Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109606 articles
Browse latest View live

WABUNIFU WA BIDHAA ZA KILIMO WAKUTANISHWA NA TASISI ZA FEDHA

0
0

Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Jumla ya Vikundi 16 kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini vinavyojihusisha na masuala ya kilimo vimekutanishwa na Tasisi za kifedha na mabenki ili kuwezeshwa kama mpango wa taasisi ya Land O Lakes.

Akizungumza na Globu ja Jamii,Mshauri wa biashara bunifu kutoka tasisi hiyo ,Renalda Lema amesema kuwa katika vikundi hivyo 16 wamewakilishwa na watu wawili wawili,ili kuwasilisha ubunifu wao kwa taasisi hizo na kupata fursa ya kupanua biashara yao.

“Kama ambavyo unaweza kuona wabunifu walivyotengeza mashine mbalimbali, ambazo zitaweza kumuondoa mkulima kutoka sehemu moja hadi nyingine, hasa katika serikali hii ambayo inahamasisha uchumi wa viwanda, hivyo sisi tumeona uchumi wa viwanda hauwezi kufanikiwa bila ya kuanza kuwawezesha wakulima katika hatua ya awali kabisa” amesema Renalda.

Ametoa wito kwa wadau na taasisi mbalimbali ambazo zinahitaji kuwawezesha wakulima hao kwa namna moja ama nyingine,kuwasiliana na taasisi ya Land O’ Lakes kuwakutanisha na wakulima hao.
Mkurugenzi wa tasisi ya fedha ya Brac, Mahufuzii Ashrafu , akizungumza na baadhi ya wabunifu waliokutanishwa na kampuni hiyo ili waweze kuwezeshwa kama mpango wa tasisi ya Land O Lakes ili waweze kufikia malengo waliyojiwekea.
Mbunifu wa mashine ya kukamua matunda kutoka mkoa wa Songwe, Yohana Mwanzyunga(wa kwanza kulia) akiwaonyesha washiriki wengine mtambo wa kukamua matunda.
Baadhi ya washiriki wakiangalia mashine ya kupukucha halizeti

YALE YALEEEE.......

0
0
 Mtembea kwa miguu ambaye jina lake halikufahamika mara moja, akiwa amesimama katikati ya barabara kutaka kuvuka katika eneo lisilokuwa na alama za kivuko, huku magari yakiendelea kupita kwa kumkwepa, katika Barabara ya Kigogo Jijini Dar es salaam.

VIKWAZO VISIVYO VYA KIKODI KATI YA TANZANIA NA RWANDA VYATAKIWA KUONDOLEWA KATIKA KUKUZA BIASHARA

0
0
Picha ya pamoja ya viongozi waandamizi kati ya Tanzania pamoja na wafanya biashara wa Rwanda.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Edwin Ngonyani amesema ushirikiano kati ya Tanzania na Rwanda ni wa kimaendeleo hivyo lazima kuondolewa kwa vikwanzo visivyo vya kikodi.

Ngonyani ameyasema hayo leo wakati wa mkutano wa siku mbili kati Tanzania na Rwanda kujadili masuala ya maendeleo ya biashara kati ya nchi hizo, amesema kuondolewa kwa vikwanzo visivyo vya kikodi kutaongeza maendeleo katika nchi zote mbili katika ukuaji wa uchumi.

Amesema bidhaa zinazozalishwa nchini  Tanzania  zikifika Rwanda ziweze kukubalika hivyo hivyo na bidhaa za Rwanda zikubalike na mamlaka zilizopo hapa nchini.

Ngonyani amesema Tanzania imeweka mazingira bora ya uwekezaji ambapo wananachi wa Rwanda wanaweza kuwekeza  hapa nchini .

Naye Waziri wa Biashara , Viwanda na Jumuiya ya Afrika Mashariki wa nchini Rwanda, Francois Kanimba amesema kuwa ushirikiano kati ya Tanzania ni maendeleo ya kibiashara katika sekta mbalimbali ikiwemo ya sekta ya usafirishaji.

Aidha amesema  mkutano huo utatoa matumaini mapya kwa nchi hizi mbili kuweza kunufaika na kibiashara pamoja na  kutatua changamoto  wanazozipata wafanyabiashara wa nchi hizo.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasilano, Mh. Edwin Ngonyani akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji katika mkutano kujadili masuala ya biashara kati ya Tanzania na Rwanda leo jijini Dar es Salaam. 
Sehemu ya washiriki wa mkutano wa mamlaka za Rwanda na Tanzania pamoja na wafanyabiashara wa Tanzania.

