Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110171 articles
Browse latest View live

MKUU WA WILAYA YA KIGAMBONI AONGOZA WANANCHI WAKE KATIKA ZOEZI LA USAFI WA MAZINGIRA LEO

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni,Hashim Mgandilwa, akitoa maelekezo kwa wakazi wa wilaya hiyo waliojitokeza kushiriki kazi za usafi ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli la kufanya usafi kila ifikapo Jumamosi ya mwisho wa mwezi.
Mbunge wa Kigamboni Faustine Ndugulile (kushoto) akiwa na Mkuu wa Wilaya hiyo,Hashim Mgandilwa (wapili kulia) wakishiriki kazi za usafi eneo la Feri Kigamboni jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli la kufanya usafi kila ifikapo Jumamosi ya mwisho wa mwezi.
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni,Hashim Mgandilwa akizungumza na waandishi wa habari.
Mmoja ya watoto waliojitokeza kwenye kazi hiyo ya kufanya usafi.


MASAUNI AONGOZA MSAFARA WA MABALOZI WA USALAMA BARABARANI KUJIFUNZA KAZI ZA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI, JIJINI DAR

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na Mabalozi wa Usalama Barabarani pamoja na Askari na Maafisa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mara baada ya Naibu Waziri huyo na Mabalozi hao kuonyeshwa shughuli mbalimbali zinazofanywa na Jeshi hilo. Katika hotuba yake Masauni aliwataka Mabalozi hao waendelee kushirikiana na Wizara yake katika kupambana na ajali nchini. Tukio hilo lilifanyika katika Kituo cha Zimamoto, Mkoa wa Ilala, jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto (meza kuu), Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo, Thobias AndengenyeNaibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (wapili kulia) akipokea maelezo kutoka kwa Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ambaye pia ni Kamanda wa Jeshi hilo Mkoa wa Ilala, Ully Mbuluko jinsi chumba cha mawasiliano kinavyopokea miito mbalimbali ya matukio ya majanga. Masauni aliongoza msafara wa Mabalozi wa Usalama Barabarani ambao walifanya ziara ya kujifunza kazi za Jeshi hilo katika Kituo cha Zimamoto, Mkoa wa Ilala, jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akiangalia Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakizima moto wakati tukio la moto linapotokea. Masauni aliongoza msafara wa Mabalozi wa Usalama Barabarani ambao walifanya ziara ya kujifunza kazi za Jeshi hilo katika Kituo cha Zimamoto, Mkoa wa Ilala, jijini Dar es Salaam.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

MKWASA AAHIRISHA KAMBI TAIFA STARS

$
0
0
Kutokana na maombi ya klabu nyingi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kutaka kuandaa wachezaji kwa ajili ya Ligi Kuu msimu unaoanza sasa, umemlazimu Kocha Mkuu timu ya Mpira Tanzania ‘Taifa Stars’, Charles Boniface Mkwasa kuahirisha kambi iliyokuwa ianze Jumatatu Agosti mosi, mwaka huu, imefahamika.

Wachezaji ambao Mkwasa amewaita wanatoka kwenye klabu mbalimbali na ambazo zinaongoza kutoa nyota wengi ni Simba SC, Young Africans SC, Azam FC na Mtibwa Sugar FC.

Hivyo basi, Mkwasa sasa atakuwa anafuatilia mwenendo wa nyota 24 aliowaita kwenye michezo mbalimbali ya kirafiki wa klabu hizo inayofanyika kabla ya kuanza Ligi Kuu Tanzania Bara (Pre-season matches) na michezo ya raundi ya kwanza na pili ya Ligi Kuu kabla ya kukiita tena kikosi hicho kwa ajili ya safari ya kwenda Nigeria.

Taifa Stars ina mchezo na jijini Lagos, Nigeria Septemba 2, 2016 ambao ni wa kukamilisha ratiba katika kundi G baada ya Misri kusonga mbele wakati Chad kujitoa. Wachezaji ambao Mkwasa aliwaita mapema wiki hii ni: Makipa: Deogratius Munishi, Aishi Manula, Benny Kakolanya, Mebeki: Kelvin Yondani, Aggrey Morris, Oscar Joshua, Mohamed Husein ‘Tshabalala’, Juma Abdul, Erasto Nyoni, Viungo: Himid Mao, Mohamed Ibrahim, Shiza Kichuya, Jonas Mkude, Ibrahim Jeba, Mwinyi Kazimoto, Farid Mussa, Juma Mahadhi, Hassan Kabunda, Washambuliaji: Simon Msuva, Joseph Mahundi, Jamal Mnyate, Ibrahim Ajib, John Bocco, Jeremia Juma

Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Mhe. Asia Abdallah aendelea kuhamasisha usafi kila jumamosi ya mwisho wa mwezi wilayani humo

$
0
0
 Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Mhe. Asia Abdallah (kushoto) akiwa na watumishi wa Zahanati ya Kilolo, Dr. Selemani Jumbe na Muuguzi wa zahanati hiyo ndugu Flora Hezron katika mwendelezo wa kuhamasisha usafi kila Jumamosi  ya mwisho wa mwezi Wilayani Kilolo 

WAZIRI MHAGAMA AKUTANA NA WAFANYAKAZI WA KIWANDA CHA ZFG, MKURANGA MKOANI PWANI

$
0
0
Wafanyakazi wa viwanda wilayani Mkuranga wamempongeza Mbunge wao Abdalla Ulega kwa kufanikisha kumleta Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu), Jenista Mhagama kwa lengo la kutembelea viwanda hivyo ili kujuwa kero wanazokutananazo huku akiagiza wanafanyakazi kupewa mikataba ya ajira zao.

 Waziri Jenista Mhagama ameagiza halmashauri ya wilaya ya Mkuranga kutengeneza sheria ndogo zitakazo kuwa zinasimamia masuala mazima ya kazi hususani viwandani na pia aliagiagiza viwanda hivyo kuhakikisha wanaweka awamu tatu za kuingia kazini ili kutoa fursa kwa wafanyakazi hao kufanya kazi kwa masaa nane kama sheria ya kazi inavyoelekeza kinyume na hapo lazima walipwe muda wa ziada kazini.

Jensta alitoa maagizo hayo leo wilayani hapa baada ya kufanya ziara ya kutembelea viwanda vya kuzalisha viatu na ndala aina ya yeboyebo huku akikemea vitendo vya unyanyasaji vinavyofanywa na baadhi ya wamiliki wa viwanda hivyo,ambapo ilidaiwa kuwa inafikia hatua ya kuwataka kimapenzi wanawake.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu), Jenista Mhagama akiwasili katika kiwanda cha ZFG kilichopo wilaya ya Mkuranga Kwa lengo la kusikiliza kero za wafanyakazi wa viwanda hivyo leo mkoani Pwani.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu), Jenista Mhagama akizungumza na wafanyakazi wa viwanda vya kutengeneza viatu na ndala aina ya yeboyebo kuhusu kukemea vikali vitendo vya unyanyasaji vinavyofanywa na baadhi ya wamiliki wa viwanda hivyo leo mkoani Pwani.
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega akizungumza na wafanyakazi wa viwanda vya kutengeneza viatu na ndala aina ya yeboyebo katika ziara ya kutembelea viwanda hinyo mkoani Pwani, kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu), Jenista Mhagama.
Wafanyakazi hivyo wakimsikiliza Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu), Jenista Mhagama wakati alipofanya ziara mkoani Pwani. (Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii)

RAIS DKT. MAGUFULI AENDELEA NA ZIARA YAKE KATIKA WILAYA ZA IGUNGA NA NZEGA MKOANI TABORA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 30 Julai, 2016 ameendelea na ziara yake katika Mkoa wa Tabora akitokea Mkoa wa Singida.

Kabla ya kuingia Mkoani Tabora, Rais Magufuli amezungumza na wananchi wa Mji wa Misigiri katika Wilaya ya Iramba ambapo amemuagiza Meneja wa Wakala wa Barabara katika Mkoa wa Singida kuhakikisha mkandarasi anayejenga daraja la Sibiti anarejea kazini mara moja kukamilisha ujenzi wa daraja hilo.

Rais Magufuli amesema serikali yake imejipanga kumlipa fedha mkandarasi huyo na hivyo hakuna sababu ya kuendelea kusimamisha ujenzi huo.Mkoani Tabora, Rais Magufuli amezungumza na wananchi waliosimamisha msafara wake katika vijiji vya Nanga na Ziba na amefanya mikutano ya hadhara katika miji ya Igunga na Nzega ambako amewahakikishia wananchi kuwa serikali yake itahakikisha inatekeleza ahadi zilizopo katika Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya Mwaka 2015.

Katika mkutano wa hadhara uliofanyika Igunga, Rais Magufuli amepokea malalamiko ya wananchi kuhusu kutoanza kutumika kwa kituo cha mabasi na soko na amewaagiza viongozi wa Mkoa wa Tabora kuhakikisha kituo cha mabasi cha Igunga na soko la Igunga vinaanza kutumika kuanzia Jumatatu ijayo ya tarehe 01 Agosti, 2016.

