Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 110193

MFANO WA BARUA YA KUOMBA NAKALA YA HUKUMU HUU HAPA.

$
0
0
Na  Bashir Yakub.

Nakala ya hukumu ni haki yako ikiwa ulikuwa mhusika katika kesi au shauri. Unakuwa mhusika katika kesi au shauri pale unapokuwa mshitaki au mshitakiwa,  mlalamikaji au mlalamikiwa, au mhusika mwingine mwenye maslahi.  Hapa ndipo unapohesabika kuwa mhusika katika kesi au shauri na hapa ndipo unapokuwa na haki ya kuomba kupatiwa nakala ya hukumu.


Makala yaliyopita yalieleza kuwa nakala ya hukumu ni muhimu hasa ukitaka kukata rufaa au kuchukua hatua zaidi , lakini pia ni muhimu kama nyaraka ya kumbukumbu kwa ajili ya kesho, pia ni muhimu kwa ajili ya utekelezaji wa kile kilichoamuliwa.  Leo tuone mfano halisi wa barua ya  maombi ya  nakala ya hukumu 

kama ulivyo hapa chini ;-




Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,                                                        24 / 5 / 2018

S.L.P..............................

Dar es salaam.

YAH ; MAOMBI YA KUPATIWA NAKALA YA HUKUMU.

Nilikuwa mlalamikiwa katika shauri namba  13 la mwaka 2018,  ambalo limetolewa hukumu tarehe 22 / 3 / 2018, mbele ya Mhe. Kijana Mponela. Ninaomba kupatiwa nakala ya hukumu  kwa kumbukumbu au hatua zaidi.

Wako

Mti Mkavu

( Aliyekuwa mlalamikiwa ).

0717600900

Sahihi...............................

               


Viewing all articles
Browse latest Browse all 110193

Latest Images

Trending Articles





Latest Images