Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110171 articles
Browse latest View live

NHC YASAIDIA UPATIKANAJI WA NYUMBA ZA WATUMISHI WA SERIKALI WANAOHAMIA DODOMA

$
0
0
1
Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba NHC Bw. Nehemia Mchechu akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya shirika hilo Upanga jijini Dar es salaam kuhusu wadaiwa sugu wa pango katika shirika hilo moja ya wadaiwa waliotajwa ni Jengo la Club Billicanas ambali linadaiwa Bilioni moja, Kulia ni Meneja Mauzo wa NHC Bw. Itandula Gambalagi na katikati ni Muungano Saguya Meneja katika ofisi ya Mkurugenzi.
2
Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba NHC Bw. Nehemia Mchechu akisisitiza jambo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya shirika hilo Upanga kushoto ni Hamad Abdalla Mkurugenzi wa Miliki NHC na katikati ni Suzan Omari Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano NHC. Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA

DTB BANK ZANZIBAR BRANCH DONATES 40 CHAIRS TO AGHAKHAN FOUNDATION MADRASA IN ZANZIBAR

$
0
0
Diamond Trust Bank Tanzania (DTB) donated 40 classroom chairs to the Agha Khan Foundation (AKF) Madrasa Early Childhood Program in Stone Town, Zanzibar yesterday.

Aim was to support the Government efforts in education improvement in Zanzibar.

The centre caters for students from underprivileged families in Unguja Island.

In the centre, Students also taught both religious education and Tanzanian syllabus under National Examination Council of Tanzania (NECTA).
Diamond Trust Bank Tanzania (DTB) Zanzibar Branch, Head of Finance, Shahr Mohammed (Second Left) handover classroom chairs to Program Director of Agha Khan Foundation (AKF) Madrasa, Early Childhood Program, Mr. Khamis Said Abdallah during a short ceremony held in Zanzibar yesterday. The bank donated 40 classroom chairs to the Institution, where students from underprivileged familias in Unguja Island are taught both religious education and Tanzanian syllabus under National Examination Council of Tanzania (NECTA). Looking on are the bank’s and the centre's staff.

MAGAZETINI LEO ALHAMISI AGOSTI 25

DIPLOMATIC PROTOCOL TRAINING BY AMB. CHARLES SANGA ON 10 SEPT

$
0
0
ECONOMIC DIPLOMACY - TRAINING ACADEMY 

DIPLOMATIC LECTURE SERIES ANNOUNCEMENT ON: 
Diplomatic Protocol 

Date: 10th September 2016 

1.0 Introduction 

The Economic Diplomacy ñTraining Academy and Economic Diplomacy Consultants Bureau specifically, is registered firm and run independently. The bureau was established with the aim of coordinating the use of expertise and other resources to contribute effectively to the industrial and Socio-economic development of Tanzania. Emphasis is placed on providing complete, comprehensive and integrated consultancy services and Diplomatic Training. 

Through our Diplomatic MasterClass training Courses, Diplomatic Training short courses and Executive tailor-made Diplomatic training Programmes as well as outreach programs, the Academy promotes interest in and understanding of the indispensability of diplomacy to the most challenging problems facing our foreign and national security interests, committed to be the best knowledge partner our clients can find for their quality diplomatic training need for mutually sustainable social economic development. 

The Economic Diplomacy ñTraining Academy offers professional expertise and a deep wealth of knowledge about International Relations and Economic Diplomacy. Building upon over a decade of experience delivering focused, relevant, competence needs-based training, our expertise is used to create in-house customized and executive training programmes that support our clients. In every training program, facilitation is always led by our team of senior academicians and Ambassadors, career Diplomats and experts to create competence -based effective, scalable, and engaging learning solutions. 

DIPLOMATIC LECTURE SERIES are monthly lecture series, mainly focused on ECONOMIC DIPLOMACY, and facilitating speakers are AMBASSADORS and CAREER DIPLOMATS. It is in this ground that, the Economic Diplomacy ñTraining Academy is announcing Septemberís lecture on the Diplomatic Protocol, Which will be delivered by Ambassador Charles Asilia Sanga. 

1.1 Justification and Rationale of the Diplomatic Protocol lecture 

To manage Protocol related duties and functions, there needs fundamental art, skills, knowledge and 
experience that will helps stakeholders/practitioners to handle their businesses with promising results, through the use of intelligent, tactful, constructive strategies. This Diplomatic Protocol lecture seeks to build capacity and develop analytical tools, skills and experience to all those engaged in various types of Protocol related activities. 

1.2 Targeted participants 

This Diplomatic lecture is designed for career Diplomats, officials from the government, Ministries officials, Districts officials, Personal Assistants, Administrators and Managers, Directors, Executives and CEOís, all employers and employees from private and public sectors in general, as well as all those who wish to develop career and build their capacity in this discipline 

1.3 Lecture module 

The lecture will also reflects on Stress Management for Protocol practitioners, Visits and Ceremonies, Orders and arrangements, Table manners, treating and handling VIP and , role and Quality of good 
protocol officer 

DELIVERY METHOD: 

Duration: One (1) day (full time, from 9.00hr ñ 16.00hrs) 

Delivery: Lectures, discussions and case studies 

Assessment: Non-examinable 

Award: Certificate of attendance 

Fees: Tsh. 100,000/= only, which also covers Breakfast and lunch, 

Payment: NMB BANK 2361 000 1369 A/C Name: ECOMOMIC DIPLOMACY -TRAINING 

Venue: The National Museum ñ Shaaban Robert Street - DAR ES SALAAM (Opposite IFM). 

FOR MORE INFORMATION PLEASE CONTACT: 

Coordinators: Directorate of Training and Operation 

ECONOMIC DIPLOMACY -TRAINING ACADEMY 

0713 667 303, 0763 65 75 87, 0779 900 440, 

info@economicdiplomacy.ac.tz www.economicdiplomacy.ac.tz 

WAZIRI MKUU ATOA SIKU MBILI KWA MAOFISA ARDHI KUMALIZA KERO ZA WANANCHI

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa siku mbili kwa Mkuu wa Idara ya Ardhi na Miundombinu wa mkoa wa Rukwa pamoja na Ofisa Ardhi wa Manispaa ya Sumbawanga kutatua matatizo ya ardhi yanayowakabili wakazi wa Manispaa hiyo.

“Ijumaa kuanzia saa 3.00 asubuhi wenye kero za ardhi wote waende kwenye ukumbi wa Manispaa mkuu wa idara atakuwa na watumishi wote na hapa mtasikilizwa kero zenu na kupatiwa ufumbuzi. Nasiku hiyo hakuna kazi nyingine ni kusikiliza wananchi tu,” alisema.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana jioni (Jumatano, Agosti 24, 2016) wakati akizungumza na maelfu ya wakazi Mji wa Sumbawanga waliojitokeza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kiwanja cha Mandela katika jimbo la Sumbawanga mjini ambapo aliwasisitiza watendaji hao kuwasikiliza wananchi na kutatua kero zao.

