Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110014 articles
Browse latest View live

TAIFA STARS KUCHEZA NA THE SUPER EAGES SEPTEMBA 3 BADALA YA SEPTEMBA 2, 2016 HUKO NIGERIA

$
0
0
Shirikisho la Mpira wa Miguu Nigeria (NFA), limesogeza mbele kwa siku moja mchezo kati ya timu ya taifa ya Nigeria ‘The Super Eagles’ na Tanzania ‘Taifa Stars’ ambako sasa utafanyika Septemba 3, 2016 badala ya Septemba 2, 2016 iliyotangazwa awali. 
Na Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa kesho anatarajiwa kutangaza kikosi ambacho atakiandaa maalumu kwa mchezo huo. Mkwasa amesema kwamba anatarajia kuita wachezaji 20 ambao atasafiri nao kwenda Nigeria kwa ajili ya mchezo huo.
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

RAIS DKT. MAGUFULI APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO KUTOKA KWA MABALOZI WA NCHI MBALIMBALI IKULU JIJINI DAR LEO

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Italia hapa nchini Roberto Mengoni Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Korea hapa nchini Kim Yong Su mara baada ya kupokea Hati zake za Utambulisho Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Balozi wa Somalia hapa nchini Mohammed Hassan Abdi mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati zake za Utambulisho.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Ireland hapa nchini Paul Sherlock Ikulu jijini Dar es Salaam.

TRL YAFANYA MABADILIKO YA RATIBA YA SAFARI ZA ABIRIA KWENDA BARA NA KUONGEZA MOJA KUANZIA SEPTEMBA 01 , 2016

$
0
0
 Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) umeamua kuongeza safari ya tatu ya treni ya abiria ya kawaida kwenda bara  ambayo itaondoka  Dar es Salaam kila Jumapili, safari ya kwanza itakuwa Jumapili hii ya  Septemba 04, 2016 saa 9 alasiri. 
Taarifa imeainisha kuwa treni hiyo ya huduma ya kawaida itakuwa na mabehewa  12 kutokea   Dar  es  Salaam ikiwa na mabehewa manane ya daraja la 3, mawili daraja la pili kulala na mawili daraja la kwanza. Katika  stesheni za Morogoro na Dodoma yataongezwa  mabehewa mawili mawili ya daraja la 3.

Aidha treni ya Deluxe imebadilishwa siku ya kuondoka badala ya Jumapili kwa sasa kuanzia Septemba Mosi, 2016 itakuwa inaondoka siku ya Alhamis saa 2 asubuhi kutoka kituo kikuu cha Dar es Salaam. 
Halikadhalika mabadiliko haya pia yataongeza safari za treni ya kwenda Mpanda kutoka Tabora badala ya 2 za sasa zitakuwa 3 kwa wiki ambazo ni Jumatatu, Jumatano na Jumamosi..

Wakati huohuo  Uongozi wa TRL umefanya uamuzi wa kihistoria wa kupeleka huduma za kuuzwa  tiketi za safari zake  mjini Kasulu ambapo kuanzia Septemba Mosi itafungua kituo cha Reli ambacho kitafanya kazi ya kuto huduma hiyo kwa  wasafari wanaotoka Kasulu mjini na maeneo ya jirani . Kwa uamuzi huo TRL imetoa nafasi za tiketi za  behewa moja la daraja la 3. Mpango pia uko mbioni  wa  kufungua kituo kama hicho siku zijazo mjini Kibondo hali itakaporuhusu kulingana na mahitaji halisi ya abiria. 
Taarifa imesisitiza kuwataka wasafiri na wananchi kwa jumla nchini  hususan wale wa Mpanda na Kibondo kutumia fursa ya kuongezewa safari na huduma kuletewa karibu kwa kufuata sheria , taratibu na  kanuni ili hatua iliyochukuliwa na TRL iwe na tija iliokusudiwa.

Aidha taarifa zaidi zinaarifu kuwa hatimaye TRL imefanikiwa kuongeza mabehewa mawili zaidi ya treni ya Pugu na kufikia idadi ya behewa 18 hadi jana Agosti 22, 2016. Ni matarajio ya Uongozi ifikapo Agosti 31, 2016 treni hiyo ya Jiji  itakuwa na mabehewa 20 iloahidi ili kupunguza msongamano unaosababishwa na abiria kuwa wengi katika safari mbili za awali katika awamu zote 2 ya asubuhi na ya jioni. 

Imetolewa na Afisi ya Uhusiano kwa Niaba ya :

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TRL,

Nd Focus Makoye Sahani,

Dar es Salaam,

Agosti 23, 2016.


