Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live

MAGIC FM BAMIZA TOP 20 COUNT DOWN MAY 7TH 2016

$
0
0
92.9Dar & Mtwara, 93.3Dodoma,
 98.6Arusha, 101.7Mwanza &Tanga, 98.7Morogoro.



SONG

ARTIST

PRODUCER

PEAK/POS

20. My life

Janjaro

Daxo &Makochali

NEW

19. Niroge

Vanessa

Nahreel


18. Mabawa

Msami

Abidadi


17. Samaki

Garatone

Dunga/ Christone


16. Fundi

Mh Temba ft Malomboso & Jokate

Makochali


15. Ndi ndi

Lady Jay Dee



14. Mahaba niue

Mau Sama

Ema the Boy


13. OG

G.Nako

Nahreel


12. Kwetu

Raymond

Lizer


11. Walk it off

Fid Q ft Taz

Taz


10. Nakuchana

Jux & Ben Pol

Manecke


  9. Ahsanteni kwa kuja

Mwana F.A

Hermy B

2 WEEKS ON NO.1

  8. Una Akili Wewe

Roma & Baghdad

ISSAM & GEOF MASTER.


  7. Kamatia chini

Navy Kenzo

Nahreel

2 WEEKS ON NO.1

  6. Sweeti sweetie

Chege ft Run Town&Uhuru

Uhuru

2 WEEKS ON NO.1

  5. Kama utanipenda

Darasa ft Mavoko

Abba


  4. Make me sing

Diamond & AKA

Tuddy Thomas


  3. Kwa hela

Linex

Tuddy Thomas

2 WEEKS ON NO.1

  2. Siwezi

Baraka da Prince

Manecky

2WEEKS ON NO.2.

  1. Zigo rmx

Ay ft Diamond Platnumz

Nahreel,Hermy B,Marco Chali

2ND WEEK ON NO. 1.


TUZO ZA WANAFUNZI BORA AFRIKA MASHARIKI "ALL-STARS STUDENTS AWARDS" ZAANZISHWA

$
0
0
 Aaron Ally(Dj Aaron Tanzania)Mratibu wa All-stars Students Awards Akiongea Kwenye Kipindi cha Morning Trumpet kuelezea tuzo hizo.
Dj wa zamani wa Clouds FM, Aaron, yeye na Team yake(Ms Chiku Lweno, Mwl. Dany Mtanga) wameanzisha   Tuzo walizoziita All-stars Students Awards. Hizo ni tuzo zitakazotolewa kwa wanafunzi wa shule za sekondari A-level na O-level za Afrika Mashariki.

Alhamisi hii Dj Aaron alialikwa kwenye kipindi cha Morning Trumpet cha Azam TV kuongelea tuzo hizo zitakazofanyika jijini Dar es Salaam.

Aaron amesema tuzo hizo zina dhumuni la kuwapa hamasa wanafunzi wa shule za Afrika Mashariki. Tuzo hizo zitatolewa kwa wanafunzi watakaofanya vizuri kwenye mitihani ya kidato cha nne na sita. pia na walimu husika ambao ni chachu ya wanafuzi ambao wamefanya vizuri kwenye hayo masomo.
Tuzo hizo zitaaangalia  namba moja wote waliongoza katika nchi zote za Africa Mashariki. Masomo yakayotolewa tuzo ni Kiswahili, Hesabu, Fizikia, Kemia, Bailojia na Kiingereza. Mchakato wa tuzo utaanza katikati ya mwezi wa sita.pia Special Talents, Michezo na  Shule bora

