Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live

WANAFUNZI IFM WATEMBELEA DUKA JIPYA LA AIRTEL EXPO.

$
0
0
  Mkuu wa kitengo cha huduma za wateja wa Airtel Bi Adriana Lyamba (kushoto) ,akifafanua jambo kwa baadhi ya wanafunzi wa chuo cha usimamizi wa fedha kitengo cha IT,wakati walipofanya ziara ya kimafunzo katika duka jipya la Airtel Expo katika ofisi za makao makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam .
 Afisa mauzo wa Airtel Juma Hassan (katikati) ,akifafanua jambo kwa baadhi ya wanafunzi wa chuo cha usimamizi wa fedha kitengo cha IT,wakati walipofanya ziara ya kimafunzo katika duka jipya la Airtel Expo katika ofisi za makao makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam.
 Wanafunzi wa chuo cha usimamizi wa fedha kitengo cha IT wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa kitengo cha huduma za wateja wa Airtel Bi Adriana Lyamba (katikati) na baadhi ya wafanyakazi wa Airtel wakati walipofanya ziara ya kimafunzo katika duka jipya la Airtel Expo katika ofisi za makao makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam.
Wanafunzi wa chuo cha usimamizi wa fedha kitengo cha IT wakimsikiliza afisa masoko wa Airtel Tanzania Prosper Mwanda ( kulia) wakati walipofanya ziara ya kimafunzo katika duka jipya la Airtel Expo na kuweza kutembelea baadhi ya sehemu za katika ofisi za makao makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam.
 
-Wanafunzi wa IT wa chuo IFM wahimizwa kushirikiana na Airtel 
WANACHUO kutoka chuo cha usimamizi wa fedha (IFM) kitengo cha IT , wamefanya ziara ya mafunzo kwenye duka la kisasa la Airtel Expo lililopo katika ofisi kuu za Airtel mtaa wa morroco Dar es salam ikiwa ni mwendelezo wa kutanua wigo wa kutoa huduma zenye ubora za kibunifu kwa wateja wake.

Wanachuo hao waliweza kujifunza mambo mengi juu ya kampuni hiyo inavyofanya kazi kuanzia huduma zake hadi bidhaa zinazouzwa na kampuni hiyo. Ikiwemo Modem iliyozinduliwa hivi karibuni maarufu kama modem ya maajabu Wingle Modem inayouweza kutumika na zaidi ya watu 10 kwa wakati mmoja, Simu za Kisasa za gharama nafuu na zenye OFA nzuri 

Wanafunzi hao pia wamejionea jinsi duka la Airtel Expo linavyohudumia wateja wengi kwa kutumia teknolojia ya hali ya juu ya kidigitali.

Mkurugenzi wa Airtel huduma kwa wateja Bi Adriana Lyamba amewapongeza wanafunzi hao kwa dhamira yao ya kutaka kujifunza katika ulimwengu wa technolojia na kuwakaribisha wengine kuhudhuria' 

tumefarijika sana kuona wanafunzi toka vyuo vya ndani ya nchi yetu kama nyie IFM mnafunga safari na kuja kushuhudia hili, hongereni sana tunawakaribisha wote sio tu wanafunzi bali kila mpenda maendeleo ya technolojia kutembelea duka hili la kisasa na kujionea au kushauriana na Airtel kufanya mambo mengi bora zaidi ya ulimwengu wa mawasiliano" alisema Bi Lyamba.

KATIBU MKUU, WIZARA YA NISHATI NA MADINI PROF. JUSTIN NTALIKWA AFANYA ZIARA KATIKA KISIWA CHA SONGOSONGO NA KUSHUHUDIA KAZI KUBWA YA UENDELEZAJI WA GESI ASILIA INAYOFANYWA NA PANAFRICAN ENERGY.

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya PanAfrican Energy David K. Roberts (kulia) akimuelezea jambo Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa wakati wa ziara yake huko Songosongo katika visima vya gesi asilia.
 Ni katika ziara ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa katika visiwa vya Songosongo.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa akipata maelezo ya mradi kutoka PanAfrican Energy Operational SH Engineer Onestus Mujemula kuhusu mradi wa uchimbaji gesi asilia katika visima vinne uliomalizika kwa kutumia mtambo wa kisasa wa “RIG”
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa akiongea na wana habari wakati wa ziara yake ya kikazi katika visiwa vya Songosongo.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

UWEKEZAJI WA MRADI MKUBWA WA MAJI SAFI NA SALAMA WA RUVU CHINI NA RUVU JUU SASA INAELEKEA KUKAMILIKA.

WAAJIRI WAASWA KUTOUZA FOMU ZA OPRAS KWA WATUMISHI.

$
0
0
Na Beatrice Lyimo-Maelezo
OFISI ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imewataka waajiri wote nchini kuhakikisha watumishi wao wanapata Fomu ya wazi ya Mapitio na Upimaji Utendaji Kazi( OPRAS) wa utekelezaji bila usumbufu.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kitengo cha mawasiliano cha Ofisi hiyo imeeleza kuwa, kuna baadhi ya Taasisi za Umma watumishi wanaelekezwa kununua fomu za OPRAS kutoka kwa watu binafsi, kitendo ambacho ni kinyume cha Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo.

Fomu za OPRAS haziuzwi hivyo watumishi hawatakiwi kuzinunua, endapo mtumishi atashawishiwa au kulazimishwa kununua fomu hizi atoe taarifa Dawati la Malalamiko Ofisi ya Rais- Utumishi na Utawala Bora ili hatua stahiki zichukuliwe, imefafanua taarifa hiyo.

Pia Fomu hizo zinapatikana katika Tovuti ya Ofisi ya Rais-Menejiment ya Utumishi wa Umma yenye anwani ya www.utumishi.go.tz, hivyo waajiri wanaelezwa kutembelea tovuti hiyo.

Aidha, Serikali ilianzisha matumizi ya mfumo wa wazi wa mapitio na Tathimini ya Utendaji Kazi OPRAS mwezi Julai mwaka 2004 kupitia waraka wa Utumishi Na.2 wa mwaka 2004 na kufuta mfumo wa zamani wa kupima utendaji kazi wa mtumishi kwa njia ya siri.

Mabadiliko ya kutathimini UtendajI kazi wa Watumishi wa Umma kwa uwazi yanakwenda sambamba na Sera ya Menejiment na Ajira katika Utumishi wa Umma ya mwaka 1998 kama ilivyorekebishwa mwaka 2008 na kusisitiza uwekaji wa mifumo ya Menejimenti ya utendaji bora wa kazi inayojali matokeo.

SASA WATANZANIA KUONGEA KWA SAA MOJA BURE KILA SIKU.

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania,Ian Ferrao(wapili kushoto) Balozi wa Vodacom Tanzania, Nasibu Abdul (Diamond Platinum) Kaimu Mkurugenzi wa Uhusiano na Mawasiliano wa Kampuni hiyo, Rosalynn Mworia(kulia) na Zarina Hassan(kushoto)wakionesha mabango yenye ujumbe wa jinsi ya kujiunga na Promosheni ya “Ongea Deilee”, wakati wa uzinduzi wa promosheni hiyo leo jijini Dar es Salaam, Itakayowawezesha wateja wa mtandao huo kuongea kwa muda wa saa 1 bure kila siku pindi wakiongea jumla ya dakika 10 Vodacom kwenda Vodacom.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania,Ian Ferrao( kushoto) na Zarina Hassan(Kulia) wakionyeshwa tangazo la promosheni ya”Ongea Deilee” kwenye simu lililofanywa na msaanii wa muziki wakizazi kipya Abdul Nasibu”Diamond Platinum”( katikati) wakati wa uzinduzi wa promosheni hiyo leo jijini Dar es Salaam, Promosheni hiyo itawawezesha wateja wa mtandao huo kuongea kwa muda wa saa 1 bure kila siku pindi wakiongea jumla ya dakika 10 Vodacom kwenda Vodacom.
  Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania,Ian Ferrao(kushoto) akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa promosheni ya”Ongea Deilee” Itakayowawezesha wateja wa mtandao huo kuongea kwa muda wa saa 1 bure kila siku pindi wakiongea jumla ya dakika 10 Vodacom kwenda Vodacom leo jijini Dar es Salaam,anayeshuhudia kulia ni Balozi wa Vodacom Tanzania,Nasibu Abdul (Diamond Platinum)
 Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania,Ian Ferrao(wapili kushoto) akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa promosheni ya”Ongea Deilee” Itakayowawezesha wateja wa mtandao huo kuongea kwa muda wa saa 1 bure kila siku pindi waongeapo jumla ya dakika 10 Vodaocom kwenda Vodacom, leo jijini Dar es Salaam,wengine katika picha kutoka kushoto,Zarina Hassan, Balozi wa Vodacom,Nasibu Abdul (Diamond Platinum) Kaimu Mkurugenzi wa Uhusiano na Mawasiliano wa Kampuni hiyo,Rosalynn Mworia.


SASA ni wakati wa watanzania kuongea, ambapo kuanzia leo wateja wa Vodacom, mtandao unaongoza nchini wataweza kuongea bure kwa saa nzima!

Kupitia ofa yake maalum kwa wateja ya Ongea Bure Deilee, itakayokuwa ya miezi mitatu mfululizo, wateja wa Vodacom wataweza kuongea kwa muda wa saa moja bure kila siku.

Ili kujiunga na ofa hii ambayo haijawahi kutokea nchini, mteja anachotakiwa kufanya ni kuongea kwa dakika 10 kila siku kwa viwango ya malipo vya kawaida na hapo hapo atapata ofa ya kuongea kwa muda wa saa moja bure.

Ofa hii ya Ongea Bure Deilee pia imemuhusisha mwanamuziki nguli wa muziki wa Bongo Fleva nchini, Diamond Platnumz, ambaye moja ya kibao chake kinachotamba ni ‘Number One’, ambao pia ni mwito wa simu maarufu kwa watumiaji wa mtandao wa Vodacom.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa ofa hii, Mkurugenzi Mkuu wa Vodacom Tanzania Bw. Ian Ferrao amesema “Ongea Bure Deilee ni ofa ya aina yake kutolewa kwa wateja wa Vodacom popote walipo nchini. Ofa hii imebuniwa kubadilisha maisha ya wateja wetu walio wengi na kuendelea kuyafanya kuwa murua!”

