Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110182 articles
Browse latest View live

BALOZI WA CUBA AMUAGA KINANA LEO

$
0
0
  Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na Balozi wa Cuba, Jorge Luis Lopez (kushoto), alipofika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, kumuaga kufuatia kumalizika kwa mda wake wa kazi hapa nchini. (Picha na Bashir Nkoromo-MAKAO MAKUU YA CCM).
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimkaribisha Balozi wa Cuba, Jorge Luis Lopez (kushoto), alipofika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, kumuaga kufuatia kumalizika kwa mda wake wa kazi hapa nchini. (Picha na Bashir Nkoromo-MAKAO MAKUU YA CCM).


GOLF JWTZ LUGALO WATAKIWA KUTOBWETEKA NA MFULULIZO WA USHINDI WANAOUPATA

$
0
0
Na Luteni Selemani Semunyu, JWTZ.

Wachezaji wa Golf wa klabu ya Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania ya Lugalo wametakiwa kutobweteka na mfululizo wa ushindi waliopata katika mashindano mbalimbali badala yake wemewatakiwa kujiweka tayari na mashindano ya Kimataifa.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa klabu  hiyo Brigedia Jenerali Michael Luwongo mara baada ya kurejea kwa Timu  hiyo iliyokuwa ikishiriki Mashindano ya Chairman Troph yaliyofanyika kwa siku Mbili Moshi Mkoani Kilimanjaro ambako ilinyakua vikombe Vinne.

“Najua sie ni Klabu bora ya Golf nchini na yenye wachezaji wazuri kitaifa lakini sasa ni wakati wa kujiandaa Kimataifa ambako tutaitangaza nchi vyema katika mchezo huo na kuliletea Sifa jeshi letu.” Alisema Brigedia Jenerali  Luwongo.

Aliongeza kuwa licha ya kuweka maandalizi ya ushiriki wa kimataifa kwa mwaka 2017 lakini ni fursa kwa wanaotaka kujifunza golf wakati huu wa likizo za mwisho wa mwaka kujitokeza klwani shughuli zote za golf katika uwanja wa Lugalo zitaendelea  kama kawaida.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

MHARIRI WA HABARI MSTAAFU WA MAGAZETI YA UHURU, MZEE NAKAJUMO ATINGA NEWSROOM LEO KUWANOA VIJANA

$
0
0
 Mhariri wa Habari Mstaafu wa Uhuru Publications Ltd, Wachapishaji wa Magazeti ya Uhuru Mzalendo na Burudani Mzee Joe Nakajumo akimpiga msasa Kaimu Mhariri wa Makala Selina Wilson, katika chumba cha habari cha kampuni hiyo, Mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam. Mzee Nakajumo alifika leo katika chumba cha habari kwa mwaliko rasmi wa Kaim Mhariri Mtendaji wa UPL, Ramadhani Mkoma ili kuwapiga msasa waandishi wa habari. Kulia ni Mpigapicha Mwandamizi wa UPL, Bashir Nkoromo ambaye kwa sasa ameazimwa Katika Idara ya Itikadi na Uenezi, Kitengo cha Mawasiliano ya Umma, Makao Makuu ya CCM.
 Kaimu Mhariri wa Makala, Selina Wilson akimshukuru Mzee Nakajumo kwa msasa aliompiga
 Mpigapicha Mwandamizi wa UPL, Bashir Nkoromo ambaye kwa sasa ameazimwa Katika Idara ya Itikadi na Uenezi, Kitengo cha Mawasiliano ya Umma, Makao Makuu ya CCM, akimshukuru Mzee Nakajumo baada na yeye kupata nasaha na kukumbushwa namna kazi zilivyokuwa zikifanyika wakati akipigapicha UPL ambapo picha zilikuwa lazima zitathminiwe ubora  wake na Mzee huyo, Nakajumo wakati akiwa bado hajastaafu UPL
Mzee Nakajumo akiendelea kusikiliza kila liyetaja kulifahamu kwa undani jambo linalohusu uandishi wa habari ulio wa makini zaidi. PICHA ZOTE NA JUMAANE GUDE 

NEWS ALERT: MTOTO WA IBRAHIM SANYA AINGIA KATIKA KINYANG'ANYIRO CHA UBUNGE WA DIMANI ZANZIBAR

$
0
0
Mtoto wa aliyekuwa, Mbunge wa jimbo la Mji Mkongwe, Ibrahim Sanya (CUF),  Waheed Muhammad Sanya aingia kwenye kinyang'anyiro cha kugombea ubunge kwa jimbo la dimani kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo.
Waheed Muhammad sanya ,mhadhiri wa Chuo kikuu cha taifa Zanzibar -SUZA.

