Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live

Dkt. Kitima; Bodi ya Ithibati ya Wanahabari haitazuia uhuru wa habari.

$
0
0
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Stella Marios cha Mtwara Padre, Dkt. Charles Kitima akichangia mada katika moja ya Kongamano la Maadhimisho ya Kumbukizi za Mwalimu Julius Nyerere.( PICHA KUTOKA MAKTABA)

……………………………………………………


Na: Frank Shija, MAELEZO

Uanzishwaji wa Bodi ya Ithibati ya Wanahabari kama ilivyoainishwa katika Muswada wa Huduma za Habari wa mwaka 2016 hautaminya uhuru wa kutafuta na kusambaza habari.

Hayo yamebainishwa na Mhadhiri wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Stella Marios kilichopo Mtwara Dkt. Charles Kitima katika mahojiano maalum na mwandishi wa habari hii leo.

Dkt. Kitima amesema kuwa msingi wa haki ya kutafuta taarifa na kusambaza habari unatokana ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivyo watu wasiwe na hofu ya kuwa Bodi hiyo itawaminya watu kutoa mawazo yao.“Bodi ya Ithibati ya Wanahabari haiwezi kuwa kizuizi cha watu kutafuta na kusambaza habari kwani haki hiyo ipo kikatiba kupitia ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania” Alisema Dkt. Kitima

Amesema kuwa haoni sababu yoyote ya kupinga uanzishwaji wake kwa kuwa malengo yake ni kuhakikisha inasimamia kanuni za maadili ya wanahabari hapa nchini na kuijengea heshima tasnia.Aidha aliongeza kuwa pamoja na kuanzishwa kwa Bodi hiyo hakuna maana kwamba uanzishwaji wake utachukua majukumu ya taasisi zingine za habari zilizopo na kuongeza kuwa waandishi wa habari duniani kote wanafanya kazi kwa kufuata miiko ya maadili ya uandishi wa habari.

Alisema kuwa suala kubwa kwa mwanahabari ni kuzingatia maadili na weledi wa taaluma yake ili kutekeleza majukumu yake pasipo kusababisha usumbufu kwa mtu au kikundi kingine.Bodi ya Ithibati ya Wanahabari ipo katika muswada wa huduma za Habari sehemu ya Tatu na kuelezewa kwa kirefu katika kifungu cha 10 hadi 20 katika muswada huo unaopatikana katika Tovuti ya Bunge ambayo ni www.bunge.go.tz.

Balozi wa Tanzania nchini Malawi awataka Polisi Ileje kudhibiti Magendo mipakani

$
0
0
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii Ileje

BALOZI wa Tanzania nchini Malawi, Victoria Mwakasege, amewataka Polisi kuimarisha ulinzi katika mipaka kati ya Tanzania na Malawi katika Wilaya ya Ileje.

Balozi Mwakasege amesema hayo wakati wa ziara yake ya ujirani mwema kati ya Wilaya ya Ileje ya Tanzania na Chitipa ya Malawi katika mpaka wa Isongole.

“lazima tukomeshe na kufunga njia zote za panya hasa zile ambazo zinapitisha bidhaa haramu kwa aupande wetu wa tanzania” amesema Mwakasege.

Ameongeza kuwa kuna bidhaa zingine nchini Malawi ni halali lakini kwetu ni haramu, jambo ambalo linaleta shida kwa vijana wetu hasa pombe nyingi zinazotoka nchi hiyo, kwetu zimepigwa marufuku.

Amesema kuwa pombe za viroba na Sukari vimekuwa zikitumia kuvushwa kwa njia za panya hali inayo hatarisha afya ya mlaji na kuikosesha serikali mapato.
  Balozi wa Tanzania nchini Malawi,Victoria Mwakasege, akizungumza na baadhi ya  viongozi wa Wilaya ya  ileje wakati wa ziara yake ya kukagua mpaka kati ya Tanzania na Malawi.
Balozi wa Tanzania nchini Malawi,Victoria Mwakasege akisaini kitabu cha wageni kilichoshikwa na katibu Tawala wa Wilaya ya Ileje, Mary Joseph.   
 Mkuu wa Wilaya ya Chitipa,Grace Chirwa akizungumza na baadhi ya watendaji wa Tanzania na Malawi wakati wa ziara ya kukagua mipaka.
 Balozi wa Tanzania nchini Malawi,Victoria Mwakasege, akiwa na watendaji wa wa nchi zote mbili katika mpaka wa Tanzania na Malawi.
Picha ya pamoja ya watendaji wa Tanzania na Malawi.