Alisema tangu alivyoanza ziara yake katika mikoa ya Rukwa na Katavi kila eneo alilopita amekutana na wananchi wakiwa na mabango yanaeleza changamoto na hii inatokana na viongozi wa mikoa hiyo kushindwa kutenga siku maalumu kwa ajili ya kusikiliza kero hizo.

Waziri Mkuu alibainisha kwamba baadhi ya mikoa na halmashauri mbalimbali nchini zimeshaanza utaratibu huo wa kutenga siku maalumu katika wiki na kusikiliza matatizo yanayowakabili wananchi jambo ambalo limeanza kuonesha mafanikio ya utatuzi wa kero hizo.

Awali akizungumza katika mkutano huo mbunge wa jimbo la Sumbawanga Mjini Aeshi Hilaly alisema wakazi wa Manispaa ya Sumbawanga wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya migogoro mikubwa ya ardhi, hivyo alimuomba Waziri Mkuu kuwasaidia katika kuipatia ufumbuzi.

Mbunge huyo alisema migogoro hiyo ambayo imedumu kwa muda mrefu imewasababishia usumbufu mkubwa wakazi wa jimbo hilo kukosa haki  zao na muda mwingi wamekuwa wakiutumia kufuatilia hatma ya ardhi yao bila ya mafanikio hivyo kurudi nyuma kimaendeleo.

Pia mbunge huyo alimuomba Waziri Mkuu kuwaondolea zuio la kuuza mazao yao nje ya nchi kwa sababu kitendo hicho kimesababisha kushuka bei ya mahindi na kusababisha hasara kubwa kwa wakulima ambao wametumia gharama kubwa katika kuandaa mashamba.

Akizungumzia zuio hilo Waziri Mkuu alisema lengo la Serikali kuzuia uuzwaji wa mazao nje ni kutaka kujiridhisha na uwepo wa chakula cha  kutosha nchini ili kuepuka kukumbwa na baa la njaa na kisha kwenda kuomba msaada kwenye nchi tuliowauzia.

 Kuhusu suala la soko la mahindi Waziri Mkuu alisema Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) watanunua kwa bei ya soko na kwamba wataruhusiwa kuuza nje ya nchi baada ya Serikali kujaza maghala yake huku wataalam wakimalizia kufanya tathmini ya hali ya chakula nchini.

RC SIMIYU ATOA UFAFANUZI SAHIHI WA TAARIFA KUHUSU WALIMU WAKUU KUVULIWA MADARAKA

$
0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthon Mtaka akizungumza na Maafisa Elimu na Viongozi wa CWT wa Mkoa huo katika kikao maalum cha kutoa ufafanuzi wa agizo lililotolewwa na Serikali Mkoani humo la kufanya mabadiliko ya Walimu wakuu na Waratibu Elimu kata, ambalo liliripotiwa tofauti katika vyombo ya habari na mitandao ya kijamii. kuwa Serikali imetangaza kuwavua madaraka.

Na Stella Kalinga, Simiyu

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka ametoa ufafanuzi wa agizo la kufanya mabadiliko ya Walimu wakuu, Wakuu wa Shule na Waratibu Elimu Kata mkoani humo, ambalo Serikali ya Mkoa ililitoa tarehe 17 Agosti ,2016 katika kikao ambacho alipokea Vishikwambi (tablets) 637 kutoka EQUIP Tanzania (Mpango wa Kuinua Ubora wa Elimu Nchini) kwa ajili ya Walimu wakuu na Waratibu wa Elimu Kata

Mkuu huyo wa Mkoa ametoa ufafanuzi huo kufuatia kuwepo kwa taarifa za upotoshaji wa agizo hilo kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii., kuwa Mkuu wa Mkoa ametangaza kuwavua madaraka Walimu wakuu, Wakuu wa Shule na Waratibu Elimu Kata wote wa Mkoa huo; hali iliyopelekea baadhi ya Walimu wakuu na Waratibu kukosa ari ya kufanya kazi, kwa kigezo cha kusubiri kuvuliwa madaraka.
Baadhi ya Wajumbe wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu (hayupo pichani) katika kikao maalum cha kutoa ufafanuzi wa agizo lililotolewa na Serikali Mkoani humo la kufanya mabadiliko ya Walimu wakuu na Waratibu Elimu kata, ambalo liliripotiwa tofauti katika vyombo ya habari na mitandao ya kijamii. kuwa Serikali imetangaza kuwavua madaraka, 

Mtaka amesema Mkoa ulipokea taarifa za takwimu za wanafunzi hewa, vyumba vya madarasa, idadi ya walimu na idadi ya madawati, baada ya kupokea taarifa hizo ulionekana utofauti mkubwa wa takwimu hizo ndipo Serikali mkoani humo, ikaahidi kupitia mapungufu ya udanganyifu wa takwimu hizo kwa kila shule na kuchukua hatua ikiwa ni pamoja na kuwawajibisha Walimu wakuu na Wakuu wa Shule waliodanganya idadi ya wanafunzi.

Aidha, Mtaka amesema Mkoa wa Simiyu umepata bahati ya kuwa na Mradi wa EQUIP Tanzania ambao umewawezesha waratibu kupata pikipiki na posho, walimu wakuu wamepewa vishikwambi kwaa jili ya utunzaji wa takwimu, hivyo Serikali inao wajibu wa kuangalia mahitaji ya Mkoa katika elimu ambapo alielekeza yafanyike mabadiliko ya Walimu wakuu Msingi, Sekondari na Waratibu wa mkoa mzima.

SOMA ZAIDI HAPA

JESHI LA POLISI ZANZIBAR KUPAMBANA NA WANAOTUMIA KAZI ZA WASANII BILA YA LESENI YA HAKIMILIKI

$
0
0
Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Hamdani Omar Makame akizungumza na wandishi wa habari kuhusu wajibu wa Jeshi la Polisi katika usimamizi wa kazi za wasanii, Makao Makuu ya Polisi Kilimani Zanzibar leo. Picha na Mkame Mshenga/Maelezo Zanzibar.
Jeshi la Polisi Zanzibar limedhamiria kupambana na uharamia wa kazi za hakimiliki kwa kudhibiti maeneo ya uingizaji hakimiliki haramu katika maeneo ya bandarini na uwanja wa ndege .

Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamdani Omari amesema hayo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari huko Makao Makuu ya Polisi Zanzibar kuhusu usimamizi na wajibu wa Jeshi la Polisi katika usimamizi wa hakimiliki .

Amewataka wananchi kuelewa kwamba kutoa kopi ,kuuza vinasa sauti na picha za kieletroniki vikiwemo CD,DVD na vyenginevyo bila ya leseni ya hakimiliki ni miongoni mwa makosa ya jinai.

