Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109589 articles
Browse latest View live

WANAMUZIKI WA NYIMBO ZA INJILI WAJIUNGA NA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA (NHIF)

0
0
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa, kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Joyce Hagu (wa pili kushoto), akimkabidhi Katibu wa Chama cha Muziki wa Injili Tanzania (Chamuita), Stellah Joel, kadi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), katika hafla ya uzinduzi wa huduma hiyo kwa waimbaji wa nyimbo za injili uliofanyika Dar es Salaam jana. Kutoka kushoto ni Mlezi wa chama hicho, Askofu Dk. Rejoyce Ndalima na Rais wa chama hicho, Ado Novemba.
Hapa mwimbaji nguli wa nyimbo za injili Mzee Kitenzogu Makassy akikabidhiwa kadi yake baada ya kujiunga na NHIF.
Burudani kutoka Kwaya ya Victorous Station ya Mwananyamala ikiendelea.

PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

SPIKA AFUNGUA MKUTANO WA CHAMA CHA WABUNGE WANAOPAMBANA NA RUSHWA

0
0
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akifungua Semina wa Chama cha Wabunge wanaopambana na Rushwa-Tanzania Mjini Dodoma leo tare 8 Mei, 2016.Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akifungua Semina wa Chama cha Wabunge wanaopambana na Rushwa-Tanzania Mjini Dodoma leo tare 8 Mei, 2016Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai ( katikati pamoja na viongozi wengine wakifuatilia uwasilishwaji wa mada wakati wa Semina wa Chama cha Wabunge wanaopambana na Rushwa-Tanzania. Wengine katika ni , Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angela Kairuki (kushoto) na Cecilia Paresso (Mb) – Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho.Wakili wa kujitegemea Bw. Said Yakubu akiwasilisha mada wakati wa Semina wa Chama cha Wabunge wanaopambana na Rushwa-Tanzania.Picha na Ofisi ya Bunge)

Viongozi wa CCM Wilaya ya Arusha washiriki kikao Mwenyekiti wa Shina ,Daraja II

0
0
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Arusha Ndg Wilfred Soileli akiongea wananchi wa Mtaa wa Jamhuri kwenye kikao cha Mwenyekiti wa Shina Mtaa wa Jamhuri,Kata ya Daraja ii, Ndg Khalifa leo asubuhi,ambapo pia Mwenyekiti  huyo alimshukuru Mwenyekiti wa Shina Mtaa wa Jamhuri,Kata ya Daraja ii, Ndg Khalifa kwa kumkaribisha na kufanikisha kikao chake katika Shina lake leo asubuhi.

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN, AWAHUTUBIA WANAWAKE KWENYE MAADHIMISHO YA SIKU YA MAMA MJINI DODOMA

0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akihutubia Wanawake kwenye maadhimisho ya siku ya Mama na sherehe za kumpongeza kwa kuchaguliwa Makamu wa Rais Mwanamke wa kwanza yaliyoandaliwa na Jumuiya ya UWT Taifa yaliyofanyika leo Mei 8,2016 katika viwanja vya Nyerere Square mjini Dodoma.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiangalia Bidhaa za aina mbalimbali zinazotengenezwa na Wajasiriamali wadogowadogo kwenye maonesho ya maadhimisho ya siku ya Mama na sherehe ya kumpongeza kwa kuchaguliwa Makamu wa Rais wa kwanza Mwanamke. Maadhimisho hayo yaliyoandaliwa na Jumuiya ya UWT Taifa yamefanyika leo Mei 8,2016 katika viwanja vya Nyerere Square mjini Dodoma.
Baadhi ya Wajasiriamali wadogowadogo wakifuatilia maonesho ya maadhimisho ya siku ya Mama na sherehe ya kumpongeza kwa kuchaguliwa Makamu wa Rais wa kwanza Mwanamke. Maadhimisho hayo yaliyoandaliwa na Jumuiya ya UWT Taifa yamefanyika leo Mei 8,2016 katika viwanja vya Nyerere Square mjini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimkabidhi cheti mmoja kati waliofanya vizuri kwenye maonesho ya maadhimisho ya siku ya Mama na sherehe ya kumpongeza kwa kuchaguliwa Makamu wa Rais wa kwanza Mwanamke. Maadhimisho hayo yaliyoandaliwa na Jumuiya ya UWT Taifa yamefanyika leo Mei 8,2016 katika viwanja vya Nyerere Square mjini Dodoma.