WAIGIZAJI WA KIKE WAPIGWA MSASA KUONGEZA USHIRIKI WAO KWENYE TASNIA YA FILAMU NCHINI

$
0
0
Afisa Mipango wa Bodi ya Filamu Tanzania Mfaume Said akiwasilisha mada inayohusu historia, majukumu na mipango ya baadae ya bodi hiyo mbele ya wasanii wa kike waliohudhuria mafunzo ya kuongeza ushiriki wao kwenye tasnia ya filamu. Mafunzo hayo ya siku mbili ni mwendelezo wa juhudi za Bodi ya Filamu kuongeza ubora wa filamu za Kitanzania.
Mkufunzi Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam Dkt. Mona Mwakalinga akisisitiza jambo wakati akiwasilisha mada inayohusu njia mbalimbali zinazotumika kuongeza uwezo wa mwigizaji kuuvaa uhusika kwenye michezo ya kuigiza na filamu.
Baadhi ya waigizaji wanaoshiriki mafunzo ya siku mbili ya kuwaongezea ushiriki waigizaji wa kike wakifuatilia mada inayowasilishwa na Mkufunzi Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam Dkt. Mona Mwakalinga. Mafunzo hayo ya siku mbili yanafanyika ukumbi wa Habari Maelezo, jijini Dar-es-salaam
Mwigizaji wa michezo ya kuigiza na filamu Bi. Madina Mjatta (Zawadi) akichangia mada wakati wa mafunzo ya siku mbili yanayolenga kuongeza ushiriki wa waigizaji wa kike kwenye tasnia ya filamu nchin

Sauti Za Busara announces 2017 artist line-up

$
0
0
East Africa’s leading music festival Sauti Za Busara has announced the line-up for the 2017 edition, which will be held between 9 and 12 February 2017 in Zanzibar. The line-up presents a diverse selection from around the continent and the diaspora and includes 25 acts from within East Africa.
Members of Wahapahapa band from Tanzania. Photo: www.busaramusic.org
Members of Wahapahapa band from Tanzania. Photo: www.busaramusic.org
For more CLICK HERE
For many of the artists, this will be their debut performance at the festival and in East Africa. The line-up includes:
  • Moroccan roots-reggae superstars Bob Maghreb, who reinterpret Bob Marley classics with fresh North African flavours
  • Roland Tchakounté, a rocking African blues musician from Cameroon (now based in France)
  • Kyekyeku, a young, conscious Ghanaian singer-songwriter taking traditional palm wine and highlife music to new directions.

RAIS DK. ALI MOHAMED SHEIN AKUTANA NA UONGOZI WA OFISI YA RAIS,TAWLA ZA MIKOA,SERIKALI ZA MITAA NA IDARA MAALUM ZA SMZ

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Uongozi wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa,Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ katika kikao cha Mpango kazi wa mwaka 2016-2017 katika utekelezaji wa robo mwaka ya kwanza ya Julai-Septemba 2016 kilichofanyika leo Ikulu Mjini Unguja,
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akitoa maelekezo wakati alipokuwa akizungumza na Uongozi wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa,Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ katika kikao cha Mpango kazi wa mwaka 2016-2017 katika utekelezaji wa robo mwaka ya kwanza ya Julai-Septemba 2016 kilichofanyika leo Ikulu Mjini Unguja
Baadhi ya maafisa wa Vikosi vya SMZ wakiwa katika kikao cha Mpango kazi wa mwaka 2016-2017 katika utekelezaji wa robo mwaka ya kwanza ya Julai-Septemba 2016 cha Uongozi wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa,Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ,kilichofanyika leo Ikulu Mjini Unguja chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(hayupo pichani).

