Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117374

MAKAMU WA RAIS KUZINDUA KAMPENI YA MIMI NA WEWE MJINI UNGUJA

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amewasili mjini Unguja – Zanzibar akitokea mkoani Dodoma ambapo hapo kesho anatarajiwa kuzindua ya kampeni maalum inayojulikana kama Mimi na Wewe mjini Unguja.

Lengo la kampeni hiyo ni kuhamasisha jamii kuchangia kwa hali na mali katika uboreshaji wa huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo elimu, afya, mazingira na kusaidia watu wasiojiweza katika Mkoa wa Mjini Magharibu, Unguja.

Katika uwanja wa ndege wa Zanzibar, Makamu wa Rais amepokelewa na Mkuu wa mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Ayoub Mohamed Mahmoud pamoja na Viongozi Mbalimbali wa Serikali na wa Vyama vya siasa.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM  Mkoa wa Mjini Magharibi,Borafya Silima mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege  wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume. #Picha na Adam H. Mzee/ VPO 

Viewing all articles
Browse latest Browse all 117374

Trending Articles