Kuhusu kero ya maji, Dkt. Magufuli amesema Tanzania imepata mkopo wa dola za kimarekani Milioni 268.35 kutoka nchini India ambazo zitatumika kutekeleza mradi wa kusambaza maji ya ziwa Viktoria katika Miji ya Tabora, Igunga, Nzega, Sikonge na Uyui pamoja na vijiji vilivyopo kandokando mwa bomba kuu kuanzia mwaka huu ambapo watu milioni moja na laki moja (1,100,000) watanufaika.

Dkt. Magufuli ameongeza kuwa pamoja na juhudi hizo Serikali imefanya usanifu na upembuzi yakinifu kwa ajili ya kutekeleza mradi wa kusambaza maji ya kutoka mto Malagarasi kwa ajili ya Miji ya Urambo, Kaliua na Nguruka pamoja na vijiji vilivyopo kandokando mwa bomba kuu ambako watu laki sita (600,000) watanufaika.

Aidha, Rais Magufuli amepiga marufuku wakulima wadogo kutozwa ushuru wa mazao watokapo na mazao mashambani.

"Ninapenda tukusanye kodi, lakini sio kukusanya kodi kutoka kwa watu masikini, mtu ametoka shambani na magunia yake mawili au hata matano halafu nyinyi mnamtoza kodi."Mimi sipendi kuwanyanyasa hawa watu wanyonge, mtu akiwa na mazao lori zima hapo sawa lakini sio kwa mtu mnyonge mwenye gunia moja" Amesema Rais Magufuli.

Kuhusu maombi ya Mkoa wa Tabora kutaka kuanzishwa Mkoa mwingine kutokana na ukubwa wa baadhi ya Wilaya Rais Magufuli amesema haioni umuhimu wa kuanzisha Mikoa mipya hapa nchini kwa sasa, na badala yake fedha zitaelekezwa katika huduma kwa wananchi kama vile maji, barabara, miundombinu na huduma za afya.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Nzega
30 Julai, 2016 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wakazi wa Igunga mkoani Tabora mara baada ya kuwahutubia Wilayani hapo.  
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wakazi wa Igunga mkoani Tabora mara baada ya kuwahutubia Wilayani hapo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwenyekiti wa Kijiji cha Nanga Wilaya ya Igunga Ndugu Masesa Kishiwa Makala kutoka Chadema wakati akiwa safarini kuelekea Nzega Mkoani Tabora.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa Ziba Wilayani Igunga mkoani Tabora hawaonekani pichani wakati akielekea Nzega Mkoani Tabora.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na wabunge wa Mkoa wa Singida wakati akiwahutubia wakazi wa Misigiri Mkoani Singida wakati akiwa njiani kuelekea Mkoani Tabora.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwasalimia wakazi wa Misigiri Mkoani Singida. PICHA NA IKULU

Ruvu Shooting yazitishia nyau Yanga, Simba VPL

$
0
0
Klabu ya mpira wa miguu ya Ruvu Shooting ya mkoani Pwani, inayoshiriki ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara(VPL) imetamba kufanya makubwa msimu ujao wa Ligi hiyo na kuwataka mabingwa wa ligi hiyo, Yanga kutarajia upinzani mkali kutoka kwao katika kupigania taji hilo.

Akizungumza kutoka Mlandizi yalipo maskani ya timu hiyo, Ofisa Uhusiano wa Ruvu Shooting, Masau Bwire, alisema kuwa malengo yao msimu ujao ni kuwa miongoni mwa timu tatu za juu na ikiwezekana kutwaa ubingwa kama walivyofanya Leicester City ya England ambayo msimu uliopita ilipanda daraja na kubeba taji.

Alisema kuwa kikosi chao kipo katika maandalizi kabambe na kwamba Jumatatu wanatarajia kutambulisha wachezaji wao, wakati watakapovaana na Mbeya City katika mchezo wa kirafiki utakaopigwa kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi.

“Baada ya kupanda daraja, matarajio yetu ni kucheza kandanda maridadi kama ilivyo kawaida yetu, lakini pia kupambana ili tuweze kuwa katika nafasi za juu, hivyo hizo timu zinazojiita kubwa, yaani Simba na Yanga, zikae chonjo,” alisema Bwire.

Alisema kwamba kwa jinsi wanavyojipanga, iwapo waamuzi watazingatia sheria zote 17 za soka, ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom msimu ujao lazima utue Mlandizi yalipo maskani yao.

