Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117361

MAKUMBUSHO NA NYUMBA YA UTAMADUNI KUADHIMISHA SIKU YA MAKUMBUSHO DUNIANI.

$
0
0
Bw Achiles Bufure, Mkurugenzi Makumbusho 
na Nyumba ya Utamaduni Dar es salaam 

Tarehe 18 May ni siku ya Makumbusho Duniani kwa apata Tanzania, Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni itaungana na Makumbusho zote katika kuadhimisha siku hii muhimu hivyo watanzania wameshauriwa kuudhuria katika maadhimisho hayo ili waweze kupanua uwelewa zaidi wa mambo mbali mbali yanayo huyu maisha yao na nchi kwa ujumla. 
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar Es Salaam Bwana Achiles Bufure ofisini kwake, Bwana Bufure ameongeza kuwa katika Maadhimisho hayo, kutakuwa na Onesho maalum litakalo onesha vifaa mbali mbali vya ofisi alivyotumia Muhasisi wa Taifa hili Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julias Kambarage Nyerere, Mafunzo shirikishi kwa watoto juu ya shughuli za kimakumbusho na Onesho la jukwaani.  
Wananchi mbali mbali wameisifu Mkumbusho na Nyumba ya Utamaduni kwa kuadhimisha siku hiyo kwa kufungua milango hata kwa watu wasio na uwezo wakulipia pindi wanapo tembelea Makumbusho hiyo kwakuwa na wao watapata nafasi adhimu ya kujifunza mambo yanayo husu nchi yao kwa kupitia vioneshwa vilivyopo ndani ya Makumbusho. 
 Maadhimisho hayo ya Siku ya Makumbusho Duniani yatadumu kwa muda wa wiki moja kuanzia leo ili kutoa nafasi kwa watanzania warika mbali mbali kutembelea Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni na kwa tarehe 18 May hakutakuwa na kiingilie cha kuingia na kutembelea maonesho mbalimbali yaliyopo Makumbusho hiyo iliyopo mkabala na chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) Dar es Salaam, Posta.



Viewing all articles
Browse latest Browse all 117361

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>