Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live

WAZIRI NAPE ATOA WITO KWA WADAU KUTOA MAONI ILI KUUBORESHA MUSWADA WA SHERIA YA HUDUMA ZA HABARI WA MWAKA 2016.

$
0
0


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa Michezo Mhe. Nape Nnauye (MB) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) ambapo alitoa wito kwa wadau mbalimbali katika sekta ya habari kutoa maoni ili kuuboresha
Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari wa Mwaka 2016(The Media Service Bill, 2016) uliosomwa kwa mara ya kwanza leo Bungeni Mjini Dodoma, Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji wa Serikali Bw. Hassan Abbas.

Baadhi ya waandishi wa Habari wakimsikiliza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa Michezo Mhe. Nape Nauye (MB) katika mkutano aliufanya na kutoa wito kwa wadau kuboresha Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari wa Mwaka 2016(The Media Service Bill, 2016) uliosomwa kwa mara ya kwanza leo Bungeni Mjini Dodoma. PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO

TPSF WAKUTANA NA WADAU WA SEKTA BINAFSI KUTENGENEZA AGENDA YA BIASHARA YA TAIFA (NATIONAL BUSINESS AGENDA)

$
0
0
 .Mkurugenzi wa Uhamasishaji Sera na Utafiti wa TPSF,Gili Teri akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wakujadili Agenda maalum inayohusisha masuala mbalimbali yakiwemo ya Kilimo,Nishati,Elimu na mengineyo.
.Baadhi ya Wadau wa Sekta Binafsi na Wafanyabiashara wakiwa katika semina hiyo.

Taasisi ya Sekta Binafsi nchini(TPSF) imekutana na Wafanyabiashara pamoja na wadau wa Sekta Binafsi ili kutengeneza Agenda ya Biashara ya Taifa.

Agenda hiyo ina lengo la kukusanya maoni pamoja na matarajio ya wadau wa Sekta Binafsi hususan kuelekea katika Uchumi wa Viwanda miaka 5 na 10 ijayo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika semina maalum iliyowakutanisha Wadau wa Sekta Binafsi,Mkurugenzi wa Uhamasishaji Sera na Utafiti wa TPSF,Gili Teri amesema Agenda hiyo inahusisha masuala mtambuka lakini masuala halisi ya Kisekta yakiwemo ya Kilimo,Nishati,Elimu na Sekta nyingine mbalimbali.

"Mazingira ya Biashara yanapoboreshwa mimi na wewe tunaofanya biashara tunaweza kufaidika zaidi,tukaajiri watu wengi na tukalipa kodi zaidi,"amesema Teri

Amesema wanatengeneza agenda ya pamoja ambayo itatumika kama kitu cha ambacho kitaongoza mawasiliano kati ya Sekta Binafsi pamoja na wadau wengine wakiwemo Serikali.

MICHUANO YA WUSHU KUANZA KUTIMUA VUMBI KESHO

$
0
0
Rais wa Mchezo wa Wushu, Mwalami Mitete akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uzinduzi wa mashindano ya Wushu yanayotarajiwa kuanza kesho kwenye Uwanja wa Ndani wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Kulia ni Katibu Mkuu Gola Kapipi na Kushoto ni Makamu wa Raisi Kawina Hadji Konde.
MKUU wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa michuano ya Wushu Tanzania inayoanza kesho Septemba 17 na 18 kwenye uwanja wa Taifa kuanzia saa 4 asubuhi.

Mchezo wa Wushu ambao asili yake ni nchini China unajumuisha Karate, Kung Fu, Judo na aina zote za michezo yote ya mapigano kitu ambacho kitakuwa ni kivutio kikubwa kwa watakaohudhuria.

Mashindano hayo yatahusisha washiriki mbali mbali toka mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Pwani,Morogoro, Lindi, Mtwara, Pemba pamoja na Mbeya.

Rais wa chama cha Wushu Tanzania Mwalami Mitete amesema washindi wa mashindano hayo watapata medali, fedha taslimu, vikombe, Simu za mkononi pamoja na vyeti vya utambulisho ambavyo vitawawezesha kushiriki mashindano mbali mbali ndani na nje ya nchi.

Mitete amesema kuwa kumekuwa na dhana potofu kuwa michezo ya mapigano ndiyo chanzo cha machafuko lakini amekanusha vikali na kusema ni kama zilivyo fani nyingine na ajira pia kwakua inaweza kuwaingizia washiriki kipato.

Naye Balozi wa Utamaduni wa China nchini Gao Wei amesema wataendelea kushirikiana na chama hicho ili kuhakikisha mashindano hayo yanaendelea kufanyika kila mwaka yakiwa yameboreshwa.

VOA: Rais Filipe Nyusi wa Msumbiji azungumza na Abdushakur Aboud

MAGIC FM WATAKIWA KUOMBA RADHI, RADIO 5 WAFUNGIWA MIEZI MITATU NA KUPIGWA FAINI YA MILIONI 5.

$
0
0

KITUO cha Redio cha Magic FM  cha jijini Dar es Salaam wamepewa onyo kali na kumwomba radhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, DKT.John Pombe Magufuli, wasikilizaji na wanaanchi kwa ujumla kwa kosa la kukiuka kanuni za huduma za utangazaji (Maudhui) za 2005.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA),  Bw. Joseph Mapunda 
amesema kuwa Magic FM wanatakiwa kuomba radhi kwa siku tatu mfululizo katika taarifa za habari za kuanzia saa kumi alasiri hadi saa tatu usiku kuanzia Septemba 17-19 mwaka huu.
Kwa upande wa Kituo cha utangazaji cha Redio 5 cha jijini Dar es Salaam kimepigwa faini ya shilingi milioni tano kwa kosa la kukiuka kanuni za huduma za utangazaji (Maudhui) za 2005 kupitia kipindi chake cha Matukio kilichorushwa hewani kati ya saa mbili na saa tatu usiku.