Aliendelea kusema kuwa Vodacom Tanzania imedhamiria kuendelea kuvuka kile ambacho wateja wake wanakitarajia, kwa kuwaunganisha kwa viwango nafuu ambavyo wanazoweza kuvimudu, lengo kubwa likiwa ni kuweza kuwainua kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.

Ofa hii itatolewa kwa wateja milioni moja wa kwanza watakaojiunga kila siku kupitia ujumbe mfupi wa maneno ambapo watakuwa huru kuongea wakati wowote watakao, iwe usiku au mchana, ili mradi watakaowasiliana nao ni watumiaji wa mtandao wa Vodacom.

“Huu ni mwendelezo wa kampeni yetu ya Maisha ni Murua ambayo jitihada zetu katika kuwaletea wateja ofa za kipekee na ambapo kupitia ubunifu wa kutumia mtandao, tunawezesha maisha ya wateja wetu wote nchini kuwa murua. Kama ambavyo tunasema siku zote, tutaendelea toa huduma zinazowawezesha wateja wetu kuwasiliana kwa urahisi na wapendwa wao na hata katika shughuli zao za uzalishaji mfululizo,” aliongeza Ferrao.

Kwa upande wake, Diamond Platinumz, ambaye sasa ni balozi wa Vodacom alisema “Ninayo furaha kuwa sehemu ya kampeni hii kabambe kutoka Vodacom. Nilipopata taarifa kwa mara ya kwanza kuhusu ofa hii nilipata mshtuko na kusema dah, Vodacom imeleta tena bonge la ofa, kwa hakika ofa hii itaniunganisha na washabiki wangu, marafiki, familia na wafanyabiashara wengine”.

Aliongeza “Nitawaelezea washabiki wangu, familia na marafiki jinsi wanavyoweza kufanya maisha yao kuwa murua kupitia kampeni hii mpya kutoka Vodacom. Wanachotakiwa kufanya ili kujiunga na kufurahia ofa ya Ongea Bure Deilee ni rahisi tu, yaani ni kupiga simu *149*01#.

ONYESHO LA LADY IN RED 2016

Serikali yaimarisha Huduma ya Afya Mama na Mtoto

$
0
0
Na Raymond Mushumbusi-MAELEZO

Serikali inafanya jitihada kubwa kuimarisha upatikanaji wa Huduma za Uzazi salama katika mikoa mbalimbali kwa kujenga na kukarabati vyumba vya upasuaji,majengo ya Huduam za Afya ya Mama na Mtoto na nyumba za watumishi.

Akijibu swali la Mhe.Fatuma Hassan Taufiq Mbunge wa Viti Maalum (CCM) lililouliza serikali lini itamaliza jengo la kitengo  cha Afya ya Mama na Mtoto  lililopo katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma ili kunusuru maisha ya wakina mama wakati wa uzazi,Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Hamisi Andrea Kigwangalla amesema serikali imelipa kipaumbele suala la kupunguza vifo vya akina mama na Watoto vinavyotokana na uzazi kwa kuimarisha upatikanaji wa huduma za uzazi salama katika vituo vya kutolea huduma za Afya nchini.

” Kwa upande wa Hospitali ya Dodoma,Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI inakamilisha ujenzi wa Martenity Complex katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa na kazi hii iko katika hatua za mwisho za kukamilisha mifumo ya maji,kupaka rangi na kazi ndogo ndogo za nje ya jengo hilo na ununuzi wa samani.

“ Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto itashirikiana na na Ofisi ya Rais TAMISEMI kuhakikisha ujenzi huo unakamilika kwa wakati ili kuwezesha wananchi wa mkoa wa Dodoma na maeneo ya jirani kupata huduma bora za uzazi salama” Alisema Mhe.Kigwangalla.

Mhe. Hamisi Andrea Kigwangalla ameongeza kuwa Wizara yake ilifanya tathmini na kubaini mikoa ambayo ina idadi kubwa ya vifo vya akina mama na watoto vinavyotokana na uzazi na katika kuondoa tatizo hilo mradi wa kuharakisha kupunguza vifo vya akina mama wajawazito vinavyotokana na uzazi(Strengthening Martenity Mortality Reduction Program-SMMRP) na program hii ilielekezwa katika mikoa mbalimbali.

Ameitaja mikoa ambayo ilibaikika kuwa na idadi kubwa ya vifo vya akina mama na watoto vinavyotokana na uzazi kuwa ni Mtwara,Tabora na Mara na jitihada zinaendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma za uzazi salama katika mikoa mbalimbali kwa kujenga na kukarabati vyumba vya upasuaji,majengo ya Huduma za Afya ya mama na Mtoto na nyumba za watumishi ili kupunguza ama kuondoa kabisa tatizo hili.

Serikali kupitia Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto ikishirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI imejipanga kuboresha Huduma za Afya ili kuwapa wananchi unafuu wa kupata huduma hizo katika ubora unaotakiwa ikiwa pamoja kuhakikisha wananchi wanakuwa na Bima ya Afya zinazotumika katika madaraja yote ya vituo vya Afya.

KAMATI ZA MAAFA ZATAKIWA KUFANYA TATHIMINI ZENYE UHALISIA.

