Na Ripota wa Mafoto Blog, Dar
UBABE na unafiki wa baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) inaelezwa kuwa ndio chanzo cha kupoteza jimbo la Ukonga na mengine ya Mkoa wa Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Rodrick Mpogolo, alisema hayo jana wakati alipozungumza na wanachama na viongozi wa Chama katika majimbo ya Ukonga na Segerea.
Alisema viongozi hao waliendekeza mizengwe na umimi, ambapo matokeo yake waliwavuruga wanachama na jimbo likachukuliwa na upinzani,sasa wanajuta.
"Tumewasababishia wanachama kubaki kama wakiwa, hawana mbunge,na sehemu zingine hawana madiwani. Yote ni kutokana na ubinafsi na makundi yaliyokiumiza Chama,"alisema.
Mpogolo alisema CCM haiwezi kukubali viongozi wachache wenye roho za chuki waendelee kuwanyanyasa wanachama wenzao kwa sababu ya maslahi ya makundi yao."Naomba kila mwanachana afanye mabadiliko ndani ya nafsi yake.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Rodrick Mpogolo, akizungumza na Wanachama, Viongozi wa CCM Kata ya Tabata, Jimbo la Segerea, wakati akiwa katika ziara yake ya kuimarisha Chama Mkoa wa Dar es Salaam, jana. Picha Zote na Muhidin Sufiani (MAFOTO).
Wanachana wa CCM Jimbo la Segerea wakiinua mikono kufurahia hotuba ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Rodrick Mpogolo,jana.
Wanachama wa CCM Jimbo la Ukonga wamsikiliza Naibu Katibu Mkuu, Rodrick Mpogolo,wakati akiwahutubia kwenye Ukumbi wa Check Point jana.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA