Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live

C-SEMA , TAJOC WAJADILI ULINZI MTOTO

$
0
0
 Afisa Mtendaji Mkuu wa C-SEMA, Kiiya Kiiya akizungumza na Waandishi wa Habari za Watoto (TAJOC) na Wadau Watunga Sera katika kampeni Nijali Mtoto wa Tanzania iliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
Mshauri Mwandamizi wa Kituo cha Huduma ya Simu kwa Mtoto wa C-SEMA, Thelma Dhaje akizungumza na Waandishi wa Habari za Watoto (TAJOC) na Wadau Watunga Sera katika kampeni Nijali Mtoto wa Tanzania iliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
Wadau wa Watoto wakiwa katika picha ya pamoja jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
WATOTO  wametakiwa kupewa ulinzi katika jamii katika kuweza kuwa na kizazi kinachojiamini na kufanya watoto kuwa wanajiamni ni kuondokana na mila potofu ambazo zinawakandamiza ikiwemo ukeketaji kwa watoto wa kike.

Akizungumza katika mkutano na Waandishi wa Habari za Watoto (TAJOC) na Wadau Watunga Sera katika kampeni Nijali Mtoto wa Tanzania, Mkurugenzi wa C-SEMA, Michael Kehongoh amesema ulinzi wa watoto unatakiwa kupewa kupaumbele ikiwemo kutenga bajeti ya watoto.

Kehongoh amesema katika mazingira yaliyopo mtoto anatakiwa ulinzi wa kumuwezeha kuishi ikiwa ni pamoja na serikali kuunda timu za ulinzi ambapo ni Halmashauri chache ambazo zimeweza kufanya hivyo.
Amesema maafisa ustawi wa jamii ni kiungo katika usimamizi wa watoto kwa serikali kuweka kipaumbele cha bajeti ya kuweza kutekeleza majukumu yao.

Kehongoh Maafisa ustawi wa jamii kwa nchi zilizoendelea zimeweka kipaumbele kutokana na kazi wanazozifanya zinahusiana moja kwa moja na jamii na watu wengine wanatakiwa kupata taarifa kwa watu hao.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa TAJOC, Edward Qorro amesema waandishi kuhabarisha masuala yanayohusu watoto ni jukumu letu hivyo kunahitaji ushirikiano katika kupeana taarifa juu ya ulinzi wa watoto.

Amesema kazi ambayo imekuwa kikwazo ni kuwafikia watoto pale inapotokea tatizo hapo hapo kutokana na changamoto ya rasilimali fedha.

WAZIRI MKUU MAJALIWA AHUTUBIA- MANDAWA

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akimtambulishasha diwani wa kata ya Mandawa kwa tiketi ya CUF, Said Abdallah `Nachinga na kuahidi kuwa atashirikiana nae kwa karibu katika kazi za kuwaletea maendeleo wananchi wa kata hiyo bila kujali tofauti za vyama. Alikuwa ktika mkutano wa hadhara kwenye kijiji cha Mandawa Desemba 22, 2015.   
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wananchi wa kijiji cha Mandawa wilayani Ruangwa kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara kijijini hapo desemba 22, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Mkesha wa kuiombea amani Tanzania.

$
0
0

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Makanisa ya Kipentekoste (Tanzania Fellowship of Churches) Askofu Godfrey Malassy (kushoto) akiongea na waandishi wa Habari (hawapo pichani) leo 22 Desemba, katika Ukumbi wa Idara ya Habari jijini Dar es Salaam kuhusu maandalizi ya Mkesha Mkubwa wa Kitaifa wa kuliombea Taifa pamoja na dua maaum ya kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Joseph Magufuli ambaye anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika dua hiyo. Kulia ni Mwanakamati wa Jumuiya hiyo, Mchungaji Olivia Mallonga.
Mwanakamati wa Jumuiya ya Makanisa ya Kipentekoste (Tanzania Fellowship of Churches) Mchungaji Mchungaji Olivia Mallonga (kulia) akichangia mada wakati wa mkutano na waandishi wa Habari (hawapo pichani) leo 22 Desemba, katika Ukumbi wa Idara ya Habari jijini Dar es Salaam kuhusu maandalizi ya Mkesha Mkubwa wa Kitaifa wa kuliombea Taifa pamoja na dua maaum ya kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Joseph Magufuli ambaye anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika dua hiyo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Makanisa hayo Askofu Godfrey Malassy.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Makanisa ya Kipentekoste (Tanzania Fellowship of Churches) Askofu Godfrey Malassy akionyesha kitabu mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kilichozinduliwa na Jumuiya ya Makanisa hayo kinachohusu siri ya amani kwa taifa.



WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AKUTANA NA ASKOFU NGONYANI WA LINDI

$
0
0
 Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akisalimiana na Askofu wa Jimbo Katoliki la LindI Mhashamu, Anthony Ngonyani kwenye Ikulu ndogo ya Ruangwa Desemba 22, 2015.
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi Mhashamu Anthony Ngonyani kwenye Ikulu ndogo ya Ruangwa Desemba 22, 2015.
(Picha na Ofisi ya Wazri Mkuu)

ABIRIA WAKIWA STENDI KUU YA MABASI YA KWENDA MIKOANI (UBUNGO)

$
0
0
Abilia wakiwa katika Stendi Kuu ya mabasi ya kwenda mikoani Ubungo jijini Dar es Salaam wakisubiria usafiri wa kuelekea Mikoa mbalimbali, leo.

Abilia wakiwa katika Stendi Kuu ya mabasi ya kwenda mikoani Ubungo jijini Dar es Salaam, wakiimarisha usalama wa malizao, leo.
Abilia wakiwa wamejipumzisha chini ya mti katika Stendi Kuu ya mabasi ya kwenda mikoani Ubungo jijini Dar es Salaam leo.
Picha na Emmanue Massaka wa Globu ya jamii.

Naibu Spika wa Bunge Mhe Dkt Tulia Ackson akutana na Rais wa Baraza la Maseneta la Jamhuri wa Burundi Mhe Reverien Ndikuriyo

$
0
0
Naibu Spika wa Bunge Mhe Dkt Tulia Ackson akisalimiana na Rais wa Baraza la Maseneta la Jamhuri wa Burundi Mhe Reverien Ndikuriyo aliyemtembelea leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Naibu Spika wa Bunge Mhe Dkt Tulia Ackson akisalimiana na Balozi wa Rwanda nchini Mhe Mhe. Prefere Ndayishimiye aliyesimama katikati ni Rais wa Baraza la Maseneta la Jamhuri wa Burundi Mhe Reverien Ndikuriyo.
Naibu Spika wa Bunge Mhe Dkt Tulia Ackson akimsikiliza kwa umakini Rais wa Baraza la Maseneta la Jamhuri wa Burundi Mhe Reverien Ndikuriyo alipofanya mazungumzo naye ofisi kwake jijini Dar es Salaam.
Naibu Spika wa Bunge Mhe Dkt Tulia Ackson (aliyeko katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Burundi nchini Mhe. Prefere Ndayishimiye (kulia), Rais wa na Rais wa Baraza la Maseneta la Jamhuri wa Burundi Mhe Reverien Ndikuriyo (kushoto).

HENNESSY'S 250 YEARS EXHIBITION AT OASIS BAR MASAKI, DAR ES SALAAM

$
0
0
The owner of Oasis Bar and Lounge Nuru Mosha clarifying something to journalists at the The Hennessy 250's  Exhibitions.


Some pictures related to Hennessy

The Amazing Hennessy bottle
Some paints related to Hennessy 
The event was accompanied by live music

The Hennessy' s bar at Oasis Masaki
*************
By Staff Reporter
The four-day exhibition to mark the 250 years of Hennessy was launched in Dar es Salaam this Monday,  at Oasis Bar, Masaki and it has attracted many people including artists, socialites as well as other arts stakeholders.

The event was accompanied by a live music performance and involved artwork and limited edition bottles done by different artists, profiling the history and heritage of Hennessy.
Speaking with journalists at the Oasis Bar on Monday where the exhibition is taking place, the owner of Oasis Bar and Lounge Nuru Mosha clarified that, The Hennessy 250 Exhibitionis a multidisciplinary event in which the exhibition showcases the treasures of its heritage.
He added that it reflects the vision that Hennessy has always had of itself and the world around it, a taste for the avant-garde and the pull of distant horizons.

" This hybrid cultural event and exhibition at Oasis Wine Bar with accompanying music and live performances, is a reflection of the unique bond that Hennessy has always maintained with the art world" he added.
He also added that since the Hennessy family were early patrons of the arts and have always been close to artists themselves, the exhibition would of course involve the arts.
"This has given us reflections of the longevity and permanence of its products in limited editions with prestigious signatures and even here in Tanzania. Hennessy is very proud to support artistic activities" he said.