Viongozi wa waandamizi wa Tanzania na Rwanda wakitembeleo baadhi ya bidhaa zinazozalishwa nchini na Kampuni ya Rwanda leo jijini Dar es Salaam.

RAIS DKT. MAGUFULI AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika leo tarehe 07 Desemba Ikulu jijini Dar es Salaam. Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa. PICHA NA IKULU

RC Gambo kukabidhi Pikipiki 200 – Jumamosi.

0
0

Nteghenjwa Hosseah, Arusha.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo mapema leo amekutana wa waendesha boda boda 200 watakaonufaika na mradi wa kuwainua vijana kiuchumi katika Jiji la Arusha kwa kupatiwa Pikipiki zisizokuwa na riba.

Mhe. Gambo amekutana na vijana hao ili kukamilisha taratibu za mwisho na kuangalia masuala ya usalama kabla hawajakabidhiwa Pikipiki hizo.Katika Kikao hicho vijana hao wamekubalina kwa Pamoja kwamba watarejesha Tsh 7,000 kwa siku na pia na kwa atakayeweza kwa wiki Tsh 49,000 ama kwa Mwezi itakua Tsh210,000.

Pia walikubaliana kwamba ni ruksa kwa yeyote atakayeweza kulipia zaidi ya kiasi icho ili aweze kumaliza mkopo wa Pikipiki yake na aweze kumilikshwa Pikipiki hiyo.Haikatazwi kwa mtu yeyote kuleta zaidi ya Tsh 7,000 kwa siku ili uweze kumalizia mkopo wako mapema na ikitokea umekamilisha mkopo huo hata kwa miezi miwili unamilikishwa Pikipiki alisema Mhe. Gambo.

Vijana hao pia walihoji kuhusu service ya Pikipiki hizo na Mwakilishi wa Kishen Enterprises Ltd ambao pia ni mawakala wa Pikipiki aina ya Toyo Mkoani hapa alisema Pikipiki hizo zina warrant wa meizi sita na endapo zitapata hitilafu kwenye Engine katika kipindi hicho wataweza kuifanyia matengenezo bila gharama yeyote au kubadilishiwa Pikipiki nyingine.

Kwa hesabu za kawaida vijana hawa watarejesha Tsh 2,135,000 kwa mchanganuo ufuatao:

Tsh 2,000,000 ni Bei ya Pikipiki

Tsh 135,700 ni gharama ya Bima Kubwa hivyo

Vijana hao watarejesha Tsh 7,000 X siku 305 = 2,135,000.

Tunaposema watalipia kwa kipindi cha mwaka mzima tunaamisha siku 60 zitakua kwa ajili ya service na dharura nyingine na siku 305 ndio watakazoleta marejesho Alimalizia Mkuu wa Mkoa.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha amesema Pikipiki hizo zitakabidhiwa siku ya Jumamosi tarehe 10/12/2016 saa nne Asubuhi kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akizungumza na waendesha boda boda 200(hawapo pichani) watakaopatiwa Pikipiki zisizokuwa na riba wakati wa kikao na vijana hao kukamilisha taratibu na masuala ya usalama kabla ya kukabidhiwa Pikipiki hizo.
Kijana muendesha boda boda(aliyesimama) akichangia kuhusiana na kiasi gani cha Fedha kirejeshwe kwa siku ili kukamilisha mkopo wa Pikipiki watakazopewa. Kwa wakati.
Umoja wa waendesha bodaboda Jiji la Arusha (UBOJA) wakiwa katika Kikao na Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Charles Mkubwa akitoa maelezo ya mafunzo ya udereva yatakayotolewa bure kwa vijana hao kuanzia tarehe 08/12/2016 kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete afanya Mazungumzo na Waziri Mkuu wa Ethiopia

