Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117395

TRA Yatoa siku 39 kodi ya majengo iwe imelipwa Mwanza

$
0
0

Na Atley Kuni- Afisa habari Mwanza.

Mamlaka ya mapato nchini imetoa muda hadi kufikia  Juni 30, mwaka huu wananchi wote wanaodaiwa kodi ya majengo kuhakikisha wanailipa kodi hiyo ilikuepuka kufikishwa mahakamani na kutozwa faini.

Kauli hiyo imetolewa na kamishina mkuu wa TRA nchini ndugu Charles Kichere, alipokuwa akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Jijini Mwanza hii leo.

“Mwisho wa kulipa kodi ya majengo bila adhabu ni tarehe 30 Juni, 2017. Hivyo wenye majengo yaliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza (Nyamagana), na Manispaa ya Ilemela wafike ofisi za TRA zilizopo karibu nao kuchukua ankara zao endapo hawajazipokea kutoka kwa viongozi wa serikali za mitaa yao au kujisajili  na kulipa kupitia benki yoyote ya biashara” alisema Kichere. 

Kichere amefafanuakuwa kwa walioko sehemu ambazo nyumba zimethaminishwa watalipa kiwango cha asilimia ya thamani ya jengo kama inavyoonesha kwenye ankara zao na walioko maeneo ambayo hayajapimwa au kuthaminishwa watalipa viwango maalum vilivyopitishwa na mabaraza ya madiwani na kutangazwa na TRA kwenye vyombo vya habari.

Kichere amevitaja viwango hivyo vilivyopitishwa kuwa, ni shilingi za kitanzania (20,000) kwa Jiji la Mwanza na kumi na tano elfu (15,000) kwa Manispaa ya Ilemela. 
 Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella, akiogea katika kikao hicho cha TRA na Waandishi wa habari Jijini Mwanza, katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.
Kamishna Mkuu wa TRA nchini,Charles Kichere, akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani ( Picha zote na Ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Mwanza)
 Viongozi wa Tanzania Chamber of Commerce Mkoa wa Mwanza wakimsikiliza Kamishna wa TRA nchini wakati wa kikao hicho na waandishi wa habari Mkoani Mwanza.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Viewing all articles
Browse latest Browse all 117395

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>