Mstahiki meya wa Jiji la Dar es salaam Mheshimiwa Isaya Mwita Charles leo amekabidhi rasmi magari mawili aina ya Suzuki Carry maarufu kama (Kirikuu) kwa washindi wa shindano la shika ndinga linaloandaliwa na kuendeshwa na kituo cha utangazaji cha EFM redio, washindi waliopatikana katika fainali iliyofanyika tarehe sita mwezi wa tano mwaka huu katika viwanja vya Tanganyika Packers Kawe Jijini Dar es Salaam.

Mstahiki Meya akitoa pongezi zake kwa washindi Kutoka Kulia ni Meneja mkuu Dennis Busulwa, Mshindi (Michael Peter), akifuatiwa na Mshindi Joyce Daniel pamoja na Rukia Mtingwa Meneja masoko Zantel

Washindi wa shindano hilo wakiwa wameshikilia kadi za gari Kutoka kulia ni Michael Peter na Joyce Daniel

Shamla Shamla zikiendelea

Wasindikizaji wa mshindi Michael Peter kutoka Salasala