$
0
0
 Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa ya Wilaya Monduli, ambaye pia ni Mkuu wa wilaya hiyo, Francis Nyamiti akiongoza kikao cha kamati hiyo kujadili urejeshaji hali katika shule ya sekondari Edward Lowasa iliyopata maafa ya moto,, (wa kwanza kushoto) ni Mkurugenzi wa Idara ya uratibu maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, Brig. Jen. Mbazi Msuya, tarehe 4 Februari, 2016. 
 Mkurugenzi wa Idara ya uratibu maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, Brig. Jen. Mbazi Msuya, (wakwanza kushoto) pamoja na wajumbe wa Kamati ya maafa wilaya Monduli wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati hiyo, ambaye pia ni Mkuu wa wilaya hiyo, Francis Nyamiti (hayupo pichani) wakati wa kikao cha kamati hiyo kujadili urejeshaji hali katika shule ya sekondari Edward Lowasa iliyopata maafa ya moto tarehe 4 Februari, 2016. 

Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa Wilaya ya Monduli, ambaye pia ni Mkuu wa wilaya hiyo, Francis Nyamiti (Mbele wa kwanza kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati hiyo mara baada ya kikao cha kamati hiyo kujadili urejeshaji hali katika shule ya sekondari Edward Lowasa iliyopata maafa ya moto, (Mbele wa pili kushoto) ni Mkurugenzi wa Idara ya uratibu maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, Brig. Jen. Mbazi Msuya, tarehe 4 Februari, 2016. 
(Picha zote na Ofsi ya Waziri Mkuu).

Na. Mwandishi maalum.
Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu maafa imezitaka Kamati za Maafa za Mikoa, Wilaya na Vijiji zote nchini kufanya tathmini zenye uhalisia wa athari za maafa yanapotokea wakati wanapokuwa wanatekeleza jukumu hilo ambalo husaidia kuainisha hatua zinazopaswa kuchukuliwa katika Kuzuia/Kupunguza, Kujiandaa, Kukabili na Kurejesha hali baada ya maafa kutokea. 

Akiongea wakati alipokutana na Kamati ya maafa ya Wilaya ya Monduli Tarehe 4 Februari 2016, Mkurugenzi wa Idara ya uratibu maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, Brigedia Jenerali Mbazi Msuya amebainisha kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu imekuwa inapokea maombi ya misaada ya maafa ambayo tathmini zake huwa zimefanywa na Kamati za maafa ikiwa na aidha thamani kubwa au idadi kubwa kulingana na hali halisi ya athari ya maafa. 

“Ofisi ya Waziri Mkuu idara ya uratibu maafa inalojukumu la kuratibu shughuli za maafa katika hali ya kujiandaa, kuzuia, kukabili na kurudisha hali ya kawaida pindi maafa yanapotokea. Katika ngazi ya wilaya maafa yakiwashinda kuyakabili huomba msaada katika ngazi ya mkoa halikadhalika mkoa ukishindwa huomba msaada katika ngazi ya kitaifa. Mfano mzuri ni maombi ya chakula cha msaada tumekuwa tunapokea maombi ya maefu ya tani lakini wataalamu wetu wakifanya tathmini ya kujiridhisha maombi hayo huwa mamia ya tani na wananchi huridhika” amesema Brig. Jen. Msuya 

Msuya aliongeza kuwa kamati hazinabudi kuelewa kuwa nchi yetu inakumbwa na majanaga ya asili na yale ambayo husababishwa na wanadamu ambapo kimsingi serikali inalojukumu la kuzuia au kupunguza athari za maafa hayo. Hivyo uongezaji wa thamani na idadi ya mahitaji ya misaada ya maafa hufanya waathirika wengine kutopata misaada kwa wakati pamoja na iliyopungufu kwa kuwa serikali huanza kutafuta rasilimali za ziada ili kuweza kukabili na kurejesha hali ya maafa husika. 

“Kamati ya maafa ya wilaya hii imefanya tathimini kwa uhalisia kwa maafa ya moto yaliyotokea shule ya sekondari ya Edward Lowasa, uhalisia wa tathimini hii umewezesha Kamati ya wilaya kuweza kumudu kurejesha hali ya shule hii kwa kuwa hakuna uongezaji wa thamani wala idadi. Tukifanya hivi kwa kamati zote nchini katika ngazi zote tutaweza kuwa na menejimenti nzuri ya maafa nchini”, alisisitiza Brig. Jen. Msuya. 

Awali akiongea katika kikao hicho Mkuu wa Wilaya ya Monduli Franicis Nyamiti alifafanua kuwa mara baaada ya maafa ya moto kutokea katika shule ya sekondari Edward Lowasa, kamati ya maafa imekutana ili kuweza kujadili urejeshaji hali wa shule hiyo ambapo taarifa ya tathimini ya athari ya maafa iliyofanywa na Kamati ya Wilaya ndiyo iliyokuwa inawaongoza katika utekelezaji. 

“Ni dhahiri kuwa taarifa ya tathimini ikiwa na uhalisia mara nyingi idadi na thamani mnaweza kuimudu kwa kushirikiana na wadau wa maafa. Sisi tumewashirikisha wadau hao ambao tayariwamejitokeza kutupatia magodoro yote 72 yaliyoungua, mansanduku ya wanafunzi hao pamoja na mchanga wa ujenzi. .”alisisitiza Nyamiti.

