Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110185 articles
Browse latest View live

BARAZA LA WAFANYAKAZI WA WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (SEKTA YA UJENZI) LAKUTANA

$
0
0
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Sekta ya Ujenzi ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Eng. Joseph Nyamhanga, akiongea na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi sekta ya ujenzi kabla ya kulifungua rasmi baraza hilo lililofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Watendaji Wakuu wa Sekta ya Ujenzi wakiwa katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi sekta ya ujenzi lililofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi (sekta ya ujenzi) wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Sekta ya Ujenzi ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wa sekta hiyo Eng. Joseph Nyamhanga, katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi kililofanyika jijini Dar es Salaam.
Mtafiti wa masuala ya Hifadhi ya Jamii kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) Bw. Michael Semiono akifafanua jambo kwa wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Sekta ya Ujenzi.

AGA KHAN UNIVERSITY-ARUSHA CAMPUS CONSTRUCTION IN THE OFFING

$
0
0
East African Community (EAC) Headquarters, Arusha, Tanzania: April 22, 2016: Construction of the Aga Khan University (AKU) is in the offing in Arusha, Tanzania and the move is viewed as a catalyst for positive transformation that will see the city expand as the intellectual, social and political hub for East Africa. The project which is part of a planned USD $500 million expansion in East Africa by H.H the Aga Khan, seeks to enroll health sciences and arts students from across the region, notably from Kenya, Tanzania, Uganda, Rwanda, Burundi and South Sudan.

In solidarity, EAC Executives paid a visit to the proposed site situated 4km from Arusha Airport on Dodoma road. The site covers 3200 acres out of which the potential area for investment rests on 1700 acres.
A depiction of the Aga Khan University-Arusha Site Plan

On behalf of the EAC Secretary General Amb. Dr. Richard Sezibera, the Deputy Secretary General in charge of Productive and Social Sectors; Hon. Jesca Eriyo accompanied the Speaker of the East African Legislative Assembly; Rt. Hon. Daniel Kidega and the East African Court of Justice Judge President; Hon. Justice Emmanuel Ugirashebuja to the Aga Khan University (AKU) site in Arusha.

Receiving the Executives from EAC was the Director, Aga Khan University Campus Development in Tanzania; Nizar Jaffer Somji. Others were the Diplomatic Representative of the Aga Khan Development Network (AKDN) in Uganda; Mahmood H. Ahmed, the Project Director, Arusha Campus; Nasir Peerani, the Resident Representative; Amin Kurji, the Reforestation Manager; Roshan Hemani and the Community Engagement Officer; Lazaro Ole Mongoi.

In 2007, H.H the Aga Khan announced plans to build a major new University campus in Arusha. The decision to erect a new campus in Arusha stemmed from his faith in the future of the East African Region. The new development represents the biggest expansion for AKU since it opened its first campus in Karachi, Pakistan about 25 years ago.
The Director, Aga Khan University Campus Development in Tanzania and Jaffer CEO; Nizar Jaffer Somji (front right) welcomes and ushers in the EALA Speaker; Hon. Daniel Kidega (Front left), EACJ Judge President; Hon. Justice Emmanuel Ugirashebuja (back left) and EAC Deputy Secretary General in charge of Productive and Social Sectors; Hon. Jesca Eriyo (back right).

AKU’s ambitious 15 year-plan includes a significant commitment of global resources to the East African region through the expansion of the University’s presence in Arusha, transforming EAC’s capital into a “regional intellectual epicenter“.

Before a tour of the site was a presentation on the site plan outlining some of the facilities the project will offer. These include; a primary and secondary school, a university and a university hospital, housing for students and staff, a training hotel and retail outlets.