Akiuzungumzia udhamini wa ligi hiyo, alisema angalau unawasaidia kufanikisha ushiriki wao wa ligi hiyo kwenda vizuri, japo wamekuwa wakikabiliana na changamoto mbalimbali.

Aliipongeza kampuni ya Vodacom Tanzania ambao ni wadhamini wa ligi hiyo kwa kuendelea kudhamini ligi hiyo na kuboresha sehemu ya udhamini wao kila mara,Pia aliitaka kampuni hiyo kuangalia kama wanaweza si tu kuwahisha kuwapa fungu la maandalizi ya ligi, lakini pia kuongeza kiwango zaidi kwa mkataba ujao ili timu nyingi zinazoshiriki ligi hiyo zisiwe zinapata usumbufu wa kujiendesha.

IGP MANGU AKAGUA MIUNDOMBINU YA KIPOLISI MKOANI SHINYANGA

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu, akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu ya kipolisi katika wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga jana, kulia ni kamanda wa Polisi mkoani humo, Muliro J. Muliro.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu, akifuatilia jambo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Mhe. Fadhil Nkhulu (aliyesimama) anayefuata ni Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab R. Telack, pamoja na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoani humo wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu ya kipolisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu, akifafanua jambo wakati alipomtembelea ofisini kwake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala mkoani Shinyanga, Mhe. Simon S. Berege (katikati), akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu ya kipolisi, kulia ni kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga, Muliro J. Muliro.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu, akiangalia kwa umakini ramani ya mipango miji inayoonesha mahala itakapokuwepo Makao Makuu ya Halmashauri ya Msalala mkoani Shinyanga, katikati (aliyevaa tai) ni Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Msalala Mhe. Simon S. Berege, wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu ya kipolisi katika mkoa wa Shinyanga. (Picha na Demetrius Njimbwi – Jeshi la Polisi).

DC IKUNGI AMTAKA DED WAKE KUMPA TAARIFA YA KUTOANZA UJENZI WA NYUMBA ZA WALIMU ZINAZOGHARAMIWA NA BENKI YA DUNIA

$
0
0
MKUU wa Wilaya ya Ikungi,Mkoani Singida amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya hiyo kuwa ifikapo Agosti mwaka huu ampatie taarifa za sababu zilizochangia Mkandarasi aliyepewa kazi ya ujenzi wa nyumba sita za shule ya msingi Minyughe kutoanza kazi kwa wakati uliopangwa ya ujenzi wa nyumba sita za walimu wa shule ya msingi Minyughe licha ya kupokea malipo ya kazi hiyo.

Mkuu huyo wa wilaya, Miraji Mtaturu alitoa agizo hilo katika Kijiji cha Minyughe, muda mfupi baada ya uzinduzi wa uchangiaji wa damu salama, mfuko wa afya ya jamii (CHF) pamoja na daftari la ufuatiliaji akina mama wajawazito uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Minyughe,wilayani Ikungi.

Kwa mujibu wa Mtaturu kuchelewa kuanza kwa shughuli ya ujenzi huo wa nyumba za walimu utasababisha pia ukamilishaji wa nyumba hizo kutokamilika pia kwa wakati na huduma kwa walimu kucheleweshwa.

Akitoa taarifa kwa Mkuu huyo wa wilaya juu ya Mkandarasi kutoanza kazi za ujenzi wa nyumba hizo licha ya kupokea fedha za malipo ya shughuli hiyo, Mbunge wa jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu alisema miradi inayofadhiliwa na Benki ya dunia yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 750 katika Halmashauri hiyo imekwamishwa na Mkandarasi licha ya kulipwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hizo za walimu, jambo linalosababisha walimu wa shule hizo kuishi katika nyumba zisizo na ubora unaotakiwa.

Hata hivyo Mbunge huyo kijana aliweka bayana kwamba baada ya kuonekana kila Mkandarasi anayetenda anatoa bei ya juu, yeye alimshawishi Waziri wa Tamisemi ili aweze kuiruhusu Halmashauri ifanye taratibu za manunuzi yenyewe ili kufanikisha shughuli hiyo iweze kufanyika mapema badala ya kuendelea kutegemea utaratibu wa wizara ambao unatumia fedha nyingi huku kukiwa na mwanya wa fedha za serikali kuliwa na baadhi ya watendaji wasiokuwa waaminifu.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo,Athumani Salumu akitoa utetezi wa sababu za kutoanza kwa shughuli hizo za ujenzi ni pamoja na ukosefu wa mchanga wa kuanzisha ujenzi wa nyumba hizo.
Mkuu wa wilaya ya Ikungi, Miraji Mtaturu akiwapungia mkono wananchi waliohudhuria kwenye uzinduzi wa uchagiaji wa damu salama,mfuko wa afya ya jamii(CHF) pamoja na daftari la ufuatiliaji akina mama wajawazito uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Minyughe,wilayani Ikungi.
Mkuu wa wilaya ya Ikungi,Mkoani Singida,Miraji Mtaturu(wa kwanza kushoto) akimkabidhi Mbunge wa jimbo la Singida Magharibi(CCM), Elibariki Kingu daftari la ufuatiliaji akina mama wajawazito,mara baada ya kuzindua mpango huo uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Minyughe,wilayani hapa.
Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Minyughe waliohudhuria uzinduzi wa uchangiaji wa damu salama lililofanyika kiwilaya katika kata ya Minyughe,tarafa ya Ihanja,wilaya ya Ikungi.