TANZANIA YAWAKARIBISHA WAKOREA KUSINI KUWEKEZA SEKTA YA VIWANDA

$
0
0

Benny Mwaipaja,WFM, Seoul, Korea 

WAFANYABIASHARA wakubwa kutoka KOREA ya Kusini, wamekaribishwa kuja kuwekeza nchini Tanzania katika sekta ya viwanda vitakavyoongeza thamani ya bidhaa za kilimo, mifugo, mazao ya bahari pamoja na kutumia malighafi zinazopatikana nchini ili kusisimua uchumi wa taifa na kukuza ajira. 
Wito huo umetolewa Jijini Seoul nchini Korea, na Mkurugenzi wa Uhamasishaji uwekezaji kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania-TIC, JOHN MNALI, wakati akiwasilisha mada kuhusu fursa za uwekezaji zinazopatikana Tanzania, wakati wa mkutano wa 5 wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea ya Kusini na nchi za Afrika(KOAFEC). 
Mnali amesema kuwa Tanzania imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji ikiwemo kuondoa urasimu wa upatikanaji wa vibali vya kuwekeza na ardhi kwa ajili ya uwekezaji huo ili kuvutia mitaji na teknolojia kutoka nje ya mipaka yake. 
Amewashauri wawekezaji hao kufufua viwanda ambavyo havifanyi vizuri nchini, ili kuanza uzalishaji wa bidhaa zitakazotumia malighafi zinazopatikana nchini pamoja na kutumia soko kubwa lililopo katika ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na soko la AGOA la Marekani. 
Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Utafutaji Rasilimali, kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar, Sabra Issa Machano, amewahimiza wawekezaji wa Korea kwenda kuwekeza Visiwani humo na Tanzania kwa ujumla katika sekta za kilimo, viwanda na uvuvi wa samaki na mwani katika Bahari Kuu ili wakazi wa nchi hiyo na wawekezaji waweze kunufaika na rasilimali zilizoko visiwani humo. 
Amewahimiza wawekezaji hao kujenga hoteli za kisasa kwa ajili ya kuhudumia soko la utalii ambalo ni kubwa nchini humo, pamoja na kutumia mandhari ya Mji Mkongwe wa Zanzibar ambao ni kivutio kikubwa cha watalii baada ya kutangangazwa na Shirika la Kimataifa linaloshughulika na masuala ya sayansi na utamaduni-UNESCO kuwa mji wa urithi wa Dunia. 

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akifuatilia kwa makini wakati Mkurugenzi wa Uhamasishaji Uwekezaji kutoka kituo cha uwekezaji Tanzania-TIC, John Mnali, akiwasilisha mada kuhusu fursa za uwekezaji zinazopatikana Tanzania, wakati wa mkutano wa 5 wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea ya Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC), Mjini Seoul, Korea Kusini. Kulia kwake ni Mkuu wa Kitengo cha Utafutaji Rasilimali kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Zanzibar-Sabra Issa Machano.
Mkurugenzi wa Uhamasishaji uwekezaji kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania-TIC, John Mnali, akiwasilisha mada kuhusu fursa za uwekezaji zinazopatikana Tanzania, wakati wa mkutano wa 5 wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea ya Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC), Jijini Seoul, Korea Kusini.
Mkuu wa kitengo cha utafutaji Rasilimali, kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Zanzibar, Sabra Issa Machano, akiwasilisha mada kuhusu fursa za uwekezaji zinazopatikana Tanzania Zanzibar, wakati wa mkutano wa 5 wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea ya Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC), Jijini Seoul, Korea Kusini.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb), akisalimiana na mwanafunzi wa Kitanzania anayesomea Chuo Kikuu kimoja nchini Korea Kusini kuhusu masuala ya biashara ya kimataifa na uchumi, Alice Mwamzanya, baada ya kushiriki mkutano wa 5 wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea Kusini na Nchi za Afrika (KOAFEC), Jijini Seoul nchini Korea Kusini.(Picha na Benny Mwaipaja-Wizara ya Fedha na Mipango)

UZINDUZI WA BODI YA HOSPITALI YA TAIFA YA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA WILAYANI SIHA MKOANI KILIMANJARO

$
0
0
 Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Hamisi Kigwangwalla akiongea na wajumbe pamoja na watumishi wa hospitali ya Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro  wakati wa  uzinduzi wa bodi ya hospitali hiyo inayotoa huduma ya kifua kikuu sugu
 Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Hamisi Kigwangwalla akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa  bodi ya hospital ya Wilaya ya Siha inayotoa huduma ya kifua kikiu sugu

Baadhi ya wajumbe wa bodi hiyo mpya(wanne mbele) wakimsikiliza mgeni rasmi,wa kwanza  kushoto ni Dkt.Sayoki Mfinganga,Dkt.Said Egwaga(Mwenyekiti wa bodi),Dkt.Janeth Mghamba na Justice Mkita ambaye bi mwakilishi toka jamii inayotumia huduma za hospitali hiyo. 