0
0
Rais Mstaafu na Kamishna wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa ya Kugharamia Fursa ya Elimu Duniani (UN Education Commission on Financing Global Education Opportunity) amekutana na Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mheshimiwa Haile Mariam Desale alipomtembelea ofisini kwake jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Katika nafasi yake ya Mjumbe Maalum wa Kamisheni hiyo, Rais Mstaafu amemkabidhi Waziri Mkuu wa Ethiopia Ripoti ya Kamisheni hiyo yenye mapendekezo ya namna Dunia inavyoweza kukabili janga la Elimu kwa kuwekeza katika Mpango wa Kizazi cha Elimu (A Learning Generation). Mpango huo unalenga kuleta mapinduzi makubwa ya Elimu katika nchi zinazoendelea ndani ya Kizazi Kimoja (miaka 30). Azma kuu ya Mpongo huo ni kuwezesha ifikapo mwaka 2040, watoto wote kote duniani wawe wanaopata elimu iliyo bora na kwa kiwango kinachofanana dunia nzima.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kwa sasa, hali ya elimu katika nchi zinazoendelea inalingana na ile ambayo nchi zinazoendelea zilikuwapo miaka 70 iliyopita. Aidha, ripoti inasisitiza kuwa, ikiwa nchi zinazoendelea zitaendelea kwa kasi ya sasa, itazichukua nchi hizo kati ya miaka 90 na 110 kufikia viwango vya sasa vya nchi zilizoendelea.
Kwa ajili hiyo, Kamisheni inapendekeza njia mpya na bora za kufanya mageuzi katika elimu ikiwemo kuongeza usimamizi, kupanua fursa, kuingiza ubinifu na teknolojia na kuongeza uwekezaji katika elimu kwa kushawishi ushiriki wa Jumuiya ya Kimataifa na Sekta Binafsi. Iwapo mapendekezo hayo yatatekelezwa, nchi zinazoendelea zinaweza kufikida pengo hilo ndani ya miaka 30 ijayo.
Rais Mstaafu ameiomba Ethiopia kujiunga na Mpango huo ambapo Waziri Mkuu wa Ethiopia ameelezea nia ya nchi yake kujiunga na Mpango huo. Ethiopia ni moja kati ya nchi za Afrika ambayo imepiga hatua kubwa katika utoaji wa fursa ya elimu kwa watoto na vijana wake. Pamoja na mafanikio makubwa bado zipo changamoto zinazohitaji hatua madhubuti ili kufikia lengo la kizazi cha elimu ifikapo 2040.
Ziara ya Rais Mstaafu itamfikisha katika nchi 14 barani Afrika ambapo zimechaguliwa katika awamu ya kwanza ya mpango huo. Tayari amekwishazitembelea nchi za Uganda na Malawi na kufanya mazungumzo na viongozi wakuu wa nchi hizo.
Rais Mstaafu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Mheshimiwa Haile Mariam Desale, Waziri Mkuu wa Ethiopia jijini Addis Ababa.

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akimkabidhi Ripoti ya Kamisheni ya Elimu Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Ethiopia Haile Mariam Desale jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Rais Mstaafu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Mheshimiwa Haile Mariam Desale, Waziri Mkuu wa Ethiopia.

News Alert: Rais Magufuli afanya mabadiliko ya Makatibu wakuu, Naibu Katibu Wakuu na Wakuu wa Mikoa

0
0



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 07 Desemba, 2016 amefanya uteuzi wa Katibu Mkuu mmoja na Mkuu wa Mkoa mmoja na pia amefanya mabadiliko madogo katika Wizara na Mikoa kama ifuatavyo;
Dkt. Magufuli amemteua Prof. Faustin Kamuzora kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais.Kabla ya uteuzi huo, Prof. Kamuzora alikuwa Katibu Mkuu Mawasiliano.
Rais Magufuli amemteua Mhandisi Mathew Mtigumwe kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Uvuvi na Mifugo anayeshughulikia Kilimo. Mhandisi Mathew Mtigumwe anachukua nafasi ya Dkt. Frolence Turuka ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.
Kabla ya uteuzi huo Dkt. Frolence Turuka alikuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi aliyekuwa akishughulikia Kilimo. Anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Mhe. Job Masima ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.

Rais Magufuli amemteua Dkt. Maria Sasabo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na atakuwa akishughulikia Mawasiliano. Dkt. Maria Sasabo anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Prof. Faustin Kamuzora ambaye ameteuliwa Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais.