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO NA BALOZI WA JAPANI NCHINI TANZANIA WAJADILI MAENDELEO YA MIUNDOMBINU

$
0
0
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akisisitiza jambo kuhusu kuharakisha maendeleo ya ujenzi wa miundombinu itakayokuwa chachu ya kufikia uchumi wa kati unaotegemea viwanda, wakati Balozi wa Japan na ujumbe wake walipomtembelea na kufanya mazungumzo na Waziri huyo Makao Makuu ya Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (wa kwanza kulia) akisikiliza maelezo toka kwa Mwakilishi Mkazi Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Japani (JICA) kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo hasa ujenzi wa barabara mkoani Arusha na maeneo mengine ya nchi, Kikao hicho kimefanyika Makao Makuu ya Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es salaam.

 Balozi wa Japani Nchini Tanzania, Masaharu Yoshinda (kushoto) akielezea mtazamo wake kuhusu umuhimu wa kufungua mikoa ya Kanda ya Kati na Magharibi mwa Tanzania kwa miundombinu ikiwemo barabara na reli ambayo Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.  Dkt. Philip Mpango (Mb) alimweleza Balozi huyo kuwa ina faida kwa maendeleo ya nchi, walipokutana na kufanya mazungumzo Makao Makuu ya Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es salaam.
 Balozi wa Japani Nchini Tanzania Masaharu Yoshinda (kushoto) na Mwakilishi Mkazi Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Japani (JICA) Bw.  Toshio Nagase, (kulia), wakimsikiliza Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (hayupo pichani) kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Maendeleo inayofadhiliwa na Japan katika sekta ya Miundombinu zikiwemo barabara nchini Tanzania, Mazungumzomyaliyofanyika Makao Makuu ya Wizara,Jijini Dar es salaam.
 Ujumbe   kutoka Japani ukiongozwa na Balozi wa Japani Nchini Tanzania, Masaharu Yoshinda, ukisikiliza kwa Makini maelezo ya Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.  Dkt. Philip Mpango (hayupo pichani) kuhusu azma ya Tanzania kuwa na Bandari itakayo himili ushindani barani Afrika.
 Maafisa  kutoka Tanzania walioambatana na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.  Dkt. Philip Mpango (hayupo pichani), katika kikao na Balozi wa wa Japani Nchini Tanzania, Masaharu Yoshinda wakinukuu Maelezo yaliyokuwa yakitolewa, kuhusu umuhimu wa Miundombinu ikiwemo barabara na reli kwa manufaa ya watanzania, wakati walipokutana na kufanya mazungumzo Makao Makuu ya Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es salaam.

IN LOVING MEMORY OF MAMA ROSE SHOMARI

$
0
0
Its is 11 years since you departed from us, in this day a memory of a life so beautifully lived and a heart so deeply loved. We will always remember you and the lessons of life you gave us. May God hold you in the palm of his hand. In our hearts, you will always be remembered by your sons and daughters, grandsons and granddaughters and the whole Shomari's clan.
 
We thank the Lord for your life, great advice, teacher, counselor and a big blessing for us. May the almighty Lord rest your soul in Peace until we meet again.Our hope comes from the Lord as he says he will wipe every tear from their eyes there will be no more death or mourning or crying or pain…Rev 21:4.

JESHI LA POLISI MKOANI KIGOMA LAKAMATA RISASI 408 ZILIZOKUWA ZIKIMILIKIWA NA MTU MMOJA WILAYANI KASULU MKOANI KIGOMA

$
0
0
Na Rhoda Ezekiel -Globu ya Jamii,Kigoma.

JESHI la polisi Mkoani Kigoma limefanikiwa kukamata risasi 408 za bunduki zilizo kuwa zikimilikiwa na Mtu mmoja ambaye jina lake halikutajwa mkazi wa Kijiji cha Makere Wilayani kasulu Mkoani Kigoma.

Akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake leo Kamanda wa Jeshi la polisi Mkoani Kigoma,DCP Fredinand Mtui alisema mnamo tarehe 5Desemba majira ya 08:20 huko maeneo ya makere Center katika kijiji cha Makere askari wakiwa doria walipokea taarifa kutoka kwa raia wema wanao chukia uhalifu kuwa kuna mtu wana wasiwasi nae kuwa anamzigo usio kuwa wa kawaida.

Mtui alisema Askari walianza ufuataliaji na kufanikiwa kukamata mtuhumiwa mmoja ambaye jina lake limehifashiwa kwa shughuli za kiusalama, alipo fanyiwa upekuzi mtuhumiwa huyokatika Sanduku lake alilokuwa amebeba alikutwa akiwa na risasi 408 za bunduki aina ya SMG/SAR alizokuwa amezifunga ndani ya nguo zake .

Aidha Mtui alisema upelelezi bado unaendelea ,Mtuhumiwa atapelekwa mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria pindi upelelezi utakapo kamilika ilikutoa fundiaho kwa wananchi wengine wanao nunua siraha kwa lengo la kufanyia uhalifu.

"nichukue fursa hii kuwaasa wahalifu wanao jihusisha na biashara ya kuuza na kununua risasi na siraha nyingine waache biashara hiyo, wafanye kazi nyingine ambazo zinatambulika kisheria vyombo vya ulinzi na usalama viko imara kuwatafuta wahalifu hao na kuwachukulia hatua za kisheria,"alisema Mtui.

Sambamba na tukio hilo alisema mnamo tarehe 6Desemba huko maeneo ya Mwanga Vamia Manispaa ya Kigoma ujiji Hussen Athuman (36) Mkazi wa mwanga Vamia alikutwa chumbani kwake akiwa amejinyonga kwa kutumia kamba ya katani. 

Mtui alisema usiku wa tarehe5 marehemu alimpigia simu Dada yake na kudai kuwa walikuwa na ugomvi na mkewe ugomvi huo uliopelekea mkewe kuondoka siku nne zilizo pita , na kumwambia amueleze kaka yake kwamba atachukua maamuzi magumu.

Alisema chanzo cha kujinyonga ni ugomvi baina ya baina ya marehemu na mkewe, mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospital ya rufaa maweni kusubili kukabidhiwa kwa ndugu kwa taratibu za mazishi.
 Risasi 408 za bunduki zilizo kuwa zikimilikiwa na Mtu mmoja ambaye jina lake halikutajwa, mkazi wa Kijiji cha Makere Wilayani kasulu Mkoani Kigoma. 
Kamanda wa Jeshi la polisi Mkoani Kigoma,DCP Fredinand Mtui akizungumza na Waandishi wa habari (hawapo pichani),kuhusiana na tukio hilo la kukamatwa risasi za moto 408,zilizokuwa zikimilikiwa na mtu mmoja mkoani humo.

WANANCHI WA SINGIDA KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME WA UPEPO

$
0
0
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano Mh. January Makamba amesema kuwa mpango wa serikali ni kuwa na vyanzo vingi vya uzalishaji umeme ili kuwa na vyanzo vya nchi endelevu na kuunga mkono juhudi za benki ya dunia kuzalisha umeme wa upepo katika nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania.

Makamba amesema hayo wakati wa Kongamano la wadau wa Nishati ya umeme walipokutana kuzungumzia matumizi ya Nishati ya umeme inayozalishwa kwa njia ya upepo itakayounganishwa kwenye gridi ya taifa na mfumo huo utawasaidia wananchi wa Singida .

"Kwa kuwa umeme huo utazalishwa kwenye maeneo ya vijijini, wananchi wanatakiwa kupata umeme kwa bei rahisi kulingana na uchumi wao na sio kuuziwa umeme kwa bei juu, na zaidi Wizara yake inapenda kuweka  wazi kuwa huu mradi una faida kubwa sana kulingana na mfumo wa nchi ulivyo,"amesema Makamba.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya kuzalisha umeme wa upepo Afrika Mashariki Six Telecoms,  Rashid Shamte amessema kuwa mfumo huu wa gridi ndogondogo una faida kubwa sana kwa wananchi kwani asilimia kubwa kulingana na ripoti ya benki ya dunia wananunua umeme wa bei nafuu kwahiyo serikali imekubaliana na kampuni yetu na  imeweza kukubali kuwa mradi huu una  tija na  utasimamiwa na serikali yenyewe kupitia kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida pamoja na Halmashauri.

