Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110173 articles
Browse latest View live

MMOJA KATI YA HAWA KUMRITHI SEPP BLATTER, FIFA

$
0
0
Na Bakari Issa Madjeshi

Shirikisho la Kandanda Duniani (FIFA) leo,Februari 26  linatarajiwa kupata Rais mpya ambaye atakuwa mrithi wa Rais anayemaliza muda wake, Sepp Blatter.

Katika uchaguzi huo utakaofanyika mjini Zurich nchini Uswizi, wapiga kura wapatao 207 watakusanyika nchini humo, kwa ajili ya kukamilisha zoezi hilo.

Lakini Kiongozi huyo anayemaliza muda wake, akiwa kama Kiongozi wa Bodi ya Mpira wa Miguu tangu mwaka 1998, Blatter (79) alisema mwaka jana “ilikuwa ajiuzulu kutokana na kashfa ya rushwa.”

Katika Uchaguzi huo,Wagombea watano wanatarajiwa kumrithi,Blatter.

Uchaguzi huo unatarajiwa kuanza saa 6 kwa saa za mjini Zurich;sawa na saa 4 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.

Wagombea hao ni  
Sheikh Salman bin Ebrahim al-Khalifa
 Gianni Infantino
Prince Ali bin al-Hussein
Tokyo Sexwale
Jerome Champagne.

MAZISHI YA MAREHEMU GERVASE RUTAGUZA YAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM LEO.

$
0
0
Ndugu wa Marehemu wakiwa katika ibada nyumbani kwa Marehemu Kurasini jijini Dar es Salaam ibada ya kumuaga marehemu Gervase Rutaguza aliyefariki dunia Februari 23 mwaka huu.
Padre wa kanisa Katoliki la Mtakatifu Maurus, Kurasini jijini Dar es Salaam akiombea mwili wa marehemuGervase Rutaguza aliyefariki dunia Februari 23 mwaka huu kwaajili ya kwenda kwenye mazishi katika makaburi ya Chang'ombe Maduka mawili jijini Dar es Salaam leo Februari 26, 2016.
Baadhi ya ndugu na Jamaa wa Marehemu Gervase Rutaguza aliyefariki dunia Februari 23 mwaka huu wakiaga mwili wa marehemu leo katika kanisa Katoliki la Mtakatifu Maurus, Kurasini jijini Dar es Salaam leo Februari 26, 2016.
Ndugu jamaa na marafiki wa Marehem Gervase Rutaguza aliyefariki dunia Februari 23 mwaka huu wakiwa katika ibada katika Katoliki la Mtakatifu Maurus, Kurasini jijini Dar es Salaam leo na kuelekea katika makaburi ya Chang'ombe Maduka mawili jijini Dar es Salaam leo.

AIRTEL FURSA YAINUA KIKUNDI CHA VIJANA WAJASIRIAMALI MJINI LINDI.

$
0
0
 Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (wa pili kushoto), akiwapongeza kikundi cha vijana watano wajasiriamali  kijulikanacho kwa jina la Sauti ya Jamii baada ya kuwakabidhi msaada wa Zizi jipya la mbuzi, mbuzi 44 na vitendea kazi  kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’ mjini Lindi katika mtaa wa Kariakoo. Wanaoshuhudia (kutoka kulia) ni Afisa maendeleo ya vijana mkoa wa lindi Sauda Mponjoli akifuatiwa na Afisa Utamaduni Mkoa, Makalaghe Shekhalaghe.
 Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (wa pili kushoto), akiwapongeza kikundi cha vijana watano wajasiriamali  kijulikanacho kwa jina la Sauti ya Jamii baada ya kuwakabidhi msaada wa Zizi jipya la mbuzi, mbuzi 44 na vitendea kazi  kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’ mjini Lindi katika mtaa wa Kariakoo. Wanaoshuhudia (kutoka kulia) ni Afisa maendeleo ya vijana mkoa wa lindi Sauda Mponjoli akifuatiwa na Afisa Utamaduni Mkoa, Makalaghe Shekhalaghe.
Meneja wa Huduma za jamii Kampuni ya Airtel Tanzania,Bi Hawa Bayumi (kati) akitoa elimu Kwa Afisa Utamaduni Mkoa,Makalaghe Shekhalaghe (kulia) pamoja na Afisa Vijana mkoa Lindi Bi Sauda Mponjoli (wa pili kulia Jinsi Airtel inavyotoa Fursa kwa Vijana Kupitia Airtel Fursa wakishuhudiwa na vijana wa kikundi cha Sauti ya Jamii waliowezeshwa na mradi huo wa Airtel Fursa kwa kupatiwa  Zizi jipya la mbuzi, mbuzi 44 na vitendea kazi vyenye dhamani ya shs milioni 10.