Mmoja wa wataalamu wa kitengo cha kukusanya damu salama akiwa katika jingo la darasa moja la shule ya msingi Minyughe,tarafa ya Ihanja wakati wa uzinduzi wa uchangiaji wa damu salama,mfuko wa afya ya jamii(CHF) na daftari la ufuatliji wajawazito kuhudhuria kliniki akikusanya chupa za damu zilizotolewa na wanafunzi wa shule ya sekondari ya kata aya Minyughe. (Picha Na Jumbe Ismailly).

Mpigie kura millard ayo ashinde tuzo ya blogger bora Afrika katika tuzo za AEA Marekani

$
0
0
Mtu wa Nguvu Millard Ayo anamshukuru Mungu kwa kuchaguliwa kuwania tuzo ya blogger bora Afrika tuzo za AEA Marekani. Anaomba kura yako ukipata muda. BOFYA HAPA kisha nenda namba 23

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI

MWILI WA MAREHEMU JOSEPH SENGA WAANGWA LEO JIJINI DAR

$
0
0
 Jeneza lenye Mwili wa Marehemu Joseph Senga likiwa katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri jijini Dar es salaam wakati wakimuaga kwenda Kwimba, Mwanza kwa Maziko. Mwili wa Marehemu Joseph Senga unatarajiwa kuzikwa mara baada ya kufika. 
 Jeneza la Mwili wa Joseph Senga likipewa heshima ya mwisho.
 Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Joseph Senga, aliekuwa Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, aliefariki Dunia hivi karibuni, wakati wa shughuli ya kuaga mwili huo, iliyofanyika katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri, Jijini Dar es salaam.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Joseph Senga, aliekuwa Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, aliefariki Dunia hivi karibuni, wakati wa shughuli ya kuaga mwili huo, iliyofanyika katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri, Jijini Dar es salaam.
 Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Joseph Senga, aliekuwa Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, aliefariki Dunia hivi karibuni, wakati wa shughuli ya kuaga mwili huo, iliyofanyika katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri, Jijini Dar es salaam.
 Baadhi ya Wapiga Picha wa Vyombo mbalimbali vya Habari nchini, wakibeba Jeneza la Marehemu Joseph Senga wakati wakilipeleka kwenye gari tayari kwa safari ya kwenda Kwimba, Jijini Mwanza kwa Mazishi.

WATUMISHI 3 HALMASHAURI SIKONGE WAFUKUZWA KAZI

$
0
0
Na Allan Ntana, Sikonge

BARAZA la Madiwani la halmashauri ya wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora limewafukuza kazi watumishi watatu wa halmashauri hiyo huku mmoja akisubiri kufikishwa mahakamani na wengine nane wakipewa onyo kali.

Akitangaza uamuzi huo, Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo Peter Nzalalila alitaja watumishi waliofukuzwa kwa tuhuma mbalimbali ikiwemo uzembe kuwa ni aliyekuwa Afisa Ushirika wa halmashauri hiyo Justin Kapufi, Afisa Sheria wa halmashauri Rebecca Liyanga na Mtendaji kata ya Kipanga Emmanuel Kalumay.
Aidha alisema Mweka Hazina wa halmashuri hiyo Evance Shimdoe na Mhasibu Richard Ndalo waliokuwa wamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi baraza hilo limejiridhisha pasipo shaka kuwa watumishi hao walifanya uzembe katika utendaji wao hivyo kupewa onyo kali.

Katika maamuzi hayo aliyekuwa Afisa Utumishi wa halmashauri hiyo Elly Aketch ambaye alikumbwa na rungu hilo na kusimamishwa kazi awali, Mwenyekiti alisema halmashauri inaandaa utaratibu wa mashataka ili kufikishwa kizimbani kwa uzembe ulioisababishia hasara kubwa halmashauri hiyo.

