Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 117285

WAZAZI WATAKIWA KUWAEPUSHA WATOTO NA MIMBA NA NDOA ZA UTOTONI.

$
0
0
Na Hassan Silayo-MAELEZO 

Wazazi nchini wametakiwa kutekeleza wajibu wao kwa watoto kwa kuhakikisha wanawaendeleza na kuwawezesha wafanikishe ndoto zao kwa kuwaepusha na ndoa pamoja na mimba za utotoni. 

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi.Sihaba Nkinga katika Mahafali ya 5 ya kidato cha sita ya shule ya sekondari Mwendakulima iliyopo Halmashauri ya Mji wa Kahama. 

Bi.Sihaba amesema kuwa wazazi wanajukumu la kuhakikisha wanawalea na kuwalinda kwani wazazi wanahaki ya kisheria ya kuwalinda watoto dhidi ya viashiria vyote vinavyoweza kuwaweka katika mazingira hatarishi. 

Bi.Sihaba aliongeza kuwa wazazi na walezi wana haja ya kushirkiana na serikali katika kuwalinda watoto wakike kwani watoto wa kike ni nyenzo muhimu hasa kwenye mpango wa serikali katika kuelekea uchumi wa kati kupitia viwanda. 

Aidha,Bi.Sihaba kuwa Serikali imefanya marekebisho ya Sheria ya Elimu sura namba 33 inayotoa katazo kumpa ujauzito motto wa shule chini ya miaka 18 hivyo wazazi wahakikishe wanalisimamia kwa pamoja ili kuweza kufanikisha sheria. 
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi.Sihaba Nkinga akikata utepe kuashiria kuanza kwa mahafali ya 5 ya kidato cha sita katika shule ya Sekondari Mwendakulima iliyopo Halmashauri ya Mji wa Kahama. 
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu kutoka Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi.Deodatha Makani akiongea jambo na Mkurugenzi wa Ubora na Maendeleo wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Save the Children Amy Schmiot mahafali ya 5 ya kidato cha sita katika shule ya Sekondari Mwendakulima iliyopo Halmashauri ya Mji wa Kahama. 
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi.Sihaba Nkinga akitoa vyeti pamoja na zawadi kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari Mwendakulima iliyopo Halmashauri ya Mji wa Kahama alipohudhuria mahafali ya 5 ya kidato cha sita ya shule hiyo. 


Viewing all articles
Browse latest Browse all 117285

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>