Shamte ameendelea na kusema, kwa Phase ya kwanza watatoa umeme megawati 100 na itaendelea mpaka kufika megawati 300 na wataunganisha kwenye gridi ya taifa, na huu mradi utakuwa na faida kwa wananchi pamoja na wale watakaotolewa kwenye maeneo yao watafaidika kwa kulipa stahiki zao.

Kwa upande wa Wizara ya Nishati na Madini, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Juliana Pallangyo amewataka wawekezaji hao kuuza umeme kwa bei rahisi kwani mara nyingi mipango ya serikali imekuwa haiendani na mikakati ya wawekezaji kwahiyo wanategemea kuona kuwa mradi huu uwe nafuu ya wananchi wa vijijini kupata umeme kwa bei rahisi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira na Muungano Mheshimiwa January Makamba akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa umeme kujadili mkakati ya kuzalisha nishati ya Umeme kwa njia ya Upepo leo katika ukumbi wa Hotel ya Hyatt Jijini Dar.


WAHARIRI WAKUTANA KUPITIA SHERIA YA HUDUMA YA VYOMBO VYA HABARI ILIYOPITISHWA NA BUNGE

$
0
0
Na Dotto Mwaibale.

WAHARIRI wa vyombo vya habari wamekutana katika mkutano maalumu wa siku mbili kwa ajili ya kujadili mambo kadhaa yanayohusu tasnia hiyo nchini.

Akizungumza wakati akifungua mkutano huo Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Theophil Makunga alisema mkutano huo utawajumuisha wadau wa sekta ya habari kutoka ndani na nje ya nchi.

"Tumewaalika wenzetu wa nje ili watupe uzoefu wa jinsi wanavyofanya katika tasnia ya habari katika nchi zao" alisema Makunga.

Alisema katika mkutano huo ambao unafanyika Hoteli ya Protea Court Yard mambo yatakayo zungumziwa ni kupitia sheria ya huduma ya vyombo vya habari iliyopitishwa na Bunge na kusainiwa na Rais Dk. John Magufuli pamoja na kujadili mpango mkakati wa Jukwa la Wahariri wa kuendeleza tasnia ya habari nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Habari Tanzania (TMF), Ernest Sungura alisema ni muhimu kwa wanahabari kuwa na mpango mkakati wa miaka 10 ili kupata majibu sahihi ya tasnia hiyo.
 Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Theophil Makunga (kulia), akizungumza Dar es Salaam leo wakati akifungua mkutano wa siku mbili wa wahariri  kupitia sheria ya huduma ya vyombo vya habari uliyopitishwa na Bunge pamoja na kujadili mpango mkakati wa TEF wa kuendeleza tasnia ya habari nchini. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Habari Tanzania (TMF), Ernest Sungura.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Habari Tanzania (TMF), Ernest Sungura.
 Makamu Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile akizungumza kwenye mkutano huo.
 Taswira ndani ya ukumbi wa mkutano huo
Wahariri ndani ya chumba cha mkutano.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

SERIKALI YAOMBWA KUWAPATIA BIMA YA AFYA WALEMAVU WA NGOZI

$
0
0
Na Anthony John Globu ya Jamii.


CHAMA cha watu wenye ualbino Tanzania (TAS) kimetoa wito kwa Serikali kuwapatia bima ya Afya watu wenye ulemavu wa ngozi ili kuweza kuwasaidia pale wanapokuwa na matatizo ya kiafya.

Akiongea  na waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam katika Ofisi ya chama hicho iliyopo hospitali ya Ocean Road, Muweka hazina Abdilah Omary amesema watu wenye ualbino hasa waliopo vijijini wanapata changamoto kubwa ya upatikanaji wa matibabu hasa pale wanapo sumbuliwa na magonjwa mbali mbali.

 Abdilah ametoa wito kwa jamii na familia zenye watu wenye ualbino kuwapa malezi yanayoendana na hali yao tofauti na Jamii nyingi kwa hivi sasa wanawalazimisha watu wenye ualbino kufanya kazi ngumu kama kuchunga ngo'mbe na kulima.