 WAFANYAKAZI wa kampuni ya simu za mkoni ya Airtel mkoani Lindi wamejumuika katika mradi wa kijamii wa  kampuni yao wa Airtel FURSA kwa kuwawezesha vijana wajasiriamali wa kikundi cha sauti ya jamii mkoani humo kwa kuwainua kibiashara na kuwajengea banda la ufugaji wa mbuzi la kisasa na kuwaongezea mbuzi 44 pamoja na vitendea kazi kama vile majembe na rato kwa ajili ya kuanza kilimo.

Vijana hao wapatao watano waliamua kuungana kwa pamoja baada ya kupata mafunzo kwenye mradi wa Kijana Jiajiri uliokuwa unaendeshwa na shirika la Restless Development ambao ulilenga vijana walio nje ya shule; kuwajengea uwezo ili waweze kujiajiri wenyewe na kupunguza ukosefu wa ajira nchini.

Kikundi cha Sauti ya Jamii kimesajiliwa na halmashauri, na kiliomba ardhi serikali za mitaa kwa ajili ya kilimo na kikapewa ekari 50, hivyo ukosefu wa mtaji ndio uliwakwamisha kuanza shughuli za  kilimo.

Akiongea wakati wa ujenzi wa banda hilo la kisasa la mbuzi  kiongozi wa msafara wa ziara hiyo na meneja mauzo kanda ya Lindi Edmund Lasway  alisema “Airtel tunayofuraha kuona tunaweza kusaidia vijana wenye moyo wa kujiendeleza kama hawa. Kabla ya hapa wamekuwa na mbuzi wapatao kumi na nne ambapo hawakuweza kuwapatia faidi ya kutosha, lakini kutokana na ongezeko hili la mbuzi na vitendea kazi kwa ajili ya kuinua biashara yao  ili waweze kutimiza malengo yao mengine makubwa waliyojiwekea  kama vile ya ukulim” .

Ni matumaini yetu kuwa fursa hii itawawezesha kufika mbali kibiashara na kutanua wigo wa biashara yao kwa kupata masoko na kuuza mifugo na kulima mazao yao katika ubora zaidi . Tunatoa wito kwa vijana wengine  kujitokeza na kutokukata tamaa ya maisha na kuchangamkia fursa kama hizi pale zinapojitokeza.

Kwa upande wake mwakilisha wa kikundi cha Sauti ya jamii, Shabani Kikotokeki, alisema “tunawashukuru sana Airtel kwa kutuwezesha kuinua biashara yetu na kutupa nguvu zaidi ya kujiendeleza kibiashara na hata kuwatia moyo vijana wenzetu wanaotuzunguka. Tunategemea kuinua kipato chetu na hata familia zetu  hivyo tunawahimiza vijana wengine hapa nchini kutokukata tamaa ya maisha na kuchangamkia fursa hizi zinapojitokeza.


Airtel kupitia huduma zake za jamiii imeweza kuwafikia vijana zaidi ya 20 kwa kuwapatia vitendea kazi katika msimu huu wa pili wa Airtel FURSA na kwa upande wa mafunzu ya biashara ya ujasiriamali imewafaidisha vijana wapatao 1000 katika  msimu huu wa pili wa  Airtel FURSA ambapo lengo ni  kufikia vijana wengi zaidi.

Waziri Jenista Mhagama atembelea Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA)

$
0
0

Mkurugenzi Mkuu wa SSRA Bi. Irene Isaka akikabidhi vitendea kazi kwa Mh. Jenista Mhagama Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Walemavu.
Mkurugenzi Mkuu wa SSRA Bi. Irene Isaka akifafanua jambo wakati wa kikao cha pamoja na Mheshimiwa Waziri Jenista Mhagama (kushoto), ofisini hapo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Walemavu Jenista Mhagama akizungumza na wafanyakazi wakati alipotembelea Mamlaka hayo kwa lengo la kujionea utekeleza wa Sheria ya Mamlaka ya Hifadhi ya Jamii.
Mkurugenzi Mkuu wa SSRA Bi. Irene Isaka akifafanua jambo wakati wa kikao cha pamoja na Mheshimiwa Waziri Jenista Mhagama (kushoto), ofisini hapo.

MTOTO ALIYETENGENEZA JEZI YA LIONEL MESSI KWA MFUKO WA PLASTIKI, ATUMIWA JEZI HALISI NA NYOTA HUYO

$
0
0
Mtoto wa kiume mwenye uraia wa taifa la Afghanistan ambaye hivi karibuni aligonga vichwa vya mitandao ya kijamii kwa ku vaa fulana ya mfuko wa plastiki ilio na jina la Lionel Messi hatimaye amepata jezi nzuri kutoka kwa mshambuliaji huyo wa Argentina.