Currently, the design plan for the construction of the project is at its final stages and execution of the design plan is expected to commence soon after its completion. On-site activities within the project include a reforestation programme which is ongoing and community engagement activities such as health camps, community based savings groups, fodder distribution among others.
EALA Speaker; Hon. Daniel Kidega, EACJ Judge President; Hon. Justice Emmanuel Ugirashebuja and EAC Deputy Secretary General in charge of Productive and Social Sectors; Hon. Jesca Eriyo pause for a group photo at the site with representatives from the Aga Khan Development Network (AKDN) led by the the Director, Aga Khan University Campus Development in Tanzania and Jaffer CEO; Nizar Jaffer Somji and other EAC officials.

In his remarks, the Speaker was impressed with the project plan and commended AKDN’s efforts to not only invest in a bid to make profit but also to benefit the surrounding population, an effort he termed as ‘humanitarian capitalism’. He remarked that the Assembly was keen to enact relevant piece(s) of legislation that would anchor the vision of the Aga Khan.

Being her first visit to the Arusha Campus site, the Deputy Secretary General Hon. Eriyo stated that she was eager to see the project materialize. Hon. Eriyo emphasized that; “The community needs to know that the project is for their benefit therefore raising awareness about the project, creating job opportunities for the youth within the project and identifying areas of co-investment and partnerships with the locals by engaging CSOs and other community based interest groups is key in order to build the capacity of the community economically as underpinned in the project’s objectives.”

The EACJ Judge President concluded with a congratulatory message to H.H the Aga Khan for the success of the Aga Khan Foundation projects so far, adding that the EAC is highly committed to offer as much support to ensure that the upcoming project is a success for the benefit of future EAC generations.

Safari za Treni ya Mwakyembe zaongezwa sasa treni kusimama Kamata awamu ya jioni kuanzia Jumatatu!

$
0
0
Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) umetangaza kuongezwa kwa safari moja ya ziada kwa kila awamu ya usafiri huo kuanzia siku ya Jumatatu Aprili 25, 2016. Hivyo basi awamu ya asubuhi na ile ya jioni itakuwa na safari 4 badala ya 3 za sasa, halikadhalika muda wa kuanza safari nao umebadilishwa. 
Kwa awamu ya asubuhi treni ya kwanza itaondoka Ubungo Maziwa kuja kituo kikuu cha Dar es Salaam saa 12:15 ambapo itawasili saa 12:55. Safari ya mwisho ya nne itaondoka Ubungo Maziwa saa 5:15 asubuhi kwenda Kituo Kikuu cha Dar es Salaam. 
Kwa awamu ya jioni kutoka Kituo Kikuu cha treni cha Dar es Salaam safari ya kwanza itaanza saa 10:00 jioni  itawasili Ubungo Maziwa saa 10:40 jioni. Safari ya pili kutoka Kituo cha Dar es Salaam itaanza saa 11:40 na kuwasili Ubungo  Maziwa saa 12:20 jioni. Halikadhalika safari ya 3 itaanza kutoka kituo cha Dar es Salaam saa 01:20 usiku na ile ya 4 saa 3:00 usiku kwenda Ubungo Maziwa. 
Halikadhalika taarifa hii ya mabadiliko ya safari za treni ya jiji imeainisha kuwa Kituo cha Kamata kitatumika kwa safari zote 4 za awamu ya jioni kwenda Ubungo Maziwa  na kurudi Kituo cha Dar es Salaam.

Uamuzi huu umechukuliwa ili kukidhi maombi ya abiria waliokuwa wanataka kituo cha Kamata kitumike kwa huduma ya treni ya Jiji awamu ya jioni.

Aidha wito maalum umetolewa na Uongozi wa TRL kuwa abiria na wadau wote wa huduma ya treni ya Jiji kufuata kwa makini maelekezo ya wahudumu wa treni hiyo ili kuongezwa kwa safari za huduma hiyo kuwe na tija kwa abiria na Kampuni ya TRL.


