Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live

BREAKING NYUZZZ....: MSANII SNURA AFUNGIWA KUTUMBUIZA NA WIMBO WAKE CHURA PIA WAFUNGIWA

$
0
0
Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo leo imetangaza kuufungia wimbo na video ya Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Snura Mushi unafahamika kwa jina la CHURA kutokana na kutokuwa na maadili ya Mtanzania.

Wimbo huo pia umezuiwa kutumbuizwa mahala popote na kufungiwa kuchezwa kwenye redio na runinga nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo, Mkuu wa Kitengo cha mawasiliano wa wizara hiyo, Zawadi Msalla, amewaonya watu kutousambaza wimbo huo kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo WhatsApp na Istagram na kuongeza kuwa wale watakaokiuka agizo hilo watashtakiwa kwa kutumia sheria ya makosa ya mtandao.

Pia Wizara hiyo, imesitisha maonyesho yote ya hadhara ya Msanii huyo, mpaka pale atakapo kamilisha taratibu za usajili wa kazi zake zote kwa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).

Serikali imewataka wanasii mbali mbali nchini, kujiuliza mara mbili kabla ya kubuni kazi zao za sanaa.

Kumbukumbu

$
0
0
Hayati Mwalimu Michael Kapaya Kayila

Sasa ni miaka 16 tangu Baba yetu mpendwa Michael Kapaya Kayila ulipotutoka tarehe 15 Aprili 2000 saa 1.30 asubuhi katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama na kumfuata Mama yetu mpendwa Martha Nyamvula Lugenzi, aliyekutangulia tarehe 27 Desemba 1990 saa 9 usiku. 

Tunawakumbuka sisi watoto wenu tuliosalia Aurelia, Patrick, Grace, Mateo, na William.

Wajukuu zenu pia wanawakumbuka. Tunamshukuru sana Mungu kutupa nguvu na ujasiri wa kuendelea kuishi kwa upendo na mshikamano. Mwenyezi Mungu awaangazie raha za milele.

Kijipu upele Mtaa wa Kalenga, Upanga, karibu na hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam

$
0
0
 Barabara hii inaelekea hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam ambako kila dakika wagonjwa hupelekwa kwa ambulance. Na hapa mvua ndio imetuama mashimo hayo ni balaa kwa gari la wagonjwa


KUMBUKUMBU/IN LOVING MEMORY OF THE LATE JULIANA BANKOLWA MASHIBA 1934-2015

$
0
0
                                           JULIANA BANKOLWA MASHIBA
1934-2015

Mwaka mmoja umepita tangu mama yetu mpendwa ulipoitwa na mwenyezi Mungu tarehe 04 Mei, 2015 na kupumzishwa Kisesa, Mwanza siku ya tarehe 07 Mei, 2015.
Umetuacha katika majonzi makubwa lakini tukiwa na matumaini ya kuonana tena na tukimtukuza Mungu pamoja na Malaika na Watakatifu wote Mbinguni. Hatutasahau upendo, ucheshi, upole, hekima, bidii yako, Moyo wa kujitoa kuwahudumia wengine na kutopenda makuu.
Unakumbukwa na Mume wako mpendwa Martin, watoto wako Leah, Ben, Thobias, Sophia, Francis, Evarist, Venance, Renatus, George, na Leocadia, Wakwe zako, Wajukuu, Ndugu, Jamaa na Marafiki.

Familia itatoa sadaka ya shukrani katika ibada itakayofanyika siku ya Jumamosi tarehe 7 Mei, 2016 saa 3 Asubuhi Nyumbani kwa Mzee Martin Mashiba, Kisesa-Mwanza.

Raha ya Milele Umpe Ee Bwana na Mwanga wa Milele umwangazie, Apumzike kwa Amani. Amina

                                              THE LATE JULIANA BANKOLWA MASHIBA
1934-2015
Departed on 4th May, 2015
Time passes but fond and treasured memories remain, A year has gone but we still cannot bring ourselves to accept the fact that you are not here with us anymore.

Always warmly remembered with love, laughter, and affection by your husband Martin, Children Leah, Ben, Thobias, Sophia, Francis, Evarist, Venance, Renatus, George, Leocadia, In laws, Grandchildren, Relatives and Friends.


Thanks-giving mass will be held on Saturday 7th May, 2016 at Martin Mashiba’s Residence, Kisesa-Mwanza

TIB Corporate Bank yadhamini mkutano mkuu wa Bodi ya usajili wa Wakandarasi nchini

$
0
0
Mkurugenzi wa TIB Corporate Bank, Bwana Frank Nyabundege akimuelezea jambo Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa.

TIB Corporate Bank imefadhili mkutano mkuu wa bodi ya usajili wa wakandarasi nchini unaotarajiwa kufanyika jijini Mwanza kwenye hoteli ya Malaika kuanzia tarehe 5 hadi 6 mwezi huu wa tano ikifuatiwa na mkutano mwingine utakaofanyika jijini Dar es salaam katika ukumbi wa Daimond Jubilee kuanzia tarehe 26 hadi 27 mwezi huu wa tano. 

