Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live

MADAKTARI MABINGWA WA UPASUAJI TOKA NCHINI INDIA WAANZA HUDUMA BURE YA KUTIBU NA UPASUAJI WAGONJWA WA MOYO KATIKA HOSPITALI YA BUGANDO JIJINI MWANZA

$
0
0
Mkuu wa Kitengo cha upasuaji wa Kifua na Moyo BMC, Prof. William Mahalu akizungumza (kulia) kwenye mkutano na waandishi wa habari wakati wa kuwakaribisha madaktari bingwa wa upasuaji wa Moyo kutoka Madras Medical Mission, Chennai, India katika hafla iliyofanyika kwenye Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mwanza, pembeni yake ni Rais wa Jumuiya ya Shia Imami Islaili Muslims, Kanda ya Magharibi Bw. Altaf Hirani.
 Gharama za upasuaji wa Moyo ni kubwa si chini ya shilingi Millioni 6 za Tanzania. Kwa wagonjwa hawa tunashukuru Wizara ya Afya,Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando Medical Centre (BMC) lakini shukurani nyingi ziende MMI ambao wamenunua vifaa vingi ba ambavyo watatuachia hapa, ili tuendelee naupasuaji huu.
Sehemu ya madaktari wageni toka nchini India wakiwa kwenye mkutano na waandishi wa habari wakati wa kuwakaribisha madaktari hao mabingwa wa upasuaji wa Moyo kutoka Madras Medical Mission, Chennai, India katika hafla iliyofanyika kwenye Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mwanza. Wa pili kutoka kushoto ni Bingwa wa Moyo kwa watoto daktari mzalendo aliyerejea nchini Dr. Glory Joseph ambaye ndiye aliyekuwa akisimamia zoezi hilo. 

Kwa mujibu wa Rais wa Jumuiya ya Shia Imami Islaili Muslims, Kanda ya Magharibi Bw. Altaf Hirani (katikati) amesema kuwa kila mwaka Hospitali ya Aga Khan inatumia shilingi za Kitanzania bilioni 2 kuwahudumia wagonjwa bila malipo yoyote ambapo hadi sasa zaidi ya wagonjwa 600 wamefanyiwa upasuaji wa moyo.
Watanzania madaktari 10 walipelekwa nchi za nje kupata mafunzo zaidi. Aidha Wakfu wa Afya wa Aga Khan umewekeza shilingi za kitanzania bilioni 167 katika ujenzi wa Hospitali ya kisasa ya kutoa mafunzo ya udaktari ambayo tayari imeanza kujengwa. 
Pia kujengwa vituo 35 vya afya vitajengwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini, vitano vikiwa katika mkoa wa Mwanza. Kupata zaidi BOFYA HAPA

TANGAZO LA MDAHALO WA WANA DIASPORA WA UK KUHUSU ARDHI TANZANIA

$
0
0
Wana Diaspora wa UK mnaalikwa kuhudhuria kongamano litakalojadili mstakabali mzima wa haki ya Mwana Diaspora kikatiba ikiwemo haki ya kumiliki ardhi Tanzania iwapo wewe ni mzawa. Mdahalo unatarajia kutoa elimu na mapendekezo juu ya swala hili.
Patakuwepo na wataalam mbali mbali wa maswala haya. 
Karibu University of Coventry, School of Engineering Tarehe 3 December, 2016 Saa 4 asubuhi Uwepo wenu ni mhimu.
Umoja ni nguvu Kwa tarifa zaidi walisilian na simu +44 7960811614 
Ahsanteni 
WOTE MNAKARIBISHWA

MSHINDI WA MILIONI MIA MOJA ZA VODACOM M-PAWA AKABIDHIWA KITITA CHAKE

$
0
0
Hapa kazi tu ni kaulimbiu inayohamasisha watu kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia fursa mbalimbali zilizopo, usemi huu umetimia kwa Mama Paulina Kulwa mkazi wa Mwanza baada ya kukabidhiwa kitita cha shilingi milioni mia moja kutoka kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya CBA. 
Paulina alikabidhiwa hundi hiyo katika ofisi za Vodacom jijini mwanza na Meneja Masoko na huduma za Kifedha Vodacom Tanzania, Noel Mazoya na kusema lengo la kuanzisha huduma hii ni kuwasaidia Watanzania kuwa na utamaduni wa kuweka akiba. 

 Bi Paulina Kulwa (Kulia) akikabidhiwa hundi ya mfano wa Tsh Milioni 100 baada ya kuibuka mshindi katika promosheni ya Jiongeze na M-Pawa

 Bi Paulina Kulwa (Kulia) akiwa na pacha wake katika duka la Vodacom City Mall jijini Mwanza katika hafla ya kumpongeza na kumkabidhi hundi baada ya kuibuka mshindi katika promosheni ya Jiongeze na M-Pawa

Mshindi wa Jiongeze na Mpawa akiwa na maafisa toka Vodacom na CBA katika hafla fupi ya kumkabidhi mfano wa hundi na kumpongeza. Toka kushoto ni Ayubu Kalufya Mkuu wa Vodacom Kanda ya Ziwa, Meneja Masoko wa huduma za Kifedha wa Vodacom Noel Mazoya, mshindi wa milioni 100 Bi Paulina Kulwa, Solomoni Kawiche Mkuu wa masoko - CBA na Eric Luyangi Mkuu wa MPawa - CBA. Video ya hafla hii BOFYA CHINI

RAIS DKT. MAGUFULI AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUAGA MWILI WA MZEE JOSEPH MUNGAI JIJINI DAR LEO

$
0
0

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa heshima zake za mwisho kwa  mwili wa aliyekuwa Waziri wa Zamani na Mbunge Mzee Joseph Mungai katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam leo Novemba 10, 2016.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimfariji mjane wa  marehemu baada ya kutoa heshima zake za mwisho kwa  mwili wa aliyekuwa Waziri wa Zamani na Mbunge Mzee Joseph Mungai katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam leo Novemba 10, 2016
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mh. Benjamin Mkapa akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Mzee Joseph Mungai, aliewahi kuwa Waziri katika Wizara mbalimbali za Serikali ya Jamhuri ya Muungano kuanzia Awamu ya kwanza mpaka ya nne, ulioagwa leo katika ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es salaam.
Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohamed Gharib Bilal akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Mzee Joseph Mungai, aliewahi kuwa Waziri katika Wizara mbalimbali za Serikali ya Jamhuri ya Muungano kuanzia Awamu ya kwanza mpaka ya nne, ulioagwa leo katika ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es salaam.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli (wa nne kushoto), Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mh. Benjamin Mkapa (wa tatu kushoto), Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohamed Gharib Bilal (wa tatu kulia), Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye (kushoto), Mke wa Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mama Salma Kikwete (kulia) pamoja na viongozi wengine wakifatilia wasifu wa Marehemu Mzee Mungai, uliokuwa ukisomwa na Mtoto wake Mkubwa, Jimmy Mungai.
 Sehemu ya familia ya aliyekuwa Waziri wa Zamani na Mbunge Mzee Joseph Mungai katika hafla ya kuuaga mwili wa marehemy katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam  leo Novemba 10, 2016

ANKAL AKIHOJIWA NA VIJIMAMBO JUU YA GLOBU YA JAMII

OBAMA USO KWA USO NA TRUMP KWA MARA YA KWANZA IKULU YA WHITE HOUSE LEO

BBC DIRA YA DUNIA ALHAMISI 10.11.2016

RAIS DKT MAGUFULI ATEMBELEA WAGONJWA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0

 Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiweka sawa mkono wenye drip wa mkewe Mama Janeth Magufuli, ambaye amelazwa kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam akipatiwa matibabu leo Novemba 10, 2016.
Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongea na mkewe Mama Janeth Magufuli ambaye amelazwa kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam akipatiwa matibabu leo Novemba 10, 2016. Kulia ni Dkt Edward Ngwale akiwa na wauguzi katika wodi hiyo. 
 : Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimjulia hali Waziri wa Zamani Balozi Omar Ramadhani Mapuri ambaye amelazwa kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam akipatiwa matibabu leo Novemba 10, 2016.
  Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwashukuru na kuwapongeza kwa kazi nzuri baadhi ya madaktari na wauguzi kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam alipotembelea wagonjwa pamoja na mkewe ambaye anapatiwa matibabu leo Novemba 10, 2016.
Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwafariji baadhi ya wagonjwa kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam alipotembelea kuona wagonjwa pamoja na mkewe ambaye anapatiwa matibabu hapo leo Novemba 10, 2016. 
Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipungia wananchi alipokuwa akitoka  Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam alipotembelea wagonjwa pamoja na mkewe ambaye anapatiwa matibabu leo Novemba 10, 2016.
Picha na IKULU

MWILI WA MZEE SAMUEL SITTA WAWASILI KARIMJEE TAYARI KWA KUTOLEWA HESHIMA ZA MWISHO

MAGAZETI YA LEO IJUMAA NOVEMBA 11

KUNDI LA MUZIKI LA "WAPANCRAS" KUTOKA KANDA YA ZIWA LAELEZA MAFANIKIO YA WIMBO WA "NITUNZIE SIRI".

$
0
0


Wapancras ni kundi la Muziki kutoka Kanda ya Ziwa linaloundwa na wasanii Mecrass na Payus. Ni kundi linalofanya vizuri na nyimbo kadhaa ikiwemo Chausiku pamoja na Nitunzie Siri ambayo wamefanya na msanii Abuu Mkali.

Wamezungumza na BMG Habari na kuelezea furaha yao kwa hatua kubwa waliyofikia kwenye muziki na kuwapongeza mashabiki zao.
TAZAMA VIDEO HAPO CHINI

MAENDELEO YA UJENZI WA NYUMBA ZA WALIMU WILAYANI RUFIJI

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Watumishi Housing Compay Dr Fred Msemwa akiwa na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mjawa wilaya ni Rufiji Ndugu Joel İrigo pamoja na Fundi Harun wakizungumza juu ya maendeleo ya ujenzi wa nyumba za walimu shuleni hapo.

SPIKA MSTAAFU SITTA KUAGWA BUNGENI LEO.

$
0
0

Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO, Dodoma.

Mwili wa aliyekuwa Spika wa Bunge la 9 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samuel Sitta unatarajiwa kuagwa leo mchana na wabunge wa Bunge hilo katika viwanja vya Bunge vya mjini Dodoma.

Kauli hiyo imetolewa mjini hapo na Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai alipokuwa akitoa ratiba ya kuuaga mwili wa spika mstaafu itakayoanza mara baada ya kumalizika kwa shughuli za Bunge za kipindi cha asubuhi.

Mhe. Ndugai amesema kuwa Bunge linatarajia kuupokea mwili wa mpendwa huyo leo mnamo majira ya saa 8 mchana kutoka katika uwanja wa ndege wa Dodoma na kupelekwa moja kwa moja ndani ya Bunge hilo kwa ajili ya kupewa heshima za mwisho na wabunge.

“Baada ya mwili wa mpendwa wetu kuwasili katika viwanja hivi, tutakuwa na kikao maalum cha Bunge kitakachofanyika mida ya saa 8:30 mchana ambapo wabunge watapata nafasi ya kutoa salamu za rambirambi na baadaye utaratibu wa kutoa heshima za mwisho utafuata”, alisema Mhe. Ndugai.

Spika Ndugai ameongeza kuwa baada ya utoaji wa heshima za mwisho utakaoongozwa na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa pamoja na Kiongozi wa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni Mhe. Freeman Mbowe, kwa mwili wa marehemu Samuel Sitta utasafirishwa kwa ndege mnamo majira ya saa 10 jioni kwenda wilaya ya Urambo, mkoani Tabora kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika Novemba 12 mwaka huu.