SINTOFAHAMU YA VYAMA VYA SIASA INATATULIWA KWA KUKAA NA KUZUNGUMZA PAMOJA-JAJI MUTUNGI

$
0
0


MSAJILI wa vyama vya Siasa nchini, Jaji Mstaafu, Francis Mutungi 
Na Chalila Kibuda , Globu ya Jamii.
MSAJILI wa vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amesema masuala yote ya  sintofahamu kwa vyama vya siasa yatatuliwa katika meza ya majadiliano na si vinginevyo.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Jaji Mutungi amesema kuwa kuna taharuki au hofu ambayo inajengwa kwa wadau wa siasa ambayo inahitaji kuwepo mazungumzo kutokana na taratibu zinazohusu utawala bora.
Amesema kuwa utawala bora ni kuheshimu miundombinu iliyowekwa kwa kufuata sheria zake na bila kufanya hivyo miundombinu haitakuwa imetendewa haki kwa watu kufanya chochote bila kuangalia misingi iliyowekwa katika miundombinu hiyo.
Amesema kuwa Baraza la vyama vya siasa limeandaa mkutano wa wadau wa vyama vya siasa pamoja na watu wengine kuweza kuzungumza masuala mbalimbali ambayo yamejitokeza katika kipindi hiki na kupatiwa ufumbuzi wa sintofahamu miongoni mwa  wadau.
Jaji Mutungi amesema kuwa baraza la vyama vya siasa linatarajia kukaa  Agosti 29 na 30 kutaka wadau wote waweze kushiriki ili kutafuta suluhu kwa yale ambayo yamejitokeza sambamba na kuyatafutia suluhu katika kuendelea kulinda amani ya nchi yetu.
Amesema  siku zote watu wanatafuta mwafaka wa jambo lolote katika meza ya mazungumzo na kupata suluhu katika kulinda amani ya nchi yetu.
Aidha amesema suala la Chama cha Wananchi (CUF) anaangalia na kuona jinsi gani anaweza kushauri kutokana na kuwa mlezi wa vyama vyote ambavyo vimepata usajili katika ofisi yake.

Waziri Ummy Mwalimu aweka jiwe la msingi awamu ya pili ya jengo la hospitali ya Agakhan, aitaka ijenge ingine Dodoma

$
0
0
Serikali imeuomba uongozi Wa Agakhan kujenga hospitali nyingine kubwa katika mkoa Wa Dodoma ili kuendana na agizo la Rais Wa awamu ya tano Dkt.John Magufuli na kuboresha huduma bora za afya Mkoani humo. 
 Akizungumza hayo wakati wa ufunguzi wa awamu ya pili ya jengo la hospitali ya Agakhan Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu amesema kuwa Agakhan wanatakiwa wajenge hospitali nyingine kubwa mkoani Dodoma ili kueneza Huduma bora za kiafya. 
 "Kutokana na Agizo la Rais Wa awamu ya tano Dkt. John Magufuli la kuhamia Dodoma inabidi na nyinyi mjenge hospitali kule" alisema Mhe. Ummy. Mhe. Ummy ameongeza kuwa kwa kujengwa hospitali hiyo Serikali itakua iokoa shilingi billion 20 mpaka 25 kwa ajili ya wagonjwa kwenda kutibiwa nje ya nchi. 
 Aidha Mhe.Ummy amesema kuwa anaushukuru uongozi Wa Agakhan kwa kuanza kujenga jengo ilo linalogharimu Billioni 112 ili kuondoa kero kwa wagonjwa Wa magonjwa yasioambukiza na kurahisiaha huduma na matibabu bora kwa wagonjwa nchini.
 Mbali na hayo Mwenyekiti wa kamati ya bodi hospitali ya Agakhan Bi. Zahra Aga Khan amesema kuwa wanampango Wa kumaliza jengo hilo kwa ajili ya kutoa Huduma bora za kiafya nchini ili kutokomeza maradhi ya mara kwa mara. 
 "Tuna morali kubwa ya kumalizia jengo hili ili tuweze kuboresha Huduma ya afya nchini kwa kutoa tiba zenye uhakika na za kisasa" alisema Bi Zahra
Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Wazee, Jinsia na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wa tatu kulia akitia udongo kwenye kichanja cha nondo kuashiria kuzindua rasmi ujenzi wa awamu ya pili wa jengo la hospitali ya Agakhan katika uzinduzi huo uliofanyika leo jijini Dar es salaam, na wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa kamati ya bodi hospitali ya Agakhan Bi. Zahra Aga Khan.

KOREA KUSINI KUTOA BILIONI NNE KUJENGA KITUO CHA TAARIFA KATIKA HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI

$
0
0
 Wajumbe wa Bunge la Korea Kusini wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na watumishi wa Shirika la Hifadhhi za Taifa (TANAPA ) na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. 

Na Dixon Busagaga Globu ya Jamii, Kanda ya Kaskazini.

Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa kushirikiana na serikali ya Korea ya Kusini imeanza mchakato wa ujenzi wa kituo cha kimataifa cha kutunza tarifa za mienendo ya Wanyamapori kitakachojulikana kama Serengeti Internatinal Media Centre.

Kituo hicho kinachotarajiwa kugharimu zaidi shilingi bilioni nne kitajengwa katika Hifahi ya Taifa ya Serengeti .

Tayari serikali ya Korea Kusini imeshatuma wajumbe wake kuja nchini tanzania kujionea eneo kitakapojengwa kituo hicho na kukamilisha taratibu nyingine muhimu ambapo kiongozi wa wajumbe hao Park Joosung amesema mradi huo ni mwendelezo wa ushirikiano wa Korea Kusini na Tanzania katika kuimarisha uhifadhi.

Akizungumza na ujumbe huo mkuu wa hifadhi ya taifa ya serengeti Wiliam Mwakilema amesema kituo hicho kikikamilika kitaongeza chachu utalii na kitatoa fursa kwa wageni kuona aina nyingi zaidi za wanyama.

