Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 110192

MKURUGENZI MANISPAA YA DODOMA GODWIN KUNAMBI AKABIDHI VITAMBULISHO KWA MMACHINGA 140

$
0
0
Na Ramadhani Juma-Ofisi ya Mkurugenzi

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi amekabidhi vitambulisho kwa Wafanyabiashara ndogo maarufu kama m Machinga wanaofanya shughuli zao katika soko la jioni ili waweze kufahamiana wakati wa biashara zao na hata kusaidia kuimarisha masuala ya ulinzi na usalama.

Wafanyabiashara ndogo wapatao 140 wanaofanya shughuli zao katika eneo la Viwanja vya Nyerere wamekabidhiwa vitambulisho hivyo na Mkurugenzi huyo katika hafla fupi iliyofanywa katika viwanja hivyo mchana wa leo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Kunambi amewaasa wafanyabiashara hao kuwa na utamaduni wa kutunza akiba ili kukuza mitaji yao huku akiwaahidi kuwaboreshea mazingira ya kazi zao na kwamba hakuna kiongozi atakayewaondoa katika maeneo hayo mpaka watakapatiwa maeneo mbadala na rafiki kwa biashara zao.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi (wa pili kulia) akimvisha kitambulisho rasmi mmoja ya Wafanyabiashara ndogo wa soko la jioni katika eneo la viwanja vya Nyerere Mjini Dodoma wakati wa hafla ya kuwapatia vitambulisho wafanyabiashara hao iliyofanywa leo Februari 2, 2018. Jumla ya Wafanyabiashara 140 wa eneo hilo wamepatiwa vitambulisho hivyo. Kulia ni Ofisa Masoko wa Manispaa hiyo Steven Maufi.
Baadhi ya Wafanyabiashara Ndogo wakifuatilia hotuba ya mgeni Rasmi
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi (kushoto) akizungumza na Wafanyabiashara ndogo wa soko la jioni katika eneo la viwanja vya Nyerere Mjini Dodoma wakati wa hafla ya kuwapatia vitambulisho wafanyabiashara hao iliyofanywa leo Februari 2, 2018. Jumla ya Wafanyabiashara 140 wa eneo hilo wamepatiwa vitambulisho hivyo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi (wa pili kulia) akimvisha kitambulisho rasmi mmoja ya Wafanyabiashara ndogo wa soko la jioni katika eneo la viwanja vya Nyerere Mjini Dodoma wakati wa hafla ya kuwapatia vitambulisho wafanyabiashara hao iliyofanywa leo Februari 2, 2018. Jumla ya Wafanyabiashara 140 wa eneo hilo wamepatiwa vitambulisho hivyo. Kulia ni Ofisa Masoko wa Manispaa hiyo Steven Maufi.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 110192

Latest Images

Trending Articles





Latest Images