Wakati huo huo wajumbe wa chama cha watu wenye ualbino Tanzania wamemchangia kiasi cha sh.milioni moja Leonard Gaspar mwenye ulemavu wa ngozi Mkazi wa Morogoro Matombo anayesumbuliwa na kansa ya ngozi.

Hata hivyo Leonard  amewashukuru wajumbe wa chama hicho kwa mchango huo huku akiomba jamii na wadau mbalimbali kuwapa msaada pale wanapoweza ili apate mtaji wakumsaidia katika maisha ya kila siku na matibabu.

Chama hicho cha watu wenye ualbino Tanzania wametoa wito kwa jamii kumsaidia kijana Leonard anaye sumbuliwa na tatizo la kansa ya ngozi kwa muda mrefu.

Hata Hivyo Abdilah ameomba Jamii ya watanzania watakaoguswa na tatizo alilonalo Leonard wanaweza kutoa michango yao kwa kuwasiliana na Ofisi za Chama Cha Watu Wenye Ualbino kilichopo Katika Hospital ya Ocean Road.


Muweka hazina wa Chama cha Watu wenye Ualbino Tanzania, Abdilah Omari  akiwa pamoja Leonard Gasper anayesumbuliwa na tatizo la kansa na kumpatia msaada wa kiasi cha fedha milioni moja kwa ajili ya matibabu.

KATIBU MKUU WA TIMU YA RYHNO RANGERS AFUNGIWA MIEZI MITATU

$
0
0
KATIBU Mku wa klabu ya Rhino Rangers, Dickson Cyprian Mgalike amefungiuwa miezi mitatu kwa kosa la kuidanganya kamati kwa kutoa taarifa potofu katika barua aliyoiandikia Bodi ya Ligi.

Maamuzi hayo yametolwa na Kamati ya usimamizi na uendeshaji baada ya kupitia ripoti nzima na kugundua kuwa Mgalike aliwadanganya na imeamua kumpa adhabu ya Kumfungiwa miezi mitatu.Hapo awali, Kamati ilimuadhibu Mchezaji Sameer Mwinyishere kwa kosa la kumrushia chupa ya maji mwamuzi.

Katibu aliandika barua kusema kwamba Sameer hakufanya kosa hilo na alimtaja mchezaji Yusuf Mputa kwamba ndiye aliyefanya kitendo cha utovu wa nidhamu kwa kumrushia Mwamuzi chupa ya maji.

Kamati ya Usimamizi na Uendeshaji kwa kushirikiana watendaji wa Bodi ya Ligi ilifanya uchunguzi na kubaini mchezaji Yusuph Mputa hakuwepo kwenye Orodha ya Wachezaji wa siku hiyo. Adhabu hiyo imetolewa kwa kufuata kanuni ya 41(6).

Wateja 15,345 wafaidika na Mradi wa Umeme wa KIA

$
0
0
Na Teresia Mhagama
Imeelezwa kuwa zaidi ya wateja wa awali 15,345 wameunganishwa na huduma ya umeme baada ya kukamilika kwa mradi wa Kituo cha Kupoozea Umeme cha KIA mkoani Kilimanjaro.

Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo mara baada ya kufanya ziara ya kikazi katika Kituo hicho.

Dkt. Pallangyo alisema kuwa, mradi huo ulihusisha ujenzi wa Transfoma mbili zenye uwezo wa Megawati 20 kila moja (2x20MVA) pamoja na jengo la kuendeshea mitambo ambapo Kituo kinasambaza umeme kwa wateja kupitia njia 6 za msongo wa kilovoti 33.

“Niseme tu kuwa, mradi huu ni muhimu sana kwani kukamilika kwake kumeboresha hali ya upatikanaji wa umeme katika maeneo ya Wilaya ya Hai, migodi ya Mirerani na maeneo mengine ya mkoa wa Kilimanjaro na Arusha,” alisema Dkt. Pallangyo.

Aliongeza kuwa Kukamilika kwa kituo hicho kumeimarisha pia upatikanaji wa umeme katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Alisema kuwa, utekelezaji wa Mradi huo ulianza rasmi tarehe 22 Machi, 2010 na gharama za mradi ni Shilingi bilioni 15.3 sawa na Dola za Marekani milioni 7.08.