160225110545__88438940_messi_boy

Murtaza wa Afghan akivalia jezi nzuri aliyotumiwa na Messi

BBC ilimsaidia Messi kumtafuta mtoto huyo ambaye anajulikana kuwa shabiki mkubwa wa mchezaji huyo wa Argentina. Murtaza Ahmadi mwenye miaka 5, anatoka katika wilaya ya Jaghori mashariki mwa mkoa wa Ghazni nchini Afghanistan.

Timu ya usimamizi wa Messi ilithibitisha siku ya Alhamisi kwamba Murtaza alitumiwa jezi ya mshambuliaji huyo wa Argentina iliotiwa saini pamoja na mpira kutoka kwa mshambuliaji huyo wa Barcelona.

“Ninampenda Messi na fulana yangu inasema Messi ananipenda,”Murtaza alisema,tayari akimuigiza mshambuliaji huyo anavyosheherekea bao lake.
Msako wa mtoto huyo katika mtandao ulisababishwa na picha moja iliyoenea katika mitandao ikimuonyesha amevaa fulana ya plastiki ya Messi.

160127133410_afgha_boy_messi_640x360_twitterjoynaw5

Hii ndio jezi aliyotengeza nyumbani na kuvaa

Source: BBC

WAZIRI MAKAMBA AKUTANA NA BALOZI WA KUWAIT NCHINI

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mh. January Makamba (kushoto) akiongea na Balozi wa Kuwait Bw. Jasem Al-Najem, Balozi huyo alimtembelea Mh. Makamba Ofisini kwake leo Mtaa wa Luthuli jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujadiliana masuala ya hifadhi na usimamizi wa Mazingira.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mh. January Makamba (kushoto) akiongea na Balozi wa Kuwait Bw. Jasem Al-Najem, Balozi huyo alimtembelea Mh. Makamba Ofisini kwake leo Mtaa wa Luthuli jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujadiliana masuala ya hifadhi na usimamizi wa Mazingira. Wengine katika picha ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makumu wa Rais Bw. Mbarak Abdulwakil na Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje Bw. Barthlomew Jungu.

Tanzania kunufaika na Dola Bilioni 60 za China sekta ya Nishati

$
0
0
Na Asteria Muhozya, Dar es Salaam,

Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China imeitaja nchi ya Tanzania kuwa na nafasi kubwa ya kunufaika na fedha kiasi cha Dola Bilioni 60 kupitia uwekezaji sekta ya nishati, fedha zilizoahidiwa kutolewa na nchi hiyo wakati wa Mkutano wa Sita wa Jukwaa la Ushirikiano baina ya China na Afrika, uliofanyika nchini Afrika Kusini mwezi Desemba,2015.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es Salaam na Balozi wa China nchini, Dkt. Lu Youqing na ujumbe wake alipokutana na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ofisini kwake jijini Dar es Salaam na kuongeza kuwa, China ina imani kubwa na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna anavyosimamia masuala mbalimbali nchini, pia Profesa Sospeter Muhongo kutokana na namna anavyoisimamia sekta ya Nishati na Madini.

Miongoni mwa Sekta zinazopewa kipaumbele katika fedha hizo ni pamoja na pamoja na miundombinu, afya, biashara, uwekezaji na kupunguza umaskini, barani Afrika.

Kutokana na mahusiano mazuri ambayo yamekuwepo kwa miongo kadhaa baina ya nchi hizo mbili, Balozi Youqing amemwakikishia Waziri Muhongo kuwa, China itaendeleza ushirikiano huo kwa kuhakikisha inazishawishi kampuni kubwa na zilizobobea kitaalamu na kiteknolojia za China, ili ziweze kushirikiana na Tanzania katika sekta ya nishati, na zaidi katika uzalishaji umeme kwa kutumia Makaa ya Mawe kutokana na namna ambavyo Wizara inavyokipa kipaumbele chanzo hicho kuzalisha umeme nchini.

Wakati huo huo, China imesema itaendelea kutoa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi Watanzania kusoma masuala ya mafuta na gesi katika vyuo mbalimbali nchini humo kutokana na umuhimu wa sekta hiyo na kwamba, China inapenda Tanzania ifanikiwe katika kuzalisha wataalam wa kutosha katika fani hizo na kuongeza kuwa, anatambua juhudi zinazofanywa na Waziri Muhongo kuhakikisha wanafunzi wengi wa kitanzania wanapata fursa ya kusoma masuala ya mafuta na gesi maeneo mbalimbali Duniani, ikiwemo China.