introducing "Usiende mbali" by Nedy ft Ommy Dimpoz

0
0
PKP ENT. Present the official Video of Brand new hit USIENDE MBALI by @nedymusic feat The bowss Himself @ommydimpoz. Lovely  Tune Produced by @Nahreel & Directed by @gorilla_films 

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI

Katibu wa Jukwaa Huru la Wazalendo Tanzania.Mtela Mwampamba alaani hujuma dhidi ya Rais Dkt Magufuli

0
0
 Katibu wa Jukwaa Huru la Wazalendo Tanzania.Mtela Mwampamba (Katikati) akizungumza na waandishi  mjini Dodoma Mara baada ya kusoma tamko la Jukwaa Huru la Wazalendo Tanzania kuhusu Hujuma dhidi ya Mhe.Rais John Pombe Magufuli. Wengine pichani ni wajumbe wa jukwaa hilo,Halphan Hamis kushoto na Mariam Fundi.
Picha na  Deusdedit Moshi wa Globu ya Jamii, Kanda ya Kati

RAIS DKT MAGUFULI ALIPOZUNGUMZA KANISANI ARUSHA JUMAPILI


Kuelekea Tanzania ya Viwanda, TANTRADE Yapongezwa Kwa Kuanza na Sekta Ndogo ya Ngozi.

0
0
Mamlaka ya Biashara Tanzania, TANTRADE, imepongezwa kwa kuichagua sekta ndogo ya ngozi, na kuifanyia maboresho, katika kutimiza azma ya serikali ya Awamu ya Tano, ya kujenga Tanzania ya Viwanda. 
 Pongezi hizo  zimetolewa na wadau wa ngozi wa machinjio ya Vingunguti na Ukonga, wakati wa kufanya tathmini ya mafunzo ya kuwajengea uwezo, yaliyofanywa na Tantrade kwa ushirikiano na Chuo cha Teknolojia cha Dar es Salaam, DIT, Kampasi ya Mwanza, ambapo kimeendesha mafunzo ya nadharia ya utunzaji ngozi, yakafuatiwa na mafunzo kwa vitendo ya unjinjaji, uchunaji, na utunzaji bora wa ngozi, na kukamilishwa na mafunzo ya utengenezaji wa bidhaa bora za ngozi yaliyofanyikia DIT kampasi ya Mwanza. 
 Wadau hao wameipongeza TANTRADE kwa kubaini fursa zilizopo kwenye sekta ndogo ya ngozi na kuamua kutoa kipaumbele maalum kuiendeleza sekta hiyo, kwa kuwaelimisha wafugaji, wasafirishaji, wajinjaji, na wasindikaji ngozi, ili Tanzania itoe mazao ya ngozi yenye daraja la juu.
   Akizungumzia uamuzi huo Kaimu Mkurugenzi wa TANTRADE, Bw. Edwin Rutageruka amesema “Sisi kama taasisi tumijipanga kuwajengea uwezo wajasiriamali, waweze kutumia vizuri fursa za biashara zilizopo kupitia sekta hii muhimu ya ngozi na hatimaye kuwaongezea kipato binafsi na kuchangia katika maendeleo ya uchumi wetu kwa ujumla, ili kufikia malengo ifikapo mwaka 2025 nchi iwe na uchumi wa kati,” alisema Rutageruka. 
 Pia aliiomba serikali ya mikoa na wilaya kupitia manispaa na halmashauri zao, kutenga maeneo maalum yatakayotumiwa na wajasiriamali wadogo na wa kati , kuzalisha bidhaa za ngozi, ambao TANTRADE kwa upande wake itawapatia fursa za kuyafikia masoko kupitia fursa mbalimbali zikiwemo za maonyesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam, DITF, ambapo TANTRADE itawatengea maeneo maalum ya kuonyesha bidhaa za ngozi. 
 Tantrade kwa ushirikiano na Chuo cha Teknolojia cha Dar es Salaam kampasi ya Mwanza, wameamua kuitekeleza kwa vitendo kauli ya rais Magufuli ya Tanzania ya viwanda, kwa kuwapatia mafunzo ya kuwajengea uwezo Watanzania kuweza kuendesha viwanda vidogo vidogo vya sekta ya ngozi nchini. 
Mafunzo hayo ya unjinjaji wa kisasa yalitanguliwa na mafunzo ya ufugaji wa kisasa wa kutunza ngozi, na kufuatiwa na mafunzo ya utengenezaji bidhaa za ngozi, yatakayoendeshewa mjini Mwanza.