Pia kituo hicho cha Redio 5 kimefungiwa kwa miezi tatu kuanzia leo na vile vile kituo hicho kimewekwa chini ya uangalizi maalumu kwa muda wa mwaka mmoja baada ya kipindi cha Kufungiwa Kumalizika.
Amesema kuwa haki ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi huo iko wazi ndani ya siku 30 kuanzia leo.
Uamuzi wa Kamati ya Maudhui Kuhusu lalamiko la ukiukaji wa Kanuni za huduma za Utangazaji (Maudhui), 2005 wawakilishi wa vituo vyaMagic FM na Radio 5 jijini Dar es Salaam leo.







Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA), Joseph Mapunda akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kutoa hukumu ya Vituo vya Redio  vilivyukuwa vimefungiwa  jijini Dar Salaam leo.
 Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA), Joseph Mapunda akiwakabidhi  wamiliki wa vituo hivyo hati za hukumu.Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.

GAVANA WA BENKI KUU PROFESA BENNO NDULU AZUNGUMZIA HALI YA UCHUMI NCHINI

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AFUNGUA MKUTANO WA WAKUU WA MAJESHI YA POLISI WA NCHI ZA KUSINI MWA AFRIKA (SARPCCO)

$
0
0
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan (kulia) akihutubia wakati wa Ufunguzi wa mkutano wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi kutoka nchi za Kusini mwa Afrika (SARPCCO) kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa AICC jijini Arusha. 
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Ernest Mangu ambaye amekabidhiwa Uenyekiti wa Shirikisho la Wakuu wa Majeshi ya Polisi Kusini mwa Afrika (SARPCCO) akipeana mikono na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Msumbiji Dos Santos JANE (kushoto) ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Shirikisho hilo mara baada ya kukabidhiana Uenyekiti katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa AICC jijini Arusha
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan (kulia) akimpa mkono wa pongezi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Ernest Mangu mara baada ya kukabidhiwa Uenyekiti wa SARPCCO kwenye mkutano wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi wa Nchi za Kusini mwa Afrika.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Hamad Masauni akihutubia kwenye mkutano wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi wa nchi za kusini mwa Afrika.

..........................................................................

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewataka Wakuu wa Majeshi ya Polisi Kusini mwa Bara la Afrika kuweka mipango na mikakati madhubuti ya kukabiliana na vitendo mbalimbali vya uhalifu vinavyotokea katika ukanda huo kama hatua ya kuhakikisha wananchi wanafanya kazi zao kwa amani na utulivu.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo 16-Sep-2016 wakati anafungua mkutano wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi Kusini mwa Afrika katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC jijini Arusha.

Makamu wa Rais amesisitiza kuwa anaimani kubwa kuwa mkutano huo utakuwa ni chachu katika kuibua changamoto mbalimbali za kihalifu na kuzifanyia kazi ipasavyo kwa manufaa ya ukanda huo.

Amesema ni wajibu wa wakuu hao wa majeshi ya polisi ya kusini mwa Afrika kujiepusha na malalamiko yasiyo ya msingi kutoka kwa raia ambayo yanasababishwa na vitendo vya urasimu, uzembe na rushwa ili kujenga uwazi na uwajibikaji.Makamu wa Rais pia amehimiza kudumishwa kwa ushirikiano miongoni mwa wakuu wa majeshi ya polisi kusini mwa Afrika katika kubadilishana mbinu bora za kukabiliana na vitendo vya uhalifu wa kuvuka mipaka.

Katika mkutano huo Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini –IGP- Ernest Mangu amekabidhiwa uenyekiti wa Shirikisho la wakuu wa Majeshi ya Polisi kusini mwa Afrika (SARPCCO) kutoka kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi wa Nchi ya Msumbiji Dos Santos JANE.

Shirikisho la SARPCCO lilianzishwa mwaka 1995 kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa majeshi ya polisi kusini mwa Afrika katika kukabiliana na vitendo vya uhalifu katika ukanda huo.

Shirikisho hilo linaundwa na nchi wanachama 15 ambapo baadhi ya nchi hizo ni Angola, Botswana, Msumbiji, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo- DCR-,Malawi, Zambia, Zimbabwe, Madagascar,Swaziland, Afrika Kusini,Lesotho, Syshelles na Tanzania ambayo ni mwenyekiti mpya wa SARPCCO.

Tanzania imekabidhiwa uenyekiti wa SARPCCO wakati ndio Mwenyekiti mpya wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika inayojulikana kwa jina la (SADC TROIKA).

Kesi ya mauaji ya wafanyabiashara wa madini watatu na dereva teksi mmoja: Christopher Bageni ahukumiwa kunyongwa hadi kufa, zombe na wenzie wawili waachiwa huru

$
0
0
 Aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Ilala Christopher Bageni amehukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya Mahakama ya Rufani Tanzania kutengua hukumu iliyomwachia huru na kumtia hatiani kwa kosa la mauaji ya wafanyabiashara wa madini watatu na dereva teksi mmoja.
Kadhalika mahakama hiyo imewaachia huru  Mkuu wa Upelelezi wa zamani (wakati huo Mkoa wa Dar es Salaam) (RCO), Kamishna Msaidizi wa Polisi  mstaafu Abdallah Zombe na wenzake wawili baada ya ushahidi wa rufaa hiyo kushindwa kuwatia hatiani.
Mara baada ya hukumu kusomwa, ghafla Bageni aliduwaa wakati wenzake wakimkumbatia huku  wakibubujikwa na machozi wakiwa kizimbani. 
Wanaodaiwa kuwa wanafamilia wa washtakiwa hao waliangua vilio huku washtakiwa wenzake walisikika wakieleza masikitiko yao. Wengine walisikika wakisema angejua asingekuja mahakamani kusikiliza hukumu hiyo.
“Namshukuru Mungu...Lakini nasikitika kwa Bageni kukutwa na hatia sina raha kabisa....” alisema ASP Makele wakati akitoka katika ukumbi namba moja wa mahakama hiyo. 
Akizungumza baada ya hukumu hiyo,  ACP mstaafu Zombe alisema anamshukuru Mungu na kuhusu Bageni alisema hana cha kuzungumzia.
Hukumu hiyo imesomwa leo na Msajili wa mahakama hiyo Mhe. John Kahyoza baada ya rufani iliyokatwa na upande wa Jamhuri  kusikilizwa na jopo  la majaji watatu likiongozwa na Mwenyekiti, Jaji Bernard Luanda, Jaji Sauda Mjasiri na Jaji Semistocles Kaijage.
Msajili alisema awali Mahakama Kuu iliyoketi chini ya Jaji Salum Massati (wakati huo kabla ya kupanda kuwa jaji wa rufani), ilimuona Zombe na wenzake hawana hatia na kwamba haiwezi kuwahukumu kwa kosa la kusaidia kufanyika mauaji hayo.
Alisema Mahakama ya Rufani inakubaliana na Jaji Massati  kwamba mtuhumiwa hawezi kutiwa hatiani bila kuthibitisha mtu aliyetenda kosa hajashtakiwa na kutiwa hatiani.

Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA



TCU yaongeza muda wa udahili wa vyuo vikuu

$
0
0
 Na: Lilian Lundo - MAELEZO
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imeongeza muda wa udahili wa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na vyuo vikuu mwaka wa masomo 2016/2017 ili kuwapa fursa  waombaji ambao wana sifa lakini hawakupata vyuo kutokana na ushindani wa vyuo na kozi walizozichagua.

Hayo yamesemwa na Kaimu Katibu Mtendaji wa TCU Prof. Eleuther Mwageni alipokuwa akiongea na waandishi wa habari juu ya mwenendo mzima wa udahili kwa mwaka wa masomo 2016/2017, leo  Jijini, Dar es Salaam.
“ Tume imekamilisha awamu ya kwanza ya udahili kwa waombaji wenye sifa ya kidato cha 6, ambapo jumla ya waombaji wote ilikuwa 55,347, waombaji wenye sifa ni 47,203 sawa na asilimia 85.3 ya waombaji wote. Katika waombaji hao wenye sifa waliopata vyuo ni 30,731 sawa na asilimia 65 na waombaji 16,472 ambao wana sifa sawa na asilimia 35 hawajapata vyuo hadi sasa, waombaji waliokosa sifa ni 8,144,” alifafanua Prof. Mwageni.

Amesema kuwa Tume imeamua kuongeza muda wa udahili kuanzia Septemba 12 mpaka Septemba 23, 2016 ili kuwapa nafasi waombaji wenye sifa, fursa ya kuomba tena vyuo na kozi zenye nafasi kutokana na  wengi wao kuomba vyuo na kozi za aina moja.
Prof. Mwageni alivitaja vyuo ambavyo vimeombwa na waombaji wengi na tayari vimeshajaa kuwa ni Chuo cha Ardhi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Afya na Sayansi Shirikishi, Chuo Kikuu cha Kikristo cha Tiba Kilimanjaro(KCMUCo) na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili.
Pia alizitaja kozi ambazo zimechaguliwa na waombaji wengi kuliko nafasi zilizopo kuwa ni kozi ya Ualimu, Udaktari wa Binadamu, Ufamasia, Uhandisi, Sayansi ya Uthamini wa Ardhi na Sheria. Alitoa mfano wa kozi ya Ualimu Chuo Kikuu Kishiriki cha Ualimu Dar es Salaam ilikuwa na waombaji 15,803 wakati nafasi ni 1,000.
Hivyo amewashauri waombaji waliokosa nafasi kuomba vyuo na kozi zisizo na ushindani ili waweze kupata nafasi kwa awamu hii ya pili.

Aidha Tume hiyo imepunguza viwango vya udahili kwa waombaji wenye sifa ya stashahada kutoka GPA 3.5 mpaka 3.0. Hivyo wamewataka waombaji wenye vigezo hivyo kuomba vyuo na kwa wale waliomba awamu ya kwanza hawatatakiwa kuomba tena bali kusubiri matokeo ya waombaji wenye sifa ya stashahada. 