RAIS DKT MAGUFULI AKIONGEA NA WANANCHI AKIWA NJIANI KUTOKA DODOMA KWENDA ARUSHA IJUMAA

MAKATIBU WAKUU WA VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA WAKUTANA NCHINI ZIMBABWE

$
0
0
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahaman Kinana akitoa mada kwenye Kongamano la siku Nne la Makatibu Wakuu wa vilivyokuwa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika. Kongamano hilo linafanyika Victoria Falls Zimbambwe lilianza tarehe 4 – 8 Mei, 2016. Vyama hivyo ni ANC ya Afrika Kusini, FRELIMO ya Msumbiji, MPLA ya Angola, SWAPO Party ya Namibia na CCM ya Tanzania.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahaman Kinana akimpongeza Katibu Mtendaji Mkuu wa ZANU-PF Ndugu Ignatius Morgen Chombo kwa kufanikisha Kongamano la Makatibu Wakuu wa vilivyokuwa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika na anaeshuhudia katikati ni Katibu Mkuu wa FRELIMO Ndugu Eliseu Machava. Kongamano hilo linafanyika Victoria Falls, Zimbabwe tarehe 4 – 8 Mei 2016
Picha ya pamoja ya Makatibu Wakuu wa vilivyokuwa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika(FLM) wanaoshiriki Kongamano la siku Nne la kutafakari uimarishaji na uendelezaji wa ushirikiano wao na namna ya kukabiliana na changamoto walizonazo. Kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa ANC ya Afrika Kusini Ndugu Ndugu Gwede Mantashe, Katibu Mkuu wa FRELIMO ya Msumbiji Ndugu Eliseu Machava, Katibu Mkuu wa CCM ya Tanzania Ndugu Abdulrahaman Kinana, Makamu Waziri wa Uhusiano wa Kimataifa wa Chama cha Kikomnisti cha China (CPC) Ndugu Guo Yezhou, Katibu Mtendaji Mkuu wa ZANU-PF ya Zimbabwe Ndugu Ignatius Morgen Chombo, Katibu Mkuu wa MPLA ya Angola Ndugu Juliao Mateus Paulo na Katibu Mkuu wa SWAPO Party ya Namibia Ndugu Nangolo Mbumba. Kongamano hilo linafanyika Victoria Falls, Zimbabwe tarehe 4 – 8 Mei 2016.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahaman Kinana akibadilishana mawazo na Katibu Mkuu wa ANC ya Afrika Kusini, Ndugu Gwede Mantashe kwenye Kongamano la Makatibu Wakuu wa vilivyokuwa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika(FLM) linalofanyika Victoria Falls, Zimbabwe tarehe 4 – 8 Mei 2016 BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

TRA kugawa bure mashine 5700 za (Electronic Fiscal Devices) EFD’s kwa wafanyabiashara wadogo wadogo nchini

$
0
0

 Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Alphayo Kidata  akizungumza na waandishi wa habari (Hawapo pichani) kuhusu mwenendo wa makusanyo ya mapato nchini. Kulia ni Kamishna wa kodi za ndani Bw. Yusufu Salum. 
(Picha na Raymond Mushumbusi MAELEZO)
 
Na Lilian Lundo MAELEZO
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imejipanga kugawa jumla ya mashine 5700 za (Electronic Fiscal Devices) EFD’s kwa wafanyabiashara wadogo wadogo nchini ikiwa ni jitihada za Serikali katika kukusanya mapato nchini.
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA)  Bw. Alphayo Kidata amesema wameamua kuanza kugawa mashine hizo kwa wafanyabiashara wadogowadogo ambao wengi wao hawana uwezo wa kugharamia manunuzi ya mashine hizo.
“ Mamlaka imeona changamoto wanayoipata wafanyabiashara wadogo hivyo imeamua kuanza kugawa mashine hizi ili kuondokana na tatizo la kutotoa risiti za mauzo kwa wafanyabiashara hao ambao walio wengi walikuwa na kisingizio cha kutokuwa na mashine hizo”, alisema Kidata.

Kamishna Kidata ameongeza kuwa Mamlaka yake imeshaagiza mashine hizo na zipo tayari kuanza kugawiwa mwezi huu kwa wafanyabiashara  hao ikiwa ni awamu ya kwanza ya ugawagaji wa mashine hizo ambao utafanyika nchi nzima.
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeazimia kugawa mashine laki mbili kwa wafanyabiashara wadogo wadogo nchini ikiwa ni jitihada za kuweza kukusanya mapato yatokanayo na kodi za biashara kwa urahisi na ufanisi mkubwa.

introducing Cipha Headz Music studio @ Chang'ombe Serengeti, Dar es salaam

$
0
0
Cipha Headz Music ni label inayotoa huduma tofauti kwenye ukanda wa Music, Tunafanya kazi na wasanii wenye vipaji na wana ndoto za kujiendeleza kimziki ili tuweze kuwasaidia vipaji vyao.
Ni studio mpya na yenye vifaa vya kisasa kabisa. Tupo maeneo ya Chang'ombe Serengeti, Dar es salaam



HUDUMA TUNAZOTOA:
      >Muda wa studio
      >kurecord single, mixtape, e.p na album
      >song writing/producing session
      >Video production
      >Sound tracks
      >Mixtape/album artwork
      >Promotion
      >Mixing na Mastering
      >kubook show
*kwa maelezo zaidi wasiliana nasi :ciphaheadzent@hotmail.co.uk
instagram ciphaheadz.
 Ni studio mpya na yenye vifaa vya kisasa kabisa. 
 Vifaa vya kisasa kabisa. 
 Producer aliienda shule
Ni studio mpya na yenye vifaa vya kisasa kabisa. 

UCHUNGUZI DHIDI YA TUHUMA ZA KUFICHA SUKARI

$
0
0
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa inafanya uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazowahusu  wafanyabiashara wa sukari nchini kwa kuficha bidhaa hiyo ili  kusababisha upungufu katika soko na hivyo kuleta usumbufu kwa jamii ya watanzania wanaohitaji bidhaa hiyo kwa matumizi jambo ambalo limesababisha kupanda kwa bei hadi kufikia shilingi elfu nne kwa kilo moja ya sukari. 
 Taasisi imeanza uchunguzi dhidi ya Tuhuma hizi kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi na tayari tumeweza kutembelea Maghala ya mfanyabiasha Haruni Daudi Zacharia ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Al-Naeem yaliyoko Mbagala na Tabata ambaye ni miongoni mwa wafanyabiashara wakubwa nchini wa sukari na anayetuhumiwa kuficha bidhaa hii. 
Mnamo tarehe 05 Mei, 2016 timu ya uchunguzi ilitembelea maghala ya Tabata na kubaini uwepo wa sukari yenye jumla ya tani 4,579.2 iliyonunuliwa toka Kiwanda cha Kilombero Sugar Company. 
Aidha uchunguzi ulibaini kuwepo kwa njama za dhati za kutouza kwa sukari kulikofanywa na mfanyabiashara huyu kwani hata sehemu ya Maghala ilipo sukari hapa kuwepo dalili za upakiaji wa sukari na baada ya kufika Kitumbini tulibaini uwepo wa wananchi wengi waliokuwa wakihitaji bidhaa hiyo na wachache sana waliweza kuuziwa tena kwa kiwango kidogo sana kuliko mahitaji yao. 
Wananchi wengi walikosa huduma hiyo licha ya ukweli kwamba sukari ilikuwepo. 
Uchunguzi uliofanyika umebaini kuwepo kwa mikakati ya dhati iliyokuwa ikifanywa na mfanyabiasha huyu kwa kununua sukari yote toka viwanda vya ndani na kisha kuihifadhi na kuuza bidhaa hiyo kidogo kidogo kwa wastani wa tani 250 kwa siku wakati alikuwa na uwezo wa kuuza zaidi jambo lililochangia uhaba wa sukari katika soko. Kuficha bidhaa ni kosa la uhujumu uchumi na ni  kinyume na Aya ya 3 Jedwali la kwanza Sheria ya Uhujumu Uchumi Sura ya 200 [Chapisho la Mwaka 2002]. Serikali haitavumilia hujuma za namna hii na itachukua hatua kali dhidi ya mfanyabiashara yeyote ataekwenda kinyume na sheria hii. 
Kuanzia sasa TAKUKURU inatoa wito kwa wafanyabiashara wote wa sukari kuacha vitendo vya kuficha sukari na vyombo vya uchunguzi vinafuatilia kote nchini na yeyote atakayebainika kufanya hujuma hizo atakabiliwa na mkondo wa Sheria. 
VALENTINO MLOWOLA

 MKURUGENZI MKUU WA TAASISI 
YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA

7 MEI, 2016



RAIS DKT MAGUFULI AAPA KUWASHUGHULIKIA WANAOFICHA SUKARI - ARUSHA 07 MAY 2016


CNBC Profiles 13 Year Old Film Maker - ZURIEL ODUWOLE

$
0
0
As part of the largest global media company in the world comprising NBC, MSNBC and CNBC, Zuriel Oduwole has now been featured on CNBC Africa, and broadcast on DSTV across 43 African Countries. It is part of an extended new series focusing on the future leadership and creative direction of the next generation that would shape the exciting growth and exponential development of the African continent

In it, she shares her filmmaking core, talks about the essence of her foundation launched in December 2015, and why she is also making the case to educating the children of the African Continent - especially the Girl Child.