Aidha, Mhe. Ndugai amefafanua kuwa katika msiba huo Bunge litawakilishwa na wabunge 10 watakaochaguliwa na Tume ya Huduma za Bunge kwa kuzingatia uwakilishi wa vyama ukiongozwa na yeye Spika Mhe. Ndugai kwenda mkoani Tabora kwa ajili ya mazishi.

Kutokana na msiba huo, Mhe. Ndugai amesema kuwa Bunge litajenga misingi ya kuwaheshimu viongozi wa kitaifa wanaopatwa na jambo la namna hiyo kwa kupewa heshima hizo za kuletwa Bungeni kwa ajili ya kuagwa kwa msingi wa Bunge kuwa ndio nyumba ya uwakilishi wa Watanzania wote.

TANZIA

HOSPITALI YA KAIRUKI KATIKA KUBORESHA HUDUMA ZAKE KUPUNGUZA MSONGAMANO WA WAGONJWA

$
0
0

Hospitali ya kairuki katika kuboresha huduma zake kwa wagonjwa imeanza kutumia kitengo kipya kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wa kutwa hususani wale wanachama wa mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).
Kitengo hicho kipya (OPD 3) kilichopo nyuma ya Jengo kuu la hospital mkabala na kitengo cha magonjwa ya viungo ( Physiotherapy Unit).
 

 kina sehemu kubwa ya mapokezi, vyumba mbalimbali vikiwemo vyumba 10 via madaktari, maabara,Duma la dawa,sehemu ya sindano na kufunga vidonda,chumba cha ultrasound,mapokezi , huduma za chanjo ya watoto (RCH),chumba cha wauguzi na duka dogo la vinywaji na vitafunwa nk .
Kitengo hicho kipya kitaiwezesha hospital hiyo kutoa huduma kwa haraka na ufanisi kwa wagonjwa wasiopungua 120000 kwa mwaka hivyo kupunguza Kero ya foleni na msongamano iliokuwepo siku za nyuma.
Aidha kitengo hicho (OPD3) kitazinduliwa rasmi hivi karibuni pamoja na vitengo vipya vya kusafishia figo ( Dialysis Unit) na kile cha huduma za dharula ( Emergency Unit)
Pichani ni Majengo mapya ya kisasa yatakayokuwa yakitumika kutoa huduma.
Pichani wagonjwa wakisubiri kupata huduma Muda mfupi Mara baada ya majengo hayo kufunguliwa.
Pichani wagonjwa wakisubiri kupata huduma Muda mfupi Mara baada ya majengo hayo kufunguliwa. Na Afisa Mahusiano;Arafa Mohamed

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi yakamilisha rasmi taratibu za ajira za uhamiaji kwa ngazi ya askari na maafisa

VYUO VIKUU WAASWA KUEPUKA MIGOMO NA MAANDAMANO YASIYO NA TIJA KWA TAIFA.

$
0
0
Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya juu kote nchini wametakiwa kutumia muda mwingi kujisomea na kuepuka kujiingiza kwenye vitendo vya vurugu , migomo na maandamano yasiyo na tija kwa taifa ambayo yamekuwa yakiwapunguzia ufanisi katika masomo yao.

Wito huo umetolewa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Suzan Kaganda wakati akizungumza na Jumuiya ya wanataaluma wa Chuo cha Elimu ya Biashara Dar es salaam (CBE) kwenye kongamano la 3 lililowakutanisha wahitimu wa chuo hicho mwaka huu, wanataaluma waliopo na wale waliowahi kusoma katika chuo hicho (CBE Alumni Association) na wadau mbalimbali jijini Dar es salaam.

Akiwa mgeni rasmi katika kongamano hilo na mmoja wa wahitimu wa siku nyingi wa chuo hicho Kamanda Suzan Kaganda amesema wanafunzi wa vyuo vya Elimu ya juu wanapaswa kutambua kuwa elimu wanayoipata katika vyuo hivyo sio kwa ajili ya manufaa yao binafsi bali ni kwa manufaa ya taifa zima hivyo wanatakiwa kuwa makini na kuwa mfano wa kuigwa katika jamii.