CRDB YATOA MADAWATI 90 KWA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO

$
0
0
Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Songea mkoani Ruvuma Enock Lugenge kushoto akikabidhi jana, madawati 90 yenye thamani ya shilingi milioni 5 kwa makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Titus Ng'oma ikiwa ni msaada wa benki hiyo kwa ajili ya kuwanusuru wanafunzi wa shule za msingi wilayani humo kukaa chini.
Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Titus Ng'oma kulia akipokea moja kati ya madawati 90 yenye thamani ya shilingi milioni 5 yaliyotolewa na Benki ya CRDB Tawi la Songea kutoka kwa meneja wa Benki hiyo Enock Lugenge kushoto, ikiwa ni kuitikia wito wa Rais Dkt John Magufuri ya kuwataka wadau mbalimbali wa maendeleo kushirikiana na serikali yao kupunguza uhaba wa madawati kwa shule za msingi na sekondari hapa nchini,wanaoshuhudia kwa nyuma ni wajumbe wa kamati ya fedha uchumi na mipango wa halmashauri ya wilaya hiyo.
Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Titus Ng'oma aliyekaa katikati,meneja wa benki ya CRDB Tawi la Songea Enock Lugenge wa kwanza kushoto,na afisa elimu ya msingi wa wilaya ya Namtumbo Alberto Mbilinyi kulia wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati ndogo ya fedha uchumi na mipango ya baraza la madiwani wa halmashauri hiyo mara baada ya benki ya CRDB kukabidhi msaada wa madawati 90 yenye thamani ya shlingi Mil 5 kwa halmashauri hiyo. PICHA NA MUHIDIN AMRI

Waziri Mahiga apokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mteule wa Uingereza nchini

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Uingereza Mhe. Sarah Cooke na kufanya mazungumzo naye. Mazungumzo yao yalijikita katika kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Uingereza katika nyanja mbalimbali za maendeleo. Tukio hilo lilifanyika Wizarani tarehe 16 Septemba, 2016.
Dkt. Mahiga akizungumza na Balozi Mteule wa Uingereza nchini, Mhe. Cooke mara baada ya kupokea Nakala zake
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Itifaki Bw. James Bwana (wa kwanza kulia) akielezea jambo kwa Dkt. Mahiga na Balozi Cooke
Mazungumzo yakiendelea.

JACQUELINE MENGI AFANYA UZINDUZI WA DUKA LA SAMANI “AMORETTE”

$
0
0

Mrembo wa taji la Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi akizungumza na wageni walikwa pamoja na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa duka lake la samani za ndani "Amorette" lililopo katika jengo la Village Walk gorofa ya kwanza karibu na Sea Cliff Hotel, Masaki jijini Dar es Salaam.
Bi. Jacqueline Mengi akiongozana na baadhi ya wageni waalikwa kuingia ndani ya duka la "Amorette"
Balozi Juma Mwapachu na baadhi ya wageni waalikwa wakiangalia moja ya meza ya chakula (dining table) iliyotengenezwa kwa mbao aina ya Mninga baada ya kuzinduliwa duka hilo lililopo katika jengo la Village Walk, Masaki jijini Dar. Kwa habari na picha zaidi BOFYA HAPA

Tume ya Mipango yakamilisha Mafunzo ya Usimamizi wa Uwekezaji wa Umma Mikoa ya Singida, Manyara na Dodoma

$
0
0
Na Adili Mhina, Dodoma

Tume ya Mipango imehitimisha mafunzo ya Usimamizi na Utayarishaji wa Miradi ya Uwekezaji katika sekta ya Umma yaliyowahusisha maofisa mipango wa Sekretarieti za Mikoa na Halmashauri kutoka Mikoa ya Singida, Manyara na Dodoma yaliyofanyika tarehe 12-16 Septemba, 2016 katika ukumbi wa VETA mjini Dodoma.

Akifunga mafunzo hayo Kaimu Katibu Mtendaji kutoka Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri aliwasihi washiriki kutumia ujuzi waliyoupata katika kuandaa, kutekeleza miradi ya Umma kwa njia za kisasa ili kuongeza ufanisi wa miradi na kuharakisha maendeleo ya wananchi.

Alisema kuwa Tume ya Mipango imefanikiwa kutekeleza wajibu wake wa kuwajengea uwezo maafisa hao katika hatua zote muhimu zinazopaswa kuzingatiwa katika kufanya maandalizi, kutekeleza, kusimamia, kufuatilia na kufanya tahmini ya miradi ya maendeleo.

“Ni matumaini yangu kuwa hizi siku tano hazijapotea, mmepata elimu ya kutosha kutoka kwa wataalamu wetu katika masuala yote muhimu yanayohusu miradi ya Umma. Jukumu mlilonalo kwa sasa ni kuhakikisha mnatumia mbinu mlizofundishwa katika kutekeleza miradi ya serikali kwa usahihi ili tufikie malengo ya  mpango wa pili wa maendeleo wa miaka mitano,” Alisema.

Nao washiriki wa mafunzo hayo walieleza kuwa wamepata elimu muhimu ambayo itarahisisha utendaji katika kusimamia miradi na kutoa ushauri wa kitaalamu katika ngazi mbalimbali za maamuzi.

Walieleza kuwa mafunzo hayo yamewasisitiza kutumia vigezo muhimu wakati wa kufanya uchambuzi wa kiuchumi na kifedha ili kufikia uamuzi wa kutambua miradi ipi ina manufaa na inaweza kupata mikopo katika soko la mitaji.

“vigezo kama mzunguko wa mradi (project cycle) ikiwa ni pamoja na andiko la awali (concept note), mchanganuo wa faida na hasara (cost-benefit analysis) vigezo vya kuchanganua mradi kama vile uwezo wa uzalishaji (internal rate of return)  na thamani halisi ya uwekezaji (Net Present Value) vimetolewa ufafanuzi mzuri na vimeeleweka na tumevielewa” Alisema mmoja wa wakufunzi aliyejulikana kwa jina la Jemsi.

Tume ya mipango inaendelea na zoezi lake la kutoa mafunzo kwa walengwa wakuu ambao ni wataalam wa Sera na Mipango ambapo kuanzia Septemba 19 wataalamu wa mafunzo hayo watakuwa Mkoani mbeya kwa ajili ya zoezi hilo.
Kaimu Katibu Mtendaji kutoka Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (katikati) akitoa hotuba ya kufunga mafunzo ya Usimamizi na Utayarishaji wa Miradi ya Uwekezaji katika Sekta ya Umma kanda ya kati iliyojumuisha mikoa ya Dodoma, Singida na Manyara katika ukumbi wa VETA mjini Dodoma. Kulia ni mkufunzi wa mafunzo hayo, dkt. John Mduma kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kushoto ni Kaimu Naibu Katibu Mtendaji, Klasta ya Uchumi Jumla,Tume ya Mipango, dkt. Lorah Madete.
Washiriki kundi la kwanza wakijadili maswali waliyopewa na wakufunzi kabla ya kuhitimishwa kwa mafunzo hayo Septemba 16, 2016.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

KATIBU MKUU OFISI YA WAZIRI MKUU AFANYA ZIARA KATIKA VIZUIZI VYA BARABARANI (MIZANI)

$
0
0
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua akiweka sahihi katika kitabu cha wageni wakati wa ziara yake katika Vizuizi vya barabarani (Mizani) na Mipakani kwa lengo la kufanya Tathimini ya Utekelezaji wa mpango wa maboresho ya mazingira ya biashara na uwekezaji nchini Septemba 15, 2016.
Msimamizi wa Kituo cha Mamlaka ya Mapato TRA kilichopo Mkoani Pwani Bw. David Kisanga akitoa maelezo juu ya utendaji wa ofisi zao kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua wakati alipotembelea ofisi hizo Mkoa wa Pwani.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua akimsikiliza Msimamizi wa Kizuizi cha Vigwaza Mkoani Pwani Bw. Titus Michael wakati wa ziara yake kujionea hali halisi ya vituo hivyo kwaajili ya Maboresho ya mazingira ya biashara na Uwekezaji nchini.
Baadhi ya magari yakipima uzito wa mizigo katika Mizani ya Vigwaza mkoa wa Pwani, Septemba 15, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

SIMBA NA AZAM NI VITA KUWANIA KUSHIKA USUKANI WA LIGI KUU UWANJA WA UHURU LEO

$
0
0
Timu ya Azam FC "Wanalambalamba" na Wekungu wa Msimbazi Simba SC wanakutata kukipiga jioni ya leo katika mtanange wa kuwania nafasi ya kuongoza Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara mchezo utakaopigwa kwenye Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam. 

Timu hizo zinakutana leo ikiwa zote zinatiana kabali kwa kuwa na pointi na wastani wa magoli yao pia, baada ya mechi nne za awali huku kila moja ikiwa imeshinda mechi tatu na kutoa sare moja moja, hivyo ayakayefanikiwa kupata ushindi kwenye mtanange huo, ndie ataushikilia usukani wa Ligi kuu kwa sasa.

Timu ya Globu ya Jamii iko tayari tayari kukuletea matukio mbalimbali katika picha ya Mchezo huo, hivyo usikae mbali na libeneke lako hili pendwa kupata taswira mwanana kabisa za Mchezo huo.
Kikosi cha Azam Fc.

JOGGING SIO UHUNI,KUNA WATU WALITAKA KUPENYEZA MAMBO YAO NA KUTAKA KUICHAFUA JOGGING- DC ILALA -

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh Sophia Mjema (pili kulia) akiwa sambamba na Katibu Tawala wa wilaya hiyo Edward Mpogolo (tatu kushoto) wakishiriki mazoezi ya pamoja ya kikundi cha klabu ya Mazoezi cha New Life Jogging,na vikundi vingine mbalimbali vya mazoezi , mapema leo asubuhi katika viwanja vya Kimanga,Tabata Mawenzi,jijini Dar,ambapo Mkuu wa Wilaya alialikwa kuwa mgeni rasmi kwenye hafla fupi ya kikundi cha New Life Jogging kilipokuwa kinatimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake.PICHA NA MICHUZI JR-MMG.
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh Sophia Mjema akikabidhiwa Risala na Mwenyekiti wa kikundi cha Newa Life Jogging,Baraka Urio akiwa ameambatana na wanachama wa kikundi hicho,mara baada ya kuisoma na kuelezea changamoto na fursa mbalimbali zilizopo ndani ya kikundi hicho.Kikundi hicho chenye makazi yake Tabata Mawenzi leo kimetimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake.
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh Sophia Mjema akizungumza mbele ya vikundi mbalimbali vya mazoezi (havipo pichani),vilivyoshiriki kwenye hafla hiyo fupi ya kutimizwa mwaka mmoja wa kikundi cha New Life Jogging.Mh.Mjema aliwataka viongozi wa vikundi hivyo kuelezea changamoto zao walizo nazo ikiwemo na fursa zilizopo ili serikali kupitia Ofisi yake ziweze kufanyiwa kazi kwa wakati.Mh Mjema alisema kuwa Jogging sio uhuni,isipokuwa kuna watu walitaka kupenyeza mambo yao katika Jogging.

"Lakini wale waliotaka kuyapenyeza hayo,waliotaka kuingiza uhalifu,waliotaka kupenyeza madawa ya kulevya ,waliotaka kuingiza siasa,waliotaka kuingiza Panya rodi washindwe na walegee,hatutaki Jogging zetu zichafuke,tunataka Jogging zitumike kuona fursa zilizopo",alisema Mh Mjema.
Katibu Tawala wilaya ya Ilala,Ndugu Edward Mpogolo akiwasalimia na kuwatia moyo vikundi hivyo vya Jogging,ambaye pia aliwaeleza kuwa wakati wa kujituna na kufanya kazi ni sasa,hivyo amewaomba viongozi wa vikundi hivyo kukutana nao ili kuhakikisha fursa na changamoto walizozieleza katika risala yao zinafanyiwa kazi kwa wakati.
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh Sophia Mjema akikabidhiwa jezi na Mwenyekiti wa kikundi cha New Life Jogging,Baraka Urio,pichani kati ni Katibu Tawala wilaya ya Ilala,Ndugu Edward Mpogolo na wadau wengine wakishuhudia tukio hilo.
Mgeni rasmi,Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh.Sophia Mjema na viongozi wengine waandamizi kutoka ofisi ya Mkuu wa wilaya wakiwa katika picha ya pamoja na Kikundi cha New Life Jogging,ambacho leo kinasherehekea kutimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake.
Vikundi mbalimbali vilishiriki kwenye mazoezi hayo ya pamoja.

Waziri Nape kutoa laki tano kwa kila goli la Serengeti Boys

$
0
0
Na Lorietha Laurence-WHUSM.

Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye ameahidi kutoa shilingi laki tano kwa kila goli litakalofungwa na timu ya Serengeti Boys katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 utakaofanyika kesho katika Uwanja wa Taifa dhidi ya Congo-Brazzaville.

Akiongea na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Mhe.Nape amesema milango ipo wazi kwa wadau wengine wa michezo kujitolea katika kuiwezesha timu na hivyo kufanya vizuri katika mechi hii ambayo ni muhimu sana kushinda ili kufuzu kwa fainali hizo.

“Hii timu ni yetu sote hivyo inahitajika tuimiliki, tuepe nguvu, tuiombee ili iweze kufanya vizuri na hatimaye kufuzu kuingia fainali kwa kuitoa timu ya Congo-Brazzaville” alisema Mhe. Nape.

Aidha aliongeza kuwa kesho asubuhi atakutana na wachezaji wa timu hiyo ili kuwapa maneno ya faraja kabla ya kuanza kwa mechi na kuwataka watanzania kujitokeza kwa wingi uwanjani ili kuwapa motisha wachezaji kwa kuwashangilia na kuwatia moyo.

Mbali na hayo Waziri Nape alitoa ufafanuzi kuhusu matumizi ya kadi za kieletroniki zilizozinduliwa hivi karibuni kwa kueleza kuwa kadi hizo bado hazijaanza kutumika rasmi ili zitaanza kutumiwa katika mchezo baina ya Wabunge wa Simba na Yanga pamoja na Bongo Fleva.

Timu ya Serengeti Boys inaundwa na vijana wa Kitanzania wenye umri chini ya miaka 17 ambapo katika mchezo wa kesho watahitaji ushindi na baadaye kufanya mechi ya marudiano mnamo Oktoba 2 mwaka huu nchini Congo-Brazzaville.

Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye akizungumza na waandishi wa Habari (hawapo Pichani) kuhusu mchezo kati ya Serengeti Boys na Congo-Brazaville utakaofanyika Septemba 18 katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam. Picha na May Simba WHUSM

MKUU WA MKOA WA MTWARA,HALIMA DENDEGO ATOA WITO KWA WANANCHI KUPANDA MITI YA MIKOROSHO

$
0
0

Wakati serikali ikihamasisha jamii kutekeleza adhma yake ya upandaji wa miti, Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Halima Dendego amesema katika mkoa huo kila kaya inatakiwa kupanda miti 30 ya mikorosho kwaajili ya kutekeleza agizo la serikali sambamba na kukuza uchumi wa kaya.

Dendego aliyasema hayo wakati aliposhiriki zoezi la usafi na upandaji wa miti katika hospitali ya rufaa ya Ligula lililoandaliwa na waandishi wa habari wa mkoa huo kwa kushirikiana na kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania.

Alisema mkoa huo kwa kiasi kikubwa uchumi wake unategemea zao la korosho hivyo katika kutekeleza agizo la serikali wananchi wa mkoa huo hawatapanda mti ni mti bali watatakiwa kupanda miti ya mikorosho ambayo pia itawasaidia kukuza uchumi wao kwa faida.

"Wazo la waandishi wa habari kufanya usafi na kupanda miti linapaswa kuigwa na watu wote, tunataka nchi yetu iwe nadhifu na serikali imetoa agizo la upandaji miti,sisi kwa mkoa wa Mtwara hatutapanda mti ni mti tumeamua kila kaya itapanda miti 30 ya mikorosho ambapo itasaidia kuinua uchumi wa kaya,mkoa na taifa kwa ujumla lakini pia tutakuwa tumetekeleza agizo la kiserikali la upandaji miti kwa hiyo miti tutakayopanda sisi itakuwa na faida zaidi,"alisema Dendego

Akizungumza Mkuu wa taasisi ya 'Vodacom Tanzania Foundation' Renatus Rwehikiza alisema kampuni hiyo imekuwa ikijihusisha na mambo mbalimbali ya maendeleo ya kijamii kupitia taasisi ya Vodacom Foundation kwa kuhamasisha na kutekeleza kwa kufadhili pale jamii inapohamasika.

Aidha alisema suala la usafi linalenga maeneo mbalimbali ili kuboresha mazingira na kuwa na afya bora kwa maendeleo ya taifa.

"Kampuni imekuwa ikijihusisha na mambo mbalimbali ya maendeleo ya kijamii kupitia taasisi yake ya misaada kwa jamii ya Vodacom Tanzania Foundation ambayo inagusa elimu, afya,kujikimu, na mazingira katika kutekeleza adhma ya afya kwa mazingira kwani tunahamasisha watu wakihamasika wanatekeleza kwa kuwafadhili, kwasababu usafi ni wa wote,kazini na pahala popote pa kazi ili kuwa na afya bora kwa maendeleo,"alisema Rweikiza

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Mtwara Hassan Simba alisema zoezi la kufanya usafi na kupanda miti litakuwa likitekelezwa kila mwaka mwezi Septemba ikiwa ni moja ya njia ya kuhamasisha jamii juu ya upandaji wa miti na utunzaji wa mazingira.

"Sisi tulianzisha huu utaratibu mwaka jana kwa kushirikiana na Vodacom Tanzania na itakuwa ni zoezi endelevu kwasababu tunapaswa kuelimisha na kuhabarisha jamii, hivyo hatuna budi tukiwa kama wanahabari ni lazima tushiriki pia,alisema Simba.

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara,Halima Dendego(wapili kushoto)akiambatana na Mkuu wa Vodacom Tanzania Foundation,Renatus Rwehikiza(kushoto) Meneja uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu(kushoto kwake)wakifanya usafi katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula, kwa kushirikiana na Chama cha waandishi wa habari cha mkoni humo sambamba na kupanda miti katika maeneo ya wazi ya hospitali hiyo,Zoezi hilo lilidhaminiwa na Vodacom Tanzania. 

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara,Halima Dendego(wapili kushoto aliepiga magoti)pamoja na Mkuu wa Vodacom Foundation,Renatus Rwehikiza wakimshuhudia Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Mtwara,Hassan Simba(kushoto)akimwagia maji mti uliopandwa na Mkuu wa Mkoa huo katika zoezi la kufanya usafi katika hospitali ya rufaa ya Mkoa huo, kwa kushirikiana na Chama cha waandishi wa habari cha mkoa huo sambamba na kupanda miti katika maeneo ya wazi ya hospitali hiyo.Zoezi hilo lilidhamiwa na Vodacom Tanzania.


Mdau wa habari mkoani Mtwara,Taabu Mtingita(kushoto)na Meneja uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu wakizoa taka wakati wa zoezi la kufanya usafi katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula, kwa kushirikiana na Chama cha waandishi wa habari cha mkoni humo sambamba na kupanda miti katika maeneo ya wazi ya hospitali hiyo.Zoezi hilo lilidhamiwa na Vodacom Tanzania.

KAMPUNI YA ASAS IRINGA YAPONGEZWA KWA KUJITOLEA MIRADI YA ZAIDI YA TSH MILIONI 400 HOSPITALI YA MKOA

$
0
0
  Na MatukiodaimaBlog.
SERIKALI  ya  mkoa  wa  Iringa   imepongeza  msaada mkubwa uliotolewa na kampuni ya  Asas  ya  mkoa hapa wa ujenzi wa jengo la  kituo  cha  damu  salama  cha  kisasa na ujenzi wa  jengo la  watoto  wanaozaliwa  njiti katika  Hospitali  teule ya  mkoa  wa  Iringa pamoja miradi  itakayogharimu zaidi ya  Tsh  milioni 400

Katika  taarifa   iliyosomwa na mganga  mkuu  wa  Hospitali ya rufaa ya  mkoa wa Iringa Dr Robert salim wakati wa  hafla ya  uwekaji wa jiwe la msingi   katika miradi hiyo leo  mbele ya mgeni rasmi   mkuu wa  mkoa wa Iringa  Amina Masenza  alisema  kuwa awali  uongozi wa hospitali  hiyo  ulimwandikia  barua  mfanyabiashara    huyo  ili  kusaidia  msaada wa kontena ambalo  lingetumika katika  kituo cha benki ya  damu salama ila mfanyabiashara   huyo alijitolea  kujenga jengo  hilo la  kisasa na kuongeza msaada wa jengo la watoto  wanaozaliwa  njiti .

“Kutokana na agizo la Serikali la kuanzisha Benki za damu salama katika Mikoa..... Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kushirikiana na Mfadhili  Salim F. Abri Mkurugenzi wa Kampuni ya ASAS iliona ni vyema kujenga jengo la Kituo Kidogo cha damu salama katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ili kufikia azma hiyo. ...Hospitali ilimuomba Mfadhili huyo atoe msaada wa “Container” kwa ajili ya shughuli hiyo, lakini Mfadhili kwa kuona umuhimu wa huduma ya damu salama katika Mkoa aliomba apewe ramani ili ajenge kituo hicho badala ya kutumia“Container”.”alisema

Dr Salim alisema  kuwa Hospitali   hiyo kabla ya  mfanyabiashara   huyo  kujitolea  ujenzi wa  jengo  hilo  kituo cha  kidogo  cha damu  salama  ulikuwa  ukitegemea  damu  kutoka  kituo  cha kanda  kilichopo  mkoani  Mbeya  ila  sasa  wataweza  kukusanya  damu  kupitia  kituo  hicho.