Her last film was first showed in 2 cinemas [movie theater chains] in Nigeria, before screening in Ghana, South Africa, the United Kingdom and in Tokyo - Japan in 2015.

President Hage Geingob of Namibia commended her at a meeting in the State House - Windhoek a few weeks ago, after she launched her Film Making for Youths Workshop series in that South Western African country in February 2016, in conjunction with her Foundation.

It is her second feature on CNBC Africa, the first in March 2015 on the marquee business show "Power Lunch". She has also been featured on BBC, Bloomberg TV, CCTV and CNN.

WANANCHI WATAKIWA KUFUATA SHERIA NJIA ZA MRADI WA DART

$
0
0
 Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), Mhandisi Ronald Lwakatare akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam kuhusu kuzingatia sheria za barabarani katika kuhakikisha kuwa mradi huo unafanikiwa na kuepusha ajali.

Wakala wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) umeonya watuamiaji vyombo vya moto kufuata sheria na kanuni za barabarani ili kurahisisha uendeshaji wa mradi huo na ajali.Wito huu unakuja katika kipindi ambacho mradi huo uko katika maandalizi ya mwisho kabla ya kuanza kwa mradi huo katika kipindi cha mpito.

Akiongea na waandishi wa habari mwishoni mwa wiki, Kaimu Mtendaji Mkuu wa wakala huo, Mhandisi Ronald Lwakatare alisema kutozingatia sheria za barabara za mradi huo, kufikia Ijumaa iliyopita, vyombo vingine vya moto vimesababisha ajali 14 za mabasi ya mradi.

“Ajali hizi zimetokea wakati madereva wa mradi wakiendelea na mazoezi wakijitayarisha na kuanza kipindi cha mpito cha mradi kinachotarajia kuanza hivi karibuni,” alisema.Alisema ajili hizo zimesababishwa na vyombo vingine kuingilia barabara za mradi.Kati ya ajali hizo, tisa zilisababishwa na pikipiki maarufu kama bodaboda, nne zilisababishwa magari na moja ilisababishwa na mwenda kwa miguu.

Alitoa wito kwa madereva wa vyombo vya moto kutotumia barabara za mabasi hayo ambazo ni za zege na badala yake kutumia barabara za lami.Pia alisema waendesha bodaboda waache mara moja kutumia vituo vya mabasi ya mradi kwa ajili ya kupakia na kushusha abiria kwani vituo hivyo si kwa kazi hiyo.

Alifafanua kuwa madereva bodaboda wanapotaka kuvuka kwenye alama za waenda kwa miguu kutoka upande mmoja kwenda mwingine sharti wazizime na kuzikokota na siyo kuziendesha.“Watambue kuwa sheria inawazuia waendesha bodaboda kuvuka pamoja na waenda kwa miguu katika alama hizo huku wakiziendesha,” alionya.

Akizungumzia maandalizi alisema yanakwenda vizuri kwa madereva kuendelea na mazoezi huku wataalamu wengine wakiendelea kukamilisha kufunga mifumo ya utozaji nauli.

DONDOO ZA MAGAZETI LEO

MKUU WA WILAYA BUKOMBE AAGIZA MAAFISA TARAFA KUSIMAMIA HIFADHI YA MAVUNO KWA WANANCHI

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Mhe. Amani K. Mwenegoha ameagiza maafisa tarafa kusimamia kwa karibu shughuli za hifadhi ya mavuno yaliyopatikana katika Mvua za vuli Msimu wa 2015/2016 kwa kuhamasisha wananchi wenye mavuno mengi kila mahali kuhifadhi vizuri ili mavuno hayo yasiharibike na kuweka akiba ya kutosha kwaajili ya kaya zao.