 Mkufunzi na mtaalam wa ngozi, Patrick Mshana, mwenye uzoefu wa zaidi miaka 40 akiwafunda wachinjachi na wasindikaji ngizi wa mchinjio za Vingunguti na Ukonga, wakati wa mafunzo ya uchinjaji, uchunaji na usindikaji  bora wa wanyama ili kuzalisha ngozi bora, yaliyoendeshwa na TANTRADE kwa ushirikiano na Chuo cha DIT Kampasi ya Mwanza, yaliyoendeshwa  katika katika machinjio ya Vingunguti hapa Jijini Dar es Salaam, na kuhitimishiwa Mwanza kwenye Kampasi ya DIT, yalihudhuriwa na wachinjaji na wasindikaji wa ngozi kutoka machinjio Vingunguti na Ukonga jijini Dar es Salaam wajasiliamali wa bidhaa za ngozi wa Kanda ya Ziwa.
 Mkufunzi na mtaalam wa ngozi, Patrick Mshana, mwenye uzoefu wa zaidi miaka 40 akiwafunda wachinjachi na wasindikaji ngizi wa mchinjio za Vingunguti na Ukonga, wakati wa mafunzo ya uchinjaji, uchunaji na usindikaji  bora wa wanyama ili kuzalisha ngozi bora, yaliyoendeshwa na TANTRADE kwa ushirikiano na Chuo cha DIT Kampasi ya Mwanza, yaliyoendeshwa  katika katika machinjio ya Vingunguti hapa Jijini Dar es Salaam, na kuhitimishiwa Mwanza kwenye Kampasi ya DIT, yalihudhuriwa na wachinjaji na wasindikaji wa ngozi kutoka machinjio Vingunguti na Ukonga jijini Dar es Salaam wajasiliamali wa bidhaa za ngozi wa Kanda ya Ziwa.
 Wachinjaji wa ng'ombe wa machinjio ya Vingunguti, wakifundishwa mbinu mbalimbali za kumbembeleza mnyama kabla ya kumchinja, ili asikarike, mnyama akichinjwa kwa ukatili, harisa zinaingia kwenye nyama, hivyo walaji kujikuta wanakula nyama yenye hasiri na wao kupata hasira, Mafunzo ya uchinjaji, uchunaji na usindikaji  bora wa wanyama ili kuzalisha ngozi bora, yaliyoendeshwa na TANTRADE kwa ushirikiano na Chuo cha DIT Kampasi ya Mwanza, yaliyoendeshwa  katika katika machinjio ya Vingunguti hapa Jijini Dar es Salaam, na kuhitimishiwa Mwanza kwenye Kampasi ya DIT, yalihudhuriwa na wachinjaji na wasindikaji wa ngozi kutoka machinjio Vingunguti na Ukonga jijini Dar es Salaam wajasiliamali wa bidhaa za ngozi wa Kanda ya Ziwa.
Katibu Mkuu wa Biashara na Uwekezaji wa Wizara ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji Profesa  Adolf Mkenda akifungua semina ya siku tano ya mafunzo ya bidhaa za ngozi kwenye chuo cha DIT Mwanza jana,akiwa ameshika kiatu kilichotengenezwa hapa nchini chenye viwango vya kimataifa,kushoto ni Mkuu wa Chuo cha DIT tawi la Mwanza Dk Albert Mmari na Kaimu Mkurugenzi wa Tantrade Edwin Rutageruka.