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI

$
0
0

SIMU.TV: Waziri mkuu amesema amefurahishwa na jumuiya ya kikristo Tanzania CCT na kanisa katoliki kwa kuamua kujenga makao makuu yake mkoani Dodoma. https://youtu.be/_4IJVGWqyBM

SIMU.TV: Hospitali ya rufaa ya Kitete mkoani Tabora inakabiliwa na uhaba wa vitanda na majengo ya wagonjwa hali inayowalazimu mama wajawazito kulala wawili hadi watatu. https://youtu.be/lYzPEYHmXEs

SIMU.TV: Baraza la taifa la uhifadhi wa mazingira NEMC limeitoza faini ya shilingi milioni 25 shule ya Al muntazir ya jijini Dar es Salaam kwa kutiririsha maji taka kwenda eneo la bahari. https://youtu.be/jUVgeN1JCgs

SIMU.TV: Ukosefu wa mabweni kwa shule za sekondari umetajwa kuwa changamoto inayosababisha vitendo viovu kama uvutaji wa bangi. kwa wanafunzi. https://youtu.be/_eiftjWtiL0

SIMU.TV: Kampuni ya mafuta ya Lake Oil imetoa jumla ya madawati 50 kwa shule ya msingi Kibugumo jijini Dar es Salaam  ikiwa ni kuunga mkono juhudi za kumaliza tatizo la madawati. https://youtu.be/QsiGDXH3FMs

SIMU.TV: Utafiti umeonesha kuwa ongezeko la watoto wa mitaani na wanaoishi kwenye mazingira magumu unasababishwa na migogoro katika familia pamoja na kipato duni. https://youtu.be/RLNrJp3u10Q

SIMU.TV: Kampuni ya bia ya TBL imelenga kupanua wigo wa kuuza bidhaa zake hapa nchini ili kuongeza mapato ya kampuni na ulipaji wa kodi. https://youtu.be/t_rxsJln168

SIMU.TV: Wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama machinga wamepewa siku kumi na nne kuondoka maeneo yote yasiyo rasmi na kwenda maeneo waliyopangiwa. https://youtu.be/5B0Re1b-KtI

SIMU.TV: Makampuni nchini yamekumbushwa kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali katika kusaidia kuendeleza huduma za kijamii kama elimu na maji. https://youtu.be/OfpFqsDyYI0

SIMU.TV: Jumla ya timu kumi na mbili zinatarajia kushiriki katika ligi ya wanawake nchini inayoanza Novemba mosi mwaka huu na kuoneshwa moja kwa moja na vituo vya televisheni vya Azam. https://youtu.be/l7ZvdnPC79U

SIMU.TV: Timu nyingi zimeshindwa kushiriki katika mashindano ya netball yanayofanyika mkoani Ruvuma na kufanya timu tatu tuu kushiriki. https://youtu.be/UJfsmztBQrk

MPIGIE KURA KARIM MICHUZI KWENYE SHINDANO LA AIRTEL VIDEO CHALLENGE

SHULE YA SEKONDARI YA ALMUNTANZIR YA JIJINI DAR ES SALAAM YATOZWA FAINI KWA UCHAFUZI WA MAZINGIRA

$
0
0
Shule ya sekondari ya Almuntazir iliyopo upanga jijini Dae es salaam imetozwa faini ya shilingi milioni ishirini na tano kwa kosa la uchafuzi wa mazingira kwa kutirirsha maji taka ya chooni katika mto msimbazi ndani ya eneo la mikoko katika eneo la daraja la salenda na kujenga uzio wa ukuta bila kuzingatia mita sitini zinazotakiwa kisheria.

Faini hiyo inatakiwa kulipwa ndani ya wiki moja imetokana na ziara ya Naibu waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina iliyofuatia malalamiko ya wakazi wa Upanga iliyompelekea Naibu Waziri kufanya ziara yakwenda kujionea uchafuzi huo.

Akiongea kwa Niaba ya shule meneja wa shule hiyo Bw. Serialis Rwechungura amesema kuwa, watalipa faini hiyo kama ilivyoelekezwa na serikali na hakuwa tayari kuongelea swala la ukuta wa shule hiyo.

Naibu Waziri Mpina amesisitiza kuwa serikali haitakuwa tayari kuwavumila wawekeajia wakiukaji wa sheria hasa ya mazingira, na kuweka rehani maisha ya watanzania.