Naye mratibu wa ujenzi bw Victor Ketance amesema ujenzi utaanza mwezi october mwaka huu na unatarajiwa kumalizika baada ya miezi 14.

 Wajumbe wa Kamati ya Maendeleo kwa Afrika katika Bnge la Korea Kusini wakiwasili katika uwanja mdogo wa ndege uliopo katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. 

 Meneja Masoko wa Shirika la Hifadhi za Taifa,TANAPA,Victor Ketance akipokea ugeni wa wajumbe kutoka Bunge la Korea Kusini walipotembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa ajili ya kutizama eneo la uwekezaji wa kituo cha kisasa cha taarifa za hifadhi hiyo.

 Mkurugenzi wa Kampuni ya Kibo Safari's ,Willy Chamburo (katikati) akizungumza jambo na kiongozi wa ugeni wa Korea Kusini Won Yul Chui (kushoto) baada ya kukutana katika uwanja mdogo wa ndege uliopo Hifadhi ya Taifa ya Serengeti .kulia ni Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti William Mwakilema. 

INTRODUCING BEN SWAX FT KALA JEREMIAH

NEWS ALERT: ASKARI POLISI WANNE WAUWAWA USIKU HUU HUKO MBAGALA MMBANDEJIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0

Taarifa iliyotufikia usiku huu inaeleza kuwa, kuna tukio la kuuwawa kwa Askari Polisi wanne na raia kadhaa kujeruhiwa  lililotokea huko Mbagala Mmbande


jijini Dar.
Inadaiwa kuwa askari hao walikuwa wakibadilishana lindo katika Benki ya CRDB tawi la Mbagala Mmbande na mara wakaibuka watu wanaodhaniwa kuwa ni Majambazi na kuanza kuwashambulia kwa risasi na baada ya shambulizi wanadaiwa kuondoka na pikipiki wakielekea maeneo ya Mvuti.
ASKARI WALIOFARIKI ni
E5761 CPL YAHAYA
F4660 CPL HATIBU NA
G9544 PC TTITO.
Inasemekana kuwa tukio hilo limetokea mnamo saa 1: 30 ni katika tukio la UVAMIZI WA BANK CRDB MBANDE na inadaiwa kuwa wahalifu hao waliondoka na silaha moja aina ya SMG.
Tukio hili limetokea wakati askari wakibadilishana lindo. Mmoja aliyefariki alikuwa anaingia, mmoja alikuwa anatoka na mwingine alikuwa dereva.
Inadaiwa kuwa majambazi hayo  hayakuingia ndani ya benki. 
Gari la Polisi (Leyland Ashok) limeharibiwa  kwa risasi.
Kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam Simon Sirro amethibitisha na kusema: "Ni kweli kumetokea tukio la uvamizi hapa mbagala lakini kwa taarifa kamili ntazitoa kesho kwakuwa bado nipo eneo la tukio kwa ajili ya uchunguzi zaidi".
-------------------------------------------
"Usiku huu nimefika Mbande-Temeke,eneo lilipofanyika tukio baya la uhalifu wa kutumia silaha ambapo watu/majambazi zaidi ya saba wakiwa na silaha wamevamia eneo la Benki ya CRDB-Mbande na kuua askari 4 waliokuwa wakishuka  kwenye gari tayari kwa kupokezana lindo.
Pia wamejeruhi raia wa kawaida wawili,nimewajulia hali zao na wote wanaendelea vizuri.
Hatutaishia kulaani tu tukio hili na matukio mengine kama haya,natoa rai kwa wahusika kujisalimisha.Vilevile wananchi na raia wema tunaomba ushirikiano wenu katika vita hii ya kupambana na wahalifu hawa na wanaotuzunguka kwenye maeneo yetu."

Mwigulu Nchemba
23.08.2016






MAGAZETI YA LEO AGOSTI 24

HAKUNA MWANASIASA ATAKAYERUHUSIWA KUVURUGA AMANI - WAZIRI MKUU MAJALIWA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali itahakikisha inalinda amani ya nchi kwa gharama zozote na kamwe haitoruhusu mwanasiasa yeyote kusababisha vurugu zitakazochochea uvunjifu wa amani.

“Hatuzuii kuwa na vyama vya siasa ila haturuhusu vurugu kupitia vyama vya siasa na hakuna jambo lisilokuwa na mipaka. Mambo ya kuhamasishana kufanya vurugu hatutayaruhusu, tunataka watu wafanye kazi,” alisisitiza.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo jana jioni (Jumanne, Agosti 23, 2016) wakati akizungumza na viongozi wa dini pamoja na wazee wa mkoa wa Rukwa mara baada ya kuwasili mkoani hapa kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa Sabasaba mjini Nkansi akiwa katika ziara ya mkoa wa Rukwa, Agosti 23, 2016.

Alisema Serikali inataka Watanzania wawe na uhakika wa kuendelea kufanya kazi zao za kuwaingizia kipato na kuwaletea tija, hivyo suala la kudumisha amani ni muhimu kwani vurugu zikitokea hawatakuwa na mahali pa kukimbilia na hakuna shughuli ya maendeleo itakayofanyika.