Profesa Muhongo azindua Tovuti na Mpango wa Ugawaji Madawati, Musoma Vijijini.

0
0

Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini ambaye pia ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ( wa kwanza Kulia) akielekea kupanda Boti ya kumpeleka Musoma Mjini mara baada ya kuzindua Mpango wa ugawaji madawati katika Jimbo hilo uliofanyika katika shule ya Rukuba iliyopo katika kisiwa cha Rukuba ambayo ilipata madawati 100 huku zoezi hilo likiwa ni endelevu. Wa Pili kutoka kulia ni Mhandisi Joseph Kumburu.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Rukuba katika Jimbo la Musoma Vijijini wakiwa wamekalia madawati yaliyotolewa na Mbunge wa Jimbo hilo ambaye pia ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo mara baada ya kuzindua Mpango wa ugawaji madawati katika Jimbo hilo ambapo shule hiyo iliyopo katika kisiwa cha Rukuba ilipata madawati 100 huku zoezi hilo likiwa ni endelevu.
Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini ambaye pia ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ( wa Pili kushoto) akipeana mkono na mmoja wa Wanafunzi katika Shule ya Msingi Rukuba iliyopo jimboni humo ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Mpango wa ugawaji madawati katika Jimbo hilo ambapo shule hiyo iliyopo katika kisiwa cha Rukuba ilipata madawati 100 huku zoezi hilo likiwa ni endelevu.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

BONGO CARNIVAL YAKUSANYA WATOTO WA JIJINI DAR KUFURAHI PAMOJA.

0
0
Bongo Carnival yawakusanya pamoja watoto wa jijini Dar es Salaam kwa kucheza na kufurahi pamoja katika viwanja vilivyopo Oysterbay jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Bongo Carnival imedhaminiwa na Azam, Superdoll, Blue Band, Alliance Auto pamoja na wajasiliamali mbalimbali kwaajili ya kuwaweka watoto wa maeneo mbalimbali pamoja.
Watoto wakiwa wamepanda mnyama katika mchezo wa watoto wa Bongo Carnival jijini Dar es Salaam.
Watoto wakiwa kwenye banda la Blue Band wakicheza michezo mbalimbali.

RAIS DKT MAGUFULI ASHIRIKI IBADA YA JUMAPILI YA KUPAA KWA BWANA KATIKA PAROKIA YA TOLEO LA BWANA JIMBO LA ARUSHA

0
0



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipokea zawadi ya Biblia Takatifu kutoka kwa Padri Kiongozi Peter Pinto  aliposhiriki ibada ya Jumapili ya Kupaa kwa Bwana katika Parokia ya Toleo la Bwana jimbo la Arusha leo Mei 8, 2016.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akishiriki katika  ibada ya Jumapili ya Kupaa kwa Bwana katika Parokia ya Toleo la Bwana jimbo la Arusha leo Mei 8, 2016.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimia waumini aliposhiriki ibada ya Jumapili ya Kupaa kwa Bwana katika Parokia ya Toleo la Bwana jimbo la Arusha leo Mei 8, 2016.
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimia baadhi ya watawa aliposhiriki ibada ya Jumapili ya Kupaa kwa Bwana katika Parokia ya Toleo la Bwana jimbo la Arusha leo Mei 8, 2016.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimia na wanakwaya  aliposhiriki ibada ya Jumapili ya Kupaa kwa Bwana katika Parokia ya Toleo la Bwana jimbo la Arusha leo Mei 8, 2016.



AAGIZA WALIOFICHA SUKARI WAIFICHUE MARA MOJA.

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewataka wafanyabiashara wote walioficha sukari katika maghala yao, kuanza kuisambaza mara moja, vinginevyo serikali itachukua hatua kali ikiwa ni pamoja na kuinyang'anya sukari hiyo na kuisambaza kwa wananchi bure.