Aidha Naibu Waziri alitembelea maeneo  ya mwenge kijijini na kuonea uchafu wa mazingira uliotokana na kuvuja kwa maji taka ya choo kutoka kwenye miundombinu ya majitaka ya DAWASCO hali inayosababibsha wakazi na wafanyabiashara wa maeneo ya mwenge kushindwa kustahimili hali hiyo na kuwa hatarini kupata magonjwa ya maambukizi kama kipindupindu na homa ya matumbo.

Akiikemea DAWASCO kwa mara nyingine kwa kutokuonyesha uwajibikaji na utii kwa mamlaka za juu, Naibu Waziri Mpina ameita NEMC kuiandikia DAWASCO faini ya shilingi milioni ishirini na tano kwa kutelekeza miundombinu yao na kutakiwa kulipa adhabu hiyo kwa muda wa wiki mbili.

 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. Luhaga Mpina (katikati) alipofanya ziara ya kukagua mazingira katika kiwanda cha kutengeneza viroba vya mifuko Unberg International kilichopo jijini Dar es salaam.     
 


Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. Luhaga Mpina akikagua sehemu ya kuyeyushia viroba ya mifuko katika kiwanda cha Unberg International kilichopo jijini Dar es salaam mapema hii leo.

 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. Luhaga Mpina (kushoto) mara baada ya kuwasili na kutembelea kiwanda cha kutengeneza sabuni ya unga cha Murzer kilichopo jijini Dar e s salaam.   

Rais Dkt Magufuli amthibitisha Samwel Kamanga kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa NIC

$
0
0
  
Bw. Samwel Kamanga -Mkurugenzi Mtendaji wa NIC

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MWALIKO WA WADAU KUTOA MAONI KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA HUDUMA ZA HABARI

Mfalme wa Morocco aagwa na Rais Magufuli Jijini Dar es Salaam

$
0
0

Mfalme wa Morocco Mtukufu Mohammed VI leo tarehe 27 Oktoba, 2016 ameondoka Jijini Dar es Salaam na kuelekea Zanzibar.


Katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam Mtukufu Mohammed VI ameagwa na Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyeambatana na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan.


Akiwa Jijini Dar es Salaam Mtukufu Mohammed VI aliyewasili nchini tarehe 23, Oktoba 2016 kwa ziara ya kiserikali ya siku tatu amekutana na kufanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais Magufuli na pia viongozi hao wameshuhudia utiaji saini wa mikataba 21 inayohusu ushirikiano wa Tanzania na Morocco katika masuala mbalimbali ya kiuchumi.


Baada ya kumaliza ziara ya kiserikali ya siku tatu, Mtukufu Mohammed VI anaendelea na ziara binafsi hapa nchini.

  
Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

27 Oktoba, 2016.
ano1
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akajadiliana jambo na Mfalme wa Morocco Mohamed VI kabla ya kuagana nae katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNIA) jijini Dar es Salaam.
ano2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpokea Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakati alipowasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNIA) jijini Dar es Salaam.
ano3
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mfalme wa Morocco Mohamed VI kabla ya kuagana nae katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNIA) jijini Dar es Salaam.
ano5
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mfalme wa Morocco Mohamed VI kabla ya kuagana nae katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNIA) jijini Dar es Salaam.

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MKURUGENZI MKUU WA MFUKO WA MAENDELEO WA ABU DHABI MOHAMED AL SUWAIDI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Abu Dhabi Mohamed Al Suwaidi aliyefika Ikulu kwa ajili ya mazungumzo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu nchini Abdullah Ibrahim Al Suwaidi aliyefika Ikulu pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Abu Dhabi Mohamed Al Suwaidi kwa ajili ya mazungumzo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Abu Dhabi Mohamed Al Suwaidi mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

KUMBUKUMBU YA MIAKA MITATU YA KIFO CHA KOMANDO LUTENI RAJABU MLIMA

$
0
0
 Marehemu Komando wa vikosi maalum Luteni Rajabu Mlima
Marehemu Komando Luteni Rajabu Mlima akipokea tuzo enzi za uhai wake