Pia Rais Magufuli amemteua Mhandisi Angelina Madete kuwa Naibu Katibu Mkuu Katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Mhandisi Angelina Madete anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dkt. Maria Sasabo aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Mawasiliano.
Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. Aloyce K. Nzuki kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii.
Wakati huo huo, Rais Magufuli amemteua Bw. Christopher Ole Sendeka kuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe.Bw. Christopher Ole Sendeka anachukua nafasi ya Dkt. Rehema Nchimbi ambaye amehamishwa kituo cha kazi na kuwa Mkuu wa Mkoa wa Singida.
Dkt. Rehema Nchimbi anajaza nafasi iliyoachwa na Mhandisi Mathew Mtigumwe ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Uvuvi na Mifugo anayeshughulikia Kilimo.Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amemteua Dkt. Osward J. Mashindano kuwa Msajili wa Hazina. 

Dkt. Osward J. Mashindano anachukuwa nafasi ya 
Bw. Lawrence Mafuru ambaye atapangiwa kazi nyingine

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasilino ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

07 Desemba, 2016

ZINGATIENI MAADILI NA UWAJIBIKAJI KATIKA KUTEKELEZA MAJUKUMU YENU: NAPE

0
0

Na Raymond Mushumbusi -WHUSM.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye amewataka watendaji na watumishi wa Wizara yake kuzingatia maadili na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu yao.

Ameyasema hayo wakati akifungua Baraza la wafanyakazi la Wizara yake na kusisitiza kwa watendaji kuwasimamia watumishi walio chini yao kuzingatia maadili na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu yao katika kutoa huduma kwa wananchi.

Ameongeza kuwa kuwepo kwa ushirikiano kati ya uongozi na watumishi utasaidia kufanikisha masuala mbalimbali ya maendeleo ya Wizara, Taasisi zake na watumishi katika kuleta maendeleo ya Wizara katika kutimiza wajibu wao.

“Nawataka watumishi wazingatie maadili katika kutekeleza wajibu wao na naamini kwa juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano  tutarudisha maadili ya Utumishi wa Umma na bado taratibu zinaendelea kusimamiwa ipasavyo”asisitiza Mhe Nnauye.

Mhe. Nnauye amesisitiza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli ana mpango wa dhati wa kurujesha maadili katika Utumishi wa Umma na kuhakikisha heshima yake inarudi.

Alieleza kuwa endapo kuna mtumishi yoyote atakayeshindwa kusimamia suala zima la maadili anapoteza utumishi wake.

“ Wananchi ndiyo tunaowatumikia na ndiyo wanaotufanya tuwepo hapa tulipo wanahitaji huduma bora. Kama hatutazingatia suala la maadili ni hakika hatutaweza kuwatumikia vema” alieleza.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akizungumza na watumishi wa Wizara yake wakati wa ufunguzi wa Baraza la wafanyakazi la Wizara  katika kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam Desemba 08, 2016.
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel akizungumza katika kikao cha Baraza la wafanyakazi wa Wizara hiyo kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam Desemba 08, 2016.
 Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bibi Magreth Mtaka akitoa hoja za wafanyakazi katika kikao cha Baraza la wafanyakazi wa Wizara hiyo lililofanyika katika Ukumbi wa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam Desemba 08, 2016.
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel akipokea hotuba ya wafanyakazi kutoka kwa Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Wizara hiyo Bibi Magreth Mtaka katika kikao cha Baraza la wafanyakazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam Desemba 08, 2016.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

PROFESA MBARAWA ATETA NA MAKAMU WA RAIS WA JICA.

0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akijadiliana jambo na Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Bi Suzuki Noriko (wa kawanza kulia), kuhusu maendeleo ya miradi ya ujenzi wa barabara nchini inayotekelezwa na shirika hilo. Kushoto kwa Waziri ni Katibu Mkuu (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akifurahia jambo na Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Bi Suzuki Noriko (wa kawanza kulia), walipokutana jjijini Dar es salaam leo. Kushoto kwa Makamu wa Rais wa JICA ni Mwakilishi Mkuu wa JICA Tanzania Bw. Toshio Nagase.
Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Bi Suzuki Noriko, akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa walipokutana jijini Dar es salaam.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (wa tatu kulia), na Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Bi Suzuki Noriko (wa tatu kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na wataalamu wao mara baada ya kujadili mikakati ya kuboresha miundombinu nchini.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

