Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110167 articles
Browse latest View live

In loving memory

$
0
0
Dr. Henry C. M. M. Nyamubi 13.02.1958 ~ 28. 03. 2015

A great husband, father, son, brother, uncle, grandfather and friend.

You are physically gone but spiritually ever present. We will never forget your kindness, wisdom and your selflessness in assisting others despite personal difficulties you were going through.

Words, however kind, cannot mend the loss we feel. However we rejoice knowing that you are now with our Lord Jesus and that we will meet again when He calls us.

Thanks Givin mass will be at st Batholomew Anglican Church Ubungo 16:00 Pm.

Mwakilishi Maalum wa AU kuhusu Libya Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete Afanya Mazungumzo na Waziri wa Nchi Anayeshughulikia Mambo ya Nje na Mgogoro wa Libya Dkt. Anwar Mohamed Gargash Al-Awadhi wa UAE jijini Dubai Leo

$
0
0
 Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Afrika kuhusu Libya Rais Mstafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipokelewa na Mwenyeji wake Waziri wa Nchi anayeshughulikia Mambo ya Nje Mhe Dkt. Anwar Mohamed Gargash Al- Awadh ofisini kwake Dubai

Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Afrika kuhusu Libya Rais Mstafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete katika mazungumzo na Waziri wa Nchi wa Mambo ya Nje wa UAE Dr. Anwar Mohamed Gargash Al- Awadhi ofisini kwake Dubai.

RAIS DKT MAGUFULI AITAKIA HERI TAIFA STARS DHIDI YA TIMU YA CHAD HAPO KESHO UWANJA WA TAIFA

RAIS MAGUFULI AHUDHURIA IBADA YA PASAKA KANISA LA KKKT LA AZANIA FRONT JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akilakiwa na Askofu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dkt. Alex Malasusa alipowasili kwa Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Mkewe Mama Magufuli wakishiriki na waumini wengine Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimia waumini huku akisikilizwa na Askofu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dkt. Alex Malasusa na Mchungaji Chalres Mzinga baada ya Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  na Mkewe Mama Janeth Magufuli pamoja na Mama Rebecca Malasusa na Askofu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dkt. Alex Malasusa baada ya Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  akiwapungia waumini baada ya  Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  akisalimiana na mtoto Javiera Lyimo (9) anayesoma darasa la tano shule ya Genesis jijini  baada ya  Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016. 

mdororo wa kiuchumi Chad wafuta mchezo wa timu ya nchi hiyo na Taifa Stars kesho

$
0
0
CHAMA cha soka nchini Chad FTFA kimetuma barua kwa CAF na TFF kuelezea kushindwa kwao kusafiri kuja nchini Tanzania kwa ajili ya mchezo wa marudiano dhidi ya timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' uliopangwa kuchezwa kesho kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Sababu ya kushindwa kwao kusafiri kama ilivyoelezwa kwenye barua hiyo ni nchi hiyo kuathiriwa na mdororo wa kiuchumi. Ifuatayo ni tafsiri fupi ya barua hiyo iliyoandikwa kwa lugha ya kifaransa.

"TAARIFA YA CHAD KWA CAF NA TFF
Timu yetu haiwezi kusafiri hadi Dar kwa mechi ya tarehe 28
Nchi yetu imeathirika na mgogoro wa uchumi duniani...hivyo ushiriki wetu kwenye mashindano mbalimbali umepata pigo kubwa kutokana na ukosefu wa fedha.
Tunaomba radhi kwa usumbufu huu ambao ni nje ya uwezo wetu na nia yetu"

kipa wa zamani wa simba toka uganda Abel Dhaira afariki dunia

$
0
0

Klabu ya Simba imepokea kwa mshtuko taarifa ya msiba wa mchezaji wake wa zamani mganda Abel Dhaira.
Taarifa za msiba huo zimethibitishwa na mitandao mikubwa ya Uganda ikiwemo ya gazeti mashuhuri nchini humo la New Vision.
Mchezaji huyo aliyekuwa akichezea nafasi ya golikipa na ambae alipata pia kuichezea timu ya taifa ya Uganda.alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kansa ya utumbo.
Kwetu sisi ni pigo kubwa sana na msiba mzito sana.umetufanya tupate fadhaa kubwa.lakini hatuna la kufanya.zaid ya kumtakia mapumziko mema ya milele.
Dhaira anakumbukwa sana na wana Simba hasa kwa uwezo wake wa kudaka krosi na nidhamu yake iliyokuwa mfano kwa wachezaji wote waliokuwepo kipindi kile..
Tunawaomba familia ya marehemu iwe na subira kwenye kipindi hiki kigumu sana kwao

Imetolewa na
Haji S Manara
Mkuu wa habari Simba sports club

Machi 27, 2016

TFF YATHIBITISHA KUJITOA KWA CHAD KATIKA MICHUANO YA AFCON 2017

$
0
0
Shirikisho la Soka nchini TFF  limethibitisha taarifa yetu ya awali  kwamba timu ya Taifa ya Chad  ‘Les Sao’ (pichani) imejiondoa katika michuano ya kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa Afrika (AFCON) itakayofanyika mwaka 2017 nchini Gabon.

Tovuti ya TFF inasema kwamba taarifa ya kujitoa kwa Chad imetolewa na Shirikisho la Mpira wa miguu barani Afrika (CAF) leo baada ya Les Sao kuandika barua ya kujitoka katika mashindano hayo ikiwa katika kundi G pamoja na timu za Tanzania, Nigeria na Misri.

Chad ilitarajiwa kucheza kesho Jumatatu dhidi ya Tanzania katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, ikiwa ni mchezo wa marudiano wa kundi G baada ya kucheza mchezo wa awali jijini N’Djamena katika ya wiki.
Katika mchezo wa awali uliochezwa uwanja wa Idriss Mahamat Ouya, Taifa Stars iliibuka na ushindi wa bao 1- 0 , bao lililofungwa na nahodha Mbwana Samatta dakika ya 30 ya mchezo.

Kufuatia kujitoa kwa Chad, matokeo ya michezo yote iliyoihusisha timu hiyo yanafutwa, na msimamo wa kundi G kwa sasa unaongozwa na Misri yenye pointi 4, Nigeria pointi 2 na Tanzania pointi 1.

TAMASHA LA PASAKA LAPAGAWISHA MASHABIKI WA MUZIKI WA INJILI CCM KIRUMBA JIJINI MWANZA

$
0
0
11
Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akiongoza na viongozi mbalimbali pamoja na baadhi ya maaskofu kucheza wakati mwimbaji Upendo Nkone alipokuwa akiimba jukwaani.
12
Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akipiga picha ya pamoja na waimbaji wa muziki wa injili mara baada ya tamasha hilo kumalizika kutoka kulia ni Bonny Mwaiteje. Jesca BM na Upendo Nkone.
13
Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akicheza wakati mwimbaji Bonny Mwaiteje alipokuwa akitumbuiza.
30
Mwimbaji Christopher Mwahangila akiwapa upako mashabiki kupitia injili ya uimbaji.
33
Mwimbaji Ephraimu Sekereti kutoka nchini Zambia naye akaimba nyimbo za kusifu na kuabudu.
34
Solomon Mukubwa akiafunga kazi na nyi,bo zake kali zilizowafanya mashabiki kuwa wima wakati wote kama wanavyoonekana.

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI

$
0
0

SIMU.TV: Mkuu wa mkoa wa Geita Meja Generali mstaafu Ezekiel Kyunga awataka mabalozi wa nyumba 10 kuimarisha ulinzi katika maeneo yao kwa kuwa wako karibu sana na makazi ya wananchi. https://youtu.be/CTup2l1P9v4

 SIMU.TV: Wadau wa elimu wilaya ya Mpanda mkoani Katavi wachangia na kuahidi zaidi ya shilingi milioni 5 za madawati pamoja na mifuko 10 ya simenti ili kunusuru wananfunzi 800 wanaokaa chini. https://youtu.be/5_aLHkI8Hsg

SIMU.TV: Waziri Luhaga Mpina aipa NEMC siku 7 kuibana Dawasco kukomesha utiririshaji wa maji taka kwenye mitaro ya maji ya mvua.https://youtu.be/k9nTECX2628  
   