Mradi huo wa KIA umetekelezwa kupitia Mradi wa TEDAP ulio chini ya Wizara ya Nishati na Madini ambao unahusika na uboreshaji wa njia za usafirishaji, usambazaji na ujenzi wa vituo vya umeme katika Mikoa ya Dar es salaam, Arusha na Kilimanjaro. 

Mradi wa TEDAP unahusisha Ujenzi wa njia za kusafirishia umeme wa msongo wa kilovolti 132, ujenzi wa vituo vitano vya kupozea umeme jijini Dar es salaam pamoja na Kituo cha kupozea Umeme cha KIA.

Mradi pia unahusisha ujenzi wa vituo vipya 19 vya kusambaza umeme wa msongo wa kilovolti 33 pamoja na njia za usambazaji umeme kwa urefu wa kilomita 102.497 za msongo wa kilovolti 33 na kilomita 34.018 za msongo wa kilovolti 11 katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha na Kilimanjaro.
 Naibu Katibu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (katikati) akikagua Chumba cha kuongozea Mitambo ya Umeme kwenye Kituo cha kupoozea  Umeme cha KIA mkoani Kilimanjaro.  Kulia ni Mhandisi Neema Rushema, Mhandisi Nishati kutoka Wizara ya Nishati na Madini.
 Naibu Katibu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (katikati) akikagua Mitambo ya Umeme kwenye Kituo cha kupoozea Umeme cha KIA mkoani Kilimanjaro.  Kushoto Mhandisi Neema Rushema, Mhandisi Nishati kutoka Wizara ya Nishati na Madini.


Baadhi ya mitambo ya Umeme katika Kituo cha Kupoozea Umeme cha KIA.

SAANYA, MPENZU, MROPE WAONDOLEWA KWENYE RATIBA YA LIGI KUU

$
0
0

WAAMUZI waliochezesha mchezo namba 49 kati ya Yanga na Simba, Martin Saanya na Samweli Mpenzu wametolewa kwenye ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, huku suala lao likipelekwa kwenye Kamati ya Waamuzi ili ishughulikie tatizo lao kitaalam.

Maamuzi hayo yamefanyika baada ya Kikao cha Kamati ya Usimamizi na Uendeshaji ya Bodi ya ligi, kuwaita na kuwahoji na kuangalia mkanda wa mchezo husika. Kamati imebaini mapungufu mengi ya kiutendaji yaliyofanywa na waamuzi hao, na hivyo kuitaka kamati ya waamuzi ishughulikie.

Pia Mwamuzi Rajabu Mrope aliyechezesha mchezo namba 108 kati ya Mbeya City na Yanga naye ametolewa kwenye Ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom msimu 2016/2017 na kurudishwa kwenye Kamati ya Waamuzi ili waweze kumpangia daraja lengine la uamuzi.

Mrope alitiwa hatiani kwa kosa la kutojiamini mchezoni na kwenye uamuzi wake na kushindwa kuudhibiti mchezo.Miongoni mwa matatizo ya mwamuzi huyo ni kukubali goli, kisha kukataa na mwisho kukubali tena hali iliyoonyesha kutokujiamini na kusabisha mtafaruku mkubwa katika mchezo huo.

Katika ligi ya Daraja la kwanza, Mwamuzi Thomas Mkombozi aliyechezesha mechi namba 15B kati ya Coastal Union na KMC ameondolewa kwenye orodha ya waamuzi kutokana na kushindwa kuudhibiti mchezo na kutoshirikiana na wasaidizi wake.

Adhabu hiyo ametolewa baada ya Kamati ya usimamizi na uendeshaji wa ligi kuwaita waamuzi wa mchezo huo na kufanya mahojiano nao na kugundua Mkombozi alikuwa na maamuzi mengi bila umakini na hakushirikiana kiufundi na wasaidizi wake. Kutokua makini kulisababisha mchezo huo kumalizika kwa vurugu. 