Nyamiti alifafanua kuwa uhalisia wa tathmini ya athari za maafa hufanya urejeshaji hali kuwa kwa wakati kwani tayari mdau mwingine amaeshajitolea kubomoa mabaki ya jingo la bweni lililoungua tayari kwa kuanza ujenzi, aidha Mmiliki wa shule jirani ya Tumaini sekondari amejitolea bweni lake, vitanda na magondoro amabavyo wanafunzi hao watakuwa wanatumia wakati ujenzi ukikamilika.

Shule ya Sekondari ya Edward Lowasa inao wanafunzi 700 ambapo wanafunzi 72 ndio walioathirika na maafa ya moto yaliyotokea tarehe 27 Januari, 2016 kwa kuungua bweni la wanafunzi hao. Aidha kutokana na maafa hayo hakuna mwanafunzi aliyepoteza maisha wala kujeruhiwa . 

KINANA AANZA SHUGHULI MBALI MBALI ZA MAENDELEO KUELEKEA SIKU YA MAADHIMISHO YA MIAKA 39 YA KUZALIWA KWA CCM

$
0
0

Kaimu Katibu wa CCM Mkoa wa Singida Mary Maziku (kushoto)akisoma taarifa ya maandalizi ya maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ,Ndugu Kinana anatarajia kukagua na kushiriki miradi mbalimbali ya chama na ushiriki wa wananchi katika kujiletea maendeleo yao.
Wajumbe wa Kamati ya Siasa CCM mkoa wakisikiliza wakati Kaimu Katibu wa Mkoa Ndugu Mary Maziku akiwakilisha taarifa za maandalizi ya maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye ofisi za CCM mkoa wa Singida. 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisisitiza jambo alipokuwa akizungumza na kamati ya siasa ya CCM mkoa wa Singida mara baada ya kupokea taarifa za maandalizi ya maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupaka rangi jengo la CCM mkoa wa Singida ikiwa sehemu ya maandalizi ya maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM.

PICHA NA MICHUZI JR-MMG-SINGIDA

WATENDAJI WA HALMASHAURI KINDONDONI WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA RUSHWA

$
0
0
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Kinondoni, tarehe 02/02/2016 imewafikisha washitakiwa wafuatao mahakamani:-Bw.Bryceson Kajigiri Mwangoma mwenye umri wa miaka 54, Bw.Abel Sebabil Slaa mwenye umri wa miaka 44 na Bw.Bernard Thomas Mkude mwenye umri wa miaka 42 kwa kuiibia Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni  Tsh.33,681,780.

Washitakiwa hawa Bw.Mwangoma na Bw.Slaa wakiwa Maafisa watendaji wa Kata ya Kimara kwa vipindi tofauti, na Bw.Mkude akiwa Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Kimara Baruti walitenda makosa kinyume na kifungu cha 31, 22, 28 (1) 3 vya sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11 ya mwaka 2007 pamoja na kifungu cha 258, 270 vya sheria ya Kanuni za Adhabu. Washitakiwa wanadaiwa kutumia madaraka yao vibaya na kujipatia manufaa kwa kufanya wizi wa fedha hizo zilizokua zimewekwa na Wananchi katika akaunti ya Urasimishaji Ardhi kata ya Kimara iliyopo benki ya Wananchi wa Dar – es- Salaam (DCB) tawi la Magomeni kwa ajili ya kupimiwa maeneo yao.

Mshitakiwa wa kwanza Bw. Mwangoma akiwa mtendaji wa kata kwa kipindi cha tarehe 01/04/2011 hadi tarehe 30/11/2011 kwa kushirikiana na Mshitakiwa wa tatu Bw.Mkude ambaye ni mshitakiwa wa pili walitumia madaraka yao kwa kushirikiana  kuiba kiasi cha Tsh. 24,764,280. Bw. Slaa akiwa mtendaji kata kwa kipindi cha tarehe 01/06/2013 hadi tarehe 31/01/2014 kwa kushirikiana na Bw.Mkude waliiba kiasi cha Tsh. 8,917,500.

Washitakiwa walifikishwa Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni na kufunguliwa kesi namba 51/2016 inayosimamiwa na Mhe. Hakimu Mushi. Watuhumiwa wako nje kwa dhamana na kesi imepangwa kusikilizwa tena tarehe 16/02/2016.


IMETOLEWA NA   MKUU WA TAKUKURU (M) KINONDONI
BENN LINCOLIN
04/02/2016

GEITA MACHI 26 TAMASHA LA PASAKA 2016

$
0
0
KAMATI ya maandalizi ya Tamasha la Pasaka 2016 limeutangaza mkoa wa Geita kuanza na Tamasha la Pasaka mwaka huu kabla ya Mwanza.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi, Alex Msama Machi 27, tamasha litahamia jijini Mwanza.

Msama alisema Kamati yake bado inaendelea na mchakato wa kufanikisha tamasha la Pasaka ambalo mwaka huu litakuwa na miaka iliyopita.“Geita ni mkoa ambao ulionesha kulihitaji Tamasha la Pasaka kama ilivyokuwa Mwanza ndipo tulipoona kwamba tuanze na mkoa huo kwani maombi yalikuwa ni mengi zaidi,” alisema Msama. 

Aidha Msama alisema wamesikia kilio cha wakazi wa Geita baada ya maombi yao ya muda mrefu, tamasha litafanyikia mkoani humo ikiwa ni heshima yao.