Aidha alisema kutumia hakimiliki biila ya ridhaa ya mwenye haki kama vile kurudufu kusambasa na kuonyesha kazi kwa umma ama kuibadilisha kazi na kuwa kwa mtindo mwengine ni kosa kwa mujibu ya sheria ya hakimiliki No. 14 ya mwaka 2003.

Amesema hakimiliki ni mali ya anaemiliki ,ni kazi yake inaestahili ulinzi kwani kuitumia bila ya ridhaa ya mwenye haki ni kosa kisheria Katika kusimamia sheria ya hakimiliki Jeshi la Polisi limetoa taaluma kwa askari wake wakiwemo makamanda wa mikoa yote ya Zanzibar katika mwaka 2008 -2009 ofisi ilianzisha kikundi kazi cha hakimiliki .

Alieleza kuwa jumla ya polisi 100 wa Unguja na Pemba walipatiwa mafunzo ya utambuzi wa makosa ya hakimiliki kupitia mtalamu wa utambuzi wa jinai za hakimiliki SP Omar Muwowo kutoka jeshi la polisi Zambia na Interpol.

Kamishna huyo alieleza kuwa Jeshi la Polisi lilifanikiwa kupambana na uharamia wa hakimiliki kwa kushirikiana na Afisi ya hakimiliki kufanya ukaguzi katika maeneo yote ya Unguja na kukamata nakala haramu za vinasa sauti na picha vya kielektroniki vikiwemo CD , DVD‘S na MP3 zenye uzito wa tani mbili .

Aidha alisema nakala haramu hizo ziliangamizwa kwa kushirikiana na Idaraya Mazingira Zanzibar .

BARAZA LA TAIFA LA USALAMA BARABARANI LAKUTANA KUJADILI MAENDELEO YA MKAKATI WA KUPUNGUZA AJALI

$
0
0
Wajumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, wakiongozwa na Mwenyekiti wa baraza ambae pia ni Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(katikati), katika kikao cha kujadili maendeleo ya Mkakati wa Kudhibiti Ajali za Barabarani , ambao ulizinduliwa rasmi mwanzoni mwa mwezi wa nane,ukiwa na lengo la kupunguza ajali kwa asilimia kumi ifikapo mwezi Februari, mwakani.Wa kwanza mkono wa kulia kwa Naibu Waziri ni Katibu Mtendaji wa baraza ambae pia ni Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani , Mohamed Mpinga. Kikao kilifanyika katika ukumbi wa wizara,jijini Dar es Salaam.
Mjumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Henry Bantu, akizungumza wakati wa kikao cha kujadili maendeleo ya Mkakati wa Kudhibiti Ajali za Barabarani , ambao ulizinduliwa rasmi mwanzoni mwa mwezi wa nane,ukiwa na lengo la kupunguza ajali kwa asilimia kumi ifikapo mwezi Februari, mwakani. Kikao kilifanyika katika ukumbi wa wizara,jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani nchini ambae pia ni Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza wakati wa kikao cha kujadili maendeleo ya Mkakati wa Kudhibiti Ajali za Barabarani , ambao ulizinduliwa rasmi mwanzoni mwa mwezi wa nane,ukiwa na lengo la kupunguza ajali kwa asilimia kumi ifikapo mwezi Februari, mwakani. Kikao kilifanyika katika ukumbi wa wizara,jijini Dar es Salaam.
Mjumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, ASP Deus Sokoni, akizungumza wakati wa kikao cha kujadili maendeleo ya Mkakati wa Kudhibiti Ajali za Barabarani, ambao ulizinduliwa rasmi mwanzoni mwa mwezi wa nane,ukiwa na lengo la kupunguza ajali kwa asilimia kumi ifikapo mwezi Februari, mwakani. Kikao kilifanyika katika ukumbi wa wizara,jijini Dar es Salaam.(Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

WAJUMBE WA BODI YA STAMICO WATEMBELEA MGODI WA TANZANITEONE MIRERANI

$
0
0
Wajumbe wa bodi ya STAMICO wakipanda scip kwa ajili ya kuingia kwenye mgodi wa madini ya Tanzanite uitwao CT.
Wajumbe wa bodi ya wakurugenzi wa shirika la madini nchini (STAMICO) wakiwa na baadhi ya watumishi wa kampuni ya TanzaniteOne walipotembelea mgodi wanaoumiliki kwa ubia na kampuni hiyo uliopo mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara.
Wajumbe wa bodi ya shirika la madini nchini (STAMICO) wakiwa na Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi Balozi Alexiander Muganda, (wa pili kushoto) baada ya kutembelea mgodi wanaoumiki kwa ubia na kampuni ya TanzaniteOne uliopo mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la madini nchini (STAMICO) Zena Kongoi akizungumza na waandishi wa habari, kwenye mgodi wanaoumiliki kwa ubia na kampuni ya TanzaniteOne.

Moro Kids yatwaa ubingwa Airtel Rising Stars Morogoro

$
0
0
Timu ya vijana ya Moro Kids imefanikiwa kutwaa ubingwa wa michuano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars baada ya kufanya kazi ya ziada na kuishinda timu ngumu ya Angrikana 1-0 katika mchezo wenye upinzani mkali uliochezwa kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro jana.

Goli hilo la ushindi liliwekwa kimiani na mshambuliaji machachari Nyamawi Juma katika dakika ya 22 baada ya kuwazidi mbio walinzi wa Angrikana na kuachia shuti kali lililotinga wavuni. Goli liliibua nderemo na vifijo kutoka kwa mashabiki waliojitokeza kwa wingi kushangilia timu yao.

Angrikana walijibu mapigo kwa kufanya mashambulizi mfululizo ambayo hata hivyo hayakuweza kuzaa matunda. Kipingi cha pili walikianza kwa matumaini ya kupata goli la kusawazisha lakini hadi dakika ya mwisho matokeo yalibaki kuwa 1-0.

Akikabidhi kikombe kwa washindi, Meya wa manispaa ya Morogoro Pascal Kihanga ambaye alikuwa mgeni rasmi aliwapongeza Morogoro Kids kwa mafanikio makubwa na kuwataka kuendelea kufanya mazoezi kwa kujituma huku wakifuata maelekezo ya walimu wao. “Kwa kufanya hivyo kutawaweka katika nafasi nzuri ya kutimiza ndoto zenu za kufanikiwa katika maisha kupitia soka”, alisema.

Aliwataka viongozi wa soka mkoani Morogoro pamoja na makocha kuhakikisha wanachagua vijana wenye vipaji ili kuuwakilisha vyema mkoa wa Morogoro kwenye fainali za taifa za Airtel Rising Stars zinazotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Septemba 6 hadi to 11.