Pia Klabu ya Coastal Union imepewa adhabu ya kucheza bila ya mashabiki kwa mechi mbili za nyumbani na mechi moja ya nyumbani kuchezwa uwanja wa ugenini kwa kosa la mashabiki wa timu hiyo kumshambulia Mwamuzi Thomas Mkombozi na kumsababishia majera ha maumivu makali.

kuhusu Mwamuzi Ahmed Seif, Kamati ya Usimamizi na Uendeshaji ya bodi ya Ligi, imemfungulia na kumtoa kwenye orodha ya waamuzi wa Ligi kuu mwamuzi huyo aliechezesha mchezo namba 28 kati ya African Lyon na Mbao FC. hivyo, Mwamuzi Ahmed Seif atarudishwa kwenye kabati ya waamuzi ili apangiwe majukumu mengine.

DKT. SHEIN MGENI RASMI MAHFALI YA 14 CHUO KIKUU CHA TUNGUU ZANZIBAR

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi wakati alipowasili katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Tunguu (Zanzibar University) Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja akiwa mgeni rasmi katika Mahfali ya Kumi na Nnne yaliyofanyika Chuoni hapo.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu,pia Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Prof.Suleiman Bin- Nassry Basahal alipokuwa akiwatunuku Stashahad na Shada wahitimu katika fani mbali mbali wa mwaka 2016 wakati wa sherehe ya Mahfali ya kumi na nne yaliyofanyika leo katika Chuo hicho huko Tunguu Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipokea zawadi kutoka wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu,pia Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Prof.Suleiman Bin- Nassry Basahal wakati wa sherehe ya Mahfali ya kumi na nne iliyofanyika leo katika Chuo hicho huko Tunguu Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitoa hutuba yake wakati wa sherehe ya mahfali ya kumi na nne (14) katika Chuo Kikuu cha Tunguu (Zanzibar University) Wilaya ya Kati,Mkoa wa Kusini Unguja,(kulia) Prof.Saleh Idriss Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo na (kushoto) Mkuu wa Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu,pia Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Prof.Suleiman Bin- Nassry Basahal.

TAARIFA KWA UMMA


MAJENERALI WAPYA WAVISHWA VYEO MAKAO MAKUU JWTZ

$
0
0


Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mwamunyange (Kushoto), akimvisha cheo cha Meja Jenerali,Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Anga Brigedia Jenerali George William Ingram,Makao Makuu JWTZ Upanga Dar es Salaam.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mwamunyange (kushoto) akimvisha cheo cha Meja Jenerali Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Brigedia Jenerali Michael Isamuhyo, Makao Makuu JWTZ Upanga Dar es Salaam.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange (Wa pili kushoto) pamoja na mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Salvatory Mabeyo (Wa pili kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na ma Meja Jenerali wapya, Makao Makuu JWTZ Upanga Dar es Salaam.

Picha kwa hisani ya kurugenzi ya habari na uhusiano JWTZ

UKOSEFU WA HUDUMA YA KWANZA KWENYE VIWANJA MIKOANI KUNAWEZA KULETA MAAFA MAKUBWA

$
0
0
Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

BAADA ya kufariki uwanjani kwa mshambuliaji wa timu ya vijana ya Mbao FC Ismail Khalfan siku ya Jumapili ya December 4, Hospitali wametoa ripoti ya kilichosababisha kifo cha mchezaji huyo wakati wa mchezo kati ya Mbao FC dhidi ya Mwadui FC.


 Ripoti iliyotolewa na hospitali ya mkoa wa Kagera kuhusiana na kifo cha mchezaji huyo, kupitia kwa jeshi la Polisi, Ismail alifariki uwanjani kutokana na kupata tatizo la kusimama ghafla kwa moyo (Sudden Cardiac Arrest-SCA).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi (SACP) Augustin Ollomi ametoa taarifa baada ya uchunguzi wa madaktari kuhusu kifo cha mchezaji huyo ambaye hakuwa na jeraha lolote ila baada ya uchunguzi walibaini kusimama ghafla kwa moyo (Sudden Cardiac Arrest) kulisababisha kifo.

Kulifunguliwa jalada la uchunguzi, bahati nzuri madaktari walifanya huduma ya haraka, kwa mwonekano huyu marehemu Ismail Mrisho Khalfan ambaye ndiye alikuwa ameanguka pale uwanjani kwa nje hakuonekana kuwa na jeraha kwa hiyo madaktari wakatueleza lazima afanyiwe uchunguzi wa kina.