Pia ameagiza Wakulima washauriwe kuuza ziada tu ya mavuno yao kwaajili ya kukidhi mahitaji yao muhimu na kila kaya isimamiwe kuhakikisha imehifadhi mazao ya chakula cha kuwatosha huku akiagiza Wafugaji washauriwe kuvuna sehemu ya mifugo yao kwaajili ya kukidhi mahitaji yao muhimu na kununua nafaka kwaajili ya kaya zao.

Amesisitiza maelezo haya yawafikie viongozi ngazi za kata,vijiji na vitongoji kwaajili ya utekelezaji na taarifa iwasilishwe kwa Mkuu wa Wilaya kabla ya 13/05/2016.

Imetolewa na

Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Bukombe
Geita 

RAIS DKT. MAGUFULI ATUNUKU KAMISHENI MAAFISA WAPYA 586 KATIKA CHUO CHA MAAFISA WAPYA WA JESHI LA WANANCHI MONDULI

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe Magufuli akikagua gwaride kabla ya kutunuku Kamisheni kwa Maafisa Wapya 586 wa jeshi la Wananchi wa Tanzania kundi la 58/15 katika chuo cha kijeshi cha Monduli TMA mkoani Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe Magufuli akitunuku kamisheni kwa maafisa wapya 586 wa jeshi la Wananchi wa Tanzania kundi la 58/15 katika chuo cha Mafunzo ya kijeshi cha Monduli TMA mkoani Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Afisa Mpya wa cheo cha Luteni Usu, Nasra Rashid ambaye alifanya vizuri zaidi kuliko Maafisa Wanafunzi wanawake katika chuo cha kijeshi cha Monduli TMA mkoani Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya wananchi General Davis Mwamunyange mara baada ya kuwasili kwenye chuo cha Mafunzo Kijeshi cha Monduli TMA mkoani Arusha.
Maafisa Wanafunzi wakipita kwa mwendo wa haraka mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe Magufuli kabla ya kutuniwa Kamisheni .

SIMU TV: HABARI KUTOKA VITUO VYA TELEVISHENI NCHINI

WAKAZI WAWILI MKOA WA KAGERA WAIBUKA WASHINDI PROMOSHENI YA SHINDANO LA PATA PATIA YA NMB BENKI

$
0
0

Na Editha Karlo blog ya Jamii, Kagera.
WAKAZI wawili wa Mkoa wa Kagera wameshinda fedha taslimu kupitia shindano la pata patia linaloendeshwa na bank ya NMB katika matawi yake yote nchini.

Wakiongea na mtandao huu mara baada ya kushinda fedha hizo mmoja wa washindi hao Jafram Mohamed ambaye ni askari polisi Wilayani Ngara alisema kuwa anaupongeza uongozi wa NMB kwa kuanzisha shindano hilo kwa wateja wao kwani lina lenga kuwahamasisha kujiwekea akiba mara kwa mara.

Mohamed alisema kuwa yeye ni mtumishi wa serekali lakini amekuwa akijiwekea akiba mara nyingi kadiri awezavyo katika akaunti yake hali iliyopelekea kuingia katika droo ya kucheza bahati nasibu hiyo.

"Nilifurahi sana baada ya meneja kunipigia simu na kuniambia nimeingia faini za bahati nasibu ya shindano la pata patia, hizi fedha nilizoshinda shilingi laki nane ntazifanyia jambo la msingi na ambalo ni kumbukumbu kwangu na familia yangu"alisema Mohamed.Naye mshindi mwingine Philbert Robart mjasiliamali na mkazi wa Wilaya ya Muleba alisema kuwa amefarijika kushinda kiasi cha shilingi laki nne katika bahati nasibu ya pata patia toka bank ya NMB.

"Kwakweli bank ya NMB unatujali sana wateja wake, hizi fedha nilizoshinda leo zitanisaidia katila biashara zangu, nina wasihi wateja wote wa bank ya NMB nchi nzima wale wapya na wazamani kujiwekea fedha mara kwa mara katika akaunti yao itawapa nafasi ya kuingia katika shindano hili"alisema Rogati

Meneja wa NMB Mkoa wa Kagera Victorine Kimario alisema kuwa shindano hilo la pata patia kwa wateja wao ni endelevu hivo amewataka wateja kujiwekea fedha kwenye akaunti zao mara kwa mara ili waweze kupata nafasi ya kuingia kwenye droo ya kushinda.