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN, AKUTANA NA MABALOZI WA KUWAIT NA RWANDA OFISINI KWAKE IKULU DAR

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Balozi wa Rwanda nchini Tanzania, Mhe. Eugene Kayihura, alipofika Ofisini kwake Ikulu jini Dar es Salaam, leo Desemba 22, 2015 kwa mazungumzo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Mhe. Jasem Al Najem, alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Desemba 22, 2015 kwa mazungumzo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akipokea zawadi kutoka kwa Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Mhe. Jasem Al Najem, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam,leo Desemba 22, 2015.


KUMBUKUMBU

$
0
0
LUTENI KANALI (MSTAAFU) WILLY JOHN MASOI. 

Sekunde, dakika, saa, siku, wiki, miezi imepita na leo ni mwaka tangu usiku ule ulipoitwa na Bwana Mungu na kutuachia uchungu usioelezeka. Pengo ulilotuachia kamwe haliwezi kuzibika bali tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwani kazi yake haina makosa na upendo uliotuachia ndio unatuwezesha kusonga mbele. 
Tunaendelea kumuomba Mwenyezi Mungu akupumzishe kwa amani hadi hapo tutakapokutana kwani sisi wote ni wapitaji katika ulimwengu huu. 

Tumebaki na kumbukumbu za imani yako iliyotukuka, mapenzi yako ya dhati, wema na ukarimu wako ambao hatutasahau daima. Tangu ile siku Bwana Mungu alipokuita kwenye ufalme wake tumekuwa na wakati mgumu kwa kuwa maisha yetu sasa hatuwezi kuyafananisha hata chembe na wakati tulipokuwa tunaisikia sauti yako, tunafurahi pamoja na kushauriana juu ya mambo mbali mbali ya familia zetu. 
Unakumbukwa na mke wako mpendwa Mary Salome (Ndewioshindo), watoto, wakwe zako, wadogo zako, wajukuu, ndugu pamoja na majirani zako wote. 
Raha ya milele umpe, ee Bwana, na mwanga wa milele uingazie roho ya marehemu Luteni Kanali (Mstaafu) Willy John" Masoi. Apumzike kwa amani" Amina
“NIMEVIPIGA VITA VILIVYO VIZURI, MWENDO NIMEUMALIZA, IMANI NIMEILINDA” 
(2 Timotheo 4:7)

RAIS MAGUFULI AFANYA MAZUNGUMZO NA SPIKA WA BARAZA LA SENETI NA MJUMBE MAALUM WA RAIS WA JAMHURI YA BURUNDI,PIERRE NKURUNZINZA

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Ndugu Reverien Ndikuriyo, Spika wa Seneti na Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Burundi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Ndugu Reverien Ndikuriyo, Spika wa Seneti na Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Burundi.

 PICHA NA IKULU.

DIRA YA DUNIA JUMANNE 22.12.2015

MWAKILISHI MKAZI WA UNHCR AMTEMBELEA WAZIRI KITWANGA, WAZIRI ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA NIDA JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kushoto) akimkaribisha ofisini kwake Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), Joyce Mends-Cole, kwa ajili ya kufanya naye mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali ya Wakimbizi nchini. 
 
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kulia) akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), Joyce Mends-Cole, kuhusu masuala mbalimbali ya Wakimbizi. Mazungumzo hayo yalifanyika katika ofisi ya Waziri Kitwanga, jijini Dar es Salaam
 Chini Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), Joyce Mends-Cole (wapili kushoto) akizungumza na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati), kuhusu masuala mbalimbali ya Wakimbizi. Mazungumzo hayo yalifanyika katika ofisi ya Waziri Kitwanga, jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi, Harrison Mseke, na kushoto ni Naibu Mwakilishi Mkazi wa UNHCR, Robert Tibagwa.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga akiwasili Makao Makuu ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Kinondoni jijini Dar es Salaam na kupokewa na Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dickson Maimu (kushoto). Waziri Kitwanga alifanya ziara ya kikazi katika ofisi hizo kwa lengo la kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanywa na mamlaka hiyo. 
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dickson Maimu akimfafanulia jambo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) wakati Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya NIDA, Kinondoni, jijini Dar es Salaam leo.  Watano kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abduwakil, wanne kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, John Mngodo. 

 Afisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Brenda Joshua akimfafanulia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (aliyevaa tai), jinsi wanavyosajili taarifa mbalimbali za waombaji wa vitambulisho. Waziri Kitwanga alitembelea Kituo hicho cha Usajili na kujifunza kazi mbalimbali zinazofanywa na NIDA, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil na kulia kwa Abdulwakil ni Naibu Katibu Mkuu, John Mngodo. 
Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.



MFUMO WA KIELETRONIKI KURATIBU SHUGHULI ZA SERIKALI - MH. MHAGAMA

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu), Jenista Mhagama (Mb), akisisitiza umuhimu wa kutafuta majibu ya maswali kwa wakati yaliyoelekezwa Serikalini kipindi cha Bunge wakati alipokutana na Maafisa wa Bunge wa Wizara za Tanzania Bara leo, Tarehe 23 Desemba, 2015, Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya maafisa Bunge kutoka Wizara za Tanzania Bara wakiendelea na uchambuzi wa maswali yaliyoelekezwa serikalini kipindi cha Bunge leo, Tarehe 23 Desemba, 2015, Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Idara ya Bunge na Siasa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Yona Mwakilembe, akieleza jinsi maafisa Bunge wa Wizara za Tanzania Bara walivyojipanga kutoa majibu kwa wakati maswali yaliyoelekezwa serikalini kipindi cha Bunge leo, Tarehe 22 Desemba, 2015, Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya maafisa Bunge kutoka Wizara za Tanzania Bara wakiendelea kufuatilia maelekezo ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu), Jenista Mhagama (Mb), alipokutana nao wakati wa uchambuzi wa maswali yaliyoelekezwa serikalini kipindi cha Bunge leo, Tarehe 23 Desemba, 2015, Jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

SHIRIKA LA NDEGE LA ETIHAD LAZINDUA MFUMO MPYA WA KISASA WA USIMAMIZI WA MIZIGO KWENYE VIWANJA VYA NDEGE

$
0
0
SHIRIKA la ndege la Etihad ambalo ndio shirika rasmi la nchi ya Falme za kiarabu, leo hii limetangaza makubaliano na kampuni ya Luggage Logistics kuboresha mfumo mzima wa usimamizi wa mizigo katika viwanja vake vya ndege dunia nzima.


Kupitia mfumo wa kisasa wa Baggage Management System (BMS) unaosimamiwa na kampuni ya Luggage Logistics, shirika la ndege la Etihad litaweza kuboresha usimamizi ikiwemo kusafirisha mizigo ya wasafiri kwa wakati. Mfumo huo pia utawezesha kufuatilia kwa urahisi mizigo iliypotea njiani dunia nzima.

Mfumo wa BMS utahusisha ratiba za ndege, taarifa za wasafiri pamoja na mifumo ya udihibiti safari zote ka pamoja. Hii itasaidia kuongeza kasi taratibu za kutambua mizigo ya abiria na kisha kuhamisha mizigo toka kwenye ndege hadi uwanja wa ndege na hatimaye kwenda kwenye ndege ya kuunganisha safari husika, ikisaidia safari kutochelewa.

Mfumo huu umeunganishwa katika kituo kimoja cha udhibiti ambapo taarifa zote za mizigo kutoka vyanzo mbalimbali hutunzwa. Taarifa hizi zinaweza kusambazwa haraka na uwepesi baina ya vitengo husika dunia nzima.

Geert W. Boven, Makamu rais wa Huduma za viwanja vya ndege kutoka Etihad, alisema: “Ushirikiano na kampuni ya Luggage Logistics kutaongeza ufanisi zaidi katika kutambua, kusimamia na kusafirisha mizigo ya abiria duniani kote kwenye viwanja vyetu tukianzia na hapa Abu Dhabi. 