Mkutano huo, ambao mwaka huu una kauli mbiu ya ‘Kuwajengea Uwezo Wakandarasi wa Ndani kwa ajili ya Uchumi Endelevu: Changamoto na Mipango ya baadae?, unalenga kuwakutanisha wadau na wakandarasi kujadili mchango wa wakandarasi na ushiriki wao katika kukuza uchumi wa nchi.

Akizungumzia udhamini wa katika mkutano huo, Mkurugenzi wa TIB Corporate Bank, Bwana Frank Nyabundege alisema benki yake inazifahamu changamoto zinazowakabili wakandarasi wengi nchini ikiwemo ukosefu wa fedha ambao unazuia kupanua na kuendeleza uwezo wao wa kushindana katika sekta ya ujenzi hasa katika kupata zabuni na utekelezaji wa mikataba.

TIB Corporate Bank imeweka misingi ya kuhakikisha inatoa huduma bora kwa wateja wake na ndio maana tumeweza kuja na suhulisho kwa ajili ya kuwasaidia wakandarasi kuweza kuendesha shughuli zao kwenye mazingira yao ya kazi’ alisema Bw.Nyabundege.

Bwana Nyabundege pia alisema udhamini wa mkutano wa wakandarasi unalenga kujenga na kuimarisha uwezo wa wakandarasi kupata fursa ya kuendeleza sekta ya ujenzi nchini.TIB Corporate Bank ilianzishwa kwa lengo la kutoa huduma za nyongeza za kibenki kama mtaji wa kufanyia kazi, mikopo pamoja na uwezeshaji wa kibiashara kwa ajili ya wateja mbalimbali kupitia ubunifu wa teknolojia, kukuza thamani kwa wadau na pia kuchangia katika ujenzi wa taifa kwa kutoa huduma mtambuka za kifedha na kuchangia ukuaji wa uchumi shindani sambamba na Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025.

TIB imefanya mabadiliko ya kitaasisi ili kuweza kuwa kituo cha huduma zote za kifedha kwa kushughulikia mahitaji ya wawekezaji wa ndani wote kwa lengo la kusukuma maendeleo ya uchumi wa taifa.

TRA YAAZIMISHA SHEREHE ZA KODI JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Victor Kimaro (wa kwanza kushoto) akizugumza na wadau mbalimbali (hawapo pichani) juu ya uwezo wao wa kumudu ukusanyaji wa kodi vizuri ili waweze kufanikisha vizuri malengo waliyo jiwekea mwaka huu. Pia aliwashukuru (ITA) kwa kujitolea kutoa elimu kwa wawekezaji wote wanaofika hapa nchini iliwaweze kulipa kodi wanapo wekekeza hapa nchini. alizungumza hayo Siku ya maadhimisho ya sherehe ya siku ya kodi zilizofanyika kwenye ukumbi wa mikutano (TRA) Mwenge jijini Dar es Salaam 2016
Mdau akifafanua jambo kwenye sherehe ya siku ya kodi zilizofanyika kwenye ukumbi wa mikutano (TRA) Mwenge jijini Dar es Salaam 2016.
Sehemu ya wadau mbalimbali waliohudhuria hizo wakimsikiliza Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Victor Kimaro kwenye sherehe ya siku ya kodi zilizofanyika kwenye ukumbi wa mikutano (TRA) Mwenge jijini Dar es Salaam 2016. 

ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 8 KUTUMIKA KWA RUZUKU YA WACHIMBAJI WADOGO.

$
0
0
Teresia Mhagama na Mohamed Saif

BENKI ya Dunia (WB) imeahidi kutoa Dola za Marekani milioni 4 sawa na zaidi ya shilingi Bilioni 8, kwa ajili ya Ruzuku  katika shughuli za uchimbaji mdogo wa madini nchini.


Hayo yamebainishwa hivi karibuni jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo mara baada ya kumaliza kikao na watendaji Wakuu wa Benki ya Dunia wanaosimamia Miradi ya Sekta ya Madini.


Profesa Muhongo alisema kuwa sehemu ya fedha hizo za Ruzuku ambayo ni ya Awamu ya Tatu zitatolewa mwezi Septemba, 2016.

Aliongeza kuwa fedha hizo zitatumika kufadhili uendelezaji wa vituo Saba vya mfano vya utafutaji na uchimbaji mdogo wa madini ambavyo vitachaguliwa na Wizara baada ya kufanya tathmini ya maeneo yanayoweza kuwekwa vituo hivyo.


“Sio hivyo tu, Fedha hizi za Benki ya Dunia zinalenga kuwafadhili wanawake kwenye shughuli za uchimbaji mdogo wa madini, ukataji na uchongaji wa madini ya vito ili idadi ya wanawake wanaojishughulisha na Sekta ya Madini iongezeke,” alisema Profesa Muhongo.