KIPINDI CHA BBC- DIRA YA DUNIA

MHE. KAIRUKI NA BALOZI WA JAPANI NCHINI WAFANYA MAZUNGUMZO KUHUSU USHIRIKIANO KATI YA TANZANIA NA JAPANI

0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) (wa pili kulia) akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Masaharu Yoshida (wa pili kushoto) alipomtembelea ofisini kwake leo kuzungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Japani hususan suala la wataalam wa kujitolea wanaokuja kufanya kazi nchini katika sekta mbalimbali.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Balozi wa Japani nchini Tanzania, Mhe. Masaharu Yoshida (hayupo pichani) alipomtembelea ofisini kwake leo kuzungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Japani hususan suala la wataalamu wa kujitolea wanaokuja kufanya kazi nchini katika sekta mbalimbali.
Balozi wa Japani nchini Tanzania, Mhe. Masaharu Yoshida (kushoto) akizungumza na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) (hayupo pichani) alipomtembelea ofisini kwake leo kuzungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Japani hususan suala la wataalamu wa kujitolea wanaokuja kufanya kazi nchini. Kushoto kwake ni Afisa wa Ubalozi wa Japani nchini, Bi. Yoko Kamiyana.

MKUTANO WA BARAZA KUU LA 24 LA SHIRIKA LA POSTA TANZANIA WAFUNGWA RASMI JIJINI DAR ES SALAAM

0
0
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujnzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mawasiliano), Profesa Faustin Kamuzora, akizungumza wakati alipokuwa akiufunga mkutano wa 24 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania, jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Mwenyekiti wa baraza hilo, Kaimu Postamasta Mkuu wa shirika, Fortunatus Kapinga na kushoto ni Kaimu Meneja Biashara wa shirika, Janeth Msofe. Kwa sasa Profesa Kamuzora amehamishiwa kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais. 
Baadhi ya Wajumbe wa Mkutano wa 24 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania, wakimsikiliza mgeni rasmi katika ufungaji wa mkutano huo, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mawasiliano), Profesa Faustin Kamuzora, wakati akizungumza nao, jijini Dar es Salaam jana.
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujnzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mawasiliano), Profesa Faustin Kamuzora, akizungumza na wajumbe wa mkutano wa 24 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania, wakati alipokuwa akiufunga jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Mwenyekiti wa baraza hilo, Kaimu Postamasta Mkuu wa shirika, Fortunatus Kapinga, kushoto ni Meneja rasilimali wetu wa shirika, William Makumba na wapili kushoto ni Kaimu Meneja Biashara wa shirika, Janeth Msofe. 
Baadhi ya Wajumbe wa Mkutano wa 24 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania, walipo kuwa wakimsikiliza mgeni rasmi katika ufungaji wa mkutano huo, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mawasiliano), Profesa Faustin Kamuzora, wakati akizungumza nao, jijini Dar es Salaam jana. 

DKT. MPANGO AKUTANA NA MAKAMU WA RAIS WA JICA

0
0

Benny Mwaipaja, WFM, Dar es salaam.

Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA), Bi. Noriko Suzuki, amesema kuwa nchi yake itaendelea kuisaidia Tanzania katika Nyanja mbalimbali za kiuchumi na kijamii ili iweze kufikia malengo yake ya kuondokana na umasikini.

Suzuki ametoa ahadi hiyo baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, ofisini Kwake Jijini Dar salaam.Makamu huyo wa Rais wa JICA, amesema kuwa nchi yake inatumia zaidi ya dola za Marekani Milioni mia moja kila mwaka kusaidia shughuli mbalimbali za maendeleo hapa nchini katika sekta za miundombinu ya barabara, maji, nishati, afya na kilimo.

Miongoni mwa miradi mikubwa inayofadhiliwa na serikali hiyo ya Japan ni barabara ya juu ya mzunguko inayojengwa katika makutano ya barabara katika eneo la Tazara, Jijini Dar es salaam. “Tuko tayari kushirikiana na Tanzania katika kutekeleza Mpango wake wa Pili wa Taifa wa Maendeleo kwa kuwekeza fedha katika miradi mbalimbali ya maendeleo mliyoipa kipaumbele kuiwezesha nchi kufikia malengo yake ya kuwa nchi ya viwanda ifikapo mwaka 2025” alisisitiza Makamu huyo wa Rais wa JICA.