Ilipotimu safari,kamanda yupo tayari

Tena kwenye msitari,kutekeleza amri

Hakukifanya kiburi,Kusema ninasubiri

Mungu akulazepema kamanda Rajabu Mlima


Uliifanya safari,Niyako wewe hiyari

Ulifahamu hatari,zaweza kukukabiri

Molla atakusitiri,kuufanya ujasiri

Mungu akulazepema kamanda Rajabu Mlima


Tulijiweka tayari,kwahamu  kukusubiri

Urejeapo safari,utapikiwa futari

Bakulini na mtori,upate kujisitiri

Mungu akulazepema kamanda Rajabu Mlima


Kifo hakina hiyari,Huwezi ukatabiri

Hakiwezi kusubiri,Imepitishwa amri

Linakuaga kaburi,hiyo ndiyo yake siri

Mungu akulazepema kamanda Rajabu Mlima


Siri ndiyo siri,Haitakuwa dhahiri

Japo uwe mashuhuri,maiti hawi jasiri

Huna tena ufahari,Nyumba yako nikaburi

Mungu akulazepema kamanda Rajabu Mlima


Kaburi imekua siri,masikini na tajiri

Hatuna yetu hiyari umekatiwa shauri

Mimi ninafikiri,Nasubiri hiyari

Mungu akulazepema kamanda Rajabu Mlima


Mitatu imedhihiri,Ndani yalako kaburi

Allah amekukiri,Usijekua kiburi

Hujafanya ufedhuri,Hili jambo si fahari

Mungu akulazepema kamanda Rajabu Mlima


Uhai tutafakari,Hakuna aliye hatari

Hii ni yake kahari,Asokuwa namshauri

Tena niyake fahari,Chumvi iwe sukari

Mungu akulazepema kamanda Rajabu Mlima


Mazuri huwa mazuri yasipopata dosari

Kuchota kwenye buri Siyosawa nabahari

Lazima tutafakari mja hana hiyari

Mungu akulazepema kamanda Rajabu Mlima


Nakiri nikisubiri zamu yangu ndiyo siri

Haina chakutabiri,ninasubiri kaburi

Siku itapo dhihiri,Sitakua jasiri

Mungu akulazepema kamanda Rajabu Mlima


Rabbi atusitiri, Ndani yahilo kaburi

Usipate ufakiri,mazuri nayawe mazuri

Kwenye lako daftari yaandikwe yaso shari

Mungu akulazepema kamanda Rajabu Mlima


MTUNZI: WAKO MAMA TUNGURI RAJABU TAMBWE




DC KAKONKO,KANALI NDAGALA AWAASA WAKULIMA, KULIMA MISIMU MIWILI KUPAMBANA NA BAA LA NJAA

$
0
0
Na Rhoda Ezekiel-Globu ya Jamii, Kigoma.

MKUU wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala amewaasa wakulima wa Bonde la Mto Katengela Kijiji cha Kinonko Wilayani Kakonko kulima mazao yao kwa misimu miwili ya Kiangazi na masika .Aidha pia amewashauri waanze kulima kwa kitaalamu zaidi ili wapate mazao ya kutosha.pamoja na kuwaeleza yote hayo lakini pia akawasisitizia umuhimu wa kujiunga kujiunga kwenye vyama vya ushirika na kuacha tabia ya kuuza mazao yote kutokana na hali ya hewa ya mwaka huu inayoweza kupelekea maeneo mengi kukosa chakula.

Akizungumza na wakulima wa Bonde la Mto katengera jana wakati wa ziara yake , vijiji vya Kinonko,Nyamibuye na Rumashi Ndagala alisema wakulima wengi wamekuwa na tabia ya kuuza mazao yote na kupelekea kubaki wakilia njaa baada ya mazao yao waliyo lima kuisha ,pia wakulima wanatakiwa kuunda vikundi vya ushirika vitakavyo wasaidia kupata mikopo,pembejeo na masoko yatakayo wasaidia kuuza bidhaa zao kwa bei ya juu.

Alisema Wakulima wakiweza kulima misimu yote miwili ya Kiangazi na masika,bonde hilo lina uwezo wa kuhudumia wananchi wote wa Kakonko kutokana na mkulima mmoja kuwa na uhakika wa kulima hekali moja na kuzalisha gunia nane  za mpunga kwa msimu mmoja wa mavuno na hali inayo weza kuikomboa wilaya hiyo isikumbwe na janga la njaa.

Aidha Ndagala amewaomba maafisa kilimo wa Wilaya hiyo kuwawezesha wakulima kulima kwa misimu miwili na kuwapa mbinu za kulima kitaalamu kwa kutumia pembejeo zinazotolewa na Serikali, ili kuweza kupata Mazao mengi na kuweka tahadhali kutokana na hali ya hewa inayo weza kupelekea ukosefu wa mvua.