Aliongeza kuwa aliyekuwa Mganga Mkuu Mfawidhi wa zahanati ya Kitunda Dk.Fredrick Mtao, Mtendaji wa kata ya Kitunda Ally Kicko, Mtendaji kata ya Kipanga Emmanuel Kalumay, Afisa Mipango miji wa Halmashauri Emmanuel Magembe wao wamepewa onyo na kutakiwa kuwa makini katika utendaji wao.

Aidha Watendaji Kata 4waliokuwa wamesimamishwa kwa tuhuma za upotevu wa vitabu vya kukusanyia mapato ya halmashauri wamepewa onyo kali na kutotakiwa kurudia uzembe wa aina hiyo kwani walichangia kwa kiasi kikubwa kupata hati yenye mashaka huku Godfrey Sungura shauri lake likiendelea kuchunguzwa kutokana na uzito wake.

Baada ya kusoma maamuzi hayo, Nzalalila aliwataka watumishi wote wa halmashauri na ujumla kwa ujumla kutekeleza wajibu wao kwa kufuata sheria, kanuni, taratibu na maadili ya kazi zao ili kuepuka kutumbuliwa jipu.

Aidha aliwataka kwenda na kasi ya Rais wa serikali ya awamu ya tano kwa kuwajibika ipasavyo huku wakitumia utaalamu wao kwa manufaa ya wananchi na aliahidi kuendeleza tumbuatumbua kwa watumishi wote wasiotaka kubadilika kiutendaji.

SAFARI ZA MAJARIBIO ZA TRENI YA PUGU KUANZA, JUMATATU NA JUMANNE KUWA BURE

$
0
0
Huduma ya 2 ya treni ya Jiji kutoka Pugu kwenda kituo kikuu cha Dar es Salaam kuanza kesho Jumatatu Agosti 01, 2016 saa 12 asubuhi.

Aidha taarifa Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL ) inafafanua huduma hiyo ya majaribio ya siku 2 Jumatatu na Jumanne itakuwa bure kwa Wakazi wa vituo husika.

Vituo hivyo pamoja na Pugu stesheni ni Mwisho wa Lami, Gongo la mboto, FFU Mombasa, Banana (Njia panda Segerea) na Karakata. Vingine ni pamoja na Vingunguti Mbuzi, SS Bakhressa, Kamata na Kituo kikuu cha reli Dar es Salaam!

Huduma hiyo itakuwa ya awamu 2 ya safari 3 kila awamu. Safari ya kwanza ya awamu ya 2 itaanza saa 9:55 Alasiri kutoka Dar stesheni.

Wito unatolewa kwa Wasafiri wa treni hiyo kuzingatia maelekezo ya Maafisa wa TRL watakaosimamia safari hiyo ya majaribio na kutoa ushirikiano kikamilifu.

RAIS DKT. MAGUFULI AFANYA MKUTANO TINDE, ISAKA NA KAHAMA MKOANI SHINYANGA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mamia wa wakazi wa Kahama mara baada ya kuwasili akitokea Nzega mkoa Tabora.
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameambatana na Mbunge wa zamani wa Kahama James Lembeli ambaye ni mwanachama wa Chadema mara baada ya kumaliza kuhutubia mkutano mjini Kahama mkoani Shinyanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akicheza pamoja na Wanakwaya wa Haleluya Kuu kutoka Kanisa la KKKT- Usharika wa Yeru Ndala Shinyanga mara baada ya kumaliza kuhutubia mkutano Kahama mjini mkoani Shinyanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akicheza jukwaani wimbo wa kwaya ya Haleluya Kuu kutoka Kanisa la KKKT- Usharika wa Yeru Ndala Shinyanga kabla ya Kuhutubia mamia ya wakazi Kahama mkoani Shinyanga.