Ameahidi kuwa Shirika lake pia linaagalia uwezekano wa kuishirikisha sekta binafsi nchini Japan kujenga barabara  katika eneo la  Gerezani ili kupunguza msongamano mkubwa wa magari hasa yanayotoka Bandari ya Dar es salaam na Katikati ya Jiji la Dar es salaam.

Kwa upande wake Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, ameeleza kuwa uhusiano kati ya Japan na Tanzania ni wa muda mrefu na kwamba nchi hiyo imekuwa mdau wake mkubwa wa maendeleo.

Amesema katika mazungumzo kati yake na Makamu huyo wa Rais wa JICA, wamekubaliana kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa barabara eneo la Bendera tatu na Gerezani ili kupunguza msongamano wa magari kutoka katikati ya Jiji la Dar es salaam
“Mradi Mwingine ni ujenzi wa barabara kutoka eneo la Moroco hadi Mwenge, Jijini Dar es salaam, ambayo Japan waliahidi  kuijenga muda mrefu uliopita” Aliongeza Dkt. Mpango
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (wa pili kulia), akisisitiza jambo wakati alipokuwa akizungumzia umuhimu wa Nishati ya umeme katika kuchochea maendeleo ya viwanda nchini, wakati alipokutana na Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) Bi. Noriko Suzuki, Makao Makuu ya Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini dar es salaam.

 Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA), Bi. Noriko Suzuki (kulia), akisikiliza kwa makini maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (hayupo Pichani), alipomtembelea na kufanya mazungumzo naye Ofisini kwake Jijini Dar es salaam. Katikati ni Mwakilishi Mkuu Mkazi wa JICA nchini Tanzania, Bw. Toshio Nagase na kulia ni Afisa wa Shirika hilo anayeshughulikia masuala ya usafiri na usafirishaji Bi. Lilian Masalu.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (kulia), akizungumzia namna Serikali ya Tanzania ilivyojipanga kutekeleza miradi mbalimbali ya kipaumbele ikiwemo ujenzi wa viwanda mbele ya Makamu wa Rais wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) Bi. Noriko Suzuki (hayupo pichani), alipomtembelea na kufanya naye mazungumzo ofisini kwake Jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Sheria Bw. Elias Kalist, na kulia kwake ni Mchumi Mkuu, Yosephe Tamamu, wote kutoka Wizara ya Fedha na Mipango.
 Mchumi Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Yosephe Tamamu (kushoto), akifafanua jambo katika kikao kati ya Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) na Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) Bi. Noriko Suzuki. Aliyekaa kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Sheria wa Wizara hiyo Bw. Elias Kalist.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

WAZIRI WA BIASHARA, VIWANDA NA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI NCHINI RWANDA, FRANCOIS KANIMBA ATEMBELEA BANDARI YA DAR ES SALAAM

0
0
Waziri wa Biashara, Viwanda na Jumuiya ya Afrika Mashariki nchini Rwanda, Francois Kanimba akizungumza na waandishi habari mara baada ya kutembelea bandari ya Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumtembeza Waziri wa Biashara , Viwanda na Jumuiya ya Afrika Mashariki nchini Rwanda, Francois Kanimba katika bandari ya Dar es Salaam leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Biashara, Viwanda na Jumuiya ya Afrika Mashariki nchini Rwanda, Francois Kanimba akipata maelezo ya Bandari ya Dar es Salaam kwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Biashara , Viwanda na Jumuiya ya Afrika Mashariki nchini Rwanda, Francois Kanimba akitembelea bandari ya Dar es Salaam ikiwa sehemu ya mkutano wa siku mbili wa kujadili masuala ya biashara kati ya Tanzania na Rwanda leo jijini Dar es Salaam. Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

TAMASHA LA SIFA ZA YERIKO ARUSHA

0
0
Miaka 25 ijayo, Takribani asilimia 75 ya wakazi wa Afrika Mashariki watakuwa vijana,na hii inamaanisha nguvukazi kubwa itakuwa mikononi mwao.

 Lakini kama watasalia kuwa idadi kubwa basi na kuwa na maarifa ya kuendesha nchi, basi changamoto itakuwa kwa ukuaji wa nchi.Vijana wao huona kama wana mchango katika jamii, hasa kwenye makusanyiko ya kijamii mathalani misiba, ambapo hutakiwa kuchangamkia kwenye shughuli zenye uhitaji wa nguvu. 