Aidha, Profesa Muhongo alitoa wito kwa wataalam wote wanaosimamia miradi inayofadhiliwa na Benki ya Dunia katika Sekta ya Madini kuhakikisha kuwa utekelezaji wa miradi hiyo uende kwa kasi ili kuleta matokeoyaliyotarajiwa.                                                                                                                                                                                                                                                           
Benki ya Dunia kupitia Wizara ya Nishati na Madini imeendelea kutoa Ruzuku katika Uchimbaji madini mdogo ambapo katika mwaka wa Fedha 2015/16 zilitengwa takribani Shilingi bilioni 7.2 ambazo zilitolewa kwa vikundi 111 vya wachimbaji wadogo na watoa huduma mbalimbali katika sekta ya uchimbaji madini mdogo.


Vilevile, katika mwaka wa Fedha 2013/2014, Fedha za Ruzuku zilizotolewa kwa Wachimbaji Wadogo zilikuwa ni Dola za Marekani 500,000 sawa na takribani Shilingi Bilioni 1 zilizotolewa kwa waombaji 11. Fedha hizi ziliwalenga wachimbaji madini wadogo pekee tofauti na awamu zilizofuata.


Utoaji huo wa Ruzuku unaenda sambamba na utoaji wa elimu na mafunzo kwa wachimbaji wadogo wa madini waliopata ruzuku husika ili kuhakikisha kuwa shughuli zilizopata ufadhili zinaleta tija.

NEWS ALERT: "Filamu ya Imebuma" yabuma, Bodi ya Filamu Tanzania yaipiga stop

$
0
0
Muhusika Mkuu katika filamu ya “Imebuma” Bw. Eliasa Mkaly (Rashidi kisoda) akimbembeleza muigizaji na mtayarishaji wa filamu hiyo  Bi Sarah  Nyika (Asha Mauno) mara baada ya Bodi ya Filamu Tanzania kusitizasha  usambazaji wa filamu hiyo leo. Picha na Raymond Mushumbusi MAELEZO

Benki ya Exim yazindua kampeni kuhamasisha huduma bora kwa wateja

$
0
0
BENKI ya Exim Tanzania imezindua kampeni maalumu kuhamasisha matumizi ya kituo chake cha  huduma  kwa wateja kwa njia ya mawasiliano ya simu ikiwa ni sehemu ya mkakati wa benki hiyo kuhakikisha inawarahisishia wateja wake upatikanaji wa huduma  zake kupitia  teknolojia ya mawasiliano.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki wakati wa hafla fupi ya kuzindua kituo hicho,  Meneja Mwandamizi Huduma kwa wateja  wa Benki hiyo Bw. Frank Matoro alisema matumizi ya kituo hicho  yatawawezesha wateja wa benki hiyo kupata taarifa za kina kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo.
“Ni matarajio yetu kwamba wateja wetu watafurahia zaidi huduma bora kutoka kwa wahudumu wenye vigezo na uelewa wa kutosha kuhusiana na masuala ya kibenki kila siku za Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 1:00 jioni na siku za Jumamosi kuanzia saa 3 kamili asubuhi hadi saa 7:00 mchana kupitia namba yetu ya 0784 107 600,’’ alisema.
Kwa mujibu wa Bw Matoro kituo hicho tayari kimekwisha anza kutoa huduma huku akibainisha kuwa malengo ya kampeni hiyo ni kuhakikisha wateja wa benki hiyo wanatambua uwepo wa kituo hicho na kutumia ipasavyo huduma zitolewazo na kituo hicho.
“Katika kuhakikisha kwamba kampeni hii inaleta mafanikio, itaambatana na  droo ndogo ndogo zitakazowezesha utoaji wa zawadi mbalimbali kwa wateja  zikiwemo fulana zenye nembo ya benki, muda wa maongezi pamoja na simu mpya aina ya iPhone 5s,’’ alitaja.
Aliongeza kuwa huduma zinazotolewa na kituo hicho zinatolewa kupitia mazungumzo kwa njia simu, mitandao ya kijamii ikiwemo ukurasa wa Facebook na njia nyingine za kimtandao kama vile website na barua pepe.
Bw. George Shumbusho, mkuu wa kitengo cha hazina aliongeza kwamba: “Pia tunatarajia kwamba mafanikio ya huduma hii yatatuongezea ukubwa wa soko kwa kuwa itapanua wigo wa kuwafikia wateja, kujiongezea ukuaji wa fursa  sambamba na kutoa fursa kwa wateja wetu waweze kutupa mrejesho wa huduma mbalimbali tunazowapatia,’’
 Meneja Masoko Msaidizi wa Benki ya Exim Tanzania Mariam Mwapinga akisisitiza jambo mbele ya waandishi (hawapo pichani)  kuhusu kampeni maalumu kuhamasisha matumizi ya kituo  cha  huduma  kwa wateja kwa njia ya mawasiliano ya simu cha benki hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni.. Wengine ni pamoja na Mkuu wa kitengo cha hazina wa benki hiyo , Bw. George Shumbusho (katikati) na Meneja Mwandamizi Huduma kwa wateja  wa Benki hiyo Bw. Frank Matoro (kushoto).
Mkuu wa kitengo cha hazina benki ya Exim Tanzania , Bw. George Shumbusho (kulia), akikata utepe kuzindua kampeni maalumu kuhamasisha matumizi ya kituo cha  huduma  kwa wateja kwa njia ya mawasiliano ya simu cha benki hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Wanaoshuhudia ni pamoja Meneja Mwandamizi Huduma kwa wateja  wa Benki hiyo Bw. Frank Matoro (kushoto).