“Suala la uhamasishaji wananchi juu ya utunzaji wa amani ni la lazima hivyo viongozi wa dini na wazee kwa pamoja tushirikiane katika kukemea vitendo vya uchochezi kwasababu vurugu zikitokea Watanzania hatuna mahali pa kukimbilia,” alisema.

Aidha, Waziri Mkuu aliwaomba viongozi wa dini kuendelea kuliombea taifa pamoja na viongozi wake kwa sababu kazi ya uongozi ni ngumu na inachangamoto nyingi.Pia aliwaagiza viongozi wa dini wa mkoa wa Rukwa kuharakisha uundwaji wa Kamati ya Amani ya mkoa huo.

Awali, Sheikh wa mkoa wa Rukwa, Sheikh Rashid Akilimali amesema madhehebu ya dini hayawezi kuvuruga amani ya nchi ila anahofu na viongozi wa vyama vya siasa kutokana na vitendo vyao vya kuhamasisha vurugu.
Baadhi ya watumishi wa Halmashauri na mkoa wa Rukwa wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye ukumbi wa St Maurus mjini Sumbawanga Agosti 23, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Kufuatia hali hiyo Sheikh Akilimali aliwaomba wanasiasa nchini kutovuruga amani kwani machafuko yakitokea watashindwa kufanya ibada mbalimbali ikiwemo kufunga mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Sheikh Akilimali alisema kwa sasa wananchi wako huru kwenda kufanya ibada misikiti na makanisani kutokana na uwepo wa amani, hivyo aliwasisitiza wanasiasa kutothubutu kuichezea amani.

“Tafadhalini wanasiasa msituharibie amani ya nchi yetu. Amani haichezewi tunaona kwa wenzetu wanavyohangaika, wanaishi kwa tabu sisi hatujazoea  kukimbia. Sisi Watanzania ni moja na tunaishi kwenye nyumba moja hivyo hatuna budi kushirikiana kuilinda amani yetu,” alisema.

Kwa upande Katibu wa Wazee mkoani Rukwa, Kanali Mstaafu, John Mzurikwao alimuomba kiongozi huyo kuwasaidia  kutatua kero mbalimbali zinazoukabili mkoa huo zikiwemo za malipo ya pembejeo kwa mawakala wa kilimo pamoja na mgogoro wa ardhi katika shamba ya Efatha.

Waziri Mkuu alisema suala la malipo kwa mawakala wa pembejeo za kilimo linafanyiwa kazi na watalipwa baada ya Serikali kukamisha zoezi la uhakiki wa madeni hayo ili kujiridhisha kama kweli wakulima wapatiwa pembejeo na kwa kiwango gani.

SALIM KIKEKE NDIO MTANZANIA WA KWANZA KUSOMA HABARI KATIKA TELEVISHENI YA KIMATAIFA KWA LUGHA MBILI (KIIGEREZA NA KISWAHILI)

$
0
0
Salim Kikeke anakuwa mtangazaji wa kwanza kutoka Tanzania kusoma habari (News anchor) katika Televisheni ya kimataifa, na kwa lugha mbili- Kiingereza na Kiswahili - bilingual presenter. BBC Focus on Africa na BBC Dira ya Dunia ya BBC Swahili TV.

WAZIRI MKUU MAJALIWA AFUNGUA RASMI WODI MPYA YA HOSPITALI TEULE YA NKASI MKOANI RUKWA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua pazia kuashiri ufunguzi rasmi wa wodi mpya ya Hospitali Teule ya Wilaya ya Nkansi, katika ziara ya mkoa wa Rukwa Agosti 23, 2016. nyuma yake ni mkewe Mary na kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Said Mtanda.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mkewe Mama Mary Majaliwa kwa pamoja na Mkuu wa mkoa wa Rukwa, Zelote Stephene na Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, wakikata utepe kuashiri ufunguzi rasmi wa wodi mpya ya Hospitali Teule ya Wilaya ya Nkansi, katika ziara ya mkoa wa Rukwa Agosti 23, 2016. nyuma yake ni mkewe Mary na kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Said Mtanda.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua vitanda katika wodi mpya ya Hospitali Teule ya Wilaya ya Nkansi baada ya kuizindua akiwa katika ziara ya mkoa wa Rukwa Agosti 23, 2016. Kushoto kwake ni mkewe Mary na wapili kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Rukwa, Zelote Stephene.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitoka kwenye Hospitali Teule ya wilaya ya Nkansi baada ya kufungua wodi akiwa katika ziara ya mkoa wa Rukwa Agosti 23, 2016.  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MAHAKAMA YA ARDHI KUJA NA MIKAKATI YA KUONDOSHA MASHAURI YA MUDA MREFU

$
0
0
Na Mary Gwera.

Mahakama ya Tanzania ‘Ardhi ni mali, ardhi ni uhai, ardhi ni uchumi,’ haya ni maneno yaliyosemwa na Mhe. Gad Mjemmas aliyekuwa Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu, Divisheni ya Ardhi. Hii ni kutokana na ukweli kuwa migogoro ya ardhi inazidi kushika kasi kila kukicha.

Aliongeza kuwa kutokana na umuhimu wa ardhi kwa maana ya kuwa na madini ndani yake, matumizi ya barabara, nyumba na miundombinu mingine kumekuwa na uhitaji mkubwa wa ardhi kwa ajili ya matumizi mbalimbali kama kilimo, ujenzi na kadhalika.