Lakini kama fursa ya uwepo wa vijana katika jamii itatumiwa vema, basi nyanja zote za maendeleo zitaendeshwa vema, na watakuwa na uwezo wa kutatuza matatizo yaliyo kwenye jamii – sawasawa na malengo endelevu namba 2 na namba 8 za umoja wa mataifa, zinazolenga kumaliza masuala ya njaa, na pia uhakika wa kazi na ukuaji wa uchumi, ikiwemo pia lengo namba 4 – kuwa na elimu bora.

Uwepo wa Tamasha la Sifa za Yeriko ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa Maono Foundation Limited na washirika wake kuwa sehemu ya kutatua matatizo haya kwa kuanzisha kituo cha ukuzaji wa vipaji kwa vijana, kusudi waweze kuwa sehemu ya suluhu ya changamoto kwenye jamii.

Mkakati wa muda mfupi, ni kuhudumia moja ya kituo cha watoto yatima cha Guardian Angels House of Hope chenye uhitaji wa taaluma za watoto kukuzwa,lakini changamoto ikawa kukosekana kwa ada na mahitaji mengine ya shuleni.Kwa kujumuika kwenye tamasha hili, si tu kwamba watakuwa wanamuaibisha mwovu shetani kwa kuangusha ngome zinazowasumbua kwenye Nyanja mbalimbali maishani, bali pia watakuwa wamechangia katika kutimia kwa malengo ya Maono Foundation.





MFUMUKO WA BEI WAONGEZEKA KUTOKA ASILIMIA 4.5 MWEZI OCTOBA MPAKA ASILIMIA 4.8 MWEZI NOVEMBA

0
0
 kurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii Epharaim Kwesigabo akiongea na wanahabari (hawapo pichani) kuhusu hali ya mfumuko wa bei kwa mwezi Novemba mwaka huu, kulia kwake ni Mtakwimu Bw. Muhidini Mtindo.
Wanahabari wakimsikilizaMkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii Epharaim Kwesigabo (hayupo pichani) wakati akielezea hali ya mfumuko wa bei kwa mwezi Novemba mwaka huu. (Picha na Benjamin Sawe-Maelezo).

MSD WAASWA KUBORESHA UPATIKANAJI DAWA NCHINI

0
0

Na Dotto Mwaibale

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Mpoki Ulisubisya amewaasa watumishi wa Bohari ya Dawa (MSD) kuhakikisha kuwa wanatekeleza majukumu yao ipasavyo ili kupunguza malalamiko ya wananchi juu ya ukosefu wa dawa.

Katibu Mkuu huyo ameyasema hayo Dar es Salaam leo wakati akizindua Baraza la tatu la Wafanyakazi la Bohari ya Dawa (MSD) ambapo pia amesisitiza kuwa Baraza hilo libuni mbinu na mikakati mbadala za kuboresha utendaji bila kusahau kutii miiko ya utumishi wa umma.

Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi MSD, ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu amemweleza Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya kuwa tayari MSD imeanza kununua dawa na vifaa tiba kutoka kwa wazalishaji, ambapo hadi sasa wanawazalishaji 20 ambao wanamikataba, na wazabuni wengine 76 wadawana 79 wa vifaa tiba zabuni zao zinaandaliwa.

Mkutano huo umehudhuriwa na wajumbe kutoka Makao Makuu ya MSD na Kanda zote nane za MSD ambao ni pamoja na Mwenyeviti wa Tughe na matawi pamoja wawakilishi wa wafanyakazi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Mpoki Ulisubisya (kushoto), akihutubia wakati akizindua Baraza la tatu la Wafanyakazi wa Bohari ya Dawa (MSD), Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi MSD, ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu (kulia), akizungumza kwenye mkutano huo.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wakifuatilia kwa makini yaliyokuwa yakielezwa na viongozi wao katika mkutano huo.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wakiwa kwenye
mkutano huo. 

Azam FC kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Mtibwa Sugar

0
0

KATIKA kujiandaa vilivyo kuelekea mechi za raundi ya pili ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, inatarajia kukipima kikosi chake kwa kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Mtibwa Sugar utakaofanyika Uwanja wa Azam Complex, Jumamosi ijayo Desemba 10 saa 1.00 usiku.