RATIBA MPYA YA TRENI YA JIJI KUANZIA APRILI 25, 2016


AWAMU     YA ASUBUHI

KITUO

KUWASILI

KUONDOKA



UBUNGO MAZIWA

SAA 12:05

SAA 12:15



DAR

SAA `12:55

SAA 01:05



UBUNGO MAZIWA

SAA 01:45

SAA 01:55



DAR

SAA 02:35

SAA 02:45



UBUNGO MAZIWA

SAA 03:25

SAA 03:35



DAR

SAA 04:15

SAA 04:25



UBUNGO MAZIWA

SAA 05:05

SAA 05:15



DAR

SAA 05:55



AWAMU YA JIONI






DAR


SAA 10:00



UBUNGO MAZIWA

SAA 10:40

SAA 10:50



DAR

SAA 11: 30                                                     

SAA 11:40



UBUNGO MAZIWA

SAA 12:20

SAA 12:30



DAR

SAA 01:10

SAA 01:20



UBUNGO MAZIWA

SAA 02:00

SAA 02:10



DAR

SAA 02:50

SAA 03:00



UBUNGO MAZIWA

SAA 03:40

SAA 03:50



DAR

SAA 04:30




Imetolewa na Afisi ya Uhusiano kwa Niaba ya :

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TRL,

Nd Masanja Kungu Kadogosa

Dar es Salaam,

Aprili 22, 2016.



SERENGETI BOYS KUCHEZA NA TIMU YA TAIFA MAREKANI U17

$
0
0
 Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini India (AIFF) limetoa ratiba ya michuano ya vijana (AIFF Youth Cup 2016 U-16) itakayoanza kutimua vumbi Mei 15 -25 katika mji wa Goa nchini India kwa Serengeti Boys kufungua dimba na Marekani.

Michuano ya AIFF inashirikisha timu tano za vijana wenye umri chini ya miaka 17 kutoka nchi za Korea Kusini, Marekani, Malysia, Tanzania na wenyeji India.

Mashindano hayo yatafanyika katika uwanja wa Tilak Maidan, Vasco, Goa kuanzia Mei 15, ambapo Tanzania itacheza mchezo wa ufunguzi dhidi ya Marekani, huku mchezo wa pili ukiwa kati ya wenyeji India dhidi ya Malysia.

Serengeti Boys watashuka dimbani tena Mei 17, kucheza na wenyeji India mchezo wa kwanza, Mei 19 Serengeti Boys watacheza dhidi ya Korea Kusini na mchezo wa mwisho watamaliza dhidi ya Malysia Mei 21.

Fainali ya michuano hiyo itachezwa Mei 25 ambapo kabla ya mchezo wa fainali, utchezwa mchezo wa mshindi wa tatu katika uwanja huo huo Tilak Maidan, Vasco, Goa.

Kikosi cha Serengeti Boys kianatarajiwa kuingia kambini mwishoni mwa mwezi Aprili, 2016 kujiandaa na michuano hiyo ya vijana na kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 mwakani nchini Madagascar.

Jumuiya ya Wakurugenzi wa Serikali za Mitaa Kutoka UGANDA Watembelea Kampuni ya Maxcom Africa - Maxmalipo

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Maxmalipo  Juma Rajabu akifafanua jambo kwa wakurungezi wa serikali za mitaa kutoka Uganda , Kulia ni Mkuu wa Uendeshaji Kanda Group COO – Maxcom Africa Jamson Kassati , Kushoto Mwanzo Mr. Moses Kimaro Kutoka ALAT (jumuiya ya serikali za MItaa Tanzania)  na pembeni yake katikati ni Mwenyekiti wa wakurugenzi wa Serikali za Mitaa Kutoka Uganda Dunstan Balaba ambapo Jumuiya hiyo ya wakurugenzi wa serikali za Mitaa wapatao 60 Kutoka Uganda leo wametembelea Ofisi za Maxmalipo Kujifunza ni jinsi Gani kampuni hii imeweza kugundua teknolojia inayosaidia kudhibiti makusanyo kwenye vyanzo mbalimbali vya mapato katika Halmashauri za miji na majiji Nchini Tanzania.