Wakati wa mechi hizo za mkoa makocha walipata fursa ya kuwatathimini uwezo wa kila mchezaji na kuchagua vijana wenye vipaji kuunda kombaini ya mkoa. Mikoa mingine ambayo tayari imeshaunda vikosi vyake ni kwa fainali hizo ni Ilala, Kinondoni, Temeke and Mwanza.

Fainali hizo za kila mwaka itazikutanisha timu za wavulana na wasichana kutoka mikoa ya kisoka ya Ilala, Kinondoni na Temeke. Washiriki wengine watatoka Mwanza, Morogoro, Mbeya, Lindi, Arusha na Zanzibar.
Wachezaji wa timu ya moro kids wakishangilia baada ya kunyakua kombe la mashindano ya Airtel Rising Stars kwa kuifunga timu ya Angrikana 1-0 katika uwanja wa Jamhuri Morogoro jana.
Kapteni wa timu ya Moro Kids Abdul Rashid akipokea kombe la mshindi wa kwanza wa mashindano ya Airtel Rising Stars kutoka kwa mgeni rasmi ambae ni Meya wa Manispaa ya Morogoro pascal kihanga, Moro Kids imenyakua kombe hilo baada ya kuifunga timu ya Angrikana 1-0.
Mchezaji wa timu ya Moro Kids Ibrahimu Ally mwenye jezi nyeupe wakiwania mpira na mchezaji wa timu ya Angrikana Baraka Omary katika mchezo wa fainali ya Airtel Rising Starkwenye uwanja wa Jamhuri Morogoroo. Moro Kids ilinyakua kombe hilo kwa ushindi wa 1-0.
Mshambuliaji wa timu ya Angrikana Saidi Mohamed akidhibitiwa kikamilifu na beki wa timu ya Moro Kids Ibrahim Yohana katika pambano la fainali ya Airtel Rising Stars iliyofanyika uwanja wa Jamhuri Morogoro ambapo moro kids ilinyakua kombe hilo baada ya kushinda 1-0.

TAARIFA KWA WATEJA WA NMB NA UMMA KWA UJUMLA

HAL yafanya kazi miaka 8 bila kibali cha TBS

$
0
0
KAMPUNI inayojulikana kama Hanspaul Automechs Limited (HAL) iliyopo Arusha imekuwa ikifanya kazi nchini kwa takriban miaka nane sasa bila kuwa na idhini ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS).

HAL ilianzishwa mwaka 2007 ikijishughulisha na utengenezaji na uuzaji ndani na nje ya nchi mabodi ya magari maalumu kwa safari za kitalii maarufu kama ‘Safari’.

Hayo yamefahamika hivi karibuni baada ya TBS kuthibitisha kuwa haijawahi kuipa HAL cheti cha ubora kwa ajili ya mabodi hayo, hivyo kuliweka njiapanda shirika hilo katika vita vya kusaka haki ya kutengeneza mabodi hayo yanayofahamika pia kwa jina la ‘War Bus’.

Kesi ya kutafuta haki hiyo ipo mahakamani kwa muda mrefu sasa kati ya HAL na kampuni nyingine ya utengenezaji mabodi ya aina hiyo iliyopo Mjini Moshi, RSA Limited, ambao wanadai wao ndio wabunifu wa awali wa mabodi hayo.

Wiki iliyopita, kilifanyika kikao kwenye Makao Makuu ya TBS jijini Dar es Salaam chini ya Mwanasheria wa Shirika hilo, Humphrey Shonga, kati ya maofisa wa TBS na wanasheria wa RSA Limited.

Katika kikao hicho cha Agosti 18 mwaka huu, wanasheria wa RSA Limited walihoji sababu za TBS kuruhusu bidhaa zisizokuwa na cheti cha ubora kuingizwa katika soko la Tanzania na pia kuuzwa nje ya nchi zikitokea Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani ya kikao hicho, ili TBS iweze kuwapa HAL cheti cha kuthibitisha ubora wa bidhaa zao, waliwaagiza kuwasilisha vielelezo na michoro ya utengenezaji wa mabodi hayo ambavyo haviendani na vya mshindani mwingine yeyote.

“HAL wameshindwa kuwasilisha vielelezo hivyo hadi leo,” alisema mmoja kati ya watu waliohudhuria kikao hicho ambaye hakupenda jina lake liandikwe na kuongeza:

“Hata hivyo, pamoja na kutotambuliwa na TBS, HAL imekuwa ikipata upendeleo wenye shaka wa kutengeneza na kuuza ndani na nje ya nchi bidhaa hizo.”

Barua ya Wakala wa Usajili wa Leseni na Biashara (BRELA) kwa wanasheria wa RSA Limited ya Julai 25 mwaka huu, inaweka wazi kuwa, Februari 24, 2016, HAL ilipewa leseni ya muda (Temporary Industrial License) namba 00000928 ikitakiwa kuwasilisha taarifa ya maendeleo za kila mwaka huku bidhaa zinazozalishwa zithibitishwe ubora na TBS.

“Hii inathibitisha kuwa kwa miaka nane, HAL imekuwa ikibadili na kutengeneza mabodi ya magari ya kitalii bila kuwa na leseni huku mamlaka husika zikishindwa kuchukua hatua,” alisema mtoa habari wetu.

Kwa mujibu wa kanuni za TBS na Mamlaka ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), magari yote yenye dhamana ya kubeba abiria lazima yathibitishwe na TBS kabla ya kuingia barabarani.

“Lakini hadi sasa TBS haijaonyesha nia ya kutekeleza kanuni hiyo kwa walau kuionya HAL kwa kosa la kuingiza bidhaa zake sokoni bila kibali chao, au kuuambia umma kwmba mabodi yao (Safari Tourist Bodies) ni salama na halali kubeba abiria au la,” alisema.

Ukimya wa TBS unazidisha shaka kwa sababu ni wazi kuwa maofisa wao waliopo kwenye mipaka kama Namanga, Sirali au Mutukula na wengine wanaofanya ukaguzi maeneo mbalimbali nchini wamewahi kukutana na bidhaa za HAL.

“Au basi hata barua za RSA Limited za mwaka 2008, 2014, 2015 na 2016 (nakala zake tunazo) kuitaarifu TBS suala hili, zingetosha kuwaamsha wakaguzi wa shirika hili muhimu kwa afya na usalama wa Watanzania na kuchukua hatua,” alisema.

Alipotafutwa jana kwa njia ya simu kwa ajili ya kupata ufafanuzi zaidi, Afisa habari wa TBS, Bi Rhoida Andusamile alisema hawakuwa tayari kuizungumzia swala hilo kwani shirika hilo ilikuwa katika maandalizi ya kutoa taarifa rasmi hapo baadaye, bila kutaja ni lini taarifa hiyo itatoka.