“Wakazi wa Geita walipokee kwani litashirikisha idadi kubwa ya waimbaji wa ndani ni shereje, raha, vifijo,” alisema Msama.

MPOKI ATEMBELEA STUDIO ZA EFM LEO JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0
Mchekeshaji wa orijino Komedi alimaarufu kama MPOKI ametembelea kituo cha radio cha Efm 93.7 katika ofisi zao na kuonana na wakurugenzi pamoja na watangazaji wake kwa lengo la kubadilishana mawazo sambamba na kuona jinsi gani kituo hicho kinavyoendesha shughuli zake za utangazaji.
Mchekeshaji wa orijino Komedi alimaarufu kama MPOKIakiteta jambo na mkurugenzi mkuu wa Efm radio Francis Siza leo asubuhi.
Akiwa pamoja na watangaziji wa kipindi cha Sports HQ (kulia) Maulidi Kitenge na (kushoto) Ibrahimu Masoud (Maesro)
Picha ya pamoja na mtangazaji wa kipindi cha UHONDO Dina Marios na Mchekeshaji wa orijino Komedi alimaarufu kama MPOKI.

SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR IMEAMUA KUANZISHA UTARATIBU WA KUTUMIA NJIA YA UPANDE MMOJA.

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mjimkongwe Issa Said Makarani akizungumza na waandishi wa habari pichani hawapo juu ya kutumia njia moja ya kuingilia Mjimkongwe kuanzia tarehe 8/2/2016.
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Mkadam Khamis Mkadam akizungumzia namna Jeshi la Polisi lilivyojipanga kuhakikisha Wananchi wananchi wanafuata sheria zitakazowekwa na Mamlaka ya Mjimkongwe kuanzia Februari 8 mwaka huu.

Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Mji Mkongwe Issa Said Makarani akijibu masuala ya waandishi wa habari.

Mwashungi Tahir Maelezo Zanzibar.
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imeamua kuanzisha utaratibu wa kutumia njia ya upande mmoja kubwa ya kuingia Mji Mkongwe kuanzia tarehe nane mwezi huu ili kupunguza usumbufu unaowapata wageni na watumiaji wengine wa Mji huo.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mamlaka ya Mji Mkongwe Forodhani, Mkurugenzi Mkuu Issa Saidi Makarani amesema uwamuzi huo umefikiwa kutokana na ongezeko kubwa la vyombo vya moto linalohatarisha usalama wa mji huo ambao ni urithi wa kimataifa.

Amesema mji wa Zanzibar umekuwa ukipokea watalii na wageni wengi na wakati wa matembezi yao wamekuwa wakipata usumbufu mkubwa kutokana na kuongezeka vyombo hivyo.

Ameongeza kuwa ongezeko hilo la magari pia limepelekea athari kubwa kwenye majengo kutokana na mtikisiko mkubwa wa magari yenye uzito mkubwa na kubomoa baadhi ya majengo ya mji.

“Watumiaji wa Mji huu na wanaofika kila siku kwa shughuli zao za kimaisha wanapata usumbufu na kubwa zaidi wingi wa vyombo hivyo tayari vimesababisha athari ya baadhi ya majengo,”alisisitiza Mkurugenzi Makarani.

Amesema njia kubwa ya ndani ya kuingilia Mji Mkongwe itaanzia Vuga kupitia Afrika House , Hoteli ya Serena , Wizara ya Ardhi , Makaazi, Maji na Nishati , Benki ya NBC , Jengo La zamani la Watoto Forodhani , njia ya Mizingani hadi kuishia lango kuu la kuingia bandarini Malindi.

Amezitaja njia zitakazofungwa kuanzia tarehe nane kuwa ni ile inayoanzia jengo la Wizara ya zamani ya Mawasiliano na Uchukuzi kupitia Kiponda na kumalizikia Darajani, njia inayoingia Mkunazini na kumalizikia Skuli ya Sunni Madrassa na njia inyozunguka nyuma ya jengo la sinema ya zamani Majestic.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Mkadam Khamis amesaema lengo la kuweka zoezi hilo ni kuweka usalama kwa wenye magari na wanaokwenda kwa miguu.

Amewaomba wananchi kuunga mkono zoezi hilo ambalo litaweka mji Mkongwe katika hadhi na ubora wake uliopelekea kuwa miongoni mwa Miji ya Urithi wa kimataifa duniani.

Mkurugenzi wa Baraza la Manispaaa Aboud Hassan Serenge amewataka wananchi wanaoishi katika maeneo ya Mji Mkongwe kubadilika na kuanzisha utamaduni wa kuimarisha suala la usafi.