Mfumo mpya huu utasaidia kuboresha huduma kwa abiria kwa kupunguza upotevu wa mizigo, kupunguza idadi ya safari zinazochelewa juu ya kupotea kwa mizigo pamoja na kuongeza ufanisi wa huduma zetu za uwanja wa ndege”

Adam Dalby, Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Luggage Logistics, alisema “Tunayofuraha kushirikiana na shirika la ndege la Etihad, shirika ambalo tupo pamoja katika kutambua umuhimu wa uvumbuzi na huduma bora. Kupitia mfumo huu wa kisasa wa BMS, taarifa za papo hapo hupatikana na hutumika kuhakikisha mizigo ya abiria inasimamiwa kwa ufanisi zaidi safari nzima”


Shirika la ndege la Etihad lilichagua mfumo wa BMS kwani unakidhi mahitaji na vigezo vyote vya usimamizi mizigo, ikiwemo ICAO Annex 17 pamoja na maazimio ya IATA, mfumo huu unaweza kuunganishwa na mitambo ya shirika hili la ndege bila ugumu wowote pia. Suluhisho hili limewiana na uendeshaji na mahitaji ya miundombinu ya Shirika la ndege nay ale ya kituo cha Abu Dhabi.

UDHAIFU WA USIMAMIZI WA MIRADI MBALIMBALI NI CHANGAMOTO KATIKA KULETA KASI YA MAENDELEO NDANI YA JAMII

$
0
0
Tanzania ya leo, imepitia mabadiliko mengi yanayogusa kila sekta tangu ilipojikomboa na kuwa nchi huru baada miaka 53 ya utawala wa kikoloni. Kwa mfano, katika kipindi hicho hadi sasa, nchi imeshuhudia kuimarika kwa huduma mbalimbali za kijamii. Kwa uchache, huduma hizi ni pamoja na afya, elimu, demokrasia, utalii, viwanda na miundombinu mbalimbali. 

 Katika sekta ya elimu, ongezeko kubwa la shule kuanzia ngazi ya awali hadi chuo kikuu limeshuhudiwa. Hii ni moja ya hatua kubwa kuwahi kufikiwa tangu nchi ilipoanza kujitawala. Katika sekta ya afya, hospitali, zahanati na vituo vya afya vimejengwa kwa wingi kutegeme mahitaji ya watu.

Miundombinu ya barabara imeimarika maradufu na kuifanya Tanzania kuongoza Afrika Mashariki kuwa na barabara zenye lami kwa kilomita nyingi. Lakini pamoja na mafanikio hayo, nchi imekuwa ikikumbana na changamoto mbalimbali katika kila hatua ya kujaribu kuboresha huduma na mahitaji ya kijamii. 
Waraghbishi toka kijiji cha Pandagichiza wakiwa katika picha ya pamoja mbele ya tanki la maji, ambalo baadhi yao ndio wasimamizi wake kutokana uaminifu wao.

Miongoni mwa changamoto hizo ni usimamizi wa miradi mbalimbali ya maendeleo na ubora wa huduma zinazotolewa. Viwango vya ubora kwa huduma zinazotolewa, vimekuwa vikipungua kadri siku zinavyokwenda na sababu kubwa ni udhaifu wa usimamizi kutoka kwa mamlaka husika. 

Udhaifu huu umesababisha wananchi ambao kimsingi ndiyo walipa kodi za serikali kulalamika kila siku. Ikumbukwe kuwa ukusanyaji mzuri wa kodi na kuweka matumizi wazi husaidia kuboresha huduma mbalimbali ndani ya jamii. Ili kuepukana na utawala mbovu usiojali wala kuheshimu misingi ya utawala bora, kuna haja ya wananchi kufanya kazi pamoja.

 Hapa ndipo tunapouona mpango wa Chukua Hatua kama mkombozi kupita uraghbishi, yaani kuwahuisha na kuwahamasisha watu walionyimwa haki kujiona kama watendaji wakuu na siyo kama watu wa chini mbele ya matabaka mengine. 
Mkurugenzi wa Shirika la CABUIPA Bw. David Rwegoshora akitoa ufafanuzi wa kina namna shirika lao linavyofanya kazi. 

Ni sahihi, kuona wananchi wakisimama imara, kujithamini na kujenga uelewa wa misingi ya uchambuzi wa hali ya maisha yao. Lakini pia, kuwawezesha watu kuwa na utamaduni wa kuthubutu kujaribu mambo mbalimbali ya maendeleo. 