Rais Magufuli ametoa maagizo hayo leo tarehe 06 Mei, 2016 katika mikoa ya Singida na Manyara wakati akizungumza na wananchi kwa nyakati tofauti waliosimamisha msafara wake uliokuwa ukitoka Dodoma kwenda Arusha.

Dkt. Magufuli ameviagiza vyombo vya dola kuwafuatilia wafanyabiashara wanaofanya njama za kuficha sukari na kusababisha upungufu wa bidhaa hiyo, na ameapa kuwa serikali yake itawachukulia hatua kali watakaobainika kufanya hivyo.

Pamoja na kutoa maagizo hayo Rais Magufuli amewaondoa shaka watanzania juu ya upungufu wa sukari, kuwa serikali imeagiza sukari kutoka nje ya nchi ambayo itasambazwa kwa wananchi kwa bei nafuu ili kufidia upungufu uliopo.

"Wale wote waliokuwa wameficha sukari waiachie, wasipoiachia sukari, huwezi kuificha kama sindano, nimeshaagiza vyombo vya dola, vikague magodown yote, atakayekutwa na sukari ameificha, yule ni mhujumu uchumi kama wahujumu wengine, asije akanilaumu, asijee-akanilaumu, na ninasema kwa dhati, wewe mfanyabiashara uliyepata nafasi ya Tanzania kuleta bidha za sukari,  halafu unanunua unakwenda kuficha ili kusudi wazee hawa wahangaike, ili mwezi mtukufu wa Ramadhani utakapoingia watu wakose sukari, dawa yao ninayo" Amesema Rais Magufuli.

Aidha, akizungumza katika miji ya Katesh, Babati, Dareda na Magugu Mkoani Manyara Dkt. Magufuli amepokea malalamiko ya wananchi kuhusu kukosa maeneo ya kuendesha shughuli za kilimo na ufugaji, na amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Manyara Bw. Joel Bendera na wakuu wilaya za mkoa huo kukamilisha mchakato wa kuyapitia mashamba yote yaliyotelekezwa na wamiliki wake, kisha wawasilishe taarifa kwake ili afute hati za umiliki wa mashamba hayo na kuamuru wagawiwe wananchi.

"Kero kubwa katika maeneo haya, pamekuwa na mashamba makubwa ambayo yalichukuliwa na wenye pesa, halafu yale mashamba hawayaendelezi, na wanapoacha kuyaendeleza wanawachukua wananchi masikini na kuanza kuwakodisha, kwa kukusanya fedha, mniachie hili ndugu zangu nitalishughulikia" Amesisitiza Dkt. Magufuli.

Mjini Babati Rais Magufuli amepokea kilio cha wananchi waliodai kudhulumiwa haki zao na kujikuta wakipoteza mali ikiwemo nyumba za kuishi na mazao na amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Manyara kupanga siku za kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
Rais Magufuli amewasili Mjini Arusha akitokea Dodoma kwa njia ya barabara na kesho anatarajia kutunuku kamisheni kwa maafisa wapya wa Jeshi la wananchi Tanzania (JWTZ) kundi la 58/15 katika chuo cha mafunzo ya jeshi Monduli.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Arusha
06 Mei, 2016

Wasanii wa Injili wanufaika na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

0
0
 Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Joyce Hagu akizindua kujiunga kwa wanachama wa Chama cha Muziki wa Injili Tanzania (CHAMUITA) katika huduma ya Bima ya Afya kutoka kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) mapema wikiendi hii jijini Dar es Salaam.Kutoka kushoto ni Mlezi wa chama hicho Askofu Dkt. Rejoyce Ndalima,Rais wa Chama cha Muziki wa Injili Tanzania Addo November, Meneja wa NIHF Mkoa wa Kinondoni Constantine Makala na Mwimbaji wa nyimbo za Injili David Nyanda.
 Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Joyce Hagu akimkabidhi kadi ya uanacha wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) mwimbaji nguli wa muziki wa Injili mzee Makasi mapema wikiendi hii wakati wa hafla ya uzinduzi wampango wa wanachama wa chama cha muziki wa Injili Tanzania (CHAMUITA) kujiunga katika huduma ya Bima ya Afya. Katikati ni Meneja wa NIHF Mkoa wa Kinondoni Constantine Makala na Rais wa CHAMUITA Addo Novemba.