Kwa upande mwingine, HAL pia imekuwa ikipata mauzo makubwa kwa kuungwa mkono na Toyota Tanzania Limited (TTL) inayotambua bidhaa hizo wakati ubora wake haujathibitishwa.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa HAL Group, Satbir Hanspaul, kampuni hiyo ina uwezo wa kuzalisha kati ya mabodi (war bus) 30 na 35 kwa mwezi lakini hutengeneza mabodi aina ya Winnebago kwa oda maalumu.

Mwaka jana, Hanspaul aliwaambia waandishi wa habari kuwa Kenya, Uganda na Afrika Kusini ni miongoni mwa nchi zinazoagiza 'War Buses' kutoka Arusha kwa ajili ya kusafirisha watalii kwenye mbuga zao.

Zipo taarifa kuwa mataifa mengine ya ughaibuni huagiza mabodi yaliyotengenezwa maalumu na kampuni hiyo kwa ajili ya kutumiwa na majeshi ya huko.

RC SIMIYU ATOA UFAFANUZI SAHIHI WA TAARIFA KUHUSU WALIMU WAKUU KUVULIWA MADARAKA

$
0
0




Na Stella Kalinga, Simiyu

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka ametoa ufafanuzi wa agizo la kufanya mabadiliko ya Walimu wakuu, Wakuu wa Shule na Waratibu Elimu Kata mkoani humo, ambalo Serikali ya Mkoa ililitoa tarehe 17 Agosti ,2016 katika kikao ambacho alipokea Vishikwambi (tablets) 637 kutoka EQUIP Tanzania (Mpango wa Kuinua Ubora wa Elimu Nchini) kwa ajili ya Walimu wakuu na Waratibu wa Elimu Kata

Mkuu huyo wa Mkoa ametoa ufafanuzi huo kufuatia kuwepo kwa taarifa za upotoshaji wa agizo hilo kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii., kuwa Mkuu wa Mkoa ametangaza kuwavua madaraka Walimu wakuu, Wakuu wa Shule na Waratibu Elimu Kata wote wa Mkoa huo; hali iliyopelekea baadhi ya Walimu wakuu na Waratibu kukosa ari ya kufanya kazi, kwa kigezo cha kusubiri kuvuliwa madaraka.

Mtaka amesema Mkoa ulipokea taarifa za takwimu za wanafunzi hewa, vyumba vya madarasa, idadi ya walimu na idadi ya madawati, baada ya kupokea taarifa hizo ulionekana utofauti mkubwa wa takwimu hizo ndipo Serikali mkoani humo, ikaahidi kupitia mapungufu ya udanganyifu wa takwimu hizo kwa kila shule na kuchukua hatua ikiwa ni pamoja na kuwawajibisha Walimu wakuu na Wakuu wa Shule waliodanganya idadi ya wanafunzi.

Aidha, Mtaka amesema Mkoa wa Simiyu umepata bahati ya kuwa na Mradi wa EQUIP Tanzania ambao umewawezesha waratibu kupata pikipiki na posho, walimu wakuu wamepewa vishikwambi kwaa jili ya utunzaji wa takwimu, hivyo Serikali inao wajibu wa kuangalia mahitaji ya Mkoa katika elimu ambapo alielekeza yafanyike mabadiliko ya Walimu wakuu Msingi, Sekondari na Waratibu wa mkoa mzima.

“Nililisema mwanzo na leo nalirudia tutafanya mabadiliko makubwa kwa Wakuu wa Shule za Msingi, Sekondari na Waratibu Elimu kata kwa kujiridhisha na maendeleo ya shule zetu, idadi ya walimu waliopo,idadi ya wanafunzi, kiwango cha ufaulu wa wanafunzi na mazingira ya shule ; lakini tutatoa upendeleo kwa shule 10 bora katika kila wilaya kwa Mitihani ya Kitaifa ya Darasa la IV, VII Kidato cha II na IV , hiki ni kipimo kimojawapo cha walimu wa kuendelea nao. Nasisitiza hakuna mtu atakayeonewa wala kufedheheshwa”, alisema Mtaka.

Mtaka amesema azma ya Serikali ni kuibua vipaji vipya vya viongozi wa Elimu katika ngazi ya Wilaya ambapo alisema ameshaagiza Maafisa Elimu wa Wilaya kuwasilisha taarifa ya walimu waliojiendeleza katika ngazi shahada ya kwanza na shahada ya uzamili ili watakaokuwa na sifa waweze kuteuliwa katika nafasi za Walimu wakuu, Wakuu wa Shule na Waratibu Elimu Kata ambao watafanyiwa upekuzi (vetting) na Vyombo vya Ulinzi na Usalama.

Sanjari na hilo , Mkuu huyo wa Mkoa amesema Walimu wakuu na Wakuu wa shule wa zamani ni tofauti na wale wa sasa, kwa kuwa sasa hivi wamekuwa maafisa masuuli wa shule zao ambapo wanapokea fedha za Elimu bila malipo kupitia akaunti za shule zao, hivyo ni lazima wapatikane watu waadilifu, wenye sifa na uwezo wa kuongoza shule na kusimamia fedha za Serikali.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthon Mtaka akizungumza na Maafisa Elimu na Viongozi wa CWT wa Mkoa huo katika kikao maalum cha kutoa ufafanuzi wa agizo lililotolewwa na Serikali Mkoani humo la kufanya mabadiliko ya Walimu wakuu na Waratibu Elimu kata, ambalo liliripotiwa tofauti katika vyombo ya habari na mitandao ya kijamii. kuwa Serikali imetangaza kuwavua madaraka.Baadhi ya Wajumbe wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu (hayupo pichani) katika kikao maalum cha kutoa ufafanuzi wa agizo lililotolewa na Serikali Mkoani humo la kufanya mabadiliko ya Walimu wakuu na Waratibu Elimu kata, ambalo liliripotiwa tofauti katika vyombo ya habari na mitandao ya kijamii. kuwa Serikali imetangaza kuwavua madaraka, 
Katibu wa CWT Mkoa wa Simiyu, Said Mselema(kulia) akizungumza na Maafisa Elimu na Viongozi wa CWT wa Mkoa huo (hawapo pichani) katika kikao maalum cha kutoa ufafanuzi wa agizo lililotolewa na Serikali Mkoani humo la kufanya mabadiliko ya Walimu wakuu na Waratibu Elimu kata, ambalo liliripotiwa tofauti katika vyombo ya habari na mitandao ya kijamii, kuwa Serikali imetangaza kuwavua madaraka.
Baadhi ya Wajumbe wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu (hayupo pichani) wa kikao maalum cha kutoa ufafanuzi wa agizo lililotolewwa na Serikali Mkoani humo la kufanya mabadiliko ya Walimu wakuu na Waratibu Elimu kata, ambalo liliripotiwa tofauti katika vyombo ya habari na mitandao ya kijamii. kuwa Serikali imetangaza kuwavua madaraka.


HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

TEA KUFADHILI UJENZI WA NYUMBA ZA WALIMU KATIKA MAENEO YASIO RAHISI KUFIKIKA

$
0
0
Mkurugenzi  Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania Joel Laurent (wa kwanza kushoto) akijadiliana suala  na viongozi wa Halmashauri ya KilosaMamlaka ya Elimu  Tanzania inatarajia kutekeleza na kufadhili mradi wa kujenga nyumba za walimu kupitia Watumishi Housing Ltd katika Ujenzi katika maeneo yasio rahisi kufikika, katika shule ya Sekondari Uleling'ombe iliyopo Wilaya ya Kilosa.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania,Joel Laurent akiongea na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, kamati ya shule ya Uleling'ombe,uongozi wa kijiji cha Uleling'ombe wakijadilana utekelezaji wa Mradi wa kujenga nyumba za walimu katika maeneo yasio rahisi kufikika, katika shule ya Sekondari Uleling'ombe iliyopo Wilaya ya Kilosa.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania,Joel Laurent akioneshwa  eneo lililotengwa kwa ajili ya kujenga nyumba za walimu katika shule ya Sekondari Uleling'ombe mradi unaotekeleza na kufadhili na Mamlaka ya Elimu Tanzania ikiwatumia Watumishi Housing Ltd katika Ujenzi katika maeneo yasio rahisi kufikika.

BOFYA HAPA KWA HABARI ZAIDI

WAZIRI MKUU ATOA SIKU MBILI KWA MAOFISA ARDHI KUMALIZA KERO ZA WANANCHI

$
0
0

 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa siku mbili kwa Mkuu wa Idara ya Ardhi na Miundombinu wa mkoa wa Rukwa pamoja na Ofisa Ardhi wa Manispaa ya Sumbawanga kutatua matatizo ya ardhi yanayowakabili wakazi wa Manispaa hiyo.

“Ijumaa kuanzia saa 3.00 asubuhi wenye kero za ardhi wote waende kwenye ukumbi wa Manispaa mkuu wa idara atakuwa na watumishi wote na hapa mtasikilizwa kero zenu na kupatiwa ufumbuzi. Nasiku hiyo hakuna kazi nyingine ni kusikiliza wananchi tu,” alisema.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana jioni (Jumatano, Agosti 24, 2016) wakati akizungumza na maelfu ya wakazi Mji wa Sumbawanga waliojitokeza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kiwanja cha Mandela katika jimbo la Sumbawanga mjini ambapo aliwasisitiza watendaji hao kuwasikiliza wananchi na kutatua kero zao.

Alisema tangu alivyoanza ziara yake katika mikoa ya Rukwa na Katavi kila eneo alilopita amekutana na wananchi wakiwa na mabango yanaeleza changamoto na hii inatokana na viongozi wa mikoa hiyo kushindwa kutenga siku maalumu kwa ajili ya kusikiliza kero hizo.

Waziri Mkuu alibainisha kwamba baadhi ya mikoa na halmashauri mbalimbali nchini zimeshaanza utaratibu huo wa kutenga siku maalumu katika wiki na kusikiliza matatizo yanayowakabili wananchi jambo ambalo limeanza kuonesha mafanikio ya utatuzi wa kero hizo.

Awali akizungumza katika mkutano huo mbunge wa jimbo la Sumbawanga Mjini Aeshi Hilaly alisema wakazi wa Manispaa ya Sumbawanga wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya migogoro mikubwa ya ardhi, hivyo alimuomba Waziri Mkuu kuwasaidia katika kuipatia ufumbuzi.

Mbunge huyo alisema migogoro hiyo ambayo imedumu kwa muda mrefu imewasababishia usumbufu mkubwa wakazi wa jimbo hilo kukosa haki  zao na muda mwingi wamekuwa wakiutumia kufuatilia hatma ya ardhi yao bila ya mafanikio hivyo kurudi nyuma kimaendeleo.

Pia mbunge huyo alimuomba Waziri Mkuu kuwaondolea zuio la kuuza mazao yao nje ya nchi kwa sababu kitendo hicho kimesababisha kushuka bei ya mahindi na kusababisha hasara kubwa kwa wakulima ambao wametumia gharama kubwa katika kuandaa mashamba.

Akizungumzia zuio hilo Waziri Mkuu alisema lengo la Serikali kuzuia uuzwaji wa mazao nje ni kutaka kujiridhisha na uwepo wa chakula cha  kutosha nchini ili kuepuka kukumbwa na baa la njaa na kisha kwenda kuomba msaada kwenye nchi tuliowauzia.

 Kuhusu suala la soko la mahindi Waziri Mkuu alisema Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) watanunua kwa bei ya soko na kwamba wataruhusiwa kuuza nje ya nchi baada ya Serikali kujaza maghala yake huku wataalam wakimalizia kufanya tathmini ya hali ya chakula nchini.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU, 

MAABARA ZA GST, TIRDO ZATEULIWA KUTHIBITISHA UBORA WA MAKAA YA MAWE.

$
0
0
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe (kushoto kwa Waziri), wakifuatilia majadiliano yaliyokuwa yakiendelea wakati wa Mkutano baina ya Wizara na wachimbaji pamoja na watumiaji wa makaa ya mawe, uliofanyika Agosti 24 wizarani, jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akifafanua jambo katika mkutano na wachimbaji pamoja na watumiaji wa makaa ya mawe (hawapo pichani) uliojadili changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo. Mkutano huo ulifanyika Agosti 24, mwaka huu, Makao Makuu ya Wizara, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe.
Wajumbe mbalimbali walioshiriki Mkutano baina ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Wachimbaji pamoja na Watumiaji wa Makaa ya Mawe, wakifuatilia mijadala mbalimbali katika Mkutano huo uliofanyika Agosti 24 mwaka huu Makao Makuu ya Wizara jijini Dar es Salaam.

Veronica Simba na Devota Myombe.
SERIKALI imeziteua maabara za Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) na Shirika la Umma linalojishughulisha na tafiti mbalimbali pamoja na kutoa ushauri wa kitaalam kuhusu Viwanda (Tanzania Industrial Research and Development Organization – TIRDO), kupima na kuthibitisha ubora wa makaa ya mawe yanayozalishwa nchini.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, alisema Maabara hizo za GST na TIRDO zitatumika kupima na kuthibitisha ubora wa makaa hayo pale inapotokea mgogoro wa kutokukubaliana kuhusu ubora wake baina ya wazalishaji na watumiaji wake.

Aliyasema hayo hivi karibuni jijini Dar es Salaam alipokutana na kuzungumza na wazalishaji na wamiliki wa Viwanda vinavyotumia makaa ya mawe nchini kuhusu changamoto wanazokabiliana nazo.