Azam FC iliyoanza maandalizi ya mzunguko huo wa pili Jumatatu iliyopita, itautumia mchezo huo kuwapima wachezaji wake kabla ya kuanza mikikimikiki ya ligi, ambapo inatarajia kufungua pazia kwa kucheza na African Lyon Desemba 18 mwaka huu kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Baadhi ya wachezaji wapya itakaowatumia katika mchezo huo ni washambuliaji Yahaya Mohammed (Aduana Stars) na Samuel Afful (Sekondi Hasaacas), ambao wametua nchini alfajiri ya leo Jumatano wakitokea nchini kwao Ghana sambamba na beki wa kati, Yakubu Mohammed (Aduana Stars) aliyekuja kufanya majaribio ya kujiunga na Azam FC.

Mabingwa hao wanawafanyia majaribio wachezaji wengine wawili kutoka Cameroon, beki wa kati Batetakang Flavius (Canon Yaoundé) na kiungo mkabaji Stephane Kingue (Coton Sport FC de Garoua), ambao nao wanatarajia kuwemo kwenye mtanange huo.

Hadi inamaliza raundi ya kwanza ya ligi, Azam FC inayodhaminiwa na kinywaji safi cha Azam Cola kinachochangamsha mwili na kuburudisha koo pamoja na Benki bora kabisa nchini kwa sasa ya NMB, imejikusanyia jumla ya pointi 25 katika nafasi ya tatu kwenye msimamo ikiwa nyuma pointi 10 dhidi ya Simba (35).

Mbali na kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi, Azam FC pia inayatumia mazoezi hayo kujiandaa ipasavyo na michuano mingine ya Kombe la Mapinduzi, Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) na Kombe la Shiikisho Afrika (CC), ili iweze kufanya vizuri.
Nahodha wa Azam FC, John Bocco, akimiliki mpira mbele ya kiungo mkabaji, Stephane Kingue na beki Bruce Kangwa, wakati wa mazoezi ya timu hiyo leo Jumatano asubuhi.
Winga wa kushoto, Enock Atta Agyei, akitafuta mchezaji wa kumpa pande.

Kocha wa Makipa wa Azam FC, Jose Garcia, akimpa mazoezi kipa Aishi Manula.


SKAUTI WA TANZANIA WAZURU KENYA

0
0
 Kaimu Balozi, Bi. Talha Mohamed  Waziri (Kushoto) akisalimiana na Maskauti kutoka Tanzania.

Skauti 27 kutoka shule mbili za msingi za Dar es Salaam wako nchini Kenya kwa ziara ya wiki moja kwa mwaliko wa Chama cha Maskauti cha Kenya.
Watoto hao kutoka shule za msingi za Canossa na Libermann, na maofisa wa Chama cha Maskauti Tanzania waliowasindikiza, Kamishina Anthony Joachim na Kamishina Saidi Debwani, leo wametembelea Ubalozi wa Tanzania Nairobi na kusalimiana na Kaimu Balozi, Bi.Talha Mohamed Waziri.

Maskauti hao walimwambia Kaimu Balozi kuwa wametembelea maeneo mbalimbali ya Kenya na kujifunza mambo mengi.Kamishina Joachim amesema watoto hao wanatarajiwa kurejea nyumbani kesho.
Maskauti kutoka Tanzania na viongozi wao katika picha ya pamoja na Kaimu Balozi, Bi. Talha Mohamed  Waziri.

BALOZI WA CUBA AMUAGA WAZIRI MWAKYEMBE

0
0
 Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akimpatia kadi ya mawasiliano Mgeni wake Balozi wa Cuba Mhe. Jorge Luis Lopez alipofika ofisini kwake leo (8/12/2016) kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi hapa nchini.
 Balozi wa Cuba Mhe. Jorge Luis Lopez akiandika ujumbe wa kumuaga Waziri  wa Mambo ya Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe kwenye kitabu cha wageni ofisini kwa Waziri huyo alipofika kwa ajili ya kumuaga.
Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akibadilishana mawazo na Mgeni wake Balozi wa Cuba Mhe. Jorge Luis Lopez  alipofika ofisini kwake leo (8/12/2016) kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi hapa nchini.
Viewing all 109606 articles
Browse latest View live




Latest Images