Mkuu wa Kitengo cha Biashara Kutoka Maxmalipo Bw. Deogratius Lazari Akifafanua Jambo kwa Wakurugenzi hawa kutoka Uganda, Akielezea Jinsi mfumo wa Ukusanyaji Kodi na tozo mbalimbali ulivyorahisisha upatikanaji wa mapato katika halmashauri mbalimbali na Taasisi za Serikali kwa Ujumla na kuzuia mianya ya upoteaji wa mapato katika vyanzo mbalimbali vya halmashauri.
Mwenyekiti  na Msemaji wa Umoja wa wakurugenzi kutoka Uganda  Bwana Dunstan Balaba Akieleza Jambo kwa Hadhara na Kukiri kushangazwa na watanzania Kuweza Kugundua Teknolojia kama hii. Pia Kumwomba Mkurugenzi wa Maxmalipo Afungue Ofisi Uganda Mapema iwezekanavyo.

Jarida la Wiki la Wizara ya Nishati na Madini, Toleo la 116

LIBENEKE JIPYA LA BONGO BLOGS

MKUU MPYA WA WILAYA YA HAI MHE. GELASIUS GASPER BYAKANWA AJITAMBULISHA KWA MADIWANI

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro, Mhe. Gelasius Gaspar Byakanwa, akijitambulisha leo kwenye Baraza Maalumu la Madiwani wa Halmashauri ya Hai. 

WAZIRI UMMY MWALIMU AWASIMAMISHA WATENDAJI WA NHIF KWA UBADHIRIFU WA FEDHA

$
0
0
IMG_0724
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu (pichani) amewasimamisha kazi kupisha uchunguzi kwa watendaji Wakuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa ubadhirifu wa fedha za mfuko huo kwa Mkoa wa Mara.
New Doc 1_1 (1)New Doc 1_2

MKUU WA WILAYA YA TEMEKE, SOPHIA MJEMA AZINDUA MICHUANO YA UMISETA UWANJA WA UHURU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
 Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema ambaye alikuwa mgeni rasmi wa uzinduzi wa Michuano ya Shule za Sekondari Nchini (UMESETA), akipiga dana dana wakati wa uzinduzi huo uliofanyika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam leo.
 Wanafunzi wa shule za sekondari za mkoa wa Dar es Salaam wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema (kushoto), akikabidhi vifaa vya michezo kwa Shule ya Sekondari ya Azania vilivyotolewa na Kampuni ya Coca Cola. Kulia Ofisa kutoka kampuni ya Coca Cola wadhamini wakubwa wa michuano hiyo kwa mwaka 2016.
 DC Mjema akisalimiana na mwamuzi wa mchezo kati ya timu ya Sekondari ya Tirav ya Yombo na Makongo uliopigwa katika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Makongo ilishinda mabao 2-1.
 DC Mjema akiwasalimia wachezaji wa timu ya Tirav.

FULL MOON PARTY IN DAR

$
0
0
Kwa Mara Ya Kwanza Dar Es Salaam Official FullMoonPartyInDar 2016 Tunasogeza Bata Zote Ndani Ya ‪‎Escape1Beach 
Ni BeachParty Haijawai Kutokea. Jumamosi 23rd April. Kuanzia Saa Sita Kamili Mchana. Patakuwa Na Nyama Choma, Sea Food Tables, Burudani Ya Music Djku255  na Dj Cartel_yankee  Pamoja na wengine kibao. 
Bonfire. Hakuna Kukosa. 
KIINGILIO TSH 10,000 Njoo wewe Na Wenzako.


