Diwani Kata ya Mecco Manispaa ya Ilemela, Godlisten Kisanga (CCM) akizungumza wakati wa hafla ya chakula cha pamoja na waalimu wote wa Shule tatu za Msingi (Nundu, Nundu D na Nyamwilekelwa) katika Kata hiyo iliyolenga kuwapongeza waalimu hao kwa juhudi zao za kuimarisha ufaulu kwa wanafunzi wanaohitimu darasa la saba.
Afisa Elimu Kata ya Mecco Manispaa ya Ilemela, Mwl. Agnes Mugyabuso (kushoto), Shule zilizofanya vizuri kwa kila somo katika Kata hiyo kwenye mtihani wa darasa la Saba mwaka huu ambapo Shule hizo zilikabidhiwa cheti cha pongezi na Diwani wa Kata ya Mecco, Godlisten Kisanga.
Diwani Kata ya Mecco Manispaa ya Ilemela, Godlisten Kisanga (kulia), akimkabidhi Cheti cha pongezi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Nyamwilekelwa, Mwl. Lyatura Mukama (kushoto) baada ya Shule yake kuibuka kidedea kwenye masomo ya Kiswahili na Kiingereza.
Diwani Kata ya Mecco Manispaa ya Ilemela, Godlisten Kisanga (kulia), akimkabidhi Cheti cha pongezi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Nundu D, Mwl. Lucas Robert (kushoto) baada ya Shule yake kuibuka kidedea kwenye masomo ya Hisabati na Maarifa ya Jamii.
Utaratibu huu wa kushindanisha Shule za Msingi Kata ya Mecco umelenga kuongeza kiwango cha ufaulu kwa alama A na B tu.