Alisema  kuwa lengo la mradi huu ni Kuboresha upatikanaji wa huduma za damu salama katika Mkoa wa Iringa kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya damu salama katika Vituo vya kutolea huduma za afya na kupunguza vifo vya Uzazi, Watoto wachanga, Watoto na Wahanga wa ajali za barabarani na kuwa lengo la Mkoa kwa mwezi ni kukusanya chupa 784 na kwa mwaka ni chupa 9,413 (units).

Hata  hivyo  alisema mahitaji ya damu kwa mwezi katika Mkoa ni chupa 700 (unit) na katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ni chupa 160-200 Units kwa mwezi kuwa tangu kituo kianze kutumika mwezi Februari,2016 Mkoa umekusanya chupa 2,065 (22%) hadi sasa.

“Tunakushukuru mkuu wa mkoa  kwa kukubali mwaliko wetu wa kuwa Mgeni Rasmi katika hafla hii ya kuweka mawe ya msingi katika miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Mfadhili wetu Salim F. Abri Mkurugenzi wa Kampuni ya ASAS ya Iringa. Katika hafla hii fupi tutakuomba uweke jiwe la Msingi katika Mradi wa jengo la Kituo Kidogo cha Damu Salama na Jengo la Wodi ya Watoto wachanga vyote  vikiwa ni  hisani  kutoka kwa mfadhili wetu  Salim F Abri “

Alisema kuwa ujenzi huo  unafanywa namkandarasi anayenga mradi huu ni Buyungu General Enterprise wa Iringa chini ya usimamizi wa  Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ambaye amechangia kuchora ramani za jengo hili na kusimamia mradi mpaka ulipokamilika, mchango wake kama angelipwa ni Tshs.13,939,200.00.

Na kuwa  utekelezaji wa mradi ulianza kutekelezwa mwezi Novemba, 2014 na umekamilika mwezi Agosti, 2015. Jengo limeanza kutumika mwezi Februari, 2016. Pamoja na kujenga jengo hili Mfadhili pia ametoa msaada wa samani, mafriji makubwa 4 ya kutunzia damu na Computer 1 wenye thamani ya Tshs.30,000,000.00.
 
Mkuu  wa  mkoa  wa  Iringa Amina Masenza (kushoto)  akimpongeza Salim Asas   (kulia) mara  baada ya  kuweka  jiwe la msingi katika miradi  mikubwa  miwili iliyofadhili   kampuni ya Asas ukiwemo  mradi wa jengo la  kituo cha  damu  salama Hospitali ya  Rufaa ya  mkoa wa Iringa na jengo la  watoto  wanaozaliwa njiti yote yaliyofadhiliwa kwa zaidi ya Tsh milioni 400  na  kampuni hiyo ya  Asas ya  mkoa wa Iringa(picha na matukiodaimaBlog )
Damu  iliyochangiwa

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

DC ILALA,SOPHIA MJEMA AONGOZA WAFANYABIASHARA KARIAKOO KUCHANGIA WAATHIRIKA NA TETEMEKO LA ARDHI MKOANI KAGERA

$
0
0

1
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema akipokea kiasi cha shilingi milioni zaidi ya milioni 6 kutoka kwa mmoja wa wafanyabiashara wa Kariakoo Bw. Deo Senya wakati Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo (JWK) walipofanya Harambee ya kuchangia waathirika  wa Tetemeko la Ardhi kule Bukoba mkoani Kagera ambapo Mkuu wa wilaya hiyo aliongoza harambee hiyo, Kuliani ni Katibu Tawala wa wilaya ya Ilala Bw. Edward Mpogolo na katikati ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanya Biashara Kariakoo Bw.Philimin Lomano Chonde.

Katika harambee hiyo jumla ya shilingi milioni 13,708,000/= fedha taslimu zilikusanywa na vitu mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni 31564800/= jumla ya michango kwa ujumla ni shilingi milioni 45,672,800/= harambee hiyo leo ilikuwa inazinduliwa rasmi na michango inaendelea mpaka siku ya jumamosi ijayo ambapo ndiyo harambee hiyo itafungwa rasmi na wafanyabiashara mbalimbali wametakiwa kuendelea kuchangia kwa kupitia jumuiya yao ya wafanyabiashara mpaka siku ya jumamosi.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
2
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema akipokeamsaada wa viatu kutoka kwa wafanyabiashara wa kikundi cha Raha Square wafanyabiashara ambao wametoa mchango ubwa sana wa fedha na vitu mbalimbali katika harambee hiyo.
3
Wafanyabiashara wa Raha Square Kariakoo wakikabidhi mcahngo wao wa fedha kwa mkuu wa wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema.huka na vitu vingine mbalimbali katika harambee hiyo. 
10
Mfanyabiashara Mohammed Abdallah Nofa akizungumza mara baada ya kukabidhi mchango wake wa shilingi 500,000/=  kwa Mkuu wa wilaya Ilala Mh. Sophia Mjema wa pili kutoka kulia . katika picha kulia ni Edward Mpogolo Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala na Kushoto ni Katibu wa JWK Bw. Abdallah Mwinyi
11
Wafanyabiashara kutoka Raha Square wakikusanya michango yao ya fedha taslimu na vifaa mbalimbali kabla ya kuvikabidhi leo.
12
Kiongozi wa Wafanyabiashara wauza Simu za mkononi Bw.Stanley Mwakipesile akizungumza machache mara baada ya kukabidhi mchango wao zaidi shilingi milioni 1,500,000 /=kwa mkuu wa wilaya ya Ilala katika Harambee hiyo.
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live




Latest Images