#OfficialFullMoonParty2016 Imeletwa kwenu na @legendaryMusic @choicefmtz @autoexpertjp na @escape1mikocheni 



REDIO DREAM FM 91.3 MBEYA KWA KUSHIRIKIANA NA MICHUZI BLOG NA PEPSI WANAKULETEA MISS MBEYA 2016

$
0
0
Pichani ni Mshiriki wa Miss Mbeya 2016 Anitha Patric, Redio Dream FM 91.3 Mbeya kwa kushilikiana na Michuzi Blog, Pepsi, Ufunuo Clinic, Access Computer Limited, Viva Night Club, Milo Group Limited, New karim Hardware, City Pub, Paradise Inn Hotel, Club K-Mo, Ace Classic Wear, Ally Rich Sanaa Art, New Mama Land Pub na Manyanya Inn Hotel and Tours wanakuletea Miss Mbeya 2016,  anaetarajiwa kupatikana Ijumaa ya Tarehe Sita ya Mwezi wa Tano (06-05-2016) Mwaka huu Paradis Inn Hotel, Pia kutakuwa na Burudani Mbalimbali ikiwemo Shoo kali kutoka kwa Mwanamuziki Izzo Bisnes na wasanii wanaofanya vizuri Nyanda za juu Kusini.
Eunice John moja kati ya Washiliki wa Miss Mbeya 2016
Julitha Mponela moja kati ya Washiliki wa Shindano la kumpata Miss Mbeya 2016.
Afrodisia Chapa miongoni mwa Washiliki wa Miss Mbeya 2016.
PICHA ZOTE NA MR,PENGO MMG MBEYA.

Zuriel & H.E. Muhammadu Buhari - One Year Anniversary as President

TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA YAPATA UONGOZI MPYA WA CHAMA CHA WAFANYAKAZI (TUGHE) Tawi la TUMESHERIA

$
0
0
  Mwenyekiti mpya wa Chama cha Wafanyakazi  (TUGHE) tawi la TUMESHERIA Bi. Anjela Shila akiwashukuru wajumbe wakati wa uchaguzi wa viongozi.
  Afisa Tawala wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Bi. Suzana Magoti akizungumza machache kwa niaba ya uongozi wa Tume wakati wa uchaguzi wa viongozi wa TUGHE tawi la TUMESHERIA.
Viongozi pamoja na Wajumbe wapya wa TUGHE tawi la TUMESHERIA wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufanya uchaguzi, wa kwanza kulia ni muwakilishi wa TUGHE mkoa Bw. Alquine Masubo.

Updates kesi ya Kamishna Mkuu wa Zamani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya na wenzake