WAZIRI MWIGULU ATOA HOJA YA KUIDHINISHIWA KWA BAJETI YA 2016/2017 MBELE YA MWALIMU WAKE WA DARASA LA KWANZA.

$
0
0
Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mwigulu Nchemba akitoa hoja kwa Bunge kuidhinisha makadirio na matumizi ya fedha ya wizara hiyo kwa mwaka 2016/2017 leo mjini Dodoma huku akishudiwa na mwalimu wake Maria Mnkumbo (hayupo pichani) aliyemfundisha darasa la kwanza na la pili katika shule ya msingi Makunda iliyopo wilaya ya Iramba Mkoani Singida.(Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO, Dodoma)
Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mwigulu Nchemba akiwa katika picha ya pamoja na mwalimu wake Maria Mnkumbo (katikati) aliyemfundisha darasa la kwanza na la pili katika shule ya msingi Makunda iliyopo wilaya ya Iramba Mkoani Singida mara baada ya waziri huyo kutoa hoja ya Bunge kuidhinisha makadirio na matumizi ya fedha ya wizara yake kwa mwaka 2016/2017 leo mjini Dodoma. Kushoto ni mke wa Waziri Mwigulu Neema.
Mwalimu msataafu Maria Mnkumbo aliyemfundisha Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mwigulu Nchemba darasa la kwanza na la pili katika shule ya msingi Makunda iliyopo wilaya ya Iramba Mkoani Singida akiwa ndani ya ukumbi wa Bunge leo mjini Dodoma.Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mwigulu Nchemba akiwa na mwalimu wake Maria Mnkumbo aliyemfundisha darasa la kwanza na la pili katika shule ya msingi Makunda iliyopo wilaya ya Iramba Mkoani Singida mara baada ya waziri huyo kutoa hoja ya Bunge kuidhinisha makadirio na matumizi ya fedha ya wizara yake kwa mwaka 2016/2017 leo mjini Dodoma.

WANAODAI BUNGE KUONYESHWA LIVE WATAKIWA KUOMBA KWA UTULIVU

$
0
0
Katibu Mkuu wa National Reconstruction Alliance (NRA) Hassan Kisabya Almas amewataka Watanzania wanaoomba Bunge  la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuonyeshwa  kupitia matangazo ya moja kwa moja (Live) kuomba  kwa utaratibu bila kuharibu amani ya Tanzania.

Aidha Katibu Mkuu wa Chama hicho, amesema  kwamba   amani iliyoko ni hazina kubwa ambayo nchi nyingine inatamani kuwa nayo. 

Almas aliyasema hayo leo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Idara ya Habari(MAELEZO). 

“Leo hii tupo tunaopigania kutaka kuona Bunge Live, lakini yote haya ni kwa kuwa Tanzania amani tunayo, sidhani kama nchi kama Afghastan siku watakayoamua kuonyesha Bunge Live kwa mwaka mzima, kwa saa 24 kama wataweza kukaa kuangalia Bunge hilo, hivyo basi wale wanaotaka hayo, kwanza tudumishe amani  yetu,” alisema Almas.

Almas alieleza kuwa, amani ya Tanzania ni zaidi ya dhahabu ambayo Tanzania inajivunia hivyo ni lazima Watanzania kuitunza na kuithamini amani ambayo ipo kwa sasa na kuacha kuchochea mambo ambayo yanaweza kuleta machafuko katika nchi na amani ambayo leo haithaminiwi ikaja kukumbukwa siku moja.

Pia, alisema yeye ni mmojawapo wa watu wanaopenda kuona Bunge Live lakini jambo hilo halishadadii kama inavyofanywa na watu wengine kwani anajua kwa kufanya hivyo anaweza kuhatarisha Amani ya Tanzania na hata hilo Bunge halitaweza kuliona tena kutokana na kutokuwa na Amani ndani ya nchi.

Vilevile, amewataka waandishi wa habari kuandika yale yaliyo mazuri ya nchi kuliko mabaya machache ili kuzidi kuitangaza Tanzania vyema kimataifa, kwani sio uzalendo kuona mambo yote mabaya yanakuwa ukurasa wa kwanza, bali kwanza yarekebishwe kwakuwa ni makosa yanayoweza kurekebishwa. Kalamu za waandishi wa habari ni chachu ya amani na maendeleo ya Taifa la Tanzania.