"Nniwaombe wananchi kwa mwaka huu mlime mazao yanayo weza kustahimili ukame kama Vile mihogo, mtama na viazi na yale yanayo stawi haraka kutokana na mabadiliko ya tabia ya Nchi iliyojitokeza, hali inaweza kusababisha mwaka huu chakula kika kosekana kabisa, pia mjenge tabia ya kuhifadhi chakula msikiuze chote tusije tukaanza kuomba misaada wakati uwezo wa kuhifadhi chakula tunao",alisema Ndagala.

Kwa upande wake Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko,Muhdin Alfani alisema bonde hilo lina zaidi ya kilomita 29 na linawakulima 310 na mradi wa kukamilisha ujenzi wa bonde hilo la umwagiliaji ni shilingi milioni 312 na kila hekali moja linaweza kuzalisha gunia 18 kwa msimu mmoja wa kilimo.

Alisema lengo la Halmashauri  kuanzisha mradi huo ni kuwasaidia wananchi wa Wilaya hiyo kulima na kupata mazao ya kutosha yatakayo wasaidia kuilisha wilaya na Nchi jirani ya Burundi ambayo inategemea chakula kingi kutoka kwa Watanzania katika masoko ya ujirani mwema na kuweza kuiongezea serikali pato la taifa.

Nao baadhi ya wakulima wa bonde hilo,Issa Masumo na Shedrack Milembe wameiomba Halmashauri hiyo kuwawezesha kupata masoko na kupangiwa bei maalumu itakayo wasaidia kuepukana na unyanyasaji wa Wafanya biashara wanaokuja kununua mpunga na kuwapunja wakulima na kukosa haki yao ya msingi wao kama wakulima. 

Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala ,akizungumza jambo na baadhi ya wakulima walioko katika bonde la Katengele,wakati alipokuwa akikagua kilimo cha umwagiliaji katika Bonde la Katengela kijiji cha Kinonko Wilayani Kakonko katika mashamba ya Mpunga,mkoani Kigoma.Dc Ndagara aliwaeleza wakulima hao kuwa kuanza kulima mazao yao kwa misimu miwili ya Kiangazi na masika kitaalamu zaidi na kujiunga kwenye vyama vya ushirika na kuacha tabia ya kuuza mazao yote kutokana na hali ya hewa ya mwaka huu inayoweza kupelekea maeneo mengi kukosa chakula. 
Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala ,akiwasikiliza baadhi ya  wakulima walioko katika bonde la Katengele,wakati alipokwenda kukagua kilimo cha umwagiliaji katika Bonde la Katengela kijiji cha Kinonko Wilayani Kakonko katika mashamba ya Mpunga,mkoani Kigoma.
DC Ndagala akishiriki kulima kwenye moja ya shamba linaloandaliwa kwa ajili ya kilimo cha Mpunga,katika Bonde la Katengela kijiji cha Kinonko Wilayani Kakonko katika mashamba ya Mpunga,mkoani Kigoma.


Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagaa ,akipima kina cha maji yanayotumika katika kilimo cha umwagiliaji kwenye bonde la Katengele,wakati alipokuwa akikagua kilimo cha umwagiliaji katika Bonde hilo kijiji cha Kinonko, Wilayani Kakonko katika mashamba ya Mpunga,mkoani Kigoma.

MAFANIKIO YA KIUCHUMI KUTOKANA NA JITIHADA MBALI MBALI ZILIZOFANYWA NA SERIKALI YA AWAMU YA TANO KATIKA KIPINDI CHA MWAKA MMOJA - BENKI KUU YA TANZANIA

$
0
0
GAVANA WA BENKI KUU YA TANZANIA PROFESA BENNO NDULLU

Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, alipoingia madarakani mwezi Novemba 2015 aliendeleza jitihada za kukuza uchumi wa nchi yetu kwa kuweka mkazo na kutoa maagizo kwenye maeneo kadhaa.
Maeneo hayo ni pamoja na; kuongeza nguvu kwenye ukusanyaji wa kodi, kupiga vita rushwa, kuweka msisitizo mkubwa wa nidhamu ya matumizi ya fedha za umma, kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na kuelekeza matumizi katika sekta za vipaumbele vya maendeleo. 
Aidha, kuzitaka Wizara, Wakala na Taasisi za Umma kuweka fedha zao Benki Kuu na kuhimiza kila mtu afanye kazi na kula kwa jasho lake ili kutekeleza falsafa ya ‘Hapa kazi tu’. 




