Aliyekuwa mtangazaji wa muda mrefu wa Radio Free Africa, Zuberi Msabaha amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumatano Januari 10, 2018, huko jijini Mwanza.
Zuberi Msabaha alikuwa ameugua kwa muda mrefu huku akipatiwa matibabu yake sehemu tofauti tofauti hapa nchini. Msiba wake upo Mabatini jijini Mwanza na mazishi yatafanyika Jumatano ya leo.
Marehemu Zuberi Msabaha alijijengea umaarufu mkubwa kupitia kipindi chake cha Bolingo Time kinachorushwa hewani na kituo cha Radio cha RFA.
Zuberi Msabaha alikuwa mchambuzi mzuri sana wa muziki wa Dansi hasa muziki wa Kongo ambao mara nyingi unaimbwa kwa lugha ya Kilingala, Kikongo, kikasai, na Kifaransa.
Mungu ailaze Mahali Pema Peponi Roho
ya mpendwa wetu Papa Zuberi Msabaha.
#darmpya