''Kampeni hii ya pata patia ya kuwataka wateja wetu kuweka fedha katika akaunti zao imeanza mwezi wa pili mwaka huu, wateja wanatakiwa kuweka fedha katika akaunti zao kuanzia kiasi cha shilingi elf hamsini na kuendelea mara kwa mara ili aweze kuingia katika faini za kushinda"alisema Meneja

Alisema kila mteja ambaye anaingia fainali lazima ashinde sababu atatakiwa kuzungusha gurudumu lenye lenye nba kuanzia laki moja hadi milioni tatu na mshale wa gurudumu utakaposimama ndiyo kiasi ambacho atakuwa kashinda.Meneja Kimario amewataka wateja wapya na wazamani wa bank ya NMB kuendelea kuweka fedha kwenye akaunti zao mara kwa mara ili kujiweka katika nafasi ya kushinda bahati nasibu ya pata patia.
Mshindi wa shindano la pata patia linaloendeshwa na bank ya NMB matawi yote nchini Jofram Mohamed akizungusha gurudumu na kushinda shilingi laki 8 taslimu.
Mshindi mwingine wa shindano la pata patia linaloendeshwa na bank ys NMB kwa matawi yote nchini kutoka Mkoa wa Kagera Filbert Rogati akizungusha gurudumu  na kushinda shilingi laki 4
Washindi wa shindano la pata patia wakisikiliza maelekezo toka kwa meneja wa NMB Mkoa wa Kagera kabla ya kuzungusha gurudumu la bahati nasibu
Baadhi ya wateja na wafanyakazi wa bank ya NMB tawi la bukoba mjini wakishuhudia washindi wanavyojipatia fedha zao kwa kuzungusha gurudumu
 

NE-YO kutua nchini mwezi huu, Kuwasha moto tamasha la Jembeka na Vodacom jijini Mwanza, Kushiriki shughuli za kijamii kupitia Vodacom Tanzania Foundation

$
0
0
Ni wakati mwingine tena Vodacom Tanzania inawaletea burudani wateja wake na watanzania wote kwa ujumla,Ili waweze kufurahia kwa pamoja kwa kufanikisha hili sasa  Vodacom Tanzania,Kushirikiana na Jembe Media Limited tumeamua kumleta mwanamuziki nguli kutoka nchini Marekani NE-YO ambaye ataingia hapa nchini mnamo mwezi huu tarehe 19.NE-YO atawasili nchini kwa ajili ya kutoa burudani ya aina yake katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kwenye tamasha la Jembeka na Vodacom 2016 chini ya udhamini mkuu wa Vodacom Tanzania.
Akiongea na mtandao huu,Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu alisema Vodacom wameamua kumleta mwanamuziki huyu wakiwa na sababu kuu tatu alisema Nkurlu.
1.      Kwa ajili ya kuwapatia burudani ya kimataifa wateja watu na watanzania wote kwa ujumla  kupitia tamasha la Jembeka 2016.
2.     Kuwaunganisha wasanii wetu nchini na msanii huyo wa kimataifa ili waweze kufanya kazi siku za usono nasi tuweze kuutangaza muziki wetu katika Nyanja za kimataifa.
3.     Kushiriki katika shughuli za kusaidia jamii kupitia taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation hapa nchini.
 Msimamizi Mkuu wa  Itifaki wa Jembe Media Limited,Leah Guya(kushoto) na Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(Katikati) wakimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi wa Tamasha la Jembeka festival 2016, Costantine Magavilla(kulia) akifafanua jambo kwa waandishi wa habar jijini Dar es Salaam,(hawapo pichani)wakati wa kutangaza ujio wa Mwanamuziki nguli kutoka nchini Marekani NE-YO, atakayewasili nchini Mei 19  na Mei 21 atatoa burudani katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kwenye tamasha la Jembeka Festival 2016 liloandaliwa na kampuni ya Jembe chini ya udhamini mkuu wa Vodacom Tanzania.
Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(Katikati)akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,(hawapo pichani)wakati wa kutangaza ujio wa Mwanamuziki nguli kutoka nchini Marekani NE-YO, atakayewasili nchini Mei 19  na Mei 21 atatoa burudani katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kwenye tamasha la Jembeka Festival 2016 liloandaliwa na kampuni ya Jembe chini ya udhamini mkuu wa Vodacom Tanzania,kushoto ni Msimamizi Mkuu wa  Itifaki wa Jembe Media Limited, Leah Guya na Mwenyekiti wa  kamati ya maandalizi wa Tamasha hilo, Costantine Magavilla.
Baadhi ya waandishi wa habari na wafanyakazi wa kampuni ya Jembe Media Limited na Vodacom Tanzania,wakiwa kwenye mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, wakati wa kutangaza ujio wa Mwanamuziki nguli kutoka nchini Marekani NE-YO, atakayewasili nchini Mei 19  na Mei 21 atatoa burudani katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kwenye tamasha la Jembeka Festival 2016 liloandaliwa na kampuni ya Jembe chini ya udhamini mkuu wa Vodacom Tanzania.

