Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Bw. Lephy Gembe (Katikati) akizungumza na maafisa wa kutoka TADB wakati walipomtembelea Ofisini kwake. Wanaomsikiliza ni Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Robert Paschal (Wapili kushoto) na Meneja wa Maendeleo ya Biashara wa TADB, Bw. Geofrey Mtawa (Kulia) na Afisa Maendeleo ya Biashara Mwandamizi wa TADB, Bw. George Nyamrunda (Kushoto).
Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Lephy Gembe (Kulia) akimsikiliza Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Robert Paschal (Kushoto) wakati akitoa maelezo kuhusu Wajibu wa TADB katika kuendeleza kilimo nchini.
Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Robert Paschal (Kushoto) akimsikiliza i Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Lephy Gembe (Kulia) walipomtembela Ofisini kwake.
Na Mwandishi wetu.
Benki mpya ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imeaswa kutoa elimu kuhusu kilimo bora ili kuchagiza na kusaidia Mapinduzi ya Kilimo kutoka kilimo cha kujikimu kwenda cha kibiashara ili kuchangia kwenye ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini.
Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Bw. Lephy Gembe wakati akiongea na Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Robert Paschal alipomtembelea Ofisini kwake.
Bw. Gembe alisema kuwa ili kuinua uzalishaji wenye tija katika Sekta ya Kilimo kwa kuendeleza TADB ina wajibu wa kutoa elimu ya kina kuhusu kilimo cha kisasa kwa kutilia mkazo kuhusu miundombinu muhimu ya kilimo mathalani skimu za umwagiliaji za kilimo ili kuongezea tija shughuli hizo za kilimo.
“TADB muna wajibu wa kuhamasisha kilimo cha kisasa na cha kibiashara kwa wakulima wadogo wadogo ili waweze kubadilisha fikra zao kutoka kilimo cha mazoea na kufikiria kilimo cha kisasa chenye tija kitakachoongeza kipato cha wakulima hao,” alisema Bw. Gembe.