takwimu pale unapo ulizwa swali nje ya ofisi yako juu ya idadi ya watoto waliozaliwa ndani ya siku tatu katika wilaya yako au Afisa Elimu wa Halamashari unashindwa kutoa jibu la ni Walimu wangapi katika Halmashauri yako hawakuingia kazini kwa sabau za kiafya. Sinto penda hali hii iendelee kujitokeza katika Mkoa wa Singida. Aliongeza Dkt Nchimbi.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dr Rehema Nchimbi (wa pili kutoka kushoto) akishiriki kupalilia zao la mtama Mtama katika ziara aliyoifanya Mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dr Rehema Nchimbi akishiriki kupanda Mihogo katika ziara aliyoifanya Mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dr Rehema Nchimbi (wapili kutoka kulia) akishiriki kikamilifu katika shughuli za kilimo katika ziara aliyoifanya Mkoani humo.
Mkoa wa Singida Dr Rehema Nchimbi akishiriki chakula cha mchana baada ya kukaribishwa na wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Mwenge Singida katika ziara aliyoifanya Mkoani humo.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA