Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live

VODACOM YAKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO VYA TAMASHA LA MZIKI MNENE.

$
0
0
 Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu (katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati kampuni ya Vodacom Tanzania ilipokabidhi vifaa mbalimbali vya michezo kwa ajili ya tamasha la Mziki Mnene litakaloanza kufanyika katika mikoa ya Pwani na Dar es Salaam mwishoni mwa wiki hii. Wengine pichani ni waratibu wa tamasha hilo litakaloendeshwa na kituo cha redio cha Efm, Dennis Busulwa maarufu Ssebo (kulia) na Gerald Hando.
 Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu (kushoto) akionyesha moja ya T-shirt wakati kampuni ya Vodacom Tanzania ilipokabidhi vifaa mbalimbali vya michezo kwa ajili ya tamasha la Mziki Mnene litakaloanza kufanyika katika mikoa ya Pwani na Dar es Salaam mwishoni mwa wiki hii. Wanaoangalia ni  waratibu wa tamasha hilo litakaloendeshwa na kituo cha redio cha Efm, Dennis Busulwa maarufu Ssebo (katikati) na Gerald Hando.
Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu (kushoto) akikabidhi vifaa mbalimbali vya michezo vilivyotolewa na  kampuni ya Vodacom Tanzania kwa ajili ya tamasha la Mziki Mnene litakaloanza kufanyika katika mikoa ya Pwani na Dar es Salaam mwishoni mwa wiki hii. Wanaopokea ni   waratibu wa tamasha hilo litakaloendeshwa na kituo cha redio cha Efm, Dennis Busulwa maarufu Ssebo (katikati) na Gerald Hando.

KATIKA juhudi za kuendeleza sekta ya michezo nchini,Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania leo imekabidhi jezi za michezo kwa Uongozi wa Tamasha la Mziki Mnene na Vodacom ulioandaa tamasha mahusisi kwa timu mbalimbali zitakazoshiriki katika mpira wa miguu wa maveterani katika tamasha hilo katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani wakati wa tamasha hilo lililoandaliwana kituo cha EFM linalotarajiwa kuzinduliwa Jumamosi ijayo chini ya udhamini wa Vodacom Tanzania.
 Akiongea katika hafla ya kukabidhi  kwa uongozi huo,Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu alisema Vodacom Tanzania inafurahi kudhamini tukio hili muhimu lenye lengo la kutoa burudani kwa jamii kupitia tasnia  ya muziki na michezo.

 “Vodacom tunafurahi kushiriki katika tukio hili la kuleta burudani kwenye jamii na ndio maana kampuni imekuwa mstari wa mbele kudhamini  michezo na Sanaa kwa kuwa inaamini kupitia sekta ya michezo watanzania  wengi wanaweza kupata burudani wazipendazo na kupumzisha akili  pia kupitia tamasha hili wananchi  watapata fursa ya kupata na kununua bidhaa mbalimbali za mawasiliano kutoka Vodacom popotelitakalofanyika tamasha hili huduma zetu zitakuwepo na tutaendelea kudhamini  matukio ya burudani kwa ajili ya kuinua vipaji vya Sanaa na michezo kama ambavyo kwa sasa tunavyoendelea kudhamini ligi kuu ya soka ya Tanzania bara na mashindano ya kucheza muziki wa dansi ya Dance 100%  na tuzo za wasanii ya EATV”Alisema.

Akiongea baada ya kupokea vifaa hivyo vya michezo Mratibu wa tamasha hilo,Denis Sebbo amesema kuwa tamasha la muziki mnene mwaka huu, litafanyika kwa kipindi cha muda wa wiki 12  ambapo muziki utapigwa katika baa 12 za Jijini Dar es salaam na Mkoa wa Pwani.
Baadhi ya wasanii ambao watapamba tamasha hilo aliwataka kuwa ni Machupa,Msaga Sumu,Dula Makabila,Easy Man,Khalid Chokoraa,Mc KKoba,Shoz Dear,Peter Msechu,AT,Majid Migoma, Dogo Niga na Rublay.

Alisema tamasha la muziki mnene mwaka huu litaenda sanjari na kampeni ya NJE NDANI ambapo vipindi vinne  mbalimbali vya redio hiyo viratushwa  live  naaliwataka wapenzi wa michezo na burudani kuhudhuria  tamasha hili ambalo ni mwisho wa burudani  na  tayari limeishaanza kuwa gumzo ya jiji.

PSPF WATOA ELIMU YA KUJIUNGA NA MFUKO WA KUJICHANGIA KWA HIARI KWA WANANCHI WASIO KATIKA SEKTA RASMI ZANZIBAR.

$
0
0
Afisa wa PSPF Bi. Faidha Katavi akitowa maelezo jinsi ya kujiunga na Mfuko wa PSPF Kujichangia kwa Hiara Mafao katika mfuko huo.
Afisa wa Idara ya Uvuvi na Maendeleo Zanzibar Ndg Mohammed Chum akitowa maelezo wakati wa mkutano huo na Mfuko wa PSPF kwa Wavuvi wa Zanzibar kujiunga na Mfuko huo.
Waziri wa Uvuvi Mhe Hamad Rashid Mohammed akisisitiza jambo wakati wa kufungua Mkutano wa Wadau Wasiokuwa katika Sekta Rasmin kujiunga na Mfuko wa PSPF kupitia Michango ya Hiara ili kupata fursa mbalimbali zinazotolewa na PSPF kwa Wanchi wa Tanzania.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA: TATIZO LA MAJI SUMBAWANGA KUWA HISTORIA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa inatarajiwa kupata huduma ya maji safi na salama kuanzia mwezi ujao baada ya kukamilika kwa mradi mkubwa wa maji uliokuwa unajengwa.
 
Mradi huo unajengwa kwa usimamizi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira, Manispaa ya Sumbawanga (SUWASA), kwa ufadhili wa nchi za Umoja wa Ulaya (EU) na Serikali ya Ujerumani kupitia benki yake ya Maendeleo (KfW), sh. bilioni 31 utakapokamilika.

Waziri Mkuu alitoa kauli hiyo jana  (Jumatano, Agosti 24, 2016) wakati na akiweka jiwe la msingi la mradi wa maji safi na usafi wa mazingira katika Manispaa ya Sumbawanga na kuitaka kampuni ya kampuni ya Techno Fab Gammon Joint Venture ya India kumaliza ujenzi wa mradi huo haraka iwezekanavyo.

Alisema mradi huo ambao tayari umekamilika kwa asilimia 85 unatarajiwa kukamilika Septemba mwaka huu, hivyo aliwataka wananchi kuhakikisha wanashirikiana na Manispaa katika kulinda miundombinu ya mradi huo mara utakapokamilika pamoja na kutunza vyanzo vya maji.

“Pamoja na Serikali kutumia fedha nyingi kwa ajili ya kugharamia miradi ya maji inayojengwa katika maeneo mbalimbali nchini,changamoto ya upatikanaji wa huduma hiyo imekuwa kubwa kutokana na baadhi ya visima vimeanza kukauka hali inayosababishwa na uharibifu wa mazingira,” alisema.

Alisema kumekuwa na uvamizi mkubwa katika maeneo ya vyanzo vya maji ambapo wananchi wanajishughulisha na shughuli za ulimaji, uchungaji wa mifugo, ujenzi wa nyumba za makazi na uchomaji misitu hivyo kusababisha uchafuzi wa mazingira na hatimaye vyanzo hivyo hukauka.

Kufuatia hali hiyo Waziri Mkuu amewaagiza wakuu wote wa wilaya na wenyeviti wa vijiji nchini kuyasimamia maeneo yenye vyanzo vya maji na kuwaondoa watu wotewalioyavamia kwa kuwachukulia hatua kali za kisheria pamoja na kuwafikisha mahakamani.

Naye Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe ambaye alimuwakilisha Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge katika hafla hiyo alisema aliishukuru Serikali ya Ujerumani na Umoja wa nchi za Ulaya kwa kufadhili mradi huo.

Hata hivyo Mhandisi Kamwelwe alisema suala la kuhifadhi mazingira ni msingi endelevu wa upatikanaji wa maji safi na salama, hivyo aliwaomba wananchi kujiepusha na uchafuzi wa vyanzo vya maji na uharibifu wa mazingira ili kuepuka athari ya Taifa kukubwa na janga la ukame.

“Wananchi wanatakiwa kuacha kufanya shughuli za maendeleo ikiwemo kulima, kufuga ndani ya mita 60 kutoka katika mito, maziwa na vyanzo vingine vya maji ili kuepusha uharibifu wa mazingira ambao madhara yake ni makubwa kwa viumbe wote,” alisema.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

ALHAMIS, AGOSTI 25, 2016

JESHI LA POLISI ZANZIBAR KUPAMBANA NA WANAOTUMIA KAZI ZA WASANII BILA YA LESENI YA HAKIMILIKI

$
0
0

Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamdani Omar Makame akizungumza na wandishi wa habari kuhusu wajibu wa Jeshi la Polisi katika usimamizi wa kazi za wasanii, hafla hiyo imefanyika Makao Makuu ya Polisi Kilimani Zanzibar. Picha na Mkame Mshenga/Maelezo Zanzibar.

Jeshi la Polisi Zanzibar limedhamiria kupambana na uharamia wa kazi za hakimiliki kwa kudhibiti maeneo ya uingizaji hakimiliki haramu katika maeneo ya bandarini na uwanja wa ndege .

Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamdani Omari amesema hayo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari huko Makao Makuu ya Polisi Zanzibar kuhusu usimamizi na wajibu wa Jeshi la Polisi katika usimamizi wa hakimiliki .

Amewataka wananchi kuelewa kwamba kutoa kopi ,kuuza vinasa sauti na picha za kieletroniki vikiwemo CD,DVD na vyenginevyo bila ya leseni ya hakimiliki ni miongoni mwa makosa ya jinai.