 Meneja wa NHIF Mkoa wa Kinondoni Constantine Makala akielezea namna wanachama wanavyonufaiki na huduma za mfuko huo mapema wikiendi hii wakati wa hafla ya uzinduzi wampango wa wanachama wa chama cha muziki wa Injili Tanzania (CHAMUITA) kujiunga katika huduma ya Bima ya Afya.
 Rais wa Chama cha Muziki wa Injili Tanzania (CHAMUITA) Addo November akizungumza na wanachama wa chama hicho wakati wa hafla ya uzinduzi wa mpango wa wanachama wa Chama cha Muziki wa Injili Tanzania (CHAMUITA) kujiunga katika huduma ya Bima ya Afya KUTOKA Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

MJASIRIAMALI ALIYEWEZESHWA NA AIRTEL FURSA AISHUKURU AIRTEL.

0
0
Kijana mjasiriamali Diana Moshi (Kulia) akimkabidhi keki Mkurugenzi wa kitengo cha Mawasiliano Airtel, Beatrice Singano Mallya (Kushoto) kama shukrani yake kwa Airtel baada ya kuwezeshwa  kupitia mpango wa Airtel FURSA "Tunakuwezesha" kwa kukabidhiwa vifaa vya kisasa vilivyomsaidia kuboresha biashara yake ya kupika keki na kumsaidia kupata mafanikio. Makabidhiano hayo yalifanyika katika makao makuu ya ofisi za Airtel Morocco jijini Dar es Salaam.

NAIBU WAZIRI ANGELINA MABULA AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA NHC

0
0
001Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline Mabula akifungua rasmi mkutano wa Baraza la wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye makao makuu ya shirika hilo Upanga jijini Dar es salaam ambapo alilipongeza shirika hilo kwa kazi nzuri ambayo wafanyakazi wake wanaifanya kwani ndiyo shirika pekee la Serikali linaloendeshwa kwa ufanisi mkubwa na kuiletea heshima serikali, Waziri Mabula amewaambia wafanyakazi wa shirika hilo pamoja na Menejimenti yake kuendelea na kazi nzuri ambayo wamekuwa wakiifanya ili kuleta maendeleo zaidi nchini katika sekta ya nyumba.
PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE.
11 Mkurugenzi wa Shirika hilo Bw. Nehemia Mchechu na Naibu Waziri Angelina Mabula wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa shirika hilo baada ya kuufungua rasmi mkutano huo.

Serikali yawataka wananchi kutumia mpango wa msaada wa kisheria.

0
0
 Wakili wa Serikali Mkuu kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Charles Mmbando akiwaeleza waaandishi wa Habari (Hawapo pichani) kuhusu huduma za msaada wa kisheria kwa wananchi ambao ni wahitaji wa msaada hiyo juu ya masuala mbalimbali yanayowakabili, Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Wizara hiyo Bi. Sheiba Bulu.
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia Mkutano huo.

TIB imetoa mikopo ya bilioni 550 kwa Watanzania.

0
0
Naibu Waziri, Wizara ya Fedha na Mipango, Mhe. Ashatu Kijaji akijibu maswali mbalimbali kuhusu Benki ya TIB na TADB katika kupunguza umaskini, leo Bungeni mjini Dodoma.

Na Benedict Liwenga-MAELEZO, Dodoma.
HADI kufikia mwaka jana (2015) Benki ya Uwekezaji Tanzania (TIB) imewawezesha Watanzania wengi kupambana na umaskini kwa kutoa mikopo ya zaidi ya shilingi bilioni 550 katika sekta mbalimbali za kiuchumi.