JESHI LA POLISI KITENGO CHA USALAMA BARABARANI PAMOJA NA VODACOM TANZANIA WAENDELEA KUTOA ELIMU KWA MADEREVA NA ABIRIA KUPAZA SAUTI

$
0
0
Mkuu wa kitengo cha elimu kwa Umma kitengo cha Usalama barabarani makao makuu ya Polisi ASP,Abel Swai(kushoto) akitoa ufafanuzi kwa Maofisa wa Jeshi la Polisi – Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Morogoro pamoja na Ofisa wa Vodacom Tanzania, Heladius Kisiwani(katikati) kabla ya kuanza zoezi la kutoa elimu kwa madereva kutokutumia simu na kilevi wakati wote wakitumia vyombo vya moto ikiwa ni mwendelezo wa kampeni ya”Wait to Send”inayoendeshwa na Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kitengo cha Usalama Barabarani,ilifanyika jana katika Stendi kuu ya mabasi ya Msamvu mkoani Morogoro.

Abiria wa Mabasi yaendayo mikoani wakimsikiliza Mkuu wa kitengo cha elimu kwa Umma kitengo cha Usalama barabarani makao makuu ya Polisi ASP,Abel Swai,wakati alipokuwa anawalelimisha abiria hao ndani ya basi linalofanya safari zake mikoani ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa kampeni ya”Wait to Send”inayotoa elimu kwa madereva kutokutumia simu na kilevi wakati wote wakitumia vyombo vya moto.Kampeni hiyo inaendeshwa na Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kitengo hicho ilifanyika jana katika Stendi kuu ya Msamvu mkoani Morogoro.
Maofisa wa Jeshi la Polisi Usalama Barabarani Mkoani Morogoro,wakimsikiliza Kaimu mkuu wa kanda ya kati wa Vodacom Tanzania,Heladius Kisiwani(kulia)wakati alipokuwa akiwapa maofisa hao maelezo kuhusiana na pete ya kidoleni inayotolewa na Kampuni hiyo kwa kushirikiana na jeshi hilo yenye ujumbe“Wait To Send” unaohamasisha madereva wa vyombo vya moto kutokutumia simu za mkononi wakiwa wanaendesha vyombo hivyo,Zoezi hili lilifanyika jana katika kituo cha mabasi yaendayo mkoani cha Msamvu mkoani Morogoro.
Askari wa Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani mkoa wa Morogoro,SGT. John Masawe(kushoto)akimpima kiwango cha pombe mwilini dereva wa basi la kwenda mikoani,Rajabu Abdallah ikiwa ni mwendelezo wa kampeni ya”Wait to Send”inayoendeshwa na Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kitengo hicho.

RAIS MAGUFULI AONANA NA MJUMBE MAALUMU WA RAIS PAUL KAGAME WA RWANDA NA MABALOZI WA USWISI NA KUWAIT

$
0
0
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na balozi wa Kuwait hapa nchini Mhe. Jasem Al Najem Ikulu jijini Dar es salaam leo Disemba 23, 2015.
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akizungumza na Mjumbe Maalum wa Rais Paul Kagame wa Rwanda ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Mhe. Louise Mushikwabo Ikulu jijini Dar es salaam leo Disemba 23, 2015.
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiongea na balozi wa Uswisi hapa nchini Mhe. Florence Tinguely Ikulu jijini Dar es salaam leo Disemba 23, 2015.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
USWISI imeahidi kuendeleza ushirikiano na Tanzania katika nyanja mbalimbali za maendeleo huku mkazo mkubwa ukiuelekeza katika kuendeleza elimu ya mafunzo ya ufundi stadi.

Balozi wa Uswisi hapa Nchini Mheshimiwa Florence Tinguelly Mattli, amesema hayo leo tarehe 23 Desemba, 2015 alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu Jijini Dar es salaam.

Balozi Florence amemueleza Rais Magufuli kuwa pamoja na kuwepo kwa miradi mingine ambayo nchi hiyo inaendelea kuitekeleza kwa kushirikiana na Tanzania, katika awamu hii Uswisi itatilia mkazo katika elimu ya ufundi stadi ili kuwawezesha vijana wanaosoma kuwa na ujuzi unaowawezesha kuzalisha bidhaa na kujipatia kipato kama ambavyo nchi ya Uswisi inafanya.

Maeneo mengine ambayo viongozi hao wamezungumzia ni kuimarisha ushirikiano katika uwekezaji, ambapo Rais Magufuli amewaalika wawekezaji kutoka Uswisi kufanya biashara na Tanzania, kuimarisha huduma za bandari na pia kuongeza uwezo katika kukabiliana na vitendo vya Rushwa.