MAADHIMISHO YA MIAKA 39 YA CCM YAPAMBA MOTO MKOANI SINGIDA

$
0
0
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa maabara katika shule ya Sekondari  ya Unyianga,kata ya Unyianga mkoani Singida.Shule hiyo mpya yenye madarasa manne ikiendelea kujengwa kwa nguvu za wanannchi.
Sehemu ya jengo la ujenzi wa maabara ukiendelea kwa nguvu za Wananchi
Badhi ya Wananchi waliokuwa wakishiriki ujenzi wa maabara hiyo,wakielekea kumsikiliza Katibu MKuu wa chama cha CCM Ndugu Kinana aliyefika katika shule hiyo ya sekondari ya Unyianga kushiriki ujenzi na kuwahimiza wananchi kushiriki kujenga maendeleo yao.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akiwa akiongozwa na mwenye shamba la Mtama Bwa.Elisha Abdallah sambamba na Mbunge wa jimbo la Singida Mjini Mussa Ramadhani alipokwenda kushiriki palizi la mkulima huyo wa mfano katika kata ya Mtamaa,mkoani Singida
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana pichani kati akisukuma jembe la Plau linalokokotwa na N'gombe (kama aonekanavyo pichani) ikiwa sehemu ya kushiriki palizi katika shamba  hilo la Mtama lenye ukubwa wa Ekari moja na nusu  lililopo katika kata ya Mtama mkoani humo.Ndugu Kinana na ujumbe wake yuko mkoani Singida kwenye maandalizi ya sherehe za kuadhimishwa miaka 39 ya CCM,zinazotarajiwa kufanyika Februari 6 katika uwanja wa Namfua mkoani humo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akitoa ufafanuzi kwa Wajasiria Mali hao mara baada ya kusikiliza kero na malalamiko mbalimbali ambayo yanatakiwa kufanyiwa kazi haraka iwezekanavyo,ili kuendana kasi ya Rais Dkt Joseph Magufuli ya kuwahimiza wananchi kufanya kazi kwa kujituma kupitia kauli yake ya Hapa kazi Tu.
 Katibu Mku wa CCM Ndugu Kinana akiwa katika ukumbi wa ofisi za chama mkoa akisikiliza kero na mambo mbalimbali ya Wananchi ikiwemo kuyafanyia kazi,Ndugu Kinana amekutana na wajasiriamali (Mama Lishe,Boda boda,Wauza Mitumba na Wafanyabiashara nyingine ndogo ndogo.

MADA MAUGO NA ABDALLAH PAZI KUONESHANA UBABE UWANJA WA NDANI WA TAIFA SIKU YA PASAKA

$
0
0
Mabondia Mada Maugo (kushoto) na Abdallah Pazi wakitunishiana misuli baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga siku ya sikukuu ya pasaka katika ukumbi wa uwanja wa ndani wa Taifa jijini Dar es salaam. katikati ni Mratibu wa Mpambano huo kocha wa masumbwi nchini, Rajabu Mhamila 'Super D'.
Mratibu wa mpambano wa masumbwi, Rajabu Mhamila 'Super D' (katikati) akiwa na mabondia Mada Maugo (kushoto) na Abdallah Pazi wakati wa utambulisho wa mpambano wao utakaofanyika siku ya sikukuu ya Pasaka kwenye uwanja wa ndani wa Taifa.
Bondia Mada Maugo akikabidhiwa mkataba wake na mratibu wa mpambano wa masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D' kati yake na Abdallah Pazi mpambano utakaofanyika siku ya sikukuu ya Pasaka katika uwanja wa ndani wa Taifa.
Bondia Abdallah Pazi kushoto akipokea mkataba wake kutoka kwa mratibu wa mpambano uho Rajabu Mhamila 'Super D' baada ya kusaini kwa ajili ya kupigana na Mada Maugo siku ya sikukuu ya Pasaka katika uwanja wa ndani wa taifa. Picha na SUPER D BOXING NEWS

AfDB approves US $16.5 million for Institutional Support Project for Good Governance in Tanzania

$
0
0
The Board of Directors of the African Development Bank (AfDB) approved on Wednesday, February 3 in Abidjan a loan of US $16.5 million to finance the Tanzania Institutional Support Project for Good Governance (ISPGG III). The objective of this project is to support the Government of Tanzania in promoting inclusive growth and macroeconomic stability by enhancing economic and financial governance through more effective public financial management and improved business environment.

By supporting the Government of Tanzania’s Public Financial Management (PFM) reform agenda, this project will contribute to efforts geared towards enhancing capacity, and improving accountability, transparency and integrity in the management of public resources. 

The project will also contribute to an improvement in the business enabling environment, by strengthening capacity to fight corruption, the streamlining of business registration and licensing processes and operationalization of the public-private partnership (PPP) framework.

During the Board presentation, the Bank’s Director of Governance, Economic and Financial Management Department, Jacob Mukete, noted that “the project builds upon Bank-supported capacity building and PFM reforms in Tanzania, and complements the ongoing Power Sector Reform and Governance Support Programme IV and other interventions of development partners.”

The Bank has provided support to Tanzania’s governance institutions over the years through two preceding interventions (ISPGG I and II). These have contributed to major improvements in public financial management, particularly in the areas of public procurement, anti-corruption and external audit. This follow-up operation, approved by the Board on Wednesday, builds on those achievements and contributes to preparing Tanzania to meet new and emerging challenges in public sector management.

The approval of this project comes at a time when the Government of Tanzania is demonstrating renewed commitment to transparency, accountability and effective public service delivery, under the leadership of President John Magufuli. Since taking office just three months ago, the new President has declared war on corruption and is taking bold steps to enhance the performance of the public sector. 

This project is therefore very timely. Together with the Bank’s other interventions, including the ongoing budget support operation, the project will contribute to enhancing economic management capacity and ultimately improve the quality of life of the people of Tanzania.