Aidha, leo tarehe 26 Februari, 2016, Wizara ya Nishati imetangaza nafasi za Masomo kwa wanafunzi wa Kitanzania kuomba kusoma katika Vyuo vya China katika fani za Mafuta na Kazi katika ngazi za Shahada ya Uzamili (Masters) na Uzamivu (Phd). Maelezo zaidi ya kuomba nafasi hizo yanapatikana kupitia tovuti ya wizara www.mem.go.tz
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati), akiongea jambo na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China, Dkt. Lu Youqing (wa pili kushoto) wakati alipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni Afisa Ubalozi wa China.
Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini, Dkt. Lu Youqing (wa tatu kushoto), akimweleza jambo Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala Utumishi Wizara ya Nishati na Madini, Lusias Mwenda. Wengine ni ujumbe ulioambatana na Balozi wa China.

MTAMBUE KIJANA WA KITANZANIA DESMOND ANDREW ALIYEANZISHA KAMPUNI YA MAWASILIANO YA CW NET

$
0
0
Kijana wa Kitanzania Desmond Andrew alimeanzisha kampuni ya Mawasiliano ya CW Net  ambayo inatengeneza Power Bank, Smart Bracelet na Modem. Hakika Tanzania kuna vijana wengi kama Desmond Andrew lakini tatizo kubwa linalowakabili ni upatikanaji wa mtaji wa kuendeleaza vipaji vyao.
Mwanzilishi na mmiliki wa Kampuni ya Mawasiliano ya CW Net akimtoa ufafanuzi Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF, Geoffrey Simbeye (aliyevaa suti) kuhusu Smart Bracelet na kazi zake katika maonesho yaliyoandaliwa na shirika la Viwango nchini Tanzania(TBS) yanayoendelea katika ukumbi wa Mlimani Cityjijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF, Geoffrey Simbeye (aliyevaa suti) akiuliza swali mara alipotembelea banda la CW Net maonesho ya Makampuni ya Kitanzania yanayotoa bidhaa yenye viwango vya kutosha hapa nchini.
Smart Bracelet hiki ni kifaa mojawapo kinachotengenezwa na kampuni ya Mawasiliano ya CW Net ambacho kifaa hicho kinahesabu hatua ambazo mtu ametembea nani kwa kiasi gani nguvu uliyoitumia pamoja na kukontrol muda unaolala na unaoamka, pia pia kifaa hicho kinaweza kuunganishwa na simu ya smartphone yako na kutambua simu ikiwa inaita kwa umbali wa mita kumi(10)

Hakika penda cha nyumbani

MBUNGE COSATO AFANYA ZIARA JIMBONI KUJIONEA SHUGHULI MBALIMBALI.

$
0
0
Mbunge wa Mafinga Vijijini, Cosato Chumi  (Mwenye diary mkononi) akipata maelekezo katika kiwanda cha kiwanda cha Sao Hill katika ziara ya kutembelea Taasisi Binafsi na za Umma. 
 Mbunge wa Mafinga Vijijini, Cosato Chumi (wa pili kutoka kushoto)akionyeshwa shughuli zinazofanywa katika kiwanda cha Sao Hill.
Wengine  ni Denis kutemile anayefuatia na Hezron Vuhahula ambaye ni katibu wa mbunge.
 Baadhi ya wafanyakazi wa sao hill wakiwa kazini.
 Sehemu ya nguzo zinazozalishwa  na kiwanda cha Sao Hill.

MBUNGE wa Mafinga Vijijini, Cosato Chumi amefanya ziara kutembelea  Taasisi za Umma na Binafsi kwa kutembelea Sao Hill Industries, Sao Hill Forest, Kiwanda cha Pareto na kampuni ya simu ya TTCL.

Katika ziara hiyo mbunge ametembelea Vituo vya Polisi, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB), NSSF , Bank za Mucoba, NMB na CEDB,Magereza ,pamoja na Taasisi za Elimu.

Amesema kufanya ziara ni kujitambulisha, kufahamiana na kufahamu changamoto wanazokabiliana nazo.

Chumi amesema nguzo za umeme, kutoka Afrika Kusini  sio sahihi wakati  zinaweza kupatikana na uwezo wa kuzalisha  nguzo 90000 kwa mwaka.

Amesema kutokana na maelezo ya kiwanda hicho  na wamesema ikiwa watapata nafasi ya kuongezewa uwezo wa kuvuna kutoka Shamba la Taifa la Msitu wa Sao Hill, wanaweza kusambaza nguzo zaidi.

 Mgao wa kuvuna wa cubic 120,000 Changamoto ni kuwa wakipewa kitalu lakini ndani ya kitalu sio kila mti unafaa kwa nguzo kwa hiyo ombi lao, wapewe kwa mfumo wa kwamba wavune kile ambacho kinafaa kwa nguzo harafu miti inayofaa labda kwa karatasi ibaki kwa ajili ya Kiwanda cha mgololo.

wakati huohuo wawekezaji Mafinga waiomba Tanesco kuwafungia laini madhubuti ya Umeme katika kiwanda cha Pareto ambacho kiko chini ya Kampuni ya Pyrethrum Company of Tanzania (PCT).

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Charles Mwijage azungumzia uagizaji wa sukari nchini

TAMWA YASIKITISHWA KESI ZA UBAKAJI/ULAWITI KWA WATOTO KUTOHUKUMIWA.

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Bi. Edda Sanga(katikati) akizungumzia mbele ya waandish wa habari (hawapo pichani) ni kwa jinsi gani wamepata malalamiko kutoka kwa familia zinazofanyiwa unyanyasaji wa kijinsia hasa ubakaji na ulawiti katika ngazi za mahakama, polisi na baadhi ya hospitali hapa nchini. 
Mratibu wa Kituo cha usuluishi cha TAMWA, Bi. Gladness Hemedi Munuo akizungumza mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati walipokuwa wakilaani vikali ucheleweshwaji na upotoshaji wa kesi za vitendo vya ukatili. 
Mwanasheria wa TAWLA, Mary Richard (wa kwanza kulia) akizungumza ni kwa jinsi gani wanavyowasaidia wanawake wanaofanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia leo katika mkutano na waandishi wa habari leo. 

CHAMA cha Wanahabari wanawake nchini Tanzania(TAMWA) kimelaani vikali ucheleweshwaji na upotoshwaji ushahidi wa kesi za vitendo vya ukatili wa kijinsia hasa ubakaji na ulawiti katika ngazi ya mahakama, polisi na baadhi ya madaktari hospitalini. Hali hiyo imekuja baada ya TAMWA kubaini kesi sitini na mbili (62) za ubakaji zimeshindwa kutolewa hukumu au uamuzi na mahakama mbalimbali jijini Dar es Salaam katika kipindi cha mwaka 2014 hadi 2015. 

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Bi. Edda Sanga amesema kati ya kesi 63 za ubakaji, ni kesi moja tu mtuhumiwa amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela, kesi arobaini na tatu (43) bado ziko mahakamani, kesi kumi na saba (17) zimeshindwa kufika mahakamani ambapo kesi mbili zimefutwa kwa kukosa ushahidi. 

Pia aliongezea kwa kusema kuwa uongozi wa TAMWA umesikitishwa kuona kesi hizo zikicheleweshwa na vyombo mbalimbali vya serikali ikiwemo jeshi la polisi na mahakama. Na kuna baadhi ya viongozi wanapokea rushwa ili kuzima kesi za watoto wanaofanyiwa ukatili wa kijinsia, pia baadhi ya polisi wamekuwa wakishindwa kutoa ushirikiano kwa mlalamikaji ambapo wanatoa maneno ya vitisho na kupelekea mlalamikaji kukosa ujasiri wa kuhifadhi na kutetea kesi yake na wakati mwingine mama mzazi anaandikwa kama mlalamikaji badala ya mtoto mwenyewe aliyefanyiwa ukatili huo. 

Pia wameunga mkono tamko la Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliposema wakati wa siku ya sheria duniani kuwa "Kila Hakimu wa Mahakama anapaswa kuhukumu kesi si chini ya 260 kwa kila mwaka na kwa haki", Hivyo basi wao kama TAMWA wanaamini ndani ya mwaka huu Mahakama hapa nchini zitafanya kazi yao kiweledi ili kuweza kupunguza ukatili wanaofanyiwa watoto wa kike.

ONE STOP BORDER POST SET FOR LAUNCH AT HOLILI-TAVETA ON 27TH FEB 2016

$
0
0


East African Community Headquarters, Arusha, 26th February, 2016: The East African Community (EAC) is officially launching the One Stop Border Post (OSBP) at Holili and Taveta border between Kenya and Tanzania tomorrow 27th February 2016, in order to enhance trade facilitation and quicken clearance of people in a conducive and secure environment.