Aidha alisema kutumia hakimiliki biila ya ridhaa ya mwenye haki kama vile kurudufu kusambasa na kuonyesha kazi kwa umma ama kuibadilisha kazi na kuwa kwa mtindo mwengine ni kosa kwa mujibu ya sheria ya hakimiliki No. 14 ya mwaka 2003.

Amesema hakimiliki ni mali ya anaemiliki ,ni kazi yake inaestahili ulinzi kwani kuitumia bila ya ridhaa ya mwenye haki ni kosa kisheria

Katika kusimamia sheria ya hakimiliki Jeshi la Polisi limetoa taaluma kwa askari wake wakiwemo makamanda wa mikoa yote ya Zanzibar katika mwaka 2008 -2009 ofisi ilianzisha kikundi kazi cha hakimiliki .

Alieleza kuwa jumla ya polisi 100 wa Unguja na Pemba walipatiwa mafunzo ya utambuzi wa makosa ya hakimiliki kupitia mtalamu wa utambuzi wa jinai za hakimiliki SP Omar Muwowo kutoka jeshi la polisi Zambia na Interpol.

Kamishna huyo alieleza kuwa Jeshi la Polisi lilifanikiwa kupambana na uharamia wa hakimiliki kwa kushirikiana na Afisi ya hakimiliki kufanya ukaguzi katika maeneo yote ya Unguja na kukamata nakala haramu za vinasa sauti na picha vya kielektroniki vikiwemo CD , DVD‘S na MP3 zenye uzito wa tani mbili . Aidha alisema nakala haramu hizo ziliangamizwa kwa kushirikiana na Idaraya Mazingira Zanzibar . 

Article 24

Article 23

MIILI YA ASKARI WALIOUAWA NA MAJAMBAZI YAAGWA LEO JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0

 Waziri wa  Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, akipita kutoa heshima za mwisho mbele ya majeneza yaliyobeba  miili ya askari waliouawa baada ya kuvamiwa na majambazi    katika eneo la Mbande, Temeke ,bada hiyo ya kuaga miili ilifanyika katika viwanja vya polisi  vilivyopo barabara ya Kilwa,jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Ernest Mangu, akizungumza wakati wa maombolezo na kuaga miili ya askari waliouawa katika eneo la Mbande, Temeke baada ya kuvamiwa na majambazi.Ibada hiyo ya kuaga  ilifanyika katika Viwanja vya  polisi vilivyopo barabara ya Kilwa,jijini Dar es Salaam.
 Naibu Waziri wa   Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni , akitoa mkono wa pole kwa mmoja wa ndugu wa  askari waliouawa baada ya kuvamiwa na majambazi  katika eneo la Mbande, Temeke ,ibada hiyo ya kuaga miili  ilifanyika katika Viwanja vya Kambi Kuu ya Polisi iliyopo barabara ya Kilwa,jijini Dar es Salaam.
(Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)
IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.

WASANII WAPENDA AMANI WAUNGANA KUPINGA MAANDAMANO YA UKUTA.

$
0
0
 Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Wasanii wapenda Amani nchini, Asha Baraka akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya tamko lao la kuungana pamoja kupinga Maandamano ya UKUTA, Septemba 1.  
Mwenyekiti wa Umoja huo, Steven Mengere (Steve Nyerere) akizungumza juu ya kupinga maandamano ya UKUTA yanayotarajiwa kufanyika  Septemba Mosi kote nchini.
Mwanamziki na Malkia wa Nyimbo za Taarab, Khadija Kopa akizungumza katika mkuatano wa Kupinga maandamano ya UKUTA jijini Dar es Salaam leo.
Mwanamuziki wa Bendi ya Twanga Pepeta, Ally Choki akizungumza katika Mkutano wa Kupinga maandamano ya UKUTA jijini Dar es Salaam leo.

WASANII mbalimbali wanaopenda amani wameungana kwa pamoja kupinga maandamano ya UKUTA yanayotarajiwa kufanyika Septemba Mosi, mwaka huu.
Akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari, Mwenyekiti wa Wasanii hao wapenda amani, Steve Nyerere amesema hamna haja ya maandamano bali tunahaja ya kufanya kazi hususan kwa vijana.
"Vijana ndio muhimili mkubwa kulinda amani ya nchi,tusiwaze maandamano bali tuwaze je Akinamama na Watoto wanapata huduma hospitali"alihoji Steve Nyerere.
Kwa Upande wa Makamu Mwenyekiti wa Wasanii hao, Asha Baraka amesema wameamua kupaza sauti zao kwa niaba ya Wasanii wote wanaopenda amani.
Amesema Tanzania ni nchi ya Amani sio nchi ya vita hivyo wanapofanya shughuli za UKUTA shughuli zote za kijamii zitasimama.
Hatahivyo ameomba Septemba 1,  UKUTA wasimamishe maandamano hayo, pia watafute njia muafaka ya kuweza kuongea Vyama kwa Vyama na wakapata muafaka ili nchi iweze kwenda mbele. 

DIRA YA DUNIA ALHAMISI 25.08.2016

SOMO LA MITANDAO: UHALIFU MTANDAO NA ATHARI KIUCHUMI

$
0
0
 Yapo maeneo mengine ambayo yanaweza kuathiriwa vibaya na uhalifu mtandao – UCHUMI, ni moja ya eneo muhimu ambalo wahalifu mtandao wanaweza kuliletea athari. Aidha, Unapotazama kinacho wapelekea wahalifu mtandao kufanya uhalifu moja wapo ni kujipatia fedha.

Ni wazi kua Raisi wa awamu ya Tano ana pambana kwa dhati kuhakiki wa Tanzania wanaondokana na umasikini ulio kithiri ambapo anaendelea kuchukua jitihada na hatua mbali mbali hadi sasa.

Mfano: Kumekua na uhimizaji mkubwa wa ukusanyaji wa kodi ki elektriniki – Kwa njia ya mtandao ambapo amesisitiza anataka aone TEHAMA inatumiwa vizuri katika eneo hili ili kuhaliki hakuna upotevu wa pesa katika ukusanyaji wa kodi Nchini.

Aidha, Mabenki yameendelea kuboresha mifumo ya Kimtandao kuhakiki miamala inafanyika zaidi kupitia mtandao na nikitolea mfano, mabenki Nchini yamekua yaki hamasisha huduma mtandao kama vile (Huduma za kifedha kupitia simu, kutumia kadi zetu kufanya manunuzi pamoja na matumizi ya mashine za kutolea fedha “ATM”)

Makampuni ya simu nayo hayajakubali kubaki nyuma – Yame hakiki yanaingiza huduma inayoshika kasi zaidi Nchini ya kuweza kufanikisha miamala ya kifedha kupitia simu zetu (Mobile money) ambapo wana nchi wengi wameendelea kuona huduma hizi ni rahisi na wengi wanazitumia.
Maeneo mengine nayo yameona huu ndio muelekeo – Mabasi ya mwendo kasi yamehamasisha miamala kufanyika kwa kadi, huku ulipaji wa bili mbali mbali nao kuendelea kufanyika kupitia mitandao.

Hali hii ni nzuri sana – Kitendo cha mtu kuweza kufanya miamala ya kifedha bila kuhangaika kutoka shemu moja kwenda nyingine kunapelekea uokoaji wa muda na kuongeza ufanisi kwa tunayo yafanya. LAKINI – Je, Upande wa pili wa shilingi, kuna jitihada zozote tumechukua kuangazia? Hapa nazungumzia wahalifu mtandao ambao pia wana uwezo mkubwa wa kupelekea upotevu mkubwa wa pesa tunazozizungusha mitandaoni.

The Sebastian Kolowa Memorial University (SEKOMU) in Tanga invites you

$
0
0
SEKOMU WELCOMES YOU TO JOIN  IN ITS DIFFERENT ACADEMIC PROGRAMS THE UNIVERSITY OFFERS. THE  COURSES RANGE FROM MASTERS  TO CERTIFICATE LEVEL.  IT HAS A MAIN CAMPUS AT MAGAMBA LUSHOTO AND TWO CENTERS AT BUMBULI LUSHOTO AND TANGA.

COURSES OFFERED BY THE UNIVERSITY:
 *MASTER OF EDUCATION IN SPECIAL EDUCATION 
* MASTER OF ART IN DIACONIC MANAGEMENT
 *BACHELOR OF LAW BACHELOR OF EDUCATION SPECIAL NEED (SCIENCE SUBJECTS) 
*BACHELOR OF EDUCATION SPECIAL EDUCATION NEEDS (ARTS SUBJECTS) 
*BACHELOR OF SCIENCE IN ECO TOURISM AND NATURE CONSERVATION 
 *BACHELOR OF SCIENCE IN MENTAL HEALTH AND REHABILITATION 
 *BACHELOR OF SCIENCE WITH EDUCATION DIPLOMA IN BUSINESS ADMINISTRATION 
* DIPLOMA IN FINANCE AND ACCOUNTANCY 
 *DIPLOMA IN COMPUTING, INFORMATION AND COMMUNICATION TECHNOLOGY 
* DIPLOMA IN THEOLOGY 
*DIPLOMA IN PRIMARY EDUCATION (NTA LEVEL 5) 
*DIPLOMA IN PRIMARY EDUCATION (NTA LEVEL 4) 
*ORDINARY DIPLOMA IN CLINICAL MEDICINE 
*TECHNICIAN CERTIFICATE IN CLINICAL MEDICINE
 *BASIC TECHNICIAN CERTIFICATE IN COMMUNITY HEALTH  
*CERTIFICATE IN LAW 
 *CERTIFICATE IN BUSINESS ADMINISTRATION 
 *CERTIFICATE IN FINANCE AND ACCOUNTANCY 

 For more information call 
0788-637635, 0757-432268

MAGAZETI YA LEO AGOSTI 26

Kamati ya Bunge ya TAMISEMI watembea UDART jijini Dar leo

$
0
0
Baadhi ya Wabunge wa Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa wakiwa kwenye mabasi ya mwendokasi, ikiwa ni sehemu ya ziara yao ya kutembelea mradi wa Mabasi hayo (Udart) leo Jijini Dar es salaam.
Wabunge hao wakiwa kwenye Basi.
Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa wakipata maelezo juu mfumo wa mabasi ya mwendokasi katika ofisini za Udart jangwani Jijini Dar es salaam leo.

Tahadhari ya msanii nguli wa Bongo movies, GABO ZIGAMBA, kuhusu matapeli wanaotumia jina lake

$
0
0
Msanii nguli wa Bongo Movies, Gabo Zigamba, anatoa tahadhari kuhusu matapeli mbalimbali wanaotumia jina lake. Awali, msanii huyo alipoteza simu mbili za mkononi, ambazo baadaye zilikuwa zikitumiwa na matapeli hao kuomba misaada kwa watu mbalimbali wakijifanya kuwa wao ndio Gabo.
Kadhalika, majuzi, akaunti ya Facebook ya msanii huyo ilidukuliwa na ikatumika kwa muda na matapeli hao kwa kujifanya wao ndio msanii huyo. Hatimaye alifanikiwa kuirejesha akaunti hiyo katika himaya yake.
Gabo ameeleza kuwa anahisi kuwa yeye ndio msanii anayeongoza kwa jina lake kutumiwa na matapeli kwa sababu amekuwa akipata taarifa mbalimbali kuhusu watu wanaotumia jina lake, kwa mfano binti mmoja aliyejifanya ndiye Gabo na amekuwa akitapeli kwa kudai anauza mabegi.
Msanii huyo ametoa wito kwa Watanzania kuwa makini na watu wanaotumia majina ya watu wengine, hususan watu maarufu, kwa minajili ya kutapeli. Amesema kuwa yupo katika mchakato wa uzinduzi mpya wa akaunti zake mbalimbali za mitandao ya kijamii ili, pamoja na sababu nyingine, iwe rahisi kwa watu kuwasiliana nae pindi wanapokumbana na matapeli hao wanaotumia jina lake.

PSPF YAKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA JESHI LA MAGEREZA UKONGA JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 
Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Abdul Njaidi, (kushoto), akimkabidhi seemu ya vifaa vya michezo, Mkuu wa Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Rajabu Nyange Bakari, Agosti 25, 2016. Vifaa hovyo ni vya michezo ya ngumi, mpira wa miguu na mpira wa pete. 

MFUKO wa Pensheni wa PSPF, umekabidhi vifaa vya michezo kwa wanamichezo wa Jeshi la Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam na kasha kufuatiwa na PSPF bonanza la michezo ya mpira wa miguu, mpira wa pete, Ngumi na Judo. 


Akikabidhi vifaa hivyo vya michezo Agosti 25, 2016, Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko huo, Abdul Njaidi, alisema, PSPF imeamua kutoa vifaa hivyo ili kuunga mkono juhudi za serikali katika kuinua michezo nchini. 

“Nyinyi mkiwa kama sehemu kubwa ya wanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, tunayo furaha kutoa vifaa hivi vya michezo kwani baada ya kutekeleza majukumu mazito ya kitaifa mnahitaji kushiriki michezo ili kujenga afya lakini pia kuinua vipaji vyenu,” alisema na kuongeza, 


“Nichukue fursa hii kuwahamasisha mjiunge na PSPF kwani kuna faida nyingi mtapata kutokana na kutoa mafao mbalimbali yatakayoboresha maisha yenu kama ambavyo kauli mbiu yetu inavyosema, PSPF ni chaguo lako sahihi na kamwe hutajutia uamuzi wako wa kujiunga na Mfuko huu.” Alisisitiza Njaidi. 


Akipokea vifaa hivyo kwa niaba ya wanamichezo hao, Mkuu wa Kikosi Maalum cha Magereza-Ukonga, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Rajabu Nyange Bakari, aliishukuru PSPF kwa msaada huo wa vifaa vya michezo kwani vitawawezesha wanamichezo hao kushiriki michezo katika mazingira bora ya kiuanamichezo. 

Baada ya makabidhiano hayo, wanamichezo hao walionyesha uwezo wao katika michezo ya mpira wa miguu, ngumi, mpira wa pete, na judo. 
Afisa Masoko wa PSPF, Magira Werema, (kushoto), akimkabidhi sehemu ya vifaa hivyo, Mkuu wa Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Rajabu Nyange Bakari. NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID
Afisa Matekelezo (Compliance), wa PSPF, George Mnasizu, (kushoto), akigawa vipeperushi vyenye maelezo ya kina ya huduma zitolewazo na Mfuko huo kwa baadhi ya wanamichezo wa Jeshi la Magereza.
Njaidi akiwa na Mkuu wa Kikosi hicho, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Kikosi Maalum cha Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam, Rajabu Nyange Bakari, na wacheza judo wa kikosi hicho wakiwa katika picha ya pamoja na vipeperushi vya PSPF.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

MBEYA CITY KUWAFUATA TOTO AFRIKANS, KUKIPIGA KIRUMBA JUMAPILI HII

$
0
0
Mlinda mlango mahiri Owen Chaima (pichani juu) ni mmoja wa nyota wa kikosi cha Mbeya City Fc kinachondoka leo hapa mjini Shinyanga kuelekea Mwanza tayari kwa mchezo mwingine wa ligi kuu ya soka Tanzania bara dhidi ya wenyeji Toto Africans uliopangwa kuchezwa jumapili hii kwenye uwanja wa CCM Kirumba.

Mapema asubuhi hii meneja wa kikosi hiki Godfray Katepa amesema maandalizi yote kuelekea mchezo wa jumapili tayari yamekalika kinachosubiriwa sasa ni dakika 90 za uwanjani siku hiyo ya mchezo ambazo anaamini zitakamilika kwa City kuibuka na ushindi na kubeba pointi tatu muhimu kabisa ambazo zitaisukuma timu yake kwenye nafasi nzuri katika msimamo wa ligi.

“Hakika tumekamilisha kila kitu kuhusu mchezo huo, hii ina maana kuwa maandalizi yote kwa vijana wetu yamekenda sawa, baada ya suluhu na Kagera Sugar tuliendelea kubakia Shinyanga lengo letu lilikuwa ni kupata wasaa mzuri wa kufanya mazoezi kwa utulivu, hilo lilifanikiwa tumefanya mazoezi ya kutosha kwenye uwanja wa Kambarage, kwa sababu tunakwenda mwanza leo tutakuwa na siku moja nyingine ya mazoezi ccm kirumba, hivyo basi hakuna shaka kuwa tuko kamili na tayari kwa mchezo wa jumapili”.
Kuhusu hali za wachezaji, Katepa aliweka wazi kuwa nyota wote wako kwenye hali nzuri kwa sababu hata baada ya mchezo na Kagera Sugar hakukuwa na majeraha yeyeto kikosini hivyo uhakika wa kucheza kwa kiwango cha juu na kushinda mchezo huo ni mkubwa kutokana na uimara wa wa chezaji hivi sasa.

“Timu yetu imeimarika zaidi, hatuna shaka na kupata ushindi dhidi ya Toto, vijana wako ‘fiti’ hakukuwa na majeruhi yeyote hata baada ya mchezo uliopita pamoja na mazoezi mazito ya siku kadhaa, tunasaifiri kwenda mwanza leo kwa lengo moja tu la kushinda ikiwezekana kwa idadi kubwa ya mabao”

JACQUELINE MENGI AUNGA MKONO JUHUDI ZA JPM KWA KUKARABATI NA KUNUNUA VITABU VYA MAKTABA

$
0
0


Kwa kutambua umuhimu wa elimu kwa kizazi cha sasa na baadae, Jacqueline Mengi kupitia Taasisi yake ya Dk. Ntuyabaliwe ameamua kuunganisha nguvu kwa serikali ya awamu ya tano iliyo chini ya Rais Magufuli kwa kusaidia kuboresha upatikanaji wa elimu bora kwa kufanya marekebisho ya maktaba katika shule ya msingi Kinondoni.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo ambao uliambatana na uzinduzi wa Taasisi ya Dk. Ntuyabaliwe, Jacqueline amesaidia kufanya ukukarabati wa maktaba katika shule hiyo na kuweka vitabu ikiwa ni sehemu ya kumkumbuka baba yake Dk. Ntuyabaliwe kutokana na kupenda kwake kusoma vitabu.

  Afisa Elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Raymond Mapunda akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa maktaba ya Shule ya Msingi Kinondoni jijini Dar es Salaam.  Wanaoshuhudia tukio hilo ni Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi (katikati) pamoja na Diwani wa Kata ya Mwananyamala, Songoro Mnyonge.

Alisema baba yake alikuwa akiamini zaidi katika vitabu hivyo alipenda hata watoto wake wasome vitabu na anachokifanya yeye kwa sasa ni kuendeleza juhudi ambazo alikuwa akiifanya baba yake ya kuona watu wakisoma vitabu na matarajio yake ni kuona vitabu hivyo vikiwasaidia wanafunzi wa shule hiyo kuwaongezea uwezo wa kufaulu katika masomo yao ya darasani.

"Ndoto yangu ya muda mrefu leo imetimia, kila mtu ambaye alikuwa akimfahamu baba yangu Dk. Ntuyabaliwe alikuwa akifahamu kuwa alikuwa anapenda vitabu na hata sisi alituzoesha kusoma vitabu na hata kuanzishwa kwa taasisi hii ni sehemu ya kumkumbuka yeye.

  Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi akimwonyesha baadhi ya vitabu Afisa Elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Raymond Mapunda vinavyopatikana katika maktaba hiyo.

"Naamini kuwa usomaji wa vitabu unaweza kumsaidia mtu kufika mbali hata kama sio katika elimu unaweza kumsaidia kwa jambo lingine hata katika maisha ... ndoto yangu ni kuona watanzania wote wanapenda kusoma kama baba yangu alivyokuwa anapenda kusoma vitabu," alisema Jacqueline.

Nae mgeni rasmi katika shughuli hiyo, Afisa Elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Raymond Mapunda alisema sio jambo rahisi serikali kuweza kumaliza changamoto zote zilizopo na kupitia watu wenye moyo kama wa Jacqueline ambao wanaunga mkono juhudi za serikali kunaweza saidia upatikanaji wa elimu bora.

 Mkurugenzi wa Dr.Ntuyabaliwe Foundation na Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi (wa pili kushoto) akiwa ameongoza na Afisa Elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Raymond Mapunda (kushoto), Diwani wa Kata ya Mwananyamala, Songoro Mnyonge (wa tatu kushoto) pamoja na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kinondoni, Emmanuel Ntenga mara baada ya kuwasili shuleni hapo.

Alisema kupitia maktaba hiyo anaamini ipo siku kutatokea mtu ambaye atakuwa na msaada kwa Tanzania ambaye wakati akisoma alikuwa akitumia maktaba ambayo imefanyiwa ukarabati na Jacqueline Mengi.

"Nimeona hali ambayo ilikuwa awali katika eneo hili na niseme tu Jacqueline atakuwa na yeye aliguswa na hali hiyo na nitumie fursa hii kumshukuru sana kwa msaada ambao ameutoa, shule inatakiwa kutoa elimu bora lakini ili kufikia malengo hayo kunahitajika kuwe na nyenzo za kutosha ambazo zitasaidia malengo ya kielimu kufikiwa," alisema Mapunda.
Mkurugenzi wa Dr.Ntuyabaliwe Foundation na Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi na uongozi wa shule hiyo kwa pamoja wakiimba na wanafunzi wa shule ya Msingi Kinondoni.

Kwa upande wa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kinondoni, Emmanuel Ntenga alimshukuru Jacqueline Mengi kwa msadaa wa kukarabati maktaba ya vitabu ili wanafunzi kujisomea, maktaba ambayo awali hawakuwahi kuwa nayo.


"Tunakushukuru sana kwa maktaba hii sasa wanafunzi wataweza kujisomea, tunafahamu juhudi za Dk. Mengi katika kusaidia elimu kwa kutoa madawati sasa na wewe umemuunga mkono tunawashukuru kwa hilo," alisema Ntenga.

JARIDA LA WIZARA YA NISHATI NA MADINI TOLEO NA. 134

MKUTANO WA TICAD KUFANYIKA AFRIKA KWA MARA YA KWANZA

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Kenya, Balozi Monica Juma (mwenye nguo ya kijani) akifuatiwa na Bw. Takeshi Osuga, Balozi wa TICAD kutoka Japan na Mhe. Cherif Mhamat Zene, Balozi wa Chad, Ethiopia wakiongoza moja ya vika vya Maafisa Waandamizi ikiwa ni maandalizi ya Mkutano wa Sita wa TICAD. 
Mkutano wa 6 wa Kimataifa kuhusu Ushirikiano wa Maendeleo kati ya Japan na Afrika (Tokyo International Conference on African Development-TICAD VI) unatarajiwa kufanyika tarehe 27 na 28 Agosti, 2016 Jijini Nairobi, Kenya. Hii ni mara ya kwanza kwa mkutano huu kufanyika nje ya Japan tangu kuanzishwa kwake mwaka 1993.


Mkutano huu wa Sita ambao umetanguliwa na kikao cha Maafisa Waandamizi wakiwemo Makatibu Wakuu na Mabalozi tarehe 24 na 25 Agosti, 2016 utafuatiwa na kikao cha Mawaziri tarehe 26 Agosti, 2016 unatarajiwa kupitisha Azimio la Nairobi ambalo litajikita katika kushughulikia changamoto mbalimbali zinazolikabili Bara la Afrika katika kufikia maendeleo na ustawi.


Changamoto hizo ni pamoja na kuporomoka kwa bei za bidhaa zinazotegemewa na nchi za Afrika katika ustawi wake kama vile mafuta, gesi na madini na hivyo kupelekea kuathirika kwa ukuaji wauchumi katika nchi nyingi za Afrika; kulipuka kwa magojwa kama Ebola na kusababisha vifo vilivyopelekea kusitishwa kwa shughuli za kiuchumi na kupotea kwa nguvu kazi; na Kuongezeka kwa vitendo vya ugaidi.

Agenda nyingine zitakazojadiliwa ni pamoja na: Kuhamasisha mageuzi ya kiuchumi kupitia uendelezaji wa viwanda; Kuboresha sekta ya Afya kwa maisha bora na Kusaidia jitihada za kudumisha amani na utulivu katika jamii.


