Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda akizungumza na wazazi ambao watoto wao wanasubiri kufanyiwa upasuaji wa moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati alipotembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuwajulia hali watoto ambao wametibiwa kwa ufadhili wa wadau waliomchangia fedha kwa ajili ya matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Mafuta ya PUMA Energy Tanzania Dominic Dhanah ambaye kampuni yake imechangia kiasi cha shilingi milioni 40 kwa ajili ya upasuaji wa moyo kwa watoto 20.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Mafuta ya PUMA Energy Tanzania Dominic Dhanah wakimsikiliza Mama wa mtoto Aidan Mfunya mkazi wa Kigoma ambaye mtoto wake anasubiri kufanyiwa upasuaji wa moyo kwa ufadhili wa mkuu wa mkoa huyo ambaye wadau wake mbalimbali walimchangia fedha kwa ajili ya matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo. Hadi sasa jumla ya Watoto 50 wameshafanyiwa upasuaji kwa ufadhili wa Mhe. Makonda na wadau wake na hali zao zinaendelea vizuri.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Mafuta ya PUMA Energy Tanzania Dominic Dhanah wakimjulia hali mtoto Jasin Ally mkazi wa Arusha ambaye anasubiri kufanyiwa upasuaji katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ufadhili wa mkuu wa mkoa huyo ambaye wadau wake walimchangia fedha kwa ajili ya matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo. Kampuni ya PUMA Energy imemuunga mkono kwa kuchangia kiasi cha shilingi milioni 40 kwa ajili ya upasuaji wa moyo kwa watoto 20.
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Mafuta ya PUMA Energy Tanzania Dominic Dhanah wakimjulia hali mtoto Doreen Likweri ambaye anasubiri kufanyiwa upasuaji wa moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ufadhili wa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda ambaye wadau wake walimchangia fedha kwa ajili ya matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo. Kampuni ya Mafuta ya PUMA Energy Tanzania imemuunga mkono mkuu wa mkoa huyo kwa kuchangia kiasi cha shilingi milioni 40 kwa ajili ya upasuaji wa moyo kwa watoto 20.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) akiwaeleza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Mafuta ya PUMA Energy Tanzania Dominic Dhanah huduma zinazotolewa katika chumba cha wagonjwa watoto walioko katika uangalizi maalum (JKCI) wakati ugeni huo ulipotembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuwajulia hali watoto waliotibiwa kwa ufadhili wa wadau waliomchangia fedha mkuu wa mkoa huyo kwa ajili ya matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo. Hadi sasa jumla ya Watoto 50 wameshafanyiwa upasuaji na hali zao zinaendelea vizuri.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda akimfundisha jinsi ya kupiga picha mtoto Jovin Muniko ambaye amefanyiwa upasuaji wa moyo kwa ufadhili wa mkuu wa mkoa huyo na wadau wake kwa ajili ya matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya PUMA Energy Dominic Dhanah ambaye kampuni yake imemuunga mkono Mhe. Makonda na kuchangia kiasi cha shilingi milioni 40 kwa ajili ya upasuaji wa moyo kwa watoto 20.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya PUMA Energy Dominic Dhanah wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), wazazi na Watoto ambao wamefanyiwa upasuaji wa moyo kwa ufadhili wa mkuu wa mkoa huyo mara baada ya kampuni ya Mafuta ya PUMA Energy Tanzania kukabidhi mfano wa hundi ya shilinngi milioni 40 kwa ajili ya upasuaji wa moyo kwa watoto 20.
Zainabu Mundera mkazi wa Kyela mkoani Mbeya akimshukuru Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda kwa kumfadhili mtoto wake kufanyiwa upasuaji wa moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Hadi sasa jumla ya Watoto 50 wameshafanyiwa upasuaji kwa ufadhili wa Mhe. Makonda pamoja na wadau wake na hali zao zinaendelea vizuri.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda akizungumza na baadhi wa wafanyakazi wa chumba cha wagonjwa walioko katika uangalizi maalum (ICU) na upasuaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati alipotembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuwajulia hali watoto ambao wamefanyiwa na wanaosubiri kufanyiwa upasuaji wa moyo kwa ufadhili wa mkuu wa mkoa huyo pamoja na wadau wake.Picha na JKCI
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda akimfundisha jinsi ya kupiga picha mtoto Jovin Muniko ambaye amefanyiwa upasuaji wa moyo kwa ufadhili wa mkuu wa mkoa huyo na wadau wake kwa ajili ya matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya PUMA Energy Dominic Dhanah ambaye kampuni yake imemuunga mkono Mhe. Makonda na kuchangia kiasi cha shilingi milioni 40 kwa ajili ya upasuaji wa moyo kwa watoto 20.