SIMU.TV: Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam juu ya ujenzi wa barabara ya Makumbusho hadi Mwananyamala laanza kuzaa matunda baada ya mkandarasi kuendelea na ukarabati. https://youtu.be/nl387NcTwF0  
  
SIMU.TV: Wakazi wa kijiji cha Amani wilyani Nanyumbu mkoani Mtwara wagomea kujiunga na mfuko wa afya ya jamii CHF baada ya kudai awali kupewa kadi zilizoisha mda wake. https://youtu.be/W9mPI3UClZY  
   
SIMU.TV: Wadau mbalimbali wa elimu jijini Dar es salaam waendelea kutoa misaada mbalimbali kusaidia ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi ya Maji Matitu iliyoko Mbagala kutokana na kufurika kwa wanafunzi. https://youtu.be/BF8vzHAqkb8

NGOMA AZIPENDAZO ANKAL: Sam Wa Ukweli - Hata Kwetu wapo

WANAWAKE WA DODOMA WAJITOKEZA KWA WINGI KUCHANGAMKIA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI KUTOKA MANJANO FOUNDATION

$
0
0
Wanawake wa Mkoa wa Dodoma wanaonufaika na Mradi wa Manjano Dream Makers wakikisikiliza kwa Makini Mada Kuhusu Elimu ya Biashara na namna ya kuendesha Ujasiriamali Kwenye Mafunzo Yanayoendelea Mkoani Dodoma .

Mafunzo ya kuwawezesha wanawake kiuchumi kupitia vipodozi vya LuvTouch Manjano yameanza mkoani Dododma. Jumla ya Washiriki 30 wamechaguliwa katika fursa hiyo na wanajulikana kama Manjano Dream Makers. Mafunzo hayo yamegawanyika katika awamu mbili. Awamu ya kwanza wanawake hao kutoka Manispaa ya Dodoma watapatiwa elimu kuhusu sifa za ujasiriamali, changamoto zake na namna ya kukuza na kuendesha biashara ikiwa pamoja na nidhamu ya kutunza pesa na mahesabu yaani 'Financial literacy'. Pia washiriki watanufaika namna ya kutoa huduma nzuri na bora kwa wateja na kujua mbinu zipi watumie kujiwekea
akiba.
 
Afisa Mtendaji Mkuu wa Shera Illusions Africa na Mkurugenzi wa Manjano Foundation Mama Shekha Nasser Akieleza Machache leo wakati wa Mafunzo ya Ujasirimali kwa Wanawake wa Mkoa wa Dodoma.

Awamu ya pili washiriki watapatiwa elimu kuhusu matumizi sahihi ya Vipodozi hasa "Make-Up Artistry". Awamu hii hapa washiriki watajua matumizi yenye ueledi (professional) wa kutunza ngozi, kutumia vipodozi na namna ya kuwapamba maharusi na wakazi wa Dodoma na maeneo jirani kwa kutumia vipodozi sahihi na salama. Mara baada ya mafunzo haya washiriki watapata fursa ya kukopeshwa mitaji kwa ajili ya biashara kwa lengo la kuwakwamua washiriki wote kuondokana na ukosefu wa ajira na kujikita katika kujiajiri katika tasnia ya vipodozi.
Mafunzo haya yanaratibiwa na Taasisi ya Manjano Foundation kwa kushirikiana na Kampuni ya Shear illusions kupitia vipodozi Pendwa vya LuvTouch Manjano. Mafuzo kama haya tayari yamesha wanufaisha wanawake Zaidi ya 150 Kutoka Dar es Salaam, Mwanza, Arusha na Visiwani Zanzibar. Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo kutoka Mkoa wa Dodoma wameishukuru Taasisi ya Manjano Foundation kwa kuwapa nafasi hiyo na kuwaletea mradi huo.
Picha ya Pamoja ya Washiriki wa Mafunzo ya Ujasiriamali kutoka Mkoa Dododma.