Vile vile Mkutano huu umetoa kipaumbele kwa ushiriki wa sekta binafsi hususan wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Japan na Afrika. Hivyo mkutano utatoa fursa kwa taasisi zenye dhamana ya kuvutia uwekezaji, biashara na utalii nchini kutangaza fursa zilizopo kwa kampuni za Japan.


Mkutano huu wa 6 wa TICAD ambao unashirikiana kwa karibu na Kamisheni ya Umoja wa Afrika unalenga kuiwezesha Afrika kujitegemea katika kukua na kufikia maendeleo yaliyokusudiwa ikiwemo utekelezaji wa Agenda 2063 ambayo viongozi wa Afrika walikubaliana wakati wakuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika. Agenda 2063 inalenga kuliunganisha Bara la Afrika katika masuala ya kukuza uchumi; kuhamasisha utawala bora na utawala wa sheria; kuhakikisha maendeleo kwa mtu mmoja mmoja; kuhakikisha amani na usalama unaimarika na kuiweka Afrika kwenye nafasi ya mchangiaji mkuu wa uchumi duniani.


Mkutano wa kwanza wa TICAD uliofanyika Jijini Tokyo mwaka 1993 ulijikita zaidi katika agenda ya kuongeza misaada kwa nchi za Afrika. Kufuatia mkutano huo misaada ya Japan kwa nchi za Afrika iliongezeka kutoka Dola za Marekani bilioni 0.6 mwaka 1993 na kufikia Dola bilioni 0.8 mwaka 1998. Hadi kufikia mwaka 2013 msaada wa Japan (ODA) kwa nchi za Afrika ulifikia Dola za Marekani bilioni 2.8.


Mkutano wa 6 wa TICAD ambao kwa mara ya kwanza katika historia unafanyika Afrika utawezesha majadiliano ya ana kwa ana kati ya Wakuu wa Nchi na Wawakilishi kutoka Sekta binafsi.


Kadhalika, mbali na mwenyeji wa Mkutano huu ambaye ni Rais wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta mkutano utahudhuriwa pia na Waziri Mkuu wa Japan, Mhe. Shinzo Abe, Viongozi Wakuu kutoka nchi 54 za Afrika pamoja na wawakilishi kutoka mashirika ya kimataifa na makundi mbalimbali.


Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huu utaongozwa na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa.

TEEC kuzinduliwa rasmi Agosti 27.

$
0
0
Na Ally Daud-Maelezo

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira, Kazi, vijana na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama anatarajia kuzindua rasmi Taasisi yenye jukumu la kuboresha ubunifu na ushindani wa kibiashara katika sekta binafsi (TEEC).

Akizungumza na Waandishi wa habari jijini Dar es salaam Mkurugenzi Mtendaji TECC, Bw. Sosthenes Sambua amesema kwamba sambamba na uzinduzi huo, leo taasisi hiyo itaendesha kliniki ya biashara katika viwanja vya Mlimani City leo.

“Mbali na Uzinduzi wa TEEC leo kutakuwa na maonesho ya wajasiriamali katika viwanja hivyo na kutakuwa na kliniki ya biashara kutoka kwa taasisi 15 zitakazotoa ushauri na ujuzi kwa vijana wanaotaka kujiajili bila malipo siku nzima” alisema Bw. Sambua.

Aidha Bw. Sambua amesema kuwa TECC ni kuimarisha ubunifu na ushindani wa biashara ndogo na za kati za Tanzania kwa kuwavuta wajasiriamali waliopo ndani ya sekta isiyo rasmi, wahitimu wa vyuo na wengine wenye kutaka kuanzisha biashara zinazoongeza thamani kwa mazao ya Tanzania na kutengeneza bidhaa kwa maendeleo ya nchi.

Mbali na hayo Bw. Sambua alisema kliniki hiyo itakuwa ni fursa ya kukutana na wataalamu kwenye nyanja za ujuzi, mitaji, kodi, usajili, leseni, viwango, mitandao ya biashara na malezi miongoni mwa wataalamu wengine.

Taasisi hii imeundwa kwa pamoja na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) na Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH).

Kwa upande wa Katibu Mtendaji wa NEEC, Bi. Beng’i Issa alisema ushirikiano wa COSTECH na TPSF katika kuunda TECC unaendana na sera ya baraza hilo linalotaka kuona watanzania wanamiliki sehemu kubwa ya uchumi wao kwa kuwafanya kuwa washiriki. 

“Tunatambua umuhimu wa sayansi, teknolojia na ubunifu katika kuwainua wajasiriamali wadogo na wa kati ili waweze kuzalisha bidhaa na kutoa huduma bora, kuwa washindani kimataifa ili kufikia dira ya taifa ya maendeleo 2025,” alisema Bi. Issa.

Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF, Bw. Godfrey Simbeye aliwataka watanzania kujitokeza kwa wingi leo ili kufaidika na kliniki hiyo ya biashara kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi kwa jamii na Tanzania kwa ujumla.
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live




Latest Images