Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117361

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigela akagua mitambo ya kiwanda cha Cement kitachojengwa mkoani mwake

$
0
0
RC Shigela alipotembelea Kampuni inayojenga mradi mkubwa wa kiwanda cha Saruji Tanga. Kiwanda hicho muhimu kwa uchumi wa Tanzania kitazalisha zaidi ya Tani milioni 7 za Saruji kwa Mwaka.
Alionana na Mwenyekiti wa Kampuni hiyo pamoja na Viongozi wa Mji wa Yangzhou ambao kwa upande wao walikubaliana kuanzisha ushirikiano wa Maendeleo baina ya Miji hiyo miwili (Sister Cities).
Tanga tujiandae kwa uwekezaji huu mkubwa na wa mfano!
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigela (kati) akiwa nchini China akikagua mitambo na mashine zilizofungwa tayari kwa kusafirishwa kupelekwa mkoa Tanga kwa ajili ya uwekezaji wa kiwanda cha Cement kitakachogharimu Dola za  Kimarekani 1.4 bilion kitakachozalisha tani milioni saba na kuajiri watanzania 4000.  Ujenzi wa kianda hicho unatarajiwa kuanza mwezi ujao. Kushoto ni Ndg. Suleiman Serela, Mtanzania aliye masomoni nchini China akichukua PhD ya Sheria
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigela (kati) akiwa na wenyeji wake nchini China akikagua mitambo na mashine zilizofungwa tayari kwa kusafirishwa kupelekwa mkoa Tanga kwa ajili ya uwekezaji wa kiwanda cha Cement 
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigela na  Ndg. Suleiman Serela wakiwa nchini China wakioneshwa mfano wa kiwanda cha cement kitachojengwa mkoani Tanga 
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigela (kati) akiwa na mwenyeji wake nchini China akiendelea kukagua mitambo na mashine zilizofungwa tayari kwa kusafirishwa kupelekwa mkoa Tanga kwa ajili ya uwekezaji wa kiwanda cha Cement 

Viewing all articles
Browse latest Browse all 117361

Trending Articles