Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 110186

RIPOTI YA CAG YASABABISHA MAGUFULI KUSIMAMISHA WAKURUGENZI WAWILI

$
0
0
*Aagiza wachunguzwe dhidi ya tuhuma zilizobainika kwenye ripoti
*Ataka iwe fundisho kwa wakurugenzi wengine nchini, atoa angalizo
*Azungumzia ucheleweshaji kesi unaosababsha Serikali kukosa Trilion 4.4/-

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

RAIS Dk.John Magufuli amewasimamisha kazi kuazia leo wakurugenzi wa 
Halmashauri ya Kigoma Ujiji na Pangani baada ya Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) kubaini madudu yakiwemo ya kupata hati chafu.

Ametoa maagizo hayo leo asubuhi hii baada ya kupokea ripoti ya CAG Profesa Juma Asaad ambapo mbali ya kumshukuru kwa kazi nzuri aliyoifanya akatangaza kuanza kuchukua hatua kwa kuwasimamisha wakurugenzi hao ili iwe fundisho kwa wakurugenzi wengine.

"Ripoti ya CAG imezitaja halmashauri mbili iko ya Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Ujiji na Pangani ,Nitoe maagizo wakurugenzi hao wawili wasimamishwe kazi mara moja na hata kama si vizuri kuchukua hatua basi ni vema nikachukua hatua haraka ili uchunguzi ufanyike kuhusu tuhuma ambazo CAG amezisema kwenye ripoti yake.

"Wakati natangaza kuchukua hatua za kuwasimamisha wakurugenzi hawa naona mmenyamaza najua kwasababu wengine hawependi hatua zichukuliwe lakini nimeanza kuchukua hatua iwe fundisho kwa wengine kwani tusipochukua hatua wengine wataendelea,"amesema Rais Magufuli.

Amesisitiza ni bora kuanza kuchukua hatua na kwamba hata CAG kwenye 
maelekezo yake kwa Serikali amezungumzia umuhimu wa kuchukua hatua na hivyo amenza kutekeleza hapo hapo baada ya kukabidhiwa ripoti na mengine wataendelea kuyatekeleza kwa kuchukua hatua mbalimbali ili mambo yaende.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Mussa Assad Ikulu jijini Dar es Salaam. 



Viewing all articles
Browse latest Browse all 110186

Latest Images

Trending Articles



Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>