ALICHOONGEA MBUNGE WA ZAMANI WA KAHAMA JAMES LEMBELI MBELE YA RAIS DKT. MAGUFULI MJINI KAHAMA LEO

MOTO WATEKETEZA GHALA YA KUHIFADHI VIFAA VYA MAGARI, SINZA LEGHO JIJINI DAR LEO

$
0
0

 
Ghala moja lililokuwa linatumika kwa kuhifadhia mataili pamoja na vifaa vyenginevyo vya magari lililopo Sinza Lego ambalo mmiriki wake hakufahamika kwa mara moja limeteketea kwa moto jioni ya leo, chanzo cha moto huo inadaiwa kuwa ni mataili chakavu yaliyokuwa yakichomwa moto. Pia katika eneo hilo kuna Gereji ambayo haikuathirika na moto huo mkubwa, mpaka tunaingia mitamboni, kikosi cha kuzima moto na uokoaji kilikuwa eneo la tukio kuendelea kusaidiana na wananchi kuhakikisha moto huo unazimika. Taarifa kamili itatolewa na Jeshi la Polisi.
Mmoja wa kijana ambaye alifika kushuhudia tukio hilo akipanda juu ya Ghorofa baada ya kunusurika kudondokea katika moto huo.
Ghala likiwa linateketea kwa moto jioni hii Sinza Lego
Moto ukiendelea kuwaka katika Ghala hilo.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI

TIMU YA KUOGELEA YAAHIDI KURUDI NA MEDALI ZA OLIMPIKI

$
0
0
Na Zainab Nyamka,Globu ya Jamii

WAWAKILISHI wa Tanzania katika michuano ya Olimpiki inayotarajiwa kufanyika katika mji wa Sao Paulo, Rio De Jeneiro nchini Brazil , timu ya kuogelea imefanya mazoezi yake ya mwisho kabla ya kukabidhiwa bendera na Kamati ya Olimpiki nchini TOC kwa ajili ya kuiwakilisha vyema katika mashindano hayo.

Timu hiyo itakayowakilishwa na waogeleaji wawili ambao ni Magdalena Moshi anayeenda kwa mara ya tatu kwa upande wa wanawake huku Hilal Hilal akienda kwa mara ya kwanza na wote watakuwa ni waogeleaji katika upande wa mita 50. Akizungumzia maandalizi ya mwisho Kocha wa timu hiyo Alexandra Mwaipasi amesema kuwa wachezaji wake wameiva kwani mwanzoni walikuwa na changamoto ya kupata mabwawa yenye viwango vinavyoendana na mashindano hayo ila kwa mwaka huu washiriki wote wameweza kuweka kambi katika nchi mbili tofauti ambapo Magdalena amekuwa Australia huku Hilal akijifua nchini Dubai.

Amesema, ana imani na wachezaji wake kwani kwa kipindi alichokaa nao ameona uwezo waliokuwa nao na  wanaweza kurudi na medal nyumbani. Naye Katibu mkuu wa chama cha kuogelea TSA Ramadhan Namkoveka amesema kuwa tofauti na wengine wao hawajapata wadhamini ila wachezaji wao wamejiandaa vizuri na wana imani kubwa kuwa wataweka historia.

Moja ya washiriki, Magdalena Mosha amesema kuwa amejiandaa vizuri na anaamini miaka aliyoshiriki kwenye mashindano ya Olimpiki ya Beijing na London yamempa uelewa zaidi wa nini anatakiwa kufanya mwaka huu na katika mazoezi yake nchini Australia  ameyafanyia kazi. Amesema kuwa kwa sasa macho ya watanzania yapo kwao na wanatoa ahadi ya kufanya vizuri kwani hata mshiriki mwenzie  Hilal amekuwa kwenye mazoezi mazuri nchini Dubai tena katika kituo kinachojihusisha na masuala ya uogeleaji.

Timu hiyo kesho inakabidhiwa bendera na TOC kabla ya Agosti 02 kuondoka kuelekea nchini Brazili.
Magdalena na Hilal wakiwa katika mazoezi ya mwisho.
Magdalena Mosha akiwa pamoja na mshiriki mwenzie Hilal Hilal wakiwa kwenye mazoezi ya mwisho kabla ya kuondoka kuelekea nchini Brazil.
Viongozi wa Chama cha Kuogelea TSA wakiwa pamoja na washiriki Hilal Hilal na Magdalena Mosha, Kushoto ni mkurugenzi wa ufundi Amina Mfaume, Mwenyekiti wa TSA Alex Mosha, Katikati ni Kocha wa timu ya kuogelea Alexandra Mwaipasi na mwisho kulia ni Katibu mkuu TSA Ramadhan Namkoveka.

Michuano ya Airtel Rising Stars kuanza kutimua vumbi jijini Dar

$
0
0
Mashindano ya kusaka vipaji vya soka kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars Jumamosi, Julai 30 yameanza rasmi kutimua vumbia katika ngazi ya mkoa jijini Dar es Salaam ambapo Rais wa Shirikisho la soka nchini (TFF) Jamali Malizi amewataka vijana kujituma ili kutimiza ndoto zao za kuwa wachezaji nyota.