Wakieleza zaidi wamesema walikuwa na hamasa sana tangu walipopata taarifa kwa wanawake wenzao wa mikoa ya Dar es salaam, Mwanza, Arusha na Zanzibar kunufaika na mradi huu na walikuwa wanasubiri kwa hamu kubwa sana mafunzo hayo. Wakiendelea zaidi wamesema wapo tayari kupigana na kujikita vizuri kupitia mradi huu kwa lengo la kujikwamua na kujiongezea kipato kupitia kazi ya mikono yao

WAFANYABIASHARA WA MAFUTA WATAKIWA KUTUMIA FURSA ZA UWEKEZAJI WA BOMBA LA MAFUTA LINALOGHRAIMU DOLA BILIONI NNE.

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Justin Ntalikwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na Bomba la Gesi litakalokuwa likisafirisha kutoka Tanga kwenda uganda.
Mwenyekit wa Chama cha wafanyabiashara wa mafuta nchini(NICOL), Gidion Kaunda akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mara baada ya Katibu mkuu kuzungumzia bomba la mafuta la Tanga kwenda Uganda.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Justin Ntalikwa(aliye mbele) jijini Dar es Salaam leo.
Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii. 
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa amesema kuwa wafanyabiahara wa mafuta wanafursa mbalimbali katika ujengaji wa bomba la mafuta kutoka Tanga hadi Uganda.

Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Profesa Ntalikwa amesema kuwa bomba la mafuta likianza mchakato wafanyabiashara wanaweza kuomba zabuni mbalimbali zitakazojitokeza.

Mradi wa ujenzi wa bomba hilo unagharimu dola za Kimarekani Bilioni Nne ambapo utaongeza ajira nyingi pamoja na kodi.

Amesema kuwa bomba hilo litajengwa nchini kwa asilimia 90 kutokana na amani iliyopo ukilinganisha na nyingine zilizo katika mradi huo.

Profesa Ntalikwa amesema kuwa kigezo cha kwanza cha kujenga bomba nchini ni kutokana na Bandari ya Tanga kuwa na kina kirefu cha kufanya kila meli kuweza kuingia hapo na tofauti bandari ya Mombasa nchini Kenya.

Amesema kutokana na vigezo vinaashiria kujengwa nchini licha ya kuwepo kwa majadiliano yanayoendelea juu ya bomba hilo litajengwa wapi.

Amesema kuwa nchi ya Kenya ndio inayofanya kuwa katika mchakato wa mwisho hivyo wenyewe ni watu wa kuangalia tu jinsi ya mradi utapofanyika.

Aidha Profesa Ntalikwa amesema kuwashirikisha wafanyabiashara wa mafuta ni kutaka kukujua fursa zilizo katika ujenzi wa bomba la mafuta wa kuweza kuomba zabuni.

RAIS MAGUFULI AMUAPISHA MKUU WA MKOA MPYA WA SONGWE MHE. CHIKU GALLAWA IKULU DAR ES SALAAM

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimuapisha Luteni Mstaafu Chiku Gallawa kuwa mkuu wa mkoa mpya wa Songwe Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 28, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimshuhudia Luteni Mstaafu Chiku Gallawa akiweka sahihi katika hati ya kiapo mara baada ya kuapa kuwa mkuu wa mkoa mpya wa Songwe Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 28, 2016.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisaini hati ya kiapo cha Luteni Mstaafu Chiku Gallawa  mara baada ya kumuapisha  kuwa mkuu wa mkoa mpya wa Songwe Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 28, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimkabidhi nyenzo za kazi  Luteni Mstaafu Chiku Gallawa  mara baada ya kumuapisha  kuwa mkuu wa mkoa mpya wa Songwe Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 28, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais Mhe Samia suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe Kassim  na  Luteni Mstaafu Chiku Gallawa  baada ya kumuapisha  kuwa mkuu wa mkoa mpya wa Songwe Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 28, 2016.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipeana mikono na Luteni Mstaafu Chiku Gallawa  mara baada ya kumuapisha  kuwa mkuu wa mkoa mpya wa Songwe Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 28, 2016. Kulia ni mume wa mkuu huyo wa Mkoa Bw. Juma` Boma na kushoto ni bintiye.