Mhe. Jaji Mjemmas anaendelea kufafanua kuwa kufuatia migogoro ya ardhi iliyokuwa ikiongezeka kila kukicha, Serikali iliona kuna haja/umuhimu wa kuundwa Tume ya Shivji iliyokuwa ikitambulika kama ‘Presidential Commission of Inquiry into Land Matters’ lengo la Tume hii ilikuwa ni kuja na mikakati ya jinsi gani ya kutatua migogoro ya ardhi.
Mhe. Jaji Gad Mjemmas, aliyekuwa Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu- Divisheni ya Ardhi (katikati), Mhe. Frank Mahimbali, Naibu Msajili, Mahakama Kuu, Divisheni ya Ardhi (kushoto) na Bw. Leonard Magacha, Mtendaji, Mahakama Kuu, Divisheni ya Ardhi wakiwa katika kikao pamoja na wadau wa Mahakama, lengo likiwa ni kupata maoni ya pamoja ya kuboresha huduma, katika kikao hicho walikubaliana kushirikiana kwa kufanya kazi kwa pamoja kuondoa kero mbalimbali.

Pamoja na mikakati mingi waliyokuja nayo, Tume hii pia ilipendekeza ianzishwe Divisheni maalum ya Mahakama kwa ajili ya kushughulikia mashauri ya ardhi, yaanzishwe pia Mabaraza ya Ardhi ya Wilaya pamoja na vijiji hii yote ililenga katika kutatua migogoro ya ardhi.

Hata hivyo; Mhe. Jaji Mjemmas aliongeza kuwa kufuatia ongezeko la mashauri na changamoto mbalimbali, Mhe. Jaji Mkuu alitoa waraka wa kuruhusu kesi za ardhi kusikilizwa na Jaji yeyote wa Mahakama Kuu ili kuweza kupunguza msongamano wa mashauri.
Mmoja wa wadau wa Mahakama (Mawakili) akieleza jambo katika kikao maalum kati ya Mahakama ya Ardhi pamoja na wadau wake (Mawakili, wadaawa n.k), kikao hicho kililenga katika kuainisha changamoto zilizopo katika usikilizaji wa Mashauri ya ardhi na mikakati ya kuzitatua ili kuondokana na mlundikano wa mashauri ya ardhi.

Jaji Mfawidhi huyo, aliainisha mikakati mbalimbali ambayo Mahakama ya Ardhi imejiwekea katika kuondoa mlundikano wa mashauri katika Mahakama hiyo.

”Mpaka kufikia mwaka jana 2015, divisheni hii ya ardhi ilikuwa na mashauri yenye umri kati ya miaka mitano (5) hadi kumi (10) 526, hivyo katika hili sisi Majaji 9 wa Mahakama ya ardhi pamoja na Wasajili tulijiwekea mikakati thabiti ya kufikia lengo la kumaliza mlundikano huu,” alisema Jaji Mjemmas.

Kuainisha matatizo ya kesi hizo: Katika hili Mhe. Mjemmas, alisema waliainisha matatizo ya kesi  hizo kwa kuchambua jalada kwa jalada ili kujua nini tatizo la kila kesi, pia walifanya uhakiki wa majalada (stock taking) kujua jala husika lipo kwa nani na kuwashirikisha Mawakili kujitoa ili kuweza kufanikisha  zoezi la kumaliza mashauri hayo.
Mjumbe akitoa maoni yake katika kikao hicho cha wadau.

Kuandaa vikao maalum ‘special session’; “ili kuweza kujikita katika kushughulikia mashauri haya, tuliandaa vikao maalum kuanzia Machi 16, 2015 hadi Aprili 30, 2015 lengo ili kufikia malengo tuliyojiwekea ya kumaliza mlundikano wa mashauri,” alifafanua, Jaji Mjemmas. 

MBUNGE MAHMOUD MGIMWA AKABIDHI MIFUKO 100 YA SARUJI NA NDOO KUMI ZA RANGI KWA SHULE YA SEKONDARI YA MDABULO.

$
0
0

Na Fredy Mgunda,Mufindi.


MBUNGE wa jimbo la Mufindi kaskazini Mahamood Mgimwa amekabidhi mifuko 100 ya saruji na ndoo kumi za rangi, zenye ujazo wa lita ishirini kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za Serikali ya ya kukarabati majengo ya shule ya sekondari ya Mdabulo iliyopo Kijiji cha Mdabulo wilayani mufindi.

Akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini Mdabulo, alisema kuweza kujenga jamii imara ni lazima kuhakikisha elimu inapewa kipaumbele cha pekee.

“Sina budi kuunga mkono juhudi zenu za ujenzi wa Shule ya sekondari ya Mdabulo, ambayo imejengwa kwa nguvu za wananchi, nami kama mwakilishi wetu ninaungana nanyi kwa dhati na katika hili napenda kukabidhi mifuko ya saruji.huo.Alisema lengo la kutoa msaada huo, ni kutokana na shule hiyo kuwa chakavu katika maeneo muhimu kama kwenye mabweni na bwalo ambalo hutumiwa na wanafunzi kwa ajili ya chakula.