The launch will be conducted by Phyllis J. Kandie, EGH, Cabinet Secretary, Ministry of Labour and East African Affairs, the Republic of Kenya and Hon. Amb. Dr. Augustine P.Mahiga (MP), Minister for Foreign Affairs, East African Regional and International Cooperation; the United Republic of Tanzania, in the presence of other Ministers/Cabinet Secretaries from the other Partner States. The occasion will also be graced by Amb. Dr. Richard Sezibera, the EAC Secretary General and the representatives of the financiers Trademark East Africa (TMEA) and the Business Community, led by the East African Business Council. 
The OSBP is a concept that reduces the number of stops incurred in a cross border trade transaction by combining the activities of both countries' border organizations at a single location with simplified exit and entry procedures and joint processing, where possible. Motor vehicles and pedestrians only stop in the country of entry and perform exit and entry border formalities. One-stop is achieved by placing the border officials of two adjoining countries at each other's adjoining border post so that each border post controls only the traffic entering the country. The exit formalities of the exit country and the entry formalities of the country of entry are carried out at the border post in the country of entry. 
At Holili and Taveta OSBP, Kenyan Government officials performing exit functions have been deployed at Holili and are working with the Tanzanian Government officials performing entry functions. For Tanzanian Government officials performing exit functions, they have been deployed at Taveta and are working within the same building with the Kenyans that are performing entry functions. 
Traffic in either direction is thus bypassing the exit border post and going directly to the border post of entry in the other country. The main feature of the OSBP concept is that traffic crossing the border stops once instead of stopping at the border post of exit for exit formalities and at the border-post of entry for entry formalities. Hence One-Stop Border Post.  
In the East African Community all OSBPs will operate using a regional framework and in this regard, the EAC OSBP Act 2013 has been assented to by all Partner States and is being gazetted. The OSBP Regulations have been drafted to operationalize the OSBPs at regional level and await the Council of Ministers' approval. The OSBP Procedure Manual is being developed to guide and ensure uniform operations of the OSBP. 
The Holili and Taveta OSBP has been constructed with the financial support of the Trade Mark East Africa (TMEA). The OSBP is operating in conformity with the regional OSBP requirement as most of the bilateral arrangements are based on the regional legal and administrative instruments. 

From commencement of the OSBP at Holili and Taveta, a number benefits to the people and trade have been noticed. 
Some of the benefits are; quick clearance of pedestrians and passengers as they are now not stopping in the country of exit; saving of time as travelers are only stopping once for border formality; increased turnaround of commercial traffic as compliant traders are now spending little time at the border; reduced time spent at the border for inspection as it is only conducted once; reduced cost of doing business as interventions are reduced from two to one and cooperation among border agencies as they are now sharing information in a more organized and transparent manner entrenching regional integration.

Mama Lucy Mwandosya Akabidhi Kituo cha Ufundi Stadi

$
0
0
Kituo cha kulea na kuendeleza watoto na wanafunzi yatima na wanaotoka katika mazingira magumu Lucy's Hope Centre kimesomesha watoto zaidi ya 400 (mia nne) kuanzia shule za msingi, vyuo vya elimu, vyuo vya ufundi, mpaka vyuo vikuu. 
Wanafunzi zaidi ya ishirini ama wako vyuo vikuu au tayari wamehitimu shahada ya kwanza. Ili kukabiliana na changamoto ya ongezeko la wanafunzi wasiopata nafasi ya kuendelea na elimu ya kawaida, Kituo, kwa kushirikiana na wananchi wa Lufilyo, Busokelo, na wafadhili wapenda maendeleo kimejenga kampasi katika eneo la eka zaidi ya kumi,lengo likiwa ni kuanzisha mafunzo ya stadi mbalimbali. 
Ili kupanua mawanda ya mafunzo hayo na ili Kituo kiweze kusaidia jamii katika Halmashauri ya Busokelo na Wilaya ya Rungwe na Taifa kwa ujumla, Mama Lucy Mwandosya na jamii ya Lufilyo wametoa Kituo hicho kwa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo.
Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo nayo imekitoa Kituo hicho kwa VETA ( Vocational Education and Training Authority ) ili kianzishwe Kituo cha VETA cha ufundi stadi( Vocational Education Training Centre). 
Makabidhiano hayo yalifanyika katika sherehe fupi na iliyofana kijijini Lufilyo, mgeni rasmi akiwa Mheshimiwa Stella Manyanya, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia, na Ufundi.Pichani juu  Mama Lucy Mwandosya na Prof. Mark Mwandosya wakimkabidhi Mwenyekiti wa Halmashauri ya Busokelo Mhe. Anyosisye Njobelo ufunguo wa Kituo ili amkabidhi Mheshimiwa Waziri. 
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundu Mhe. Eng Stella Manyanya akikabidhiwa hati rasmi ya kituo hicho 
Mandhari ya kituo cha kulea na kuendeleza watoto na wanafunzi yatima na wanaotoka katika mazingira magumu Lucy's Hope Centre

TANZANIA WOMEN OF ACHIEVEMENT UNVEILS PLEDGE FOR PARITY CAMPAIGN

$
0
0
Tanzania Women of Achievement (TWA) has announced the launch of the Pledge for Parity Campaign in commemoration of this year's International Women's Day care celebration. The campaign is a clarion call for this year’s International Women’s Day (IWD) that calls on everyone to take concrete steps to accelerate the achievement of gender parity in the country. It also calls on the society to practice gender-balanced leadership, respect and value differences, develop more inclusive and flexible cultures and also root out workplace bias.

Speaking in a press conference at TWA offices in Dar es Salaam today, TWA President, Ms Irene Kiwia said that the aim of the Pledge for Parity Campaign is to call upon men and women to join forces and collectively help women advance equally and realize their limitless potential.

“This campaign is meant to call on all the stakeholders including the media, individuals and organizations to identify and create awareness on the gaps that hinder the progress towards gender parity and to pledge to take concrete steps to accelerate change.” Ms Kiwia said. 

 "The World Economic Forum predicted in 2014 that it would take until 2095 to achieve global gender parity. Then one year later in 2015, they estimated that a slowdown in the       already glacial pace of progress meant the gender gap wouldn't close entirely until 2133. This is a lot of years to wait on. TWA is therefore joining the world by urging Tanzania to put gender in the country's agenda and speed up the clock to achieve gender parity quicker" further said Ms. Kiwia.

Mrs Sadaka Gandi, TWA Chairperson calling on individuals, organizations, the government and others stakeholders to participate, said that the campaign will start with a six kilometer walk on the 5th of March morning from the ‘Goat Race Grounds’, popularly known as ‘Uwanja wa Farasi”, through the junction of International School of Tanganyika (IST) and pass through St. Peter’s Catholic Church, through the Kenyan High Commission and back to the starting point.

"The walk will be followed by an International Women’s Day Conference that will take place on the 6th of March 2016 at the Hyatt Regency, The Kilimanjaro Hotel. The conference  will bring together men and women from different arena to share and inspire each other, show-case and train on what has been achieved on "Gender Parity" so far since The Beijing Conference 21 years ago, what gaps still exists and how we all can play a role to accelerate change. We believe that your support will not only contribute to the advancement of women’s cause but will also show-case your company’s contribution to the achievement of gender parity”.

"The Pledge for Parity Campaign will address issues affecting women in regard to education, health, leadership and economy all being important aspects of society development since they are all linked to economic growth. Women’s advancement and leadership are central to business performance and economic prosperity”, Mrs. Gandi concluded.

Article 4


STOP PRESS: MAWAZIRI WOTE WALIOPEWA HADI LEO JIONI KUJAZA NA KUREJESHA TAMKO LA MALI NA MADENI, HATI YA UADILIFU WAMETEKELEZA AGIZO LA RAIS KATIKA MUDA MUAFAKA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema agizo lilitolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli la kuwataka mawaziri ambao hawajajaza Tamko la Rasilimali na Madeni wakamilishe kabla ya saa 12 leo jioni limetekelezwa. 

Waziri Mkuu amepokea barua kutoka kwa Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Jaji (Mst.) Salome Kaganda ikithibitisha kuwa mawaziri na naibu mawaziri wote wametekeleza agizo hilo. 

“Hadi kufikia saa 9.30 leo alasiri (Ijumaa, Februari 26, 2016) mawaziri wote walikuwa wamekamilisha fomu zao za kuzikabidhi katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma,” alisema Waziri Mkuu. 

Rais Magufuli leo asubuhi alitoa maelekezo kwamba Mawaziri ambao hawajajaza Tamko la Rasilimali na Madeni ifikapo leo Ijumaa tarehe 26 Februari, 2016 saa 12.00 jioni wawe wamejaza na kurejesha Fomu ya Tamko la Rasilimali na Madeni katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Dar es Salaam. Waziri ambaye atashindwa kutekeleza agizo hili atakuwa amejiondoa mwenyewe kwenye nafasi yake.

Mawaziri waliotakiwa kurejesha fomu za tamko la rasilimali pamoja na hati ya ahadi ya uadilifu kuwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Charles Kitwanga na Waziri wa Nchi (OMR – Muungano na Mazingira), Mhe. January Makamba. 
Wengine ni Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa, Dk. Augustine Mahiga ambaye alitakiwa kurejesha hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako ambaye alitakiwa kutoa tamko la rasilmali na madeni.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nchi (OMR – Mazingira), Mhe. Luhaga Mpina aliyetakiwa kurejesha fomu za tamko la rasilmali na madeni pamoja na hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S.  L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM.
IJUMAA, FEBRUARI 26, 2016

BREAKING NEWZZZZZ: MAWAZIRI WAPEWA MWISHO LEO KUJAZA NA KUREJESHA TAMKO LA MALI NA MADENI, HATI YA UADILIFU

$
0
0

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli amesema mawaziri ambao hawajajaza Tamko la Rasilimali na Madeni wawe wamejaza fomu hizo na kuzirejesha katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Dar es Salaam ifikapo leo saa 12.00 jioni (Ijumaa, Februari 26, 2016).