THE 7TH PROF. HUBERT KAIRUKI MEMORIAL LECTURE

WAMILIKI WALIOBADILI MATUMIZI YA ARDHI KINYUME CHA SHERIA KUTOZWA FAINI

$
0
0
Na Fatma Salum (MAELEZO)

Serikali inatarajia kutekeleza zoezi la utozaji faini kwa wamiliki waliobadili matumizi ya ardhi kinyume cha sheria kwa kuzingatia Sheria ya Ardhi namba 4 ya mwaka 1999 na Sheria ya Mipango Miji namba 8 ya mwaka 2007.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Kitengo cha Kodi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw. Denis Rugemalila wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mpango kazi wa utekelezaji wa zoezi hilo.

Akifafanua kuhusu zoezi hilo Bw. Rugemalila amesema kuwa kuanzia Februari 8, 2016 Wizara ya Ardhi kwa kushirikiana na Halmashauri za Temeke, Kinondoni na Ilala itaanza operesheni jijini Dar es Salaam ya kukagua na kutoa adhabu ikiwemo kutozwa faini kwa waendelezaji wote waliobadili matumizi ya Ardhi na kuongeza majengo kinyume cha sheria.

Aidha Bw. Rugemalila ameeleza kuwa licha ya tozo za faini hatua nyingine stahiki zitachukuliwa dhidi ya maendelezo ya ardhi ambayo yamefanyika bila vibali kama vile viwanda, vituo vya mafuta na shughuli nyingine zinazoathiri mazingira na kuleta kero kwa jamii.

“Endapo kutabainika kuwepo kwa vibali vinavyotia mashaka, vitaainishwa ili vifanyiwe uhakiki kwa ajili ya kuchukua hatua stahiki dhidi ya wahusika.” Alisema Rugemalila.

Sanjari na zoezi hilo pia wizara ya Ardhi inaendelea na zoezi la usambazaji wa hati za madai kwa wadaiwa sugu wa kodi ya ardhi na watakaokaidi watafikishwa mahakamani pamoja na kushika mali zao, kufilisi au kufutiwa kwa miliki zao.

“Tunawaomba wamiliki wote wa ardhi nchini kulipa kodi ya pango la ardhi na kutoa ushirikiano kwa maafisa wetu watakapokuwa wanapita kufanya ukaguzi” alisema Rugemalila.

Serikali imeamua kuendesha zoezi la utozaji faini baada ya kubaini kuwa kuna baadhi ya waendelezaji wa ardhi wamekuwa wakibadili matumizi ya ardhi kiholela na kusababisha kero kwa umma, pia baadhi ya waendelezaji wanaongeza majengo tofauti na yale yaliyoidhinishwa kujengwa katika kiwanja husika.
Mkuu wa Kitengo cha Kodi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw. Denis Rugemalila akiwaeleza waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu mpango kazi wa utekelezaji wa mkakati wa utozaji faini kwa wamiliki waliobadili matumizi ya ardhi kinyume cha sheria. Kushoto ni Afisa Sheria Mwandamizi Bi. Martha Isaga.

MUDHIRI AJA NA KITABU CHA MWELE BIN TAABAN.

$
0
0
 Aliekuwa Mbunge wa Mchinga,Mudhihiri Mudhihiri Akizungumza na waandishi wa habari hawapo picha juu ya kitabu cha ‘‘Mwele Bin Taaban’’ ambacho kina ujumbe mbalimbali.leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Abdallah Makumbila aka Muhogo Mchungu. 
 .Mwana muziki Mrisho Mpoto akifafanua jambo kushoto ni Abdallah Makumbila aka Muhogo, leo jijini Dar es Salaam. 
Waandishi wa habari wakimsikiliza Aliekuwa Mbunge wa Mchinga,Mudhihiri Mudhihiri, leo jijini Dar es Salaam. 
(Picha na Emmanuel Massaka wa Globul ya Jamii).

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
ALIYEKUWA Mbunge wa Mchinga, Mudhihil Mudhihil ametunga kitabu cha ‘‘Mwele Bin Taaban’’ ambacho kina ujumbe mbalimbali. 

Mudhihil ametunga kitabu hicho kwa kushirikisha watu mahiri ikiwa lengo ya kukuza Kiswahili kuweza kutumika sehemu ya ajira. 

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mudhihil amesema kuwa kitabu hicho kinaweza kutumika katika mtaala wa shule za Sekondari kwa kudato cha tatu na sita na hadi vyuo vikuu. 

Amesema kuwa katika Dibaji ya kitabu hicho ameandika Waziri wa Katiba na Sheria Dk. Harrison Mwakyembe ambaye ana ujumbe wake katika kitabu hicho. 

Mudhihiri amesema kuwa watanzania hawapendi kusoma na kuwataka kusoma kutafanya wajue vitu vingi na kujua nchi yao. 

Maalim Seif azungumza na viongozi wa CUF Kisiwani Pemba

$
0
0
Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad, akizungumza na viongozi wa CUF katika viwanja vya Nngoma hazingwa Chake Kisiwani Pemba.
Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui, akizungumza na viongozi wa CUF katika viwanja vya Nngoma hazingwa Chake Kisiwani Pemba.
Baadhi ya Viongozi wa Wilaya na Majimbo kisiwani Pemba wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad. (Picha na Salmin Said, OMKR).
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live




Latest Images