“Baada ya kupata taarifa hizi, nimeamua kuja na mkuu wa wilaya pamoja na mkurugenzi ili waangalie namna ya kufanya marekebisho katika madarasa pamoja na mabweni ya shule hii na nimewaagiza wahakikishe wanakarabati shule hiyo na iwe kwenye viwango vinavyotakiwa,” alisema Mgimwa.Mgimwa aliwataka wanafunzi wasome kwa bidii ili waweze kufaulu na si kusoma ili kupata ajira kama ilivyozoeleka kwa watu wengi kwani serikali inafahamu changamoto ya ajira iliyopo.

Hata hivyo aliwataka wazazi na walezi kuwalea watoto katika maadili mema huku wakisaidiana na walimu kwa kushirikiana katika nyanja ya elimu ili kupanua wingo wa ufaulu kwa wanafunzi.“Kwa kipindi cha siku kadhaa nimekuwa na ziara katika katika jimbo langu kwa lengo la kutimiza ahadi zangu pamoja na kusikiliza kero ya wananchi na kero moja wapo ni wazazi kutowajali  wanafunzi wala kutojua maendeleo ya watoto wao pindi watokapo shule”alisema Mgimwa.

Naye Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Geogrge Mgomba, aliwataka wanafunzi wake kusome kwa ajili ya ajira binafsi na si kutegemea ajira kutoka serikalini kwa kuwa serikali ina mzigo mkubwa.“Wanafunzi mnatakiwa msome kwa bidii na msitegemee ajira kutoka serikalini, mtafute ajira binafsi au kujiajiri wenyewe,”alisema



Kwa upande wake,mkuu wa wilaya ya mufindi Jamhuri Wiliamu, alimshukuru mbunge huyo kwa kuunga mkono juhudi za wananchi za kuinua sekta ya elimu katika wilaya hiyo.
MBUNGE wa jimbo la mufindi kaskazini Mahamood Mgimwa akihutubia wananchi waliofika kwenye mkutano uliyafanyika kwenye shule ya sekondary Mdabulo. 
Baadhi ya wananchi waliokuwa wamehudhuria mkutano huu wa mbunge wa jimbo la mufindi kaskazini mahamood mgimwa
 MBUNGE wa jimbo la mufindi kaskazini Mahamood Mgimwa akikabidhi mifuko 100 ya saruji na ndoo kumi za rangi zenye ujazo wa lita ishirini kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za Serikali ya ya kukarabati majengo ya shule ya sekondari ya Mdabulo kwa uongozi wa wilaya ya mufindi.

Airtel Money yagawa billion 3 kwa wateja na Mawakala

$
0
0
 Kulia Meneja wa Airtel Money Bw, Asupya Nalingigwa akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) jinsi Mr Money wa Airtel Money atakavyogawa faida ya shilingi billion 3 kwa wateja wa Airtel Money na mawakala wake nchi nzima ikiwa ni faida yao kutokana na kutumia Airtel Money kuanzia Januari hadi juni mwaka huu kushoto ni Meneja wa uhusiano wa Airtel Bw, Jackson Mmbando jana.
 Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu mpango wa kugawa gawio la faida ya shilingi billion 3 kwa wateja wa Airtel Money na mawakala wake nchi nzima ikiwa ni faida yao kutokana na kutumia Airtel Money kuanzia Januari hadi juni mwaka huu. Kulia ni Meneja wa Airtel Money Bw, Asupya Nalingigwa jana.


Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imetoa gawio la faida la kila kiasi cha shilingi billion 3 kwa wateja wake wa Airtel Money na mawakala wakubwa na wadogo nchi nzima

Airtel imetoa gawio la faida kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi juni mwaka huu ambapo kila mteja atalipwa sehemu ya faida kulingana na kiasi cha salio lake katika akaunti yake ya Airtel Money kila siku

Akiongea na waandishi wa habari , Meneja Uhusiano wa Airtel Bw, Jackson Mmbando alisema “Tunayofuraha kutoa gawio la faida la shilingi bilioni 3 kwa wateja wetu na wakala nchi nzima. Tunaamini gawio hili la faida litawawezesha wateja wetu kutatua mahitaji yao ya kifedha na hivyo kuthibitisha dhamira yetu ya kuendelea kutoa huduma za kifedha”

“Tumejipanga kuwawezesha wateja wetu kwa kupitia huduma na bidhaa tunazozitoa. huduma ya Airtel Money imelenga kuleta unafuu na kuongeza upatikanaji wa huduma za kifedha katika maeneo mbalimbali nchini hususani ya maeneo ya pembezo mwa nchi. Aliongeza Mmbando

Mpaka sasa Airtel imeshatoa kiasi cha shilingi billion 10 kwa wateja na mawakala wa Airtel money tangu  2014.

Huduma ya Airtel Money inawawezesha wateja kufanya miamala mbalimbali ikiwemo kutuma na kupokea pesa, kulipia bili, kununua vifurushi, kuamisha pesa na kutoa pesa kutoka benki pamoja na kutoa mikopo isiyo na dhamana kupitia huduma ya Airtel Timiza ambayo inatoa mikopo ya haraka, rahisi kwa wateja na mawakala.