Agizo hilo la Rais limetolewa leo na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mbele ya waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika ofisini kwake, Magogoni jijini Dar es Salaam.

“Mheshimiwa Rais ameelekeza mawaziri ambao hawajajaza tamko la rasilmali au hati ya ahadi ya uadilifu wafanye hivyo na kuzirejesha kabla saa 12 jioni na Waziri ambaye atashindwa kutekeleza agizo hili atakuwa amejiondoa mwenyewe kwenye nafasi yake,” amesisitiza Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu amesema wakati akifungua mafunzo ya Mawaziri na Naibu Waziri kuhusu Mwongozo wa Maadili ya Viongozi wa Umma na Utekelezaji wa Ahadi ya Uadilifu yaliyofanyika Ikulu jana (Alhamisi, Februari 25, 2016) alikabidhiwa majina ya Mawaziri na Naibu Mawaziri ambao hawajawasilisha Tamko la Rasilimali na Madeni kwa Kamishna wa Maadili.

Amewataja mawaziri wanaotakiwa kurejesha fomu za tamko la rasilimali pamoja na hati ya ahadi ya uadilifu kuwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Charles Kitwanga na Waziri wa Nchi (OMR – Muungano na Mazingira), Bw. January Makamba. 

Wengine ni Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa, Dk. Augustine Mahiga ambaye anatakiwa kurejesha hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako ambaye anatakiwa kutoa tamko la rasilmali na madeni.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nchi (OMR – Mazingira), Bw. Luhaga Mpina anatakiwa kurejesha fomu za tamko la rasilmali na madeni pamoja na hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma.

WAZIRI NAPE NNAUYE AONGOZA MAMIA YA WAOMBOLEZAJI KWENYE MZISHI YA MWANAMUZIKI MKONGWE NCHINI, KASSIM SAID MAPILI

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akiweka udogo kwenye kaburi la Mwanamuziki mkongwe hapa nchini, Mzee Kassim Said Mapili, wakati wa mazishi yaliyofanyika kwenye Makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam leo.
Mwili wa mwanamuziki mkongwe hapa nchini, Mzee Kassim Said Mapili ukiwasili kwenye makabuli ya Kisutu, jijini Dar es Salaam leo.
Mwili wa mwanamziki mkongwe hapa nchini, Kassim Said Mapili ukiwekwa katika kabuli wakati wa mazishi yaliyofanyika kwenye makabuli ya Kisutu, jijini Dar es Salaam leo.
Waombolezaji waliofika kumsindikiza kwenye nyumba ya milele  Mzee Kassim Said Mapili, wakipata mawaidha baada ya mazishi.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

NEWS ALERT: LADY JAYE DEE "NAAMKA TENA"

WAZIRI KITWANGA AKUTANA NA VIONGOZI WA NIDA, AWATAKA KUONGEZA KASI UANDAAJI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kushoto) akizungumza na Watendaji Wakuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) pamoja na Wakuu wa Idara wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kuhusu masuala mbalimbali ya utendaji wa kazi ndani ya Mamlaka hiyo na Wizara kiujumla. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Wa kwanza upande wa kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira akifuatiwa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara hiyo, Lilian Mapfa. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa NIDA, Dk. Modest Kipilimba.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) akizungumza na Watendaji Wakuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) pamoja na Wakuu wa Idara wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kuhusu masuala mbalimbali ya utendaji wa kazi ndani ya Mamlaka hiyo na Wizara kiujumla. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Wa tatu kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira akifuatiwa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara hiyo, Lilian Mapfa na Mkurugenzi wa Sera na Mipango wizarani hapo, Haji Janabi. Wa tatu kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa NIDA, Dk. Modest Kipilimba, anayefuata ni Mkurugenzi wa Utawala na Fedha, Avelin Momburi na Mkurugenzi wa Uzalishaji Vitambulisho, Paul Bwathondi.
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dk. Modest Kipilimba akijitambulisha kabla ya kuanza kikao cha Watendaji Wakuu wa NIDA pamoja na Wakuu wa Idara wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Kikao hicho kilichoitishwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) na kufanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Wa pili kulia meza kuu ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira, na anayefuata ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara hiyo, Lilian Mapfa. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Viewing all 110173 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>