Maelekezo hayo ya Waziri Muhongo yalitokana na wasiwasi walioonesha baadhi ya wajumbe wa kikao hicho, hususan watumiaji wa makaa ya mawe, ambao wamekuwa wakilalamika kuwa madini hayo yanayozalishwa nchini hayana ubora unaotakiwa na hivyo kuagiza kutoka nje ya nchi, kabla ya hivi karibuni kuzuiwa na Serikali na kuwataka wanunue yanayozalishwa hapa nchini. 

Akitoa maelekezo kuhusu utaratibu utakaotumika, Profesa Muhongo alisema kuwa, pande zote mbili, yaani wazalishaji na watumiaji wanapaswa kuwa na maabara zao ambazo zitatumika kupima ubora wa makaa husika.

Alielekeza kuwa, kabla ya kupeleka mzigo wa makaa ya mawe kwa watumiaji, wazalishaji wanapaswa kupima ubora wake katika maabara zao na kuweka alama inayoonesha ubora husika juu ya mzigo.

Aidha, kwa upande wa watumiaji, Waziri Muhongo alielekeza kuwa, wanapopokea mzigo husika, wanapaswa kuupima katika maabara zao, kabla ya kuutumia ili kujiridhisha kuhusu ubora wake kama ambavyo utakuwa umeainishwa katika alama iliyofungwa juu ya mzigo.

“Mkijiridhisha kuwa makaa ya mawe mliyopokea yana ubora unaotakiwa, mtapaswa kusaini kuthibitisha hilo na endapo mkigundua kuna tofauti, mna haki ya kutokusaini na kutokuyatumia makaa hayo,” alifafanua.

Waziri Muhongo aliongeza kuwa, endapo itatokea mgogoro wa kutokuelewana kuhusu ubora wa makaa yaliyowasilishwa na mzalishaji kwa mtumiaji, pande hizo mbili zitapaswa kutoa taarifa serikalini kupitia kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati iliyoundwa kushughulikia migogoro katika sekta husika.

Alisema kuwa, suala husika likifikishwa serikalini, Mwenyekiti atasimamia zoezi la upimwaji wa makaa husika katika moja ya maabara zilizoteuliwa, ambazo ni GST na TIRDO ili kuthibitisha ubora wake na hivyo kufikia muafaka.

Waziri Muhongo aliwataka wazalishaji na watumiaji wa makaa ya mawe kuacha manung’uniko yasiyo na tija na kila upande utimize makubaliano yaliyofikiwa katika vikao vyote vya awali na kwamba, Serikali kwa upande wake, itatimiza wajibu wake ipasavyo.

UCHAMBUZI WA HABARI ZA MAGAZETI YA LEO AUGUST 25, 2016.

Programu ya Kuwezesha Umilikishaji Ardhi ( LTSP ) Kupunguza Migogoro ya Ardhi, MOROGORO

$
0
0

Na Salum Mwinyimkuu, Morogoro.

Zaidi ya hatimiliki 300,000 za Ardhi zinatarajiwa kutolewa kwenye Wilaya za KILOMBERO, MALINYI na ULANGA mkoani Morogoro kupitia mradi wa kuwezesha Urasimishaji Ardhi wa LTSP, ili kupunguza Migogoro ya Mipaka kwenye Vijiji.

Miongoni mwa Changamoto inayofifiza Juhudi za Serikali kumaliza tatizo la Migogoro ya Ardhi katika Wilaya za KILOMBERO, MALINYI na ULANGA ni Rushwa kwa Baadhi ya Watendaji wasio waaminifu.

Wilaya ya KILOMBERO yenye vijiji 99 imejizolea Umaarufu kwa kuwa na maeneo mengi yenye Utata wa Ardhi,ikihusisha migogoro ya Mipaka baina ya kijiji na kijiji, hifadhi na kijiji pamoja na wakulima na wafugaji.
Godfrey Machabe Mratibu wa Program ya kuwezesha Umilikishaji Ardhi (kushoto), Renit Halimba Diwani Viti maalum Wilaya ya Kilombero (wa pili kushoto) Lucas Mwaisaka Katibu tawala msaidizi Wilaya ya kilombero (kulia) Alicie Libenanga (wa pili Kulia) na Syabomi Mwaipopo (katikati) Dkt Steven Nindi Wakikabidhiana Mpango wa matumizi Bora ya Ardhi Wilayani Kilombero Mkoani Morogoro.

Wajumbe na Viongozi wa Programu ya Kuwezesha Umilikishaji Ardhi wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kushiriki Semina ya Uhamasishaji wa Ujenzi wa Masjala za Ardhi zaVijiji, Kukabidhi Mpango wa matumizi Bora ya Ardhi wa Wilaya na kutambulisha timu ya upimaji Mipaka iliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi Mkoani Morogoro.

Ili kuhakikisha Changamoto hiyo inabaki Historia, mradi wa kuwezesha Urasimishaji Ardhi umetua Wilayani Kilombero, ukiwa na Shabaha ya kupima mipaka ya Vijiji 20,na kupatiwa Hatimiliki ya Ardhi ili kuondoa Migogoro hiyo.

MARY MAKONDO ni Kaimu kamishna wa Ardhi nchini akizungumza Wilayani humo, ameeleza umuhimu wa Mradi huo unaofadhiliwa kwa Dola Milioni 15.2, wenye lengo la Kurasimisha Ardhi ili imnufaishe Mwananchi wa Masikini na kuondoa Migogoro isiyo na tija.

Zoezi hilo la Urasimishaji Ardhi na Utoaji wa Hatimiliki za Kimila litaenda sambamba na Ujenzi wa Masjala za Ardhi kwenye Vijiji vilivyopo kwenye mpango wa LTSP,lengo likiwa ni kuweka sawa kumbukumbu za Mikataba inayohusu Ardhi.

Itakumbukwa Mradi huu ni matokeo ya Mkutano wa wakuu wa nchi zenye Uchumi Mkubwa Duniani, ambapo Tanzania ilialikwa kuhudhuria kama mshiriki, ambako kulizinduliwa Ushirikiano kati yake na Kundi la G8 kuhusu uwazi kwenye sekta ya ardhi.
Kiongozi wa Urasimishaji kutoka Mpango wa Land Tenure Support Programme, Swagile Msananga akifafanua Jambo kuhusu Masjala za Ardhi za Vijiji katika Semina ya uhamasishaji wa Ujenzi wa masijala hizo iliyofanyika katika Ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero Mkoani Morogoro.
Kaimu mkurugenzi mkuu tume ya taifa ya Matumizi ya ardhi Dkt Stephen Nindi (kushoto) na Kaimu Kamishna wa Ardhi Bi Mary Makondo wakikabidhi mpango wa matumizi Bora ya ardhi ya wilaya kwa kaimu Mkurugenzi wa Ardhi wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi, Gerald Kauki (Kulia) wakati wa Semina ya Uhamasishaji wa Ujenzi wa Masijala za Ardhi za Vijiji, Sambamba na kutambulisha timu ya upimaji Mipaka katika Halmashauri ya Wilaya hiyo mkoani Morogoro.
Timu ya Maafisa kutoka Makao Makuu ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi (Waliosimama) iliyowasili Mkoani Morogoro kwa kazi ya Kupima na kumilikisha Ardhii takayofanyika katika Wilaya za Ulanga, Malinyi na Kilombero.