Mpaka sasa mtandao wa mawakala 50,000 wa Airtel Money nchini Tanzania wanaweza kutumia huduma hii. Theluthi moja ya mawakala wote wa Airtel Money hutumia Timiza, na baadhi ya mawakala sasa hivi wanakidhi vigezo vya kupata mikopo hadi Shilingi milioni moja. 

ATAKAYEVAMIA MSITU FAINI MIL. 70, JELA MIAKA SABA- WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema mtu yeyote atakayekutwa na hatia ya kuvunja sheria kwa kuvamia na kuharibu mazingira ya msitu wa Mfili ambao ndiyo chanzo pekee cha maji cha Wilayani Nkasi atatozwa faini ya sh. milioni 70 pamoja na kifungo miaka saba jela.

Katika kuhakikisha hatua zinachukuliwa Waziri Mkuu amemkabidhi mkuu wa wilaya ya Nkasi, Said Mtanda kitabu cha sheria kitachomuangoza katika kuwachukulia hatua wale wote watakaobainika kufanya uharibifu katika chanzo hicho cha maji.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo jana jioni (Jumanne, Agosti 23, 2016) wakati akizungumza na wananchi wa mji Mdogo wa Namanyere katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanya vya Sabasaba.

“Mkuu wa wilaya akishindwa kuwachukulia hatua za kuwaondoa wananchi na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria watu wote waliovamia maeneo ya hifadhi za misitu na kuanzisha makazi au kufanya shughuli za kijamii naye atakuwa jipu,” alisema.

Waziri Mkuu alisisitiza kuwa maeneo mengi nchini yanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa maji baada ya wananchi kuvamia katika vyanzo vya maji na kufanya shughuli za kibinadamu hivyo kusababisha vyanzo vingi kukakuka

“Serikali haitakubali kuona mtu anaharibu chanzo cha maji. Wananchi mnatakiwa kuwa walinzi wa maeneo hayo na atakayekutwa anachunga mifugo, analima, kukata nyasi au kufanya shughuli zozote za kijamii ndani ya maeneo hayo atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria,” alisema.

Awali Waziri Mkuu alikagua mradi wa upanuzi wa bwawa la maji Mfili ambalo mwanzo lilikuwa na ujazo wa lita 1,500 ambapo litakapokamilika litakuwa na ujazo wa lija 248,067 hivyo kuwezesha wakazi 82,689 kunufaika.

Akizungumza kwenye eneo la mradi mara baada ya Waziri Mkuu kuwasili, Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya ya Nkasi, Julius Kaondo alisema hadi kukamilika mradi huo unatarajiwa kugharimu sh trilioni 1.011 ambapo Wizara ya Maji na Umwagiliaji imetoa sh. milioni 500 na OOfisi ya Rais TAMISEMI itatoa sh. milioni 500.

Mkurugenzi huyo alisema mradi unakabiliwa na changamoto ya ukosefu umeme ppamoja na mitambo ya kusukuma maji kwa kutumia nishati ya umeme, ambapo aliiomba Serikali kuipatia halmashauri hiyo sh. milioni 222.576 ikiwa ni gharama za kupeleka umeme kwenye eneo la mradi na kununua mitambo.


Mbali na kutembelea mradi wa upanuzi wa bwawa, pia Waziri Mkuu alitembelea hospitali teule ya wilaya ya Nkasi na kuzindua wodi mpya yenye uwezo wa kulaza wagonjwa 72 kwa wakati mmoja

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU, JUMATANO, AGOSTI 24, 2016.

Salvatory Edward, kiungo TP Mazembe kusaka vipaji Dar J’mosi

$
0
0
KIUNGO wa zamani wa timu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Ngawina Ngawina, pamoja na kiungo wa zamani wa Yanga, Salvatory Edward wameanzisha kituo cha kuibua vipaji vya wanasoka chipukizi chini ya umri wa miaka 17 na kuviendeleza.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Ngawina alisema kituo chao kinaitwa Kambiasso Sports na kwamba kwa kuanzia Jumamosi wiki hii watafanya kliniki maalum ya kusaka vipaji hivyo kwenye Uwanja wa Tandika Mabatini, Dar es Salaam, dhamira yao kubwa ikiwa ni kuhakikisha wachezaji wenye vipaji wanaendelezwa na kutafutiwa timu.

“Kila mzazi mwenye mtoto ambaye anaamini ana kipaji cha soka na anahitaji aendelezwe, amlete mwanae Tandika Mabatini Jumamosi Agosti 27,  ajitahidi saa mbili asubuhi awe ameshafika, kwani ndiyo muda tutakaoanza.

“Kliniki yetu itaendeshwa na makocha mahiri, ambao wana leseni za ukocha kutoka CAF (Shirikisho la Soka Afrika), ili kufanya hili jambo kiuweledi zaidi na kupata vijana wenye sifa,” alisema Ngawina.

Alisema dhamira yao ni kupata vijana wengi wenye vipaji kadri iwezekanavyo na kwamba suala la idadi itategemea na watakavyoona siku hiyo, lakini dhamira yao ni kuwa na vijana wasiopungua 30, lakini si lazima wote wapatikane Dar es Salaam, wataenda hadi mikoani.

Aliwataja watakaoendesha mshujo huo licha ya yeye na Salvatory, pia atakuwepo kocha Kennedy Mwaisabula, ambaye amepata kufundisha timu mbalimbali nchini ikiwemo Yanga.