Kuhusu Sekta ya afya, Rais Magufuli ameipongeza Uswisi kwa kushirikiana na Tanzania kupitia Taasisi ya Afya Ifakara katika kukabiliana na changamoto mbali mbali za kiafya ikiwemo kukabiliana na ugonjwa wa Malaria na ameahidi kuwa Serikali itaendelea kuitumia taasisi hiyo ili kusaidia juhudi za kukabiliana na magonjwa.

Wakati Huo Huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Kuwait hapa Nchini Mheshimiwa Jasem Al Najem Ikulu, Jijini Dar es salaam.

Katika Mazungumzo hayo, Balozi Al Najem amewasilisha salamu za mfalme wa Kuwait Mheshimiwa Sabah Al Ahamad Al Jaber al Sabah kwa Rais Magufuli, ambaye amempongeza kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa awamu ya tano na amemhakikishia kuwa Kuwait itaendelea kushirikiana na Tanzania katika maendeleo ikiwemo kufadhili utekelezaji wa miradi mbalimbali katika sekta za ujenzi, Maji na Kilimo.

Miongoni mwa miradi hiyo ni mradi wa ujenzi wa barabara ya Chaya - Nyahua yenye urefu wa kilometa 85 kwa kiwango cha lami ambapo Tanzania imeomba ufadhili wa dola milioni 85, Mradi wa Maji wa Same - Mwanga - Korogwe ambapo Tanzania imeomba ufadhili wa dola milioni 20 na Mradi mkubwa wa kilimo cha umwagiliaji katika bonde la Mhongo na Luhiche Mkoani Kigoma ambapo Kuwait imeonesha nia ya kuufadhili.

Aidha, Rais Magufuli amemshukuru Mfalme wa Kuwait kwa salamu zake za pongezi na amewaalika wafanyabiashara wa Kuwait kushirikiana na Tanzania katika biashara na uwekezaji.

Katika Hatua nyingine Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amekutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda Mheshimiwa Louise Mushikiwabo aliyetumwa kuleta ujumbe maalum wa Rais Paul Kagame wa Rwanda.

Katika Ujumbe huo, Mheshimiwa Kagame amemuhakikishia Rais Magufuli kuwa Rwanda itaendelea kushirikiana na Tanzania katika nyanja mbalimbali za kiuchumi, kisiasa na kijamii hasa ikizingatiwa kuwa licha ya kuwa ni nchi jirani ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Rwanda ni marafiki na ndugu wa Tanzania.

Rais Kagame pia amempongeza Rais Magufuli kwa uongozi mzuri aliounesha katika siku za mwanzo za uongozi wake wa awamu ya tano ambao amesema anauunga mkono.

Pamoja na kupokea salamu za Rais Kagame, Rais Magufuli na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda wamezungumzia mgogoro wa kisiasa unaoendelea nchini Burundi na wote kwa pamoja wameona ni muhimu kupata suluhisho kwa njia ya mazungumzo ili wananchi waweze kuishi kwa amani na kuendelea na shughuli zao maendeleo  

Gerson Msigwa 
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam

23 Desemba, 2015  

WATU SABA WAFARIKI DUNIA KWA KUUNGUA NA MOTO NA WENGINE KUMI WAJERUHIWA

$
0
0
 Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kigoma Ferdnand Mtui  akizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani) juu ya ajali ya moto iliyotokea Mkoani Kigoma.
 Majeruhi wakiendelea kupatiwa huduma katika wodi namba saba hospitali ya Mkoa wa Kigoma.
 Majeruhi wakiendelea kupatiwa huduma ya matibabu katika wodi namba saba hospitali ya Mkoa wa Kigoma.

                                               Na Editha Karlo wa blog wa jamii,Kigoma
WATU saba wamefariki duniani na wengine kumi wamejeruhiwa katika ajali ya gari walilokuwa wakisafiria kupinduka na kulipuka na kuwaka moto.

Akiongea na mtandao huu ofisini kwake Mganga Mkuu wa hospitali ya Mkoa wa Kigoma Maweni Dkt. Leonard Subi amesema kuwa jana majira ya saa 12 jioni walipokea miili ya marehemu 6 na majeruhi 11 ilipofika saa 6 usiku majeruhi mmoja alifariki duniana na kupelekea idadi ya vifo kuwa saba.

Aliwataja waliofariki katika ajali hiyo ni Ashura Mussa, Kadogo Yusuph, Kabwe Iddy, Mwamvua Juma na Peter Sungura,maremu wawili miili yao bado haijatambulika sababu ya kuungua vibaya.