Taarifa hiyo imetolewa leo Bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Ashatu Kijaji wakati akijibu swali toka kwa Mbunge wa Karagwe, Mhe. Innocent Bashungwa (Mb) lililotaka kujua Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa Benki za TIB na TADB zinajielekeza kwenye utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

Mhe. Kijaji ameeleza kuwa, madhumuni ya kuanzishwa kwa benki ya TIB na TADB kama benki za maendeleo ni kutoa mikopo ya muda wa kati na muda mrefu kwa lengo la kufadhili miradi ya kimkakati, hivyo katika kutimiza azma ya kufadhili miradi ya kimkakati ya kufungua fursa za kiuchumi na kupunguza umaskini, TIB imetoa mikopo katika maeneo ya miji kupitia NHC, Viwanda vya kubangua korosho, maghala, mabomba ya maji, sukari na kilimo cha miwa, kukoboa na kusindika kahawa, kusindika matunda, mifuko ya kuhifadhia mazao na nyaya za umeme; vinu vya pamba na uzalishaji wa mafuta yatokanayo na mbegu za pamba na hoteli.

Aidha, TIB imetoa mkopo wa shilingi bilioni 489.2 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi 181 ya kusambaza umeme vijijini kupitia REA na kaya 257,000 zimenufaika na mradi huo. Pia vikundi 17 vya wachimbaji wadogo wadogo vimenufaika na mikopo jumla ya shilingi bilioni 8.

“Mikopo ya TIB kwa sekta na taasisi mbalimbali imesaidia kwa kiasi kikubwa kutoa ajira na kuendeleza zilizopo. Pia mikopo ya TIB imetumika kuongeza uzalishaji wa bidhaa zinazouzwa nje kama vile maua, kahawa na dhahabu”, alisema Kijaji.

Aliongeza kuwa pamoja na benki ya Kilimo kuchelewa kuanza kutoa mikopo, ni wazi kuwa benki ya TIB imejielekeza kwenye utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM pamoja na utekelezaji wa Mipango na mikakati mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Dira ya Taifa ya 2025, FYDB, SDGs 2030 pamoja na Afrika 2063.

TIB imewekeza katika mashirika ya umma kama vile Shirika la Reli (TRL), pia imeiwezesha TPDC katika mradi wa gesi na kuipatia Shirika la Ugavi Umeme Tanzania (TANESCO) mkopo kwa ajili ya fidia kwa wananchi ili kuweka njia mpya ya kusafirisha umeme.

MISS MBEYA WATEMBELEA KITUO CHA TRUST HEALTH AND WELLNESS CLINIC ILIYOPO FOREST YA ZAMANI JIJINI MBEYA.

WANANCHI WA KITONGOJI CHA PERA CHALINZE WAANZA KAMPENI YA KUPAMBANA NA MLIPUKO WA KIPINDUPINDU.

0
0
Mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdogo wa Chalinze Hussein Mramba akizungumza na wafanyabiashara mbali mbali wa kitongoji cha Pera Chalinze katika mkutano ulioandaliwa kwa ajili ya kujadili namna ya kupambana na mlipuko wa ugonjwa kipindu pindu.
 Baadhi ya wafanyabishara katika kitongoji cha pera Chalinze wakiwa katika Mkutano huo wa kujadili masuala ya usafi pamoja na kupambana na kipindupindu. 

KATIKA kuunga  mkono juhudi za serikali katika kupambana na magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu  wafanyabiashara  mbali mbali katika kitongoji cha Pera halmashauri ya Chalinze  Mkoa wa Pwani  wameungana na kuanzisha kampeni maalumu kwa ajili ya kutokomeza  taka zote  zinakuwa zikitupwa ovyo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti  katika kikao  kilichoandaliwa kwa ajili ya kuweza kujadili  mambo mbali mbali  kuhusiana na suala la usafi pamoja na kupanga mikakati ya kuweza kuhakikisha wanapambana  vilivyo na mlipuko wa ugonjwa wa kipindu pindu.
Viewing all 109589 articles
Browse latest View live




Latest Images