$
0
0
HATMA ya kuliondoa ama la, shitaka la nane la kutakatisha fedha haramu dhidi ya Kamishna Mkuu wa Zamani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya na wenzake (pichani) wanaokabiliwa na mashitaka ya utakatishaji wa dola za Marekani milioni 6 mali ya Serikali kujulikana Aprili 27, mwaka huu. 
Leo mahakama hiyo kutoa uamuzi huo lakini kwa sababu Hakimu Mkazi Mwandamizi, Emmilius Mchauru anayesikiliza kesi hiyo alipangiwa majukumu mengine ya kitaifa yaliyosababisha kushindwa kukamilisha kuandika uamuzi huo. 
 “Nawaomba radhi nimeshindwa kumaliza kuandika uamuzi kwa sababu nilipangiwa majukumu mengine ... mpaka kufikia Jumanne ijayo ntakuwa nimemaliza ntausoma uamuzi huo Jumatano ijayo” alisema Hakimu Mchauru. 
 Aprili 8, mwaka huu, Mawakili wa upande wa utetezi ukiongozwa na Dk. Ringo Tenga akisaidaiana na Alex Mgongolwa, Majura Magafu ulitoa hoja za kupinga uhalali wa kisheria wa shitaka la nane kwamba kifungu kilichotumika kinamapungu uliomba shtaka hilo lifutwe. 
 Akitoa hoja kuhusu mapungufu ya kisheria katika shitaka hilo, Wakili Mgongolwa alidai kuwa kwa mujibu wa kifungu cha 12 A cha Sheria ya Makosa ya Jinai (CPA), kinachoelezea shitaka hilo katika hati ya mshitaka yanayowakabili washtakiwa hakielezei kuhusu utakatishaji wa fedha haramu. 
 “Tunaomba tafsiri ya mahakama kuhusu kifungu cha 12 A kwa kuwa kinaeleza tofauti na hakihusiani na kuhamisha fedha lakini kifungu hicho kupia B kinaeleza kuhusu utakatishaji... ili kosa la utakatishaji fedha haramu likamilike lazima kuwe na A na B, sheria lazima ipewe tafsiri inayotakiwa” alidai Wakili Mgongolwa. 
 Alidai kuwa pamoja na mambo mengine, mahakama itumie mamlaka yake kutoa tafsiri inayotakiwa na kwamba ni rai yao upande wa utetezi shitaka la nane liondolewe katika hati ya mashitaka yanayowakabili washtakiwa kwa kuwa haliko kihalali katika hati hiyo. 
 Upande wa Jamhuri uliongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Osward Tibabyekomya akisaidiana na Mawakili wa Serikali Waandamizi, Shadrack Kimaro, Christopher Msigwa na Mwendesha Mashitaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Stanlay Luoga. 
 Tibabyekomya alidai kuwa makosa yaliyopo kwenye kifungu cha 12 A cha CPA yanajitegemea na kwamba utakatishaji wa fedha haramu kifungu hicho kinaainisha makosa hayo.
 “Kila hatua ya utakatishaji fedha haramu imeainishwa kwenye kifungu hicho inayokana na kosa lenyewe kwa kuwa sheria imeharamisha lengo ni kuzuia hata jaribio la utakatishaji wa fedha haramu... hoja za utetezi hazijitoshelezi kuhusu kuliondoa shitaka hilo, sisi upande wa Jamhuri hatuna pingamizi na ombi la kupata tafsiri sahihi ya kifungu hicho” alidai Tibabyekomya. 
 Mbali na Kitilya washtakiwa wengine ni, wafanyakazi wa Benki ya Stanbic Tanzania aliyekuwa Mrembo wa Tanzania mwaka 1996, Shose Sinare na mwanasheria wa benki hiyo Sioi Solomon. 
Kufikishwa mahakamani kwa washtakiwa hao ni baada ya tuhuma za ufisadi zilizowahi kuibuka na serikali kupoteza zaidi ya Sh.trilioni 1.3. 
 Aprili Mosi, mwaka huu, Tibabyekomya aliwasomea washtakiwa hao mashitaka yao, alidai katika shitaka la kwanza kati ya Agosti 2012 na Machi 2013 ndani ya jiji la Dar es Salaam washtakiwa wanadaiwa kula njama ya kutenda makosa hayo. 
 Shitaka la pili hadi la tano yanamkabili Sinare, ilidaiwa kuwa Agosti 2, 2012 akiwa katika benki ya Stanbic Makao Makuu, kwa nia ya kudanganya alighushi hati ya mapendekezo ya uwezeshwaji wa kifedha ya tarehe hiyo kwa lengo la kuonesha kwamba,benki hiyo kwa kushirikiana na na benki ya Standard Bank ya Uingereza watatoa mkopo wa dola milioni 550 kwa serikali ya Tanzania kwa ada ya asilimia 2.4 ya mkopo huo huku akijua si kweli. 
Sinare anadaiwa kwamba Agosti 13, 2012 katika ofisi za Wizara ya Fedha aliwasilisha hati hiyo. 
Ilidaiwa kuwa Septemba 20,2012 akiwa katika Makao Makuu ya Benki ya Stanbic Tanzania iliyopo Wilaya ya Kinondoini, jijini Dar es Salaam Sinare, alighushi barua ya pendekezo la mkopo huo ya terehe hiyo akionesha kwamba Benki ya Standard Plc kwa kushirikiana na benki ya Stanbic wangetoa mkopo huo kwa serikali kama benki hizo zitapopewa kazi ya kutafuta mkopo huo kwa riba ya asilimia 2.4 huku akijua si kweli. Mshitakiwa huyo pia anadaiwa kuwasilisha nyaraka hiyo ya kughushi katika Wizara ya Fedha. 
Shitaka la sita ilidaiwa kuwa Novemba 5, mwaka 2012 washtakiwa wote watatu wakiwa katika benki ya Stanbic Tanzania Makao Makuu kwa nia ya kudanganya walighushi mkataba wa ushirikiano wa tarehe hiyo kwamba Benki ya Stanbic Tanzania Limited imeanzisha ushirikiano na kampuni ya Enterprise Growth Market Advisors (Egma) Limited kwa ajili ya kutafuta mkopo huo kwa serikali. 
Ilidaiwa kwamba Egma pia ingewezesha na kuandaa mikutano na nyaraka mbalimbali ambazo zingetakiwa na mamlaka za Tanzania huku wakijua siyo kweli. 
 Upande huo wa Jamhuri ulidaiwa katika shitaka la saba, Machi 2013, ndani ya jiji la DaresSalaam,washtakiwa wote kwa udanganyifu,,walijipatia Dola za Kimarekani Milioni 6 Kwa serikali baada ya kudanganya kwamba fedha hizo ni ada ya malipo kwa kampuni ya Egma na benki ya Stanbic kwa kuwezesha serikali kupata mkopo wa Dola za Kimarekani Milioni 600. 
 Tibabyekomya alidai katika shitaka la nane, washtakiwa wanadaiwa kutakatisha fedha hizo kwa kuzihamishia katika akaunti mbalimbali ikiwamo 0240026633702, 0240026633701, na 9120001251935 zinazomilikiwa na Egma katika benki ya Stanbic na akaunti namba 3300605539 na 3300603692 ambazo pia zinamikikiwa na Kampuni ya Egma katika benki ya KBC wakati wakijua fedha hizo zimetokana na kosa la jinai la kughushi. 
 Washtakiwa walikana mashitaka yao kwa nyakati tofauti, upande wa Jamhuri upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISION

$
0
0

Watu 3 wafariki dunia na wengine kujeruhiwa baada ya gari aina ya Prado lililokuwa likitokea Tabora kwenda Mwanza kupinduka. https://youtu.be/Yr8XDr_KIZA

Mahakama ya hakimu mkazi ya Kisutu ya jijini Dar es salaam yasongeza mbele uamuzi juu ya ombi la kuondoa shitaka la utakatishaji fedha linalowakabili aliyekuwa mkurugenzi wa zamani wa TRA Harry Kitilya na wenzake wawili.https://youtu.be/5SZmvACOK0g   

Wamiliki na madereva wa daladala mkoani Morogoro wamendelea kugoma baada kutoridhishwa na utendaji kazi wa afisa mfawidhi wa SUMATRA kwa madai ya kuwatoza faini mara mbili. https://youtu.be/Cgoo_31LNn8

Wakazi zaidi ya elfu arobaini kutoka wilayani karatu wanapata maji safi na salama kutoka msitu wa Ngorongoro jambo ambalo limetoa fursa ya maendeleo kwa wakazi hao. https://youtu.be/SutZM-sSnmI
   
Mamlaka ya chakula na dawa TFDA imekamata shehena kubwa ya vipodozi vyenye viambata vya sumu katika maduka ya vipodozi eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam.https://youtu.be/mhuhoN7QOdk 
  
Watu kumi na saba kati ya mia sita waliochukuliwa vipimo vya magonjwa yasiopewa kipaumbele wamebainika kuwa na ugonjwa wa vikope.https://youtu.be/Se5CGAq3MbA

HOTUBA YA WAZIRI MKUU, MHE. KASSIM M. MAJALIWA (MB), KUHUSU MAPITIO NA MWELEKEO WA KAZI ZA SERIKALI NA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA ZA OFISI YA WAZIRI MKUU KWA MWAKA 2016/2017

$
0
0
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasilisha  bungeni   Mapitio na Mwelekeo wa Kazi za Serikali na Makadirio ya Mapato na Matumizi  ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka 2016/2017. 