Dkt. Subi aliwataja pia majeruhi wa ajali hiyo kuwa ni Andrew Peter, Amos Thomas, Mutta Hamis, Shabaan Fadhil, Hassan Kasa, Esau Elias, Asha Kassim na Riziki Jaah.

"Majeruhi wote wamelazwa wodi namba saba na hali zao siyo nzuri wanaendelea na matibabu, mtoto aitwaye Riziki Jaah mwenye umri wa miezi nane ndiye aliyenusurika katika ajali hiyo hajaumia popote mama yake alimtupa dirishani baada ya moto kuwaka ila mama yake alifariki kwa kuungua kwenye ajali hiyo"alisema Dkt. Subi.

Naye Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Kigoma, Ferdnand Mtui amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ya gari aina ya Toyota Hiace lenye  namba T.700 ADK lililokuwa likitoka Kigoma mjini kwenda katika kijiji cha Subankala kata ya Ilagala Wilayani Uvinza kilichopo mwambao mwa ziwa Tanganyika.

Kamanda Mtui alisema kuwa ajali hiyo ilitokea katika kijiji cha Mwakizega na chanzo cha ajali hiyo ni dereva kuwakwepa watembea kwa miguu kisha kugonga gema iliyopelekea gari kupinduka na kuwaka moto.

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli Atoa Mkono wa Krismas na Mwaka Mpya kwa Wazee wa Kijiji cha Welezo Zanzibar.

$
0
0

Mlukulu wa Ikulu Zanzibar Ndg Ameir Ali Khatib akimkabidhi Mbuzi Sister Mary Gemma wa kituo cha Wazee Welezo, hafla hiyo imefanyika katika makaazi ya Wazee hao Welezo Zanzibar, Vyakula hivyo vimetolewa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli kwa ajili ya Wazee hao kujumuiika na Wananchi katika kusherehekea Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya. 
Mlukulu wa Ikulu Zanzibar Ndg Ameir Ali Khatib akimkabidhi Mafuta ya Kupikia Sister Mary Gemma wa kituo cha Wazee Welezo, hafla hiyo imefanyika katika makaazi ya Wazee hao Welezo Zanzibar, Vyakula hivyo vimetolewa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli kwa ajili ya Wazee hao kujumuiika na Wananchi katika kusherehekea Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya. 

Wazee wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wakati wa hafla hiyo ya kukabidhiwa Vyakula kwa ajili ya kusherehekea Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya vilivyotolewa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli kwa Wazee hao. kuweza kushiriki kwa vizuri katika sikukuu hizo.

MADEREVA WATAKAOZIDISHA ABIRIA KWENYE VYOMBO VYA USAFIRI KUKIONA

$
0
0
 Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Bulimba akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, kuhusiana na Jeshi la Polisdi Nnchi zima kupambana na watu watakaovunja sheria ya usafirishaji wa watu kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Bulimba leo jijini Dar es Salaam.
Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
JESHI la Polisi Nchini limewatahadharisha madereva  watakaozidisha  idadi ya abiria kuliko uwezo wa chombo cha usafari kwani ni kosa kisheria na watakaozidisha abiria kwenye vyombo vyao vya usafiri watachukuliwa hatua za kisheria.

Operesheni hiyo inaanza leo baada ya tamko la Jeshi la Polisi na kuanza kutekeleza kwa wale wote wataobeba abiria wengi tofauti na uwezo wa basi, watachukuliwa hatua madereva wa daladala,mabasi ya mikoani pamoja na magari aina ya Noah.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Bulimba amesema kuwa Jeshi la polisi linaanza operesheni ambayo ni endelevu na kuwataka watu wafuate sharia ya ubebaji wa abiria.

Advera amesema kuwa katika kipindi hiki cha siku kuu Jeshi la polisi limejipanga katika kuwadhibiti waendesha bodaboda kwa wataopandisha watu zaidi  ya wawili (mishikaki) kukiona cha mtema kuni kwa mujibu wa sheria za usalama barabarani.

Aidha amewataka wananchi kutoa taarifa za kihalifu katika msimu wa sikukuu na uimarishaji wa ulinzi wa watu na mali zao na maisha yaweze kuendelea baada ya sikukuu.
Viewing all 110186 articles
Browse latest View live




Latest Images