Serikali yaeleza Mikakati yake katika kuhakikisha Usawa wa Kijinsia Katika Elimu nchini

$
0
0
Wahitimu wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari WAMA- Nakayama wakionyesha maonyesho ya masomo kwa Mgeni Rasmi, Mhe. Ummy Mwalimu, Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete pamoja na wageni waalikwa.
Mke wa Rais Mstaafu na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akisoma hotuba yake kwa wageni waalikwa na wahitimu wakati wa Sherehe za Mahafali ya kwanza ya Kidato cha Sita ya Shule ya WAMA- Nakayama.
Mgeni Rasmi Mhe. Ummy Mwalimu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto akihutubia wahitimu, walimu na wageni waalikwa wakati wa sherehe za mahafali.
Wahitimu wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari ya WAMA - Nakayama katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa WAMA mara baada ya kumkabidhi Cheti cha Shukrani kwa mchango wake katika maendeleo ya elimu yao.

Hilal Hilal aiomba Serikali, wadau kutatua changamoto za mchezo wa kuogelea

$
0
0
Hilal Hilal wa kwanza kulia mara baada ya
kushinda medali ya Shaba nchini
Mauritius katika mashindano
ya Cana Kanda ya Nne
Muogeleaji namba mmoja nchini kwa upande wa wanaume, Hilal Hemed Hilal ameiomba serikali kufanya jitihada za kutatua changamoto mbalimbali zinazoukabili mchezo wa kuogelea nchini.

Hilal ambaye  hivi karibuni alishinda medali ya  Shaba katika mashindano ya Cana Kanda ya nne alisema kuwa Tanzania ina waogeleaji wengi wenye vipaji na malengo ya kufanya vyema katika mchezo huo, ila tatizo kubwa ni vifaa ambavyo watatumia kufikia malengo yao.

Alisema kuwa moja ya changamoto kubwa ni bwawa la kuogelea lenye vifaa vya kisasa kwa ajili ya kutimiwa na waogeleaji  wa Tanzania katika mashindano na mazoezi.  Alisema kuwa Tanzania ina mabwawa ya kuogelea ambayo hayana ubora kwa mujibu wa sheria na taratibu za mchezo huo kama za chama cha kuogelea Duniani (Fina) na chama cha Afrika (Cana).

Alifafanua kuwa mabwawa mengi ya Tanzania ni ya mita 25 ambayo hayatumiki katika mashindano ya kimataifa kama ya Cana, Michezo ya Jumuiya ya Madola, Olimpiki na mashindano ya dunia ya kuogelea.

“Mabwawa yapo, lakini si ya viwango vya Cana na Fina, mbali ya mabwawa pia tunahitaji  touchpad  kwa ajili ya kurekodi muda kwa muogeleaji   siyo kwa kutumia stop-watch kama ilivyo sasa, katika mashindano ya kimataifa, stop watch zinatumika sambamba na touchpad ambayo inaendeshwa kisasa si kwa mtu kuendesha kifaa hicho,” alisema  Hilal.

Alisema kuwa mbali ya  mabwawa ya kisasa, mabwawa hayo pia hayana vifaa vinavyotakiwa kutimia wakati wa kuanza kuogelea ‘Diving blocks’ ambazo ni za kielektroniki. Alisema kuwa mara zote wao huvitumia vifaa hivyo wanapokwenda nje ya nchi kwenye mashindano.

“Hapa hakuna jinsi, unalazimika kuwahi siku mbili kabla ili ufanye mazoezi, lakini wenzetu wanavyo katika nchi zao, pia hata vilabu vya mchezo huo wanatumia vifaa hivyo, ni changamoto kwetu kwani unaweza kufutiwa matokeo kwa kushindwa kuanza kwa mujibu wa taratibu,” alisema.

Alisema kuwa pamoja na ukweli kuwa serikali ina majukumu mengi, kwa niaba ya waogeleaji anaomba changamoo hizi zifanyiwe kazi na kuweza kupata hata bwawa moja la kisasa la kuogelea lililosheheni vifaa hivyo vya kisasa.

Aliongeza kuwa mchezo wa kuogelea kwa sasa unashika kasi kubwa, lakini viongozi wa vilabu wanaweza kukata tama kutokana na changamoto hizo.  Hilal pia amewaomba wadau kusaidia serikali kutatua tatizo hili.

KUTANA NA ‘GREEN VOICES’, SAUTI ZA AKINAMAMA WAPAMBANAO NA MABADILIKO YA TABIANCHI

$
0
0
WANAWAKE wapatao 15 hivi karibuni walihudhuria mafunzo ya kuongeza ujuzi wa jinsi ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi nchini Spain. Mafunzo na mradi huo vinafadhiliwa na Taasisi inayojihusisha na maendeleo ya wanawake wa Afrika, ijulikanayo kama Foundation for Women of Africa  inayoongozwa na Makamu wa Rais mstaafu waSpain Mama  María Teresa Fernández de laVega.