JK AMUWAKILISHA RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI MAZISHI YA LUCY KIBAKI NCHINI KENYA

$
0
0


Mwili wa mke wa Rais wa Kenya mstaafu Mhe. Mwai kibaki , Mama Lucy Kibaki ukiwasili kwa ajili ya mazishi hapo jana katika eneo la Bunge la Odhaya kaunti ya Njeri,mjini Nairobi nchini Kenya. 
Rais Mstaafu wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji  Rais Mstaafu wa Kenya Mhe. Mwai Kibaki  katika mazishi ya mke wake mpendwa Mama Lucy Kibaki mjini Nairobi, Kenya. Anayeshuhudia katikati  ni Rais wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta.
Naibu Rais wa Kenya Mhe.William Rutto na Mkewe wakimfariji Rais Mstaafu wa Kenya Mhe.Mwai Kibaki wakati wa mazishi ya Mkewe Lucy Kibaki yaliyofanyika jana katika eneo la Bunge la Odhaya kaunti ya Njeri,mjini Nairobi nchini Kenya. Kushoto ni Rais Mstaafu awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete.
Rais wa Kenya Mh Uhuru Kenyatta akizungumza jambo na Rais Mstaafu wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa mazishi ya Mama Lucy Kibaki hapo jana mjini Nairobi. Kulia ni mke wa Rais Uhuru Kenyatta, Mama  Margaret Kenyatta. 
Rais Mstaafu wa Kenya, Mh.Mwai Kibaki akiweka udogo kwenye kaburi la Mke wake Mama Lucy Kibaki,wakati wa mazishi yaliyofanyika hapo jana katika eneo la Bunge la Odhaya kaunti ya Njeri,mjini Nairobi nchini Kenya.
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta pamoja na Mkewe Margaret Kenyatta wakiweka udogo kwenye kaburi la mke wa Rais Mstaafu wa  Kenya Mhe. Mwai kibaki , mama Lucy Kibaki. Mazishi hayo yamefanyika jana katika eneo la Bunge la Odhaya kaunti ya Njeri,mjini Nairobi nchini Kenya. 
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta pamoja na Mkewe Margaret Kenyatta wakiweka shada la maua kwenye kaburi la mke wa aliyekuwa rais wa Kenya Mwai kibaki , mama Lucy Kibaki .Mazishi hayo yamefanyika jana katika eneo la Bunge la Odhaya kaunti ya Njeri,mjini Nairobi nchini Kenya,ambapo nchini Tanzania iliwakilishwa na Rais Mstaafu wa awamu ya nne ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt Jakaya Kikwete kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.

Rais Mstaafu wa Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ni miongoni mwa viongozi wa ngazi za juu katika ukanda wa Jumuia ya Afrika Mashariki kuhudhuria  mazishi ya aliyekuwa mama wa Taifa la Kenya Mama Lucy Kibaki aliyefariki akiwa na umri wa miaka 82.
Marehemu Mama  Lucy Kibaki ametajwa na wanaomjua kama kiongozi aliyetetea mazingira safi ya kifamilia na alikuwa tayari kufanya kila jambo kuhifadhi utu na wema katika familia.
Dkt. Kikwete ambaye aliwasilisha ujumbe wa Rais John Pombe Magufuli alisema kifo cha mama Lucy Kibaki kimetokea wakati mchango wake ukiwa bado unahitajika katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na Naibu wake William Ruto waliohudhuria mazishi ya Bi Kibaki eneo la Bunge la Odhaya kaunti ya Njeri wamemtaja marehemu kama kiongozi aliyekuwa tayari kuhudumia taifa la Kenya.

MTANGAZAJI WA CNN RICHARD QUEST AFURAHISHWA NA VIVUTIO VYA UTALII TANZANIA KATIKA MAONESHO YA INDABA

$
0
0
Kwa mara nyingine tena Tanzania inashiriki katika onesho la kimataifa la Utalii la INDABA yanayofanyika huko Afrika Kusini maonesho hayo yalianza jana tarehe 7 Mei na yanatarajiwa kumalizika tarehe 9 Mei, 2016. jijini Durdan, Bodi ya Utalii (TTB) ndio waratibu wa onesho kwa upande wa Tanzania. Katika onesho hili TTB inashirki pamoja na taasisi za TANAPA na Mamlaka na Hifadhi ya Ngorongoro pamoja na makampuni mbalimbali binafsi Zaidi ya 30 ya sekta ya Utalii .

Katika siku yake ya kwanza Banda la Tanzania limetembelewa na wadau wengi wakiwemo watalii, waandishi wa habari za utalii, mawakala wa Utalii nk. Miongoni mwa watu mashuhuri waliotembelea Banda la Tanzania ni Mwandishi maarufu na mtangazaji wa Kimataifa kutoka Shirika la habari la CNN la Marekani Bwana Richard Quest ambaye alifurahishwa na vivutio vua utalii nchini Tanzania mara baada ya kupata maelezo kutoka kwa Maofisa wa Bodi ya Utalii Tanzania TTB.Mkurugenzi wa Masoko kutoka Bodi ya Utalii Tanzania TTB Bwa Philip Sebastian akimuonyesha jambo Mwandishi maarufu na mtangazaji wa Kimataifa kutoka Shirika la habari la CNN la Marekani Bwana Richard Quest wakati alipotembelea katika banda la Tanzania katika maonesho ya kimataifa ya Utalii Indaba jijini Durban nchini Afrika Kusini..Mkurugenzi wa Masoko kutoka Bodi ya Utalii Tanzania TTB Bwa Philip Sebastian akimpa maelezo kuhusu vivutio vya utalii nchini Tanzania Mwandishi maarufu na mtangazaji wa Kimataifa kutoka Shirika la habari la CNN la Marekani Bwana Richard Quest wakati alipotembelea katika banda la Tanzania katika maonesho ya kimataifa ya Utalii Indaba jijini Durban nchini Afrika Kusini Katikati ni Bi Devotha Mdachi Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania TTB. Baadhi ya wagenimbalimbali waliotembelea katika banda la Tanzania katika maonesho ya Utalii ya Indaba yanayofanyika katika jiji la Durban nchini Afrika Kusini.Mkurugenzi wa Masoko kutoka Bodi ya Utalii Tanzania TTB Bwa Philip Sebastian na Bi. Devotha Mdachi Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania TTB. wakiwa na mmoja wa wageni aliyetembelea katika banda la Tanzania katika maonesho ya kimataifa ya Utalii Indaba jijini Durban nchini Afrika Kusini.
Baadhi ya wageni wakipata taarifa mbalimbali kutoka katika banda la Tanzania.Wageni mbalimbali wakiwa katika banda la Tanzania.

Happy birthday Neema Mbeyela

$
0
0
Familia ya Dr Happiness  Wimile ya Mbezi beach Dar es 
Salaam inapenda kukutakia happy birthday  
Neema mbeyela leo 8 May 2016.

TASWIRA ZA MATUKIO YA USAFI JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya usafi GENERAL WORKERS wakiendelea na usafi katika soko la Ilala jijini Dar es Salaam ili kuhakikisha wafanyabiashara wa soko hilo mazingira yanayowazunguka yanakuwa katika hali ya usafi.
 
 Wafanyabiashara wa Soko la Ilala jijini Dar es salaam wakifanya usafi ili kuhakikisha mazingira yanayowazunguka yanakuwa katika hali ya usafi.
 Wafanyakazi wa Kampuni ya usafi wakiendelea na usafi katika barabara ya Karume jijini Dar es Salaam.
PICHA ZOTE NA PHILEMON SOLOMO
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live




Latest Images