Malinzi pia ameziomba klabu zinazoshiriki Ligi Kuu pamoja na Ligi Daraja ya Kwanza kutumia fursa ya Airtel Rising Stars kwa ajili ya manufaa yao. ‘ Michuano hii inatoa nafasi nzuri kwa klabu zetu kuja na kutambua vipaji vinavyoibukia na kuwasajili kwenye timu zao’, alisema Malinzi.

Aliongeza kuwa, michuano hii ni sehemu bora ya kutambua vipaji, kwani ni fursa kwa wavulana na wasichana wanaoshiriki michuano kujitambua kwao kimaisha.

Akihutubia wachezaji wa Mikoa ya Kisoka ya Ilala, Kinondoni na Temeke, Malinzi alisema kuwa, wachezaji kufanya vizuri kwenye michuano hii ni kujitengenezea nafasi ya ajira . Aliwakumbusha jinsi soka limeweza kubadili maisha ya mchezaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu, huku akisisitiza kwamba soka inatoa ajira kwa mamilioni ya wachezaji ulimwenguni kote.

Akiongea wakati wa ufunguzi wa michuano hiyo, Mkurungenzi Mtendaji Airtel Tanzania Sunil Colaso aliwashukuru wadau wa soka kwa kusaidia na kushiriki kwao kwenye michuano ya Airtel Rising Stars kwa miaka mitano na kuwaomba makocha kuwachangua wachezaji wenye vipaji kwa ajili ya kuandaa timu ya kushiriki michuano ya taifa.

‘Tunajivunia uhusiano wetu mzuri na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Afrika kwa ujumla na tunayo furaha kuwa Klabu na Timu za Taifa zinafaidika na matunda ya Airtel Rising Stars’, alisema Colaso na kuongeza kuwa Airtel itaendelea kuthamini na kukuza soka la Tanzania.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF Salum Madadi waliwapongeza Airtel kwa program hii huku akisema imesaidia kutafuta na kukuza vipaji vya soka nchini.

Michuano ya Airtel Rising Stars ngazi ya mkoa ikishirikisha Ilala, Temeke, Kinondoni, Mbeya, Morogoro, Mwanza, Lindi, Zanzibar na Arusha itafikia tamati wakati wa fainali za taifa zitakapofanyika kwenye Uwanja wa Karume Dar es Salaam tarehe 6 mpaka 11 Septemba mwaka huu.
Mkurungenzi Mtendaji Airtel Sunil Colaso na Rais wa TFF Jamal Malinzi wakikagua timu wakati wa ufunguzi wa michuao ya Airtel Rising Stars 2016 Mkoa wa Dar es Salaam kwenye uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam Jumamosi 30 Julai 2016.
Mkurungenzi Mtendaji Airtel Sunil Colaso akikangua timu wakati wa ufunguzi wa michuao ya Airtel Rising Stars 2016 Mkoa wa Dar es Salaam kwenye uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam Jumamosi 30 Julai 2016.

MRI, CT-SCAN ZAPIGA MZIGO SAA 24 MUHIMBILI, WAGONJWA 41,101 WAPIMWA.

$
0
0
Na John Stephen, MNH
 HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH) inaendelea kutoa huduma bora hasa ya vipimo kwa wagonjwa mbalimbali na kufanikiwa kupima wagonjwa 41,101 katika mwaka 2015/2016 kutoka wagonjwa 32,010 waliopimwa mwaka wa fedha 2014/2015.

Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa Wateja, Aminiel Buberwa Aligaesha imeeleza kwamba mashine zinafanya kazi vizuri na kwamba hakuna mashine mbovu hadi kusababisha wagonjwa kukosa huduma za vipimo.

“Hospitali inahakikisha kila mgonjwa anayehitaji vipimo anapata na kwa gharama nafuu. Kama mashine ilisimama kufanya kazi tangu Januari hadu Juni, 2016 ni kwa muda wa kati ya siku moja hadi mbili kupisha matengenezo kinga,” amesema Bwana Aligaesha katika taarifa yake aliyoitoa leo kwa vyombo vya habari.
 Mgonjwa akiwa katika mashine ya MRI LEO katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). Pembeni ya mgonjwa ni Mtaalamu wa Mionzi, Medard Mallya akimsaidia mgonjwa kukaa vizuri kwenye mashine hiyo.
 Mkuu wa Idara ya Mionzi katika Hospitali Ya Taifa Muhimbili (MNH), Dk. Flora Lwakatare akifuatilia mgonjwa anavyochukuliwa vipimo leo mchana katika hospitali hiyo.
Picha na John Stephen, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
Viewing all 110171 articles
Browse latest View live




Latest Images