PICHA NA IKULU

RAIS MAGUFULI APOKEA TAARIFA YA UKAGUZI WA HESABU ZA SERIKALI KUTOKA KWA MKAGUZI NA MDHIBITI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI (CAG) IKULU DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipokea Taarifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali Professa Mussa Assad Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 28, 2016.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa wakipitia Taarifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali iliyokabidhiwa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali Professa Mussa Assad Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 28, 2016.PICHA NA IKULU

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa wakiwa na watendaji wakuu  wa Ofisi ya Mdhibiti na Mkafuzi Mkuu wa hesabu za serikali  baada ya kukabidhiwa Taarifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali Professa Mussa Assad Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 28, 2016

Rais Magufuli amwapisha RC Songwe na apokea Taarifa ya CAG ya 2014/15

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemwapisha Mkuu wa mkoa mpya wa Songwe Luteni Mstaafu Chiku Gallawa, ambaye hakuapishwa pamoja na wakuu wa mikoa wenzake Machi 15, 2016.


Uapisho huo umefanyika leo tarehe 28 Machi, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam, na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa.


Luteni Mstaafu Chiku Gallawa anakuwa Mkuu wa Mkoa wa kwanza kwa Mkoa mpya wa Songwe, ulioanzishwa kwa kuugawa mkoa wa Mbeya, Kusini mwa Tanzania.


Wakati huo huo, Rais Dkt. John Pombe Magufuli amepokea taarifa ya ukaguzi wa hesabu za serikali ya mwaka 2014/2015 kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Prof. Mussa Assad, Ikulu Jijini Dar es salaam.


Rais Magufuli amepokea taarifa hiyo yenye ripoti tano, ikiwa ni utaratibu wa kikatiba unaomtaka Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali, kukabidhi kwa Rais taarifa ya ukaguzi kabla ya mwisho wa mwezi Machi.


Baada ya kupokea taarifa hiyo, Rais Magufuli ataikabidhi mbele ya bunge katika siku saba za mwanzo za kikao kijacho cha Bunge kitakachofanyika Mjini Dodoma.Rais Magufuli amempongeza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za serikali na timu yake kwa kuandaa taarifa hiyo, na ametoa wito kwa chombo hicho kuendelea kufanya kazi kwa uhuru na ufanisi, huku akiahidi kuwa serikali itatoa ushirikiano wa kutosha kufanikisha kazi zake.

Gerson Msigwa

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU

Dar es salaam


28 Machi, 2016

NAIBU WAZIRI WA MICHEZO ANASTAZIA WAMBURA ATEMBELEA KITUO CHA UTAMADUNI KILICHOPO CHUO KIKUU CHA TUMAINI MAKUMIRA

$
0
0
Wasanii wa Kituo cha Utamaduni kilichopo chuo Kikuu cha Tumaini Makumira wilaya ya Arumeru mkoani Arusha wakicheza ngoma ya Sindimba wakati Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura (hayupo pichani) alipotembelea kituo hicho hivi karibuni kwa ajili ya kuona shughuli za kitamaduni zinazofanyika kituoni hapo.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura (wa pili kulia) akiwaangalia wasanii wa Kituo cha Utamaduni kilichopo chuo Kikuu cha Tumaini Makumira wilaya ya Arumeru mkoani Arusha (hawapo pichani) wakicheza ngoma ya kabila la wa Meru wakati alipotembelea kituo hicho hivi karibuni kwa ajili ya kuona shughuli za kitamaduni zinazofanyika kituoni hapo. Kulia ni Randall Stubbs ambaye ni Meneja Mradi wa kituo hicho kinachojengwa chuoni hapo, watatu kulia ni Afisa Michezo wa Mkoa Mwamvita Okeng’o na wa nne kulia ni Afisa utamaduni wilaya ya Arumeru Senyael Pallangyo.
 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akiangalia mchoro wa ramani ya Kituo cha Utamaduni kinachojengwa katika chuo Kikuu cha Tumaini Makumira kilichopo wilaya ya Arumeru mkoani Arusha wakati alipotembelea kituo hicho hivi karibuni kwa ajili ya kuona shughuli za kitamaduni zinazofanyika kituoni hapo. Kulia ni Afisa utamaduni wilaya ya Arumeru Senyael Pallangyo akifuatiwa na Randall Stubbs ambaye ni Meneja Mradi wa kituo hicho.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura (watatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wasanii wa Kituo cha Utamaduni kilichopo chuo Kikuu cha Tumaini Makumira kilichopo wilaya ya Arumeru mkoani Arusha wakati alipotembelea kituo hicho hivi karibuni kwa ajili ya kuona shughuli za kitamaduni zinazofanyika kituoni hapo.Picha na wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

WANANCHI WAWAKAMATA WEZI WA NYAYA ZA SIMU ZA KAMPUNI YA TTCL KIGOMA.

$
0
0
 Mkurugenzi wa kampuni ya simu ya TTCL nchini Dk Kamugisha Kazaura akimuelekeza jambo Waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliani Professa Makame Mbawala kuhusu mkongo wa mawasiliano uliopo mpakani mwa Tanzania na Burundi. 
Vijana waliokutwa na nyaya za wizi za kampuni ya TTCL waliokamatwa usiku wa kuamkia leo na wanachi (kushoto) Haroon Khamani na Amos khalidi.

Waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano akitoa maelekezo kwa viongozi wa Wilaya ya Kasulu juu ya wezi wa nyaya za simu za kampuni ya TTCL kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria haraka kwa kuhujumu mawasiliano.
  Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya simu za TTCL nchini Dk Kamugisha Rwezaura akiongea na vyombo vya habari juu wezi waliokata nyaya za simu TTCL mtaa wa Sovya Wilayani Kasulu

Editha Karlo, Kasulu

WANANCHI  wa Mtaa  wa soko la sovya Wilayani Kasulu usiku wa kuamkia leo wamewakamata wezi waliokuwa wamekata nyaya za mawasiliano za kampuni ya TTCL.

Akiongea juu ya tukio hilo Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya simu TTCL nchi Dk Kamugisha Kazaura alisema kuwa tukio hilo limetokea katika eneo la soko la sovya majura ya saa kumi na moja alfajiri. Alisema kuwa wananchi  wanaoishi karibu na eneo lililokatwa nyaya hizo ndiyo waliowakamata vijana hao baada ya kufanya uhslifu huo. Mkurugenzi huyo alisema kuwa hasara waliyoipatia kampuni kwa kukata nyaya hizo inakadiliwa ni zaidi ya milioni 20.

"Hasara waliyoingizia serekali ni kubwa sana hizo nyaya walizokata zinagharimu milioni 20,lakini kuitengeneza upya line hiyo inaweza kugharimu zaidi ya hiyo fedha''alisema Kazaura

Alisema kutokana na wezi huo umepelekea baadhi ya ofisi za serekali kukosa mawasiliano ikiwemo ofisi ya polisi Wilaya,Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Bank na Takukuru. Naye Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na mawasiliano profesa Makame Mbawala alivitaka vyombo vya dola kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wezi hao wanaohujumu mawasiliano.

"Hawa muwapeleke kwenye sheria hiki walichofanya ni kosa kwa sheria ya mwaka 2015 wanatakiwa kulipa faini isiyopungua milioni 50 au kifungo jela ili iwe fundisho kwa wengine"alisema profesa Mbawala

Dk. Pallangyo awakaribisha wazawa kwenye uzalishaji wa umeme

$
0
0
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia  masuala ya nishati Dk. Juliana Pallangyo (pichani) akifungua mkutano unaoshirikisha wakurugenzi wa mashirika ya umeme katika nchi zilizopo kusini mwa Afrika zinazoshirikiana katika biashara ya umeme.
 Sehemu ya watendaji na wakurugenzi wa mashirika ya umeme katika nchi zilizopo kusini mwa Afrika zinazoshirikiana katika biashara ya umeme, wakifuatilia hotuba iliyokuwa inatolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia  masuala ya nishati, Dk. Juliana Pallangyo (hayupo pichani).
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia  masuala ya nishati, Dk. Juliana Pallangyo (kulia) na  Kaimu  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la  Umeme Nchini (TANESCO) Mhandisi Decklan Mhaiki (kushoto) wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yanatolewa na mwenyekiti wa kamati ya nchi za kusini mwa Afrika zinazoshirikiana katika biashara ya  umeme, Josh Chifamba (hayupo pichani)
 Mwenyekiti wa kamati ya nchi za kusini mwa Afrika zinazoshirikiana katika biashara ya umeme, Josh Chifamba (kulia) akimkabidhi zawadi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia  masuala ya nishati, Dk. Juliana Pallangyo (kushoto) aliyekuwa mgeni  rasmi kwenye ufunguzi wa mkutano huo.


MAKAMU WA PILI WA RAIS BALOZI SEIF ALI IDD AKARIBISHWA OFISINI KWAKE

$
0
0
 
 Watendaji wa Taasisi zilizochini ya Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar wakimpokea na kumkaribisha kuanza kazi Ofisini kwake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi baada ya kuteuliwa tena na Rais wa Zanzibar kuendelea kushika wadhifa huo katika kipindi cha Pili cha Awamu ya Saba.
 Katibu wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Abdullah Ali Abdullah { Kitole } aliyeinama akinong’onezana kitu na Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd. Ahmad Kassim kwenye hafla ya kupokea Balozi Seif kuanza rasmi majukumu yake Vuga Mjini Zanzibar.
  Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd. Ahmad Kassim akimpongeza Balozi Seif kutokana na juhudi zake zilizopelekea watendaji wa ofisi yake kupata mafanikio makubwa ndani ya kipindi cha uongozi wake wa miaka mitano iliyopita.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiwashukuru watendaji wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi yake baada ya kufanyakazi pamoja atika kipindi cha miaka mitano iliyopita.

WATANZANIA KUNUFAIKA NA BIMA YA ELIMU KUTOKA SANLAM LIFE INSURANCE TANZANIA

$
0
0
Meneja Mkuu wa Bima ya Maisha, Wilson Mnzava (wapili kulia), wakati wa uzinduzi wa bima hiyo.Kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam Life Insurance, Julius Magabe na kulia ni Mchambuzi wa Mahesabu ya Bima wa kampuni hiyo, Kyenekiki Kyando. 
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam Life Insurance, Julius Magabe, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Bima ya Elimu ya 'Sanlam Education Care,Kulia ni Meneja Mkuu wa Bima ya Maisha, Wilson Mnzava.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam Life Insurance, Julius Magabe (wapili kushoto), akimkabidhi Hati ya Bima ya Elimu wa 'Sanlam Education Care', Meneja Mkuu wa Bima ya Maisha, Wilson Mnzava (wapili kulia), wakati wa uzinduzi wa bima hiyo, Dar es Salaam leo. Kulia ni Mchambuzi wa mahesabu ya Bima wa kampuni hiyo, Kyenekiki Kyando na kushoto ni Meneja Mkuu wa Uhusiano wa Biashara, Nura Masood.

Kampuni inayoongoza kwa utoaji wa bima za maisha TanzaniaSanlam Life Insurance, leo, imezindua bima ya elimu ya kipekee inayolenga kukupa uhakika wa elimu ya mwanao.
'Bima hiyo inayoitwa “Sanlam Education Care', inawapa wazazi mpango wa akiba wa kila mwezi pamoja na faida ya bima ya maisha ambayo inalinda uwekezaji wako katika tukio la kifo au ulemavu wa kudumu. 
Afisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam Life Insurance  amesema,"kuwekeza katika elimu ya mtoto wako ni moja ya zawadi bora ambayo wazazi wanaweza kuwapatia watoto wao”. Elimu imeanza kuwa huduma ghali katika maisha ya siku hizi, kwahiyo wazazi wanashauriwa kufanya maamuzi ya busara ya uwekezaji pale linapokuja suala la ustawi wa maisha ya baadaye ya watoto wao. Sanlam Education Care ni suluhisho kamili, kwani imebuniwa kama mpango wa akiba unaowawezesha wazazi kuwa na utaratibu mahususi wa kuweka akiba ambao unazingatia kupanda kwa gharama za elimu.

 "Hakuna huduma nyingine ya bima ya maisha inayokidhi haja ya kulinda elimu ya mtoto kama huduma hii ya Sanlam Education Care. ‘Kuongezeka kwa huduma ya Sanlam Education Care kwenye orodha ya bidhaa zetu' inatilia mkazo dhamira yetu ya kupanua wigo wa huduma zenye ubunifu na zinazokidhi mahitaji ya wateja wetu pamoja na kuboresha na kulinda ukwasi wao"
Viewing all 110167 articles
Browse latest View live




Latest Images