UTANGULIZI


1.            Mheshimiwa Spika, naomba kutoa Hoja kwamba kutokana na taarifa zilizowasilishwa leo katika Bunge lako Tukufu na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI zilizochambua Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu,Bunge lako sasa lipokee na kujadili Taarifa ya Mapitio ya Utekelezaji wa Kazi za Serikali kwa Mwaka 2015/2016 na Mwelekeo wa Kazi za Serikali kwa Mwaka 2016/2017. Vilevile, naliomba Bunge lako Tukufu likubali kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi zilizo chini yake kwa mwaka 2016/2017.

2.            Mheshimiwa Spika,huu ni Mkutano wa Bunge wa kujadili Bajeti ya Serikali baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2015. Hivyo naomba nitumie fursa hii kuwashukuru Watanzania kwa kuendelea kuwa na imani na Chama Cha Mapinduzi na hivyo kukiwezesha kushinda na kukipa tena ridhaa ya kuunda Serikali na kuiongoza Nchi yetu. Aidha, kwa njia ya pekee napenda kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuongoza Serikali ya Awamu ya Tano. Pia, nampongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

RAIS DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI AKUTANA NA MABALOZI IKULU

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana Balozi wa Vatican hapa nchini anayemaliza muda wake Francisco Montecillo Ikulu jijini Dar es Salaam. Balozi huyo wa Vatican alifika Ikulu kwa ajili ya kuagana na Rais Dkt. Magufuli mara baada ya kumaliza muda wake ya Ubalozi nchini.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na mgeni wake Balozi wa Vatican hapa nchini anayemaliza muda wake nchini Francisco Montecillo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na mgeni wake Balozi wa Vatican hapa nchini anayemaliza muda wake nchini Francisco Montecillo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Balozi wa Vatican hapa nchini anayemaliza muda wake Francisco Montecillo  Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa Algeria hapa nchini Belabed Saada akikabidhi ujumbe uliotoka kwa Rais wa Algeria kuja kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Balozi wa Canada hapa nchini Alexandre Leveque Ikulu jijini Dar es Salaam. Balozi huyo wa Canada alifika Ikulu na ujumbe wake  kwa ajili ya kufanya mazungumzo na Rais Dkt. Magufuli
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Balozi wa Canada hapa nchini Alexandre Leveque wapili kutoka kulia pamoja na waakilishi wengine wa Serikali pamoja na Ubalozi wa Canada.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiagana na Balozi wa Canada hapa nchini Alexandre Leveque mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

Article 0

Halmashauri ya Wilaya ya Meatu yapokea miche ya miti ya matunda kutoka ofisi ya makamu wa Rais

$
0
0
 Paschal Lugali, mfanyakazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Meatu akipanga miche ya miti ya matunda mapema leo, ikiwa ni ahadi ya serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira
 Afisa Misitu Mwandamizi kutoka Idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Raisi bw. George Kafumu akiangalia miche ya miti ya matunda baada ya kuiwasilisha katika Halmashauri ya Wilaya ya Meatu mapema Leo.
 Miche ya miti ya matunda, ikiwa imepangwa baada ya kupokelewa mapema Leo katika halmashauribya wilaya ya Meatu,baada ya serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira kutekeleza ahadi yake ya kugawa miti elfu ishirini na saba (27,000) Katika mkoa wa Simiyu. 


Baadhi ya wakazi wa jimbo la kisesa mkoani Simiyu katika picha pamoja na miche ya miti ya matunda waliyo ipokea kutoka serikalini kupitia Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira 
Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu wakishusha miti ya Matunda kutoka kwenye gari iliyoibeba mapema leo, miti hiyo waliahidiwa na Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira.(Picha na kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Makamu wa Raisi)
Viewing all 110185 articles
Browse latest View live




Latest Images