MAMLAKA YA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MJINI MOSHI (MUWSA) YAONGEZA VYANZO VIWILI VYA MAJI .

$
0
0
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi,Prof Faustine Bee (kushoto) akimuongoza Waziri wa Maji na Umwagiliaji ,Mhandisi Gerson Lwenge kuelekea katika chanz cha Mkashilingi kilichopo wilyani Hai kwa ajili ya uzinduzi, kulia kwa Waziri ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA).Joyce Msiru. Waziri wa Maji na Uwagiliaji ,Mhandisi Gerson Lwenge akizungumza wakati wa uzinduzi wa chanzo cha maji cha Mkashilingi kilichopo wilayani Hai mkoani Kilimanjaro.Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Said Meck Sadiki akizungumza katika uzinduzi huo.
 Baadhi ya wananchi waliohudhuria uzinduzi huo wakimsilikiliza Waziri wa Maji na Umwagiliaji (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa chanzo cha Mkashilingi. 

WAZIRI MAKAMBA AIPONGEZA JANE GOODALL INSTITUTE

$
0
0

Na Lulu Mussa- Kigoma

Shirika lisilo la Kiserikali la Jane Goodall linalojishughulisha na Mradi wa utafiti wa sokwe na wanyamapori wengine limepongezwa kwa jitihada zake za kutunza mazingira na kusaidia jamii kuhifadhi mfumo wa ikolojia ukanda wa Magharibi mwa Tanzania.

Pongezi hizo zimetolewa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba mara baada ya kutembele Ofisi zao Mkoani Kigoma. Waziri Makamba amesema kuwa Shirikal hilo la Jane Goodall limekuwa mstari wa mbele katika kubuni miradi ambayo inagusa jamii moja kwa moja.

Akitoa maelezo ya shughuli zinazotekelezwa na shirika hilo kwasasa, Naibu Mkurugenzi wa Bi. Mary Mavanza amesema kuwa wanatekeleza miradi mitatu ikiwa ni pamoja na Mradi wa utafiti wa sokwe na wanyamapori, Mradi wa Mizizi na chipukizi ambao unatekelezwa nchi nzima katika shule zote na mradi wa uhifadhi unatekelezwa katika Halmashauri za Wilaya za Mpanda, Nsimbo kwa Mkoa wa Katavi na Uvinza kwa Mkoa wa Kigoma.

Aidha, Shirika hili pia limefanikiwa kuhamasisha wanajamii 42 kufanya shughuli za kukuza kipato ambazo ni rafiki kwa mazingira kupitia ufugaji nyuki na huduma za ki ikolojia. Pamoja na mafanikio hayo shirikali hili limewasilisha hoja ya kwa Waziri Makamba kusaidia kukamilika kwa Mchakato wa kupandisha hadhi ya ardhi jumla kuwa misitu ya Hifadhi ya Wilaya ili kudhibiti idadi kubwa ya sokwe waliobaki Tanzania ambao kwa sasa hawana ulinzi thabiti.

Taasisi ya Jane Goodall liliasisiwa miaka 56 iliyopita na mtafifiti Dr. Jane Goodall kwa lengo la kufanya shughuli za kitafiti, kurejesha uoto wa asili uliopotea na kuhakikisha wanajamii wanaboresha uchumi wao kwa kutumia maliasili zinazowazunguka. Waziri Makamba pia ametembelea Hifadhi ya Taifa ya Gombe kwa lengo la kufuatilia changamoto za kimazingira Hifadhini hapo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba akiwa katika boti Maalumu kuelekea Hifadhi ya Taifa ya Gombe

Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Gombe Bw. Donatus Bayona (kulia) na Bi.Happy Kiyemi Mkuu wa Idara ya Utalii wakimuongoza Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba kutembelea Hifadhi ya Gombe

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba akizungumza na Uongozi wa Shirika lilisilo la Kiserikali la Jane Goodall, mara baada ya Mhe. Waziri Makamba kutembelea Ofisi zao Kigoma Mjini. Wa kwanza kulia ni Bi. Mary Mavanza Naibu Mkurugenzi wa Mradi wa kuhifadhi mfumo wa Ikolojia Ukanda wa Magharibi mwa Tanzania. Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Bw. Samson Anga 
……………………………………………………… 

BBC DIRA YA DUNIA ALHAMISI 27.10.2016

Viewing all 110186 articles
Browse latest View live


Latest Images