“Naomba nisisitize kuwa elimu mliyoipata na mnayoendelea kuipata chuoni hapa sio kwa ajili ya manufaa yenu binafsi bali ni kwa ajili ya manufaa ya taifa, wakati mwingine mnapoteza muda mwingi pindi mnapojiingiza kwenye migomo na maandamano barabarani kushindana na Serikali, muda ambao mgeutumia kujisomea ninyi wenyewe” Amesisitiza Kamanda Suzan.

Wanafunzi wa CBE, Adam Luhalala (kushoto) na Petro Nchimbi wakifanya ukaguzi wa Mashine ya kutengeneza vipuri mbalimbali vinavyotumika kwenye mashine za viwandani na Magari ndani ya Karakana ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) jijini Dar es salaam.
ahitimu wa chuo CBE mwaka huu, wanataaluma waliopo na wale waliowahi kusoma katika chuo hicho (CBE Alumni Association) na wadau mbalimbali waliohudhuria kongamano la 3 la chuo hicho jijini Dar es salaam.
Mwanafunzi wa Mwaka wa 2 katika fani ya Vipimo Mathew Kaizilege akitoa ufafanuzi kuhusu mashine ya kuchonga vipuri kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari Jangwani walioitembelea Karakana ya Vipimo ya CBE jijini Dar es salaam.

MAFUNZO YA UFUNGASHAJI BORA,KUWEKA NEMBO,RAJAMU NA MASOKO YAFANYIKA MASASI NA RUANGWA

$
0
0
 Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa,Mhe Joseph Mkirikiti amehimiza uzalishaji wa mafuta ya Alizeti, Ufuta na Nazi kwa wingi katika wilaya ya Ruangwa sababu ni kioo na msingi imara ya kuwawezesha ajira iwe ya kudumu na tena ajira bora kwa wananchi. 

Hayo aliyasema akiwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mafunzo kwa vitendo kwa wakulima ambao ni wazalishaji wa bidhaa za mbegu za mafuta ya ufuta, nazi na alizeti wa Ruangwa na akipokea lebo za vifungashio vya mafuta ya alizeti kwa wazalishaji wa bidhaa za mafuta ya alizeti zaidi ya 1000 zilizotengezwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade). 

Mafunzo hayo yameanza tarehe 7 hadi 10 Novemba, 2016 juu ya namna ya ufungashaji bora wa bidhaa za mbegu za mafuta ya ufuta, alizeti na nazi, kuwa na lebo bora kwenye kila bidhaa inayozalishwa, rajamu (branding) kwenye bidhaa hizo, namna ya kuboresha ubora wa bidhaa na mbinu ya kuuza bidhaa hizo kwenye masoko ya ndani na nje ya nchi kwa wazalishaji wapatao 50 wa Ruangwa na 50 wa Masasi.

“Elimu mtakayopata hapa itawachukueni kwenye hatua nyingine ya kufanya maboresho makubwa ya ajira yenu, hapa nchini mahitaji ya mafuta ya kula kwa mwaka ni lita 350,000 wakati uzalishaji kwa sasa ni asilimia 40 pekee na asilimia 60 huagizwa kutoka nje ya nchi hivyo basi, tuna fursa kubwa ya kunufaika na sekta hii.” 
Mhe Joseph Mkirikiti akikabidhi lebo za vifungashio kwa Bi Safina Selemani mzalishaji wa mafuta ya alizeti kutoka kata ya Nandagala B kikundi cha CHIUKUTE, lebo hizo zimetengenezwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara ya Tanzania (TanTrade)
Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Mhe Joseph Mkirikiti akipokea lebo za vifungashio kwa wazalishaji wa mafuta ya alizeti katika mkoa wa Ruangwa kata ya Nandagala B kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara ya Tanzania (TanTrade) Bw Edwin Rutageruka.

JARIDA LA WIZARA YA NISHATI NA MADINI TOLEO NAMBA 145

INTRODUCING PAPI CHULO SEAFOOD BAR IN DAR ES SALAAM

Viewing all 110181 articles
Browse latest View live




Latest Images