Kutokana na tatizo hilo, Ismail alitakiwa kupatiwa huduma ya kwanza mara baada ya kuanguka kwa kupata msaada ni kupata electrical shock ili kushtua mfumo wa umeme wa moyo, na hii inapaswa kufanyika ndani ya sekunde chache baada ya kubainika kuanguka na ukisimama bila kurudi katika hali yake unasababisha kifo ndani ya sekunde chache.

Kitaalamu kawaida moyo una mfumo wa umeme (heart electrical system), ambao unadhibiti mapigo ya moyo, mfumo huu ukisimama basi moyo unashindwa kusukuma damu sehemu muhimu kama ubongo na ogani kuu.


Ukosefu wa vifaa uwanjani ikiwemo daktari mkuu wa uwanja na gari la wagonjwa limekuwa kama wimbo wa taifa kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) kwa kushindwa kuwa na vifaa hivyo na pale mchezaji anapotokea anapata tatizo anashindwa kupata huduma kwa usahihi na wakati muafaka ,na ikumbukwe katika msimu huu wa ligi kuu Vodacom, Golikipa wa timu ya African Lyon aliweza kuvunjika mbavu katika mchezo wao dhidi ya JKT Ruvu lakini hakukuwa na gari ya wagonjwa na aliishia kubebwa kwenye gari aina ya Pick up.

Tumeshuhudia mchezaji wa Stand United Chidiebele akiumia uwanjani na kuvunjika taya lakini hakukuw ana huduma ya uhakika achilia hao wapo wachezaji wengi wanaopata madhara ila uhakika wa huduma katika viwanja vya mikoani ni mdogo sana na hata katika ripoti za waamuzi wamekuwa wakiandika kutokuwepo kwa gari la wagonjwa ila hakuna jitihada zinazofanywa.

MAJALIWA AKITAZAMA GARI LILILOJENGEWA BODI LA MBAO

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama gari aina ya Toyota iloyojengewa bodi la mbao wakati alipotembelea kiwanda cha Fibreboars 2000 Limited cha Arusha akiwa katika ziara ya kazi mkoani humo Desemba 5, 2016.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

BIDHAA ZA MCHELE NA CHUMVI ZAENDELEA KUPEWA KIPAUMBELE

MAMLAKA YA USAFIRI WA ANGA TANZANIA WAADHIMISHA SIKU YA USAFIRI WA ANGA DUNIANI(ICAD

$
0
0
 Wanafunzi wa shule mbalimbali za sekondari za jijini Dar es Salaam, wakimsikiliza kwa makini Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya usafiri wa Anga Tanzania(TCAA) Vallery Chamulungu wakati akiongea na kuzindua Kongamano la siku moja la maadhimisho ya siku Usafiri wa anga Duniani(ICAD) yaliyofanyika makao makuu ya (TCAA) Ukonga Banana jijini Dar es Salaam. Lengo kuu la kongamano hilo ilikuwa ni kuwahamasisha wanafunzi hao wapende masomo yanayohusiana na usafiri wa Anga.
 Afisa mwanadamizi Idara ya uongozaji ndege Mwanajumaa Kombo  akitoa elimu juu ya masuala ya uongozaji wa ndege  kwa wanafunzi wa shule mbalimbali za sekondari za jijini Dar es Salaam,  wakati wa Kongamano la siku moja la maadhimisho ya siku Usafiri wa anga Duniani(ICAD), yaliyofanyika makao makuu ya (TCAA) Ukonga Banana jijini Dar es Salaam. Lengo kuu la kongamano hilo ilikuwa ni kuwahamasisha wanafunzi hao wapende masomo yanayohusiana na usafiri wa Anga.
 Mkufunzi wa Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania Aristid Kanje akitoa mafunzo juu ya kozi mbalimbali zinazotolewa na chuo cha Usafiri wa Anga(CATC),wakati Kongamano la siku moja la maadhimisho ya siku Usafiri wa anga Duniani yaliyofanyika makao makuu ya (TCAA) Ukonga Banana jijini Dar es Salaam. Lengo kuu la kongamano hilo ilikuwa ni kuwahamasisha wanafunzi hao wapende masomo yanayohusiana na usafiri wa Anga.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Viewing all 110182 articles
Browse latest View live


Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>