Mwingine ni kipa wa zamani wa timu mbalimbali ikiwemo Simba ya Dar es Salaam na Ferroviario De Maputo ya Msumbiji, Muharami Mohammed ‘Shilton’, ambaye kwa sasa ni kocha wa makipa wa timu ya Taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ‘Serengeti Boys’ . Pia atakuwepo kocha mwingine wa makipa Terry Muhorel.

“Soka si kama paa la nyumba kwamba siku zote linakuwa juu tu. Soka inaanzia chini na ndiko tunakotaka twende,” alisema Ngawina.

Kwa upande wake Salvatory alisema dhamira yao ni kuwa na kituo ambacho kitakuwa hazina ya nchi kwa wachezaji wa siku za usoni, lakini pia kiwe kitovu cha timu mbalimbali kuchukua wachezaji.

“Tunaamini vijana wetu wakishaiva tutawauza timu mbalimbali za ndani ya Tanzania na nje, kwani kituo kina uhusiano mzuri na watu mbalimbali waliopo hapa nchini na hata nje ya nchi,” alisema Salvatory.

 “Tunaosimamia jambo hili tumecheza mpira kwa kiasi cha kutosha, tumesomea ukocha, tunajua nini cha kufanya kuendeleza vijana wetu,” alisema.

Aliwaomba wachezaji chipukizi wa umri huo wanaoamini wana uwezo wajitokeze siku hiyo ili kuwania nafasi ya kuwepo katika kituo hicho ambacho kitakuwa Temeke, Dar es Salaam.

KOREA KUSINI KUTOA BILIONI NNE KUJENGA KITUO CHA TAARIFA KATIKA HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI

$
0
0
 Wajumbe wa Bunge la Korea Kusini wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na watumishi wa Shirika la Hifadhhi za Taifa (TANAPA ) na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. 

Na Dixon Busagaga Globu ya Jamii, Kanda ya Kaskazini.

Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa kushirikiana na serikali ya Korea ya Kusini imeanza mchakato wa ujenzi wa kituo cha kimataifa cha kutunza tarifa za mienendo ya Wanyamapori kitakachojulikana kama Serengeti Internatinal Media Centre.

Kituo hicho kinachotarajiwa kugharimu zaidi shilingi bilioni nne kitajengwa katika Hifahi ya Taifa ya Serengeti .

Tayari serikali ya Korea Kusini imeshatuma wajumbe wake kuja nchini tanzania kujionea eneo kitakapojengwa kituo hicho na kukamilisha taratibu nyingine muhimu ambapo kiongozi wa wajumbe hao Park Joosung amesema mradi huo ni mwendelezo wa ushirikiano wa Korea Kusini na Tanzania katika kuimarisha uhifadhi.

Akizungumza na ujumbe huo mkuu wa hifadhi ya taifa ya serengeti Wiliam Mwakilema amesema kituo hicho kikikamilika kitaongeza chachu utalii na kitatoa fursa kwa wageni kuona aina nyingi zaidi za wanyama.

Naye mratibu wa ujenzi bw Victor Ketance amesema ujenzi utaanza mwezi october mwaka huu na unatarajiwa kumalizika baada ya miezi 14.

 Wajumbe wa Kamati ya Maendeleo kwa Afrika katika Bnge la Korea Kusini wakiwasili katika uwanja mdogo wa ndege uliopo katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. 

 Meneja Masoko wa Shirika la Hifadhi za Taifa,TANAPA,Victor Ketance akipokea ugeni wa wajumbe kutoka Bunge la Korea Kusini walipotembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa ajili ya kutizama eneo la uwekezaji wa kituo cha kisasa cha taarifa za hifadhi hiyo.

 Mkurugenzi wa Kampuni ya Kibo Safari's ,Willy Chamburo (katikati) akizungumza jambo na kiongozi wa ugeni wa Korea Kusini Won Yul Chui (kushoto) baada ya kukutana katika uwanja mdogo wa ndege uliopo Hifadhi ya Taifa ya Serengeti .kulia ni Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti William Mwakilema. 

RAIS DKT. MAGUFULI AMTEUA DKT. MODESTUS FRANCIS KIPILIMBA KUWA MKURUGENZI MKUU WA USALAMA WA TAIFA

$
0
0

Dkt. Modestus Francis Kipilimba.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 24 Agosti, 2016 amemteua Dkt. Modestus Francis Kipilimba kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Kabla ya uteuzi huo Dkt. Modestus Francis Kipilimba alikuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Dkt. Modestus Francis Kipilimba anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Rashid Othman ambaye amestaafu.

Dkt. Modestus Francis Kipilimba ataapishwa leo mchana tarehe 24 Agosti, 2016 Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Aidha, Rais Magufuli amemteua Bw. Robert Msalika kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Kabla ya uteuzi huo Bw. Robert Msalika alikuwa Afisa Ubalozi katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Bw. George Madafa kuwa Balozi na nchi atakayopangiwa, itatajwa baadaye.

Wakurugenzi na Naibu Wakurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa waliopo wanaendelea na nafasi zao.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es Salaam
24 Agosti, 2016

DON'T MISS THIS OUT!

Viewing all 110014 articles
Browse latest View live




Latest Images