Taasisi hiyo itafanya kazi na wanawake hao 15 wa kitanzania kupitia miradi inayosaidia nchi kupambana na mabadiliko ya tabianchi. Wanawake hao ambao kati yao watano ni waandishi wa habari kila mmoja atatekeleza mradi mmoja, huku waandishi wa habari wakisaidia kupaza sauti za akinamama hao kupitia vyombo mbalimbali vya habari nchini.

Mradi huu unaojulikana kama GREEN VOICES una lengo la kupaza sauti za akinamama kueneza ujuzi wao wa kupambana na mabadiliko ya tabianchi ili jamii nzima ya kitanzania iweze kujifunza zaidi na kuzitumia mbinu hizo katika kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

Mradi huo unaoratibiwa hapa nchini na Mtandao wa wanahabari wa Mazingira (EMNet) kwa niaba ya Foundation for Women of Africa unatekelezwa katika mikoa sita ya Kigoma, Kilimanjaro, Mwanza, Morogoro, Dar es Salaam na Pwani ukihusisha miradi ya kilimo, usindikaji, ufugaji na utafiti.

Mratibu wa EMNet Secelela Balisidya amesema akinamama hao wanatekeleza miradi ambayo inachangia moja kwa moja aidha kupambana au kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi. Amesema miradi hiyo ni mradi wa kilimo cha miti ya matunda mkoani Kigoma, kilimo cha viazi lishe visiwani Ukerewe mkoani Mwanza, Ufugaji Nyuki mkoani Morogoro na Pwani na ukaushaji wa mbogamboga kwa kutumia nishati ya jua mkoani Morogoro. 
Akinamama wanaoshiriki katika mradi wa kupaza sauti za wanawake wanaopambana na mabdiliko ya tabianchi – Green Vocies katika picha ya pamoja na viongozi wa Foundation For Women of Africa na wafadhili wa mradi huo, mara baada ya uzinduzi wa mradi huo Madrid, Spain hivi karibuni.
Mama Maria Tereza (katikati) - Rais wa taasisi ya Foundation for Women of Africa akiwa na waandishi wa habari wanaotekelza mradi wa Green Voices wakati wa hafla ya kuwakaribisha kinamama nchini Spain. Kutoka kushoto ni Secelela Balisidya, Tukuswiga Mwaisumbe, Farida Hamis, Siddy Mgumia na aliyechuchumaa Judica Losai.
Akinamama wanaoshiriki katika mradi wa kupaza sauti za wanawake wanaopambana na mabdiliko ya tabianchi – Green Vocies katika picha ya pamoja na uongozi wa chuo kikuu cha Universitad Automous De Madrid, mara baada ya kutembelea mazingira ya chuo hicho Madrid, Spain hivi karibuni.

TATIZO LA AJIRA LINAENDELEA KUWA CHANGAMOTO KWA VIJANA ZANZIBAR

$
0
0
Mkurugenzi wa Idara ya Ajira Ameir Ali Ameir
Na Miza Kona Maelezo- Zanzibar 

Mkurugenzi wa Idara ya Ajira Ameir Ali Ameir amesema tatizo la ajira nchini bado ni changamoto kubwa kwa vijana kutokana vijana wengi kukosa sifa za kuajiriwa na baadhi yao kuchagua kazi za kuajiriwa.

Hayo ameyasema leo katika Ukumbi wa Kidongo chekundu wakati alipokuwa akifungua mafunzo ya Kuwajengea Uwezo wa Kamati za Ajira za Wilaya za Mjini na Magharibi.

Amesema vijana ndio nguvu kazi katika jamii hivyo wana nafasi kubwa katika kulitumika Taifa kwa kufanya kazi lakini mtazamo wa vijana bado ni tatizo na baadhi wamejenga tabia ya uvivu unaopelekea kuwepo kwa vijana wengi wanaomaliza masomo wakiwa wazururaji wasio na ajira.

Mkurugenzi huyo amezitaka kamati za ajira kujipanga vizuri kuyafuatilia matatizo yanayowakabili vijana kupitia vigezo vyao, masheha, waajiri, mtazamo pamoja Utamaduni wao ili kuwanusuru kujiingiza katika vikundi viovu.

“NI kazi ya kamati kupita kwa waajiri ili kuangalia Changamoto, mafanikio attitude na Utamaduni kwa vijana pia unaweza kufahamu matatizo ya vijana kupitia vigezo vyao pia wazee wana nafasi gani katika kuwasaidia vijana,” alifahamisha Mkurugenzi Ameir.

Aidha amezifahamisha kamati hizo kutafuta taarifa yakinifu kwa vijana ili kupata kujua matatizo ya ajira yanayowakabili na kuweza kuwasaidia na kuwaingiza katika soko la ajira.Ameeleza kuwa vijana wanahaki ya kupata kazi yenye heshima inayoendana na mazingira bora ambayo yatamjenga kuweza kufanya kazi kwa ufanisi na kumpatia kipato cha kujikimu kimaisha na kuondokana na utegemezi.