MSIMU MPYA LIGI KUU YA VODACOM 2016/2017 WAANZA KWA MSISIMKO.

$
0
0
 Kwenye picha baadhi ya wafanyakazi kutoka Idara ya Masoko ya Vodacom Tanzania wakiongozwa na Mkuu wa Idara hiyo Nandi Mwiyombella (katikati) walifika kushuhudia mechi kati ya Simba na Ndanda.

 Endele Kufuata kurasa zetu kwenye mitandao ya kijamii ukitumia #VPL2016 uweze kutabiri matokeo ya mechi na kupata taarifa zaidi kuhusu ligi kuu ya Vodacom. Pia kupata live match updates kila wiki. 

Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara VPL ilifunguliwa rasmi wikiendi iliyopita kwa mechi 6 kuchezwa katika viwanja tofauti. Katika mechi ya Simba dhidi ya Ndanda FC tulishuhudia Simba ikipata ushindi wa magoli 3 – 1 huku winga mpya wa Simba, Shiza Kichuya akifanikiwa kufunga bao zuri kuhitimisha karamu ya magoli 3.
Kule Morogoro, Mtibwa Sugar wakiwa uwanja wa nyumbani waliduwazwa na Ruvu Shooting baada ya kupokea kichapo ch goli moja bila. Akizungumza siku moja baada ya mechi hiyo Kocha wa Mtibwa Sugar Salum Mayanga alisema kipigo hicho kimewazindua usingizini hivyo wanajipand zaidi kwa mechi zijazo. Azam FC ilinusurika kupokea kipigo kutoka kwa African Lyon ambapo John Bocoo aliisawazishia timu hiyo katika dakika za majeruhi. Katika mchezo huo African Lyon walionekana kucheza kandanda safi, “hii timu inacheza kana kwamba ilikuwa inacheza ligi kuu kwa muda mrefu sana, itasumbua kweli kweli” alisikika mmoja wa watazamaji akifuatilia mechi hiyo kupitia “Kibanda Umiza” maeneo ya Kijitonyama. 
Nae kocha mkuu wa klabu ya Azam FC ambayo mwaka huu imefanikiwa kuchukua Ngao ya Jamii alisema kuwa anahitaji muda zaidi ili kukisuka kikosi chake na kucheza kupitia mifumo wanayoendelea kuwafundisha wachezaji wa timu hiyo. 
“Kwa sasa tunafanya tathmini ya mchezo uliopita, kutoa makosa na kurekebishana pale tulipokosea, tukimaliza hapo kwa wiki hii tutaanza kujipanga kwa mchezo ujao (Majimaji), lakini cha kwanza tunaangalia yali yaliyotokea katika mchezo wa kwanza, mapungufu yalikuwa wapi na nani anapaswa kufanya nini,” alisema. 
Mechi ya Stand United na Mbao FC timu iliyopanda daraja haikufanikiwa kutoa mshindi na kule Songea timu ya Majimaji ilikubali kupokea kichapo cha goli 1 – 0 kutoka kwa Tanzania Prisons. Hii leo kutakuwa na mchezo mmoja utakaochezwa jijini Mwanza ambapo Toto Africans itamenyana na Mwadui FC. Msimu uliopita mechi mbili za ugenini na nyumbani za timu hizi ziliisha kwa ushindi wa goli 1 bila huku kila timu ikitamba kwenye uwanja wake.
 Vinara wa Ligi Kuu ya Vodacom msimu uliopita hawakucheza mechi yao ya ufanguzi ili kupata nafasi ya kujiandaa na mechi ya Shirikisho dhidi ya TP Mazembe. Yanga itaanza kampeni ya msimu huu hapo Jumamosi kwa kucheza na African Lyon.

WAKURUGENZI WAHAMASISHENI WALIMU KUJIENDELEZA KIELIMU-MAJALIWA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Wakurugenzi wa halmashauri na Maofisa Elimu nchini kutowaondoa katika nyadhifa zao Waratibu wa Elimu Kata na Wakuu wa shule za sekondari wasiokuwa na shahada, walimu wakuu wa shule za msingi wasiokuwa na diploma badala yake wawahamasishe kwenda kusoma.

“Maofisa Elimu na Wakurugenzi msije mkawaondoa wale walimu wakuu kwa zile sifa nilizosema bado muda ukifika tutatangaza.Msije mkawakurupusha sasa hivi waacheni waendelee na kazi zao tutatoa muda ili wajipange viziri,” aliema.

 Agosti 20 mwaka huu Waziri Mkuu alisema Waratibu wa Elimu katika ngazi ya Kata na Wakuu wa shule za sekondari wanatakiwa kuwa na shahada huku walimu wakuu kwenye shule wanatakiwa kuwa na diploma.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana jioni (Jumatano, Agosti 24, 2016) wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kiwanja cha Mandela katika jimbo la Sumbawanga mjini.

Alisema Mratibu wa Elimu katika ngazi ya Kata ni lazima awe na shahada ili aweze kutekeleza majukumu yake ya kusimamia utolewaji wa elimu katika shule za sekondari na msingi.

“Wakuu wa shule za sekondari na waratibu wa elimu kata wasiokuwa na shahada wasiondolewe katika nafasi zao kabla ya kupewa nafasi ya kwenda kujiendeleza kwa masomo ili waweze kuwa na vigezo vya kuendelea kushika nyadhifa hizo,” alisema.

Alisema katika kuboresha maslahi ya walimu Serikali imetenga zaidi ya sh. bilioni tano kwa mwezi ambazo ni posho ya madaraka. Waratibu Elimu Kata wanapewa sh 250,000 kwa mwezi huku Wakuu wa shule za sekondari na walimu wakuu katika shule za msingi wanapewa sh. 200,000.

Waziri Mkuu alisema badala ya kuwaondoa kwenye nyadhifa hizo ni vema Wakurugenzi wakawahamasisha walimu hao kwenda kusoma ili na wao wanufaike na posho ya madaraka iliyoanza kutolewa na Serikali hivi karibuni.

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu amewataka wazazi na walezi kwenda kuwaandisha watoto wenye umri wa miaka mitano katika shule za awali ambapo watapata fursa ya kujengewa msingi mzuri wa masomo kabla ya kuanza darasa la kwanza.

Pia aliagiza shule zote za msingi nchini zisizokuwa na madarasa ya awali kuhakikisha waanzisha madarasa hayo haraka na kuanza kutoa elimu hiyo.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
ALHAMIS, AGOSTI 25, 2016.
Viewing all 110171 articles
Browse latest View live




Latest Images