Akiwasilisha Mada ya Mpango Kazi wa Ajira kwa Vijana Afisa Ajira Kutoka Idara ya Ajira Mustafa Hassan Makame amesema serikali imeweka mikakati mbali mbali ili kuhakikisha inakabiliana na tatizo la ajira na kuona kwanba tatizo hilo linapungua nchini.“Ujasiri amali ni njia ya kutatua tatizo la ajira kwa vijana na sio ajira za serikali peke yake hivyo vijana wana nafasi kubwa ya kujiajiri wenyewe,” ameeleza afisa huyo. 

Nae Mtaalamu kutoka Shirika la Kazi Duniani Edmund Mushy amesema serikali pekee haiwezi kulitatua tatizo la ajira kwa vijana ni lazima pawepo mashirikiano na wadau wengine ikiwemo sekta binafsi na taasisi nyngine kwani nao wana mchango mkubwa katika kukuza ajira nchini.

Wakichangia mada washiriki wa mafunzo hayo wameiomba wizara kuweka mratibu wa ajira katika Wilaya zote atakaeshughulia masuala ya ajira ili kuondosha usumbufu uliopo katika wilaya hizo na kamati ziweze kufanya kazi walizopangiwa kwa ufanisi.

NAIBU KATIBU MKUU WA WIZARA YA NISHATI NA MADINI DK. MHANDISI JULIANA PALLANGYO AKUTANA NA WATENDAJI KUTOKA TPDC KWA AJILI YA KUJADILI MATUMIZI YA GESI ASILIA

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Dk. James Mataragio (mbele) akielezea mikakati ya shirika hilo katika matumizi ya gesi asilia inayozalishwa kwa ajili ya matumizi ya majumbani na nyingine kuuzwa katika soko la nje katika kikao kilichokutanisha Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati, Dk. Mhandisi Juliana Pallangyo kilichofanyika jijini Dar es Salaam. Lengo la kikao hicho lilikuwa ni kujadili matumizi ya gesi iliyogunduliwa nchini katika matumizi ya ndani na nyingine kuuzwa nje ya nchi.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AAGANA NA BALOZI CHIKAWE, AKUTANA NA BALOZI WA DENMARK

$
0
0
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi Mathias Chikawe ambaye ameteuliwa kuiwakilisha Tanzania nchini Japan Balozi Chikawe alipofika  kumuaga Waziri Mkuu ofisini kwake mjini Dodoma leo akiwa tayari kwenda kuanza kazi yake.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi wa Denmark nchini Tanzania Bwana Einar Jensen ambaye alifika ofisini kwa waziri mkuu mjini Dodoma kwa mazungumzo ya kikazi. 
Picha na Chris Mfinanga

KAMISHNA JENERALI ZIMAMOTO ATEMBELEA VITUO VYA ZIMAMOTO JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye aanza ziara ya kutembelea  vituo, pamoja na kujitambulisha kwa maafisa na askari kwa mara ya kwanza kwa kuanzia  mkoa wa dar es salaam.

Katika ziara hiyo Kamishna Jenerali alipata fursa ya kukagua mradi wa ujenzi wa bwalo la chakula liliopo mkoa wa kinondoni kwa ajili ya kurahisisha upatikani wa huduma kwa askari.

Pia amesisitiza kufufua visima vya maji ya kuzima moto (fire hydrant) kwa kushirikiana na ofisi ya idara ya maji  ili kurahisisha kupatikana kwa maji yanapohitajika na jeshi la zimamoto na uokoaji.

Amesema kuwa kwa kushirikiana nao itasaidia kufufua visima vilivyokufa au kuingiliwa na makazi ya wananchi na kufanya zoezi la upatikanaji wa  maji ya  kuzima moto kuwa karibu na  wazimamoto watapata maji na kurudi kwenye tukio kwa haraka zaidi.
Konstebo Said Sengendu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Kituo cha Ilala akitoa maelezo ya utumiaji wa vifaa mbalimbali vilivyopo katika magari ya kuzima moto na maokozi kwa Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo,  Thobias Andengenye . (Picha na FC Godfrey Peter)
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye (wa kwanza kushoto) akiongozwa na Kamanda wa Zimamoto Mkoa wa Kinondoni, Mrakibu Msaidi Peter Mabusi wakikagua mradi wa ujenzi wa bwalo la chakula lililopo katika kituo cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Lugalo.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye (aliyeketi kulia) akipokea taarifa ya utendaji kazi kutoka kwa Kamanda Kanda Maalumu ya Dar es salaam, Kamishna Msaidi, Jesuald Ikonko alipotembelea kituoni hapa leo hii mapema asubuhi katika ziara ya kutembelea vituo vya zimamoto nchini.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye akipokea maelezo kutoka chumba cha mawasiliano namna ya upokeaji taarifa ya miito ya dharura .

SOMETHING IN PIPELINE- WHO WOULD BE THE EARLY BIRDS IN UGANDA-TANZANIA OIL EXPORT PIPELINE

$
0
0
A few weeks ago , we heard lots of talks about the viable routes for Ugandan crude oil export pipeline. And it was the hot talking point in Tanzania’s petroleum industry, East Africa perhaps entire world.
Thankfully, Uganda picks Tanzania rather than Kenya. And I’ve strong feeling you’re happy with such achievement. Right?. Seriously,  I’m thrilled, too.

But the great question lingered in mind. Who will be the early birds in this project.?
Sound Confusing? Let me clarify.

Early birds are people who take early advantages of a situation. They have eagle eyes to notices opportunity even it’s kept under wrap. And grabs it at an alarming rate.

But wait.. Something in pipeline. Guess what? Jobs and business opportunities
Do You want to be the early bird? If so, Listen up. Here’s a deal ,for Investors and Job seekers
Investment In Oil Pipeline

Participatory environmental and social monitoring.
This is an opportunity to inform local members about environmental and social management during pipeline construction
So what I’m talking about? Just keep reading you’ll find out
The easy route to make huge Cash In Tanzania’s gas industry simply fix problems
The 1120-km pipeline crosses various landscapes and ecosystem. Most importantly, the pipeline passes through remotely located areas in which Local communities are dependent on specific ecosystem and Culture.
The proposed pipeline moves through Biharamulo Games reserves, river Kagera in Uganda and Pangani river .Many affected communities depend heavily on fishing and agriculture.
Regarding instant changes and lack of awareness. Local member might feel that the project would ruin their live hood even contribute to the poverty.

And that’s where you come in and make huge cash through consultation and engagement program undertaken through.
You inform community members about the potential benefit and impact of the projects .
 consulting with local communities their environment concerns about oil pipeline operation and how they can overcome

Ensuring Communities have clear understanding of the projects and how it’ll impacts their lives
Ensuring locals get regular information on social and environment performance of the projects.

The cool thing is, even major Oil companies that are engaging in the projects are interesting with such good practices, as they impact their business. I assure you they’ll partner with you in addressing such challenges
As you involve the local community in overall environmental and social aspect of pipeline construction. You build trust with local members and you address the wrong perception on impact of the pipeline.

Oil Pipeline Construction Jobs opportunities
As many of you know, the oil price is going down drain. Upstream Oil companies are struggling.
They cut costs. Sadly, many Oil and gas employees are kicked out of the companies. And they’ve to find an alternative source of income. 

I know the feeling. And I’ve been there.
Even so, petroleum exploration companies would not listen to you right away. They’re hurting in response to oil price drop.
So, if you’re strategy career in Tanzania’s oil and gas industry. Petroleum pipeline industries are booming.
The oil pipeline projects will create over 15000 employees. But how do you find such jobs?
Here’re few tips

Stay up to dated with the latest news in oil and gas sector.
Information is a power of you’ve you informed. Otherwise, you deformed. Knowing the trend in the industries you stand much chance of making cut in the interview

Contacts
Find who to contact, Some oil and gas jobs are never advertised anywhere and is filled because someone who know someone else. Don’t underestimate the power of network.
The more people you know, the more you move closer towards the jobs.
If you’re wondering what kinds of jobs are in the oil pipeline. Here’re some of them.
Petroleum Pipeliner Jobs.

You’ll be responsible for maintenance, repair, and laying pipe
Line Walkers jobs.

Involve detecting leakage of oil in the section of pipes. It requires problem-solving capability
Pipeline Inspector jobs:

Your main duty will be inspecting drilling and casing pipe using optical equipment and locating cracks .
Pipeline supervisor :

You’ll be a coordinator of all workers in installation of pipe valves pipeline
Are you want to be the early bird in the oil and gas in Tanzania
If  so, what are you waiting for? Tanzania oil and gas is a money making  industry. Got out there.Make it happen and get your fair share.

I’d love to know your thought. Please, call or email me and I’ll respond shortly

Hussein Boffu
Petroleum Geosciences Graduate
0655 37 65 43
Hussein.boffu@tanzaniapetroleum.com
www.tanzaniapetroleum.com

MAADHIMISHO YA SIKU MKUNGA DUNIANI KUFANYIKA KESHO JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Rais wa chama cha Wakunga Tanzania (TAMA) bi.Feddy Mwanga akizungumza leo na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu maadhimisho ya siku ya mkunga duniani yatakayofanyika kesho , jijini Dar es Salaam, Kulia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wakunga Tanzania Dkt. Sebalola Leshabari .
Katibu Mkuu wa Chama cha Wakunga Tanzania (TAMA) Dk. Sebalola Leshabari akiwasilisha maada katika mkutano wa kuelekea maadhimisho ya Mkunga Duniani, uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wadau mbalimbali waliofika kwenye mkutano wa kuelekea maadhimisho ya siku ya mkunga duniani, uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka wa Globu, Jamii)
Viewing all 110181 articles
Browse latest View live




Latest Images